Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”

Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”

Ni kwa namna gani baraka ya Bwana haichanganyi na huzuni, nyuma yake?

Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”


JIBU: Kwanza ni vema kufahamu hapo anaposema ‘Baraka ya Bwana hutajirisha’ hamaanishi kuwa kipimo cha kuwa umebarikiwa na Bwana ni utajiri unaofuata baada ya hapo, hapana, Kwasababu wapo watu ambao si wakristo na hawamchi Mungu lakini ni matajiri, na wapo ambao si matajiri na wengine ni maskini kabisa lakini ni matajiri kwa Bwana.

Ufunuo 2:9  “Naijua dhiki yako na umaskini wako, (lakini u tajiri) najua na matukano ya hao wasemao ya kuwa ni Wayahudi, nao sio, bali ni sinagogi la Shetani”.

Baraka ya Bwana haipimwi kwa mali, bali kwa mwitikio wa wokovu ndani ya mtu.

Lakini katika mstari huo, anaeleza tofuati iliyopo kati ya utajiri unaopatikana kwa Mungu na ule unaopatikana penginepo. Kwamba ule wa ki-Mungu Hauchanganyi huzuni ndani yake. Lakini ule wa kwingine unafuatana na huzuni nyingi nyuma yake.

Kwamfano mtu amepata mali kwa njia ya biashara ya madawa ya kulevya. Ni wazi mtu kama huyu hawezi kuwa na raha, kwasababu wakati wote atakuwa katika kujilinda, na mashaka ya kukamatwa na vyombo vya dola. Au mwingine kapata utajiri kwa njia ya rushwa, atakuwa na hofu sikumoja  kukamatwa na vyombo vya dola kwa kosa la kuhujumu uchumi. Au mwingine kwa njia ya uganga, atapewa masharti, atoe wengine kafara, au alale chooni sikuzote za maisha yake, ili utajiri wake uendelee.

Hivyo utajiri wowote nje ya ule unaopatikana na Mungu, unavimelea vingi vya mateso. Visasi, vinyongo, wivu, hofu, mashindano n.k. Kwa kifupi ni kuwa hauna raha, Hivyo Bwana anatushauri kama kufanikiwa tufanikiwe kwake ambapo kunaendana na kanuni ya kumcha yeye kwa bidii (Kumbukumbu 28), kufanya kazi halali, na kuwa mtoaji. Na utakapobarikiwa basi Bwana atakupa raha katika vitu hivyo.

Bwana awe nawe.

Je! Upo ndani ya Kristo? Kama ni la! Wakati ndio sasa, geuka  upokee ondoleo la dhambi zako kwasababu muda ni mchache tuliobakiwa nao, tubu pokea wokovu sasa Parapanda inakaribia kulia. Ikiwa upo tayari kutubu leo, basi fungua hapa kwa mwongozo huo. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)

KANUNI RAHISI YA KUPOKEA BARAKA MARA DUFU.

MWENDO UNAOSHANGAZA SANA!

USIIKARIBIE DHAMBI, KAA NAYO MBALI.

Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU BARAKA

Ni sahihi kwa mkristo kupokea fedha kutoka kwa mtu anayefanya kazi haramu?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
3 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Mathias
Mathias
10 months ago

Kujiunga

Derick Sauga
Derick Sauga
11 months ago

Natamani kubatizwa….namba ya simu 0753610759