Hivyo usidhani kuwa YESU hajui unachokipitia, anafahamu sana kwasababu na yeye pia alishayapitia embu fikiria yale mapigo aliyokuwa anayapata siku ile, makovu, miiba kupenyezwa kwenye kichwa chake na kupondwa kwa fimbo, mijeledi ya visu 39, misumari mikononi na miguuni, na bado misumari hiyo hiyo ndiyo aliyoitegemea imning’inize msalabani, ni taabu kiasi gani mtu anaweza kupata, unategemea vipi mtu kama huyo asipatwe na mchanganyiko wa maumivu ya magonjwa unayoyajua wewe leo, alipata HOMA kali zaidi ya mtu yeyote aliyepata hapa duniani, aliugua, alikuwa mauti uti kwasasa tunaweza kusema hali aliyokuwepo Bwana Yesu ni zaidi ya mtu aliyeko ICU leo, mwili wote ulivimba hata usiweze kumtambua tena kwa ajili ya mapigo yale, wewe leo ugonjwa ulionao hauwezi kufikia hatua ya kuteseka kaisi hicho, lakini yeye alipata ugonjwa huo mkuu kwa ajili yako. Hivyo ndugu usiwe na hofu yeye BWANA anafahamu vizuri hali unayopitia, hauhitaji kumwadithia anaijua hali yako.