Ili kuelewa maana ya ndoto yako, jambo la kwanza ni kujiuliza ni kwanini awe mchungaji, na si mwalimu wako, au boss wako, au rafiki yako, au ndugu yako au mtu mwingine yoyote?
Ukiwaza hivyo, tendo linalofuata ni kujua kazi ya mchungaji hasa ni nini?
Mchungaji ni mwakilishi wa Mungu na hivyo anafanya kazi ya kutoa mashauri bora ya kiroho kwa mafundisho sahihi (Tito 1:7-9): Kuonyesha kuwa maisha yako yanahitaji hekima ya ki-Mungu kukuongoza, zaidi ya hekima yako mwenyewe. Kila jambo au uamuzi unaojitokeza kwenye maisha yako, mshirikishe kwanza Mungu kimaombi, kisha angalia kwenye biblia jambo hilo Mungu analiagizaje, ikiwa si rahisi kutatulika, basi ni vema ukamshirikisha kiongozi wako wa kiroho kukusaidia.
Wachungaji pia wamepewa mamlaka ya kutoa maonyo kwa kondoo wao.
2Timotheo 4:2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho
Angalia pengine katika maisha yako Mungu anakuonya / anakutahadharisha katika jambo Fulani, ambalo sio sawa unalotaka kulifanya. Hivyo zingatia sana pia hilo.
Kazi ya wachungaji ni kuwalinda, kuwafariji na kuwainua waliokata tamaa. Mfano wa Yesu kristo mwokozi wetu, na faraja yetu, aliyemchungaji mkuu (Mathayo 11:28, Zab 23). Hivyo Mungu anakuonyesha kuwa yupo na wewe katika safari yako, kukuchunga, usiogope.
Lakini sababu nyingine ya mwisho (ambayo si kubwa): Yaweza kuwa ni wazo la ki-akili. Kwasababu kumbuka si ndoto zote hutoka kwa Mungu au kwa shetani, nyingine ni wazo la bongo zetu, kufuatana na mazingira yanayotuzunguka (Mhubiri 5:3). Kwamfano ikiwa mara nyingi unakuwa karibu na mchungaji wako, kuota unaongea naye mara kwa mara, itakuwa ni jambo la kawaida. Au mtu ni mpishi, kujiona yupo jikoni mara kwa mara anapika litakuwa ni jambo kawaida kabisa kwake.
Hivyo kwa ufupi ni kuwa kuota unaongea na mchungaji wako, si ndoto mbaya, bali kwa asilimia kubwa ni ya ki-Mungu. Inategemea zaidi na maudhui yake. Hakikisha tu unapiga magoti na kuomba Bwana akufunulie ni eneo lipi hasaa, ndoto yako imeegemea ukilinganisha na maisha yako, na lile eneo ambalo unaona lina uzito zaidi basi ujue hapo ndipo Mungu anasema nawe hapo. Chukua hatua.
Je! Umeokoka?
Unafahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu amekaribia sana kurudi? Ikiwa ni la! Basi muda ndio huu, mgeukie Kristo akuoshe dhambi zako, akupe uzima wa milele bure. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, fungua hapa kwa msaada wa kuongozwa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Ikiwa ndoto hii inakujia mara kwa mara, Au imekujia kwa uzito fulani, basi hwenda Mungu anasema na wewe rohoni. Ndoto hii inaweza kuja katika maumbile mengi. Wengine wanaota wakivua samaki kwa mikono, wengine kwa ndoano, wengine kwa wavu, wengine wakivua samaki wadogo/wakubwa. n.k. Kwa vyovyote vile maadamu ni kuvua basi maudhui yake ni moja.
Kiroho, uvuvi humaanisha kuwavuta watu kwa Kristo kwa kazi ya injili.
Yesu alipokutana na wale thenashara, wengi wa hao walikuwa wakifanya kazi ya uvuvi. Hivyo hiyo ilikuwa ni njia rahisi ya Yesu kuwaeleza kusudi lake timilifu juu ya hicho wanachokifanya.
Ndio maana siku ile alipomfanyia Petro muujiza ule wa kupata samaki wengi, baada ya kutaabika usiku kucha bila kupata chochote, Yesu alimwambia usiogope tangu sasa utakuwa mvuvi wa watu.
Luka 5:10
[10]na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni.Yesu akamwambia Simoni, Usiogope, tangu sasa utakuwa ukivua watu.
Kuonyesha kuwa uvuvi wa nje, ni ufunuo wa uvuvi wa rohoni.
Utaona hata huduma ya malaika siku ile ya mwisho ya kuwatenga watu waovu na wema inafananishwa na huduma ya uvuvi wa samaki.
Mathayo 13:47-50
[47]Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;
[48]hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.
[49]Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,
[50]na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Hivyo kwa namna moja au nyingine ikiwa umeokoka basi Bwana anakutaka uhihubiri injili, kwa wengine kwasababu wakati huo umefika kufanya hivyo. Usiangalie uzoefu wako, kwasababu kumshuhudia Kristo hakutegemei uzoefu bali nia ya upendo. Na Mungu mwenyewe ameahidi kukusaidia kunena uwashuhudiapo watu.
Lakini kama hujaokoka, basi Yesu anakuita na anaona wito wako kutokea mbali, kwamba ukawahubirie wengine. Hivyo ni wajibu wako kumtii na kuupokea wokovu ili kusudi hilo alilolipanga ndani yako alifanikishe juu yako, haijalishi ndoto hii umeota mtu wa dini gani au imani gani, iwe mwislamu, mhindu, mshirikina. Maana umeota msalaba. Ujue Kristo anakuita akuokoe.
Ikiwa upo tayari sasa kumpokea Yesu basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Ikiwa wewe bado hujamjua Kristo kabisa/ hujaokoka. Fahamu kuwa ndoto hii inakujuza kuwa Kristo anakuita akuokoe.
Msalaba hufunua wokovu wa Yesu Kristo, tulioupata kwa kifo chake juu ya mti huo.
Waefeso 2:16
[16]Akawapatanisha wote wawili na Mungu katika mwili mmoja, kwa njia ya msalaba, akiisha kuufisha ule uadui kwa huo msalaba.
Hivyo fungua moyo wako upokee wokovu huu bure, Kumbuka hakuna uzima wala tumaini, wala, amani,wala raha, wala faraja nje ya Kristo. Ndio maana umeota msalaba kwasababu Kristo anakupenda, hataki uangamie. Ikiwa upo tayari kumpokea leo basi fungua hapa kwa msaada…
Lakini ikiwa tayari umeokoka. Kristo anakutaka kumuangalia yeye zaidi… Kuongeza kiu yako, kwake, na mawazo yako kwake, na hiyo inaambatana na kujikana nafsi.
Luka 9:23-24
[23]Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
[24]Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.
Hivyo kwa ujumla wake ndoto ya msalaba, aidha umeushika au umeubeba, au umeuona, ni ishara ya kumtazama Kristo.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Jiunge >>> WHATSAPP <<< kwa mafundisho.
Biblia ni kitabu pekee chenye ukweli wote, umuhusuo Mungu, na mwanadamu, ni kitabu kinachoifunua njia ya uzima. Hivyo kuota unapewa biblia fahamu kuwa ndoto hiyo ni ya ki-Mungu, kwasababu kamwe shetani hawezi kukuongoza mahali ambapo utapata nuru ya maisha yako.
Zaburi 119:105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Hivyo ikiwa wewe bado hujamjua Kristo, basi fahamu Mungu anakupenda na hivyo anataka kukuongoza katika ukweli wote, Ndio maana umeota unapewa biblia haijalishi utakuwa mwislamu, mhindu, mpagani n.k Fahamu kuwa Yesu anakupenda, na anataka kukuokoa. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumkubali tu maishani mwako, ili aweze kukufikisha katika ukweli wote, na majibu yote ya maisha yako.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala hiyo ya imani >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Baada ya hapo, tafuta kitabu hichi (BIBLIA), Haraka iwezekanavyo uanze kusoma. Huku ukisaidiwa na waalimu sahihi wa Neno la Mungu. Kumbuka Wewe kufika hapa sio bahati mbaya, tovuti hii uliyopo sasa, Bwana ameiweka kwa ajili yako ina mafundisho mengi yatakayoweza kukusaidia kuielewa biblia vizuri. (www.wingulamashahidi.org). Itembelee mara kwa mara. Yapo mafundisho mengi sana, pamoja na majibu ya maswali mengi ya biblia. Lakini pia kama unatumia mtandao wa Whatsapp basi bofya hapa >>> WHATSAPP
Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani