Kitabu cha Waraka wa kwanza wa Yohana ni kitabu ambacho kilielekezwa mahususi kwa makundi matatu (3) ya watu, Watoto, vijana, na Wababa. Sasa sio Watoto au vijana au wababa kimwili, Hapana, bali alikuwa anazungumzia ngazi hizo katika roho, yaani Kundi la Watoto kiroho, vijana kiroho na wababa kiroho.
1Yohana 2:12-14
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Na kila mmoja wao ameelezwa sifa zao, zinazowafanya wawe vile. Kwamfano Watoto kiroho, anasema ni kwasababu wamesahewa dhambi, lakini pia wamemjua Baba, tafsiri yake ni nini? Kwa mtu ambaye ni mchanga kiroho, anapokuja kwa Kristo, jambo la kwanza, ambalo atalipitia kwenye maisha yake, ni kutuliwa mizigo, mizito ambayo alikuwa anasumbuka nayo, ambayo asili yake ni dhambi. Ndio hapo ataanza kujiona mwepesi, anapokuja kwa Kristo, anajiona huru, katika kifungoni, anajiona na amani ambayo hajui chanzo chake ni nini, anajiona anapendwa,..Na ndivyo ilivyo upendo wa Mungu kwa huyu mtu unakuwa wa kipekee sana, ndio sababu kwanini anasema nimewaandikia nyinyi Watoto wadogo kwasababu mmesamehewa dhambi zenu, na mmemjua Baba. Hayo ni mambo mawili ambayo walio wa changa kiroho hujapitia.
Lakini kwa vijana, anasema nimewaandikia kwasababu mmemshinda yule mwovu. Hatua hii ya ujana ni ya kipindi cha ukuaji kiroho, hapa mara nyingi mwamini hukutana sana na majaribu ya shetani, mapingamizi makubwa, vita vya kiimani, misukosuko kwa sababu ya Kristo. Kiroho mtu kama huyu huitwa kijana, kwasababu wakati huu, ijapokuwa atasongwa lakini huwa haachi kumng’ang’ania Mungu, moto wake hauzimiki, hata kidogo, kama ni maombi, kasi huwa ni ile ile,usomaji Neno haupungui, hata akiumwa haiwi vyepesi kumwacha Mungu, kwasababu ni wakati wa Nguvu za Mungu nyingi Kutenda kazi ndani yake, na kumshinda mwovu kotekote.
Lakini Wababa kiroho, sifa yao pia ni tofauti na hao wengine, Sifa yao ni kuwa “ wamemjua yeye aliye tangu mwanzo”.
Maana yake ni nini? Kwanini hasemi kwasababu mmehubiri sana?, au kwasababu mmedumu sana ndani ya Kristo? Bali kwasababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo?
Kumfahamu Mungu, tangu mbali, ni kigezo kikuu sana cha ukomavu rohoni. Mpaka mitume kuitwa baba zetu, ni kwasababu walipewa kumwona Mungu kutokea mbali, tofauti na waandishi na makuhani..Ndio maana waraka tu huu ulipoanza anasema..
1Yohana 1:1 Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;
Hili lilikuja kudhihirika pale Yesu alipoanza kuwaeleza mambo yake mwenyewe aliyoandikiwa tangu, Torati ya Musa, Zaburi na Manabii, jinsi alivyokuwepo na watu wake, jangwani, kupitia ule mwamba, Mana, nyoka wa shaba, jinsi alivyo mtokea Ibrahimu kama Melkizedeki, jinsi alivyojidhihirisha kwao kwa namna mbalimbali kupitia tumbo la Samaki kwa Yona n.k. lakini hawakumwelewa.
Luka 24:44
44 Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. 45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
Sasa, mtu akishamwona Mungu kwa namna hiyo, basi Mungu kwake hawi wa “matukio” bali wa wakati wote. Yaani alikuwa nasi jana, yupo nasi leo, na atakuwa nasi hata milele.. Watoto wachanga kiroho, hawawezi kumwona Mungu jana, wenyewe Mungu wao, ni wa matukio ya leo.
Maeneo matatu ambayo macho yako yanapaswa yafunguke kuhusu, kumjua Mungu tangu mwanzo.
Hivyo ile uwe Baba, ni lazima umjue Mungu aliyekuwepo tangu Mwanzo, usiwe mtu wa matukio ya leo leo, kama mtu uliyeokoka jana, Kaa chini, tafakari sana, hatua moja baada ya nyingine ya maisha yako, anzia kwenye maandiko uone jinsi Mungu alivyokuwa na watu wake tangu zamani, ambao wengine kwa kukosa kumjua wakawa wanalalamika tu, wanaishi kiwepesi wepesi, na hatimaye kumsulibisha, lakini wale waliomjua waligeuzwa na kuwa mitume wake,
Kuwa baba rohoni.
Mungu akubariki.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je umewaonea utungu watoto wako?
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.
Print this post
Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.
Sasa Makosa kama haya,(ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.
Tutakwenda kuona aina tano (5) vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. [2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. [3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. [4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. [6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’
Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).
Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…
Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.
Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.
Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.
Mwanzo 4:10-13
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. [11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; [12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. [13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia
Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao
Kutoka 3:7-9
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; [8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. [9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.
Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.
Ufunuo 6:9-10
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. [10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.
Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.
5) Kilio (Shangwe) cha waovu.
Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kubwe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.
Mwanzo 18:20-21
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, [21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.
Je! Umemwamini Yesu?
Je una uhakika kubwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.
Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)
ENDELEZA UPONDAJI.
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
Luka 15:20
[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..
Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..
Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..
Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..
Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..
Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…
Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…
Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?
Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.
Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.
Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?
Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU
JAWA SANA MOTO ULAO.
TENGENEZA NJIA YAKO.
Marko 9:24
[24]Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Habari ya yule mzee ambaye kijana wake alivamiwa na mapepo sugu ya kumtupa motoni tangu utoto wake, na baada ya kuhangaika sana kwa madaktari na kila aina ya matabibu, hadi mitume nao kushindwa kumponya, hatimaye akakutana na Bwana Yesu..
Akamwambia ‘Ukiweza’ Bwana neno utuhurumie na kutusaidia… lakini saa hiyo Hiyo Yesu akamjibu….Ukiweza?..
Mimi unaniambia ukiweza?
Marko 9:23
[23]Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Kuonyesha kuwa Imani yake, haikuwa kamili, lakini, saa hiyo hiyo akaweka tegemeo lake lote kwa Yesu na kumwamini..’Naamini’…lakini pia nisaidie ‘kutokuamini kwangu’..
Hiki ni Moja ya ombi ya uwazi na la ukweli kabisa ambalo tunaweza kulisoma kwenye biblia…
Ni kweli ameamini, lakini imani yake si timilifu, anapambana sana kuifanya iwe sawa.. hivyo pamoja na hilo akamwona na Bwana amsaidie…kuonyesha tabia ya kujiachia kikamilifu kwa Bwana…kwamba sio tu kutendewa muujiza lakini pia kusaidiwa..
Saa hiyo hiyo Yesu hakumfukuza, wala kumkemea, wala kumwambia kafanye hivi au vile kwanza… bali akamkemea yule pepo Na hatimaye kijana akawa mzima saa ile ile.
Imani, ya kweli haimaanishi kwamba mashaka yatapotea…bali ni kuchagua kujimimina kwa Bwana na kuweka tegemeo lako lote kwake tu, hata kama moyo wako utakuambia wewe mbona unamashaka mashaka, mbona huna imani, mbona maneno yako mwenyewe yanathibitisha umekata tamaa..
Hakika hapo usiache kuomba na kukiri, ukiulilia pia msaada wa Bwana akusaidie imani yako iwe Kamilifu, kwa kujimimina tu hivyo hatimaye utayaona mambo makubwa akikutendea..
Usianze kujilaumu kwa mashaka mia uliyoonyesha, wewe egemea tu kwa Yesu bila kuondoa mguu wako hapo…atakujenga..Yule baba hakuondoka kwa Yesu, kwasababu ya madhaifu yake bali aliendelea kukaa pale pale. Kwasababu imani inajengwa kwa mahusiano sio kwa utimilifu wetu.
neema ya Mungu hizidi mapungufu yetu..kiri.udhaifu wako kwake, lakini onyesha kumtegemea yeye, hapo nguvu za Mungu utaziona.
Shetani atataka ujilaumu, katika shida yoyte lakini sema…
“Naamini, Bwana, nisaidie kutokuamini kwangu.
MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?
WhatsApp
Waebrania 12:29
[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.
Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa
Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)
Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…
Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.
Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;
Isaya 33:14
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele? [15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..
Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.
Hii ndio mbio yetu wote…
Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.
Shalom
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)
Mwanzo 3:15
[15]nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa..
Kitu pekee Ambacho kilitabiriwa kuweza kuvunja vichwa vya majoka(shetani), ni uzao wa mwanamke tu. Aliyetabiriwa kwenye (Mwanzo 3:15)
Uzao huu wa mwanamke ni Yesu Kristo.. kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyezaliwa Bila mwanamume, sisi wote ni uzao wa mwanamume…kwasababu mbegu yetu imetoka kwa Baba zetu, lakini Kristo ni mbegu iliyoshuka Kutoka mbinguni, ndio maana hapo anatajwa Kama uzao wa mwanamke.
Yeye kwa ushindi alioupata dhidi ya nguvu za giza kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu na kupaa mbinguni..ni pigo Kubwa sana kwa shetani, ambalo lilimlenga moja kwa moja katika kichwa chake.
Kwasababu kwa njia hiyo wanadamu tumevuka kutoka mautini kwenda uzimani…
Lakini habari njema ni kuwa yeyote amwaminiye, anakuwa sehemu ya uzao huo kwa imani. Na hivyo anapokea mamlaka ile ile ya kuvunja mafuvu ya majoka…mpaka ufalme wa giza kutokomea kabisa katika uso wa ulimwengu..
Wagalatia 3:29
[29]Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
Luka 10:19
[19]Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Kumbuka uwezo huu, hakuna uzao mwingine wowote unaoweza kumuharibu shetani, waafrika hawawezi, wazungu hawawezi, wachina hawawezi, waarabu hawawezi, ukoo wa kiyahudi hauwezi, familia za kichifu, haiwezi, wanadamu wote hawawezi kuponda majoka, hata waungane kwa vifaru vyao na makombora ya nyuklia, bado hawawezi kinyume chake wao ndio watafanyika chakula cha hao majoka.Ni uzao mmoja tu wa Yesu Kristo ndio wenye nguvu hizo..
Swali ni je! Tunapondaje vichwa vya majoka.
Ni kwa kuendelea kuhubiri. Ukikaa tu bila kushuhudia habari za Kristo kwa wenye dhambi, kukaa bila kujishughulisha na shamba la Bwana..Fahamu kuwa ‘mabuti’ yako uliyopewa huko miguuni huyatendei Haki..yapo tu!
Unamridhia shetani, unafurahishwa na uwepo wake shambani mwa Bwana, ndugu njia pekee inayomdosha shetani kwa wepesi ni wewe kukutana na mwenye dhambi mmoja na kumshuhudia habari za wokovu.
Mitume walipoenda kuhubiri baada ya kutumwa na Yesu, waliporudi na ushindi, Yesu aliwaambia nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..
Luka 10:18
[18]Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
Simama tumia mabuti yako vizuri, endeleza kuponda, ponda kweli kweli, haribu kisawasawa, kwa njia ya injili.
Sio kwa kuimba “nakuponda shetani” au
Kusema “toka shetani” bali kwa injili
Kuponda kwingine ni maombi na kuishi maisha ya utakatifu, huku nako kunahubiri injili ya Kristo na hivyo shetani anaumizwa vibaya sana.
Amka tumia buti zako, kila kichaka katika shamba la Bwana ambacho majoka yamejificha Ni kwenda kuponda tu, mpaka habari njema za ufalme zifike ulimwenguni kote.
Bwana awe nawe.
Amen.
IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.
INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.
Isaya 61: 1-3
1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta …3 kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, WAPEWE TAJI YA MAUA BADALA YA MAJIVU, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.
Kitu kikishachomwa na kuteketea kabisa, kinachosalia cha mwisho kabisa huwa ni majivu. Majivu hayana thamani yoyote, ni vumbi jembamba, ambalo likikanywagwa, hutoweka kabisa.
Hivyo zipo nyakati ambazo, watu wanakuwa kama majivu mbele ya macho yao wenyewe, au kwa wengine. Yaani Kila kitu kimekufa na kuteketea kabisa, yale maono aliyokuwa nayo yamefutika, wengine afya zao zimekuwa jivu,hawana matumaini ya kupona tena, wengine maisha yamevurugika, akiangalia muda aliochezea moyo unapoa kabisa, wengine mahusiano yao yametafunwa, haoni kuendelea mbele.. Rohoni akijiangalia ni jivu tu, kila mahali ni jivu hajasaliwa na chochote, isipokuwa kukata tamaa na kupotea kabisa..
Ndio maana katika enzi za biblia mtu aliyekuwa katika maombolezo Makali, alijimwagia majivu mwilini kama ishara kuwa umepukutika kabisa..Mfano wa hawa ni Ayubu na Mordekai (Ayubu 2:8, Esta 4:1 )
Lakini Mungu afufuaye matumaini, alitoa unabii huu juu ya mwanawe atakayekuja kuukomboa ulimwengu, akasema..
Amemtia mafuta, “ili awape watu wake taji ya maua badala ya majivu..”
Tafsiri yake, ni kuwa sio tu atamwondoa kwenye majivu na kumwacha, Hapana, bali anambadilishia na kumpa taji la maua.
Maua huwakilisha heshima, cheo, hadhi, baraka, afya.
Hivyo haijalishi utakuwa katika hali isiyoeleweka kiasi gani, Yupo Yesu wa kukuondoa majivuni na kukuvika maua, ‘Majivu yako leo ndio maua yako baadaye, lakini ikiwa tu utakuwa ndani ya Kristo’.
Usihofu wala usiogope, wala usikate tamaa..Magonjwa hugeuzwa afya.
Yusufu alikuwa majivu gerezani, lakini Mungu alimfanya maua katika kiti cha Farao. Petro alikuwa jivu kwa kumkana Bwana wake, lakini ndiye alikuwa mjenzi wa kanisa la Kristo. Ruthu alikuwa mjane kwa kufiwa na mumewe, lakini Bwana alimwekwa kama mama wa uzao wa kifalme, Haijalishi hutafaa kwa jinsi gani leo, Kristo yupo kukugeuza, na kukuondoa majivuni.
Lakini hii inahitaji kumpokea na kuendelea kuishi ndani yake. Je upo tayari kuyakabidhi leo maisha yako kwake?
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
Kwanini mkono wa Musa uingie ukoma?
UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.
Siku moja Yesu alipokuwa anahubiri katika nyumba fulani, watu wengi walikusanyika mahali pale, na ghafla wakamletea mtu aliyepooza mwili mzima hawezi kufanya lolote, wakamweka Mbele yake ili amponye. Lakini tunaona mwitikio wa Yesu ulikuwa ni tofauti na matarajio yao. Bwana Yesu hakumwekea mikono na kumwambia simama uende, bali alimwambia..
Rafiki, umesamehewa dhambi zako.
Luka 5:17-20
[17]Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya. [18]Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake. [19]Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. [20]Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.
[17]Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.
[18]Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake.
[19]Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu.
[20]Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.
Jicho la mwanadamu linaona uponyaji ni kutendewa muujiza wa nje, lakini kwa Mungu Uponyaji hasaa ni kusamehewa dhambi. Mtu akishasamehewa dhambi, mengine yote hufuata..
Tunasamehewaje dhambi?
Kwa kumwamini Bwana Yesu na kumaanisha kumfuata kwa toba ya kweli. Hapo ndipo tunapopokea Msamaha Wa dhambi zetu, na hatimaye uponyaji Wa mambo yetu mengine yote.
Wakolosai 1:13-14
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; [14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
[14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
Matendo ya Mitume 26:18
[18]uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.
Ni ajabu Kuona, watu wanakwenda kwa Yesu na mapooza Yao, wengine katika afya zao kama huyu, wengine mapooza ya shughuli zao, wengine katika familia Zao n.k. wakitarajia Yesu awaponye kwa njia zao.
Lakini wanapokutana Na injili za wokovu na kuacha dhambi.. wanazikwepa wanakimbilia kwenye maombezi na mafuta Ya upako.
Ndugu fahamu kuwa asili ya kila tatizo ni dhambi..Mahali ambapo maisha yako yanawekwa wazi, yanamulikwa hapo ndipo uponyaji wako halisi upo. Usikimbie, usitange-tange.
Pokea kwanza msamaha wa dhambi mengine yafuate…kubali wokovu, kubali uzima, uponywe. Itakufaidia nini upate ulimwengu wote, afya yote, amani yote kisha ukateketee tena jehanamu milele baadaye?
Ikiwa bado hujaokolewa (yaani hujapata msamaha wa dhambi zako) basi wakati ndio huu.. wasiliana nasi kwa namba hizi kwa mwongozo wa kumpokea Yesu.
NITAACHAJE DHAMBI?
MAFUNZO YA BIBLIA KWA WATOTO
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
Mathayo 20:6
[6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Bwana Yesu alizungumza mfano ambao unagusia kabisa uhalisia wa kiroho uliopo sasa katika kazi ya Mungu (Ushuhudiaji).
Mfano huo unahusu mtu mmoja aliyetoka asubuhi sana kuajiri wafanyakazi ili kwenda kulilima shamba lake ambalo lilihitaji watu wengi kulihudumia.
Hivyo akatoka alfajiri sana, kuwatafuta na kwa bahati nzuri akawakuta, akawapeleka shambani mwake, akatoka tena saa tatu, akawakuta wengine wamekaa bila kazi, akawatuma shambani, akaenda tena saa sita na saa tisa vivyo hivyo akafanya…Mpaka ilipofika saa kumi na moja akatoka na kuwakuta watu wengine wamesimama tu toka asubuhi mpaka jioni…hawafanyi chochote wapo “Idle”
akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Mathayo 20:1-7
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. [2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. [3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; [4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda. [5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. [6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? [7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
[2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
[3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
[4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
[5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.
[7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
Embu jiulize swali moja.. Je! Unadhani watu hawa wa saa kumi na moja hawapo leo?
Kukaa bila kufanya kazi ya Mungu, wakati Kazi ipo kubwa kwa kisingizio kuwa hakuna wa kukuajiri ni ulegevu kiroho… yule Bwana hakuwa na muda wa kusikiliza sababu zao, kwamba waendelee kukaa na kumalizia tu siku kwasababu muda umeenda, bali aliwatuma haraka sana shambani.
1) Hofu ya kutumika
Kusema mimi siwezi, Mimi bado mchanga kiroho, sijui biblia vizuri, Mimi bado mdogo kiumri, mimi siwezi Kuongea nina aibu, nina kigugumizi..sina fedha, sina elimu n.k…haya ndio mambo yanayowakawiisha watu wengi wasimtumikie Mungu..
Ndugu fahamu kuwa Mungu hategemei ukamilifu wetu, kutimiza kusudi lake kamilifu, bali hututumia katika hali zetu hizi hizi, hivyo usingojee siku fulani utakuwa mzoefu ndio umtumikie Mungu..haitafika, anzia na hali yako hiyo hiyo.(1Wakoritho1:26-29)
2) Kungojea muda fulani sahihi.
Kudhani Kuwa upo muda fulani maalumu utaitwa na Bwana rasmi umtumikie, hilo pia limewafanya wengi, kungoja muda mrefu na hatimaye kutoona mafanikio.. saa ya kutumika ni sasa..tayari Wote tulishaitwa tumtumikie yeye tangu siku tulipookoka..ukishaokoka umepewa na vibali vyote na mamlaka ya kumtumikia Bwana..usingoje utokewe na Yesu kama Paulo Dameski, Usingoje usikie sauti fulani ikikwambia nenda kawafundishe watu. Anza sasa na Bwana ataungana na wewe mbele ya safari.
3) Masumbufu ya maisha
Mizigo mingi ya kimaisha, utakula nini, utavaa nini, utaishije, linawapunguza watu kasi ya kufikiria kwamba wanahitaji kwanza kuyaandaa maisha yao yawe safi ndipo waamke kwenda kumuhubiri Kristo.
Ndicho walichokifanya wayahudi walipokuwa wanajenga hekalu la pili, ilifika wakati wakaacha ujenzi kila mmoja akaenda kwenye mambo yake, Kwasababu tu, ya kujiangalia hali zao.
Hagai 1:2-4
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA. [3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, [4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA.
[3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,
[4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
Usingoje ufanikiwe, uoe, uwe na maisha ndio sasa uanze kuifanya kazi ya Mungu, ukijitazama Sana, hutamtumikia Mungu ndugu.. fahamu kuwa wengi wanaokuletea wewe habari njema sio wenye mafanikio, lakini Bwana hawaachi.
4) Ulegevu.
Kupendelea mambo ya kirahisi rahisi, zaidi ya kujitoa..wakati mwingine kukataa kutaabika kwa ajili ya injili..kutaka ijiendeshe Yenyewe, bila kuwa mfuatiliaji na mwombaji, pia hukawiisha utendaji kazi wa injili.
Hivyo, ndugu muda ni mfupi sana, tupo katika saa la kumi na moja yetu, usihudhurie tu kanisani, kuwa sehemu ya utumishi kanisani, usisikilize / kusoma tu mahubiri, hubiri na kwa wengine unachojifunza, Shamba la Bwana linatuhitaji wote.
Ni wakati wa kuamka usingizini, bado hatujachelewa, ikiwa tutatimiza kusudi la Mungu vema, basi tutalipwa sawasawa tu na wale waliowahi..Hivyo amka sasa.. anza kushuhudia.
Shiriki injili kwa kushea na wengine habari hizi
Bwana akubariki
Siku moja nilikuwa nakatiza eneo fulani la biashara ambalo limechangamka sana, Ni eneo ambalo watu wengi wanapishana..ghafla kwa mbele nikamwona kijana mmoja ameinama, baada ya muda kidogo akachuchumaa, na mara akaanza kutapika matapishi mengi sana.. Uso wake ulionekana kuumwa, hivyo moja kwa moja nilipomwangalia moyoni mwangu, niliguswa sana na ile hali aliyokuwa anapitia..
Kikawaida zipo hali ambazo ukiumwa Unaweza kuzivumilika mpaka ufike mahali fulani pa matibabu..lakini kuumwa mpaka kutapika Hakuzuiliki, na kama ulishawahi kutapika unaelewa nguvu inayotumika, hali unayoisikia wakati huo.. ni kama nusu ya kufa..
Sasa sisi ndivyo tunavyomfanya Mungu, ajisikie muda wote tunapokuwa Na aina ya mwenendo wa uvuguvugu maishani mwetu, .alisema hivi;
Ufunuo wa Yohana 3:15-19
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. [16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. [17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. [18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. [19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
[16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Uvuguvugu ni ile hali ya kuwa mtu wa kidini na sio wa kiroho, unahudhuria ibada lakini mabadiliko huna, unavaa vizuri kanisani lakini ukiwa nje unavaa nguo zisizo na adabu, unaimba kwaya, lakini wakati huo huo unasikiliza nyimbo za kidunia, ni mtumishi mzuri wa kanisani lakini bado unaishi na mume wa mtu..
Maisha ya uvuguvugu, yanamtesa Kristo isivyo kawaida..Ikiwa wewe hupendi kutapika- tapika Kwanini wewe umfanye Mungu kuwa na hali hiyo?
Ukristo ni mwendelezo sio tukio…eti mimi nimeshamkiri Yesu kwa Kinywa..inatosha nimeokoka, hapana…bali ni ukuaji wa kiroho.. ni lazima uonyeshe ukuaji…kitu chochote kilicho hai kinakua…lakini kuwa mtu yule yule kila siku wewe ni vuguvugu.
Kanisa La Laodikia, lilikuwa na sifa ya kujiona ni tajiri Kisa Lina vyombo vizuri vya miziki, lina Makongamano makubwa ya nje, lina mwonekano wa kuvutia, lina umaarufu, Lakini Yesu aliliona si la kiroho hata kidogo..Linamheshimu Mungu kwa nje tu, lakini ndani limepoa zaidi ya barafu..
Hizi ni nyakati ambazo watu wengi wanazisahau ibada za kweli, wanatafuta fedha na Midundo inayovutia masikio ya watu lakini hawajali ujumbe wa rohoni au ‘uzuri Wa utakatifu’.
Na watu ambao wakiwaona wengine wamesimama kikamilifu mbele za Mungu wanawaita “walokole” …
Embu tubu, rafiki…uzuri wako, mwonekano wako, Sifa zako, udunia wako, havina ushirika na Kristo, hizo status zisizo na staha na elimu, unampostia nani mitandaoni? Hiyo mitandao ya kizinzi unayoitembelea kila siku, na kujichua unakoendelea nako kwa siri na wakati huo huo unasema umeokoka, nini unakiunda kama sio kumfanya Bwana atapike?…maanisha kumpokea Kristo. Simama katika imani, ili umwone Mungu wa kweli na sio sanamu.
Kumbuka hizi ni nyakati za kusimama kikamilifu, kwasababu mwisho umekaribia..Unyakuo Ukipita watakaokwenda na Bwana ni walio moto tu, na sio vuguvugu.
Kutubu ni kugeuka…Geuka tu leo kwa kumaanisha na Bwana atakusamehe kabisa na kuanza na wewe..Ikiwa hujaokoka na upo tayari leo kufanya hivyo…Basi wasiliana nasi kwa mwongozo wa sala ya Toba..
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?