Wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. 

Wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika. 

SWALI: Nini maana ya Waefeso 6:24, pale inaposema “katika hali ya kutoharibika”?

[24]Neema na iwe pamoja na wote wampendao Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutokuharibika.


JIBU: Mtume Paulo alipokuwa anahitimisha ujumbe wa waraka wake kwa waefeso, alimalizia kwa kuwatamkia neno la heri watu watu wale akiwaambia ‘NEEMA  ikae pamoja nao.

Lakini tunaona hapo hakukusudia tamko hilo kwa watu wote,  bali anasema ikae kwa wale wampendao Bwana, lakini bado sio tu kwa  wampendao Bwana.. Bali wampendao katika “hali ya kutokuharibika”.

Yaani kwa ufupi upendo usio poa.. Ndio upendo usio haribika.

Ndio ule unaozungumziwa kwenye 1Wakoritho 13. Kwamba hustahimili yote, huvumilia yote, huamini yote, haupungui Neno wakati wowote.

Ni kuonyesha kuwa Bwana wetu Yesu Kristo anastahili kupendwa daima, zaidi ya vitu vyote, kwasababu ya upendo wake mkuu aliotuonyesha sisi wa kuacha vyote mbinguni kwa ajili yetu, ili tukombolewe. Na kwa rehema zake akatupa na vipawa kabisa, na uwezo wa kuitwa wana wa Mungu, kwa nguvu za Roho wake Mtakatifu aliyetupa . Hakika anastahili kupendwa  sana bila ukomo.

Zingatia: Waraka huu sio wa waefeso tu, bali ni wetu pia sote tumeandikiwa. Hivyo tutaongezewa neema ikiwa tutampenda Bwana wetu Yesu Kristo kwa upendo usio haribika. Sio njaa itufanye tumwache, au ufukara, au mke, au kazi, au uzuri, au ubaya, au ndugu, au mali, au afya, au ugonjwa.. au kitu chochote, Bali kila wakati sisi shauku yetu kwa Kristo iwe ni ile ile. Kuomba ni kule-kule, kumtafuta Mungu ni kule-kule. Amen

Neema ya Bwana iwe nasi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! SISI KAMA WAKRISTO NI DHAMBI KUSHEHEREKEA KRISMASI?.

TUNAHESABIWA HAKI BURE KWA NJIA YA IMANI.

Lalama kwa uhai wa watoto wako wachanga wazimiao kwa njaa(Maombolezo 2:19)

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments