Warumi 6:23
[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwenye vifungu hivyo tunaonyeshwa kuwa Mungu hutoa zawadi(karama), lakini dhambi inalipa mshahara.. Na mpaka ilipe mshahara ni lazima kazi fulani ilifanyika..
Watu wengi hawajua kuwa kila tendo moja la dhambi, huhesabu mshahara fulani na mwishoni mtu huyo hulipwa wote, hata kama hakujua.
Unapokwenda kuzini leo, unarudia tena na kesho, na kesho kutwa hivyo hivyo, mshahara unajilimbikiza, siku isiyo na jina utashangaa tu ghafla mshahara wako huo hapo umekufikia…
Ndio hapo mauti ya kiroho au ya kimwili au ya jambo fulani humfikia mtu.
Sasa inapofikia wakati wa mshahara wengi hujifanya haiwahusu, lakini utaupokea tu.. upende usipende…wengi humdharau Yuda kwanini alijinyonga, si kwamba alipenda lakini ulikuwa ni wakati wa mashahara, ukiona leo watu wanakutana na madhara makubwa kwasababu ya dhambi zao, sio kwamba wana bahati mbaya, bali ni wakati wa mshahara.
Epuka dhambi, ikimbie dhambi.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Print this post
Yeremia 2:13
[13]Kwa maana watu wangu hawa wametenda maovu mawili; wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji ya uzima, wamejichimbia mabirika, mabirika yavujayo, yasiyoweza kuweka maji.
Ndugu Ipo tofauti kati ya chemchemi na birika, chemchemi ni chanzo cha asili ambacho hutoa maji yake yenyewe, haihitaji kuchimbwa, wala kukarabatiwa lakini birika ni hivi visima ambavyo mtu hutumia jasho lake kuchimba na hutegemea mvua ili kuwa na maji, lakini bado huvujisha maji yake chini ya ardhi ndio maana baadaye hukauka…maji ya visima kikawaida hayawagi masafi sana kwasababu hayatembei, ni rahisi kuona vyura, ngala, ruba, tofauti na ya chemchemi.
Sasa Bwana anasema watu wake wamefanya makosa MAWILI. Kwanza wamemuacha yeye aliye chemchemi ya maji ya uzima, Maana yake wana kiu, lakini hawataki maji yaondoayo kiu…hicho huitwa kiburi, au dharau na matokeo ya kiburi ni maangamizi. Ni sawa na mtu anajijua kabisa ni mgonjwa halafu analetewa tiba anasema sinywi dawa zako.
Lakini kama hilo halitoshi, wanaenda kufanya kazi ya kuunda chemchemi zao bandia, kwa kuchimba wenyewe ili wajihifadhie maji yao ambayo ni ya muda…hii ndio huitwa ibada ya sanamu..watu wanapoona fedha inaweza kusimama badala ya Mungu, hiyo ni sawa na kujichimbia birika ..wanapoona elimu, ushirikina, anasa, ulevi, ujuzi..vinatosha kuwa mbadala wa Mungu ni kujichimbia birika lako mwenyewe..
Ndio maana wanataabika, kutafuta ukweli wote ndani yake hawapati, wanapata raha za kitambo baada ya hapo ni majuto kurudi.
Ndugu tulia kwa Kristo ambaye alishamaliza kuunda chemchemi yake, kwake yeye huhitaji kutendea kazi, nenda tu unywe maji, kiu ya dhambi na mambo mengine maovu ya kidunia ife, uishi maisha ya amani na kustawi. Maji hayo ukinywa hata ukifa utakuwa unaishi, na kumpokea Yesu ndio kuyapokea maji. Ukimwamini Yesu na kumfanya Bwana na mwokozi wa maisha yako, na kumtii baada ya hapo ujue ndani ya roho ya maji yameshawasili.
Yohana 4:13-14
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; [14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Achana na mabiriki.
Mungu atusaidie.
Mafundisho mengine:
Zaburi 42:8
[8]Mchana BWANA ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami,..
Biblia inataja nyakati mbili, ambazo mwamini anazipitia..nazo ni mchana na usiku.
Mchana ni nyakati za matumaini, nyakato za kuona njia, za kufanikiwa, za amani…hizi ni nyakati ambazo Bwana anasema ataagiza fadhili zake…maana ya fadhili ni kujitoa kwa upendo wa juu sana..Mungu huwafadhili watu wake hata katika nyakati za furaha, na amani.
Lakini pia anasema wakati wa usiku wimbo wake bado utakuwa nasi…usiku ni wakati wa huzuni, wakati wa upweke, wakati wa ukame wa kiroho, wakati wa majaribu, na mapito n.k.
Ni nyakati ambazo huoni chochote…kwasababu usiku sikuzote ni nyakati za ukimya na upofu..
Lakini pia huko Bwana anasema juu ya watu wake kuwa WIMBO WAKE, utakuwa pamoja nao.
Wimbo humaanisha faraja, kicheko, shangwe, yaani hatawaacha wawe kama walio gizani wanyonge, wapweke, bali kama watu wafurahishwao na nyimbo nzuri sana..
Kama mwana wa Mungu, nyakati za majaribu, Bwana yupo pamoja na wewe, nyakati ambazo huzielewi upo wimbo wake ndani yako.
Wakristo wafikiapo hatua hii huukimbia wimbo wa Bwana na kutazama zaidi changamoto zao, shida zao, magumu yao, na mengineyo kana kwamba Mungu amewaacha,
Lakini kama ukibakisha fikra zako kwake…utaona bubujiko kubwa sana likitiririka ndani yako, kwa jinsi ile ile ulivyokuwa katika nyakati za nuru..
Kwasababu hii ni ahadi yake. Na kamwe hawezi kudanganya. Unapojifunza kutulia uweponi mwa Mungu, kimaombi, kwa kutafakari, uwapo kwenye hizo nyakati hafifu..ghafla tu utaona furaha, amani, ushindi, kicheko, uwepo wa Bwana vinajaa ndani yako.
Kamwe usiukandamize wimbo huu?
UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.
JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
Yohana 13:34
[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..
Ni amri ipi hiyo mpya?
Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?
Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana
Mambo ya Walawi 19:18
[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.
Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…
“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”
Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.
Upendo wa upeo.
Yohana 13:1
[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.
Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..
Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..
Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo
Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.
Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.
Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)
Je amri hii mpya tunayo?
2 Yohana 1:5
Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
Bwana awe nawe.
Shalom.
NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.
JE UPENDO WAKO UMEPOA?
1 Samweli 30:6
[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake.
Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.
Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe,
Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe,
Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..
Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.
Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.
Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu.
Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.
Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.
Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.
Bwana akubariki
Wokovu ni kama farasi ambaye ana uwezo wa kusafiri kwa mwendo wa kasi sana au kwa mwendo wa taratibu sana, inategemea tu, nia ya mwendeshaji.
Halikadhalika Ikiwa wewe ni mshuhudiaji,(mhubiri wa injili) ni vema kufahamu tabia hizi, mara nyingi wokovu mpaka ukamilike ndani ya mtu, yaani kukubali toba, kuamini, kikiri, kubatizwa, kujazwa Roho, huweza kuchukua muda fulani wa wastani au mrefu kidogo, ambao huusisha kushawishi, kufuatilia, kufundisha madarasa mbalimbali imani, ya ubatizo na Roho Mtakatifu, n.k. ndipo aamini na kukamilishwa.
Lakini tembea pia ukijua kuwa si wakati wote hili litakuwa hivyo…
Zipo nyakati Mungu anabadili gia, atataka kukamilisha mambo yote hata kwa siku moja tu…yaani kumwokoa, kumbatiza na leo leo kumjaza Roho…Ukiona jambo hilo kamwe usijaribu kupunguza mwendo huo..Ni Mungu kaamua kuongeza kasi ya usafiri wake.
Je hili lipo kibiblia?
Ndio…wakati fulani Paulo na Sila walikamatwa na kutupwa gerezani, wakiwa kule usiku ule tunaona walianza kumwimbia Mungu na kumsifu sana…na mara vifungo vya gereza vikafunguka..yule askari msimamizi alipoona tukio lile aliogopa sana na kutetemeka…akasema nifanye nini ili niokoke? Wakawaambia wamwamini Bwana Yesu utaokoka. Na usiku ule ule walitubu, na kubatizwa nyumba yote, na kisha wakajazwa furaha ya Roho Mtakatifu yeye na nyumba yake yote..
Yaani kitendo cha usiku mmoja…familia nzima inaokoka, inabatizwa, inapokea tunda la Roho..
Matendo ya Mitume 16:27-34
[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. [28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. [29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; [30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? [31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. [32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. [33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo. [34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.
[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia.
[28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.
[29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;
[30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?
[31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.
[32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake.
[33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo.
[34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.
Kama ni mchakato, wengine humaliza hata wiki au miezi mpaka nyumba nzima kuamini na kubatizwa, ..lakini hapa ilikuwa ni masaa machache sana…tena ya usiku..
Utaona jambo kama hili lilijirudia kwa Kornelio..Petro alipoenda kwake, hata kabla hajamaliza mazungumzo yake, akidhani kuwa inahitaji madarasa marefu, inahitaji vyuo vya kuufafanua msalaba…pale pale katikati ya mazungumzo watu wakashukiwa na Roho Mtakatifu wakajazwa, wakapewa ile hatua ya mwisho kabisa ya wokovu ndipo wakaenda kubatizwa…(Matendo 10).
Mambo ambayo yamkini yangechukua madarasa ya muda na maombezi ya kuwekewa mikono ya kipindi kirefu..
Na yule mkushi aliyekutana na Filipo gaza naye vivyo hivyo hakusubiri kwanza alike kushi, pale pale njiani alibatizwa.
Matendo ya Mitume 8:36-39
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.] [38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. [39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
Vivyo hivyo, fahamu kuwa kuna nyakati Mungu anaisukuma mioyo ya watu kwa nguvu sana..tena sana kiasi kwamba mioyo yao hufunguka na kutamani kukamilishwa katika yote…
Ukiona hivyo, msaidie haraka, usifikiri kwamba inahitaji maarifa mengi ili mtu kuokolewa…bali moyo uliowazi..hilo tu..
Pengine wewe ni kiongozi..unaona mtu ameamini…usingoje ratiba za mwisho wa mwaka za ubatizo kanisa kwako…ndipo ambatize huyo mtu, angalia tu mwitikio wake…Ndio lipo pia kundi lingine ambalo litahitaji mafundisho kwanza…kutokana na viwango vyao vya upokeaji, ila usilisahau hili pia.
Jifunze kwenda na kasi zote za injili.
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
NI KIPI KINAKULEWESHA?
Biblia inaposema watu wakali hushika mali sikuzote, ina maana gani? (Mithali 11:16)
Kama tunavyofahamu katika maandiko Mitume walipofika mji wa Thesalonike kwa ajili ya injili, na kukutana na wenyeji wa mji ule, na kusikia walichokihubiri maandiko yanatuambia walipiga kelele sana na kusema maneno haya;
“Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako”
Matendo ya Mitume 17:6
[6]na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako,
Ulishawahi kutafakari kwa ukaribu maneno hayo walichokimaanisha?
Wanasema;
Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako,
Maana yake ni kuwa ulimwengu na wao, ni kama vitu viwili tofauti…
Wamefika na huku pia….yaani wameshaushinda ulimwengu wanakuja na huko kwao kumalizia walichokifanya kule..
Hii ikiwa na maana…mitume walishapata ushindi kabla hata ya kufika maeneo yote…
Kuna mahali pajulikanapo ulimwenguni ambapo tayari walishapashinda.
Sasa huo ulimwengu ni upi?
Chukulia mfano wa dunia ya sasa.. kuna usemi wasemao nchi za Afrika ni dunia ya tatu.. ijapokuwa wote tupo kwenye sayari moja, ujulikano dunia, lakini uhalisia dunia zipo tatu…Zile nchi zilizoendelea sana…Kama vile Marekani, urusi, China, ufaransa..ni dunia ya kwanza… na zile zilizo katika uchumi wa kati ni dunia ya pili na hizi maskini ni dunia ya tatu..
Sasa ikitokea mtu akayapiga hayo mataifa makubwa na kuyateka, maana yake huyo mtu ameiteka dunia, ameipindua dunia…..hata kama hajapigana na haya mengine madogo..lakini ikiwa nguvu zake zimewashinda wale basi hawa wengine ni maji tu.
Vivyo hivyo waamini wa wakati ule walionekana, wanamapinduzi wakubwa sana..kwasababu ushindi wao ulianzia kwenye vichwa.
Sasa huu ulimwengu ni upi?
JIBU: Ulimwengu wa Roho.
Zamani zile dini zilijulikana kama msingi mikubwa sana inayosukuma mielekeo ya mataifa.. hivyo Kristo alipokuja aliweza kuvunja misingi ya imani potofu na dhaifu kuanzia pale pale Israeli mpaka miisho ya dunia. Alileta Nuru duniani ambayo giza lolote halikuweza kulishinda..
Yohana 1:4-5
[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. [5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
[5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza.
Ndio maana kipindi cha injili utaona Wayahudi wengi waliokoka, wapagani wengi wakaacha miungu yao..wakaichoma moto, utaona hata kule Efeso mungu mke aliyeabudiwa ulimwenguni kote (Matendo 19:27), mitume walipofika habari yake ikaishia pale pale, tofauti na zamani manabii walishindana sana na mabaali lakini hawakuweza kuyashinda..kwasababu hakukuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mkuu wa ulimwengu huu(shetani)
Yohana 16:11
[11]kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
Hivyo ulimwengu wa roho uligeuzwa juu chini, mapepo yaliwakimbia wengi, watu walifunguliwa kwenye vifungo vya giza..makaburi waliwaachia wafu..kila siku watu waliongozeka kumjua Mungu…na kuachana na dhambi.
Matendo 19:19-20
[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. [20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu.
[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu.
[20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu.
Huu ndio ulimwengu sugu uliopata tiba…ulimwengu wa giza, kama kichwa cha mifumo yote mibovu ya dunia…uliwekwa chini…
Hivyo wale watu walipoona imani za watu zinageuzwa kwa kasi hata za maakida wakubwa,(Matendo 13:7-12) majemedari, watu wenye vyeo, wake kwa waume, nao pia wanaigeukia imani..wakatambua ya kuwa kila kitu kimekwisha sasa, sisi ni masalia..tu.
Walijiona kama mapanzi, ni sawa na wana wa Israeli walipoweza kuliangusha taifa la Misri, hata kabla ya kufika Yeriko, Wale watu wenyewe walishajiona kama mapanzi..Kwasababu kichwa cha ulimwengu kimeshaangushwa.
Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tujue kuwa sisi tuliomwamini Yesu…tayari tumeshaupindua ulimwengu kwa Injili iliyokwisha fika kuzimu kwenye kiti cha enzi wa shetani…
Hakuna chenye nguvu ya kutuzuia sisi tena, sisi ni watawala wa dunia.
Wanasiasi, hawawezi kutuzuia, wanadamu hawawezi kutusimamisha..wao ni kama mapanzi tu kwetu…
Hatuna budi kuuinua ujasiri wetu wote…tufikie mataifa yote kuhubiri injili kwasababu ulimwengu tayari tumeshaupindua…hatuhitaji kwenda tena kuupindua..sisi ni kumalizia tu masalia. Unasubiri nini usiamke kuihubiri injili? Amka sasa…
NI INJILI GANI UNAHUBIRI?
PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.
KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI
Kila mwanadamu maadamu amezaliwa na kuishi duniani, ndani yake lazima kuna kiwango tu cha majuto..
Wengine wana majuto makubwa sana, wengine kiasi.
Majuto ni hali ya kuhuzunishwa na matokeo ya machaguzi au maamuzi yaliyofanyika katika maisha.
Kwamfano kijana anaweza kuchagua kukatisha masomo kisha aende mtaani, kuuza peremende, sasa hayo ni maamuzi yake, lakini baadaye anapoona haoni matokeo makubwa, kinyume chake anawaona wenzake waliosoma wamepiga hatua kubwa anaanza kuingiwa na huzuni ya kujishitaki mwenyewe, sasa hayo ndio majuto.
Mwingine amechagua kuishi na mtu bila kufunga naye ndoa, hatimaye akazalishwa, watoto wengi na kuachwa..baadaye umri umeenda anataka kuoelewa, inakuwa shida…anaingiwa na majuto.
Mwingine amepoteza miaka mingi duniani kumtumikia shetani, sasa ameshakuwa mzee anajisikitikiza miaka yake ya ujana aliyoipoteza yenye nguvu alikuwa wapi asimtumikie Mungu…
Majuto yapo ya namna nyingi, na kila mtu kwa sehemu yake anayo majuto fulani, haijalishi unaishi wapi, au umefanikiwa vipi…kuna mahali ulikosea na yakaingia..
Kimsingi majuto sio dhambi, ni hali ya ki-Mungu kabisa ambayo mwanadamu ameumbiwa ndani yake..
Lakini ni vema kujua namna ya kuyaweka mahali pake..kwasababu yasipoweza kutenganishwa ipasavyo hupelekea hasara kubwa mno ndani ya maisha ya mtu.
Katika biblia kulikuwa na watu wawili ambao walihuzunishwa na maamuzi walillyoyafanya …mmoja ni Petro, mwingine ni Yuda.
Yuda alihuzunishwa lakini huzuni yake ilimpelekea kujinyonga…Petro alihuzunishwa lakini huzuni yake ilipelekea kulilia msaada wa Mungu..(badiliko)
Petro aliruhusu majuto yake yabebwe na Mungu, Yuda aliruhusu yabebwe na shetani.
Lakini majuto yalikuwa yale yale…Yuda hakukosea kujuta hadi kurudisha pesa
2 Wakorintho 7:8-11
[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu. [9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. [10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. [11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.
[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu.
[9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote.
[10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti.
[11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo.
Umeona Majuto ya ki-Mungu huleta toba.. lakini majuto ya shetani hupelekea mauti..
Ukishaanza kujiona kama wewe huwezi tena, Mungu kakuacha, hufai, huna maana, hustahili, ujue shetani yupo nyuma ya juto hilo, ambalo anataka kukusababishia usiinuke tena, ujitenge, ujiue, uache kwenda kanisani, aache maombi, uache kumtafuta Mungu, uache uchungaji …
Kinyume chake unapokosea jione kama ulikuwa unapitishwa katika funzo ambalo sasa unapewa nafasi nyingine usiitmie vibaya…
Watu wengi, unaowaona wamekata tamaa, wamepoa, hawana mabadiliko tena, wamejitenga, lakini hapo zamani walikuwa vizuri, wana mashaka na hofu ya ndani kwa ndani, asilimia kubwa ni majuto mabaya yanawasonga ndani yao.
Daudi alipoanguka katika dhambi ya uzinzi, alimrudia Bwana kwelikweli, ijapokuwa ilimgharimu pakubwa…hakwenda kujificha na uso wa Mungu kama Adamu.
Lakini ya ki-Mungu huturudisha kumtazama Mungu…Rudi umwangalie Mungu wako kisha chukua hatua nyingine, kwani hiyo huwa na nguvu na matokeo ya haraka zaidi ya mwanzo.
Petro baada ya pale alikuwa na ujasiri mkubwa wa kumshuhudia Kristo, zaidi ya mitume wengine wote, ikiwa umefeli mahali fulani embu amka tena kwa nguvu, usikubali kunyong’onyea kama Yuda na mfalme Sauli ambaye alijiua..
KUWA MWOMBOLEZAJI.
TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA
Maisha ya mwilini mara nyingi hubeba mafundisho ya rohoni, ndio maana Bwana Yesu alitumia sana mifano ya kidunia kuwafundisha siri za ufalme wa mbinguni.
Katika jamii ili mtu aitwe profesa au daktari(kitaaluma) anapaswa awe ni msomi wa kukaa darasani kwa muda mrefu, awe na ujuzi lakini pia na uzoefu wa tafiti nyingi..yaani kwa ufupi haiwezekani ukaitwa daktari(kitaaluma) halafu usiwe msomi wa elimu za juu.
Lakini kuna udaktari ambao mtu anaweza kupewa kwa kutunikiwa, na mara nyingi huu huja pale mtu anapotoa mchango fulani mkubwa katika jamii…mtu kama huyu anaweza kutunukiwa udaktari hata kama yale mafunzo ya ndani ya kitaaluma hana.
Sasa kiroho ni vivyo hivyo unaweza pia ukawa mkufunzi, mwenye ukomavu mkubwa, zaidi ya mababa zako wa kiroho, hata zaidi ya wachungaji wako, au maaskofu wako, au wazee wako wa kiimani, kwa namna gani?
Mstari ufuatao unatupa jibu;
Zaburi 119:99-100
[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote,
Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
Ukitafakari huo mistari, utaona ni mwanafunzi anayejisifia kuwa ana akili zaidi ya waalimu wake…sio kwamba ameshahitimu, hapana bado yupo chini ya waalimu wake lakini akili zake zimewapita, bado ni kijana lakini ufahamu wake umeshawazidi wazee wake.
Imewezekanikaje?
JE anasoma sana? Au ana kiwapa cha asili tofauti na wengine? Hapana…anasema kwasababu shuhuda za Mungu ndizo anazozitafakari, lakini pia anayashika mahusia ya Mungu .
Hiyo ndio siri yake, usiku na mchana ni kufikiri juu ya “KWELI”, Yaani Neno la Mungu, na na namna ya kulifanya kuwa sehemu ya maisha yake..(kujiepusha na dhambi.)
Hiyo ndio namna inayomkomaza mtu kiroho kwa haraka sana kuliko hata maarifa mengi ambayo wengi hudhani, au mafunuo mengi, au kuhubiri kwingi, au kufundisha kwingi…
Mtu mmoja anaweza akawa na uelewa mkubwa, mwalimu mzuri, mtume mwenye ushawishi mkubwa, lakini bado asimkute mwanafunzi wake ambaye maisha yake anajitahidi kuliishi Neno la Mungu.
Hivyo ndivyo Mungu anavyowatambua wakufunzi wake (kiroho), uwezo wa “kumcha Mungu” haijalishi utapoteza sifa nyingine zote za maarifa,mafunuo, lakini akiwa na hiyo huyo amefika mbali sana.
Kwasababu Biblia inasema hakuna mwisho wa usomi, (kujua maarifa), ila mtu akizingatia kumcha Mungu na kuziishika amri zake, ni zaidi ya usomi wa vitabu vyote.
Mhubiri 12:12-13
[12]Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. [13]Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
[12]Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.
[13]Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa;
Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
Tuwekeze nguvu zetu zote katika kuliishi Neno na neema ya Mungu itusaidie..
JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?
USIKWEPE CHUO CHA UTAKATIFU.
HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.
Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima
Tengeneza picha Mungu amekutokea amesimama mbele yako, wakati ukiwa na mawazo ya kumwangukia chini umsujudie, unashangaa yeye moja kwa moja anakuwa wa kwanza kuinama na kukusafisha miguu yako…
Hivi utajisikiaje? Ukweli ni kwamba hutajisikia huru hata kidogo, kwa ufupi hutakubali kitendo hicho kifanywe na yeye kutoka na ukuu wake, na heshima yake iliyozidi vyote, ni sawa na uone baba amemnunulia mtoto wake zawadi halafu yeye ndio anayekuwa wa kwanza kumshukuru mtoto, tena kwa kumwinamia..ni wazi kuwa hilo halijakaa sawa, au mtu aliyeibiwa mali zake nyingi, halafu amekutana na aliyemwibia badala ya mwenye mali kungojea kuombwa msamaha, yeye ndio anajionyesha kama ni mkosaji kwake…unaona ni jambo ambalo halina uhalisia, halikubaliki kifikra hata kidogo…
Kwa namna ya kawaida hali kama hizi akitendewa mtu hawezi kuridhia…lakini Mungu anatutendea sisi na anasema kama hutakubali kutendewa naye hivyo kamwe hutuna ushirika naye.
Ndicho kilichotokea kwa mitume na Petro. Wakati ule walipomwona Bwana Yesu, anashika kitambaa na maji kisha akaanza kuwaosha na kuwapangusa miguu yao…Petro hakuweza kuridhia akasema Bwana hutanitawadha miguu kamwe. Lakini Yesu akamwambia usipokubali huna ushirika nami.
Yohana 13:8
[8]Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami.
Hii ni kufunua nini…
Ni lazima tumjue Kristo, ni kweli anasimama kwetu kama mfalme, kama Bwana, kama Mungu…tunamwabudu…lakini pia anasimama kama mtumishi wetu..Ni jambo ambalo hatuwezi kuingia akilini lakini ndivyo alivyo, amependa yeye kuwa hivyo kwetu.
Ni mfalme mwenye taji la kifalme lakini wakati huo huo pia mfalme aliyebeba kitambaa cha kuwasafisha watu miguu.
Hiyo ndio sifa ya ufalme wake. Amesimama kama muumba wetu tumwabuduye, lakini pia anatutumikia, katika kutuponya magonjwa yetu, kutulisha, kutuvisha, kutuombea, kutulinda, kutufuta machozi, na kuchukua mizigo yetu mfano wa punda na hata kufanya mambo ambayo sisi hatuwezi stahimili akitufunulia yote kwa jinsi anavyojishusha na kujishughulisha sana na mambo yetu…. Na mfano tukitataa yeye asituhudumie hivyo anasema wazi kuwa hatuna ushirika naye.
Maana yake ni fahari yake kututendea hayo, wala yeye hayahesabu kuwa ni kitu.
Anatufundisha nini?
Tuwe watumishi pia wa wengine kwa namna hiyo, kama yeye alivyo kwetu…kujitoa kwake sio kutimiza wajibu bali ni fahari yake ambayo isipokubaliwa inaharibu moja kwa moja mahusiano.
Kumsaidia mpendwa mwenzako iwe ni furaha..kujinyenyekeza kwake isiwe ni sababu za umri au cheo bali fahari..Kumwombea iwe ni fahari yako, kumsikiliza iwe ni furaha yako…hivyo ndivyo Bwana anavyotaka.. na ndivyo alivyomwambia Petro.
Yohana 13:12-17
[12]Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? [13]Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. [14]Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. [15]Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. [16]Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka. [17]Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.
[12]Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea?
[13]Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.
[14]Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.
[15]Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.
[16]Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.
[17]Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.
Neema ya Bwana itusaidie.
WEWE NI ZAO LA MAHUSIANO NA USHIRIKA.
USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.
WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.