Ni msiba gani unazungumziwa katika 1Petro 4:12?.

Ni msiba gani unazungumziwa katika 1Petro 4:12?.

Jibu: Turejee…

1Petro 4:12 “Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho”.

Neno “Msiba” kama linavyozungumziwa hapo halimaanishi ule Msiba wa mtu kufa. La! Bali neno hilo limetumika hapo kuwakilisha “jaribu zito”.

Kama tu lile lililompata yule mwanamke aliyetokwa na damu mda wa miaka 12.

Marko 5:27 “aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake;

28 maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.

29 Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule…………………

33 Na yule mwanamke akaingiwa na hofu na kutetemeka, akijua lililompata, akaja akamwangukia, akamweleza kweli yote.

34 Akamwambia, Binti, imani yako imekuponya, enenda zako kwa amani, uwe mzima, usiwe na msiba wako tena”

Hivyo tukirejea andiko hilo la 1Petro 4:12 msiba unaozungumziwa hapo “Ni jaribu zito”.

Kwahiyo kwa kiswahili kingine mstari huo unaweza kusomeka hivi…

“Wapenzi, msione kuwa ni ajabu lile jaribu zito lililo kati yenu, linalowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho”

Na msiba huo (au jaribu hilo)…Ni “Kuteswa kwaajili ya Kristo”…tunalithibitisha hilo katika mstari unaofuata wa 13.

1 Petro 4:13 “Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

14 Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia”.

Soma pia 1Wathesalonike 3:7 unataja msiba wa dhiki katika Kristo.

Na hata leo wote watakaotaka kuishi maisha ya kumpendeza MUNGU na utauwa, watakutana na misiba ya Kuudhiwa kwaajili ya imani.

2 Timotheo 3:12 “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa”.

Lakini ukiishi maisha ya kuupenda ulimwengu, basi ulimwengu nao utakupenda kwasababu ulimwengu unawapenda walio wake.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

PIGO LA KUFA KWA WAZALIWA WA KWANZA

NYWELE ZAKO ZIKUFUNDISHE, SAUTI YA MUNGU.

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

MTAKENI BWANA NA NGUVU ZAKE.

HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments