JIBU: Baada ya Yesu kukutana na wale wenye ukoma kumi, na kuwaagiza waende kujionyesha kwa makuhani
biblia inatuonyesha walipokea uponyaji wote wakiwa bado wapo njiani, lakini tunaona yule mkoma mmoja hakuendelea na safari yake. Palepale ilimbidi ahairishe kwanza safari yake Na kuja kumshukuru Yesu, na ndipo pengine aendelee na safari yake ya kuelekea kwa makuhani.
Luka 17:14-19
[14]Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
[15]Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
[16]akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
[17]Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
[18]Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
[19]Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Kwanini afanye vile ni kwasababu aliona umuhimu wa kumshukuru Yesu Kristo kwanza zaidi ya wahudumu wake.
Jambo lolote Mungu analotaka kututendea kupitia wahudumu wake..Tujue kuwa Shukrani zetu za kwanza zinapaswa zimrudie yeye.
Amina.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini BWANA awaagize wakoma wakajionyeshe kwa Makuhani?(Luka 17:14
Rudi Nyumbani
About the author