Usisubiri mwisho wako ufike, kwasababu wengi siku ile watatazamia wafike sehemu mpya, wengine watafikiri baada ya kufa kutakuwa hakuna maisha, lakini watajikuta wamerudi pale pale kwa mwokozi wao waliomkimbia mwanzo, leo wewe usiwe mmoja wao. Kristo yupo hai , na anawapokea wenye dhambi na wote wanaomkimbilia, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kutenga dakika chache kutubu dhambi zako zote kwa kudhamiria kuziacha sasa angali muda upo..unadhamiria kwa vitendo kuacha ulevi, sigara, pornography, utukanaji, usengenyaji, wizi n.k, na ndipo Mungu atakapokupa NGUVU ya kuvishinda ……hapo ulipo yeye yupo haihitaji mtu akuombee, kwa Imani amini yupo hapo anakusikia..Mwambie akuoshe dhambi zako zote na yeye ni mwaminifu na si mwongo atakupokea na kukufanya mpya na kukusamehe..