Kuwanda ni kufanya nini?

Kuwanda ni kufanya nini?

Jibu: Turejee..

Waamuzi 3:17 “Kisha akamsongezea Egloni, mfalme wa Moabu, hiyo tunu; basi Egloni alikuwa ni mtu AYELIWANDA sana”.

Kuwanda ni kiswahili kingine cha “kunenepa sana”.. Hivyo mtu aliyewanda maana yake ni “mtu aliyenenepa sana”.

Hivyo mstari huo wa Waamuzi 3:17 unaweza kueleweka hivi…

Waamuzi 3:17 “Kisha akamsongezea Egloni, mfalme wa Moabu, hiyo tunu; basi Egloni alikuwa ni mtu ALIYENENEPA sana”.

Neno hilo pia tunaweza kulisoma katika Yeremia 50:11 na katika habari za Yeshuruni katika Kumbukumbu 32:15. 

Kwa habari ndefu kuhusiana na Yeshuruni basi fungua hapa 》》》Yeshuruni ni nani katika biblia?

Je wewe kiroho umewanda/nenepa katika nini?..katika maovu au katika haki?…

Ni hatari kubwa KUWANDA katika mabaya…

Yeremia 5:28 “WAMEWANDA sana, wang’aa; naam, wamepita kiasi KWA MATENDO MAOVU; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.

29 Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema BWANA; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii?”

Je unaye Roho Mtakatifu?. Kumbuka Roho Mtakatifu ndiye muhuri wa MUNGU (Waefeso 4:30).

Bwana YESU anarudi (Maran atha).

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments