Siku moja nilikuwa nakatiza eneo fulani la biashara ambalo limechangamka sana, Ni eneo ambalo watu wengi wanapishana..ghafla kwa mbele nikamwona kijana mmoja ameinama, baada ya muda kidogo akachuchumaa, na mara akaanza kutapika matapishi mengi sana.. Uso wake ulionekana kuumwa, hivyo moja kwa moja nilipomwangalia moyoni mwangu, niliguswa sana na ile hali aliyokuwa anapitia..
Kikawaida zipo hali ambazo ukiumwa Unaweza kuzivumilika mpaka ufike mahali fulani pa matibabu..lakini kuumwa mpaka kutapika Hakuzuiliki, na kama ulishawahi kutapika unaelewa nguvu inayotumika, hali unayoisikia wakati huo.. ni kama nusu ya kufa..
Sasa sisi ndivyo tunavyomfanya Mungu, ajisikie muda wote tunapokuwa Na aina ya mwenendo wa uvuguvugu maishani mwetu, .alisema hivi;
Ufunuo wa Yohana 3:15-19
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. [16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. [17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. [18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. [19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
[16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Uvuguvugu ni ile hali ya kuwa mtu wa kidini na sio wa kiroho, unahudhuria ibada lakini mabadiliko huna, unavaa vizuri kanisani lakini ukiwa nje unavaa nguo zisizo na adabu, unaimba kwaya, lakini wakati huo huo unasikiliza nyimbo za kidunia, ni mtumishi mzuri wa kanisani lakini bado unaishi na mume wa mtu..
Maisha ya uvuguvugu, yanamtesa Kristo isivyo kawaida..Ikiwa wewe hupendi kutapika- tapika Kwanini wewe umfanye Mungu kuwa na hali hiyo?
Ukristo ni mwendelezo sio tukio…eti mimi nimeshamkiri Yesu kwa Kinywa..inatosha nimeokoka, hapana…bali ni ukuaji wa kiroho.. ni lazima uonyeshe ukuaji…kitu chochote kilicho hai kinakua…lakini kuwa mtu yule yule kila siku wewe ni vuguvugu.
Kanisa La Laodikia, lilikuwa na sifa ya kujiona ni tajiri Kisa Lina vyombo vizuri vya miziki, lina Makongamano makubwa ya nje, lina mwonekano wa kuvutia, lina umaarufu, Lakini Yesu aliliona si la kiroho hata kidogo..Linamheshimu Mungu kwa nje tu, lakini ndani limepoa zaidi ya barafu..
Hizi ni nyakati ambazo watu wengi wanazisahau ibada za kweli, wanatafuta fedha na Midundo inayovutia masikio ya watu lakini hawajali ujumbe wa rohoni au ‘uzuri Wa utakatifu’.
Na watu ambao wakiwaona wengine wamesimama kikamilifu mbele za Mungu wanawaita “walokole” …
Embu tubu, rafiki…uzuri wako, mwonekano wako, Sifa zako, udunia wako, havina ushirika na Kristo, hizo status zisizo na staha na elimu, unampostia nani mitandaoni? Hiyo mitandao ya kizinzi unayoitembelea kila siku, na kujichua unakoendelea nako kwa siri na wakati huo huo unasema umeokoka, nini unakiunda kama sio kumfanya Bwana atapike?…maanisha kumpokea Kristo. Simama katika imani, ili umwone Mungu wa kweli na sio sanamu.
Kumbuka hizi ni nyakati za kusimama kikamilifu, kwasababu mwisho umekaribia..Unyakuo Ukipita watakaokwenda na Bwana ni walio moto tu, na sio vuguvugu.
Kutubu ni kugeuka…Geuka tu leo kwa kumaanisha na Bwana atakusamehe kabisa na kuanza na wewe..Ikiwa hujaokoka na upo tayari leo kufanya hivyo…Basi wasiliana nasi kwa mwongozo wa sala ya Toba..
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?
Print this post
Mtambo kwenye biblia ni neno linalomaanisha aidha kifaa kinachonasa kitu, au kinachorahisisha kazi Fulani.
Kwamfano tukisoma
Ayubu 18:9
[9]Tanzi litamshika kisigino chake, Na mtambo utamgwia.
Hapo ni Bildadi rafiki yake Ayubu anaeleza hatma ya mtu mwovu, anasema ni sawa na mtu atembeaye katika njia ya mitego, na ghafla hunaswa asiweze kunasuka ndio mtu mwovu katika njia zake mbaya hukumbwa na hayo.
Anasema mtambo utamgwia, maana yake kitu kinasacho Kitamkamata.
Neno hilo pia utalisoma…kwenye mistari ya juu yake..Bildadi anasema..
Ayubu 18:2
[2]Je! Hata lini utayategea maneno mitambo? Fikiri, kisha baadaye tutanena.
Akitumia lugha ya picha…
akimaanisha hata lini utayanasa maneno yako? (yaani utaacha kuongea?).
Lakini sehemu nyingine Inayolitaja Neno hili Ni..
2 Mambo ya Nyakati 26:14-15
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo. [15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo.
[15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
Inazungumzia nguvu za kijeshi alizokuwa nazo mfalme Uzia, hata kufikia kubuni mitambo mikubwa ya kivita.. ya kufyatulia silaha kwa maadui zake.
Je umeokoka?
Kumbuka saa Tulizopo ni za majeruhi, siku yoyote wakati wowote Kristo anarudi jiulize umejiandaaje ndugu?. Unyakuo wa kanisa ukipita leo utakuwa wapi mpendwa…
Jitathmini maisha yako? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote na mambo yake halafu upate Hasara ya nafsi yako. Tubu mgeukie Kristo uoshwe dhambi zako, upokee uzima wa milele.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo.. basi fungua hapa kwa mwongozo Wa Sala ya Toba.. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
WhatsApp
Haya ni mafundisho maalumu kwa viongozi aidha wachungaji, au wasimamizi ndani ya kanisa..Maadamu una kundi la watu aidha 2-3 au zaidi la kuwasimamia, basi mafunzo haya yatakusaidia sana.
Kutoka 32:9-10
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu [10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
[10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
Mungu alipomuita Musa kwenda kuwaokoa watu wake, alijua asili ya hao watu watakuwa ni wa namna gani. Pengine Musa alidhani anawaokoa watu ambao ni wema sana, watulivu, na wapole.
Lakini mambo hayakuwa kama hivyo, licha ya kuona miujiza mikubwa namna ile, bahari kupasuka, mana kushuka Mbinguni, miamba kutoa maji, nguzo ya moto kuwaongoza usiku kila siku…
Bado walitengeneza sanamu za ndama na kusema hii ndio miungu yetu iliyotutoa Misri tuiabudu..walinung’unika, walimsengenya kiongozi wao, waliasi na kujiundia Makundi..Ni watu ambao walikuwa ni wagumu kuongoza, wazito kutii na wapesi kulalamika.
Ni vema kujua kuwa kila kiongozi wa kweli kuna siku atapitia kama Musa alivyopitia..
Ikifikia hatua hii wengi wanasema kama utumishi ndio huu ni heri niache, kama naonyesha fadhila zote hizi kinyume chake narudishiwa masengenyo na uasi, ni heri niache…
Ukifikiria hivyo bado hujawa kiongozi, Mungu alijua asili yao kwamba ni watu wenye shingo ngumu..alijua Yuda ni msaliti lakini bado alimpatia mwanae, amchunge.
Hao hao bado aliwaokoa na akataka wachungwe..
Shingo ngumu ni mtu wa namna gani?. Ni mtu anayefananishwa na ng’ombe ambaye hataki kufungwa Nira na Bwana wake…shingo inakuwa ngumu kuvishwa nira..
Hii ni aina ya watu ambao Hawana utii, hawachungiki, hata waone miujiza mikubwa namna Gani, hata wasaidiweje, si rahisi kuacha tabia zao za usengenyaji, wizi, uasi. Kiburi N.k.
Lakini bado Mungu anawaacha chini ya mchungaji waangaliwe..
Musa alikutana na waabudu sanamu, wanung’unikaji, Na wasahaulifu wa fadhili za Mungu…
Lakini alifanyaje?
Hata pale ambapo Mungu alitaka kuwaangamiza Musa aliwaombea. Alisimama kufanya upatanisho kwa ajili yao.
Ni ujumbe gani tunapewa?
Kiongozi wa kweli badala ya kughahiri kumchunga kondoo wake humwombea kwa bidii ili Bwana amponye asipotee kabisa kwenye dhambi.
Kiongozi wa kweli, huwa tayari hata kupoteza maisha yake kwa kondoo wake.. Musa alisema..
Kutoka 32: 32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.
Uongozi sahihi sio Kuongoza Watu wakamilifu, lakini kuongozo Watu dhaifu Kwa Mungu mkamilifu.
Uongozi Sahihi huweka katika uwiano sahihi “neema na kweli”
Ni vema kufahamu pia si kila wakati Musa alikuwa anasimama kuwatetea Waovu, hapana wakati mwingine aliruhusu upanga wa Mungu upite, Ili dhambi iogopwe…utakumbuka wakati ule walipotengeneza Sanamu ya ndama, na hasira Ya ki-Mungu ilimvaa Musa, ndipo Akazivunja zile mbao mbili, kisha akawaita watu walio upande wa Bwana wamfuate, Na wale waliosalia waliadhibiwa vikali kwa mauti.
Dhambi iwapo kanisani, haipaswi kuvumiliwa..Kutoa adhabu na wakati mwingine kuwaondoa wale wabaya ndani ya kundi ili lisiendelee kuharibiwa..
Lakini katika yote wewe kama kiongozi, huna budi kujifunza Uvumilivu, kuwaombea kondoo wako, na kuwa mpole, lakini pia kushughulika na dhambi Vikali katika nyumba ya Bwana.
Lakini kumbuka ijapokuwa Ni kazi, yenye mapito mengi ya masumbufu na maumivu Lakini thawabu yake na faida yake haifananishwi na gharama ulizoingia.. Hivyo penda kuchunga watu wa Mungu…Ndio heshima ya juu ya upendo kwa Mungu wako.
Mithali 14:4
[4]Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe; Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.
MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.
Jina la Mwokozi YESU, Ngome Imara libarikiwe (Mithali 18:10).
Hatujaitwa kujipenda tu wenyewe, au kuwapenda wale wenye imani moja na sisi au watu wa familia zetu tu!, bali tumeitwa kuwapenda hata watu walio mbali na imani zetu, tamaduni zetu, na hata itikadi zetu (hao ndio Biblia imewatafsiri kama majirani zetu).
Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? 47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Katika Agano la kale ilizoeleka kufahamika kuwa Jirani wa mtu ni Yule wa jamii moja naye, itikadi moja naye, na hata Taifa moja naye, jambo lililowafanya wana wa Israeli wasiwe na ushirika na mtu mwingine yoyote kutoka katika Taifa lingine, na wala wasiwe na upendo na mtu wa Taifa lingine lolote na kuwaona wote maadui (Na kwa wakati huo hawakufanya kosa kwasababu hawakuujua ukweli wote wa Upendo wa Mungu).
Lakini alipokuja Bwana YESU, (mjumbe wa Agano jipya sawasawa na Waebrania 12:24) yeye alitukamilishia kweli yote..na kuwafundisha kuwa majirani zao si tu watu wa Taifa lao, au wanaowajua…
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? 47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
Jambo hili Bwana Yesu aliliweka vizuri tena, wakati alipojiwa na yule mwanasheria ambaye alitaka kujionyesha yeye ni mwenye haki (kwamba anawapenda majirani zake) pasipo kujua jirani yake ni nani,
Huyu alipokuja alimwuliza Bwana je! Jirani yangu ni nani?.. kuna jibu Bwana alilompa, tusome..
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje? 27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. 28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi. 29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani? 30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa. 31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando. 32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando. 33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia, 34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza. 35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa. 36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni YUPI ALIYEKUWA JIRANI YAKE yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi? 37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?
30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni YUPI ALIYEKUWA JIRANI YAKE yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?
37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Kufuatana na mfano huu.. ni wazi kuwa huyu Mwanasheria alijiona kuwa yeye hana upendo kabisa!… Kwasababu hapo Bwana alikuwa anaonyesha kuwa Kuhani na Mlawi ambao walikuwa ni wayahudi, walishindwa kumsaidia myahudi mwenzao, aliyeangukia katika mikono ya wanyang’anyi, na badala yake anakuja kusaidiwa na Msamaria (mtu asiye wa imani yao wala Taifa lao).
Maana yake Yule Msamaria kafanya Ujirani mwema kwa myahudi aliyeangukia kwenye mikono ya wanyang’anyi zaidi hata ya wayahudi wenyewe… Hiyo Ikifunua kuwa ujirani sio tu kwa mtu wa imani moja na wewe, au wa Taifa moja na wewe, au rangi moja na wewe.. hata mtu mwenye itikadi tofauti kabisa na zetu, huyo tumeamriwa tumpende na hata kumfadhili pale inapobidi.
Na ndicho Bwana YESU alichokuwa anajaribu kukipanda kwa wayahudi kwamba kama vile Mungu aliyemtakatifu anavyowanyeshea mvua yake wenye haki na wasio haki, na sisi pia hatuna budi kunyesha mvua zetu za upendo na Baraka kwa wanaofanana nasi na wasiofanana nasi, kama vile Mungu anavyowaangazia Jua lake waovu na wema, na sisi hatuna budi kuangaza fadhili zetu kwa watu wote (wenye haki na wasio haki), huo ndio ujirani mwema.
Lakini tukijifunga kwa imani zetu, jamii zetu, itikadi zetu na kuwadharau wengine wote na hata kutoonyesha upendo, basi tufahamu kuwa tumejifungia wenyewe fadhili za MUNGU.
Bwana Yesu atasaidie sana, kwasababu kwa nguvu zetu hatutaweza.. pale tunapoambiwa “tumpende adui”.. ni jambo zito sana… Lakini kwasababu yupo Roho Mtakatifu aliyewekwa kutusaidia udhaifu wetu, basi tutaweza na kushinda na zaidi ya kushinda..
Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.
Maran atha!a
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe.
Jenga utamaduni wa kusoma Biblia, siku za mwisho ibilisi anazidi kuwekeza nguvu nyingi kwa watu wasisome wala kulielewa Neno, badala yake wapende tu kusikiliza mahubiri au kufanyiwa maombezi, lakini si Kusoma.
Lakini ukweli ni kwamba tukitaka kuisikia sauti ya Mungu ya wazi kabisa, njia ni kusoma Neno, tukitaka kumwona Mungu suluhisho ni kusoma Neno, tukitaka kumwelewa Mungu katika viwango vingine jawabu ni kusoma Biblia, tukitaka kuishi maisha ya kumpendaza Mungu,ni kusoma tu maandiko. Usipuuzie kamwe kusoma maandiko.
Hebu tujifunze kwa Bwana YESU wakati ule alipokutana na Yule mwanasheria ni maneno gani alimwambia…
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE? 27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. 28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”.
26 Akamwambia, IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE?
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”.
Zingatia hayo maneno katika mstari wa 26, ….IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?
Najiuliza kwanini Bwana Yesu hakumpa jibu la moja kwa moja, lakini badala yake anamrudishia swali.. “IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?” maana yake kama angesema siju, ni wazi kabisa Bwana YESU asingempa jibu lolote, badala yake angemwambia akasome maandiko (akatafute katika maandiko)..Na leo hii wengi tunamwuliza sana Bwana maswali ambayo majibu yake yapo kwenye maandiko…..
Tukimwuliza Bwana swali ambalo jibu lake lipo katika biblia, anaweza kutujibu kama tu alivyomjibu huyu mwana sheria…. IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. WASOMAJE?
Hatuwezi kumlazimisha MUNGU azungumze kitu ambacho tayari alishakizungumza katika maandiko…tukimwuliza kitu ambacho tayari kipo ndani ya Biblia tunaweza tukapokea jibu kama hilo hilo tu… IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. TWASOMAJE?
Na kitu pekee anachohakikisha shetani tusikijue ni UWEZA WA MUNGU pamoja na UWEZA WA MUNGU katika hayo maandiko.. kwa namna gani?
Marko 12:24 “Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?”
Weka ratiba ya kujifunza Biblia mtu wa Mungu, usiishie tu kusikiliza mahubiri, usiishie tu kusikiliza maombi.. bali soma soma soma.. Wakati mwingine unaweza ukawa unapitia vipindi ambavyo hujui nini cha kufanya, huo ni wakati wa kusoma Biblia utapokea ni nini cha kufanya huo wakati..
Unaweza kupitia wakati ambapo hujui uombe nini, soma Biblia utapata nini cha kuombea n.k
Nabii Danieli alikuwa sana kimaarifa na hata kujua nini cha kuomba kwa kusoma maandiko na si tu kutegemea maono yake na njozi zake.
Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. 3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. 4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.
3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.
4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Na zingatia: Kusoma Biblia si tu kutafuta neno moja la siku na kutembea nalo hilo, acha hiyo desturi!. Neno la Siku liwe ni ufupisho wa kingi ulichokisoma.
Bwana atusaidie.
Kwanini biblia ni neno la Mungu?
Kitabu kifupi katika biblia ni kipi, na ujumbe wake ni upi?
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)
Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?
Mistari ya biblia kuhusu sadaka
Huu ni mfululizo wa mafunzo maalumu ya wazazi kwa watoto..
Ukiwa kama mzazi, Njia bora ya malezi, sio kumjali mtoto wako, kwa kila kitu sasa.. Hata kama ni haki yake kukipata, Usiwe mwepesi kumfanyia kila jambo leo hata kama una uwezo wa kumfanyia, Usimjali sasa, mjali kwa baadaye. Tumia nguvu hizo kumwekezea kwa baadaye lakini sasa shughulika naye kitabia, kinidhamu, ki-utu..Acha hiyo tabia ya kujali-jali utamuharibu mtoto.
Wengi wetu tunashindwa kujua, kuwa ni kanuni ya ki- Mungu mtoto aishi kama mtumwa, hata kama yeye ndio mrithi wa yote.
Wagalatia 4:1 Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote; 2 bali yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba
Mzazi mwenye Akili na maono bora kwa wanawe, haangalii mali zake anazitumiaje kwa mwanawe sasa, bali huangalia tabia gani anamjengea leo, ili kesho aweze simamia vema maisha yake, au mali zake.
Embu fikiria vema, yule Baba Tajiri aliyekuwa na wana wawili, ambao kwa siku nyingi waliishi na baba yao bila kuona faida ya utajiri wa baba yao. Mpaka siku moja mmojawao (yule mdogo) uzalendo ukamshinda, akamwambia baba yake nipe sehemu ya mali yangu inayoniangukia, hatimaye akapewa akaondoka, lakini maisha yalipo-mgeukia hali ikawa mbaya, mwishowe akazingatia kurudi kwa baba yake. Na baba yake akampokea akamfanyia karamu kubwa. Lakini yule mwana mwingine aliporudi mashambani, na kuona sherehe kubwa kwa ndugu yake, akachukizwa, ndipo akamwambia baba yake “Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, Lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;”
Tusome;
Luka 15:11-31
11 Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; 12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. 13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati. 14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. 15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. 16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. 17 Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia. 25 Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. 26 Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? 27 Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. 28 Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi. 29 AKAMJIBU BABA YAKE, AKASEMA, TAZAMA, MIMI NIMEKUTUMIKIA MIAKA MINGAPI HII, WALA SIJAKOSA AMRI YAKO WAKATI WO WOTE, LAKINI HUJANIPA MIMI MWANA-MBUZI, NIFANYE FURAHA NA RAFIKI ZANGU; 30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona. 31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.
Nataka uone sifa ya huyo baba, kwa wanawe, ijapokuwa alikuwa na mali, lakini hakutaka Watoto wake, waishi kwa mali zake, bali waishi kama watumwa wengine. Sio kwamba alikuwa anawatesa, Hapana, alikuwa anawatengeneza ili baadaye wakishajua maisha hasaa ni nini kivitendo, ndipo awaache huru, wapewe vyote na baba yao, wafurahie maisha wayapendayo.
Leo hii imekuwa kinyume chake, utaona mtu ndiye anayetumia nguvu zake, na mali zake, kumdekeza mtoto, kama yai, kumletea wafanyakazi ndani, wawapikie, wawafulie, wawapigie deki, na pasi, wenyewe wakae wakitazama muvi Netflix, na kucheza magemu, kwenye Ipad, na computa,
Akidhani anamlea mtoto, kumbe anamlea mwana-mpotevu. Mtoto akikosea tu, hawezi kuadhibiwa, mzazi anasema sitaki mtoto wangu ateseke kama mimi nilivyoteseka, kwani ni nani kakwambia mtoto akiadhibiwa ni lengo la kuteswa? Watoto hawafundishwi kufunga, hata kwa sehemu (nusu siku), au kupelekwa mikesha mara moja moja wajifunze kanuni za kiroho, wazazi wanasema hawa bado wadogo. Hivi ni kizazi gani tunakilea??
Si lazima kila siku ale mboga saba, si lazima umpe chakula anachokitaka yeye, siku nyingine fululiza ugali maharage, wiki mbili nyumbani, mwache alie, mpaka azoee..Mambo kama hayo unaweza kuona unamtesa mtoto, lakini ndio njia sahihi ya malezi..unamtengeneza mtu imara sio lege-lege.
Likizo inapofika, kuliko kumpeleka beach kwenye mabembea, na masherehe, mpeleke kijijini kwenu, aone mazingira ya asili, ale vyakula vya kule, atumie vyoo vya kule ambavyo sio vya kuflash, aende akakatie ng’ombe majani, aende na wachungaji machungani akae huko mpaka likizo iishe, ndipo arudi..
Lakini wewe mwenyewe huku nyuma unajua ni nini unafanya, ukimwandalia akiba, nzuri, ili baadaye atakapoelimika kiroho na kimwili, ukimpa vya kwako, au ukimdekeza atakavyo, ataweza kujisimamia mwenyewe, na kuwa mtu mkakamavu thabiti, na Jasiri, mwenye utu na kiongozi awezaye kuishi katika jamii, na kuwajali na walio wanyonge na wenye shida.
Hayo ndio malezi bora ya mtoto. Mfanye leo mtumwa ili kesho awe mfalme, lakini ukichagua kumfanya leo mfalme, jiandae kesho kuwa mtumwa mfano wa mwana- mpotevu.
Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee
NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?
MRUDI MWANAO NAYE ATAKUSTAREHESHA
NAFASI YAKO WEWE MAMA KWA MTOTO NA WAJUKUU WAKO NI IPI?.
JIBU: Tukiangalia mwanzo wa mstari huo, unasema..
Mithali 11:16 Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; Na watu wakali hushika mali siku zote.
Ukitazama tafsiri nyingine maana iliyonyooka zaidi ya mstari huo, unasema “mwanamke wa adabu huheshimwa daima, lakini watu wakali hushika tu mali”.
Yaani unalinganisha, sifa njema, na vitu vingi, akilinganisha mwanamke anayewekeza maisha yake katika tabia nzuri, matokeo yake heshima itakuwa kwake ambayo itadumu daima, lakini mtu mkali anayewekeza katika kujilimbikizia mali isivyo halali, akiwakandamiza wengine, akitumia ukali, akiwanyima mshahara wengine, ni kweli na yeye atapata matokeo yake ambayo ni mali nyingi tu. Lakini hana heshima yoyote nyuma yake. Haachi kitu chenye thamani kitakachoweza kuwa faida kwa wengine, hana la kuigwa, hana la kusifiwa isipokuwa, malalamiko, uchungu na machozi kwa wengine.
Hivyo andiko hilo linalinganisha sifa njema na mali. Ni heri ujijengee sifa njema ambayo hiyo itafuatwa na vizazi hata vya mbeleni, kama vile tuwaonavyo wanawake wacha Mungu kwenye maandiko, mfano wa Ana binti Fanueli, Mariamu, Sara, watu kama akina Ayubu, Danieli, Yusufu, ambao njia zao huigwa hata sasa, kuliko kuwa kama Nabali aliyetajirika lakini mpumbavu, hana chochote cha kuigwa na watu.
Ni heri maskini ahubiriye watu, na kuwaleta kwa Kristo, wanaacha dhambi, na kupokea Roho Mtakatifu, kuliko mtu yule ambaye kutwa nzima anachowaza ni kujiwekezea nafsi yake, kuiba, na kudhulumu, kutumia ukali kupata mali mambo ambayo yataishia hapa hapa tu duniani.
Mithali 22:1 Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.
Shalom.
Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’
Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,
SWALI: Tumekuwa tukisikia kuwa mtu akifa, huko aendako anakutana na mateso makali ya jehanamu. Sasa napenda kufahamu je ni roho ndio itakayoteketezwa au na miili pia?
JIBU: Maandiko yanatueleza siku ya mwisho ya hukumu, wafu wote watafufuliwa. (Iwe ni wema au waovu), wote watairudia miili yao ya asili yaliyokuwa nayo duniani.
Yohana 5:28
28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu
Ufunuo 20: 12-13
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake
Waliokufa katika Kristo (Watakatifu) watavikwa miili mipya ya utukufu, isiyoharibika (1Wakorintho 15:42-54) lakini waovu watakuwa na miili yao ya asili. Ambayo katika hiyo watahukumiwa na kutupwa katika lile ziwa la moto, lililo maalumu kwa mateso ya mtu milele.
Hivyo ni vizuri ifahamike, kuwa kitakachoteketezwa sio roho tu, bali na mwili pia, Bwana Yesu aliliweka hilo wazi katika maneno haya;
Mathayo10:28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Umeona hapo?.. Awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum. Kuonyesha kuwa mwili nao utashiriki mateso ya milele.
Tukishayajua hayo, tunapaswa tufanyaje?
Je! Umemwamini Bwana Yesu ndugu? Wokovu ni sasa, mgeukie akuponye, uwe salama, hata ukifa uwe na uhakika wa kuurithi uzima wa milele, Itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako? Fanya uamuzi wa busara.
Okoka, leo uponywe. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA
MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Swali: Maandiko yanasema katika Mathayo 5:42 kuwa tumpe kila atuombaye na kila atukopaye tusimpe kisogo?.. Je hata kama mtu ni mzembe na kila wakati anatumia vibaya vile ninavyompa, nina amri ya kumpa mara kwa mara kila atakaponiomba?
Jibu: Turejee hayo maandiko..
Mathayo 5:42 “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo”.
Haya ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo..ambayo anatufundisha umuhimu wa kutoa na kukopesha watu wote pasipo kuwa na vizuizi vingi, lakini swali ni je! Ni kila mtu anayekuja kutuomba tunapaswa tump kulingana na hilo andiko?
Jibu ni La!.. si kila mtu anayetaka kukopa tuweza kumpa, na si kila anayeomba tunapaswa tumpe!.. Kwasababu zifuatazo.
1. HUNA HIKO ANACHOKIOMBA.
Kama huna hiko anachokuomba, huwezi kumpa, kwasababu huwezi kumpa mtu kitu usichokuwa nacho au kilicho juu ya uwezo wako, kwamfano mtu anataka kukopa kwako milioni moja, na wewe huna hiko kiasi..hapo huwezi kufungwa na andiko hilo kwamba kila akuombaye unapaswa uumpe!
2. HAJAKIDHI VIGEZO VYA KUPEWA.
Vipo vigezo vya mtu kupewa kitu, kwamfano mtu anataka kukopa au kuomba pesa ya kwenda kununua pombe, au kwenda kufanya dhuluma au biashara haramu, au kwaajili ya kwenda kutoa sadaka kwa miungu hapo hata kama tunacho hiko kiasi, hatupaswi kumpa wala kumkopesha.
Hata Mungu wetu alituambia tumwombe naye atatupa
Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
Lakini ni huyo huyo Mungu wetu aliyetuambia tena kuwa, tukiomba nje ya mapenzi yake hatupati..
1Yohana 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia”.
Yakobo 4:3 “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Kwahiyo na sisi ni hivyo hivyo, ni lazima tuangalie anayekuja kuomba kama amekidhi vigezo.. wengine wanaomba kwaajili ya kwenda kufanya maasi, wengine uhalifu, wengine si makini, maana yake wana hali ya uzembe katika matumizi yao (hawa hawapaswi kurudia kupewa mara kwa mara mpaka watakapobadilika), wengine wanaomba kwa tamaa tu (mfano wa hao pia ni watoto wadogo) n.k
Kwahiyo tukirudi hapo katika hilo andiko Bwana Yesu alilosema kuwa “Kila akuombaye mpe”, tutakuwa tumeshaelewa kuwa si kutoa tu bila kufikiri wala kutafakari kwa kila mtu, bali ni kumpa kila akuombaye ambaye AMEKIDHI VIGEZO VYA KUPEWA!.
Kama mtu amekidhi vigezo vya kupewa nawe unacho hiko kitu, usimpe kisogo, kwasababu ni Mungu aliyemleta kwako huwenda ili amtengeneze na wewe pia upate thawabu, ukimpa kisogo mtu anayekuomba na ilihali unacho hicho kitu, ni dhambi!.. kwasababu uchoyo ni shina la dhambi.
Luka 12:15 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”.
Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?
Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)
USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?
Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”
Mtume Paulo, alipokamatwa kule Yerusalemu na kupelekwa mbele ya wafalme kuhukumiwa, tunaona ujasiri wake ulikuwa wa ajabu, badala atumie nafasi ile kujitetea, kimahakama, kinyume chake alitumia nafasi ile kuhubiri injili, kiasi cha kumfanya mfalme Agripa kushawishwa kwa muda mfupi kuiamini injili.. Ujasiri wa namna hiyo hakika, ni wa kuigwa sana.
Matendo 26:28
25 Lakini Paulo akasema, Sina wazimu, Ee Festo mtukufu, bali nanena maneno ya kweli na ya akili kamili. 26 Kwa maana mfalme anajua habari za mambo haya, nami naweza kusema naye kwa ujasiri, kwa sababu najua sana ya kuwa hapana neno moja katika hayo asilolijua; kwa maana jambo hilo halikutendeka pembeni. 27 Mfalme Agripa, je! Wawaamini manabii? Najua ya kuwa wawaamini. 28 AGRIPA AKAMWAMBIA PAULO, KWA MANENO MACHACHE WADHANI KUNIFANYA MIMI KUWA MKRISTO. 29 Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe kama mimi, isipokuwa vifungo hivi.
Lakini Tunaona jambo moja, huyu mfalme Agripa alichomwa sana na maneno ya mtume Paulo, alishawishwa ipasavyo na injili ile, lakini hakuwa tayari kugeuka moja kwa moja kwa Kristo, aliishia tu kushawishwa.. Ukweli ni kwamba mtu katika hatua hiyo bado hujaokolewa..
Ni sawa na leo hii, watu wengi wanapoisikia injili, ni kweli wanashawishwa, wanaiheshimu, wanaifurahia, wanachomwa mioyo yao, wengine wanaomboleza na kuhuzunika juu ya dhambi zao, lakini je! Wameikubali na kutii?
Utaona wataishia tu kusema, nimebarikiwa!, wataishia kusema Neno zuri linaonya!, wataishia kusema, Mungu nisaidie, nimeguswa leo, ndugu hiyo haimaanishi kuwa umeokoka, huna tofauti na Agripa.
Watu walioshawishwa kwelikweli, waliochomwa mioyo, ni lazima utaona kuna kitu cha ziada watafanya watauliza “Tufanyeje ndugu zetu?”
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Umeona?, hawakuishia tu kusema “asante Petro kwa Neno” hawakuishia kusema “ubarikiwe mtumishi” ..“Umetujenga mchungaji”. Walisema, tutendeje ndugu zetu?..Tuchukue hatua gani?
Utaona Wakabatizwa, wote siku ileile, wakajazwa Roho, Wakadumu katika fundisho la mitume, kila siku. Ndio hao walioisambaza injili ulimwenguni kote.
Leo ndio tunahitaji kuona Kundi la watu wa namna hii, ambao wanachukua hatua ya kumpokea Yesu kikamilifu na kumfuata kwa mioyo yao yote, kimatendo. Na sio kama akina Agripa, ambaye hakuwa na matunda ya kuitii injili.
Saa ya wokovu ni sasa, usiseme kesho nitaokoka, hakuna wokovu wa kesho, acha kujidanganya, bali ni leo. Aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi usifurahie mafundisho, usifurahie miguso ya ki-mahubiri swali ni je umeokoka? Kristo leo akirudi utaenda naye?
Na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
WOKOVU NI SASA