IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE?

IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE?

Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe.

Jenga utamaduni wa kusoma Biblia, siku za mwisho ibilisi anazidi kuwekeza nguvu nyingi kwa watu wasisome wala kulielewa Neno, badala yake wapende tu kusikiliza mahubiri au kufanyiwa maombezi, lakini si Kusoma.

Lakini ukweli ni kwamba tukitaka kuisikia sauti ya Mungu ya wazi kabisa, njia ni kusoma Neno, tukitaka kumwona Mungu suluhisho ni kusoma Neno, tukitaka kumwelewa Mungu katika viwango vingine jawabu ni kusoma Biblia, tukitaka kuishi maisha ya kumpendaza Mungu,ni kusoma tu maandiko. Usipuuzie kamwe kusoma maandiko.

Hebu tujifunze kwa Bwana YESU wakati ule alipokutana na Yule mwanasheria ni maneno gani alimwambia…

Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26 Akamwambia, IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE?

27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”.

Zingatia hayo maneno  katika mstari wa 26, ….IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?

Najiuliza kwanini Bwana Yesu hakumpa jibu la moja kwa moja, lakini badala yake anamrudishia swali.. “IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?”  maana yake kama angesema siju, ni  wazi kabisa Bwana YESU asingempa jibu lolote, badala yake angemwambia akasome maandiko (akatafute katika maandiko)..Na leo hii wengi tunamwuliza sana Bwana maswali ambayo majibu yake yapo kwenye maandiko…..

Tukimwuliza Bwana swali ambalo jibu lake lipo katika biblia, anaweza kujujibu kama tu alivyomjibu huyu mwana sheria…. IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. WASOMAJE?

Hatuwezi kumlazimisha MUNGU azungumze kitu ambacho tayari alishakizungumza katika maandiko…tukimwuliza kitu ambacho tayari kipo ndani ya Biblia tunaweza tukapokea jibu kama hilo hilo tu… IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. TWASOMAJE?

Na kitu pekee anachohakikisha shetani tusikijue ni  UWEZA WA MUNGU pamoja na UWEZA WA MUNGU katika hayo maandiko.. kwa namna gani?

Marko 12:24 “Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?”

Weka ratiba ya kujifunza Biblia mtu wa Mungu, usiishie tu kusikiliza mahubiri, usiishie tu kusikiliza maombi.. bali soma soma soma.. Wakati mwingine unaweza ukawa unapitia vipindi ambavyo hujui nini cha kufanya, huo ni wakati wa kusoma Biblia utapokea ni nini cha kufanya huo wakati..

Unaweza kupitia wakati ambapo hujui uombe nini, soma Biblia utapata nini cha kuombea n.k

Nabii Danieli alikuwa sana kimaarifa na hata kujua nini cha kuoma kwa kusoma maandiko na si tu kutegemea maono yake na njozi zake.

Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”

Na zingatia: Kusoma Biblia si tu kutafuta neno moja la siku na kutembea nalo hilo, acha hiyo desturi!. Neno la Siku liwe ni ufupisho wa kingi ulichokisoma.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini biblia ni neno la Mungu?

Kitabu kifupi katika biblia ni kipi, na ujumbe wake ni upi?

Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)

Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?

Mistari ya biblia kuhusu sadaka

Print this post

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Leave a Reply