Nini maana ya ‘kuhuluku’ kama tunavyosoma katika biblia?

Nini maana ya ‘kuhuluku’ kama tunavyosoma katika biblia?

Kuhuluku ni Neno lingine linalomaanisha KUUMBA.

Kwamfano tukisema Mungu kahuluku jua na mwezi, tunamaanisha kuwa Mungu ameumba jua na mwezi.

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu ambavyo vinalielezea Neno hilo;

Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu”.

Isaya 45: 12 “Mimi nimeiumba dunia, nimemhuluku mwanadamu juu yake; Mimi, naam, mikono yangu mimi, imezitanda mbingu, na jeshi lake lote nimeliamuru”.

Isaya 45: 7 “Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na KUHULUKU UBAYA; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote”.

Katika huu mstari wa mwisho utaona anasema sio tu ameumba vitu vya asili na wanadamu au  mambo mema tu peke yake, hapana, bali anasema yeye pia ni Mungu anayehuluku UBAYA, Yaani anaumba ubaya. Jambo ambalo wengi hatulijui.

Ndio Mungu anaumba ubaya ndugu yangu,. Alipoleta gharika ule ulikuwa ni ubaya, lengo lilikuwa ni kuwagharikisha watu wote waovu waliokuwa duniani wakati ule. Embu Soma maneno haya anavyosema;

Ayubu 38:22 “Je! Umeziingia ghala za theluji, Au umeziona ghala za mvua ya mawe,

23 Nilizoziweka akiba kwa wakati wa misiba, Kwa siku ya mapigano na vita”?

Unaona?

> Aliposhusha  pia ule moto na  kibiriti, wakati wa Sodoma na Gomora ule ni uovu aliouumba yeye mwenyewe mahususi kwa ajili ya watenda dhambi.

> Alipoleta  tena Tauni mara kadha wa kadha kwa taifa la Israeli pale walipomwasi na kumkasirisha kule jangwani na sehemu nyinginezo, ule ulikuwa ni ubaya aliohuluku, kwa watu waasi.

> Vilevile alivyoleta CORONA ulimwengu ni Ubaya uliotoka kwake yeye mwenyewe kutuadhibu sisi wanadamu tunaoishi duniani leo hii  kwa matendo yetu maovu. Hakuna mwanasayansi yoyote aliyeuunda ugonjwa huo, Huo ni ugonjwa uliotoka kwa Mungu mwenyewe kama pigo.

> Lakini hayo yote ni mwanzo tu ubaya wenyewe ambao Mungu alishaundaa tangu zamani kwa watenda dhambi wote ikiwemo ibilisi pamoja na mapepo yake yote. Na ubaya wenyewe ndio lile ZIWA LA MOTO.

Hivyo Mungu ni wa kumuogopa sana.. Ni kweli yeye ni Mungu wa rehemu na neema nyingi, kwa wale wamtiio, lakini pia ni wa ghadhabu na hasira nyingi, kwa waovu wote. Na ndio maana leo hii anakupa Muda wa kutosha wa kutubu ili umgeukie yeye akusemehe dhambi zako. Usifurahie unatenda dhambi halafu hakuna chochote kinachokutokea, usifurahie unaua, unafanya ushirikina, unazini, lakini Mungu hakufanyi chochote ukadhani utaendelea kuwa hivyo milele. Upo ubaya mbele yako. Na ni jukumu lako kufahamu hilo ili siku ile usije ukasema sikuambiwa.

Hivyo tubu dhambi zako umgeukie Mungu, akuoshe, ili ushiriki wema wa Mungu na sio ubaya wake.

Kama upo tayari kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya SALA YA TOBA, na Maelekezo mengine >> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Pia Tazama tafsiri ya maneno mengine ya kibiblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kiango na Pishi ni nini (Mathayo 5:15)?

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

Ngome ni nini?  Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?

Ni kwanini mifugo ya Yakobo iliongezeka kwa wingi kiasi kile?

Nyinyoro ni nini?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Edward Bavunah
Edward Bavunah
1 year ago

Amina

Peter watuthu
Peter watuthu
3 years ago

I’d wish to learn more about the bible