Nyongeza ya majina ya watu katika biblia

Nyongeza ya majina ya watu katika biblia

Tunaona kuna baadhi ya watu ambao majina yao yameongezwa vionjo kwa mbele, kwa mfano Simoni Petro, Yuda Iskariote, Tomaso pacha, Simoni mkananayo, Yohana Mbatizaji n.k

Watu hawa ambao majina yao yanaonekana kuongezewa vionjo mbele yake ni kwa lengo la kuwatofautisha na watu wengine wenye majina kama ya kwao. Na vionjo hivyo vilivyokuwa vinawekwa ni aidha kulingana na mahali (miji) wanayotokea, au majina ya wazazi wao, au matendo/huduma  wanazozifanya.

Wafuatao ni baadhi ya majina ya watu yaliyoongezewa vionjo kulingana na Matendo waliyokuwa wanayafanya;

  1. Yohana Mbatizaji – Ili kumtofautisha na Yohana wengi ambao walikuwepo Israeli, aliitwa hivyo Yohana Mbatizaji kutokana na kazi yake ya kubatiza watu aliyokuwa anaifanya, Hivyo palipotajwa Yohana mbatizaji wote walijua analengwa nani.
  2. Simoni Petro- Maana ya Petro ni ‘Jiwe’ dogo la kurusha, na si “mwamba” kama inavyoaminika na wengi. Bwana Yesu alimpa Simoni jina Petro, kutokana na jinsi Bwana atakavyomtumia katika huduma yake, katika kuzipiga nguvu za shetani.
  3. Yohana na Yakobo (Boanerge)- Maana ya Boanerge ni ‘Wana wa Ngurumo’ Marko 3:17. Bwana aliwaita hivi kufuatia huduma zao, na ili pia kuwatofautisha na wengine wenye majina kama yao.

Kulingana na Mahali walipotokea;

  1. Yuda Iskariote- Iskaritote maana yake ni mtu wa Keriote/Keriothi.. Na Keriothi ni mji uliokuwepo katika Nchi ya Moabu.
  2. Simoni Mkirene- Kirene ni mji uliokuwepo Kaskazini-kusini mwa nchi ya Libya, Ili kumtofautisha Simoni huyu aliyeubeba msalaba wa Bwana na Simoni aliyekuwa mwanafunzi wa Bwana, ndipo akatajwa kulingana na mji aliotokea ambao ni Kirene.
  3. Simoni Mkananayo- Aliitwa hivi kufuatia mji aliotokea ulioitwa ‘’KANA’’ ndio kule Bwana alipogeuza maji kuwa Divai (Mathayo 15:22) na pia ulikuwepo pia mji mwingine katika nchi ya Tiro ulioitwa hivyo ‘Kana’, ambapo aliishi yule mwanamke aliyemlilia Bwana amponye binti yake aliyepagawa na pepo (Soma Mathayo 15:21-22).Mtu aliyetokea Kana, aliitwa Mkananayo.. Lakini pia Huyu Simoni Mkananayo sehemu nyingine pia alijulikana kama Simoni Zelote (Luka 6:15, Matendo 1:13), maana ya Zelote ni “Mpigania dini”, hivyo watu waliokuwa wanaishindania na kuipigania dini ya kiyahudi wakati huo waliitwa Wazelote, na huyu Simoni kabla hajaitwa na Bwana alikuwa anajulikana hivyo
  4. Mariamu Magdalene- Magdalene ni mji uliokuwepo huko Galilaya.. hivyo ili kumtofautisha Mariamu mamaye Yesu na yule aliyetokwa na pepo saba, ndipo huyu akaitwa Mariamu Magdalene.

Kwahiyo ili kumtofautisha na Simoni Petro au Simoni  mwingine yeyote, ndipo huyu akaitwa Simoni Mkananayo au Simoni Zelote.

    Kulingana na majina ya Wazazi/ Ndugu

1 .Yakobo wa Alfayo:  Yakobo alikuwa ni mtoto wa Mtu aliyeitwa Alfayo, Aliitwa hivyo ili kumtofautisha na akina Yakobo wana wa Zebdayo na wengine waliokuwepo kwa wakati huo.(Marko 3:18).

2. Yuda mwana wa Yakobo: Huyu alikuwa ni mwanafunzi wa Bwana Yesu ambaye pia aliitwa kwa jina lingine “Thadayo”(Marko 3:18). Ili kumtofautisha na Yuda aliyemsaliti Bwana Yesu, ndipo kwa jina lingine akajulikana hivyo kama Yuda wa Yakobo au Thadayo.

3. Tomaso aitwaye Pacha (Yohana 20:2)– Ni kuonyesha Tomaso kuwa alikuwa na Pacha lakini hakutajwa katika maandiko huyo pacha wake alikuwa ni nani, ila aliitwa hivyo ili kumtofautisha na wakina Tomaso wengine waliokuwepo pale.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Je jina lako ni nani? Na linabeba ujumbe gani?… >>JINA LAKO NI LA NANI?

Maran atha

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

MAANA YA MAJINA NA TAFSIRI ZAKE.

Kwanini mtu afanye miujiza na bado asiende mbinguni?

Yeremia alikuwa na umri gani alipoitwa?

NGUVU YA UPENDO WA KRISTO.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments