Unaona?, Anajua hata unalokwenda kumwomba wiki ijayo,,, ashindweje kujua taabu au shida unayopitia sasa hivi, anajua unaumwa na unateseka katika magonjwa na unahitaji kupona, analijua hilo, anafahamu una haja na kuwa na maisha mazuri anajua, anajua unahitaji kuolewa na umri umeshakwenda, anajua unahitaji pesa uvae nguo nzuri upendeze, anajua unahitaji uishi katika nyumba yako mwenyewe uwe na uhuru wako binafsi, anajua kwasasa ungependa uwe na usafiri wako,,..anafahamu hayo yote…Lakini unajiuliza inakuwaje sasa?