Category Archive Mafundisho

Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Paulo kwa Timotheo (1Timotheo)

Tofauti na nyaraka nyingi za mtume Paulo, ambazo aliziandika kwa Makanisa, waraka huu aliuelekeza kwa Timotheo ambaye alisimama sio tu kama msaidizi wake wa kihuduma bali pia kama mwanae Katika vifungo vya injili. Ni waraka wa kichungaji zaidi ya wa kimafundisho,

Katika waraka huu Paulo anamwagiza Timotheo namna ambavyo kanisa linapaswa likae katika utaratibu, Mungu alioukusudia.(1Timotheo 3:15)

Maudhui makuu ya Paulo kwa Timotheo yalikuwa ni haya;

  1. Kujilinda na waalimu wa uongo.
  2. Namna ya ‘jinsia na marika’ mbalimbali yanavyopaswa yaenende/ kuhudumu ndani ya nyumba ya Mungu.
  3. Vigezo vya viongozi thabiti wa kuliongoza Kanisa.
  4. Agizo kwa Timotheo kuwa kamili katika utumishi wake.

Haya ni maelezo mafupi Kwa kila kipengele.

1) Kujilinda na waalimu wa Uongo.

Paulo anamhiza Timotheo lengo kubwa la kumtaka abaki Efeso ni ili awazuie watu wasifundishe elimu nyingine.

1 Timotheo 1:3

[3]Kama vile nilivyokusihi ukae Efeso, nilipokuwa nikisafiri kwenda Makedonia, ili uwakataze wengine wasifundishe elimu nyingine;

Elimu hiyo potofu aliyoina iliegemea kuwazuia watu wasile aina ya vyakula, Wasioe, pamoja na kuhubiriwa Hadithi za kizee, na nasaba (1:4, 4:7)

Kwa urefu wa mafundisho Hayo bofya hapa >>> HADITHI ZA KIZEE.

1 Timotheo 4:1-3

[1]Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

[2]kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe;

[3]wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

2) Namna ‘jinsia na marika’ mbalimbali yanavyopaswa yaenende ndani ya Kanisa la Mungu.

Kwa wanaume: Paulo anatoa agizo la kwamba wao wanajukumu la kusalisha kila mahali, lakini bila hasira wala majadiliano, yaani wawe safi kiibada (2:8)

Kwa Wanawake: Paulo anatoa agizo kuwa hawana ruhusa ya kufundisha katika kanisa (2:12), halikadhalika wanawajibu wa kuvaa mavazi ya kujisitiri, mapambo yao yawe yale ya rohoni na sio ya mwilini (2:9-10).

Anaendelea kusema Wanawake ambao ni wajane waandikwe katika kanisa ili Wahudumiwe kimahitaji, lakini wale ambao si wajane kwelikweli hawapaswi kuandikwa (5:4-16)

Wazee, na vijana wafanyapo makosa wasikemewe, Bali Waonywe kwa upole Kulingana na marika yao(5:1), lakini pale wafanyapo dhambi. kwa kukusudia au kuzoelea wakemewe mbele ya wote. (5:20),

Watumwa wote wanawajibu wa kuwaheshimu mabwana zao, si tu kwa wale wasiamini bali pia kwa wale waaminio wawaheshimu wote. (6:1)

Kanisa lina wajibu wa kuwaombea watu wote, na watawala, ili liishi katika utulivu, na amani, katika utauwa wote.(2:1-4)

3) Kuchagua viongozi thabiti wa kulichunga kanisa

Sehemu hii Paulo anamwagiza Timotheo juu ya vigezo vya maaskofu, na Mashemasi namna wanavyopaswa wawe, kwamba wawe watu wasio laumika, wameshuhudiwa mema na watu wa nje, waume wa wake mmoja mmoja, si watu wa kupenda fedha,si walevi, si waongofu wapya, wanapaswa wawe wakaribishaji,, wastahivu, wenye kiasi, waaminifu, wawasimamiao watoto wao vema, na wake zao, (3:1-13).

Lakini pia anawahimiza wazee wanaotawala vema wahesabiwe kuwa wamestahili heshima mara dufu (5:17).

4) Agizo la Paulo kwa Timotheo kuwa kamili katika utumishi wake.

Paulo anamwagiza Timotheo wajibu wake kama mwangalizi kuwa na upendo, Imani isiyo na unafki, na dhamiri njema, upole, saburi, na haki (1:5, 18-20, 6:11),

Anamwagiza afanye mambo yote bila upendeleo (1Timotheo 5:21).

Ajizoeshe kupata utauwa (4:8).

Awe kielelezo katika usemi na mwenendo (4:12)

Asiwaekee watu mikono kwa haraka,(5:22)

Akimbie tamaa ya fedha, na mashindano ya kidini (6:20).

Hitimisho.

Hivyo kwa ufupi, waraka huu ni wa kikanisa zaidi, na kwamba vigizo hivyo vikisimamiwa vema kanisa litakuwa imara, lenye heshima lisiloshitakiwa mabaya nje.

Ikiwa viongozi watachaguliwa hodari, na kila rika na jinsia likahudumu katika nafasi yake, yaani wanawake Kudumu katika upole, kujisitiri na kiasi na wanaume kuhudumu bila hasira wala majadiliano, huku waangalizi wakihakikisha mafundisho potofu hayapati nafasi. Ni ukweli kwamba kanisa hilo litakuwa imara sana.

Bwana akubariki

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mada nyingine:

Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)

Timotheo alikuwa wapi wakati anaandikiwa nyaraka zake na mtume Paulo?

Je ni kweli Tumejengwa juu ya Mitume na Manabii? (Waefeso 2:20)

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

Print this post

KANUNI YA KUFUNGUA MILANGO YA BARAKA.

Fahamu kanuni muhimu ya kufungua milango ya Baraka za rohoni na mwilini.

Neno la MUNGU linasema..

Waefeso 1:3 “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ALIYETUBARIKI KWA BARAKA ZOTE ZA ROHONI, KATIKA ULIMWENGU WA ROHO, NDANI YAKE KRISTO”.

Ni lini tulibarikiwa na baraka zote za rohoni?..Je ni jana au leo??.. Nataka nikuambie kuwa si jana, wala juzi wala mwaka uliopita wala si siku ile ulipozaliwa…. bali ni tangu siku ile damu ya Mwokozi YESU ilipomwagika msalabani tayari tulishabarikiwa,

Na si kubarikiwa tu, bali pia tayari tulishaponywa tangu siku ile Kristo aliposulibiwa, tayari tulishashinda tangu siku ile Kristo aliposulibiwa..

Sasa swali ni hili, kama tayari Baraka na ushindi tulishapewa tangu siku ile ya pale Kalvari, kwanini sasa hatuzioni hizo Baraka zetu katika roho na katika mwili?

Hili ndilo swali la msingi kujiuliza.. kwanini hatuzioni hizo Baraka tulizobarikiwa miaka mingi iliyopita.

Sababu kuu ya sisi kutoshiriki Baraka zote za rohoni ambazo tayari zilishaachiliwa juu yetu, miaka elfu mbili (2) iliyopita pale Kalvari ni “shetani”.

Anachokifanya adui ni kuzuia kupokea zile Baraka, na si kuzuia zisitoke!.. Tayari Mungu alishatubariki..wala hatuwezi kumwomba tena atubariki, ni sisi kupambania kilicho chetu.

Sasa ili tuweze kupokea kilicho chetu, ni lazima tupambane vita, na vita hivyo ni vile vya kiroho, kwani shetani na majeshi yake yamesimama kuhakikisha hatupokei kilicho chetu.. shetani hamzii MUNGU kutoa, bali anatuzuia sisi kupokea… Na MUNGU tayari alishatoa, ila shetani anazuia tusipokee..

Ni sawa na mzazi aliyemtumia mwanae aliyeko shuleni fedha za matumizi kupitia anwani ya shule, halafu mwalimu mmoja azifiche zile fedha zisimfikie mtoto, hapo mtoto mwenye busara akishajua katumiwa fedha ana wajibu wa kuzifuatilia, na kuulizia na kama kuna shida kwa mwalimu, na kama akiona kuna shida basi aweza kushitaki ili tatizo litatuke, kwasababu atajua shida si mzazi bali ni mwalimu (sasa huu ni mfano tu).

Na mambo ya rohoni ni hivyo hivyo, BWANA MUNGU wetu alishatubariki kwa Baraka zote za rohoni.. kazi tuliyobakiwa nayo ni kushughulika na vizuizi vya sisi kupokea hizo Baraka.

Na silaha zifuatazo ndizo zinazoweza kuvunja vizuizi vyote na kuachia kilicho chetu.

   1. MAOMBI

Maombi (hususani yanayohusisha mfungo) ni silaha ya kwanza ya kuzipinga hila za adui zinazozuia Baraka zetu.. Mtu aliyejizoeza kuomba ni rahisi kupokea Baraka zote zilizoahidiwa na MUNGU, na mtu anayepungukiwa maombi ni kinyume chake.

   2. KUSOMA NENO.

Maombi bila Neno la Mungu ni sawa na bendera iliyokosa mlingoti… Mtu aombaye huku Neno la Mungu limejaa ndani yake, ni rahisi sana kuteka Baraka zake tofauti na yule asiyekuwa msomaji wa NENO, na kusoma Neno kunakozungumziwa hapa si kushika vifungu vya biblia, La!.. Unaweza kuwa umeshika vifungu elfu vya biblia na bado usiwe umelijua Neno.

Bali kusoma Neno kunakozungumziwa hapa ni  kule kujifunza kitabu baada ya kitabu na kujua maudhui ya kila kitabu katika ufunuo wa Roho.

    3. UTAKATIFU

Utakatifu wa mwilini na rohoni ni mkuki wa kumpiga yule mwovu aachie vinavyotuhusu.. kinyume chake uchafu na maisha ya dhambi ni kifungo kinachozuia Baraka zetu.

Sasa utauliza Baraka za rohoni na mwilini ni zipi?

Mfano wa Baraka za rohoni ni Amani, furaha, upendo, uvumilivu, upole, utu wema na mambo mengine yote mema yanayofanana na hayo, kwa ufupi ni Roho Mtakatifu na matunda yake (Wagalatia 5:22).

Na baraka za mwilini hamna haja ya kuziandika maana zinajulikana, ambazo ni zile zote zinazohusu mahitaji ya mwilini.

Je umepungukiwa na Baraka?…fahamu kuwa Maombi, Neno na Utakatifu ndio dawa ya kutibu hilo tatizo, wala usimnung’unikie MUNGU kwanini hakubariki.. yeye tayari alishatubariki, ni sisi kupambana kupata vilivyo vyetu..Anza mapambano hayo kuanzia sasa ikiwa tayari umeshampokea Bwana YESU.

Na kumbuka mapambano haya hamna siku yatapoa, hata baada ya kuwa mtumishi.. ni jambo endelevu daima mpaka safari ya maisha inaisha, kwani pia kuna kupokonywa na yule aliyetuzuia tusipokee, ikiwa hatutasimama katika mambo hayo makuu matatu, na mengine yanayofanana na hayo.

Hivyo ukristo ni mapambano, ni vita, lakini vyenye nafasi kubwa ya kushinda Zaidi ya kushindwa kwa msaada wa Roho Mtakatifu.

Warumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote TUNASHINDA, NA ZAIDI YA KUSHINDA, kwa yeye aliyetupenda”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KAMA MWIZI USIKU WA MANANE.

MILANGO YA KUZIMU.

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

CHAKULA CHA ROHONI.

MILANGO YA KUZIMU.

Print this post

Je! watu wanapaswa wakemewe au wasikemewe kulingana na 1Timotheo 5:1 na 20?

SWALI: Je! watu wanapaswa wakemewe au wasikemewe pale wanapofanya dhambi kulingana na 1Timotheo 5:1 na 20?


JIBU: Tusome,

1 Timotheo 5:1-2

[1]Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 

[2]wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote. 

Na,

1 Timotheo 5:20

[20]Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope. 

 Mwandishi anatoa maelezo katika mazingira mawili tofauti. Mazingira ya kwanza ni katika eneo la marekebisho na mazingira ya pili ni katika eneo la makosa ya makusudi.

Kwamfano katika vifungu hivyo vya kwanza, anavyosema Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;analenga hasaa katika makosa ambayo yanajitokeza katikati ya huduma au maisha ya kikristo, kwamfano pengine mtu katika kuhudumu kwake kaonyesha uvunjifu fulani wa nidhani ya kimadhabahu, au kasema lugha isiyo ya staha, au kavaa vazi lisilo na heshima, au kabagua wengine, au kawadhulumu wengine, n.k. ambayo imesababishwa na uchanga wa kiroho au madhaifu ya kibinadamu.

Katika mazingira kama hayo Paulo anamhimiza Timotheo, kulingana na marika yao asitumie kukemea bali awaeleze kwa upole, nao watajirekebisha, akitambua kuwa wapo katika hatua za kuutafuta ukamilifu.

Lakini katika hivyo vifungu vya pili. Analenga Zaidi kwa wale wanaodumu kutenda dhambi. Wanaojua kabisa wanachokifanya sio sahihi, lakini wanaendelea kudumu kufanya hivyo, Paulo anasema hawapaswi kuvumiliwa bali kukemewa mbele ya watu wote.

Kwamfano mtu ni mzinzi, na tabia hiyo anaendelea nayo kanisani, au ni mlevi, au mchonganishi, sasa hawa wanapaswa wakemewe hadharani bila kujali marika yao, ili wengine wasiige Tabia hizo. Kwasababu wakiachwa wataendelea kulichachusha kanisa.

Makanisa mengi leo hii yamekumbwa na matatizo makubwa mpaka kusababisha jina la Kristo kutukanwa Nje, ni kutokana na kuvumiliwa kwa watu wa namna hii wanaodumu katika kutenda dhambi.  

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuna hukumu za aina ngapi?

Mikono iliyotakata ni mikono ya namna gani? (1Timotheo 2:8).

USIZISHIRIKI DHAMBI ZA WATU WENGINE.

Print this post

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha pili cha  Petro (2Petro).

Kama kitabu kinavyojitambulisha, “Waraka wa pili wa Petro kwa watu wote”

Petro ndiye mwandishi. Ni waraka mfupi, aliouelekeza kwa watakatifu wote duniani.

Na haya ndio maudhui yake makuu; 

  1. Kuwahimiza wakristo kuendelea kukua katika Imani.
  2.  Kuwathibitishia watakatifu ushuhuda wao kwamba haukutokana na hadithi za kutungwa kwa werevu bali ushuhuda wa macho.
  3. Kuwaonya wajiepushe udhalimu wa  manabii wa uongo.
  4.  Halikadhalika kuwapa tumaini juu ya ujio wa Bwana Yesu Kristo.
  5.  Na Uthabiti wa nyaraka za mitume kwao.

Haya ndio maelezo ya kila kipengele kwa ufupi;

1) Himizo la Ukuaji wa kiroho.

Petro anawahimiza watakatifu wasikwamwe kiroho bali waendelee kukua, mpaka kufikia utimilifu wao ambao ni upendo, Na kwamba mtu asipojitahidi kufanya hivyo matokeo yake ni kuwa atakuwa mvivu, na hatimaye atajikwaa.

 

2 Petro 1:3-8

[3]Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. 

[4]Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa. 

[5]Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa, 

[6]na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa, 

[7]na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo. 

[8]Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo. 

 

2) Uthibitisho wa ushuhuda wao.

Mtume Petro anatoa hakikisho la ushuhuda wao juu ya ujio wa Kristo, kwamba hawakuupokea katika hadithi zilizotungwa kwa werevu, bali walishuhudia wao wenyewe kwa macho, walipotokewa na Musa na Eliya juu ya mlima ule mrefu na kuisikia sauti ya Mungu mbinguni  moja kwa moja ikimshuhudia Yesu kuwa ndiye mwana wa Mungu, aliyependwa naye.

 

2 Petro 1:16-17

[16]Maana hatukufuata hadithi zilizotungwa kwa werevu, tulipowajulisha ninyi nguvu zake Bwana wetu Yesu Kristo na kuja kwake; bali tulikuwa tumeuona wenyewe ukuu wake. 

[17]Maana alipata kwa Mungu Baba heshima na utukufu, hapo alipoletewa sauti iliyotoka katika utukufu mkuu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. 

[18]Na sauti hiyo sisi tuliisikia ikitoka mbinguni tulipokuwa pamoja naye katika mlima ule mtakatifu. 

 

3) Tahadhari dhidi ya manabii wa uongo.(2:1-22)

Lakini pia anawahimiza kujiepusha na manabii wa uongo, ili  wasije wakachukuliwa na makosa Yao, wakaangamia tena. Ambao sifa zake nyingi ameziorodhesha pale (kwenye sura yote ya pili), Sifa zao ni pamoja na tamaa na uzinzi, akiwataja kama watu wasiokoma kutenda dhambi, wasaliti wa Bwana, wenye uhodari wa kutunga maneno wenye werevu, ili wawavute watu kwao, wenye kupenda ujira wa udhalimu kama Balaamu, watoao maneno ya makufuru, watu wa kujikinai, wasio na hofu ya Mungu, watu wa anasa, wa kuhadaa watu waliosimama imara, ili wawaaungushe.

2 Petro 3:17

[17]Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 

 

4) Tumaini juu ya ujio wa Yesu Kristo.

Petro pia anawahimiza watakatifu wawe na tumaini juu ya uthabiti wa kurudi kwa Bwana,

akiwatahadharisha juu ya kuibuka kwa kundi la watu wenye kudhihaki, wanaosema iko wapi ile ahadi,mbona muda mrefu umepita? lakini Petro analirekebisha kwa kulitolea maelezo kuwa Mungu hakawii kutimiza ahadi yake bali anavumilia ili watu wote wafikie toba. Lakini siku hiyo itakuja kama mwizi, na ulimwengu ukaliwao na waovu utaharibiwa.

2 Petro 3:9-13

[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. 

[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. 

[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa, 

[12]mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka? 

[13]Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 

 

5) Uthibitisho wa nyaraka za mitume. (3:15-18)

Mwisho, mtume Petro anaeleza uthabiti wa yale anayowaeleza, akiwatolea mfano kwa kurejea pia nyaraka za mitume wengine (akimtaja Paulo).Kama pia anayaeleza mambo hayo hayo ayasemayo katika nyaraka zake.

Petro 3:15-16

15 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi
Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa;
16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika
nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu,
wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao
wenyewe.

Hivyo kwa ujumla maudhui ya waraka huu ni kuwahimiza watakatifu kufanya bidii katika ukamilifu na kujiepusha na manabii wa uongo, na kuchoka kungojea ahadi za Mungu. Bali waendelee mbele kutibitika katika ukamilifu bila wala wala hila hadi siku ya kutokea kwake Bwana Yesu mara ya pili.

Je wewe kama mkristo unayemngojea Bwana. Unafanya imara wito wako na uteule wako, kwa kukua kila siku katika neema kiasi cha kukufanya ujione huna mawaa wala aibu, katika siku ile ya Bwana? 

Kama sio, basi wakati ndio huu, Maanisha kugeukia kumfuata Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

Fahamu Mwandishi wa kitabu cha Waebrania ni nani.

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha kwanza cha Petro.(1Petro)

Kichwa cha kitabu hichi kinasema “Waraka wa kwanza wa Petro kwa watu wote” Kutuonyesha kuwa Petro Ndiye mwandishi.

Waraka huu mfupi aliuelekeza kwa watakatifu wote waliotawanyika, na kuishi kama wageni maeneo ya Asia ndogo ambayo kwasasa ni nchi ya Uturuki.

Maudhui makuu ya waraka huu tunaweza kuyagawanya katika sehemu kuu nne(4):

1) Ni kuwafariji watakatifu kwa kuwaeleza juu ya utukufu walioandaliwa mbinguni utakaofunuliwa siku ya mwisho. Na kwamba kwa kulitambua hilo basi wafurahi Katika majaribu mbalimbali ya imani, yaliyo ya kitambo tu.

2) Lakini pia unalenga kuwahimiza kuishi maisha ya utakatifu ya kumpendeza Mungu katika wakati wao wa kuishi hapa duniani.

3) Vilevile wajibu wakuishi maisha ya nidhamu katika Jamii ya wasioamini inayowazunguka.

4) Halikadhalika wajibu wa viongozi kulichunga kundi la Kristo kwa uaminifu wotena wajibu wa kanisa lote kumpinga shetani.

Haya ni maelezo mafupi juu ya kila kipengele:

1) Faraja katika dhiki mbalimbali.

Petro anawahimiza watakatifu kwamba wafurahi katika majaribu mbalimbali (kuliko kuhuzunika) kwa sababu ya uthamani mkuu wa imani yao itakayolipwa siku ile ya mwisho ambayo Yesu atafunuliwa kwetu.

1 Petro 1:6-7

[6]Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;

[7]ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

> Petro Anahimiza kuiga kielelezo cha Kristo ambaye yeye alikubali kuteswa ijapokuwa hakutenda Dhambi, hata alipotukanwa hakurudisha majibu. Vivyo hivyo na sisi tukubali teso lolote kwa ajili yake katika upole wote, uvumilivu na ustahimilivu.

1 Petro 2:19-21

[19]Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.

[20]Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.

[21]Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.

1 Petro 4:12-16

[12]Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.

[13]Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.

[14]Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.

[15]Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.

[16]Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.

2) Wito wa kuishi maisha matakatifu.

Sehemu hii ya pili Mtume Petro anawahimiza watakatifu, kuwa kwasababu wanatazamia neema itakayofunuliwa siku ya mwisho ya kuja kwake Yesu Kristo (1:13), hivyo hawana budi kuishi maisha ya kiasi na utakatifu hapa duniani.

1 Petro 1:13-16

[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.

[14]Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;

[15]bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;

[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

1 Petro 2:1-2

[1]Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

[2]Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;

> Petro anaendelea kuwasihi watakatifu waishi kama wapitaji duniani, kwa kuziepuka tamaa za mwili.

1 Petro 2:11

[11]Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.

1 Petro 4:2-3

[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

> Anaeleza pia Wajibu wa kupendana kuhurumiana, kunyenyekeana, tuwe watu wasiolipa baya kwa baya, bali wenye kubariki(3:8-12, 4:7)

> Kadhalika pia anaeleza wajibu wa wanandoa. Kwamba wake wawatii Waume zao, na kujipamba kwao kunapaswa kuwe kwa mapambo ya rohoni, Lakini pia waume kuishi na wake zao kwa akili. (3:1-7)

3) Mwenendo wa nidhamu kwa watu walio nje

Katika sehemu hii ya tatu anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaopasa kwa watu wasioamini, ili wakose nafasi ya kutushitaki au kutulaumu kwa lolote.

> Anagusia katika eneo la watumwa Kwamba wawatii bwana zao, si wale tu wapole bali pia wale wakali.(2:18)

> Lakini pia Watakatifu waitii kila kilichoamriwa na mamlaka.

1 Petro 2:13-15

[13]Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;

[14]ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.

[15]Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;

> Lakini pia anahimiza watakatifu wawaheshimu watu wote(2:17)

4) Wito kwa viongozo wa kanisa.

Mwishoni Petro anatoa wito wa waangalizi wa kanisa la Mungu (wazee), kwamba walichunge kundi kwa hiari, sio kwa kulazimishwa au kutazamia malipo ya kifedha, bali kwa moyo.

1 Petro 5:1-3

[1]Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;

[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.

[3]Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.

> Pamoja na hayo anasisitiza watakatifu wote wawe na kiasi na kukesha, kwasababu adui yetu ibilisi ni mfano wa simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo wana wajibu wa kumpinga sikuzote.(5:8-9)

Hitimisho: 

Hivyo kwa maelezo machache ni kwamba Petro analihimiza kanisa kutembea katika uvumilivu wote na uthabiti Wa imani, pamoja na utakatifu, na kutimiza wajibu wao katika utakatifu na adabu kwa wanadamu wote, katika wakati ambao kanisa linasubiria neema kuu itakayofunuliwa siku ya mwisho Yesu atakaporudi.

Na ndivyo ambavyo sote tunapaswa tuishi hivyo sasa.

Kama mkristo je unaendelea kufurahi katika majaribu? Unaishi maisha matakatifu? Unaishi vema na jamii yako? unaifanya kazi ya Mungu? Unampinga shetani kwa kudumu katika sala?

Ikiwa hayo, unayazingatia basi, wewe ni mshirika wa neema hiyo kuu ya Mungu itakayofunuliwa siku ya mwisho.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Epafra ni nani katika biblia? (Wakolosai 1:7)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

Print this post

KUSUDI LA KWANZA LA KUCHAGULIWA NA MUNGU NI LIPI?

Je wewe ni miongoni mwa waliochaguliwa sawasawa na andiko hili?…

Waefeso 1:11 ”na ndani yake sisi nasi tulifanywa urithi, huku tukichaguliwa tangu awali sawasawa na kusudi lake yeye, ambaye hufanya mambo yote kwa shauri la mapenzi yake”.

Kama wewe ni miongoni mwa waliochaguliwa basi fahamu lengo/kusudi la kwanza la wito wa MUNGU kwako ni lipi?..

Hebu tuusome wito wa Mtumishi wa Mungu Paulo, tuweze kujua nia ya Kristo ipi…

Matendo 22:13 “Akanijia, akasimama karibu nami, akaniambia, Ndugu yangu Sauli, uone. Nikamwinulia macho yangu saa ile ile.

14 Akasema, Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe upate KUJUA MAPENZI YA MUNGU, na kumwona yule Mwenye haki, na kuisikia sauti itokayo katika kinywa chake”.

Hapo anasema “Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe upate kujua MAPENZI YAKE..”...Jiulize kwanini ataje jambo la kwanza “mapenzi ya Mungu”.

Kumbe lengo la kwanza la Mungu kumwita Paulo ni yeye “kuyajua mapenzi ya Mungu”. Na mengine ndiyo yafuate..

Na ni sahihi kabisa kwani Bwana YESU mwenyewe alituambia maneno yafuatayo…

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye AFANYAYE MAPENZI YA BABA YANGU ALIYE MBINGUNI”.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”

Umeona?..kwahiyo kumbe Bwana anataka tuyajue sana mapenzi yake na tuyafanye..

Je unayajua mapenzi ya Mungu??…na je unayafanya pia?.

Mapenzi ya MUNGU ni haya…

1 Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.

 1. Utakaso ni sehemu ya mapenzi ya MUNGU kwako.

(Na unatakasika kwa maombi, mifungo, kusoma Neno, na kuhudhuria ibada).

 2. Pia Kuuweza mwili katika utakatifu na heshima ni sehemu ya mapenzi ya MUNGU kwako.

(Maana yake mwili wako kuuweka katika hali ya heshima, ikiwemo kuvaa mavazi ya heshima na staha, ikiwemo kutojichubua, na kutofanya uasherati na mambo yote yanayohusika kuuchafua mwili”.

Yajue mapenzi ya MUNGU, yafanye mapenzi ya MUNGU.

Kwa urefu zaidi kuhusu Mapenzi ya MUNGU fungua hapa》》MAPENZI YA MUNGU NI YAPI?

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa pili (2Wakorintho)


Kama kichwa cha waraka Huu kinavyosema… “Waraka wa pili wa Paulo Mtume kwa Wakorintho”

Kutuonyesha kuwa Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hichi..

Tunaweza kukigawanya katika sehemu kuu tatu (3)

1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)

2) Utoaji bora kwa mkristo.(Sura ya 8-9)

3) Utetezi wa huduma ya Paulo (10-13)

Sehemu ya kwanza:

1) Utendaji kazi wa Mungu, na wajibu wa watakatifu katika huduma na maisha yao ( sura ya 1-7)

Katika sura hizi, Mtume anagusia maeneo kadha wa kadha, kama ifuatavyo.

i) Faraja ya Mungu

Paulo anatoa shukrani zake kwa jinsi Mungu anavyoweza kuwafariji watu wake katikati na dhiki na majaribu mazito. Akimtaja Mungu kama ni ndio mtoa faraja yote, katika dhiki zetu. (1-3-7)

2 Wakorintho 1:3-4

[3]Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;

[4]atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.

ii) Nafasi ya kutubu.

Sehemu inayofuata Paulo anaeleza sababu ya kutofika Korintho haraka, kama ilivyodhaniwa. Ni ili asilete tena huzuni zaidi kama akiwakuta bado hawajakamilika. Na hiyo ni kutokana na kuwa hawakuwa na mabadiliko ya haraka kwa agizo lake la kwanza, hivyo hakutaka afanye ziara ya ghafla bali wayatengeneze kwanza wao wenyewe ili ziara yake kwao, safari hii iwe ya raha na sio ya hukumu.(1:23-2:4)

 iii) Wajibu wa kusamehe. (2:5-11)

Paulo anawahimiza wakorintho kusamehe kwa wale watu wanaoleta huzuni ndani ya kanisa, Hususani waliomnenea vibaya utume wake. Anahimiza kuliko kusimamia adhabu ziwapasazo ambazo wana haki kweli ya kuzipokea. Kinyume chake wawasamehe ili wawapate tena wasipotee kabisa katika huzuni zao.

IV) Utukufu wa agano jipya.(sura ya 3-5)

Paulo Anaeleza jinsi gani, agano jipya utukufu wake ulivyo mbali na ule wa agano la kale. Kwasababu utukufu wa agano jipya umekuja Katika Roho atoaye uhuru.

Paulo anaeleza kwasababu hiyo hatupaswi kulegea kwa kuenenda kwa hila au kulichanganya Neno la Mungu na uongo. Au kwa kutohubiri injili. Bali kufanya yote bila kujali utu wetu wa nje kuchakaa. Tukijua kuwa ule wa ndani unafanywa upya siku baada ya siku na kwamba ipo siku tutasimama mbele ya kiti hukumu kutoa Hesabu ya mambo yetu yote tuliyoyatenda katika mwili.

Paulo anaeleza kwamba kama Kristo alivyopewa huduma ya upatanisho sisi pia tumepewa Neno Hilo hilo ndani yetu. Kuupatanisha ulimwengu na Mungu kupitia Yesu Kristo. Akionyesha kuwa ni wajibu wetu sote kuhubiri injili.

V) Maisha ya ukamilifu (sura ya 6-7)

Paulo anawasihi Wakoritho waikunjue mioyo yao na waishi maisha ya ukamilifu na ya uangalifu wasiwe kwazo la namna yoyote ili utumishi wao usije laumiwa siku ile ya Bwana

Lakini pia anawapa onyo wasiwe na ushirika na wasioamini.

Pamoja na hilo katika sura ya saba, Paulo anaeleza furaha yake kwa Wakorintho Kwa kuitii toba..kufuatana na waraka aliowaandikia hapo kabla wa huzuni ( Ambao haupo miongoni mwa nyaraka hizi zilizo kwenye biblia). Ambapo walipousoma walitubu na kugeuka, kwelikweli. Kuonyesha utii wa toba. Ambao unapaswa uonekane ndani ya makanisa hata sasa.

Sehemu ya Pili:

2) Utoaji bora kwa mkristo.(8-9)

Katika sura ya 8-9

Paulo anahimiza michango kwa ajili ya watakatifu walio Yerusalemu, Akitolea mfano watakatifu wa Makedonia jinsi walivyoweza kutoa kwa ukarimu hata katika umaskini wao, vivyo hivyo na wao anawahimiza wawe na moyo huo huo. Akiwaonyesha jinsi Bwana wetu Yesu alivyotupa kielelezo cha kukubali kuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

2 Wakorintho 8:9

[9]Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Kwasababu utumishi wa namna hiyo sio tu unawapata watakatifu rizki lakini pia huleta matunda ya shukrani kwa Mungu.

2 Wakorintho 9:12

[12]Maana utumishi wa huduma hii hauwatimizii watakatifu riziki walizopungukiwa tu, bali huzidi sana kuwa na faida kwa shukrani nyingi apewazo Mungu;

Sehemu ya tatu:

3) Utetezi wa huduma yake (Paulo). Sura ya 10-13

Katika sura hizi Paulo anaitetea Huduma yake dhidi ya watu wengine wanaojitukuza mbele za watu, kana kwamba ni mtume wa kweli kumbe ni mitume wa uongo, ambao huwashawishi watu kwa majivuno ya nje na ukali, lakini si ya kazi.

2 Wakorintho 11:20

[20]Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.

Hivyo Paulo anawaeleza kwa upana uthabiti wa huduma yake, tangu asili ya kabila lake, mateso aliyopitia, akionyesha mpaka kusimama vile, hakukutokea hivi hivi tu, bali katika masumbufu mengi, anawaeleza pia maono aliyoyafikia mpaka kunyakuliwa mbingu ya tatu, hiyo yote ni kuwaonyesha wakorintho kama wanataka kuamini kwa watu wanaojisifia basi yeye anawazidi wao, lakini hatumii njia hiyo, bali ya udhaifu ili asihesabiwe zaidi ya vile watu wavionavyo Kwake.

Salamu za mwisho.

Anahimiza wakoritho wanie Mamoja, watimilike na wafarijike.

Hivyo kwa ufupi mambo haya makuu tunaweza kuyapata katika waraka huu;

  1. Faraja za Mungu katika majaribu
  2. Huduma ya Upatanisho tuliyopewa ndani yetu, kuwapatanisha waovu kwa Mungu.
  3. Utukufu bora wa agano jipya, jinsi ulivyo mbali na ule wa agano la lake
  4. Nguvu tulizonazo katika udhaifu
  5. Utoaji umpendezao Mungu, kwa kukubali sisi kupoteza kwa ajili ya wengine.
  6. Lakini pia Namna bora ya kuithibitisha huduma ya kweli, si katika majivuno bali katika matunda ya kazi

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Fahamu maana ya 2 Wakorintho 8:9 alikuwa maskini ili sisi tuwe matajiri kwa umaskini wake.

Uchambuzi na mwandishi wa kitabu cha Waefeso.

Fahamu ni nani aliye mwandishi wa kitabu cha Mathayo.

Rudi Nyumbani

Print this post

WAKRISTO WA UONGO.

Je unajua nguvu ya manabii, wachungaji, mitume, waalimu na wainjilisti wa uongo inatoka wapi?

Si kwingine zaidi ya kwa wakristo wa uongo!..

Labda utajiuliza wakristo wa uongo ni wapi?

Wakristo wa uongo ni wale wenye majina ya kikristo, na madhehebu ya kikristo, na wenye kukiri ukristo lakini mioyoni mwao hawana Nia ya uzima wa milele bali vitu vya duniani,

Ni wale ambao sababu kuu ya kuomba ni kupata mali, sababu kuu ya kwenda kanisani ni kupata wapenzi, sababu kuu ya kutoa sadaka ni ili wabarikiwe wawe na vingi katika ulimwengu, lakini hawawezi kufunga na kuomba na kutoa ili Bwana awape utakatifu, hawawezi kutoa sadaka ili Bwana awakirimie vipawa vya rohoni, wala hawawezi kufunga na kuomba ili mahusiano yao na MUNGU yaongezeke.

Huwapendi kusoma Neno kabisa…

Sasa ongezeko la hili kundi la wakristo wa uongo, ndilo linalowapa nguvu na kiburi manabii wa uongo.

Kwani wateja wakubwa wa manabii wa uongo ni wakristo wa uongo…

Kama wakristo wa uongo wasingekuwepo manabii wa uongo wangepotea wote, kwani wangekosa wateja, lakini kwasababu manabii wa uongo wanaona kazi hiyo inalipa na wateja wao wa kwanza ni wakristo na tena hawatumii nguvu nyingi basi ndio wanazidi kuongezeka na kutanuka.

Kwani mali wanazozipata zote zinatoka kwa wakristo wa uongo, ambao wanatoa sadaka ili wapate vya ulimwengu, na hivyo manabii wa uongo wanachukua hiyo nafasi ya kuwadanganyia vitu vya ulimwengu na kuwachukulia mali zao.

Sasa si kwamba manabii wa uongo hawakuwepo miaka ya zamani tofauti na miaka hii…walikuwepo!! tena wengi tu!!…lakini ni kitu gani kilichowafanya wasiwe na nguvu au wasivume katika nyakati hizo kama wanavyovuma sasa katika nyakati hizi??.

Jibu ni rahisi…ni kwasababu nyakati za nyuma, hakukuwa na jopo kubwa la wakristo wa uongo ukilinganisha na sasa…

Nyakati za nyuma, mtu akitangaza maombi ya kupokea mambo ya kidunia hakuna mtu anahudhuria hiyo ibada, kanisani ilikuwa ni mahali pa mifungo na maombi kwaajili ya watu kujengwa roho zao na kuimarisha mahusiano yao na MUNGU, watu walikuwa wanajua kabisa mahusiano yao na MUNGU yakiwa sawa basi hiyo ni zawadi tosha hayo mengine watazidishiwa, hivyo hakukuwa na mtu anayedanganywa, na manabii wa uongo wakawa hawapo, kwasababu wateja hawapo..

Lakini sasa ni kinyume chake, mahali watu wanapoambiwa wafunge na kuomba ili wajazwe Roho Mtakatifu hawaendi, bali mahali wanapoambiwa wafunge na kuomba ili wapate vitu vya ulimwengu, hapo ndipo wanapojaa…unategemea vipi manabii wa uongo wasipate nguvu??…(kwao biashara imefunga, ni msimu wa kuvuna).

Ni majira yao, kwani wateja wameanza kuonekana…wakristo wamebadilika, sasa wanataka vya ulimwengu zaidi ya vya MUNGU, ni msimu wa mavuno..

Kwahiyo kuna shida kubwa katika wakristo wa siku za mwisho, zaidi ya manabii wa siku za mwisho.

Je wewe ni mkristo yupi?

Ni mkristo wa kumtafuta MUNGU ili ujenge nyumba na kuendesha gari au yupi?..

Ni kweli hayo tunayahitaji sana, lakini yamezidi kiasi kwamba sasa yamegeuka kuwa ibada, magari yamegeuka kuwa mungu, nyumba zimegeuka kuwa sifa, na fedha ndio nyimbo za kuabudu.

Ndugu, ukatae ukristo wa uongo, kwasababu ni roho kamili ya shetani….

Kwanza Bwana alisema itatufaidia nini tupate dunia yote halafu tupate hasara za nafsi zetu..

Marko 8:36 “Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?”.

Ni heri tumtafute Bwana kwanza kwa lengo la kupata matunda ya roho…

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.

Hayo mengine tumeambiwa tutazidishiwa, na hata yasipokuja katika kiwango tunachokitaka pia sio lazima…maadamu tunaye KRISTO huo ni utajiri mkubwa zaidi ya vyote vya ulimwengu.

Hebu jiulize ni lini umefunga, na kutoa sadaka ili tu MUNGU aondoe madhaifu na makosa ndani yako, ili MUNGU akutakase usimtende dhambi, ili MUNGU akuonyeshe mapenzi yake?.

Kama hujawahi kufanya hayo, au yanayofanana na hayo basi kuna shida, hebu badilisha gia, toka katika kundi la wakristo wa uongo bali kuwa bibi harusi wa kweli wa Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

USIRUDI NYUMA KATIKA IMANI

Tukiwa bado tupo mwanzo wa mwaka, ni wakati wa kushika sana vile tulivyo navyo na kuendelea mbele, wala si wakati wa kurudi nyuma kabisa.

Usiyarudie mambo ya kale uliyoyaacha, usiyatamani mambo ya kale uliyoyakimbia, usiirudie njia  ya kale uliyoikataa…

Ulikuwa upo mbali na anasa mwaka jana, basi huu si mwaka wa kuzirudia tena, usirudie ulevi uliouacha miaka ya nyuma, usirudie uzinzi ulioushinda miaka ya nyuma, usirudie kujichua ulikokuacha miaka ya nyuma,

Usirudie mavazi yasiyo na staha uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie wala kuitamani mitindo ya kidunia uliyoiacha mwaka jana.

Usirudie starehe za kidunia, mwanzo huu wa mwaka ni wakati ambao shetani anafanya kazi kubwa sana kuwarudisha watu nyuma kiroho, na atashambulia mambo yafuatayo ili kuhakikisha mwamini anarudi nyuma kiroho.

    1. Afya.

Atajaribu kukuletea mashambulizi katika eneo la afya, kwa kuitikisa afya yako au ya watu wako wa karibu, ikiwemo pia afya ya uzazi.. Simama endelea mbele usirudi nyuma!.

     2. Uchumi.

Atajaribu kutikisa uchumi wako lakini, hawezi kuondoa baraka zako za mwaka, hivyo usitishwe na vimitikisiko vya uchumi vya ibilisi vya hapa na pale, ni vya muda tu wewe endelea mbele usirudie biashara haramu wala tamaa za mali ulizoziacha huko nyuma endelea mbele kwani Bwana anakujua.

     3. Ndoa.

Atakuletea vimitikisiko vya kifamilia vya hapa na pale, pia visikutishe kwani ni kawaida yake kutishia, lakini wewe endelea mbele na imani usirudie magomvi uliyoyaacha miaka ya nyuma, usirudie anasa za kupunguza mawazo ulizoziacha huko nyuma…yapo mambo mazuri mbele yako kwaajili ya huu mwaka.

Pia ondoa hofu ya kesho…kwamba itakuwaje kesho, itakuwaje disemba…ndio usijizuie kutafakari yajayo, lakini usiufanye moyo wako kuwa mzito kwaajili ya hayo, kwani huo pia ni mlango mwingine wa ibilisi kumrudisha mtu nyuma.

Ukiwa ndani ya Kristo fahamu kuwa mambo yote yatakuwa sawa, haijalishi itachukua muda gani au mambo yanaanzaje…kushinda ni lazima! na ni AMRI.

Usirudi nyuma Baba, usirudi nyuma Mama, usirudi nyuma kaka, usirudi nyuma dada, usirudi nyuma mtoto…kwani matokeo ya kurudi nyuma ni kumfadhaisha Bwana.

1 Samweli 15:11”Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia BWANA usiku kucha”.

Utakapofika mwisho wa mwaka tena uwe na sababu ya kumshukuru Bwana kama amekulinda hujarudi nyuma.

Ayubu 23:12 “Sikurudi nyuma kuiacha amri ya midomo yake; Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu”.

Lakini kama ulikuwa umeshaanza kurudi nyuma, bado hujachelewa hebu kataa hiyo njia na leo mwombe Bwana rehema na kuziacha hizo njia utaona maajabu ya Bwana, kwani atakutia nguvu na utaendelea mbele kwa mbio kubwa, Bwana atakurehemu na utamfurahia.

Hosea 14:4 “Mimi nitawaponya kurudi nyuma kwao; nitawapenda kwa ukunjufu wa moyo; kwa maana hasira yangu imemwacha”.

Isaya 50:5 “Bwana MUNGU amenizibua sikio langu, wala sikuwa mkaidi, wala sikurudi nyuma

Lakini usipojali na kuendelea katika njia hiyo ya kurudi nyuma, ipo hatari mbele yako..

Mithali 1:32  “Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua,

Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza”

USIRUDI NYUMA! USIRUDI NYUMA!…USIRUDI NYUMA!.

Ukiwa utahitaji msaada wa maombezi ili uzidi kusimama, basi piga namba hizi 0789001312.

Bwana anakupenda, na Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.

SHIKA SANA ULICHO NACHO, ASIJE MTU AKAITWAA TAJI YAKO.

USIIGE TABIA YA NAAMANI

Rudi Nyumbani

Print this post

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza 

Kitabu hichi ni moja ya nyaraka   zilizondikwa na  mtume Paulo katika agano jipya, 

Waraka huu amegusia mambo mengi, hasahasa katika eneo la marekebisho na maonyo. Unagusia nidhani na taratibu za kikristo zinazopaswa zifuatwe ndani ya  kanisa, unazungumzia pia eneo la uhalisia wa ufufuo wa wafu katika siku ya mwisho pamoja eneo la upendo.

Na huu ndio uchambuzi wake katika maeneo mama; 

1) Matabaka ndani ya kanisa. (1:10-17, 3:1-4:21)

Paulo anatoa onyo juu ya migawanyo ambayo ilianza kutokea ndani ya kanisa iliyozaa  wivu na fitina, ambayo ilisababishwa kwa baadhi ya watu kujiwekea matabaka kwa kujivunia viongozi kwa kusema mimi ni wa Paulo, mimi ni wa Apolo, mimi ni wa Kefa. Akiwatahadharisha na kuwasihi  kwa kuwaeleza kwamba wao ni wahudumu tu katika nafasi mbalimbali, bali mkuzaji ni Kristo. Na hivyo hawapaswi kujivunia wao, bali Kristo

2) Usahihi juu ya hekima ya Mungu

Kristo ni hekima ya Mungu na nguvu ya Mungu.(1:18- 2:16)

Eneo la pili Paulo anatoa ufahamu hasaa juu ya hekima anayoitambua Mungu, akionyesha kuwa hekima ya ulimwengu huu, kwa Mungu ni upuzi, bali hekima ya Mungu ameificha ndani ya Kristo Yesu, na hivyo amewachagua watu wadhaifu na wanyonge kuwadhihirishia hiyo. Akionyesha kuwa mtu asitegemee sana kumwona Mungu katika mambo yanayodhaniwa kuwa ni makuu, bali katika Kristo Yesu.

1 Wakorintho 1:24

[24]bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu. 

3) Nidhamu ya kimwili ndani ya kanisa la Kristo, (1Wakorintho 5-6)

 Katika eneo hili Paulo anastaajabishwa kwa kuzuka kwa zinaa mbaya ambayo haionekani hata  kwa mataifa yaani mtu na mzazi wake kuzini,. Akiwaagiza kutoa hukumu juu ya watu kama hao, hata kwa kuwakabidhi shetani (lengo ni waponyeke)

Kwasababu wakiachwa mwisho wao huwa ni kulichafua kanisa, (kulitia unajisi), 

Vilevile tunaona Paulo akitoa agizo kuwa kanisa halipaswi kuchangamana na wazinzi.

Akisisitiza kuwa mtakatifu sio tu awe amehesabiwa haki bali pia awe ameoshwa  na kutakaswa na udhalimu wote.

Anawaagiza pia watakatifu hawapaswi kupeleka mashtaka yao kwa watu wa kimataifa, bali kanisa ni zaidi ya mahakama ambayo watakatifu wanapaswa watatulie migogoro yao hapo. 

4) Ndoa na useja. (1Wakorintho 7)

Paulo anaeleza kwa upana, taratibu ya kindoa, katika eneo la haki zao za ndani na kuachana, na wito wa utowashi(useja). Katika eneo la haki, anasisitiza kuwa kila mwanandoa anapaswa atambue kuwa hana haki juu ya mwili wake mwenyewe, bali mwenzake, lakini pia katika kuachana, anaeleza ikiwa mwanandoa mmoja haamini, Yule aliyeamini hapaswi kumwachwa mwenzake, ikiwa bado anataka  kuendelea kuishi naye. Lakini pia anatoa pendekezo lake Mtu akitaka kumtumikia Mungu kwa wepesi zaidi bila kuvutwa na mambo ya mwilini na dhiki za kiulimwengu. Basi akikaa bila kuoa/kuolewa afanya vema zaidi.

5) Uhuru wa mkristo.(1Wakorintho 8-10)

Anaeleza jinsi gani mkristo anapaswa kukabiliana na dhamiri yake na ile ya wengine,katika maamuzi ayafanyayo kwa ujuzi wake,  akigusia eneo la vyakula (hususani vile vilivyotolewa sadaka kwa sanamu), kwamba hivyo havituhudhurishi mbele za Mungu, lakini tukila pia tuangalie wengine wanaathirikaje. Tusije tukawakwaza kwa ujuzi wetu. Paulo anaeleza ili tuweze kufikia hapo yatupaswa kuyafanya yote katika upendo.

1 Wakorintho 8:11-13

[11]Na yule aliye dhaifu aangamizwa kwa ujuzi wako, naye ni ndugu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake. 

[12]Hivyo, mkiwatenda dhambi ndugu zenu na kuitia jeraha dhamiri iliyo dhaifu, mnamtenda dhambi Kristo. 

[13]Kwa hiyo, chakula kikimkwaza ndugu yangu, hakika sitakula nyama hata milele, nisije nikamkwaza ndugu yangu. 

Lakini pia anaeleza haki waliyonayo mitume, kwamba wanaouwezo wa kula katika fungu la kanisa, lakini hawakutumia ujuzi wao wote, ili waweze kuifikisha injili kiwepesi kwa watu bila kuwazuilia na wengine.

6) Adabu na nidhani katika kukusanyika ndani ya  kanisa la Mungu( 1Wakorintho 11)

Paulo anatoa utaratibu wa ki-Mungu wa namna ya kuhudumu, kufuatana na hali ya kijinsia. Kwamba kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha mwanamume ni Kristo na kichwa cha Kristo ni Mungu. Hivyo mwanawake anapaswa wafunikwe vichwa awapo ibadani, ili kuonyesha kichwa chake(mumewe) kinamilikiwa na Kristo. Na kwamba wanawake wanapaswa watii uongozi (1Wakorintho 14:34-40)

Paulo anaeleza pia nidhani katika kushiriki meza ya Bwana, kwamba inapaswa ifanywe katika ufahamu na utaratibu sahihi wa rohoni, vinginevyo itapelekea hukumu badala ya baraka

7) Karama za Roho (1Wakorintho 12-14)

Paulo anazungumzia kwa undani karama mbalimbali ambazo Mungu ameziweka katika kanisa na kwamba zinapaswa ziwe kwa lengo la kufaidiana na kujengana. Lakini anaeleza kipawa kilicho bora zaidi ya karama zote, nacho ni upendo, ambacho anakieleza kwa urefu katika sura inayofuata ya 13, kwamba hichi kimezidi vyote.

1 Wakorintho 13:1-8

[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 

[2]Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 

[3]Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 

[4]Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 

[5]haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 

[6]haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 

[7]huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 

[8]Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 

8) Kufufuliwa kwa wafu. (1Wakorintho 15)

Katika eneo hili Paulo anahimiza  fundisho la kufufuliwa kwa wafu, akionyesha jinsi lilivyo umuhimu katika imani ya kikristo, na hiyo ni kutokana na baadhi ya watu waliozuka ndani ya kanisa kufundisha fundisho la kisadukayo kwamba hakuna ufufuo wa wafu. 

Akieleza jinsi Bwana atakavyokuja kwamba siku ya kurudi kwake parapanda italia na wote kwa pamoja (tulio hai na waliokufa) tutaipokea miili mipya ya utukufu itokayo mbinguni.

9) Michango kwa watakatifu. (1Wakorintho 16)

Katika sehemu hii ya mwisho Paulo anawaagiza juu ya utaratibu wa changizo kwa ajili ya watakatifu, kwamba vifanyike kila siku ya kwanza ya juma wakutanikapo, anawaagiza pia wakeshe, wawe hodari, na mambo yao yote yatendeke katika upendo.

Kwa hitimisho ni kuwa waraka huu unalenga hasa marekebisho, juu ya mambo mengi yaliyokuwa yanatendeka kwasababu ya ujinga, upumbavu, na dhambi ndani ya kanisa la Kristo. Na Ukweli ni kwamba mambo kama haya haya ni rahisi kuonekana hata katika kanisa la leo. Waraka huu tuusomapo yatupasa tuutazame kwa jicho la kikakanisa je! makosa kama ya wakorintho yapo katikati yetu, kama ni ndio basi tujirekebishe haraka sana.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Warumi.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi Nyumbani

Print this post