Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
14 ambaye katika yeye TUNA UKOMBOZI yaani, MSAMAHA WA DHAMBI”.
Tusome tena Waefeso 1:7..
Waefeso 1:7 “Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao UKOMBOZI WETU, MASAMAHA YA DHAMBI, sawasawa na wingi wa neema yake”.
Kumbe! Maana ya “Ukombozi” ni “MSAMAHA WA DHAMBI”.
Kwamba Tunapopata Msamaha wa dhambi zetu, tunakuwa tumekombolewa na tena tumeokolewa na Nguvu za giza, na kuingizwa katika ufalme wa Mwana wa Pendo lake?.
Hivyo maombi makuu ya Ukombozi ni maombi ya Toba!, kwasababu tunapoomba Toba na kusamehewa katika roho tumepata ukombozi, jambo ambalo ni kuu sana.
Je umemwamini Bwana YESU na kutubu dhambi zako ili upate msamaha wa dhambi??..
Fahamu kuwa hakuna maombi yoyote ya ukombozi zaidi ya yale ya KUTUBU DHAMBI kwa kumaanisha kuziacha kwasababu adui wa kwanza wa mtu ni dhambi ikaayo ndani yake.
Hiyo ndio inayomfunga mtu, na kumharibia njia yake duniani, na njia pekee ya mtu kukombolewa na laana, vifungo, mikosi na kila aina ya vifungo ni kwa njia ya kutubu dhambi.
Ukitaka ndoa yako ikombolewe, tubu na acha uzinzi unaoufanya nje ya ndoa, kama unafanya hayo, hapo ukombozi wa ndoa utazalika wenyewe.
Ukitaka ukombozi wa kazi yako, watoto wako, na mambo yako yote suluhisho ni kutubu na kupata msamaha wa dhambi!.
Lakini tukiikwepa toba na kujitumainisha katika maombi ya kuombewa na kuvunjiwa laana, hakuna ukombozi wowote tutakaopata na hiyo ni Biblia sio theolojia wala mapokeo..
Tubu dhambi leo upate ukombozi, na ufurahie wema wa MUNGU.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Print this post
Jibu: Turejee..
Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa URUJUANI, Gari lake limenakishiwa njumu, Hiba ya binti za Yerusalemu”.
“Urujuani” ni neno lingine la rangi ya “Zambarau”..
Neno hilo pia tunalisoma katika kile kitabu cha 2Nyakati 2:7..
2Nyakati 2:7 “Unipelekee basi mtu mstadi wa kazi ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, NA YA URUJUANI, na nyekundu, na samawi, mwenye kujua kuchora machoro, pamoja na wastadi walioko Yuda na Yerusalemu pamoja nami, aliowaweka baba yangu Daudi”.
Rangi ya Urujuani/Zambarau kibiblia iliwakilisha Enzi/Ufalme… Hivyo mtu aliyevaa Mavazi yenye rangi hiyo ya Urujuani/zambarau alifahamika kama mtu mkuu, aidha mfalme, Malkia au jemedari.
Ufunuo 7:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi. 4 Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.
Ufunuo 7:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa AMEVIKWA NGUO YA RANGI YA ZAMBARAU, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake”.
Utasoma tena juu ya rangi hiyo katika.. Mithali 31:22, Yeremia 10:9, Ezekieli 27:7, na Ezekieli 27:16.
Bwana atubariki.
Mafundisho Mengine
Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)
Kimiami ni nini? (Wimbo ulio bora 2:9).
Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)
Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?
Namna sahihi ya kusoma Neno (biblia).
WhatsApp
Tunasahau sana maisha yetu ya sirini, na kuweka nguvu kubwa, katika kuonekana kwetu kwa nje mbele za watu, hatujui kuwa Darasa kubwa la Mungu kwa mwanadamu lipo katika maisha yake ya sirini. Na Mungu humlipa mtu kwa hayo na si mengine.
Mathayo 6:4….na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
Kujazi maana yake ni kulipa.
Ikiwa na maana, unayoyatenda sasa iwe ni mema au mabaya kwa siri, malipo yake utayaona baadaye kwa wazi.
Yusufu, kabla ya kuwekwa kuwa msimamizi wa mali yote ya Farao, alitumika kama wakili mwaminifu katika nyumba ya potifa, kwa muda mrefu. Baadaye Mungu akamlipa kwa kumpa Misri yote.
Yuda mpaka kuingiwa na shetani, hadi kumuuza Bwana wake, ni matokeo ya wizi aliokuwa anaufanya kwa siri kwa muda mrefu.
Daudi kabla ya kujazwa mafuta ya kumwangusha Goliathi, ni maisha ya sirini ya Imani aliyokuwa anayadhihirisha kule maporini kwa Mungu wake, mbele ya simba na dubu walipokuwa wanakuja kulishambulia Kundi. 1 Samweli 17:34-37)
Vilevile, kwa mtu yeyote yule, kupata kibali, kutumiwa na Mungu, kuinuliwa viwango vya kiroho..hutegemea sana hali zetu za sirini zinazoendelea sasa, Kwamfano utakuta labda huyu ni mwanakwaya, au mtumishi wa Mungu, lakini katika maisha yake ya sirini, anajichua, ni mzinzi, anakunywa pombe, Lakini kwa nje, anajionyesha kuwa ni mwema, anautunza ushuhuda wake, anavaa mavazi ya kujisitiri, anaongea kwa staha, ana juhudi katika utumishi, akidhani kuwa hilo ndio litamshawishi Mungu kumwongezea neema.
Ukweli ni kwamba hapo anapoteza nguvu, kwasababu tusipokuwa waaminifu katika madogo ya sirini, Bwana Yesu hawezi kutuaminisha katika makubwa.. Tabia mbaya za sirini, zinaharibu huduma zetu, utumishi wetu wa baadaye.
Mtu anataka apandishwe labda cheo kazini, lakini katika nafasi hiyo hiyo ya chini, anaiba, mwingine anataka apewe cheo lakini pale pale alipo hawajali watu walio chini yake, ni mwenye wivu, . Unategemea vipi Mungu amlipe mtu kama huyu?
Kabla hujalipwa na Mungu, unakuguliwa kwanza na Mungu.
Shughulika na maisha yako ya binafsi ya sirini, kwasababu hayo ndiyo yanayokueleza utakuwa nani mbele za watu baadaye.
Nini cha kufanya..
Mwalike Bwana, akuchunguze, sirini mwako, Mawazo yako, tabia zako, matendo yako. Kisha mwombe akuponye, na baada ya hapo anza kutendea kazi uliyoyaomba.
Simamia andiko hili;
Zaburi 139:23-24
23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu; 24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele
Mungu akubariki.
USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.
NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.
HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE
Si kila wakati maombi yatakuwa ni mazungumzo ya utulivu na amani, wakati mwingine maombi hugeuka kuwa mapambano, na ung’ang’anizi, na usumbufu. Kuna nyakati Mungu anabadilika tabia, kuonyesha kama hakujali hivi, hakusikii hivi, Sio kwamba anakuonea, au anafurahia wewe kuendelea kuteseka katika hali hiyo, hapana bali anafanya hivyo ili kukutengeneza wewe, kwa namna usiyoijua.
Ni lazima ufahamu, Mafanikio ya maombi si lazima yawe majibu, bali mafanikio ya maombi ni mabadiliko yako. Mungu akitaka kukutengeneza, ili tegeo lako lote liwe kwake, hukawia kutimiza ombi Fulani, ili uongeze tegemeo lako lote kwake.
Imani, tumaini, ukomavu, na Upendo wa ki-Mungu, mara nyingi hujengwa katika namna hiyo ya maombi ambayo yanakugharimu kumtaabisha Mungu.
Yakobo alipomtaka Mungu ulinzi, Mungu hakuonyesha kujali hata kidogo, Hivyo mazungumzo yao, yakabadilika kutoka kuwa ya amani, hadi mapambano, wakapigana mweleka usiku kucha mpaka akajeruhiwa uvungu wa paja, ijapokuwa maombi yalikuwa ni ya ung’ang’anizi sana, ya kuumwa, ya kudhoofika, ya kuchakaa, ya kukonda, ya njaa, lakini hakujua anakwenda kubadilisha hali yake ya ndani, alikuwa anaandiliwa kuwa ISRAELI, na sio Yakobo tena mdhaifu.(Mwanzo 32:24-28)
Fahamu kuwa maombi hufanya jambo la ziada juu ya majibu. Wakati mwingine unaweza usijibiwe kabisa hata hilo ombi unaloliomba lakini fahamu kuwa hutabaki kuwa yule yule.. Mtume Paulo, alimlilia sana Mungu (maombi ya ung’ang’anizi), kuhusu mwiba uliokuwa ubavuni mwake uondolewe, ukweli ni kwamba haukuondolewa, lakini alitoka na ufunuo mpya wa “Neema ya Mungu” ukambadilisha mtazamo wa maisha yake moja kwa moja kuhusu Mungu, Maana yake ni kuwa kama mwiba ule usingemtesa na kumlilia sana Mungu asingeielewa neema ya Mungu, ambayo mpaka leo hii tunajifunza kupitia masumbufu yake.
2Wakorintho 12:7-10
7 Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.8 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.10 Kwa hiyo napendezwa na udhaifu, na ufidhuli, na misiba, na adha, na shida, kwa ajili ya Kristo. Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu.
Hii ni siri ambayo wengi hawaijui, Uonapo upo kwenye Wakati mgumu na umeomba kwa namna ya kawaida huoni dalili yoyote ya kujibiwa, anza maombi ya kung’ang’ana, funga zaidi, lia zaidi, kemea zaidi, zama zaidi …Fanya hivyo kwasababu ipo kazi ya ziada Mungu anataka kuitenda ndani yako zaidi ya majibu unayoyataka,. Usiridhike tu na maombi ya utulivu, shindana na Mungu wako, ng’ang’ana sana, ikiwa hujajibiwa jana, endelea leo, tena kwa nguvu zaidi, ukiona hali imekuwa mbaya, usipoe, shughulika na Mungu zaidi na zaidi, hakuna kukata tamaa, hakuna kurudi nyuma, kwasababu Maombi hufanya kazi nyingine ya ndani zaidi ya majibu tu..
Mwisho utauna uzuri wa Mungu, jinsi atakavyokuleta katika matokeo bora zaidi, ambayo utamshukuru Mungu maisha yako milele. Hivyo fahamu kukawia kwake ni kwa faida yako.
Maombolezo 3:31-33
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha
NGUVU YA MAOMBI
MWONGOZO WA MAOMBI YA FAMILIA
MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
Ulishawahi kujiuliza, kwanini Mungu atumie namna ya “wingi”, alipomuumba mwanadamu, na sio, “umoja”, kama alivyokuwa anafanya kwenye uumbaji wa vitu vingine?
Mwanzo 1:26-28
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba
Anasema na “tumfanye” mtu kwa mfano wetu, na si “nimfanye mtu”? Ni kuonyesha hali ya asili ya anaye muumba, kwamba si wa kibinafsi, bali ya kimjumuiko..asili yake ni jumuiya. Ijapokuwa ni Mungu mwenyewe ndio aliyemuumba mwanadamu, lakini wazo lake aliwashirikisha Malaika zake, ambao walikuwepo kabla yetu sisi..Ndio maana ya hiyo “na tumfanye mtu”
Ni kufunua kuwa sisi ni zao la muunganiko, na ushirika, na ndivyo ambavyo tunaweza pia kuzaa, au kufanikiwa katika namna hiyo hiyo.. Ndio maana, hata sisi tukitaka kumleta mwanadamu mwenye asili yetu, sio jambo la mtu binafsi kujitakia pekee yake, ni lazima mwanamume, atakutana na mwanamke, kila mmoja atachangia alichonacho, na mwishowe, anatokea kiumbe kama wao. Hiyo ni kanuni..sisi kuwepo ni kazi ya “mchango” iliofanywa na watu wawili.
Hata katika maendeleo yetu, na mafanikio yetu. Jambo lolote tukitaka lifanikiwe, ni sharti tukubali michango.. Haiwezekani mtu kusimama mwenyewe mwenyewe kufanikisha kila jambo., Ukuaji wa kiroho, unahitaji kanisa, ukutanapo na watakatifu wenzako,(wawili, watatu, mia) ndipo unajengwa na kukua, tofauti na kujisukuma mwenyewe mwenyewe, hakuna mafanikio .
Vilevile na katika maendeleo ya mambo mengine yote ya mwilini na rohoni, wanaofanikiwa, ni watu wenye kuruhusu, michango, kusaidiwa, kujihusianisha, kujishusha, kujengwa, kufundishwa, kushauriwa, kuwezeshwa, na wengine..Na hatimaye kufanikiwa..Mafanikio ya moyoni yaani furaha, amani, utulivu, ni mahusiano mazuri na mema uliyonayo na wengine, katika ushirika wa Roho Mtakatifu.
Mwanadamu kamili, huishi kwa mahusiano. Kuanzia sasa usipuuzie mahusiano, Jenga mizizi yako vema, tafuta kwa bidii kuishi kwa amani na watu wote (Waebrania 12:14). Kwasababu wewe ni zao la Mahusiano, tangu mwanzo.
Jibu: Turejee….
Matendo 10:9-15 “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana; 10 akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia, 11 akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi; 12 ambayo ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao, na ndege wa angani. 13 Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule.
Matendo 10:9-15 “Hata siku ya pili, walipokuwa wakisafiri na kuukaribia mji, Petro alipanda juu darini, kwenda kuomba, yapata saa sita ya mchana;
10 akaumwa na njaa sana, akataka kula; lakini walipokuwa wakiandaa, roho yake ikazimia,
11 akaona mbingu zimefunuka, na chombo kikishuka kama nguo kubwa, inatelemshwa kwa pembe zake nne hata nchi;
12 ambayo ndani yake walikuwamo aina zote za wanyama wenye miguu minne, na hao watambaao, na ndege wa angani.
13 Kisha sauti ikamjia, kusema, Ondoka, Petro, uchinje ule.
14 Lakini Petro akasema, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi. 15 Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, Vilivyotakaswa na Mungu, usiviite wewe najisi”
14 Lakini Petro akasema, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi.
15 Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, Vilivyotakaswa na Mungu, usiviite wewe najisi”
Katika Ono hili, wale wanyama najisi aliowaona katika ile nguo, ni “Watu wa Mataifa”…Ambao kwaasili ndio waliokuwa wanaonekana najisi mbele za MUNGU, hawakuweza kuwa warithi wa ahadi za MUNGU, wala wahudumu wa utumishi wa MUNGU.
Lakini hapa Bwana MUNGU alikuwa anaongea na Petro kwa njia ya Ono kuwa Mataifa sio najisi tena mbele za MUNGU, hivyo Petro asiogope kuwapelekea Injili.
Kwahiyo kwa ufupi wale wanyama najisi waliwakilisha “Watu najisi qa mataifa”… tunazidi kulithibitisha vipi hilo?..
Tuangalie ule mstari wa 14-15 na ule wa 28..
Matendo 10:14 “Lakini Petro akasema, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi. 15 Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, VILIVYOTAKASWA NA MYNGU USIVIITE WEWE NAJISI”
Matendo 10:14 “Lakini Petro akasema, Hasha, Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu au najisi.
15 Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, VILIVYOTAKASWA NA MYNGU USIVIITE WEWE NAJISI”
………….
28 Akawaambia, Ninyi mnajua ya kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, lakini Mungu AMENIONYA NISIMWITE MTU AWAYE YOTE MCHAFU WALA NAJISI”.
Kwahiyo kwa maneno hayo ya Petro ni wazi kuwa alipewa ufunuo na Roho Mtakatifu kuwa wale wanyama najisi aliowaona ni watu ambao wao walikuwa wanawaona kama najisi mbele za Mungu (yaani watu wa Mataifa, akiwemo Kornelio na familia yake).
Ikifunua kuwa katika suala la Neema ya MUNGU, hakuna upendeleo kwa mtu yeyote myahudi au asiye myahudi.
Wagalatia 3:28 “Hapana Myahudi wala Myunani. Hapana mtumwa wala huru. Hapana mtu mume wala mtu mke. Maana ninyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu”
Lakini pia ni wanyama pia wametakaswa, katika agano jipya hakuna katazo la kula wale wanyama waliokatazwa wakati wa agano la kale, kwani walikuwa wanawakilisha tu aina ya watu, kwa ufupi wanyama walisimama kama ishara ya jamii ya watu, lakini si kwaasili kwamba ni najisi.
Bwana atusaidie.
1 Wakorintho 13:9-10
[9]Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; [10]lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
[9]Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
[10]lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
Biblia inatupa dira kamili wa maisha yetu, na namna ambavyo tunapaswa kumwelewa Mungu na utendaji kazi wake kwetu sisi. Ni vizuri wewe kama mtoto wa Mungu, kujua ni kipi umewezeshwa kujua na kipi hujawezeshwa..
Watu wengi tunapopitia hili andiko, tunashindwa kulitafakari kwa ndani zaidi, na matokeo yake yanakuwa ni kuishi maisha ya kuhangaika na kutaabika tukidhani kuwa Mungu hasemi au Mungu hajibu.
Roho Mtakatifu anatufundisha kuwa katika eneo la kujua mambo yote, sisi hatujakusudiwa kwa sasa. Hujakusudiwa kuishi duniani ujue kila kitu.
Bali kwa sehemu ndogo tu.. kwa mfano wa sasa tunasema unapewa vidokezo(trailer) vya filamu. Lakini picha nzima ya filamu yote hutaijua sasa, mpaka utakapovuka ng’ambo.
Ndivyo ilivyo katika mambo yote, kwamfano ikiwa mtu unamwomba Mungu akupe kujua jambo Fulani, au akufunulie kila kitu kinachoendelea au kitakachoendelea, au akufunulie kila kitu kinachohusu maisha yako ya sasa au ya baadaye…usitarajie utaonyeshwa taswira yote, kwamba leo itakuwa hivi, kesho vile, mwaka vile, wiki ijayo vile n.k. ndugu haiwi hivyo Mungu atakugusia kwa sehemu tu..ndogo ndogo ambazo hizo zitakupa picha fulani…lakini si taswira yote, kwasababu tumepewa kujua kwa sehemu.
Ikiwa wewe ni nabii, Mungu amekuonyesha jambo, toa unabii kama ulivyoonyeshwa usianze kuweka matukio yako ambayo hujaonyeshwa ..mwisho wa siku utajichanganya mwenyewe au jamii unayoitabiria..kwasababu hata iweje huwezi jua kila kitu, huwezi funuliwa kila jambo hata ulieje.
Ndio yaliyomkuta Yohana Mbatizaji.. aliweka matarajio yake, fikra zake, na kuziamini sana mwisho wa siku akamwona hata Kristo siye…ilihali alimshuhudia mwenyewe ndiye.
Kwamfano leo utaenda kwa nabii, kisha akaonyeshwa kwenye maono umebeba mtoto wa kiume, sasa kwasababu atataka kujifanya yeye ni nabii mwenye viwango vya juu ataanza kutoa simulizi zake za uongo…Bwana ananionyesha utabeba mtoto wa kiume hivi karibuni, hivyo andaa nguo zake, pia mwombee, mwandalie na sadaka ya shukrani.
Lakini kumbe Mungu hakumaanisha atampa mtoto, alimaanisha atamfanikisha na kumfanya mlezi wa mayatima.. kwa taswira ile ya mwanamke aliyembeba mtoto.
Matokeo yake yule mwanamke anaweka matarajio yake hapo, miaka inapita hapati mtoto, baadaye yule nabii anaonekana mwongo. Kumbe sio..ni kwasababu alijaribu kuvuka kipimo cha unabii alichopimiwa.
Angesema Bwana amenionyesha hivi na hivi.. zaidi ya hapo sijui, Mungu atakufunulia mwenyewe, ingetosha kumpa yule mama wigo wa kutafakari maono yake, na yatakapotimia atajua kuwa kumbe tafsiri yake ndio ile.
Vivyo hivyo hata wewe mwenyewe..utamwomba Mungu akuthibitishie jambo Fulani, utagundua mara nyingi hupewi taarifa za kujitosheleza juu ya hilo jambo, utapewa ishara tu, wakati mwingine alama Fulani, .
Ukiona hivyo usihangaike sana kupata picha yote ya kila kitu, bali chukua hatua na Bwana atakuwa na wewe..
Kuishi kwa Imani.
Jambo kuu tuliloumbiwa na Mungu, ni kuishi kwa imani sio kwa kuona.
Jambo lolote lifanye kwa imani, kwasababu hujapewa kujua kila kitu kwa ufasaha wote sasa..
Ikiwa na kushuhudia huwezi kungoja kwanza Mungu akuonyeshe jina la mtaa, aina ya mtu utakayekutana naye, nguo aliyovaa na jina lake ndipo uende…hapo ndugu utangoja sana..
Lakini unaenda kwa imani,.ukiamini lile Neno kwamba “nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari,” na matokeo yake unakutana na yule mtu ambaye Mungu amemkusudia kati ya wengi.
Hivyo ndugu fahamu kuwa tunajua kwa sehemu, tunatoa unabii kwa sehemu..
Ndio maana anamalizia kwa kusema;
1 Wakorintho 13:12
[12]Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
Tembea kwa Imani. Unabii, maelekezo, taarifa, vinapokuja machache, ni wakati sasa wa kuchukua hatua ya kutenda kuliko kusubiri hapo muda mrefu.
Bwana akubariki
HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.
KUSUDI LA KWANZA LA KUCHAGULIWA NA MUNGU NI LIPI?
PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.
Jibu: Tureje..
Waefeso 1:5 “Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe WANAWE kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na URADHI WA MAPENZI YAKE”.
Maana rahisi ya “Uradhi wa Mapenzi” ni “Mapenzi ya Hiari”..
Mtu anayefanya kazi fulani kwa Hiari yake mwenyewe na kwa mapenzi yake yote bila kusukumwa, kulazimishwa wala kuhamasishwa mtu huyo ni sahihi kusema amefanya kazi ile kwa “Uradhi wa Mapenzi”.
Na Mungu ametupenda alituchagua sisi tuwe “Watoto wake”.. Kwa mapenzi yake ya Hiari.. na kwa furaha ya Moyo wake, Maana yake ni jambo linalompa raha na furaha sisi kuwa watoto wake, sio uamuzi wa majuto kwake..
1Yohana 3:1 “Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, KWAMBA TUITWE WANA WA MUNGU; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye”.
Kwahiyo ni bahati na upendo mkubwa sana MUNGU kutufanya sisi kuwa watoto wake, na Kuwa Mtoto wa Mungu maana yake ni lazima utabeba tabia za Uungu, na ndio maana wana wa MUNGU wanaitwa miungu..
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, NDINYI MIUNGU? 35 Ikiwa ALIWAITA MIUNGU wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, NDINYI MIUNGU?
35 Ikiwa ALIWAITA MIUNGU wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.
Ni hii ni kweli kabisa mwana ni lazima afanane na Baba, hata mtoto wa Mtu ni Mtu, mtoto wa kondoo ni kondoo, na mtoto wa simba ni simba..vivyo hiyo ni mtoto/watoto wa MUNGU ni miungu.
Je umefanyika mtoto wa MUNGU?.. Na je unaijua kanuni ya kufanyika kuwa mtoto wa MUNGU?.. Si nyingine zaidi ya ile tunayoisoma katika Yohana 1:12..
Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”
Mpokee leo YESU nawe utapata uwezo huu mkuu wa kuwa mwana wa Mungu na mrithi wa ahadi za MUNGU… kwasababu ni Uradhi wa mapenzi yake tuwe hivyo.
Waefeso 1:9 “akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo”.
nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?
JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?
Siku ya kujiliwa inayozungumziwa katika 1Petro 1:12, ni ipi?
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?
Kibiblia ni neno lenye maana ya wale funza, ambapo hutokea palipo na mzoga, au uozo. Hivyo popote ukutanapo na Neno hilo, huashiria/humaanisha, uharibifu au maiti, au kaburi,
Kwamfano ukisoma;
Ayubu 17:14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;
Buu kama lilivyotumika hapo ni kaburi, Ayubu akimaanisha katika hatua aliyofikia, kaburi, na uharibifu ni kama familia yake (baba yake, mama yake na dada yake), kama tunavyojua familia ni kitu cha karibu sana na mtu, ndivyo Ayubu alivyojiona katika hali aliyokuwa amepitia.
Maana yake, kifo kilikuwa karibu na yeye zaidi hata ya familia yake.
Sehemu nyingine inasema;
Ayubu 25:6 iuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!
Mwandishi akimaanisha mwanadamu ni sawa na mzoga, (yaani mwili wenye uharibifu usio na umilele).
Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;
Kutoka 16:20,24, Kumbukumbu 28:39, Ayubu 7:5.
Katika maeneo mengine kwenye biblia linatajwa moja kwa moja kama funza. (Isaya 66:24)
Hii ni hatma ya kila mwanadamu asiye na Mungu, yeye ni buu, haijalishi atakuwa na afya leo, anapesa zote ulimwenguni, anacheo kikubwa au elimu, maisha yake bila Yesu Kristo kumwokoa, ni buu tu (maiti, kaburi, )..atakufa na kuishia jehanam ya moto. Lakini akiokoka, hata ajapokufa, ataishi, siku ya ufufuo ikifika, atafufuliwa na kubadilishwa mwili wake na kupewa mwili mwingine wa utukufu, kisha Kwenda kuishi na Kristo milele na milele mbinguni.
Ikiwa haujaokoka, bado na upo tayari kufanya hivyo leo, basi basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba upokee msamaha wa dhambi leo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).
Jehanamu ni nini?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?
Shalom, karibu katika kuyatafakari maandiko..
Inafahamika kuwa Kristo alimwaga Damu yake pale Golgotha, pale ambapo misumari ilipopita katikati ya mikono yake na miguu yake, pamoja na mapigo mengine mwili mzima. Kwa damu ile iliyomawagika tulipata ondoleo la dhambi na ukombozi wa Roho zetu,
Lakini Damu hiyo hiyo, tunasoma haikuanza kumwagika saa hiyo ya Mateso ya msalaba…Bali ilitangulia kumwagwa wakati Bwana akiwa anaomba pale kwenye mlima wa Mizeituni pamoja na wanafunzi wake,
Sasa ilimwagika kwa jinsi gani?.. si kwa jinsi nyingine bali kwa jinsi ya JASHO LAKE
Luka 22:44 “Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; HARI YAKE IKAWA KAMA MATONE YA DAMU YAKIDONDOKA NCHINI.]”
Sasa swali la msingi ni kwanini, itoke wakati akiwa katika MAOMBI?.. Ni kwasababu maneno pekee hayatoshi kufikisha maombi kwa Baba, bali Damu inanena zaidi kuliko maneno, na Hivyo ile damu iliyokuwa inamwagika wakati wa maombi ilinena zaidi kuliko maneno tu.. Kwa namna gani tunalithibitisha hilo??..Turejee habari ya Habili.
Biblia inasema Damu ya Habili ilinena ardhini baada ya kuuawa kwake..ijapokuwa alikufa lakini ile damu ililia na kuomboleza mbele za Mungu.. (soma Mwanzo 4:10) na Mungu akaisikia, na ikaleta kisasi kwa Kaini aliyemwua..
Vile vile maombi ya Bwana YESU pamoja na Damu yake inayomwagika ardhini kabla ya mateso ya msalaba.. ilinena zaidi na ndio maana baada ya pale, walitumwa Malaika kumtia Nguvu..na tena Damu ya YESU inanena mema kuliko ile ya Habili..
Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.
Na wakati huu tunapoomba kwa kufahamu Ufunuo huo uliopo katika Damu ya YESU, tutapenda MAOMBI!.. tukijua na kuamini kuwa ipo damu ya YESU inayochuruzika sasa kwaajili yetu tunapoomba.. na hiyo damu inanena mema zaidi ya maneno yetu.
Lakini kama tupo nje ya Imani ya kumwamini Bwana YESU KRISTO, damu yake hiyo haiwezi kunena mema kwaajili yetu, ili iweze kunena mema na kumshinda Yule Mwovu, na hata kuvuta majibu ya maombi, ni sharti kwanza kumwamini Bwana YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kubatizwa ubatizo wa maji na Roho, kuanzia huo wakati na kuendelea ile damu inakuwa inanena mema kwaajili yako na utakuwa unazo nguvu za kumshinda shetani.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
NA SISI TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI.
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.
ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.
Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?