JE YESU ALINENA KWA LUGHA?

JE YESU ALINENA KWA LUGHA?

Katika maandiko hakuna vifungu vya Moja Kwa Moja vinavyorekodi tukio la Bwana Yesu kunena Kwa lugha.

Lakini Kwa ufahamu wa Rohoni tuliopewa twajua kuwa ni wazi Yesu alinena Kwa lugha. Kutokurekodiwa Kwa tukio hilo hakumaanishi kuwa hakuwahi kunena Kwa lugha, kwasababu maandiko yanasema yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu kama yangeandikwa hata vitabu vyote duniani visingeweza kutosha, Kwa wingi wa habari zake.(Yohana 21:25)

Hivyo si Kila tukio la Bwana Yesu limeandikwa  kwenye biblia.

Halikadhalika Ifahamike kuwa taaarifa za kunena Kwa lugha aliyezieleza kwa mara ya kwanza Kwa mitume ni Bwana Yesu.(Hawakufunuliwa baadaye)   Hivyo hawezi kuwaambia watu jambo ambalo yeye mwenyewe halipo ndani yake, au hajawahi kulifanya.

Marko 16:17-18

[17]Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

[18]watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

Vilevile Yesu ndiye mwanadamu pekee aliyetiwa mafuta mengi na Roho kuliko mtu yeyote aliyewahi kutokea duniani, (Waebrania 1:9). Zile karama zote za Roho zilikuwepo ndani yake, alikuwa ni nabii, mwalimu, mwinjilisti, mchungaji, mtume, n.k. na karama za uponyaji, miujiza, upambanuzi alikuwa nazo, hivyo hatuwezi kushangaa pia na hii kunena Kwa lugha kuwemo ndani yake.

Kwa kuhitimisha ni wazi kuwa Bwana Yesu alinena Kwa lugha. Hivyo akampendeza kukimwaga  kipawa hicho na kwetu pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618

Mada Nyinginezo:

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

WANAWAKE WAOMBOLEZAJI

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

IJUE FAIDA YA KUNENA KWA LUGHA MPYA!

YEYE ATAWABATIZA KWA ROHO MTAKATIFU NA KWA MOTO.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOKUJA JUU YA MTU.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
1 Comment
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Patrick
Patrick
9 months ago

Bwana Yesu alinena kwa Lugha pale alipokuwa msalabani “Eloi Eloi lama sabakthan” Ukisoma Marko 15:34 na Mathayo 27:46