MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

MAMBO YA KUJIFUNZA KWA KLOPA NA MKE WAKE!

(Masomo maalumu kwa wanandoa).

Je unamjua Klopa au Kleopa kwenye biblia?.. na tena unamjua Mke wake?

Tuanze kwa mke wa Klopa, kabla hatujaenda kwa Klopa mwenyewe…

 Jibu: Tusome,

Yohana 19:25  “Na penye msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mamaye, na umbu la mamaye, MARIAMU WA KLOPA, na Mariamu Magdalene”.

Mariamu wa Klopa alikuwa ni mke wa mtu aliyeitwa Klopa. Na kwanini aliitwa vile kwa sifa ya jina la Mume wake?.. ni kwasababu ya mwenendo wa mume wake. Laiti kama mume wake angekuwa na sifa mbaya, basi biblia isingemtaja huyu Mariamu kwa sifa ya jina la mumewe, lakini mpaka imemtaja mumewe ni kuonyesha kuwa alikuwa na kitu cha kipekee.

Sasa huyu Klopa/Kleopa ni nani?

Huyu Klopa au Kleopa ndio yule aliyetokewa na Bwana Yesu akiwa na mwenzake walipokuwa wanaelekea kijiji kimoja kilichoitwa Emau, baada ya Kristo kufufuka,.. wakiwa katika mazungumzo yao, maandiko yanasema Yesu mwenyewe aliungana nao pasipo wao kumtambua, na baadaye walifumbuliwa macho na kumtambua na kutoweka.

Tusome,

Luka  24:13  “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.

14  Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.

15  Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.

16  Macho yao yakafumbwa wasimtambue.

17  Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.

18  AKAJIBU MMOJA WAO, JINA LAKE KLEOPA, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?

19  Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;

20  tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.

21  Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;

22  tena, wanawake kadha wa kadha wa kwetu walitushitusha, waliokwenda kaburini asubuhi na mapema,

23  wasiuone mwili wake; wakaja wakasema ya kwamba wametokewa na malaika waliosema kwamba yu hai.

24  Na wengine waliokuwa pamoja nasi walikwenda kaburini wakaona vivyo hivyo kama wale wanawake walivyosema, ila yeye hawakumwona…”

Umeona? Kumbe Kleopa alikuwa ni miongoni mwa wafuasi wa Bwana Yesu, lakini cha kipekee ni kwamba na mke wake pia alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana na ndiye aliyekuwa pale msalabani pamoja na Mariamu Magdalena na Mariamu mamaye Yesu.

Kwa kifupi walikuwa ni watu waliompenda sana Bwana Yesu, ni watu waliokuwa wanafuatilia sana habari za Bwana Yesu, wakati mke wa Kleopa akiwa kule kaburini pamoja na akina Mariamu Magdalena, Bwana aliwatokea wao wa kwanza, kabla hata ya akina Petro, na Yohana, na Andrea na mitume wengine wote. Na kabla Bwana hajawatokea mitume wake (akina Petro na wengineo), aliwatokea Kleopa na mwenzake ( hawa wawili ndio wanaume wa kwanza kumwona Bwana aliyefufuka).

Akina Petro baada ya kupewa taarifa walienda kaburini lakini hawakumwona, lakini akina Kleopa hawakufika kaburini lakini walimwona wa kwanza, tena Zaidi sana walikuwa wanaondoka Yerusalemu lakini Bwana aliwafuata huko na kuwatokea wao kwanza, na tena Bwana ndiye aliyekula nao wa kwanza, na zaidi sana aliwatumia hao kwenda kuwashuhudia mitume 12 kuwa Bwana kafufuka kweli kweli, na walipokwenda Yerusalemu kuwashuhudia ndipo Kristo alipojidhihirisha kwa mitume wake.

Luka 24:31 “Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; kisha akatoweka mbele yao.

32  Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?

33  Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao,

34  wakisema, Bwana amefufuka kweli kweli, naye amemtokea Simoni.

35  Nao waliwapa habari ya mambo yale ya njiani, na jinsi alivyotambulikana nao katika kuumega mkate. 36  Na walipokuwa katika kusema habari hiyo, yeye mwenyewe alisimama katikati yao, akawaambia, Amani iwe kwenu.

37  Wakashituka, wakaogopa sana, wakidhani ya kwamba wanaona roho.

38  Akawaambia, Mbona mnafadhaika? Na kwa nini mnaona shaka mioyoni mwenu?

39  Tazameni mikono yangu na miguu yangu, ya kuwa ni mimi mwenyewe. Nishikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili na mifupa kama mnavyoniona mimi kuwa nayo”.

Ni nini tunajifunza kwa Kleopa na Mkewe?

Kikubwa tunachoweza kujifunza kutoka kwao ni roho na moyo wa kumpenda na kumfuatilia Bwana sana, Kleopa na Mke wake walikuwa ni watu waliomsogelea sana Bwana ndio maana hata taarifa za kufufuka kwa Bwana wao ndio wa kwanza kuzipata. Wote wawili walikuwa ni watu waliompenda Bwana, hakuna hata mmoja aliyemzuia mwenzake katika kumtafuta Bwana.

Na wewe kama Baba kuwa kama Kleopa, usimzuie mke wako kumtafuta Mungu, au kuwa karibu na Mungu muda mwingi, vile vile na wewe mama, kuwa kama mke wa Kleopa, usimzuie mume wako kwenda katika kutafuta uso wa Mungu, wote mfanyeni Kristo kuwa wa Kwanza, na Kristo atawachagua nyie kumwona yeye wa kwanza kabla ya wengine.

Mtamwona Yesu katika familia yenu wa kwanza kabla ya wengine.

Mtaona wema wa Kristo kwenye ndoa yenu kabla ya wengine wote.

Nyie ndio mtakuwa wa kwanza kutoa ushuhuda wa maajabu ya Yesu kwenye maisha yenu kabla ya wengine.

Hiyo yote ni kama mtamfanya Kristo wa kwanza, na kama hamtazuiana katika kumtafuta Yesu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NEEMA YA MUNGU KWA MARIAMU.

Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”

MAMA, TAZAMA, MWANAO.

FAHAMU MAISHA YA YESU KABLA YA HUDUMA.

Je unaruhusiwa kufanya tendo la ndoa ukiwa katika mfungo?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments