Ni vema kufahamu Kanisa ni nini?
Kanisa sio jengo, au mahali, bali ni watu, walioitwa Na Mungu, waliookolewa wanakusanyika pamoja katika nia moja kumwabudu na kumtumikia yeye.
Hivyo watu hawa wanaweza kukusanyika maeneo yaliyo rasmi, lakini pia maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli zao za kiibada..maadamu tu wamekidhi vigezo hivyo vya kiroho.
Kanisa la kwanza lilikusanyika Hekaluni (mahali rasmi kwa shughuli za kiibada tu). Lakini pia lilikusanyika majumbani…wakati mwingi pembezoni Mwa mito na kwenye madarasa..
Matendo ya Mitume 2:46
[46]Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,
Matendo ya Mitume 5:42
[42]Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.
Kama tunavyojua majumbani mahali ambapo, pana shughuli nyingi wakimaliza ibada huwenda sherehe zinafanyika hapo, au vikao vya kijamii, lakini hilo halikuwazuia kutimiza makusudi ya Mungu yaliyoyakusudia.
Hivyo yaweza kuwa ni sahihi endapo, hakuna mahali rasmi bado, ibada zinaweza kufanyika kwenye majengo ya shule, kwenye mabwalo, kwenye kumbi,.viwanjani, hata chini ya miti maadamu tu umoja huo upo na nia ni Kristo..hata hivyo yapo makanisa makubwa na yamefanikiwa lakini bado hayana maeneo yao rasmi ya kukutanikia…lakini kanisa Limesimama.
Mambo tu ya kuzingatia, ni nidhani yenu, adabu na utulivu wa mazingira ya kiroho kwa wakati huo,..ikiwa haya yapo hapo Mnapokusanyikia basi Mungu yupo nanyi..wala si dhambi.
Lakini ni busara na vema zaidi kanisa likatafuta eneo rasmi la kukusanyikia litakalokuwa ni kwa shughuli zao tu za kiibada.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
Print this post
1Petro 1:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Siku ya kujiliwa ni wakati ambao, Mungu anashuka ulimwenguni, aidha kwa kuokoa au kuhukumu.
Zote mbili ni siku za kujiliwa.
Kwa mfano kwa lengo la kuokoa. Upo wakati ambao neema ya Mungu humjia mtu, au taifa, na hivyo wakati huo mara nyingi uamsho mkubwa huwa unapita, Kwamfano, kipindi cha Kristo, kilikuwa ni kipindi maalumu cha Israeli kujiliwa lakini hawakukubali ..isipokuwa wachache..(Luka 19:41-44)
Lakini kwa lengo la hukumu ni siku ambayo kila mmoja wetu atahukumiwa kulingana na matendo yake.
Hivyo tukirudi kwenye 1 Petro 1:12, inayosema ‘Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa’.
Maana yake, matendo mema ya mwamini, hupelekea watu kuupokea wokovu na kumtukuza Mungu,siku neema yao inapowafikia, kwamfano wapo watu ambapo kwa kukuangalia, kwa kipindi kirefu, siku ya kujiliwa inapowafikia inakuwa ni rahisi kuamini na kumtukuza Mungu, kwasababu walishawahi kuona watu waliokoka walivyo na sifa zao njema, mfano upendo, amani, uadilifu..Lakini ukiwa na mwenendo mbovu, siku yao ya kujiliwa inapowafikia, wakikumbuka mwenendo mbovu waliouna kwako , ni ngumu sana kumtukuza Mungu,
Ndicho ambacho mtume Petro alikuwa anakieleza hata mbeleni kidogo, kuhusiana na Wanandoa, kwa upande wa wanawake, akasema, ikiwa mtu ana mume asiyeamini, anao uwezo wa kumvuta ndani ya Kristo kwa mwenendo wake tu.. (1Petro 3:1).
Kwa ufupi ni kuwa mwenendo wako mwema hulainisha njia ya neema ya Kristo Kutenda kazi vema juu ya mtu.
Mungu akubariki.
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
MILANGO YA KUZIMU.
JIBU: Tukiangalia mwanzo wa mstari huo, unasema..
Mithali 11:16 Mwanamke wa adabu huheshimiwa daima; Na watu wakali hushika mali siku zote.
Ukitazama tafsiri nyingine maana iliyonyooka zaidi ya mstari huo, unasema “mwanamke wa adabu huheshimwa daima, lakini watu wakali hushika tu mali”.
Yaani unalinganisha, sifa njema, na vitu vingi, akilinganisha mwanamke anayewekeza maisha yake katika tabia nzuri, matokeo yake heshima itakuwa kwake ambayo itadumu daima, lakini mtu mkali anayewekeza katika kujilimbikizia mali isivyo halali, akiwakandamiza wengine, akitumia ukali, akiwanyima mshahara wengine, ni kweli na yeye atapata matokeo yake ambayo ni mali nyingi tu. Lakini hana heshima yoyote nyuma yake. Haachi kitu chenye thamani kitakachoweza kuwa faida kwa wengine, hana la kuigwa, hana la kusifiwa isipokuwa, malalamiko, uchungu na machozi kwa wengine.
Hivyo andiko hilo linalinganisha sifa njema na mali. Ni heri ujijengee sifa njema ambayo hiyo itafuatwa na vizazi hata vya mbeleni, kama vile tuwaonavyo wanawake wacha Mungu kwenye maandiko, mfano wa Ana binti Fanueli, Mariamu, Sara, watu kama akina Ayubu, Danieli, Yusufu, ambao njia zao huigwa hata sasa, kuliko kuwa kama Nabali aliyetajirika lakini mpumbavu, hana chochote cha kuigwa na watu.
Ni heri maskini ahubiriye watu, na kuwaleta kwa Kristo, wanaacha dhambi, na kupokea Roho Mtakatifu, kuliko mtu yule ambaye kutwa nzima anachowaza ni kujiwekezea nafsi yake, kuiba, na kudhulumu, kutumia ukali kupata mali mambo ambayo yataishia hapa hapa tu duniani.
Mithali 22:1 Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.
Tafsiri ya Mithali 3:27 inayosema ‘Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao’
Maana ya Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Maana ya Mithali 26:2 Kama shomoro katika kutanga-tanga kwake,
SWALI: Tumekuwa tukisikia kuwa mtu akifa, huko aendako anakutana na mateso makali ya jehanamu. Sasa napenda kufahamu je ni roho ndio itakayoteketezwa au na miili pia?
JIBU: Maandiko yanatueleza siku ya mwisho ya hukumu, wafu wote watafufuliwa. (Iwe ni wema au waovu), wote watairudia miili yao ya asili yaliyokuwa nayo duniani.
Yohana 5:28
28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu
Ufunuo 20: 12-13
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake
Waliokufa katika Kristo (Watakatifu) watavikwa miili mipya ya utukufu, isiyoharibika (1Wakorintho 15:42-54) lakini waovu watakuwa na miili yao ya asili. Ambayo katika hiyo watahukumiwa na kutupwa katika lile ziwa la moto, lililo maalumu kwa mateso ya mtu milele.
Hivyo ni vizuri ifahamike, kuwa kitakachoteketezwa sio roho tu, bali na mwili pia, Bwana Yesu aliliweka hilo wazi katika maneno haya;
Mathayo10:28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Umeona hapo?.. Awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum. Kuonyesha kuwa mwili nao utashiriki mateso ya milele.
Tukishayajua hayo, tunapaswa tufanyaje?
Je! Umemwamini Bwana Yesu ndugu? Wokovu ni sasa, mgeukie akuponye, uwe salama, hata ukifa uwe na uhakika wa kuurithi uzima wa milele, Itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako? Fanya uamuzi wa busara.
Okoka, leo uponywe. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA
MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
SWALI: nini maana ya Yohana 17:20
[20]Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Ni akina nani hao ambao wataamini Kwasababu ya Neno lao, Bwana Yesu aliotaka kuwaombea?
JIBU: Sura hiyo ya 17 ni sura iliyoelezea kwa kina dua ambayo Bwana Yesu aliifanya kwa mitume wake kwa Baba.
Ambapo aliwaombea mambo kadha wa kadha ikiwemo walindwe katika umoja wa Roho, walindwe na yule mwovu, watakaswe na ile kweli.. Lakini pia Bwana Yesu hakuishia kuwaombea wao tu, bali na wengine ambao mitume wake watawahubiria injili na kuamini baadaye. Na hao pia maombi yake yalikuwa ni yaleyale kwao.
Maana yake ni kuwa watu wote walioamini kwa injili ya mitume walishiriki dua hiyo ya Kristo, Na hao si wengine zaidi ya wale watakatifu wa kanisa la kwanza, hadi sisi tuliopo sasa, hadi na wale watakaokuja baadaye.. sisi wote ni washirika wa dua ile (Yohana 17), kwasababu tumeamini katika injili moja ya mitume..
Ndio sababu kwanini maandiko yanasema Kristo anatuombea…maana yake ni kuwa sasa anatuombea kwa yule Roho Mtakatifu auguaye ndani yetu, lakini pia analituombea alipokuwa duniani ambapo sala hiyo tunaona matokeo yake hata sasa.
Waebrania 7:25
[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Hii ni kututhibitishia Kuwa pale tunapomwamini Kristo upo ulinzi usioelezeka unawekwa juu yetu, kiasi kwamba malango ya adui hayawezi Kushinda..kinachohitajika ni kutii tu.
Warumi 8:34
[34]Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
Je na wewe ni mshirika wa sala hiyo ya Bwana? Kwa kumpokea Bwana Yesu? Kama ni la! Basi nafasi ni sasa mwamini Yesu upokee uzima wa milele.
Lakini pia Bwana anatufundisha namna sahihi ya kuomba..hatupaswi tu kuyaombea yale matunda tunaoyaona..bali hata na yale yatakayokuja baadaye..wale watakaokoka baadaye kwasababu ya Neno letu.
WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.
MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.
“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).
WhatsApp
Tofauti na Ibrahimu, Isaka na Yakobo ambao chimbiko lao linaonekana katika mtiririko wake tokea Adamu mpaka Nuru hadi wao wenyewe..
Ayubu yeye ni tofauti, kwani kitabu kinaanza kwa kumweleza yeye, na mahali tu alipokuwa ambapo ni Usi.
Usi ni nchi ambayo ilikuwa nje ya Israeli, maeneo ya aidha Arabia, Syria au Yordani..lakini eneo sahihi kwa uhakika halijulikani hivyo hakuwa na chimbuko lolote la kiyahudi ndani yake.
Maandiko yanamtaja tu kama “Mtu”, wala sio nabii, au kuhani bali mtu aliyekuwa mkamilifu na mwelekezo aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu.
Ayubu 1:1
[1]Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.
kwanini Mungu aruhusu, watu kama hawa ambao hawakuwa katika mtiririko wa kifamilia waandikwe kwenye biblia na zaidi hata wawe na sehemu kubwa katika ufalme wa Mungu…
Ni kuonyesha kuwa Mungu hana upendeleo, yeyote yule amchaye yeye hukubaliwa naye..ndicho Petro alichokiona kwa Kornelio akasema..
Matendo ya Mitume 10:34-35 [34]Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo;
[35]bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.
Mwanamke Ruthu hakuwa myahudi, lakini Bwana alimkubali.
Hata na wewe kitendo cha kutozaliwa familia ya kikristo au kichungaji haimaanishi kuwa wewe huna neema ya kumtumikia Mungu. Hapana..ukionyesha bidii ile ile wanayoonyesha wengine Mungu hukujalizilisha neema Izidiyo haijalishi ukoo wenu wote ni wa kiganga. Kila mmoja wetu ana nafasi sawa mbele za Mungu, haijalishi kama ni myahudi au mwarabu, kama ni mzungu au mwafika wote kwa Mungu wanayo neema sawa kwasababu yeye haangalii chimbuko wala sura ya mtu.
Je unamcha Mungu?
Swali: Kwanini Nabii Yeremia ailaani siku aliyozaliwa?, na je ni sahihi kulaani siku tulizozaliwa?
Jibu: Turejee maandiko hayo kuanzia ule mstari wa 14 hadi wa 17..
Yeremia 20:14 “Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu. 15 Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha. 16 Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri; 17 kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito”.
Yeremia 20:14 “Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu.
15 Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha.
16 Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri;
17 kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito”.
Utaona sababu kuu ya Nabii Yeremia kuzungumza maneno yale ni “mateso aliyokuwa anayapitia katika huduma yake”.. kwani alipitia mapigo na vifungo vingi na aliwindwa kila mahali kwasababu ya maneno ya Mungu (Soma Yeremia 20:1-2, Yeremia 37:15-16, Yeremia 38:6, Yeremia 15:5)…kama mstari wa 18 unavyoelezea.
“..18 Nalitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?”
Na si tu Nabii Yeremia aliyeilaani siku yake aliyozaliwa, bali tunaona pia Ayubu naye alisema hayo hayo..
Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. 2 Ayubu akajibu, na kusema; 3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. 4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. 5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. 6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.
Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.
2 Ayubu akajibu, na kusema;
3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.
5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.
6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.
Sasa swali ni je! Walifanya sahihi kuzilaani siku zao?, na sisi je tunapopitia dhiki zilizozidi ni sahihi kuzilaani siku tulizozaliwa na watu waliotuzaa, na matumbo yaliyotuzaa?.
Jibu ni La! Si sahihi kabisa kuzilaani siku tulizozaliwa, wala kulaani matumbo yaliyotuzaa, hata tupitie dhiki kiasi gani?..
Nabii Yeremia na Ayubu walisema maneno yale kwakuwa yalionekana kama ni mambo mapya kwao, kwamba inawezekanaje uwe Nabii uliyetumwa na Mungu, unayesema maneno ya kweli, au inakuwaje uwe mtu wa Mungu, mwelekevu na mkamilifu halafu unakubwa na mambo mazito kama yale?.
Kwahiyo yale yaliyowapata yalikuwa ni mambo mapya kwao, hawakuwa na mifano ya waliowatangulia waliopitia kama hayo katika kiwango hiko, hivyo walisema yale kwa udhaifu wa kibinadamu, lakini hawakuwa sahihi, ndio maana baadaye utaona Ayubu anakuja kutubu, kwa kusema “amesema maneno yazidiyo”
Ayubu 42:3 “Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua. 4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie. 5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona. 6 Kwasababu hiyo NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.
Ayubu 42:3 “Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.
4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.
5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.
6 Kwasababu hiyo NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.
Umeona? Hapa Ayubu anakuja kutubia maneno yake, baada ya kumjua Mungu zaidi, na ni hivyo ivyo Yeremia alikuja kuona makosa yake, soma Yeremia 15:18-19.
Na hatuoni tena Ayubu baada ya kuponywa msiba wake wala Yeremia baada ya kustahereshwa wakirudia kusema hayo maneno, hivyo wao walipitishwa katika mapito hayo ili iwe darasa kwetu sisi, kwamba ukiwa mtumishi wa Mungu, au mtu mkamilifu mbele za MUNGU, sio tiketi ya kutopitia majaribu!, LA! Majaribu yanawapata watu wote (wakamilifu na wasio wakamilifu), hivyo hatupaswi kulalamika wala kulaani yanapokuja bali kuomba na kumngoja BWANA.
Na hiyo ndio sababu ya Bwana wetu YESU kuwatahadharisha wanafunzi wake, na hivyo anatutahadharisha hata sasa kwamba tutakapopitia dhiki kwaajili ya Imani tunapaswa tuwe wapole kama hua na wenye busara kama nyoka.
Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua. 17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga; 18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.
Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.
17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;
18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba si sahihi kuzilaani siku za kuzaliwa au siku nyingine yoyote, wakati wote tunapaswa tuwe watu wenye busara, na watulivu..hakuna faida yoyote katika kunung’unika wala kulalamika.
Bwana atusaidie.
Laana ya torati maana yake ni nini?
JE NI LAANA KULELEWA NA BABA AU MAMA WA KAMBO?
Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?
NAKUJUA JINA LAKO!
SWALI: Maandiko yanasema “Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele”, Je! ni aibu gani anaomba aepushwe nayo?. Mbona tunapitia kuabishwa, ijapokuwa tumemkimbilia Mungu?
JIBU: Vifungu kadha wa kadha kwenye zaburi vinaeleza, habari hiyo,
Zaburi 31:1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye
Zaburi 25:20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe
Soma pia Zaburi 22:5, 71:1
Daudi ni mtu ambaye alizungukwa na maadui pande zote, na hivyo alijua nguvu zake zipo kwa Mungu tu, hivyo akishindwa nao basi itakuwa ni fedheha na aibu kwake, Vilevile ni mtu ambaye aliahidiwa mambo makubwa na Mungu, ikiwemo kudumishiwa kiti chake cha enzi milele, lakini kutokana na mapito na masumbufu mengi aliyokuwa anapitia na kukawia katika ufalme, ilionekana kama jambo hilo haliwezekani..Lakini hakuacha kumwomba Mungu, azitazame ahadi zake asiabike, kwa kumtumaini yeye.
Zaburi 89:49 Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako? 50 Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi. 51 Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako. 52 Na ahimidiwe Bwana milele. Amina na Amina.
Hapo ndio utaona sasa kwanini sehemu nyingi, kwenye Zaburi Daudi anamwambia Bwana, akumbuke asiabike milele, kwa kuzitumainia fadhili zake..
AGANO JIPYA.
Lakini katika agano jipya pia,
Nasi pia tunamtumaini Mungu ili tusiabike milele.Na Aibu kuu ni ile ya kutengwa na uso wa Mungu milele, ambayo watakutana nayo wenye dhambi, ile aibu ya kufukuzwa mbele ya uso wa Mungu.
2 Petro 3:13 Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa WALA AIBU mbele yake.
Hiyo ndiyo Bwana atatuepusha nayo sisi tuliomtumainia.
Ni vema kufahamu kuwa tukiwa kama watoto wa Mungu, haimaanishi kuwa hatutaaibishwa au kudhalilishwa kwa ajili ya jina lake, vipindi hivyo tutapitia, lakini mwisho wetu utakuwa ni kutukuzwa katika utukufu mkuu milele..
Ni heri leo ukubali aibu ya kidunia, kuliko kukutana na ile ya Kristo wakati ule..
Mathayo 7:23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Mathayo 25:31-34, 41
31 Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; 32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; 33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. 34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu… 41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
SWALI: Kwanini Bwana Yesu alitumia neno “wewe wasema” alipoulizwa maswali na sio kujibu moja kwa moja?(Mathayo 27:11)
JIBU: Ni kweli tunaona mahali kadha wa kadha Bwana Yesu alipoulizwa maswali Na baadhi ya wayahudi na wapagani, majibu yake hayakuwa yamenyooka moja kwa moja alitumia kauli ya “wewe wasema”…kwa mfano tazama vifungu vifuatavyo;
Mathayo 27:11
[11]Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
Luka 22:68-71
[68]Tena, nikiwauliza, hamtajibu. [69]Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi. [70]Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye. [71]Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.
[68]Tena, nikiwauliza, hamtajibu.
[69]Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi.
[70]Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.
[71]Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.
Soma pia…Luka 23:3
Maana rahisi ya neno hilo ni ipi?
Maana yake ni
“ndio, wewe umesema hivyo, sio mimi”
Au “ndio, wewe umeona kuwa ni hivyo”
Sasa kwanini Atumie kauli hiyo?
Kwasababu alijua waliokuwa wanamuuliza hawakuwa na nia ya kutaka kufahamu ukweli, bali kutafuta neno la kumshitaki, au kumdhihaki, ndio maana kujibu kwake hakukuwa kwa moja kwa moja, yaani upande mmoja anaonyesha kukubali, lakini upande mwingine anaacha hukumu watoe wao wenyewe…
Hiyo ilikuwa ni desturi yake sio tu kwenye maswali bali hata kwenye Mafundisho yake kadha wa kadha…Alizungumza na makutano kwa mifano..kisha wale waliokuwa tayari kupokea aliwafunulia yote baadaye.
Hii ni hekima ambayo tunaweza jifunza hata sisi..
Kwamfano wewe ni mchungaji, kisha ukajikuta watu wasiopenda wokovu, wamekushitaki na kukupeleka Mahakamani halafu hakimu anakuuliza je wewe ndio wale wachungaji ambao, mnaweka Makapu ya sadaka mbele, ili mle Sadaka za waumini.
Sasa unajua kabisa kauli kama hiyo ni ya mtego, kukudhihaki, au kutaka sababu ya kukushitaki, sasa Ili kuikata kauli yake..kukataa Kuwa wewe sio mchungaji watasema unadanganya, kukataa kuwa chombo cha sadaka hakiwekwi mbele watu kutoa, watakuona Pia mwongo, lakini kukusingizia unakula sadaka za waumini unajua ni uongo…
Hivyo kujibu vema hiyo kauli ni kukubali upande mmoja, na mwingmwingiwaachia wao aaamue..
“Wewe Wasema”
Yaani *ndio, wewe umesema hivyo*
“Ndio wewe Umeona kuwa ndivyo ilivyo”.
Hapo umekata maneno yote..atakachoamua, Ni kulingana na mawazo yake mwenyewe lakini sio yale yaliyothibitishwa kikamilifu na wewe..
Hivyo yatupasa tutumie busara. katika ujibuji wetu wa maswali hususani kwa wale wanaotushitaki na kutushambulia
SWALI: Kwanini Bwana Yesu alipowatuma wanafunzi wake kuhubiri aliwaambia wasihame- hame nyumba watakazo Karibishwa?
Luka 10:7
[7]Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
JIBU: Luka 10, Mathayo 10, Na Marko 6, Kristo inawafundisha mitume wakee nidhamu ya kimisheni. Pale ambapo watu wa Mungu watatoka na kwenda kuhubiri injili kwenye miji, mataifa au nyumba za Watu.
Ukisoma pale utaona Kristo anawapa maagizo kadha wa kadha mfano amri ya kutoa huduma zao bure, anawaagiza wawe wapole kama Hua, na wenye busara kama nyoka, vilevile nyumba watakazokaribishwa kisha chakula kikawekwa mbele yao wale bila kuuliza- uliza…
Lakini agizo lingine lilikuwa ni kutohama-hama nyumba moja kwenda nyingine. Kwamfano wameingia mji fulani halafu ikatokea familia moja ikawaalika kukaa kwao kwa kipindi chote cha huduma, hawapaswi kuhama- hama bali wakae pale mpaka watakapotoka na kwenda mji mwingine ikiwa yule mfadhili hana neno nao. Hata kama wakialikwa nyumba nyingine hawapaswi kuhama- hama..
Swali linakuja kwanini iwe hivyo?
Bwana Yesu alijua kuwa katika ziara mialiko kwa watumishi wa Mungu, huwa ni mingi. Na hivyo ili kuzuia dhamiri mbaya na wengine kuvunjika mioyo, akatoa agizo hilo Kwasababu mfano imetokea mtumishi amealikwa kisha kesho yake akahamia nyumba nyumba nyingine, Yule wa kwanza atajisikiaje? Pengine picha itakayoonekana hapo ni kuwa wanatafuta maisha mazuri, au matajiri wenye hadhi ya kuwatunza..
Lakini wakitulia sehemu moja huleta adabu na kuonyesha tabia ya kuridhika.
Lakini pia Kristo alitaka akili zao zijikite zaidi kwenye huduma.. Kwani kitendo cha kila siku kuhama hapa kwenda kule, hupoteza umakini kihuduma, ni sawasawa na mtu ambaye kila siku anahama nyumba moja ya kupanga kwenda nyingine…unaelewa ni usumbufu gani anaokutana nao.. kuanza tena kuyazoelewa mazingira mapya ni gharama.
Hasa sasa kama watumishi wa Mungu…tunafundishwa utulivu tuwapo ziarani…Mara nyingi ule mlango wa fadhili ambao unafunguliwa wa kwanza, huwa ni wa Mungu…tulia katika huo huo…nyumba ile ya wageni unayoingia ya kwanza…ikiwa amani ya Kristo imekaa ndani yako…tulia hiyo hiyo mpaka utakapomaliza ziara zako…usiwe mtu wa kutafuta makao mazuri, Kwasababu kumbuka upo ziarani… mahali pa muda tu.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10