Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

Vita vya kiroho, na mwamini Mpya.

SEHEMU YA KWANZA: KUELEWA VITA VYA KIROHO

1.1 Vita vya Kiroho ni Nini?

Vita vya kiroho ni mapambano yasiyoonekana kwa macho ya kawaida, yanayofanyika katika ulimwengu wa roho kati ya ufalme wa Mungu na ufalme wa giza (Shetani na mapepo yake).

Ingawa hayaonekani, lakini vita vyao ni vibaya zaidi ya vile vinavyoonekana, kwani vinamuathiri mwanadamu kotekote, mwilini lakini pia rohoni katika mawazo yetu, hisia, tabia, ndoa, huduma, na hata afya.

Biblia inasema:

Waefeso 6:12

Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho

Mfano:

Mtu anayeokoka anaweza ghafla kuanza kupata majaribu makubwa ya kuudhiwa na watenda dhambi, jambo ambalo huko nyuma hakuwahi kuliona, mpaka anawaza kwamba maisha wa wokovu ni magumu. Hili ni shambulio la kiroho, linalolenga kumrudisha nyuma kiroho.

1.2 Kwa Nini Kuna Mapambano?

Ulipompokea Yesu, uliingia katika Ufalme wa Mungu. Na moja kwa moja ulifanyija adui wa Shetani.

Shetani alikupoteza na sasa anafanya kila juhudi kukurudisha, kukuzuia usikue kiroho, au kukushawishi uishi maisha yasiyo ya ushindi.

“Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.” (Wakolosai 1:13)

 SEHEMU YA PILI: KUMFAHAMU ADUI

2.1 Shetani ni Nani?

Maandiko yanatuambia Shetani alikuwa malaika aliyeasi (Isaya 14:12–15).

Anaendesha vita kwa kutumia uongo, hofu, mashaka, tamaa, magonjwa, migawanyiko, na kushambulia akili zetu.

2.2 Mbinu za Shetani:

Uongo – Anapandikiza mawazo kama: “Hujasamehewa” au “Mungu hajasikia maombi yako.”

Vishawishi – Hutumia tamaa za mwili, pesa, au kiburi kukushawishi.

Kuchosha kiroho – Anakufanya uchoke au kupoteza hamu ya kusoma Biblia au kuomba.

Kuvuruga mahusiano – Kupitia fitina, chuki, au hasira isiyoisha.

“Yeye ni mwongo na baba wa huo.” (Yohana 8:44)

🛡️ SEHEMU YA TATU: SILAHA ZA MUNGU

Waefeso 6:10–18 inatupa silaha saba za kiroho za kujilinda na kushambulia nguvu za giza:

3.1 Kweli kiunoni.

Kuwa na ujuzi wa kweli ya Neno la Mungu na kuiishi.

Hii inasaidia kutambua uongo wa Shetani.

Mfano: Unapofikiri “Mungu hanipendi,” Neno la Mungu linasema “Hakika amekupenda kwa upendo wa milele.” (Yeremia 31:3)

3.2 Dirii ya Haki

Maisha ya uadilifu na kutokubaliana na dhambi.

Haki hii inatoka kwa Yesu, sio kwa matendo yako.

“Yeye asiyemjua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.” (2 Wakorintho 5:21)

3.3 Viatu vya Injili ya Amani (utayari miguuni)

Kuwa tayari kueneza habari njema na kuishi kwa amani.

Mtu aliye tayari kushuhudia haogopi mapambano.

3.4 Ngao ya Imani

Imani huuzima mishale ya hofu, mashaka, na huzuni.

Unaposema, “Mungu atanitetea,” hata wakati hali ni ngumu, hiyo ni imani.

3.5 Chapeo ya Wokovu

Linda mawazo yako kwa kufikiri mambo yanayohusiana na wokovu wako.

Kukumbuka kwamba umeokolewa hukufanya usiyumbishwe na hila za adui.

3.6 Upanga wa Roho (Neno la Mungu)

Neno la Mungu ni silaha ya kushambulia.

Yesu alilitumia aliposhambuliwa na Shetani (Mathayo 4:1–11).

3.7 Maombi

Maombi ni silaha ya nguvu inayoweza kubadilisha hali yoyote.

Omba kwa ajili yako, familia yako, kanisa, na hata waliopotea.

Waefeso 6:18

[18]kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;

🧭 SEHEMU YA NNE: MBINU ZA USHINDI KILA SIKU

Soma Biblia kila siku – Neno la Mungu hukujenga kiroho.

Omba kila siku – Ushindi unapatikana kwa kusali daima.

Kataa dhambi kimaamuzi – Usingojee hisia, fanya uamuzi wa kiroho.

Tembea na Wakristo wengine – Ushirika hukupa nguvu.

Fanya ibada (Sifu na abudu) – Hukuza uwepo wa Mungu na huvunja vifungo vya giza.

Tubu haraka unapokosea – Usimpe shetani nafasi ya kukushitaki.

⚠️ SEHEMU YA TANO: MAMBO YA KUZINGATIA

5.1 Vita vya Kiroho Sio:

Kila shida ni mapepo – Baadhi ya mambo ni matokeo ya maamuzi au mazingira. Hivyo ni wajibu kuchunguza chanzo cha tatizo ni je Adui kweli au!

Kukemea tu– Mamlaka ya kiroho hutegemea maisha ya utii kwa Kristo. Utiifu wako

Kuwa na hofu – Kwamba tuigope, au tuishi kwa mashaka, kana kwamba tuwezekeze nguvu zetu zote kupamba a nayo. Hapana Tuna mamlaka kupitia Yesu.

“Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge, na kushinda nguvu zote za adui; wala hakuna kitakachowadhuru.” (Luka 10:19)

💬 SEHEMU YA SITA: MANENO YA KUHIMIZA

Ukiwa ndani ya Kristo, huna sababu ya kuogopa. Mapambano yapo, lakini ushindi ni wako kupitia Yesu Kristo.

“Katika mambo haya yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” (Warumi 8:37)

📖 MISTARI YA KUKARIRI

Waefeso 6:11 – “Vaeni silaha zote za Mungu…”

Yakobo 4:7 – “Mtiini Mungu, mpingeni ibilisi naye atawakimbia.”

2 Wakorintho 10:4 – “Silaha za vita vyetu si za mwili…”

1 Petro 5:8 – “Muwe na kiasi na kukesha… ibilisi yenu… hutafuta mtu wa kummeza.”

Masomo ya ziada kukusaidia kuvishinda vya kiroho

NGUVU YA “KUKATAA” UNAPOPAMBANA VITA VYA KIROHO

Maana ya Mhubiri 9:18 Hekima ndiyo bora kupita silaha za vita;

JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA ni mtu wa vita,  BWANA ndilo jina lake.(Kutoka 15:3)

Mishale ya moto ya mwovu inayozungumziwa kwenye Waefeso 6:16 ni ipi?

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

Print this post

About the author

Devis administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments