Neno hili linatuonyesha kuwa kumbe licha ya mtu kuangaziwa nuru ya Mungu, yaani kupewa neema ya kumjua na kumwamini Yesu Kristo ambaye ndio Nuru yenyewe (Yohana 1:4-5), bado anaweza kuonja kitu kingine ndani yake, licha ya kuonja vipawa vya kimbinguni na kufanywa mshirika wa Roho Mtakatifu yaani kwa kuvuviwa karama za Roho kama vile Lugha, unabii, miujiza, utume, uchungaji, ualimu, uinjilisti n.k. mambo ambayo hapo kabla hayakuonekana kati ya watakatifu au kama yalionekana basi ni kwa sehemu ndogo sana, bado anaweza kuonja kitu kingine cha tofauti kabisa,.licha pia ya mtu kuliona Neno zuri la Mungu kama andiko hilo linavyotuambia, yaani Injili ya Yesu Kristo Bwana wetu ambayo kwa hiyo manabii wengi na wenye haki walitamani kuisikia lakini hawakupata neema kama sisi tunavyojua sasa, lakini bado lipo jambo lingine ambalo tunaambiwa mtu anaweza kulionja kwa wakati huu …Na jambo lenyewe KUONJA NGUVU ZA ZAMANI ZIJAZO..