Aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye maana yake nini?.

Aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye maana yake nini?.

Swali: Neno la Mungu limemaanisha nini kusema aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye? (1Wakorintho 6:17).


Jibu: Turejee…

1 Wakorintho 6:17 “Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye”.

Maana ya kuwa roho moja na Bwana ni kama maandiko yafuatayo yanavyoeleza..

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema Njoo!…..”.

Hapa anasema Roho (yaani wa Roho wa Mungu) na bibi-arusi (yaani kanisa la Mungu)…Wasema Njoo!!…

Maana yake hawa wawili (Roho pamoja na bibi arusi) wote wanatoa Kauli moja!.. ya Njoo!..

Maana yake Bibi arusi akisema ni Roho wa Mungu kasema na Roho wa Mungu akisema ni  Bibi arusi kasema…kwanini?…kwasababu wameungwa pamoja.

Ndio sababu Bwana YESU alisema, tukiwapokea waliotumwa na yeye, tumempokea yeye, na tukiwakataa waliotumwa na yeye, tumemkataa yeye kwasababu wameungwa na yeye.

Mathayo 10:40 “Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma”.

Je umemwamini Bwana YESU?. Je unasubiri Bwana YESU mwenyewe akutokee ndio uamini?..

Kama ndicho unachosubiri basi upo hatarini, kwasababu YESU yupo anafanya kazi ndani ya watu wake, mtumishi wa MUNGU wa kweli kukujia na kukupa habari za uzima wa milele, tayari YESU ameshakutokea kwasababu maneno akuambiayo si yake bali ya Roho wa Mungu.

Na anapokuita uingie kwenye imani/wokovu si yeye bali ni Roho wa MUNGU ndani yake..

Ufunuo 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

VIASHIRIA VINGINE VYA ROHO MTAKATIFU KUWEPO NDANI YAKO.

NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?

Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?

NDOA TAKATIFU NI MKE MMOJA/MUME MMOJA.

Biblia imemaanisha nini iliposema “hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu”

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments