Swali: Je ni vema sisi tuliookoka kushika matawi siku ya jumapili na kuingia nayo kanisani au kutembea nayo?
Jibu: Jumapili ya mitende ni jumapili moja kabla ya jumapili ya pasaka, ambapo katika historia ni siku ambayo KRISTO aliingia YERUSALEMU, na watu wakakata matawi ya mitende na kuyatandaza njiani ili Bwana YESU apite. (kumbuka, mtende ni mti unaozaa matunda ya tende).
Mathayo 21:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,
2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana punda pamoja naye; wafungueni mniletee.
3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.
6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; NA WENGINE WAKAKATA MATAWI YA MITI, WAKAYATANDAZA NJIANI.
9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.
10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?
11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya”.
Sasa swali ni je! Na sisi ni sahihi/ruksa kuisheherekea/kuiadhimisha hii siku?
Jibu: Hatujapewa agizo lolote kwenye Biblia la kuiadhimisha jumapili ya mitende, wala jumapili ya pasaka. Isipokuwa kutokana na umuhimu wa hizo siku katika historia ya Ukristo, si vibaya kuzifanya hizo siku/tarehe kuwa za ibada ya kutafakari mambo yaliyotokea wakati huo.
Kwamfano katika jumapili ya mitende, ni wakati ambao watu walimsifu YESU kwa kumwimbia Hosana Hosana (yaani Okoa). Nasi kwa kutafakari jambo hilo twaweza kutengeneza kama igizo la wakati huo, na kumwimbia Bwana kwa furaha tukisema Hosana amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la BWANA, kwa kufanya hivyo huku tumeshika matawi ya mitende sio kosa wala dhambi kwani ni sehemu ya sifa tu kama sifa nyingine zinazohusisha shangwe za kurusha rusha leso juu au matawi ya miti.
Lakini matawi yale yakifanyika kama ni vitu vitakatifu, (kwamba vimebeba nguvu Fulani ya kiungu, kama vile sanamu zinazowekwa kwenye baadhi ya makanisa) hilo ni kosa, kwani tayari hizo ni ibada za sanamu, na si tena kwa lengo la sifa za kumtukuza MUNGU.
Utakuta mtu anatembea na tawi lile si kwa lengo la sifa, wala tafakari ya mambo yaliyotokea miaka elfu mbili iliyopita, bali kama kisaidizi cha kuondoa mikosi, au matatizo, au cha kufukuzia wachawi n.k Huyu mtu anakuwa anafanya ibada za sanamu, na inaweza isiwe ni kosa lake bali la waliomfundisha.
Kwahiyo jumapili ya mitende si vibaya kuadhimishwa ikiwa itafanyika kwa ufunuo na maarifa namna hiyo, lakini kama itafanyika kidini na kidesturi, inageuka kuwa ibada ya sanamu, jambo ambalo ni machukizo kwa BWANA.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.
MUNGU AKETIYE MAHALI PA JUU PALIPOINUKA.
Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)
Jibu: Turejee maandiko machache..
“Uhai” ni hali ya kuwa “HAI” (yaani kuishi) ili kiumbe kiwe kinaishi ni lazima kipumue, kile, kikue na hata kijongee. Hizo ndizo tabia chache za viumbe HAI, Wanadamu, wanyama na mimea vyote vina uhai kwasababu vinapumua, vinaongezeka na pia kujongea.
Lakini “UZIMA” Umeenda mbali zaidi kuelezea UHAI wa kiroho ambao unapatikana kwa mtu kuwa na mahusiano na MUNGU.
Uhai unaelezea mwili lakini Uzima unaelezea roho. Mimea haina UZIMA bali ina UHAI.. wanyama hawana UZIMA bali wana UHAI maandiko yanaonyesha hivyo…
Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri UHAI WA MNYAMA WAKE; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.
Na UZIMA unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO,
Yohana 10:10 “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, kisha wawe nao tele”.
ikiwa na maana kuwa wanadamu yoyote aliye nje ya YESU KRISTO anao “Uhai” tu kama wanyama lakini hawana “Uzima”… anapumua, anakula, anatembea lakini akisha kufa hana UZIMA tena.. Lakini aliye ndani ya KRISTO, hata akiwa amekufa ataendelea kwasababu anao UZIMA wa MILELE alioupokea kutoka kwa YESU.
Je unao uzima wa milele ndani yako?…Je YESU ni sehemu ya maisha yako?
Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape UZIMA WA MILELE.
3 Na UZIMA WA MILELE ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.
Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, SHUKA UPESI, KWA KUWA LEO IMENIPASA KUSHINDA NYUMBANI MWAKO.
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.
YESU hawezi kuingia nyumbani kwako kama “hutashuka kwenye Mkuyu”..
Mkuyu ni kitu chochote kijiinuacho juu ya YESU,…. Kiburi cha mali ni mkuyu,… kiburi cha cheo ni mkuyu, kiburi cha uzuri ni Mkuyu n.k.. Mtu anavyovitumia hivi ili kumwona Bwana YESU au kumtumikia, Kristo yeye anaenda kinyume navyo..
Zakayo asingeweza kuzungumza na Bwana akiwa juu ya mkuyu..ilimpasa ashuke upesi… Sauti ile ilikuwa na mamlaka, ilipenya katika moyo wa Zakayo na kumfanya ashuke si tu chini ya Mkuyu, bali hata kiburi chake chote, kwani alikuwa ni mtu mkubwa kifedha…
Alipokubali tu kushuka na kiburi chake cha mali nacho kikashuka, kiburi chake cha cheo kikashuka akawa mtu mwingine, mnyenyekevu na YESU akaingia nyumbani mwake..
Nusu ya mali yake aliwapa maskini na wote aliowadhulumu aliwarudishia mara nne.
Luka 19:6 “Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.
8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.
Na wewe leo, shuka chini ya Mkuyu.. kiburi cha Elimu kinaweza kuwa kizuizi cha Kristo kutembea na wewe, kiburi cha pesa kinaweza kuwa kikwazo cha YESU kuingia kwako, kiburi cha cheo na uzuri ni hivyo hivyo, lakini unyenyekevu unaleta Neema.
Yakobo 4:6 “Lakini hutujalia sisi neema iliyozidi; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
ALIYOKUTANA NAYO YESU, YERIKO.
LEO WOKOVU UMEFIKA NYUMBANI HUMU
Zekaria 10:1 “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni”.
Umewahi kujiuliza kwanini hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana mvua WAKATI WA MASIKA” na si wakati mwingine wowote kama kiangazi?..
Ni kwasababu msimu wa masika ni msimu wa mvua, hivyo inapotokea hakuna mvua si jambo la kawaida, kwahiyo tukiomba mvua msimu huo ni hoja yenye nguvu, lakini tunapoomba mvua msimu wa kiangazi zinakuwa si hoja zenye nguvu!.. Ndicho maandiko yanachokimaanisha hapo.
Maombi ya kuomba kwa wakati ni mazuri na yana majibu ya haraka kuliko yale ya kuomba nje ya msimu/majira.
Unaomba mume/mke na bado ni mwanafunzi, unaomba mali na bado unasoma, unaomba umtimikie MUNGU na bado hujaokoka!, maombi ya namna hiyo ni nadra sana kujibiwa!.. ni wachache sana wanaojibiwa hayo maombi!!.. sio kwamba ni maombi mabaya au vinavyoombwa ni vitu vibaya!. La! Ni vizuri lakini vinaombwa nje ya majira yake.
Hapo maandiko yanasema “Mwombeni Bwana Mvua wakati wa Masika”.. Maana yake ni lazima ujue uhusiano wa kile unachomwomba MUNGU na majira uliyopo. Kama kitu bado majira yake usitumie nguvu kubwa kuomba, shughulika na vile ambavyo sasa ndio majira yake.
Kama wewe ni mwanafunzi usiombe MUNGU akupe hela kwa sasa….badala yake mwombe akufanikishe katika masomo ufaulu, uwe kichwa, hayo mengine bado msimu wake!..
Kama wewe ni binti/kijana na bado upo chini ya wazazi unawategemea, usiombe MUNGU akuonyeshe mume wako/mke wako, badala yake mwombe ulinzi juu ya tabia yako mpaka utakapofika wakati wa wewe kujitegemea na kufikiri kuingia katika ndoa.
Lakini kama umeshaingia katika msimu basi ni haki yako kumwomba BWANA!, Na unapomwomba Bwana jambo sahihi katika msimu sahihi, MUNGU ni mwenye huruma atakupa unachokihitaji haraka sana, na hata kikichelewa atakupa sababu kwanini kinachelewa, na sababu za BWANA zote ni Bora na wala si za kumwumiza Mtu, kwasababu yeye kamwe hawezi kuruhusu tujaribiwe kupita tuwezavyo.
Vumilia tu ukiona umeshaingia kwenye msimu na bado matokeo hujayaona!, yatakuja tu!..usikate tama a wala kuishiwa nguvu, mwamini MUNGU na mngojee, naye atakupa nguvu mpya kila siku.
Jambo la mwisho la kujua ni kwamba wokovu pia unao msimu wake, na msimu wa Wokovu ndio sasa..
Huu ndio wakati wa MUNGU kutupa wokovu na kutusikia maombi yetu, kwani utafika wakati ambapo hakutakuwa tena na wokovu wala maombi kusikiwa, ndivyo maandiko yanavyosema..
2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia; tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”
Sasa kama siku ya Wokovu ndio sasa, unasubiri nini usimpokee YESU?.. je unadhani itakuwa hivi siku zote?.. utafika wakati mlango wa Neema utafungwa, na hakutakuwa tena na msamaha wa dhambi wala ondoleo la dhambi, mti ulipoangukia huko huko utalala (Mhubiri 11:3).
Sasa unayadharau mahubiri na mafundisho ya uzima, unayoyapokea kila mahali yanayokuonya kuhusu dhambi, je unadhani hali itakuwa hivyo kila siku?…Majira yatabadilika ndugu, utafika wakati kutakuwa hakuna kuponywa tena mwili na roho!.
2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, HATA ILIPOZIDI GHADHABU YA BWANA JUU YA WATU WAKE, HATA KUSIWE NA KUPONYA”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?
MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.
JIFUNZE JAMBO KWENYE UKOO WA YESU, UWE NA AMANI
Kwanini madhabahu zilitengenezwa kwa mawe yasiyochongwa?
Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?
Swali: Kati ya Simoni Petro na Mariamu Magdalene ni yupi aliyekuwa wa kwanza kutokewa na Bwana YESU baada ya kufufuka kwake?, kwa maana katika Luka 24:34 tunasoma kuwa ni Simoni ndiye wa kwanza kutokewa na Bwana, lakini tukirudi katika Marko 16:9 tunaona ni Mariamu Magdalene je hii imekaaje?.
Jibu: Turee mistari hiyo..
Luka 24:33 “Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,
34 wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, NAYE AMEMTOKEA SIMONI”.
Hapa tunaona anatajwa Simoni, lakini turejee Marko 16:9..
Marko 16:9 “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, ALIMTOKEA KWANZA MARIAMU MAGDALENE, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.
10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia”.
Hapa tunasoma ni Mariamu Magdalena ndiye aliyetokewa kwanza, sasa swali ni yupi aliye sahihi au biblia inajichanganya?..
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi na wala haina kasoro yoyote… Sasa kama ni hivyo ni nani aliyetokewa wa kwanza?
Jibu, aliyetokewa wa kwanza na Bwana YESU alikuwa ni MARIAMU MAGDALENE, kama maandiko yanavyoonyesha hapo juu (Marko 16:9).. huyu ndiye aliyekuwa wa kwanza kumwona Bwana kwani baada tu ya kukuta jiwe limeviringishwa mbali na kaburi aliondoka na kwenda kuwafuata akina Petro kuwapasha yaliyojiri, na Petro pamoja na Yohana walipokwenda kaburini kuhakiki hizo taarifa za Magdalene, walikuta tu vitambaa vya sanda, na walipoondoka ndipo Bwana YESU akamtokea Mariamu Magdalene kama mtu wa kwanza (na saa hiyo akina Petro wameshaondoka).
Yohana 20:1 “Hata siku ya kwanza ya juma Mariamu Magdalene alikwenda kaburini alfajiri, kungali giza bado; akaliona lile jiwe limeondolewa kaburini.
2 Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.
3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.
4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.
5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu)”.
Hivyo baada ya kumtokea Mariamu Magdalena ndipo akamtokea Simoni Petro, katika tukio ambalo halijarekodiwa katika Biblia.
Kwahiyo Simoni Petro alikuwa ni Mtume wa kwanza kutokewa na Bwana YESU lakini si mtu wa kwanza, aliyekuwa wa kwanza ni Mariamu Magdalena na Simoni Petro anasimama kuwa wa kwanza kati ya Mitume wa Bwana.
Mtume Paulo analiweka hilo vizuri zaidi..
1Wakorintho 15:4 “na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
5 na ya kuwa ALIMTOKEA KEFA; tena na wale Thenashara;
6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;
7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;
8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake”.
Je umempokea YESU?.. Unao uhakika wa kwenda naye mawinguni atakaporudi?… fahamu kuwa tunaishi majira ya siku za mwisho, siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa kuungana na walio hai katika Kristo na kunyakuliwa juu, je utakuwa wapi siku hiyo?, ikiwa leo habari ya msalaba kwako ni upuuzi mtupu!.
Neema ya Bwana YESU itusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?
MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!
Nyongeza ya majina ya watu katika biblia
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe.
Wakati Fulani Bwana YESU aliuona “Mtini” (yaani mti unaozaa matuna aina ya Tini) usio na matunda na matokeo yake aliulaani.
Mathayo 21:18 “Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.
19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; AKAUAMBIA, YASIPATIKANE MATUNDA KWAKO TANGU LEO HATA MILELE. MTINI UKANYAUKA MARA.
20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?”
Sasa ukifuatilia vizuri hii habari utaweza kufikiri kwamba Bwana YESU alikuwa anaweza kuwa amekosea kuulani.., kwani ule mtini haukuwa msimu wake wa kuzaa matunda…
Hata wewe ukienda kutafuta machungwa kwenye mchungwa nje na msimu wake ni wazi kuwa hutashangazwa pale utakapokuta ule mchungwa hauna tunda lolote.Zaidi sana utashangazwa kama endapo umefika msimu halafu hukukuta machungwa.. Lakini sasa tunasoma Bwana YESU ilikuwa kinyume chake alijua kabisa si msimu wake Mtini kuzaa lakini aliulaani hivyo hivyo.
Sasa kwanini aulaani??
Sababu zipo nyingi, lakini hii yaweza kuwa kuu kuliko zote… ULE MTINI ULIONYESHA SIFA ZOTE ZA NJE KUWA NA MATUNDA lakini haukuwa na matunda! (Maana yake ulikuwa unahubiri udanganyifu).
Unaonaje umewekewa bahasha tatu mbele yako, halafu kati ya hizo bahasha tatu mbili zinaonekana kabisa kwa macho kuwa ndani hazina kitu, lakini moja inaonekana imetuna (kana kwamba ina fedha), halafu unaichagua hiyo iliyotuna kisha ndani unakuta hamna kitu, bila shaka utakwazika na unaweza ukaichana ile bahasha, ili isiendelee kudanganya wengine.
Vivyo hivyo Kristo alijua kabisa ule si wakati wa Tini kwani mitini mingine yote ilikuwa na sifa zinazofanana kwa wakati huo, lakini ajabu ni kwamba huu Mtini mmoja ulikuwa na mwonekano wa tofauti kana kwamba unao matunda, pengine wakati mitini mingine ilikuwa imekauka inapukutisha huu ulikuwa na majani mabichi, ulikuwa unahubiri udanganyifu kwamba unao matunda na kumbe hauna, na ili kuondoa udanganyifu huo suluhisho ni kukatwa/kulaaniwa.
Naam na maisha ya wakristo wengi yamejaa UDANGANYIFU, ni kama wanasifa zote za kuitwa wakristo lakini ukichunguza kwa undani hawana matunda!. Kwa nje wana majina ya kikristo, ni wahubiri, wana biblia nzuri na kubwa, wana nafasi katika kanisa, lakini ndani si wakristo, hawana matunda!, ni watu vuguvugu wale Bwana aliosema atawatapika katika Ufunuo..
Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.
Toka katika uvuguvugu, ili kuepuka laana ya KRISTO, kama umekusudia kuwa Moto, kuwa Moto mpendwa, kama umeamua kuchagua baridi maandiko yanasema ni heri uwe baridi kabisa kuliko kuwa hapo katikati, vuguvugu..
Bwana YESU atusaidie sana.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Tafsiri ya Mithali 27:18 Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake;
Je Bwana YESU alipanda mlimani na wanafunzi wake baada ya siku sita au nane?
MWISHO WA MAVUNO, NI MWISHO WA DUNIA.
Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
Jina kuu la BWANA WETU YESU KRISTO Libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko.
Endapo akitokea mtu faulani mkuu sana na kujigeuza na kujifanya mtumwa, na kuvaa nguo za chini ya hadhi yake, mtu huyo ni rahisi kupitia dharau kama watu wengine wa hadhi za chini, na kejeli, na hata kupitia mateso na kukataliwa….lakini laiti watu wanaomdharau wangemjua kwa undani ni mtu wa namna gani, hakuna hata mmoja angeonyesha kejeli au dharau!.. wote wangemheshimu na kumwogopa!.
Ni hivyo hivyo kwa Bwana YESU, walimsulibisha lakini hawakujua yeye ni nani, walidhani ni mwalifu tu, au mfano tu wa manabii wengine waliopita, kumbe! Hawakujua kuwa ni ALFA na OMEGA mwenyewe!. Naam hata mimi pengine ningekuwepo kipindi hiko, ningefanya hapo hayo! Kwasababu wanadamu sisi ni wale wale hatuna jipya!.
1Wakorintho 2:7 “bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu;
8 ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangaliijua, wasingalimsulibisha Bwana wa utukufu”.
Baada ya kuyatafakari hayo..hebu shika biblia yako ufuatilia maandiko yafuatayo maana leo utajua ya kwamba YESU KRISTO ni MUNGU mwenyewe katika MWILI wa kibinadamu!!?..na si mtu wa kawaida!.
Sasa si kwamba ukiishia kuamini tu ni Mwana wa MUNGU utakuwa umepotea!..la ni sahihi na ndio msingi!, lakini zaidi ya hapo, YESU ni zaidi ya tunavyomfikiria, ni jambo gumu kulielewa lakini unapolielewa linakuwa ni tamu na zuri..
Hebu tuyapeleleze maandiko kidogo kumhusu yeye katika kitabu cha Ufunuo..
Ufunuo 1:8 “Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi”.
Hapa MUNGU aliyeumba Mbingu na Nchi anajitambulisha kama Alfa na Omega!.. hapana shaka juu ya hilo, lakini hebu tuendelee mbele kidogo kumsoma huyu Alfa na Omega anaendelea kusemaje…
Ufunuo 21:5 “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.
6 Akaniambia, Imekwisha kuwa. MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu”.
Hapa tena huyu MUNGU wa mbingu na nchi ambaye ndiye ALFA na OMEGA, (yaani mwanzo na mwisho) anasema atayafanya yote kuwa mapya na atampa kila mwenye kiu ya maji ya uzima bure!.. Bila shaka hiyo ni karama ya MUNGU na njema sana… Lakini hebu tusogee tena mbele tumwone huyu ALFA na OMEGA anasema nini tena na anajizungumziaje..hapa ndipo tutashangaa!!.
Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.
13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.
14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.
16 MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.
Mstari wa 12 unaosema “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami,” na ule wa 16 unaosema “MIMI YESU NIMEMTUMA MALAIKA WANGU kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa.”… Mistari hii inatupa uzito kuendelea kumfikri YESU kama mtu wa kawaida, lakini inatulazimisha kumfikiri kama ALFA na OMEGA, kwamaana ndivyo alivyojitambulisha hapo.
Oo kumbe! YESU ni Alfa na Omega, na ndiye Mungu mwenyezi katika umbile la kibinadamu, sasa tunaelewa kwanini Mtume Paulo alisema siri ya UTAUWA (yaani Uungu) ni KUU, kwamba MUNGU alidhihirishwa katika mwili..
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Hayo maneno kwamba “Mungu alidhihirishwa katika mwili, na akachukuliwa juu katika utukufu” yanatufanya tufikiri mara mbili mbili kuwa YESU ni nani?.. Naam hata Bwana YESU mwenyewe kuna wakati aliwalazimisha watu kumfikiri yeye mara mbili mbili kuwa ni nani… Labda utauliza ni wapi hapo katika maandiko, twenda pamoja..
Mathayo 22:42 “Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena”
Hawa walikuwa wanamjua Masihi (YESU) kama mwana wa Daudi, na ni kweli maandiko yamesema hivyo, lakini sasa inakuwaje Daudi amwite Masihi kama Bwana wake na wakati huo huo awe mtoto wake??.. hata mimi ningeulizwa hilo swali, ningekwama!..
Maana yake kuna siri nyingine katika YESU tusizozijua, ambazo ukisoma maandiko kwa makini na kwa msaada wa Roho Mtakatifu utaziona!..
Sasa si dhambi kujua kama YESU ni mwana wa Daudi peke yake, wala si kosa kutambua kuwa ni Mwana wa MUNGU peke yake, na hiyo haiwezi kumtolea mtu tiketi ya kuingia mbinguni, lakini maandiko yanathibitisha kuwa YESU KRISTO ni zaidi ya tunavyomjua au kumfikiri, kama YEYE ni MUNGU MWENYEWE KATIKA MWILI..NUKTA KUBWA!!!.
Huenda Lugha zetu za duniani na udhaifu wetu wa kufikiri unakuwa ni mgumu kupokea hilo!, lakini huo ndio ukweli na ni lazima tuupokee, kama tu ilivyo ngumu kufikiri na kupokea kwamba inakuwaje MUNGU hana mwanzo!.. hapo ukifikiri sana unakwama!, lakini unaamini hivyo hivyo kwasababu yeye ni MUNGU, vile vile kuhusu UUNGU wa YESU usiumize kichwa kutafuta kulifanya lieleweke kichwani mwako sasa, labda tutaelewa vizuri baada ya maisha haya, lakini hatuna budi kuamini hilo!.
Na kumwelewa YESU namna hii inatufanya tusiuchezee Wokovu wetu, maana hatujakombolewa na damu ya mtu, wala myahudi bali ya MUNGU mwenyewe!.
Kwa maarifa ya ziada Kuhusu Uungu wa YESU zaidi pitia Tito 2:13, na Isaya 9:6
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
Isaya 6:1
[1]Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
Je unayajua makao hasaa ya Mungu?
Ni kweli tunafahamu Mungu anaketi katika kiti chake cha enzi, lakini ni kiti kilicho wapi hasaa?
Je! handakini? Mabondeni? Mapangoni? Kichakani? hasha!
Maandiko yanatueleza “Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana”
Kwahiyo na sisi lazima tuyajue makao hayo, ili tumfikie, vinginevyo tutajikuta tunaabudu Mungu mahali Ambapo kiti chake hakipo.
Katika biblia sehemu yoyote unapokutana na hili Neno “mahali pa juu”, Moja kwa moja utaona palihusishwa Na ibada..Yaani madhahabu zilijengwa pale ili kumtolea Mungu dhabihu. (1Samweli 9:12-13, 1Wafalme 3:2)
Yalikuwa ni maeneo yote yaliyoinuka mfano milimani. Kwasababu huko ndiko Mungu alikuchagua kujidhihirisha, na sio mabondeni, au mapangoni.
Ni kwanini?
Kwasababu Mungu anakaa sehemu Bora kuliko zote, sehemu iliyozidi vyote, sehemu ya juu ya juu kuliko zote. Hakai penginepo, Mungu hawekwi chini, haabudiwi mabondeni..kamwe hiyo sio sifa yake.
Hivyo ni vema ukafahamu sifa yake hii, ili tujue namna sahihi ya kumwendea.
1). Makazi:
(Mbinguni)
Kimakazi Mungu anaketi mbinguni.. Kwasababu Mbingu ni bora kuliko dunia hii.
Isaya 66:1
[1]BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?
Ndio maana tuna ujasiri na Mungu, akatie sehemu Bora zaidi ya hii, ambayo alisema atatukaribisha katika makao hayo baadaye.
Bwana Yesu alituambia tukisali tuseme Baba yetu uliye mbinguni.. (Mathayo 6:9). Hata alipoomba aliinua macho yake juu(Yoh 17:1), na sisi tumtakaripo Mungu, tuiweke picha hiyo akilini mwetu. Kwamba Baba yetu yupo mbinguni.
Na kutoka huko ndio tunatarajia mema yetu yaje, Na wenyeji wetu kushuka.(Yerusalemu mpya).
2) Viumbe.
(Mwanadamu).
Mwanadamu ametukuka kuliko viumbe vyote, amemvika uwezo na mamlaka (Zab 8:4-6). ndio maana amechagua kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu na sio kiumbe kingine chochote. Mungu hakai ndani ya swala, au sungura, au simba.. amechagua makao yake kuwa ndani ya mwanadamu tu.
Na aliyetufungulia lango hilo ni Yesu Kristo mwokozi wetu, kama mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alikaa ndani yake kikamilifu. Pasipo yeye kamwe Mungu asingekaa ndani ya moyo wa mwanadamu.
Ukimkosa Kristo umemkosa Mungu ndani yako.
Hivyo wewe uliyeokoka, fahamu kuwa Mungu anakaa ndani yako, hivyo wajibu wa kujichunga sana na kumpa Mungu ibada ya kweli( Warumi 12:1)
Ndio maana anapouheshimu mwili wako umemuheshimu Mungu. Kama mwanadamu ogopa sana kujiharibu kwasababu wewe ni mahali pa juu sana palipoinuka pa Mungu.
1 Wakorintho 3:16-17
[16]Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
[17]Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
3) Tabia
(Utakatifu)
Mungu ni mtakatifu, hivyo amechagua usafi zaidi ya uchafu, yeye ni Nuru si giza, ni mkamilifu si mwenye kasoro.
Hivyo tufahamu kuwa, tukimwendea yeye? kwa kupenda usafi? Lazima tutamwona.Lakini tukisema tunamtafuta na huku ni wachafu, hapo bado hatujamfikia Mahali pake pa juu anapoketi.
Isaya 57:15
[15]Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.
Sehemu nyingine anasema..
Zaburi 24:3-4
[3]Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
[4]Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.
Soma pia, Zab 15
4) Uweza:
(Imani)
Mungu si dhaifu, hivyo jambo lolote linaloonekana lina Nguvu, lililotukuka, lipitalo uwezo au ufahamu wa kibinadamu ni lake.
Ndio maana mtu anayemwendea Mungu kuomba yasiyowezekana kibinadamu, amemfikia Mungu.
Anaitwa Mungu wa miungu, Ibrahimu alimwamini Mungu kwa yasiyowezekana akawa rafiki wa Mungu, watu wote walio wa Imani ndio wanaomwona Mungu, Akiwatendea miujiza. Fahamu kuwa Mungu anavutiwa zaidi na yale yasiyowezekana Kibinadamu kuliko yale yanayowezekana..Jifunze kuishi kwa Imani, maana hapo ni mahali pake pa juu.. ondoa mashaka Ndani yako. Utamfikia Bwana hakika.
5) Ibada:
(Heshima)
Katika eneo la ibada, Mungu hafanyiwi Ibada ilimradi ibada. akiabudiwa ni lazima iwe katika Roho na kweli. Tunamtolea ibada ya juu sana..ikiwa ni sadaka Hatumpelekei kilema, bali ile ya juu zaidi, ikiwa ni sifa tunamsifu kwa nguvu zetu zote, kama Daudi,bila kujali kitu, kama ni kumtukuza Basi tunamtukuza sana na kumwadhimisha kwa viwango vyote.
Kwasababu yeye ndiye Mungu wetu astahiliye sifa zote.
Hivyo yatupasa maeneo yote hayo, tuyatambue, kisha tumwabudu kiufasaha Mahali pake pa Juu palipoinuka.
Zaburi 113:5-6
[5]Ni nani aliye mfano wa BWANA, Mungu wetu aketiye juu; [6]Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jina la Mwokozi wa pekee YESU KRISTO libarikiwe.
Je unajua tupo katika kipindi cha UFUFUO?.. Utauliza ufufuo gani?.. Turejee maandiko yafuatayo..
Yohana 5:25 “Amin, amin, nawaambia, SAA INAKUJA, NA SASA IPO, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake”.
Hapo Bwana YESU (Mkuu wa uzima) anasema “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” Je unaielewa vizuri hii kauli?
Anaposema “Saa inakuja” maana yake kipindi Fulani cha mbeleni kinachokuja…. Na anaposema “sasa ipo” maana yake ni kipindi alichopo yeye.
Sasa swali alikuwa ana maana gani kusema vile?
SAA INAKUJA: Hiki ni kipindi cha mwisho wa dunia, (wakati wa unyakuo wa kanisa) ambapo wafu waliokufa katika Kristo watatoka makaburini na kuvikwa miili ya utukufu na kisha kumlaki Bwana mawinguni.
1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.
14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba YESU ALIKUFA AKAFUFUKA, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, MUNGU ATAWALETA PAMOJA NAYE.
15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.
16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; NAO WALIOKUFA KATIKA KRISTO WATAFUFULIWA KWANZA.
17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.
Hiko ni kipindi cha Ufufuo wa siku za mwisho ambacho yoyote aliyekufa hapaswi kukikosa..kwani si wote watakaofufuliwa na kwenda kwenye unyakuo.
NA SASA IPO: Hiki ni kipindi ambacho Bwana YESU alikuwepo duniani, ambapo watu walikuwa wanafufuliwa roho zao zilizokufa katika dhambi..
Kitendo cha kumwamini YESU na kutubu na kubatizwa ni sawa na kufufuka kutoka katika WAFU, utauliza kwa namna gani?..
Turejee kidogo ile habari ya mwana mpotevu ambaye alitapanya mali kwa maisha ya uasherati na alipozingatia kurudi kwa baba yake kutubu, baba yake alimtafsiri kama aliyekuwa amekufa na sasa amefufuka.
Luka 15:29 “Akamjibu baba yake, akasema, Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu
30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.
31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.
32 Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako ALIKUWA AMEKUFA, NAYE AMEFUFUKA; alikuwa amepotea, naye ameonekana”.
Umeona? Si kwamba huyu kijana alikuwa amekufa kimwili, La! Bali kiroho, na alipotubu na kugeuka akahesabika kama aliyefufuka..
Je bado na wewe ni MFU na ilihali tunaishi katika SAA YA UFUFUO?.. Kumbuka usipofufuliwa sasa utu wa ndani kama huyu kijana mpotevu, hutaweza kuupata ufufuo wa siku ile ya Mwisho Bwana YESU atakaporudi, na siku hiyo imekaribia sana..
Maisha unayoishi ya dhambi ni uthibitisho wa MAUTI iliyopo ndani yako, na hiyo itaathiri hata mambo yako mengine uyafanyayo.
Fufuka leo kwa kumwamini BWANA YESU KRISTO, ili akuoshe dhambi zako kama maandiko yasemavyo..
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.
15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana”.
Saa ya UFUFUO Ni SASA… Saa ya Ufufuo ni Sasa, Saa ya UFUFUO NI SASA!
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).
YEYE AJAYE ATAKUJA WALA HATAKAWIA.
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe karibu tujifunze biblia.
Tabia ya kujifanya hujui na ilihali unajua ni mbaya na hatari, kwani ni sawa na kumjaribu MUNGU.. Kipo kisa kimoja kwenye biblia cha watu waliojifanya hawajui mbele ya Bwana YESU na matokeo yake hayakuwa mazuri.
Marko 11:27 “Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa MAKUHANI, NA WAANDISHI, NA WAZEE,
28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya?
29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.
30 UBATIZO WA YOHANA ULITOKA MBINGUNI, AU KWA WANADAMU? NIJIBUNI.
31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini?
32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi.
33 WAKAMJIBU YESU, WAKASEMA, HATUJUI. YESU AKAWAAMBIA, WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.
Watu hawa walikuwa wanajua kabisa ubatizo wa Yohana ulikuwa umetoka kwa MUNGU, lakini wakawa wanajifanya hawajui, na walipomwuliza Bwana YESU wakitegemea kuwa atawapa jibu la moja kwa moja, kinyume chake Bwana aliwajibu “WALA MIMI SIWAAMBII NINYI NI KWA MAMLAKA GANI NAYATENDA HAYA”.
Kwahiyo kumbe kuna maombi, au haja au dua au maulizo ambayo tunaweza kumpelekea Bwana YESU na tusipewe majibu yake!.
Ndio! kama maandiko yamesema wazi kuwa wizi ni dhambi, na tunalijua hilo hatuwezi tena kwenda tena na kumwuliza MUNGU kama kuiba ni dhambi au la! Kwani tayari tumesoma na tunajua… ukienda kumwuliza ni kumjaribu na hakuna majibu yoyote yatakayotoka..
Kama maandiko yamesema wazi kuwa uzinzi na uasherati ni dhambi, na tunajua hilo, hatuwezi tena kwenda kurudia kumuuliza MUNGU atufunulie kwenye ndoto au tuisikie sauti yake ikisema kuwa ni dhambi…hapo itakuwa ni kumjaribu.
Kama dhamiri yako inakushuhudia kabisa kuwa hilo unalolitenda, au hiko unakokivaa au unakokishikilia ni dhambi, na maandiko yamekudhihirishia wazi, huwezi tena kwenda kumwuliza MUNGU akuhakikishie, unaweza usipate majibu yoyote, na ukaishia kusema MUNGU hasikii maombi.
Sio kwamba MUNGU hasikii maombi, ni kwamba MUNGU anataka usikie kwanza Neno lake na kulitii, lililoadikwa katika kitabu chake kitakatifu BIBLIA.
Biblia ni sauti ya MUNGU isiyo na marekebisho, na iliyo ya wazi kabisa.. ukitaka kuisikia sauti ya MUNGU ya wazi kabisa, soma Biblia, wala usiende kwa mchungaji, wala askofu, wala usisubiri uote ndoto, wewe soma Biblia tu!, utapata utamsikia MUNGU.
Mwisho acha kujifanya hujui kama kuna Jehanamu, acha kujifanya hujui kuwa kuvaa kidunia ni makosa, acha kujifanya hujui kwamba ibada za sanamu ni makosa, acha kujifanya hujui kuwa matambiko na makosa, acha kujifanya hujui kuwa kuishi na mke/mume wa mtu ni dhambi!.
Usimwulize Bwana MUNGU kama pombe unazouza ni mapenzi yake au la!, na ili hali unajua kabisa pombe ni makosa, hutapata majibu yoyote, zaidi unaweza ukaisikia sauti ya shetani kinyume chake.
Yakobo 4:17 “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kama Kristo alizichukua dhambi zetu na kutusamehe kwanini kila siku tunatubu?.
KILA SILAHA ITAKAYOFANYIKA JUU YAKO HAITAFANIKIWA.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA MFUNGO.
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wathesalonike wa kwanza.