Kuishi ni tufoauti na kuwa na uhai. Hata mti ni hai, lakini hauishi. Kuishi ni maisha, yaani unasifa ya kuwa na mfumo au ustaarabu Fulani ambao unatembea nao, unaweza kuchagua mahali pa kukaa, unafanya kazi, unapumzika, unajenga, unapanda, unajichagulia burudani mfano miziki, michezo, vyakula, unafanya ibada, unauza, unanunua.. mambo kama hayo kiumbe kikitenda tunasema kinaishi.
Lakini kuwa kifungoni, ndani ya gereza huoni jua wala mwezi siku zako zote uwapo duniani, hatuwezi kusema unaishi, tunasema wewe upo hai, lakini hauishi.. Au unapokaa kwenye kitanda cha wagonjwa mauti-uti, umepooza, huwezi kuongea wala kutembea, umekata kauli, kwa sikuzote uwapo duniani, hayo si maisha ijapokuwa upo hai.
Sasa kuna maneno Yesu aliyasema, ambayo si wengi hujaelewa kwa undani na upana.. Tusome;
Yohana 11:25-26
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Hii kauli ukiisoma vizuri, unaweza ukasema inajichanganya, Embu tafakari, jambo la kwanza Yesu anasema, tukimwamini tukifa tutakuwa tunaishi, lakini pia tukiwa hai na kuamini hatutakufa kabisa hata milele.
Je! Sisi tuliomwamini hatufi?
Jibu ni Ndio hatufi kabisa, bali tunahamishwa makao. Hicho kinachoitwa kifo, ni macho ya wanadamu yanaona hivyo, lakini sisi tunakuwa kama tumefumba macho, kisha tukafumbua na kujikuta katika ulimwengu mwingine kabisa, Ndio maana lugha ambayo hutumika kueleza hali hiyo kwa watakatifu ni kulala (Matendo 7:54-60, 1Kor 15:51-58, Yohana 11:11-19)
Sisi tuliomwamini Yesu hatutaona kitu kinachoitwa kaburi, wala hatutajikuta kwenye gereza Fulani , bali kwenye ulimwengu mwingine mzuri sana uitwao pepo, sio tukiwa hai, bali tukiwa tunaishi kabisa huru.
Maana yake, tunaendeleza maisha, ikiwa kuna kutembea, huku na huko au kushughulika kwa vitu vya kimbingu, kufanya hivi, kufanya vile..Tutakuwa tunayafanya. Hayo ndio maisha anayosema mtu akimwamini yeye, ajapokufa (lala), atakuwa anaishi.. Si atakuwa na uhai
Tutakaa huko pepo, kwa kipindi chote, ambacho tunamsubiria Yesu, kulikamilisha kusudi la watakatifu wote, kisha baadaye,(mwisho ukifika), atakuja mwenyewe kuwachukua walio hai Pamoja na miili yetu tuliyoiacha duniani, na sote kwa Pamoja tutaanza ziara mpya ya kuelekea mbingu ya tatu. Makao yetu ya milele yalipo (2Wakorintho 12:2-4)
Lakini waovu wanapokufa, wenyewe watajiona kwanza wakiingia makaburini, kisha wakishuka kuzimu, Uhai wao ukitunzwa kwenye vifungo vya giza wasijue chochote, wala wasitende kazi yoyote, mpaka siku ya hukumu itakapofika, ambapo watatolewa huko kisha watasimama kwenye kiti cha enzi cheupe cha mwana-kondoo kwa ajili ya hukumu, (Ufunuo 20) baada ya kuhukumiwa ndipo watakapotupwa kwenye ziwa la moto, na kuangamia milele.
Sasa wakiwa huko kuzimu, ambapo kwa jina lingine kunaitwa Jehanamu, ni mahali pa shida, dhiki nyingi na mateso yasiyoelezeka, huko hakuna maisha, ni mateso tu vifungoni.
Hivyo ndugu, unapomwamini Yesu ipo faida kubwa zaidi ya unavyofikiri, unapokea MAISHA YA MILELE, Tangu ukiwa hapa duniani, ndani yako hakuna kitu kinachoitwa kifo, wala hutakihisi hata kidogo. Kwanini leo usimkaribishe maishani mwako? Ikiwa upo tayari basi wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba, bure.
Au sema sala hii kwa Imani, na Moja kwa moja Yesu ataingia moyoni mwako.
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
ASIYEMPENDA BWANA NA AWE AMELAANIWA.
Print this post
Maisha ya Imani, hayafuti dhiki, hayafuti hisia za kibinadamu, haijalishi mtu atakuwa na ukomavu mkubwa kiasi gani, bado mahangaiko ya ndani na nje, zipo nyakati atakutana nayo.
Mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, pamoja na kuwa walitumiwa na Mungu kipekee sana na neema ya Mungu kubwa kukaa juu yao. Bado walikiri kwa wazi kabisa bila maficho dhiki ziliwasonga kote kote,
2 Wakorintho 7:5
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Paulo anasema nje kulikuwa na vita, maana yake maadui, walioshindana naye, kuipinga imani, kutaka kumuua, kumfunga walikuwa ni wengi sana…lakini pia ndani anasema kulikuwa na hofu si nje tu,..akiwa na maana hofu ya kwenye nafsi..mfano wa hizi ni kama vile hofu za majukumu, hofu za kusalitiwa, hofu za kuvunjwa moyo, kuachwa peke yako, za kuvamiwa na wezi, mashaka ya ugenini, kushtakiwa, hofu za mwili kudhoofika, kuugua n.k. ambazo kimsingi kazi yake ni kukufanya ukate tamaa, usisonge mbele, usizae matunda.
Ndivyo ilivyo hata kwa watumishi wa Mungu wa kweli leo, mbele ya macho ya watu wanaweza kuonekana ni watu walio- mbali na mateso, lakini kwa mujibu wa kibiblia mioyoni mwao, vipo vita vingi na hofu kote kote…
Sasa swali ni je! Wanaweza kuishi na kuendelea na imani au huduma bila kukata tamaa wakiwa katika viwango vilevile ilihali nje vita ndani hofu?
Jibu ni kuwa Bwana..huwatumia faraja kwa njia mbalimbali, na faraja hizo ni kama zifuatazo;
Paulo katika dhiki zake anasema;..Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Wakorintho 7:5-7
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu. [6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito. [7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
[6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
[7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
Ni ukweli usiopingika zipo nyakati ambazo unajihisi kama kuishiwa nguvu ya kuendelea aidha na wokovu au huduma, kwasababu ya hali fulani ngumu zinazokuzunguka..
Majira kama haya, Mungu hufanya njia, habari njema za faraja zinaweza kukufikia na kukutia nguvu na hatimaye kuendelea mbele kwa hamasa mpya.
Kwamfano Paulo alikuwa katika nyakati hizo mbaya, akiona kama taabu yake kwa Mungu ni bure, hakuna matunda, lakini ghafla analetewa taarifa na Tito ya wanafunzi wake huko Korintho wamebadilika, wamesimama imara zaidi sana wana shauku naye. Hilo lilimtia nguvu tena hata kujiona tena hayupo katika dhiki.
Kwamfano unaweza ukawa unafanya huduma kwa muda mrefu, na pengine huoni matokeo uliyoyategemea, lakini ghafla unakutana na mtu anakuambia nimebadilishwa sana na huduma yako au mafundisho yako. Wakati ule unafanya maombezi nilipona ile ugonjwa, ulipokuwa unahubiri niliguswa moyoni na sasa nimeokoka.
Hiyo ni faraja kubwa sana, na kama ulikuwa umelegea unaamka tena unasema…oh! Kumbe Bwana yupo pamoja nami.
Nyakati za uzito, nyakati za dhiki, Bwana huachilia mafunuo kwa njia mbalimbali ili kukufariji katika wokovu wako au huduma yako aidha anaweza kutumia ndoto au maono, au Neno, au hata fundisho fulani kama hili unalolisoma sasa…
Paulo alipokuwa kama mfungwa anaelekea Rumi, njiani Meli ilipata shida mpaka wakakata tamaa ya kuishi..lakini Mungu alimtokea na kumtia nguvu kwa maono.
Matendo ya Mitume 27:23-24
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, [24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
[24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
Ni kawaida ya Mungu, kutufariji kwa njia za mafunuo, wewe ni mchungaji Bwana kukuonyesha ukichunga watu wengi, litakuwa ni jambo la kawaida, au anaweza kukupa andiko ambalo, litakupa sababu ya kusimama au kuendelea mbele. Au wakati mwingine hata kutumia mtumishi wake kukufundisha, na lile fundisho likawa ni nanga kubwa sana kwako, kutembea katika aina yoyote ya mapito.
Hii ni namna nyingine ambayo Mungu huwafariji watumishi wake, huwafungulia milango ya kifedha, aidha kusaidiwa na watu wa amani mahali fulani kimahitaji.
2 Wakorintho 11:9
[9]Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
Ni kawaida ya Mungu, nyakati fulani kufungua milango ya kupokea vitu kwa watu wake, lengo lake ni kukufariji, kukutia moyo ili usonge mbele katika kazi yake.
Hii ni njia nyingine ambayo Bwana huitumia sana, kutukumbusha mioyoni mwetu kuwa hizi taabu ni za kitambo, Bwana wetu ametuandalia makao na siku moja atarudi, nasi tutaishi naye milele na milele mbinguni.. katika maisha ya milele yasiyokuwa na fujo..Bwana anataka tuyakumbuke hayo, tufarijike.
1 Wathesalonike 4:16-18
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. [17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. [18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
[17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
[18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
Sikuzote kumbuka kuwa furaha yetu, urithi wetu, utajiri wetu upo kule ng’ambo unatungoja, hapa duniani ni wasafiri, hivyo hatutaona shida tuwapo katika dhiki za muda mfupi…Ni sawa na umeingia katika nyumba ya wageni, halafu ukaona mazingira si safi, aidha ya choo au vyumba..huwezi kulalamika na kuanza kusoneneka na kutaabika sana, kana kwamba umeingia kwenye matatizo makubwa…hapana utavumilia tu.kwasababu unajua hapo sio kwako, unapita tu utalala siku moja kesho yake utaondoka..na kurudi kwako palipo pasafi..hivyo utavumilia.
Bwana akutie nguvu. Songa mbele katika imani.
Amen.
MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU
WALAKINI MIMI SI PEKE YANGU.
LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.
Mathayo 8:29
[29]Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Mashetani yanajua kila jambo lipo katika mpangilio wa muda wake, yanajua kuwa tayari hukumu ilishatolewa ya wao kutupwa katika ziwa la moto lililo hatma yao ya milele..
Lakini utekelezaje wake, utakuja baadaye, ambao utakuwa ni mwisho wa dunia, utakao asisiwa na Bwana Yesu Kristo mwenyewe.(Mathayo 25:41)
Wengi tunadhani mapepo, hushindana na sisi, kwa kutuonea wivu, hilo ni kweli kwa sehemu, lakini sababu kubwa ya mapepo na shetani kushindana na sisi…ni wao kujilinda…na adhabu ijayo.
Na wanajua mwanadamu ndiye anayeweza kuiharakisha hiyo siku au kuikawiisha hiyo siku. Ndio maana yanafanya kazi kubwa sana kuwaharibu wanadamu ili siku hiyo isifike upesi.
Hizi ni njia tatu mapepo, hufanya kwa watu ili kukawiisha muhula wao usiwafikie haraka.
1) Kuchochea maovu.
2) Kukengeusha Imani za watu
3) Kukawisha injili
Maovu mengi, humsukuma Mungu kuwa mvumilivu na wanadamu, ili wafikie toba wasiangukie hukumu ya mapepo..Kama wanadamu wasingekuwa na shingo ngumu, mwisho wa dunia na hukumu yao ingeshafika zamani sana.. hivyo mapepo wanabuni kazi mbalimbali ili kuwafanya wanadamu wazidi kupotoka.
2 Petro 3:9-11
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. [10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. [11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
Luka 18:8
[8]Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Kristo anatarajia kanisa lake kusimama katika msingi wa imani kamili ambayo haijaharibiwa wala kuvurugwa na mapokeo na mafundisho ya uongo.. hii ndio sababu ya shetani kuinua makundi ya manabii wa uongo, kufundisha injili nyingine ambayo Kristo hajaileta duniani. Matokeo yake ndio kuwa na kundi kubwa la wakristo lakini dhaifu wasio tayari kumlaki Bwana mawinguni.
Mathayo 24:14
[14]Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Injili ya kweli adui huipiga vita vikubwa..Na wanajua ikihubiriwa ulimwenguni kote, basi ushuhuda wa Mungu utakuwa umefika na hakuna atakayekuwa na udhuru.
Sasa mimi na wewe hatuna budi kusimama katika utakatifu lakini pia imani na injili kuisambaza ili watu waokolewe…
Kumbuka tayari tupo kwenye siku za mwisho, Amka simama na Bwana.
MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.
Je mkristo anaweza akawa na mapepo?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?
Neno utakaso mara nyingi, tunalitazama katika jicho la Mungu kututakasa sisi(1Thes 5:23), lakini pia sisi kujitakasa wenyewe (1Petro 1:22), lakini tunasahau kuwa Kristo naye tunamtakasa… maandiko yanasema hivyo katika,
1 Petro 3:14
[14]Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.
Kama Kristo anatakaswa? Swali ni je! Anatakaswaje wakati yeye ni mkamilifu?
Hapo anasema;
‘mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu’.
Kumbe ni mioyoni mwetu, sio kwamba yeye mwenyewe tumtakase mahali alipo(hawezi kutakaswa kwasababu yeye ni msafi). Mioyo yetu ndio humfanya aonekane kivingine.
Kutakasa ni kukifanya kitu kiwe kisafi au kiwe kikamilifu tena, kurejee katika hadhi yake iliyopotezwa.
Sasa kumtakasa Yesu moyoni, ni sawa na kumfanya Yesu awe jasiri tena, ajae utukufu wake, ajawe na raha na fahari yote ndani ya mtu.
Haya ni mambo ambayo ukiyatenda/ kuyakubali basi unamtakasa sana Yesu moyoni mwako
Sawasawa na hilo andiko hapo juu anasema..
Zipo nyakati ambazo utachukiwa bure kwasababu umekataa uongo, au utafukuzwa kazi kwasababu umekataa rushwa, au utafungwa kwasababu unahubiri injili ,au utapigwa kwasababu unakemea dhambi..
Nyakati kama hizi wengine huzikwepa, na kuamua kusimama na maovu ili tu kuepusha madhara yatakawapata… hawajui kuwa wanamweka Kristo kando.
Matokeo yake Yesu anakosa kutukuzwa ndani yetu, kwasababu yeye naye alikubali kuteswa kwa kusimamia ukweli na haki, akapigwa, akasulubiwa kwa kifo cha aibu.. Hivyo atakapoona watu pia wanafuata Nyayo zake, hutakasika sana, hujitukuza sana ndani ya huyo mtu, hujithibitisha kuwa kazi yake kamilifu huendelea kumulika gizani.
Hivyo usikwepe mapito yenye gharama, wala usihuzunishwe nayo maadamu ni haki unayoisimamia. Mtakase Kristo.
Lakini pia..
Waefeso 1:6-7
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa. [7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
[6]Na usifiwe utukufu wa neema yake, ambayo ametuneemesha katika huyo Mpendwa.
[7]Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.
Kwa jinsi unavyoitambua kazi ya Kristo aliyoitenda kwa ajili yako pale msalabani kwamba kwa kupigwa kwake umepokea neema na ukombozi kupitia msamaha wa dhambi ndivyo unavyomtakasa Kristo moyoni mwako.
Tumia muda mwingi kutafakari juu ya neema ya wokovu, kisha msifu na kumtukuza na kumshukuru juu ya hilo. Kristo anapoona umeithamini kazi yake, huinuka sana moyoni mwako.
Utakumbuka yule mwanamke kahaba na Miriamu ndugu yake Martha walivunja vibweta vya marhamu vyenye thamani nyingi, wakampaka Yesu kichwani na miguuni, mpaka wengine wakasema ni upotevu mkubwa sana..lakini Yesu alipoona alisema wametenda kazi njema juu yake, (Marko 14:3-9, Luka 7:36-50).
Jifunze kumtolea Kristo sadaka zaidi hata kipimo chako cha sikuzote, sio kwamba unamshawishi Yesu kwa vitu, (yeye hashawishi na hivyo)..Lakini anapendezwa sana, na watoaji, anatakasika sana pale unapofanya kitu cha ziada kwa ajili ya Mungu wako. Jifunze kutoa sana sadaka.
Yesu anajaa utukufu na waombaji…utakumbuka alikuwa na mitume kumi na wawili…lakini waliokuwa tayari kudumu naye katika masafa ya ndani ya kimaombi walikuwa ni watatu; yaani Petro Yohana na Yakobo.
Na wakati ule alipopanda juu ya ule mlima mrefu(Mathayo 17), ghafla walimwona katika utukufu mwingine wa ajabu, nguo zake zilikuwa zikimeta-meta kwa weupe mkuu.. wakashangaa na kuingiwa na hofu..
Lakini Yesu asingeweza kubadilika mbele yao, kama wangekuwa mbali na yeye katika maombi.
Hivyo unapozama sana katika uombaji, ndivyo unavyomtakasa Kristo ndani yako. Anajiona safi na mkamilifu.
Kwa hitimisho ni kuwa, unapokubali mateso pamoja na Yesu, unapo msifu sana kwa kazi yake ya msalaba, unapotoa sadaka zako nyingi na unapokuwa mwombaji.
Moyoni unahesabika kuwa unamtakasa Bwana wako sana.
Shalom, Mungu akubariki.
WALAWI WALIKUWA WENYE MIOYO YA ADILI KWA KUJITAKASA KULIKO MAKUHANI.
Kanisa kama sehemu ya maisha ya mwamini mpya.
SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI
Warumi 6:23
[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwenye vifungu hivyo tunaonyeshwa kuwa Mungu hutoa zawadi(karama), lakini dhambi inalipa mshahara.. Na mpaka ilipe mshahara ni lazima kazi fulani ilifanyika..
Watu wengi hawajua kuwa kila tendo moja la dhambi, huhesabu mshahara fulani na mwishoni mtu huyo hulipwa wote, hata kama hakujua.
Unapokwenda kuzini leo, unarudia tena na kesho, na kesho kutwa hivyo hivyo, mshahara unajilimbikiza, siku isiyo na jina utashangaa tu ghafla mshahara wako huo hapo umekufikia…
Ndio hapo mauti ya kiroho au ya kimwili au ya jambo fulani humfikia mtu.
Sasa inapofikia wakati wa mshahara wengi hujifanya haiwahusu, lakini utaupokea tu.. upende usipende…wengi humdharau Yuda kwanini alijinyonga, si kwamba alipenda lakini ulikuwa ni wakati wa mashahara, ukiona leo watu wanakutana na madhara makubwa kwasababu ya dhambi zao, sio kwamba wana bahati mbaya, bali ni wakati wa mshahara.
Epuka dhambi, ikimbie dhambi.
Shalom
WhatsApp
Yeremia 2:13
[13]Kwa maana watu wangu hawa wametenda maovu mawili; wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji ya uzima, wamejichimbia mabirika, mabirika yavujayo, yasiyoweza kuweka maji.
Ndugu Ipo tofauti kati ya chemchemi na birika, chemchemi ni chanzo cha asili ambacho hutoa maji yake yenyewe, haihitaji kuchimbwa, wala kukarabatiwa lakini birika ni hivi visima ambavyo mtu hutumia jasho lake kuchimba na hutegemea mvua ili kuwa na maji, lakini bado huvujisha maji yake chini ya ardhi ndio maana baadaye hukauka…maji ya visima kikawaida hayawagi masafi sana kwasababu hayatembei, ni rahisi kuona vyura, ngala, ruba, tofauti na ya chemchemi.
Sasa Bwana anasema watu wake wamefanya makosa MAWILI. Kwanza wamemuacha yeye aliye chemchemi ya maji ya uzima, Maana yake wana kiu, lakini hawataki maji yaondoayo kiu…hicho huitwa kiburi, au dharau na matokeo ya kiburi ni maangamizi. Ni sawa na mtu anajijua kabisa ni mgonjwa halafu analetewa tiba anasema sinywi dawa zako.
Lakini kama hilo halitoshi, wanaenda kufanya kazi ya kuunda chemchemi zao bandia, kwa kuchimba wenyewe ili wajihifadhie maji yao ambayo ni ya muda…hii ndio huitwa ibada ya sanamu..watu wanapoona fedha inaweza kusimama badala ya Mungu, hiyo ni sawa na kujichimbia birika ..wanapoona elimu, ushirikina, anasa, ulevi, ujuzi..vinatosha kuwa mbadala wa Mungu ni kujichimbia birika lako mwenyewe..
Ndio maana wanataabika, kutafuta ukweli wote ndani yake hawapati, wanapata raha za kitambo baada ya hapo ni majuto kurudi.
Ndugu tulia kwa Kristo ambaye alishamaliza kuunda chemchemi yake, kwake yeye huhitaji kutendea kazi, nenda tu unywe maji, kiu ya dhambi na mambo mengine maovu ya kidunia ife, uishi maisha ya amani na kustawi. Maji hayo ukinywa hata ukifa utakuwa unaishi, na kumpokea Yesu ndio kuyapokea maji. Ukimwamini Yesu na kumfanya Bwana na mwokozi wa maisha yako, na kumtii baada ya hapo ujue ndani ya roho ya maji yameshawasili.
Yohana 4:13-14
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; [14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Achana na mabiriki.
Mungu atusaidie.
Zaburi 42:8
[8]Mchana BWANA ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami,..
Biblia inataja nyakati mbili, ambazo mwamini anazipitia..nazo ni mchana na usiku.
Mchana ni nyakati za matumaini, nyakato za kuona njia, za kufanikiwa, za amani…hizi ni nyakati ambazo Bwana anasema ataagiza fadhili zake…maana ya fadhili ni kujitoa kwa upendo wa juu sana..Mungu huwafadhili watu wake hata katika nyakati za furaha, na amani.
Lakini pia anasema wakati wa usiku wimbo wake bado utakuwa nasi…usiku ni wakati wa huzuni, wakati wa upweke, wakati wa ukame wa kiroho, wakati wa majaribu, na mapito n.k.
Ni nyakati ambazo huoni chochote…kwasababu usiku sikuzote ni nyakati za ukimya na upofu..
Lakini pia huko Bwana anasema juu ya watu wake kuwa WIMBO WAKE, utakuwa pamoja nao.
Wimbo humaanisha faraja, kicheko, shangwe, yaani hatawaacha wawe kama walio gizani wanyonge, wapweke, bali kama watu wafurahishwao na nyimbo nzuri sana..
Kama mwana wa Mungu, nyakati za majaribu, Bwana yupo pamoja na wewe, nyakati ambazo huzielewi upo wimbo wake ndani yako.
Wakristo wafikiapo hatua hii huukimbia wimbo wa Bwana na kutazama zaidi changamoto zao, shida zao, magumu yao, na mengineyo kana kwamba Mungu amewaacha,
Lakini kama ukibakisha fikra zako kwake…utaona bubujiko kubwa sana likitiririka ndani yako, kwa jinsi ile ile ulivyokuwa katika nyakati za nuru..
Kwasababu hii ni ahadi yake. Na kamwe hawezi kudanganya. Unapojifunza kutulia uweponi mwa Mungu, kimaombi, kwa kutafakari, uwapo kwenye hizo nyakati hafifu..ghafla tu utaona furaha, amani, ushindi, kicheko, uwepo wa Bwana vinajaa ndani yako.
Kamwe usiukandamize wimbo huu?
UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.
JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
Yohana 13:34
[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..
Ni amri ipi hiyo mpya?
Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?
Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana
Mambo ya Walawi 19:18
[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.
Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…
“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”
Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.
Upendo wa upeo.
Yohana 13:1
[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.
Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..
Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..
Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo
Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.
Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.
Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)
Je amri hii mpya tunayo?
2 Yohana 1:5
Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
Bwana awe nawe.
Shalom.
NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.
JE UPENDO WAKO UMEPOA?
1 Samweli 30:6
[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake.
Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.
Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe,
Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe,
Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..
Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.
Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.
Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu.
Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.
Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.
Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.
Wokovu ni kama farasi ambaye ana uwezo wa kusafiri kwa mwendo wa kasi sana au kwa mwendo wa taratibu sana, inategemea tu, nia ya mwendeshaji.
Halikadhalika Ikiwa wewe ni mshuhudiaji,(mhubiri wa injili) ni vema kufahamu tabia hizi, mara nyingi wokovu mpaka ukamilike ndani ya mtu, yaani kukubali toba, kuamini, kikiri, kubatizwa, kujazwa Roho, huweza kuchukua muda fulani wa wastani au mrefu kidogo, ambao huusisha kushawishi, kufuatilia, kufundisha madarasa mbalimbali imani, ya ubatizo na Roho Mtakatifu, n.k. ndipo aamini na kukamilishwa.
Lakini tembea pia ukijua kuwa si wakati wote hili litakuwa hivyo…
Zipo nyakati Mungu anabadili gia, atataka kukamilisha mambo yote hata kwa siku moja tu…yaani kumwokoa, kumbatiza na leo leo kumjaza Roho…Ukiona jambo hilo kamwe usijaribu kupunguza mwendo huo..Ni Mungu kaamua kuongeza kasi ya usafiri wake.
Je hili lipo kibiblia?
Ndio…wakati fulani Paulo na Sila walikamatwa na kutupwa gerezani, wakiwa kule usiku ule tunaona walianza kumwimbia Mungu na kumsifu sana…na mara vifungo vya gereza vikafunguka..yule askari msimamizi alipoona tukio lile aliogopa sana na kutetemeka…akasema nifanye nini ili niokoke? Wakawaambia wamwamini Bwana Yesu utaokoka. Na usiku ule ule walitubu, na kubatizwa nyumba yote, na kisha wakajazwa furaha ya Roho Mtakatifu yeye na nyumba yake yote..
Yaani kitendo cha usiku mmoja…familia nzima inaokoka, inabatizwa, inapokea tunda la Roho..
Matendo ya Mitume 16:27-34
[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. [28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. [29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; [30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? [31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. [32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. [33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo. [34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.
[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia.
[28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.
[29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;
[30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?
[31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.
[32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake.
[33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo.
[34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.
Kama ni mchakato, wengine humaliza hata wiki au miezi mpaka nyumba nzima kuamini na kubatizwa, ..lakini hapa ilikuwa ni masaa machache sana…tena ya usiku..
Utaona jambo kama hili lilijirudia kwa Kornelio..Petro alipoenda kwake, hata kabla hajamaliza mazungumzo yake, akidhani kuwa inahitaji madarasa marefu, inahitaji vyuo vya kuufafanua msalaba…pale pale katikati ya mazungumzo watu wakashukiwa na Roho Mtakatifu wakajazwa, wakapewa ile hatua ya mwisho kabisa ya wokovu ndipo wakaenda kubatizwa…(Matendo 10).
Mambo ambayo yamkini yangechukua madarasa ya muda na maombezi ya kuwekewa mikono ya kipindi kirefu..
Na yule mkushi aliyekutana na Filipo gaza naye vivyo hivyo hakusubiri kwanza alike kushi, pale pale njiani alibatizwa.
Matendo ya Mitume 8:36-39
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? [37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.] [38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. [39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
Vivyo hivyo, fahamu kuwa kuna nyakati Mungu anaisukuma mioyo ya watu kwa nguvu sana..tena sana kiasi kwamba mioyo yao hufunguka na kutamani kukamilishwa katika yote…
Ukiona hivyo, msaidie haraka, usifikiri kwamba inahitaji maarifa mengi ili mtu kuokolewa…bali moyo uliowazi..hilo tu..
Pengine wewe ni kiongozi..unaona mtu ameamini…usingoje ratiba za mwisho wa mwaka za ubatizo kanisa kwako…ndipo ambatize huyo mtu, angalia tu mwitikio wake…Ndio lipo pia kundi lingine ambalo litahitaji mafundisho kwanza…kutokana na viwango vyao vya upokeaji, ila usilisahau hili pia.
Jifunze kwenda na kasi zote za injili.
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
NI KIPI KINAKULEWESHA?
Biblia inaposema watu wakali hushika mali sikuzote, ina maana gani? (Mithali 11:16)