Kuota upo uwanjani (uwandani)

Kuota upo uwanjani (uwandani)

Nini maana ya kuota upo uwanjani/uwandani?

Jibu: Kiroho uwanja au uwanda unawakilisha mahali pa mapambano.Wanamichezo wote wanaoshindania tuzo, huwa mashindano hayo yanafanyikia viwandani/uwandani.

Kwahiyo unapoota kuwa upo Uwandani na shughuli zako hazihusiani na viwanja, basi fahamu kuwa upo katika mapambano. Na mapambano hayo yanaweza kuwa mazuri au mabaya.
Mapambano Mazuri:

Mapambano mazuri ni yale ya imani, hivyo kama umeokoka vizuri na umesimama kisawasawa na ukapata ndoto au ono unashindana na watu wengi au wachache katika uwanja/uwanda basi fahamu kuwa huenda Mungu anakuonyesha, au kukukumbush vita vya kiimani vilivyopo mbele yako. Hivyo huna budi kupiga mbio..sawasawa na kile kitabu cha Waebrania 12:1

Waebrania 12:1”Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”.

Soma pia Wafilipi 1:30, Wafilipi 1:27, na 1Wakorintho 9:24.

Lakini kama umejiona upo uwandani peke yako, basi kuna jambo la lingine Mungu anataka kusema nawe. Na hilo huenda ni jambo la tahadhari.

Na tahadhari yenyewe ni kama ile ya Kaini.

Wakati Kaini alipotaka kumwua Habili, alimtenga na kumpeleka uwandani. Na hiyo ni kanuni ya adui anapotaka kumdhuru mtu, anampeleka kwanza uwandani, mahali ambapo hapana watu, wala msaada wa kitu chochote..

Hivyo unapojiona upo uwandani/uwanjani peke yako, au upo na mtu mmoja, basi fahamu kuwa adui anatafuta kukuharibu au kuharibu mambo yako ya kiroho na kimwili.

Mwanzo 4:8 “Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani].
Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye, akamwua”.

Kwahiyo uotapo ndoto hiyo, kama hujaokoka zingatia kuokoka, na pia kama una wokovu usio thabiti (maana yake wewe ni vuguvugu) basi zingatia kuwa moto, ili adui asipate nafasi ya kukumaiza.

Lakini kama tayari upo dhani ya wokovu ulio thabiti, basi zingatia Maombi, omba maombi ya kuharibu hila zote na njama za adui, na kutakuwa shwari.
Bwana akubariki.

Tafadhalishea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

Kuota unasubiriwa mahali fulani uhutubie, halafu unachelewa.

Kuota mbwa kunamaanisha nini?

UZAO WA NYOKA.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments