Category Archive Mafundisho

HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.

Je unaelewa maana ya kuwa Mwanafunzi?

Zifuatazo ni sifa za mwanafunzi.

   1. KUFUNDISHWA

   2. KUJIFUNZA.

   3. KUFANYA MITIHANI.

   4. KUHITIMU.

Mtu akikosa hizo sifa basi sio mwanafunzi.

Na kwa upande wa BWANA wetu YESU KRISTO ni hivyo hivyo (Tutazame moja baada ya nyingine).

       1. KUFUNDISHWA

Hakuna mwanafunzi yoyote anayejifundisha mwenyewe, ni lazima awe na mwalimu

Na vile vile Ili ukidhi vigezo vya kufundishwa na BWANA YESU mwenyewe ni “lazima ujikane nafsi”.. Na matokeo ya kukosa kufundishwa na Bwana ni kushindwa mitihani ya maisha ikiwemo VIPINDI VYA KUPUNGUKIWA na VIPINDI VYA KUWA NA VINGI.

Katika biblia tunaona mtu aliyefundishwa Vizuri ni Bwana YESU na kuelewa ni Paulo… Yeye alifundishwa jinsi ya kuishi vipindi vyote vya (njaa na kutokuwa na njaa, vya kupungukiwa na kuongezekewa).

Wafilipi 4:12 “Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

13  Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”

2. KUJIFUNZA.

Hii ni sifa ya pili ya Mwanafunzi yoyote, ni lazima awe anajifunza. Na kwa upande wa Imani ni lazima kujifunza kama mwanafunzi wa Kristo…

Na tukitaka tuweze kujifunza biblia na kuielewa  vizuri ni lazima tujikane Nafsi na kubeba misalaba yetu na kumfuata Bwana YESU. (hakuna njia nyingine tofauti na hiyo).

Si ajabu leo hii inakuwa ngumu sana kuweza kuielewa biblia, pindi tuisomapo…sababu pekee ni kutojikana nafsi na kubeba msalaba na kumfuata Bwana YESU, tunapenda ule ukristo laini laini, ambao hauna matokeo yoyote kiroho.

   3. KUFANYA MITIHANI.

Hii ni sifa ya tatu ya mwanafunzi yoyote anayesoma, ni lazima awe na vipindi vya kujaribiwa kwa mitihani.

Vivyo hivyo ili tuwe wanafunzi wa YESU wa Bwana ni lazima tupitishwe katika vipindi vya kujaribiwa na Bwana YESU mwenyewe….. Na lengo la mitihani hiyo (au majaribu hayo) ni kumwimarisha mtu huyo kiimani.

Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;

3  mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi”.

Na madhara ya kukosa kujaribiwa kwa mitihani ya BWANA YESU ni kushindwa kuhitimu na hatimaye kukosa cheti.

    4. KUHITIMU.

Mwanafunzi anayehitimu ni yule aliyemaliza mitihani yote na kufaulu, (huwa anapewa cheti) kile cheti ni kibali maalumu, na fursa  pamoja na heshima ya daima kwa mwanafunzi yule.

Vile vile na mtu aliye mwanafunzi wa BWANA YESU, akiisha kumaliza majaribu yote na kuyashinda, atahitimu kwa kupewa cheti ambacho ni TAJI YA UZIMA..

Yakobo 1:12 “ Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao”.

Jiulize je wewe ni Mwanafunzi wa BWANA YESU au ni mfuasi tu?…. Waliokuwa wanamfuatilia Bwana YESU ni wengi lakini waliomfuata na kuwa wanafunzi wake walikuwa wachache sana.. Wengine wote walikuwa ni washabiki tu aidha wa miujiza au wa siasa, lakini waliojiunga na chuo cha Bwana YESU walikuwa ni wachache sana.

Na kanuni ya kujiunga na chuo hicho cha Bwana YESU na kuwa mwanafunzi wake si nyingine Zaidi ya hiyo ya “KUJIKANA NAFSI NA KUBEBA MSALABA”.

Luka 14:27 “Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU”.

Na kumbuka hakuna tafsiri nyingine ya UKRISTO au kuwa MKRISTO Zaidi ya UANAFUNZI..

Matendo 11:26  “….Na WANAFUNZI waliitwa WAKRISTO kwanza hapo Antiokia”.

Hivyo ukitaka kujijua kama wewe ni Mkristo au la!.. sipime tu kama umeshakuwa Mwanafunzi wake, kama huna sifa hizo hapo juu za uanafunzi bado hujawa MKRISTO.

Bwana YESU atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA KUWA MKRISTO?

Bwana alimaanisha nini kusema “Mwanafunzi hawi mkuu kuliko mwalimu wake”?

Mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake hawezi kuwa mwanafunzi wangu?

NITAJUAJE KUWA NIMEITWA ILI KUMTUMIKIA MUNGU?

TOA HUDUMA ILIYO BORA.

Rudi Nyumbani

Print this post

JIFUNZE JAMBO KWENYE UKOO WA YESU, UWE NA AMANI

Leo hii kumekuwa na hofu nyingi katikati ya watu, juu ya historia na machimbuko ya familia zao.  Wengine wameona maisha yao au tabia zao za sasa zimeathiriwa na chimbuko la familia zao, au koo zao, au mababu yao. Na hivyo hawajui wafanyeje.

Lakini ukweli ni kwamba hakuna hata mmoja wetu ambaye, chimbuko lake halijaathiriwa, Tukianzia na la Bwana wetu Yesu Kristo, na ndio maana biblia imeandikwa tukapewa, ili kutuonyesha sisi njia, ya kusimama na shindana na nguvu za Yule mwovu kwa ujasiri wote bila woga.

Kitabu cha Mathayo, kinaanza na kueleza ukoo wa Yesu. Kulikuwa na sababu ya kutangulizwa historia ya ukoo wake, ili Mungu kutufundisha sisi jambo. Watu wengi wakiangalia ule mtiririko, wanadhani Mungu anatuonyesha jinsi Yesu alivyotokea katika ukoo hodari, mashuhuri. Lakini Hapana. Ukweli ni kwamba hakukuwa na umuhimu wowote, kwa wengi walioorodheshwa katika ukoo wake.

Lakini nataka tuone, jinsi ukoo ule ulivyovurugwa, kiasi kwamba kama Mungu angetazama usafi basi, usingestahili hata kidogo kumleta mkombozi duniani. Katika ukoo wake hakukuwa tu na wema, lakini kulikuwa na  “makahaba” kulikuwa na pia “wazinzi-waliokubuhi”, kulikuwa na “makafiri” . Kwamfano Yule Rahabu, alikuwa ni kahaba, tena kahaba kweli kweli. Tena Kulikuwa na Ruthu, mwanamke wa kimataifa, ambaye Mungu aliwakataza kwa nguvu sana, wayahudi wasitwae wanawake wa kimataifa kuwaoa, mbegu takatifu zisichangamane na mbegu nyingine (Ezra 9:2) ni unajisi, lakini hapa ikawa tofauti, mwanamke wa kimataifa akaingizwe kwenye ukoo. kama huyo haitoshi alikuwepo mzinzi  Tamari, ambaye, yeye alifanya hila akalala na mkwe wake, kumzaa Peresi,..Jambo lisilofikirika kiakili, vilevile, alikuwepo Bersheba  mke wa wizi, wa Mfalme Daudi, ambaye miongoni mwa wake halali wa Daudi hakuwepo, lakini alichaguliwa yeye, kuupitisha uzao wa Kristo, na wale wasafi wakaachwa.

Tusome..

Mathayo 1:1  Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.

2  Ibrahimu alimzaa Isaka; Isaka akamzaa Yakobo; Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake;

3  Yuda akamzaa Peresi na Zera KWA TAMARI; Peresi akamzaa Esromu; Esromu akamzaa Aramu;

4  Aramu akamzaa Aminadabu; Aminadabu akamzaa Nashoni; Nashoni akamzaa Salmoni;

5  Salmoni akamzaa Boazi KWA RAHABU; Boazi akamzaa Obedi KWA RUTHU; Obedi akamzaa Yese;

6  Yese akamzaa mfalme Daudi. Daudi akamzaa Sulemani KWA YULE MKE WA URIA ;

7  Sulemani akamzaa Rehoboamu; Rehoboamu akamzaa Abiya; Abiya akamzaa Asa;

8  Asa akamzaa Yehoshafati; Yehoshafati akamzaa Yoramu; Yoramu akamzaa Uzia;

9  Uzia akamzaa Yothamu; Yothamu akamzaa Ahazi; Ahazi akamzaa Hezekia;

10  Hezekia akamzaa Manase; Manase akamzaa Amoni; Amoni akamzaa Yosia;

11  Yosia akamzaa Yekonia na ndugu zake, wakati wa ule uhamisho wa Babeli.

12  Na baada ya ule uhamisho wa Babeli, Yekonia akamzaa Shealtieli; Shealtieli akamzaa Zerubabeli;

13  Zerubabeli akamzaa Abihudi; Abihudi akamzaa Eliakimu; Eliakimu akamzaa Azori;

14  Azori akamzaa Sadoki; Sadoki akamzaa Akimu; Akimu akamzaa Eliudi;

15  Eliudi akamzaa Eleazari; Eleazari akamzaa Matani; Matani akamzaa Yakobo;

16  Yakobo akamzaa Yusufu mumewe Mariamu aliyemzaa YESU aitwaye Kristo.

17  Basi vizazi vyote tangu Ibrahimu hata Daudi ni vizazi kumi na vinne; na tangu Daudi hata ule uhamisho wa Babeli ni vizazi kumi na vinne; na tangu ule uhamisho wa Babeli hata Kristo ni vizazi kumi na vine.

Hivyo ukoo wa Bwana wetu Yesu Kristo, ulivurugwa-vurugwa, tunaweza kusema haukuwa msafi,  kulinganisha na koo za wayahudi wengine. Lakini huyo ndiye aliyekuja kumpendeza Mungu kuliko wote, ijapokuwa alitokea katika chimbuko lililokorongoka, huyo ndiye aliyekuja kuwa mkombozi, huyo ndiye aliyekuja kuwafungua watu na kukata mizizi yote ya laana, na kuwa Baraka kwa ulimwengu.

Ni kutufundisha nini?

Usiogope, yawezekana kweli, chimbuko lenu ni bovu, ni makahaba tu, ni walevi tu, mna magonjwa ya kurithi yanatembea, mnaudhaifu Fulani, maskini wa kupindukia, hamuoelewi, hamzai. Nataka nikuambie wacha kuhangaika kuufikiria ukoo wako. Kwasababu hata iweje hakuna aliyewahi kutokea mwenye chimbuko safi hapa duniani. Wewe mtazame  Kristo tu, aliyemaliza yote pale msalabani. Amini tu kazi yake aliyoimaliza kwako.

Unapookoka, huna laana yoyote ndani yako, haijalishi ukoo mzima walizindika, haijalishi mna mizimu na mikoba ndani.. Hiyo ndio bye! Bye!, imeisha!. Haina nguvu ndani yako, wala usiipe kibali, mwamini Yesu aliyekukomboa.

Usiwe mtu wa kuzunguka huku na huko kuvunja laana za ukoo, utavunja ngapi? Ni mababu wangapi wamepita huko nyuma, itakupasa basi urudi sasa mpaka Adamu. Uvunje laana zote. Hivyo kua kiroho, mwamini Yesu aliyekukomboa. Matatizo ya kifamilia mliyonayo, wanayo hata wale watumishi wa Mungu, isipokuwa kwa namna tu nyingine. Lakini wao wamemwamini Kristo aliyewakomboa, ndio maana hawana laana yoyote. Lakini kaulizie huko kwao kukoje watakuambia. Ndugu ukiokoka, Ya kale yamepita tazama, yamekuwa mpya. Unachopaswa kufanya baada ya kuokoka tu , ni kuendelea kumjua zaidi Kristo ili uwe na amani,sio kuchimbua tena ya kale, jifunze kwa ukoo wa Yesu .

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini  vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

UMUHIMU WA KUISHI MAISHA YAMPENDEZAYO MUNGU SASA.

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini biblia ni neno la Mungu?

Swali: Je ni kweli biblia ni Neno la Mungu?


Kabla ya kujibu kwanini biblia ni Neno la Mungu, na si kitabu kingine chochote?… hebu tujiulize kwanza na tujadili kwanini

Biblia ni Neno la Mungu kwasababu lina maneno yaliyo hai..

Vivyo hivyo biblia ni kitabu cha Mungu, kwasababu kimebeba taarifa sahihi kumhusu Mungu.. Na taarifa KUU ndani ya kitabu hiko kitukufu, ni taarifa ya mwanadamu kuondolewa dhambi kupitia YESU KRISTO (Hiyo ndiyo taarifa kuu) ambayo inaleta “UZIMA WA MILELE KWA MTU”..Na ndio karama kuu ya MUNGU kwetu.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Vitabu vingine vyote vilivyosalia havijabeba suluhisho lolote la ondoleo la dhambi za Mtu, badala yake zimebeba tu taarifa za maadili, au staha, mambo ambayo yanapatikana hata katika vitabu vya sheria za nchi.

Lakini taarifa na njia ya ondoleo la dhambi zipo katika BIBLIA TU PEKE YAKE!!!..

Kwasababu “dhambi” ndio sumu pekee ya mwanadamu, na hiyo ndio kizuizi kikubwa cha mtu kumkaribia Mungu, hivyo mtu akiondolewa hiyo anakuwa ameokoka! Hata kama maisha yake hapa duniani bado yanaendelea.

Na ni kwa njia gani mtu anaondolewa dhambi zake moja kwa moja??

Matendo 2:36 “ Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU”.

Kanuni ya kuondolewa dhambi, ni kutubu na kubatizwa (Marko 16:16). Na toba halisi ni ile inayotoka moyoni yenye madhamirio ya kugeuza mwelekeo moja kwa moja. Na ubatizo sahihi ni ule wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la BWANA YESU (Matendo 8:16, na Matendo 19:5).

BWANA YESU AKUBARIKI.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JIPE NAFASI KATI YA TAARIFA UNAYOIPOKEA NA MAAMUZI UNAYOYATOA.

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

UPEPO WA KUSI HULETA MVUA;

NENO LA MUNGU KATIKA UTIMILIFU WOTE.

UWEZA WA MUNGU NJE YA WAKATI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)

Jibu: Turejee…

Waamuzi 1:16 “Hao wana wa Mkeni, HUYO SHEMEJI YAKE MUSA, wakakwea juu kutoka katika huo mji wa mitende, pamoja na wana wa Yuda, na kuingia hiyo nyika ya Yuda, iliyo upande wa kusini wa Aradi; nao wakaenda na kukaa pamoja na watu hao”.

Wakeni walikuwa ni jamii ya watu waliokuwa wanaishi katika nchi ya “Midiani” (karibu na jangwa la Sinai).. Kwa urefu kuhusiana na waMidiani fungua hapa >>Midiani ni nchi gani kwasasa?.

Miongoni mwa hawa waMidiani ndiko alikotokea Babamkwe wake Musa aliyeitwa Yethro au jina lingine Rueli.. Huyu Yethro/Reueli ndiye aliyemzaa  Sipora aliyekuwa mkewe Musa.

Na huyu Yethro alikuwa na watoto wengine wa kiume mbali na wale mabinti wake saba tunaowasoma katika Kutoka 2:16, na mmoja wa mtoto wake wa kiume aliitwa “Hobabu” ambaye sasa “ndiye shemeji yake Musa (maana yake kaka yake Sipora, mke wa Musa)”.

Huyu Hobabu shemeji yake Musa alikataa kusafiri na wana wa Israeli, kwani wana wa Israeli walimtumaini yeye awatangulie njia kwani aliifahamu Zaidi, lakini alikataa kama maandiko yanavyosema..

Lakini maandiko mbeleni yanaonyesha alikubali, kwani uzao wake ulionekana ndani ya nchi ya Ahadi

Hesabu 10: 28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.

31 Naye akamwambia, Usituache, tafadhali; kwa kuwa wewe wajua jinsi tutakavyopanga nyikani, nawe utakuwa kwetu badala ya macho.

32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo

34 Na wingu la Bwana lilikuwa juu yao mchana hapo waliposafiri kwenda mbele kutoka kambini.

35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.

Kwa funzo refu kuhusiana na habari hii ya Hobabu na Musa fungua hapa >>>>Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?

Kwahiyo huyu Hobabu ndiye aliyekuwa shemeji yake Musa na wanawe (yaani watoto wake) ndio hao wanaotajwa hapo katika Waamuzi 1:6 na Waamuzi 4:11 na pia wanatajwa katika sehemu mbali mbali za biblia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kuiaua Nchi ni kufanya nini? (Waamuzi 18:2).

BWANA NITIE NGUVU TENA. (Waamuzi 16:28)

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU

MWANAMKE, BINTI, MAMA.( Sehemu ya 1)

Dina akatoka kuwaona binti za nchi. (Mwanzo 34:1)

Rudi Nyumbani

Print this post

Kwanini Musa amtake Hobabu na tayari kulikuwa na Wingu linalowaongoza?

Swali: Kwanini Nabii Musa amtake Hobabu (shemeji yake) kama dira yake ya kuelekea Kaanani na tayari Mungu alishawafunulia juu yao nguzo ya wingu wakati wa mchana na Nguzo ya moto wakati wa usiku kama dira yao na kama kitu cha kuwaongozea?


Jibu: Lipo jambo kubwa sana hapa la kujifunza..

Awali ya yote kama bado hujamfahamu Hobabu ni nani na inakuwaje awe shemeji yake Musa fungua hapa >>>Huyu Mkeni shemeji yake Musa alikuwa ni mtu wa namna gani? (Waamuzi 1:16)

Sasa kwa muhtasari ni kwamba kipindi wana wana wa Israeli wanatoka Misri kuelekea Kaanani, ni kweli Bwana aliwapa wingu na nguzo ya moto iwaongoze mchana na usiku.

Lakini Zaidi ya hayo Musa alitafuta tena mtu ambaye atamwongoza njia yao kuelekea nchi ya ahadi.. sasa swali ni alifanya makosa?… na tena akataka kumfanya kama “Macho” katika safari hiyo..

Waamuzi 10:28 “Ndivyo zilivyokuwa safari zao wana wa Israeli kwa majeshi: yao; nao wakasafiri kwenda mbele.

29 Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

30 Naye akamwambia, Siendi mimi; ila nitairudia nchi yangu mwenyewe, na kwa jamaa zangu mwenyewe.

31 NAYE AKAMWAMBIA, USITUACHE, TAFADHALI; KWA KUWA WEWE WAJUA JINSI TUTAKAVYOPANGA NYIKANI, NAWE UTAKUWA KWETU BADALA YA MACHO.

32 Itakuwa, ukienda pamoja nasi, naam, itakuwa mema yo yote Bwana atakayotutendea sisi, tutakutendea wewe vivyo

34 NA WINGU LA BWANA LILIKUWA JUU YAO MCHANA HAPO WALIPOSAFIRI KWENDA MBELE KUTOKA KAMBINI.

35 Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee Bwana, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao”.

Jibu ni La!.. Musa hakuwa Mjinga, wala hakuwa mtu wa kumtegemea Mwanadamu.. Daima alijua Mungu ndiye Ngao yake na watu wake, na wala hakuna mtu yeyote awezaye kumsaidia kazi.  Lakini Nabii Musa alifikiri Zaidi, Alijua watu aliona ni  watu wenye mioyo migumu, na shingo ngumu.

Alijua Imani yao kwa Mungu ilikuwa ni ndogo, na wengi wao ni watu wa mwilini, na alijua wasipopata mtu wa kuwapanga vyema kule nyikani, aliyemzoefu wa jangwa na njia, zitanyanyuka shida nyingi na hatimaye watamkufuru Mungu na kuadhibiwa wote.

Hivyo kwa faida ya watu wasiangamia aliwatafutia mwalimu wa mwilini ili awaongoze, na kuwafundisha jinsi ya kukaa jangwani, na hiyo ikawa dawa kwa sehemu kubwa sana.

Na utaona hii familia ya Yethro (babamkwe wake Musa na mashemeji zake), ilikuwa msaada mkubwa sana kiushauri katika safari ya wana wa Israeli jangwani na kwa Musa kwa ujumla. Kwani kipindi ambacho Musa alikuwa anawaamua watu wote peke yake kuanzia asubuhi mpaka jioni, alipokuja huyu babamkwe wake alimpa ushauri bora sana wa kuweka wakuu wa maelfu, wakuu wa mahamsini na wakuu wa mamia na wakuu wa makumi (Soma Kutoka 18:12-27).

NINI TUNAJIFUNZA KWA MUSA:

Musa alikuwa na “Macho juu” ambaye ni Roho Mtakatifu juu (kama wingu likimwongoza na watu wake) lakini pia alikuwa na “macho chini” (Hobabu, shemeji yake) kwaajili ya watu wake. Mambo haya yanaenda pamoja..

Wewe kwama Mzazi, unaye Roho Mtakatifu anayekuongoza wewe na familia yako kama Macho ya Juu, lakini hayo hayatoshi pekee, ni lazima watoto wako uwapatie waalimu watakaowafundisha njia za Roho Mtakatifu katika mashule yao waliopo, katika makanisa yao, katika shughuli zao n.k

Ukisema utawaacha na kuongozwa na Roho Mtakatifu kama wewe uongozwavyo, utawapoteza…wawekee waalimu.

Vilevile Mtumishi wa Mungu weka waalimu kwa watoto wako wa kiroho, weka wachungaji watakaowaangalia, itakuwa afya na heri kwao.

Bwana atusaidie

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU

NI VIZURI SISI KUWAPO HAPA.

Je Musa kumwoa Sipora, Mkushi alifanya dhambi?

Kiti cha Musa ni kipi? (Mathayo 23:2)

Rudi Nyumbani

Print this post

AINA SABA (7), ZA SIFA KIBIBLIA.

Katika biblia zipo aina mbalimbali za kumsifu Bwana, lakini kuna kuu saba ambazo zilitambuliwa na wayahudi kwa wakati wote. Hivyo ni vema kuzifahamu ili wigo wako uwe mpana zaidi katika eneo hili la sifa. Kwasababu ndio huduma kuu tuliyonayo duniani kwa Mungu wetu. Kumbuka chakula chetu ni Neno, lakini chakula cha Mungu wetu ni Sifa zetu. Hivyo ni lazima tujue tunamsifuje yeye kiufasaha kwa jinsi apendavyo.

Hizi ni aina saba za sifa.

1.) Kucheza: Kwa kiyahudi huitwa ‘Hallal’

Hii ni aina ya kumsifu Mungu ambayo, mwimbaji hujidai, hujigamba mbele za Mungu wake kwa kuuhusisha mwili wake, yaweza kuwa kuruka kuruka, au kucheza.

Agizo hilo lipo katika Zaburi 149:3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa matari na kinubi wamwimbie.

Ndio lile Daudi na Israeli wote walilolifanya walipokuwa wanalileta sanduku la Bwana Yerusalemu,

 2Samweli 6:14 Daudi akacheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote; na Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.

15 Basi Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalileta sanduku la Bwana kwa shangwe, na kwa sauti ya tarumbeta.

16 Ikawa, sanduku la Bwana lilipoingia mji wa Daudi Mikali, binti Sauli, akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi akiruka-ruka na kucheza mbele za Bwana; akamdharau moyoni mwake.

Hivyo na wewe kama mtu uliyeokolewa na Kristo, kujidai kwa ujasiri wote mbele ya Mungu wako usijizuie, angalizo tu ni kwamba usifanye kidunia, kana kwamba unacheza dansi, huku moyoni mwako hakuna ibada. Hiyo sio sawa, lakini kumwimbia Mungu kwa kucheza hakuna kosa lolote ikiwa ni jambo la kububujika  moja kwa moja kutoka moyoni mwako.

2) Kuinua mikono: Kwa kiyahudi huitwa ‘Yadah’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kuinua mikono juu, Kama ishara ya kutambua tegemeo lako kwako, kama mtoto mdogo kwa mzazi wako anapomlilia. Na kuonyesha upendo wako wa dhati kwa Mungu wako.

Zaburi 63: 3 Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.  4 Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai; Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.

Kama mtakatifu jizoeze mara nyingi, kunyanyua mikono yako juu wakati unamwabudu Mungu, au wakati mwingine unapoomba. Binafsi, nimeona tofauti kubwa sana, niinuapo mikono yangu, pindi niombapo au nisifupo, najikuta nazama rohoni kwa haraka sana, zaidi ya napoweka mikono yangu chini. Kumbuka ile habari ya Musa, alipoinua mikono juu, Israeli ilishinda, lakini alipoweka mikono chini, Waamaleki walishinda. (Kutoka 17:11) Hivyo jifunze sana, kuiinua mikono yako juu, katika ibada zako.

3) Kuinama, kujusudu, kupiga magoti: Kwa kiyahudi huitwa ‘Barak’.

Hii ni aina ya kumsifu Mungu kwa kumbariki Mungu, lakini kwa kuonyesha heshima kubwa kama mfalme, kujishusha chini, kusujudu au kupiga magoti, kuonyesha yeye ni mkuu sana wa kuogofya zaidi ya wafalme wote na wakuu wote ulimwenguni.

Zaburi 5:7 Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.

Kama mwamini, sifa zako zisiwe za mdomo tu wakati wote, jifunze kupiga magoti, au kusujudu ni ishara ya unyenyekevu  wa hali ya juu. Fanya hivyo nyakati za sifa, nyakati za maombi.

4) Kusifu kusiko na maandalizi: Kwa kiyahudi huitwa Tehillah:

Aina ya kusifu moyoni mwako, kwa namna isiyo na maandalizi Fulani maalumu, mfano wa kwaya, ni nyimbo ambazo zitainuka  katikati ya mapito yako fulani, wakati mwingine unapopitia kutendewa mema mengi na Mungu, na hapo ghafla tu moyoni mwako unasikia kumsifu Mungu, kumpa utukufu.

Kwamfano Daudi alipokuwa anapitia magumu,au anashindaniwa na Mungu, akimtafakari Mungu, mara anaachilia kinywa chake, Mungu anaanza kububujisha nyimbo mpya ulimini mwake.

Mfano mwingine wa sifa kama hizi, ni pale Mungu alipowavusha wana wa Israeli, bahari ya Shamu, na kuona maadui zao wamefunikwa na habari, ndipo Israeli wote, pamoja na Miriamu na wanawake wakasimama kumwimbia Mungu nyimbo za Furaha (Kutoka 15).

Mfano mwingine ni pale Mariamu alipomtembelea Elizabeti, na kutolewa unabii kuwa atamzaa Masihi, alishangalia na ghafla  akafungua  kinywa chake kwa wimbo, kumsifu Mungu kwa namna hii,  (Luka 1:46-56)

Hivyo kila mkristo, katika majira yote, vipindi vyote, viwe vyepesi, viwe vingine, hana budi kutafakari na kufungua kinywa chake kumsifu Mungu kwa aina hii ya sifa ya Tehillah. Ni muhimu sana, na inampendeza, Mungu, hii haina maandalizi, haina mpangilio maalumu, hutoka moyoni mwako, kwasababu Fulani Mungu alizokuonekania.

5) Kusifu kwa vyombo vya muziki: Kwa kiyahudi huitwa “Zamar”.

Mungu aliwaagiza pia watu wake, wamwimbie si kwa vinywa vyao tu na makofi, lakini pia pamoja na kuchanganya zana mbalimbali za muziki.

Zaburi 150:3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;  5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.

Ni wazi kuwa kuchanganya ala mbalimbali,kama vile gitaa, vinanda, filipi, tarumbeta, ngoma, zeze, marumba, n.k. Katika kumwimbia Mungu, huongeza ladha na hisia njema katika kumsifu, na hivyo hupendeza sana machoni pake. Wapo watu hawaamini katika matumizi ya vyombo. Lakini maandiko yanatuagiza tumsifu Mungu kwa hivyo.

6) Kusifu kwa kupaza sauti kuu: Kwa kiyahudi huitwa “Shabach”.

Aina hii ya sifa, ni kwa kupaza sauti yako juu sana kwa Mungu. Hii Huonyesha ujasiri wa Mungu unayemwabudu, na kuutangazia umati na ulimwengu kuwa yupo Mungu mahali hapo anayeabudiwa.

Zaburi 47:1 Enyi watu wote, pigeni makofi, Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

Sifa hizi zina nguvu sana, ndio zile ambazo ziliangusha kuta za Yeriko. Wana wa Israeli walipoambiwa wapaze sauti zao kwa Mungu. Zile sauti hayakuwa makelele tu, bali zilikuwa ni sauti za kumtukuza Mungu.(Yoshua 6:20).

Tumwimbiapo Mungu, hatupaswi tuwe kama mabubu, au tuimbe kinyonge, au kwa kutegea-tegea. Mungu anajivunia sana watu wale wanaomwabudu kwa ujasiri, kwa kufumbua vinywa vyao na kupaza sauti zao kwa nguvu  kumwadhimisha yeye.

7) Kusifu kwa ukiri, shukrani, kutoa: Kwa kiyahudi huitwa “Todah”.

Ni aina ya sifa inayofanana na ile ‘Yadah’,ya  kumwinulia Mungu mikono kumwimbia. Isipokuwa hii, ni kumwadhimisha Mungu, kwa matendo ambayo bado hujayaona kwa macho. Kutambua uweza wa Mungu, hata kama huoni matokeo yoyote, na kumshukuru katika hayo. Hata pale ambapo hujisikii.  .

Mfano ya sifa hizi, ni labda wewe ni mgonjwa, daktari amekuambia una siku chache za kuishi, ukiangalia umeombewa mara nyingi hakuna matokeo yoyote, lakini unakumbuka Neno la Bwana linalosema ‘kwa kupigwa kwake sisi tumepona’. Unaanza kufurahi, ukimwinulia mikono Mungu na kumshukuru ukisema asante, Bwana kwa kuniponya, huku ukimsifu katika hali yako hiyo hiyo ya udhaifu.

Sifa hizo ni muhimu sana kwetu, na zinaugusa moyo wa Mungu kwa namna ya kipekee, Kwasababu kamwe haziwezi kuwa na unafiki ndani yake.

Hizi zinapaswa ziwepo ndani yetu wakati wote. Unakumbuka ahadi za Mungu ambazo bado huoni zimetimia, unamsifu Mungu sana kwa furaha kana kwamba umekwisha vipata vyote sasa, umetafuta kazi umekosa, unamsifu Mungu kana kwamba umepokea ripoti ya kuajiriwa.

Hizi ndio aina saba za sifa, ambazo ukiziachilia katika maeneo yako yote ya kiibada. Utampendeza Mungu sana. Lakini pia zinapaswa ziwe katika Roho na Kweli, tafsiri yake, ni sharti mtu umsifuye Mungu uwe umeokoka, umeshatambua kazi ya Kristo ya ukombozi kwenye maisha yako ipoje. Tayari wewe ni  mfuasi wa Kristo. Ndipo sifa hizo zitakubalika. Vinginevyo haziwezi kumpendeza Mungu hata kama utazifanya zote kwa ufasaha.

Ikiwa bado hujaokoka, na upo tayari kufanya hivyo leo. Basi kwa msaada unaweza fungua hapa kwa msaada wa mwongozo huo wa kumkaribisha Yesu maishani mwako.>>>>  KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

SAFINA NI NINI?

Je kumwimbia Mungu kwa kucheza ni sahihi kibiblia?

(Opens in a new browser tab)

Rudi Nyumbani

Print this post

ZIDI KUTAFUTA UTAKASO WA MWILI.

Shalom.

Usiishie kutafuta tu utakaso wa roho, bali tafuta pia UTAKASO WA MWILI, kwamaana vitu hivi viwili vinaenda sambamba, kwasababu vitu hivi vikichafuka vinaiharibu pia nafsi ya mtu.

2Wakorintho 7:1“Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na UCHAFU WOTE WA MWILI NA ROHO, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Upo usemi kuwa Mungu wetu hatazami sana Mwili, lakini anatazama Zaidi Roho ya Mtu. (Hatuna budi kuwa makini na kauli hii!!)

Kutokana na kwamba asilimia kubwa ya maombi yetu yanalenga MAHITAJI YA MWILINI, basi ni wazi kuwa Mungu anaitazama pia miili yetu. Kwasababu kama mtu atamwomba Mungu Baba ampe fedha, au chakula, au makazi hayo yote si kwasababu ya “roho” kwasababu roho haili chakula, wala haivai nguo, wala haiishi kwa fedha.. bali mwili ndio unaohitaji hayo yote.

Sasa kama tutamlazimisha Mungu Baba aangalie miili yetu kwa mahitaji yetu, halafu wakati huo huo tunasema Mungu haangalii mwili, tutakuwa WANAFIKI!!.

Sasa ikiwa asilimia Zaidi ya asilimia 90 ya mahitaji yetu, yanalenga MIILI YETU, Basi ni wazi kuwa Mungu anaangalia Miili yetu na anajishughulisha nayo sana….

Ni lazima kulijua hili ili tusipotee na elimu ya uongo ya shetani,.. Ni lazima pia tujishughulishe kutafakari namna ya kuyafanya mapenzi ya Mungu katika miili yetu kama tu vile tunavyojishughulisha katika kumwomba mahitaji ya mwili..

1Wathesalonike 5:23 “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; NANYI NAFSI ZENU NA ROHO ZENU NA MIILI YENU mhifadhiwe MWE KAMILI, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo”.

Katika mstari huo biblia imetaja mambo yote matatu; Nafsi, mwili na roho. (yanapaswa yawe makamilifu, bila lawama mpaka wakati wa kuja kwake Bwana YESU).

Hivyo zingatia yafuatayo:

  1. NI NINI UNAFANYA KUPITIA MWILI WAKO.

Jipime ni nini unakifanya katika mwili,.. je shughuli au matendo unayoyafanya kupitia mwili wako ni kulingana na mapenzi ya Mungu??.. Kama unafanya kazi haramu (mfano ukahaba, au kazi ya kuuza vitu haramu kama pombe, sigara, na mengineyo), basi kazi hiyo unaifanya kupitia mwili wako hivyo ibadili ili isikupeleke jehanamu ya moto.

Kama matendo unayoyafanya katika mwili ni  haramu mfano uzinzi (1Wakorintho 6:18), wizi, au mauaji n.k geuka leo yasije yakawa sababu ya kukupeleka hukumuni.

   2. NINI UNAKIAMBATANISHA NA MWILI WAKO

Angalia ni nini unakiambatanisha/unakishikamanisha na mwili wako.. Hapa nazungumzia aina ya mavazi na urembo na michoro (tattoo). Je mavazi uvaayo ni sawasawa na Neno la Mungu?.. Je yanaipasa jinsia yako sawasawa na Kumbukumbu 22:5.

Je mavazi unayovaa ni ya kujisitiri?, kuzuia tamaa kwa upande mwingine na kutunza heshima yako? (1Timotheo 2:9 na Mathayo 5:28)

Je michoro uichorayo na rangi yako ya asili uiondoayo ni mapenzi ya Mungu? (Walawi 19:28)

Angalia ni nini kinanin’ginia mwilini mwako.. Je hizo cheni, hereni, mikufu, bangili, vikuku n.k ni mapenzi ya Mungu?? Je si ishara ya utumwa?? (hebu soma Kutoka 21:5-6 na Kumbukumbu 15:16-17).

   3. NI NINI KINAINGIA MWILINI MWAKO.

Angalia ni kitu gani unakiingiza mwilini mwako.. Je Mungu amekusudia moshi uingia katika mapafu yako ambayo yanapaswa yavute hewa safi ili kutimiza miaka uliyopewa yakuishi duniani?..

Je Mungu amekusudia uingize vilevi na madawa ya kulevya ndani ya mwili wako na kukutoa ufahamu wako kwa muda?.. Jiulize kama si ruhusu kuendesha chombo chochote cha moto ukiwa umelewa/umekunywa pombe.. vipi kuuendesha huo mwili ukiwa umelewa??.. Huoni kama huo ni uvunjaji wa sheria kubwa Zaidi, kwasababu mwili ni bora kuliko gari au chombo kingine chochote cha usafiri.

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UTAKASO NI SEHEMU YA MAISHA YA MKRISTO YA KILA SIKU.

KIJITO CHA UTAKASO.

Nini Maana ya Adamu?

WEWE SI MALI YAKO MWENYEWE!

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

Rudi Nyumbani

Print this post

TUNZA MAVAZI YAKO NA FUA NGUO ZAKO!

Vazi/Nguo kiroho linawakilisha “matendo ya mtu”, maana yake kiroho mtu mwenye mavazi masafi, maana yake matendo yake ni masafi, na kinyume chake mwenye mavazi machafu maana yake matendo yake si safi (Ufunuo 19:18).

Sasa Matendo yanatunzwa, lakini pia yanafuliwa (safishwa).. kama vile nguo inavyoweza kutunzwa lakini pia kufuliwa.

     1. TUNZA MAVAZI YAKO.

Maana ya kutunza mavazi ni kuhakikisha hayaharibiki wala kuwa na kasoro yawapo mwilini. Vazi lililotoboka au kuchanika maana yake limekosa matunzo mwisho wa siku yule mtu atabaki Tupu.

Vivyo hivyo ni wajibu wetu kuyatunza Matendo yetu mema, yasiharibike.. Kwa kujiangalia mazingira tuliyopo na mambo tuyafanyayo…

Ufunuo 16:15” (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, NA KUYATUNZA MAVAZI YAKE, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake)”.

Vitu vinavyoharibu matendo yetu mazuri/tabia nzuri ni pamoja kampani tulizonazo na mazungumzo tuzungumzayo..

1Wakorintho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema”.

Chunguza makundi uliyonayo na aina ya mazungumzo unayozungumza.

      2. FUA NGUO ZAKO.

Nguo isiyofuliwa inapoteza umaridadi na unadhifu kwa mtu, hata kama haijaharibika au kuchanika. Vile vile Matendo yasiyofuliwa yanapoteza unadhifu wa mtu kiroho.

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13  Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14  HERI WAZIFUAO NGUO ZAO, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Sasa mtu anafuaje Matendo yake?… Si kwa njia nyingine Zaidi ya kuomba na kusoma Neno.

Na Utajuaje matendo yako yameanza kuingia dosari?.. si kwa kusubiri uambiwe na mtu au watu, bali kwa kusoma Neno (biblia). Unaposoma Neno ndipo utakapojijua kama una kasoro au la!, kwasababu Neno la Mungu ni kioo.. Ili ujijue kama una uchafu mwilini, si kusubiri uambiwe, kwasababu si wote wenye ujasiri wa kukwambia kasoro zako.

Kitu pekee kitakachoweza kuutambulisha uchafu usoni mwako ni KIOO

na ni lazima usomaji wa Neno uambatane na maombi.

Hivyo Maombi ni “Maji” na Neno la Mungu ni “sabuni” kwa mambo hayo, matendo yetu yatakuwa safi daima.

Bwana atuongezee Neema yake.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?

MAVAZI YAPASAYO.

NINI TOFAUTI KATI YA MATENDO YA SHERIA NA MATENDO YA IMANI?

JE! UNA MHESHIMU MUNGU?

Rudi Nyumbani

Print this post

JITAHIDI KUJA KABLA YA WAKATI WA BARIDI.

2Timotheo 4:21  “Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia”

Mtume Paulo ni mtu aliyetambua kuwa kustawi kwa huduma yake kunategemea sana sapoti ya watendazi wenzake wengine wenye ni moja na yeye. Hivyo tunasoma wakati akiwa Rumi kama mfungwa, alimwandikia waraka mwanawe Timotheo, aiharakishe huduma yake, ili amfuate kule Rumi wasaidiane katika huduma kabla ya wakati wa bariki kuanza.

“Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi”.

Paulo alijua mazingira yanaweza kukawiisha kusudi la Mungu. Hivyo alitambua kuwa mtu akiongeza jitihada anaweza kukamilisha mambo yake mapema kabla mazingira Fulani hayajamuathiri kutenda kusudi lingine la Mungu.

Kwa ukanda waliokuwa, ilikuwa ni ngumu sana, meli kusafiri nyakati za baridi kwasababu ya barafu baharini, hivyo safari zote za majini zilisitishwa kwa miezi kadhaa mpaka baridi itakapoisha ndipo safari zianze tena, Paulo aliliona hilo akatambua ni jambo la asili haliwezi kuepukika kwa kufunga na kuomba, isipokuwa kwa kupangilia tu ratiba vizuri.

Hii ni kutufundisha sisi, tufahamu kuwa mazingira Fulani, au nyakati Fulani zisizo rafiki sana huwa zinapita, au zitakuja mbele yetu ambazo zinaweza zikawa ni kikwazo cha utumishi kwa sehemu Fulani.

Kwamfano wakati wa baridi kwako, unaweza kuwa ni wakati wa ndoa. Kama wewe ni kijana hujaoa/ hujaolewa, unanafasi sasa ya kumtumikia Mungu kwa uhuru wote. Titahidi sana kufanya hivyo sasa, kwasababu nafasi hiyo inaweza ikapungua kwa sehemu uingiapo katika majukumu ya kindoa. Usipojitahidi sasa kujiwekea msingi mzuri kwa Mungu wako, utataabika sana kuujenga huo uwapo kwenye ndoa.

Wakati wa baridi unaweza ukawa ni kipindi cha kazini au masomoni. Ikiwa bado hujapata kazi, au upo likizo kazini au shuleni, embu tumia vema wakati wako, kuongeza kitu kikubwa katika ufalme wa Mungu, kwasababu shughuli zitakapokulemea, kuujenga tena huo msingi itakuwia ngumu sana, na kama ikiwezekana yaweza kukuchukua wakati mrefu. Uwapo ‘free’ usilale, bali tumia sasa kuongeza mikesha, maombi ya masafa marefu, kusoma biblia yote.

Wakati wa baridi waweza kuwa uzee. Kwa jinsi umri unavyokwenda ndivyo uwezo wa mwili wako unavyopungua, Hivyo utengenezapo mambo yako mapema na Bwana, basi wakati huo ukikukuta hautakuathiri sana, kwasababu tayari yale ya msingi uliyopaswa uyafanye umeshayafanya mapema, uzeeni ni kumalizia tu.

Zipo nyakati nyingi za baridi. Chunguza tu maisha yako ujue wakati wako wa baridi unafika lini na ni upi, kisha jitahidi sana, kuwekeza kwa Mungu sasa, kimaombi, kiusomaji Neno, na kiuinjilisti.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MCHE MWORORO.(Opens in a new browser tab)

Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

(Opens in a new browser tab)Fahamu maana ya Mithali 25:13 Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno;(Opens in a new browser tab)

(Opens in a new browser tab)Rudi Nyumbani

Print this post

Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)

SWALI: Nini maana ya hivi vifungu?

Zekaria 13:7-9

[7]Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu, na juu ya mtu aliye mwenzangu, asema BWANA wa majeshi; mpige mchungaji, nao kondoo watatawanyika; nami nitaugeuza mkono wangu juu ya wadogo.

[8]Hata itakuwa, ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, asema BWANA; lakini fungu la tatu litabaki humo.

[9]Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.


JIBU: Unabii huu ulimtabiri Yesu, wakati wa kukamatwa kwake na wayahudi ili auawe, ukisoma Mathayo 26:31 utaona Bwana alinukuu yeye mwenyewe maneno hayo kwa kusema..

“Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika”.

Na kweli tunaona baada ya Yesu kukamatwa mwanafunzi wake wote wakamkimbia.

Kama mstari wa nane unavyosema mafungu mawili yatakatiliwa mbali, nao watakufa, lakini fungu la tatu litabaki humo.

Ni kuonyesha kwa lugha ya mifano kuwa ni idadi ndogo tu ya wanafunzi ambao hawakumuacha kabisa kabisa, mfano wa “theluthi moja”, lakini theluthi mbili zote zilirejea nyuma moja kwa moja. Na ndio maana utaona siku ile ya pentekoste ni watu 120 tu waliokuwepo pale kuingojea ahadi ya roho. Lakini yale maelfu ya makutano yaliyokuwa yakimfuata yalitawanyika.

Lakini katika mstari wa 9, anasema;

“Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwavyo, nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo; wataliitia jina langu, nami nitawasikia; mimi nitasema, Watu hawa ndio wangu; nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu.”

na hao ndio waliopitishwa katika moto, wakabatizwa na Roho, wakawa vyombo vikamilifu vimfaavyo Mungu kwa kazi ya uvuvi.

Lakini adui hakujua ulikuwa ni mpango wa Mungu iwe vile kwamba mchungaji afe, ili wokovu mkuu zaidi ya ule wa kwanza uje kwa kupitia kifo chake.Angelijua hilo hata asingedhubutu kumgusa.

Ndio hapo shetani hakuamini alipoona wale wachache waliojazwa Roho, wakivuta maelfu kwa mamilioni ya watu  kwa kipindi kifupi mpaka dunia nzima ikawa imepinduliwa. Shetani hakujua misheni ya mchungaji ilikuwa ni kuingia ndani ya kondoo, sio kuwachunga tena kwa nje, kama hapo mwanzo.

Je nini tunajifunza?

Je! Wewe ni kundi lipi? Lile la tatu, au yale mawili ya kwanza. Ambayo yanapoona mtikisiko kidogo tu wa kimaisha hurudi nyuma, yanapoona kuyumba kidogo tu kwa kanisa hutoroka, yanapoona kutetereka kidogo kwa kiongozi wao yanarudi Misri? Kumbuka ni kusudi la Kristo wote tupitishwe katika moto, ili tuimarishwe tufae kwa ajili ya kazi njema ya utumishi wake.

Aliwapitisha wana wa Israeli jangwani, ili kuwaimarisha kabla ya kwenda kuwaangusha maadui zao kule Kaanani. Aliwapitishwa mitume wako, kwanini na wewe usipitishwe?

Vivyo hivyo ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, ambaye utapenda Bwana akutumie, basi liweke kichwani kwamba kuna mahali fulani utapitishwa ili kuimarishwa, huo ndio ubatizo wa Moto ulio wa Roho Mtakatifu. Wakati huo usimwache Bwana, kuwa fungu la tatu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KWANINI KRISTO AFE?

Tofauti kati ya zaka na sadaka ni ipi?

(Opens in a new browser tab)MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.(Opens in a new browser tab)

AMELAANIWA AANGIKWAYE MSALABANI.

Rudi Nyumbani

Print this post