Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Kwanini Eliya alijulikana kama “Eliya Mtishbi”?

Je! Mtishbi ni jina la Baba yake au?

Jibu: Tishbi sio jina la mtu bali la mji, kama vile ulivyo mji wa Samaria au Nazareti.

Kwahiyo kama vile mtu aliyetoka mji wa Nazareti anavyoitwa Mnazareti, au aliyetokea mji wa Samaria anavyoitwa Msamaria, kadhalika mtu yeyote aliyetokea mji huo wa Tishbi aliitwa Mtishbi.

Mji huo wa Tishbi, ulikuwepo katika nchi ya Gileadi, iliyopo ng’ambo ya pili ya mto Yordani. Kwasasa ni maeneo ya nchi ya Yordani (Jordan).

Na katika mji huo mdogo wa Tishbi ndiko Nabii Eliya alikokulia na kuishi sehemu kubwa ya maisha yake.

1 Wafalme 17:1
“Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu”

Maandiko hayajaeleza kwa undani maisha ya Nabii Eliya, ya utotoni, na ujanani, na vile vile hayajaeleza kama alikuwa na mke au watoto.

Lakini kikubwa tunachoweza kujifunza kwa Nabii huyu, ni roho ya kuomba kwa bidii..mbali na kwamba Mungu alimtumia kwa viwango vya juu sana, lakini pia alikuwa ni mtu wa kuomba kwa bidii sana, maandiko yanasema hivyo..

Yakobo 5:16
“Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.

17 Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na mvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita.

18 Akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake”.

Na sisi tunajifunza tuwe watu wa kuomba kwa bidii kwasababu Eliya alikuwa ni MTU tu! Kama sisi na si malaika, au mtu fulani aliyeumbwa kipekee tofauti na sisi..alichokuwa na cha ziada ni bidii ya kuomba.

Hivyo na sisi tunajifunza tuwe watu wa kuomba kwa bidii, na sio tu kuomba bali pia kuombeana. Kwasababu kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana kama akiomba kwa bidii.

Bwana atujalie tuwe na bidii kama za hawa mashujaa wa Imani.

Maran atha!

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

Zeri ya Gileadi ni nini?

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments