WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

WALIO NA HEKIMA NDIO WATAKAOELEWA.

Danieli 12:8 “Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?

9 Akasema, Enenda zako, Danieli; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa mwisho.

10 Wengi watajitakasa, na kujifanya weupe, na kusafika; bali wabaya watatenda mabaya; wala hataelewa mtu mbaya awaye yote; bali wao walio na hekima ndio watakaoelewa.”

Licha ya Danieli kuonyeshwa maono mengi sana yahusuyo siku zake na siku za mwisho ukisoma sura zote za nyuma utaona hayo lakini bado mwishoni kabisa utaona Danieli anamuuliza Bwana “mwisho wa mambo haya utakuwaje?”….Alitamani kuona jinsi mwisho utakavyomalizikia…Ni jambo ambalo sio mitume tu wa Bwana walitamani kufahamu ukisoma (Mathayo 24), bali pia hata sisi wa leo tunatamani kujua mwisho wa mambo yote utakuwaje… Lakini Mungu hakumfunulia Danieli kwasababu moja tu, na sababu yenyewe ni kuwa Danieli hakuwa anaishi katika siku za mwisho, Na ndio maana Maneno yale yalifungwa hadi wakati wa siku hizo zitakapofika.

Lakini kwa bahati mbaya Danieli anaambiwa pia watakaofahamu sio wote…na kama sio wote basi lile Neno la ghafla na kama mwivi usiku wa manane litawakumba watu wengi sana, na watu hao Danieli anaambiwa ni wale waovu na watenda mabaya ndio wakati huo ukifika hawatelewa chochote, lakini wenye hekima Danieli anaambiwa watajua na kuelewa hivyo siku hiyo haitawajilia kwa ghafla kama mwivi. Watu wengi wanadhani siku ile watu watajiliwa kama mwivi usiku, ndugu nataka nikuambie hilo halitakuwa kwa watakatifu ukisoma.

1Thesalonike 5:1 inasema “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.

4 BALI NINYI, NDUGU, HAMMO GIZANI, HATA SIKU ILE IWAPATE KAMA MWIVI. 5 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.

6 Basi tusilale usingizi kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.

7 Maana walalao usingizi hulala usiku, pia na walewao hulewa usiku.

8 Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, hali tukijivika kifuani imani na upendo, na chapeo yetu iwe tumaini la wokovu”.

Unaona biblia inatuambia sisi wana wa Nuru, wenye hekima hatupo gizani, hadi siku ile itujie kama mwivi..Ndugu hizi ni nyakati ambazo Mungu hamlazimishi mtu kuchagua njia yoyote ya kuiendea katika maisha yake, Ukiwa upo nje ya wokovu, au unasuasua mguu mmoja ndani au mguu mmoja nje, fahamu kuwa utatapikwa kulingana na maandiko (Ufunuo 3:16) na Bwana atakuwa hana mpango na wewe…Na kama hana mpango na wewe basi usitazamie kuwa utafahamu chochote kinachoendelea sasa hivi, au kitakachotokea mbeleni juu ya mpango wake wa wokovu wa siku hizi za mwisho..


Na wala hutakaa ufahamu ni kwa kiasi gani tunaishi katika majira ya kumalizia..siku ile utakapoona mambo yamebadilika tu ghafla, Ukiona kuwa dunia haina miaka mingine mitatu na nusu ya kuishi mbeleni, ndipo utakapolia kilio cha kusaga meno.. siku hizo utabakia kusema mbona sikutazamia kama ingekuwa haraka hivi, mbona sasahivi ni wakati wa amani na utulivu dunia ipo kwenye ustaarabu mzuri kuliko hata kipindi cha vita ya kwanza ya dunia imekuwaje dunia inakwenda kuisha kiajabu ajabu tu..sasa wakati unafikiria hivyo wenzako wakati huo watakuwa wanang’aa kama jua mbinguni wewe umebaki hapa unangojea mauti.

Ndugu hatua za UNYAKUO zimeshaanza kama hulijui hilo, tafuta kulijua hilo au ikiwa utataka kufahamu tutumie ujumbe inbox nikutumie somo linalohusu unyakuo uone ni jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari.
Huu sio muda tena wa kutanga tanga na ulimwengu, huu sio muda tena wa kulala usingizi wa kiroho bali ni kumtafuta Bwana kwa bidii ili na sisi atuingize katika mpango wake wa wokovu aliokusudia kwetu, kama wenye hekima wengine.

Hivyo Ikiwa bado hujafanya uamuzi sahihi yaani hujatubu dhambi zako fanya hivyo sasa kwa kumaanisha kisha tafuta mahali ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa Jina la YESU KRISTO, Upate ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38) na Bwana atakupa Roho Mtakatifu kukuongoza katika kweli yote siku hizi za mwisho. Au kama unalishaamini na unasuasua rudi upande wa Bwana kwa moyo wote, kabla hazijakaribia siku utakazosema sina furaha katika hizo (Mhubiri 12). Huu ni wakati wajioni giza linakaribia kuingia ulimwenguni kote, utafika wakati watu wataitamani Nuru wataikosa.

Bwana akubariki sana,

Mwana-kondoo amechinjwa kwa ajili yetu.
Maran atha!


Mada zinazoendana:

DANIELI: Mlango wa 12.

UNYAKUO.

AMIN NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA


Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Everlyne
Everlyne
1 year ago

Amen asante kwa mandiko

Erick G Otieno
Erick G Otieno
1 year ago

Shalom! Mungu ni mwema sana.
Asante sana na ubarikiwe kwa somo zuri.
Naomba msaada wa kupata somo la UNYAKUO. kama ulivyo elezea kwenye chapisho lako, nimelinukuu hapo chini.

Ndugu hatua za UNYAKUO zimeshaanza kama hulijui hilo, tafuta kulijua hilo au ikiwa utataka kufahamu tutumie ujumbe inbox nikutumie somo linalohusu unyakuo uone ni jinsi gani tunaishi katika nyakati za hatari.