Isaka, alipofika mahali panaitwa Gerari alivikumbuka visima vilivyochimbwa na baba yake Ibrahimu zamani, lakini alipotazama na kuvikuta vimeharibiwa, alianza kazi ya kuvichimba tena, Alipokifukua cha kwanza na kutoa maji maandiko yanatuambia wachungaji wa mahali pale wakakigombania..
Akakiita Eseki, akasogea mbele kodogo akakichimbika Kingine tena nacho kikagombaniwa akikiita Sitna, akasogea tena Mbele akachimba kingine cha tatu..
Hicho hawakukigombania akakiita..Rehobothi
Kisha akasema..Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
Mwanzo 26:18-22
[18]Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye. [19]Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika. [20]Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye. [21]Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna. [22]Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
[18]Isaka akarudi akavichimbua vile visima vya maji walivyovichimba siku za Ibrahimu babaye; maana wale Wafilisti walikuwa wamevifukia baada ya kufa kwake Ibrahimu; naye akaviita majina kufuata majina alivyoviita babaye.
[19]Watumwa wa Isaka wakachimba katika lile bonde, wakapata kisima cha maji yanayobubujika.
[20]Wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema, Maji haya ni yetu. Ndipo akakiita jina la kile kisima Eseki, kwa sababu waligombana naye.
[21]Wakachimba kisima kingine, wakagombania na hicho tena. Akakiita jina lake Sitna.
[22]Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa BWANA ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
Sauti ya Mungu nyuma ya habari hii ni nini?
Fahamu ukishaokoka, kuna kisima cha maji ya uzima kinapandwa ndani yako na Yesu Kristo mwenyewe. Kisima hiki licha ya kukupa uzima wa milele..lakini kina kazi ya kukupa raha, kukustawisha na kukufanikisha, maisha yako hapa duniani na mbinguni.
Yohana 7:38
[38]Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
Anasema tena..
Yohana 4:14
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Lakini ni kazi ya adui kukifukia kisima hicho, na hatimaye uwe mkavu kabisa usione raha ya wokovu au matunda yoyote ya imani yako ndani ya Kristo.
Hapo mwanzo ulikuwa ni moto rohoni, ulikuwa unaweza kuomba, kusoma Neno, Bwana alijifunua kwako kwa viwango vya juu..Ukitembea uliuhisi uwepo wa Roho Mtakatifu karibu na wewe…lakini sasa huhisi chochote,huwezi tena kuomba, kushuhudia n.k ukiona hivyo fahamu kuwa kisima kimefukiwa…lakini tumaini ni kuwa maji yapo chini waweza kuanza tena kuchimba na kurudia viwango vyako vya juu hata na zaidi..
Ulirudi nyuma, mpaka ukafikia hatua ya kuyatenda yale machafu ya dunia uliyoyaacha, Ukahisi kama Mungu hawezi kukusamehe tena…ukweli ni kwamba tumaini lipo, anza tu kukichimba kisima chako, maji utayaona.
Ulikuwa na maono mazuri, Na shauku ya kufikia hatma yako, ulikuwa unaona mwendelezo mzuri wa kile ulichokuwa unakifanya hata katika magumu hukutukisika lakini yale maono yamekufa, huelewi ni nini kimetokea, ujue kisima kimefukiwa…anza Upya tena.
Ila ni lazima ukubali kuchukua hatua bila kukata tamaa..Ilimgharimu Isaka visima vitatu lakini hakukata tamaa, hata alipofukua cha kwanza alisumbuliwa, akaendelea tena na tena…alipofikia cha tatu..ambacho ni Rehobothi..basi ikawa ni pumziko lake la daima.
Sisi kama watoto wa Mungu ni Lazima tujue adui ana wivu na hapendi kuona chemchemi za uzima na mafanikio zinabubujika ndani yetu…atafanya juu chini kuhakikisha vinafukiwa na hatimaye kutoona matokeo yoyote ya wokovu kwenye maisha yetu, na wakati huo sio mpango wa Mungu ..ataleta majaribu, misuko-suko, tufani n.k. Lakini ukistahimili Mpaka mwisho utashinda..na hatimaye utakaa mahali pa kudumu pa raha yako kama Isaka..
Ufanye nini?
Anza sasa kujizoesha kwa nguvu kusoma Neno, hata kama mwili hautaki, omba, hudhuria Mikesha acha uvivu, jitenge na dhambi zote. Na hatimaye utaona mwanzo mpya tena wenye nguvu rohoni mpaka mwilini.
Chimba kisima chako
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Print this post
Mtu akikuuliza “Kufanikiwa nini?”..bila shaka unaweza kumjibu ni kuwa na “kazi nzuri yenye kipato kizuri na kuwa na afya njema”. (Hii ni tafsiri nyepesi na rahisi tu).
Sasa tukirudi katika roho, Uzima wa milele ni nini?..biblia imetupa majibu mafupi na marahisi..
Yohana 17:3 “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma”
Ukimjua MUNGU na YESU KRISTO unao uzima wa milele..
Sasa si kwamba MUNGU na YESU ni vitu viwili tofauti.. La! ni MUNGU mmoja katika madhihirisho mawili tofauti..
Mfano mtu anaweza kukuona wewe mubashara (live)…au akakuona kupitia picha yako. Sasa wewe kwenye picha na wewe wa mubashara sio watu wawili tofauti ni mtu mmoja katika madhihirisho mawili tofauti.
Wakati mwingine badala ya kuonekana wewe mubashara unaweza kutuma picha yako au kuibandika katika nyaraka zako muhimu kama vyeti, au vitambulisho au barua na ikawa ni wewe yule yule.
Na YESU ni picha kamili ya Mungu, aliyemwona YESU amemwona MUNGU BABA, kwahiyo hatuwezi tena kutafuta kujua Baba yupoje, tukimwona Yesu tumemwona Baba, ndivyo maandiko yasemavyo..
Yohana 14:8 “Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. 9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?”
Yohana 14:8 “Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.
9 Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba?”
Yohana 14:7 “Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona”
Sasa turudi kwenye “UZIMA WA MILELE”...anasema…“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma”.
Maana yake ukisema unamjua MUNGU halafu unamkataa YESU maana yake huna UZIMA WA MILELE, Kwasababu YESU ni ufunuo kamili wa Mungu katika mwili.
Utaona watu wanasema, mimi namwamini Mungu lakini simwamini YESU, sasa utaikanaje picha ya mtu na kumkiri mtu?..
Nimekuletea picha yangu, halafu unaikana, na bado unakiri kunijua?.. kama ukiikana picha yangu maana yake unanifanya mimi kuwa mwongo.
Vile vile ukimkana YESU na kukiri kumjua MUNGU unamfanya MUNGU kuwa mwongo. (Soma 1Yohana 5:10).
Kama humwamini YESU ni moja kwa moja umwamini MUNGU pia, hiyo haina kutafakari mara mbili..kama humjui Yesu ni moja kwa moja humjui Mungu Baba hiyo haina kutafakari mara mbili pia.
Yohana 8:19 “Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui; kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu”.
Kwahiyo wakati huu Uzima wa milele unapatikana kwa YESU tu pekee yake, zingatia hilo: YESU TU PEKE YAKE!!.…usijaribu kumtafuta Mungu nje ya YESU, ni kupoteza muda.
Usijaribu kumtumikia Mungu nje ya Yesu, ni kupoteza muda, usitafute uzima wa milele nje ya Yesu, ni kupoteza muda na uzima wako wa milele, akitokea mtu, awe nabii, mtume au mchungaji amshuhudii Yesu kama ndie njia pekee ya kufika mbinguni, mkimbie!
Akitokea kuhani na kukufundisha kuna mwingine au wengine wanaoweza kufanya kazi kama ya YESU, mkimbie!.. Kristo YESU hana pacha, wala msaidizi kwamba pia kupitia mtakatifu fulani aliye hai au aliyekufa tunaweza kumwona Mungu, kwamba tukimwamini huyo tunaweza kumwona MUNGU, kimbia!
YESU si mtu wa pembeni aliyeletwa kutuokoa, ni Mungu mwenyewe aliyevaa mwili… yaani Mungu aliyetengeneza mwili na kuweka tabia zake zote ndani ya huo mwili, akaja ili atuonyeshe njia na kutukomboa, hivyo hana msaidizi, kajitosheleza kwasababu yeye ni MUNGU. (1Timotheo 3:16).
Kwahiyo tusipomwamini Yesu kwa namna hiyo hatuna uzima wa milele, haijalishi tutajitahidi kufanya mema kiasi gani, kama tumeshamsikia na hatutaki kumwamini, hatuna uzima wa milele.
Swali ni je?.. Unao uzima wa milele?..je umemwamini YESU na kuyafanya anayoyasema?.
Luka 6:46 “Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? 47 Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake. 48 Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri. 49 Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa”.
Luka 6:46 “Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?
47 Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.
48 Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri.
49 Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa”.
Mwamini YESU na tenda ayasemayo.
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mafundisho mengine:
TENDA AGIZO LA YESU, HILO NDIO LITAKALOKULINDA.
UJIO WA BWANA YESU.
JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.
MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.
Na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa?. Ni mwamba gani huo?(Mathayo 16:18)
Isaya 30:21
[21]na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Sisi kama watoto wa Mungu tunaweza kufanya Maamuzi Sahihi katika maisha yetu lakini pia tunaweza kufanya maamuzi yasiyo sahihi katika maisha…tunaweza pita mkono wa kulia lakini pia tukakosea na kupita mkono wa kushoto..
Lakini wengi wetu tunadhani yale maamuzi sahihi tuliyoyafanya ndio kwamba njia tumeiona na yale yasiyo sahihi tumepotea…lakini ukweli ni kuwa kwa Mungu bado tunahitaji maongozo yake sahihi sio tu katika yale mabaya tuliyokosea, lakini pia katika maamuzi mazuri yote tuliyoyachukua bado tunamwita Yeye sana atuonyeshe njia.
Kwasababu kwa Mungu maamuzi sahihi sio kuona mafanikio ya kweli, unaweza kufikia yaliyo sahihi lakini mwisho wake ukapotea.
Mstari huo unasema…
“mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Mtaisikia sauti yangu ikisema njia ni hii..”
Ni ajabu kuona watu wanamlilia Mungu awaonyeshe njia kwenye nyakati za mambo mabaya tu zile za shida, nyakati za majuto, Nyakati za kupata hasara, nyakati za magonjwa, nyakati za kutafuta mwezi wa maisha, nyakati za kunyauka…nyakati za mkono wa kushoto.
Lakini hawana muda wa kumlilia Mungu awaonyeshe njia yake nyakati za mkono wa kuume..yaani za kufanikiwa, za kustawi, za kuinuka, za afya, za amani, za kupandishwa cheo, za kutajirika, nyakati ambazo chakula kipo, makazi yako, elimu ipo, Fedha ipo,
Wakiona mambo yote yapo sawa, wanadhani njia ndio wameshaiona..ndugu yangu humu duniani wapo watu wamefanikiwa sana, wapo watu imara na makini, wana bidii na ufanisi mzuri, ndoa zao zipo thabiti, watu wema, na kwasababu wamechagua njia hiyo basi juhudi zao zimewapa mafanikio sahihi ya ki- Mungu, wanatenda sawasawa wala hawana shida..si watu wajinga..pande zote wapo imara, hata wao wenyewe wanajiona hawakufanya maamuzi mabaya, lakini baadaye wanaishia katika majuto aidha ya kunaswa na mitego mibaya ya ibilisi au majuto baada ya kufa kukosa uzima wa milele..
Kwasababu maamuzi sahihi sio kuona njia sahihi…
Biblia inasema..
Mithali 16:25
[25]Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
Tunamwitaji Mungu ndugu..
Bwana Yesu alitoa mfano huu..
Luka 12:16-21
[16]Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; [17]akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. [18]Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. [19]Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. [20]Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? [21]Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.
[16]Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
[17]akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.
[18]Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
[19]Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
[20]Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
[21]Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.
Ndugu kila siku uamkapo asubuhi anza na siku ya na Bwana, ibilisi ni kama simba angurumaye kutafuta mtu kama wewe akumeze…acha kiburi cha uzima..katika nyendo zako zote mwombe Mungu akuonyeshe njia, na hiyo huja kwa kuwa mwombaji, na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu..haijalishi wewe ni mchungaji, nabii, raisi, bilionea au nani…jinyenyekeze Kwa Bwana…kuwa mwombaji uisikie sauti ya Bwana..
Na hakika atakujibu..na kukupa mwongozo wake mwema..
Mungu atakujibu daima aidha Kwa Sauti ya Roho wake Mtakatifu ndani yako, au kupitia Neno lake, au kupitia amani moyoni mwako, katika kila hatua. Kwasababu yupo sikuzote kutusaidia tusipotee.
SWALI: Maandiko yanasema “Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele”, Je! ni aibu gani anaomba aepushwe nayo?. Mbona tunapitia kuabishwa, ijapokuwa tumemkimbilia Mungu?
JIBU: Vifungu kadha wa kadha kwenye zaburi vinaeleza, habari hiyo,
Zaburi 31:1 Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye
Zaburi 25:20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe
Soma pia Zaburi 22:5, 71:1
Daudi ni mtu ambaye alizungukwa na maadui pande zote, na hivyo alijua nguvu zake zipo kwa Mungu tu, hivyo akishindwa nao basi itakuwa ni fedheha na aibu kwake, Vilevile ni mtu ambaye aliahidiwa mambo makubwa na Mungu, ikiwemo kudumishiwa kiti chake cha enzi milele, lakini kutokana na mapito na masumbufu mengi aliyokuwa anapitia na kukawia katika ufalme, ilionekana kama jambo hilo haliwezekani..Lakini hakuacha kumwomba Mungu, azitazame ahadi zake asiabike, kwa kumtumaini yeye.
Zaburi 89:49 Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako? 50 Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi. 51 Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako. 52 Na ahimidiwe Bwana milele. Amina na Amina.
Hapo ndio utaona sasa kwanini sehemu nyingi, kwenye Zaburi Daudi anamwambia Bwana, akumbuke asiabike milele, kwa kuzitumainia fadhili zake..
AGANO JIPYA.
Lakini katika agano jipya pia,
Nasi pia tunamtumaini Mungu ili tusiabike milele.Na Aibu kuu ni ile ya kutengwa na uso wa Mungu milele, ambayo watakutana nayo wenye dhambi, ile aibu ya kufukuzwa mbele ya uso wa Mungu.
2 Petro 3:13 Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake. 14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa WALA AIBU mbele yake.
Hiyo ndiyo Bwana atatuepusha nayo sisi tuliomtumainia.
Ni vema kufahamu kuwa tukiwa kama watoto wa Mungu, haimaanishi kuwa hatutaaibishwa au kudhalilishwa kwa ajili ya jina lake, vipindi hivyo tutapitia, lakini mwisho wetu utakuwa ni kutukuzwa katika utukufu mkuu milele..
Ni heri leo ukubali aibu ya kidunia, kuliko kukutana na ile ya Kristo wakati ule..
Mathayo 7:23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Mathayo 25:31-34, 41
31 Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; 32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; 33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. 34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu… 41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
Bwana atusaidie.
Ni kweli tumeumbiwa hasira ndani yenu lakini Biblia inasema hasira inakaa kifuani mwa mpumbavu.
Mhubiri 7:9 “Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako,
Maana yake Mpumbavu ndiye anayeihifadhi hasira, lakini mwenye hekima anashughulika na hasira yake na kuishinda…
Mithali 29:11 ”Mpumbavu hudhihirisha hasira yake yote; Bali mwenye hekima huizuia na kuituliza”
Mithali 14:29 “Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu”.
MADHARA YA HASIRA INAYOKAAA KIFUANI.
Biblia inasema Hasira inamwua mtu mpumbavu…
Ayubu 5:2 “Kwani hasira humwua mtu mpumbavu…”
Inaanza kuua heshima ya mtu, utu wa mtu na mwisho inamaliza mwili…
Hasira inayokaa kifuani haibadilishi chochote bali inaongeza matatizo kwa mtu..
Ayubu 18:4 “Wewe ujiraruaye mwenyewe katika hasira yako, Je! Dunia itaachwa kwa ajili yako wewe? Au jabali litaondolewa mahali pake?”
3.HASIRA INAZAA MAAMUZI YA MABAYA.
Mithali 14:17 “Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa”.
Mtu mwenye hasira hawezi kukosa ugomvi…
Mithali 15:18 “Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano”.
CHANZO CHA HASIRA.
Hivi ni vyanzo vitatu vikuu vya hasira inayokaa kifuani.
Ukiwa nje na wokovu, huwezi kuiepuka roho ya hasira, utakuwa daima mtu wa hasira, yaweza isijidhihirishe kila wakati lakini itakuwa ipo ndani yako tu.
Upo usemi uliozoelekea vinywani mwa wengi kuwa “mimi huwa na hasira sana”… kauli hiyo inatia muhuri na uhalali wa hasira kukaa kifuani mwako, ifute hiyo kauli kinywani mwako, kwani unavyojiwazi na kujinenea ndivyo utakavyokuwa..
Angalia watu unaotembea nao au unaoishirikiana nao ni watu wa namna gani, watu unaojiunganisha nao wanaweza kuathiri tabia yako njema.
Mithali 22: 24 “Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi 25 Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego”.
Mithali 22: 24 “Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi
25 Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego”.
NAMNA YA KUKOMESHA HASIRA.
Komesha hasira yako kwa kumwamini Bwana Yesu na kutubu…maana hasira mwisho wake ni hukumu..
Zaburi 37:8 “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya. 9 Maana watenda mabaya wataharibiwa, Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi”.
Zaburi 37:8 “Ukomeshe hasira, uache ghadhabu, Usikasirike, mwisho wake ni kutenda mabaya.
9 Maana watenda mabaya wataharibiwa, Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi”.
Ukimpokea Bwana YESU kwa kumaanisha kabisa na ukaamua kubadilisha mtindo wa maisha ikiwemo makundi ya watu wasio wa imani, Bwana Yesu kupitia Roho wake mtakatifu atakutakasa utu wako wa ndani na atakupa busara ambayo itaishinda hasira mbaya ya ibilisi..
Mithali 19:11”Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; Nayo ni fahari yake kusamehe makosa”.
Shiriki na wengine habari hizi njema kwa kushea
BWANA SI MWEPESI WA HASIRA, LAKINI BWANA NI MWINGI WA HASIRA.
Maana yake nini, Mwe na hofu wala msitende dhambi? (Zaburi 4:4)
Ipi tofauti ya Hasira na Ghadhabu ya MUNGU?.
MWE NA HASIRA, ILA MSITENDE DHAMBI.
Ipi tofauti ya Juhudi na bidii kibiblia. (Warumi 12:11)
SWALI: Kwanini Bwana Yesu alitumia neno “wewe wasema” alipoulizwa maswali na sio kujibu moja kwa moja?(Mathayo 27:11)
JIBU: Ni kweli tunaona mahali kadha wa kadha Bwana Yesu alipoulizwa maswali Na baadhi ya wayahudi na wapagani, majibu yake hayakuwa yamenyooka moja kwa moja alitumia kauli ya “wewe wasema”…kwa mfano tazama vifungu vifuatavyo;
Mathayo 27:11
[11]Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
Luka 22:68-71
[68]Tena, nikiwauliza, hamtajibu. [69]Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi. [70]Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye. [71]Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.
[68]Tena, nikiwauliza, hamtajibu.
[69]Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi.
[70]Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.
[71]Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.
Soma pia…Luka 23:3
Maana rahisi ya neno hilo ni ipi?
Maana yake ni
“ndio, wewe umesema hivyo, sio mimi”
Au “ndio, wewe umeona kuwa ni hivyo”
Sasa kwanini Atumie kauli hiyo?
Kwasababu alijua waliokuwa wanamuuliza hawakuwa na nia ya kutaka kufahamu ukweli, bali kutafuta neno la kumshitaki, au kumdhihaki, ndio maana kujibu kwake hakukuwa kwa moja kwa moja, yaani upande mmoja anaonyesha kukubali, lakini upande mwingine anaacha hukumu watoe wao wenyewe…
Hiyo ilikuwa ni desturi yake sio tu kwenye maswali bali hata kwenye Mafundisho yake kadha wa kadha…Alizungumza na makutano kwa mifano..kisha wale waliokuwa tayari kupokea aliwafunulia yote baadaye.
Hii ni hekima ambayo tunaweza jifunza hata sisi..
Kwamfano wewe ni mchungaji, kisha ukajikuta watu wasiopenda wokovu, wamekushitaki na kukupeleka Mahakamani halafu hakimu anakuuliza je wewe ndio wale wachungaji ambao, mnaweka Makapu ya sadaka mbele, ili mle Sadaka za waumini.
Sasa unajua kabisa kauli kama hiyo ni ya mtego, kukudhihaki, au kutaka sababu ya kukushitaki, sasa Ili kuikata kauli yake..kukataa Kuwa wewe sio mchungaji watasema unadanganya, kukataa kuwa chombo cha sadaka hakiwekwi mbele watu kutoa, watakuona Pia mwongo, lakini kukusingizia unakula sadaka za waumini unajua ni uongo…
Hivyo kujibu vema hiyo kauli ni kukubali upande mmoja, na mwingmwingiwaachia wao aaamue..
“Wewe Wasema”
Yaani *ndio, wewe umesema hivyo*
“Ndio wewe Umeona kuwa ndivyo ilivyo”.
Hapo umekata maneno yote..atakachoamua, Ni kulingana na mawazo yake mwenyewe lakini sio yale yaliyothibitishwa kikamilifu na wewe..
Hivyo yatupasa tutumie busara. katika ujibuji wetu wa maswali hususani kwa wale wanaotushitaki na kutushambulia
Jina la Mwokozi YESU libarikiwe, karibu tujifunze Biblia.
Ni muhimu kupambana sana mpaka kufikia hatua ya Mungu kuwa kila kitu kwetu, maana yake hata watu wote wakikuacha, au kukutenga, au kukusahau, bado MUNGU ni faraja tosha kwako zaidi ya watu elfu, au ndugu elfu.
Tukifikia hii hatua tutakuwa watu wa furaha siku zote, na watu wa kuishi bila kutegemea sana hamasa kutoka kwa watu au vitu.
Tukiweza kufikia kiwango kwamba faraha kutoka kwa watu haziwi sababu kuu za msukumo wetu kue delea mbele, tutakuwa watu wakuu sana mbele za Mungu.
Pia tukiweza kufikia kiwango kwamba maneno mabaya au dhihaka au kukatishwa tamaa na watu haziwi sababu ya kukata tamaa na kuumia, pia tutakuwa watu wa kuu sana mbele za watu.
Wakristo wengi tunahamasika sana pale tunapohamaishwa na watu, tunapata nguvu zaidi pale tunapotiwa nguvu na watu, na pia tunavunjika moyo sana pale tunapovunjwa moyo na watu, lakini haikuwa hivyo kwa Bwana wetu YESU KRISTO, yeye faraja yake na huzuni yake ilikuwa kwa Baba..
Kiasi kwamba hata watu elfu wangemtukuza na kumtia moyo kama kutiwa huko moyo hakujatoka mwa Baba yake, hakukuweza kumhamasisha kitu.
Hali kadhalika hata watu wote wakitoa maneno ya kuvunja moyo au watu wote wakimwacha na akabaki peke yake, maadamu anaye Baba yake haikumvunja moyo wala kumkatisha tamaa, ndivyo maandiko yasemavyo..
Yohana 16:32 “Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami”.
Hapo Bwana YESU aliona saa inakuja kwamba kila mtu atamkimbia na atabaki peke yake na kweli huo wakati ulitimia pale askari wa Herode walipokuja kumkamata Bwana Yesu pale bustanini, maandiko yanatuonyesha walikimbia wote, na hata mwengine walikimbia uchi (Marko 14:51-52).
Lakini hatuoni Bwana Yesu akivunjika moyo kwa hilo tendo, kwasababu anajua na ana uhakika kwamba Baba yupo naye..
Anajua watu wote wakimwacha haimaanisha Baba yake kamwacha…
Lakini ulipofika wakati wa Baba kumwacha kwa kitambo kwasababu ya dhambi za ulimwengu, ndipo tunaona Kristo anajali na kuhuzunika..
Mathayo 27:46 “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Na sisi hatuna budi kufika hii hatua, Mungu wetu, na Baba yetu abaki yeye kuwa faraja yetu ya mwisho, kiasi kwamba hata dunia nzima ikiondoka, Baba yetu atabaki kuwa hamasa yetu, faraja yetu, yaani awe mwanzo na mwisho kwetu.
Na hata dunia nzima ikutusifia na kutupa maneno ya hamasa, bado hamasa ya Baba yetu ndio itakayokamilisha furaha yetu.
Bwana Yesu atusaidie sana.
Zaburi 9:10 “Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, Maana Wewe, BWANA hukuwaacha wakutafutao”
UTENDAJI KAZI MWINGINE WA ROHO MTAKATIFU USIOUFAHAMU.
FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.
Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?
WALIKUWA WAKINUNUA NA KUUZA, WAKIOA NA KUOLEWA KAMA ISHARA YA KANISA !
MFALME ANAKUJA.
Ukikatazwa na Mungu, haimaanishi kuwa umenyimwa unachoomba, kinyume chake amepewa kwa uzuri wa juu zaidi.
Kuna kipindi Daudi aliingiwa na Nia ya kutaka kumjengea Mungu nyumba ..Hivyo akaanda Mali zake nyingi ili aanze ujenzi…lakini alipolileta Hilo wazo kwa Mungu, ilikuwa ni tofauti na alivyotarajia..
Mungu hakumruhusu bali kinyume chake akamwambia wewe hutanijengea mimi nyumba…kwasababu umemwaga damu ya watu wengi, lakini mwanao ndiye atakayenijengea…
1 Mambo ya Nyakati 22:7-8
[7]Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Kwangu mimi nia yangu ilikuwa kujenga nyumba kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wangu. [8]Lakini neno la BWANA likanijia, kusema, Wewe umemwaga damu nyingi, na vita vikubwa umevifanya; wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu;
[7]Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Kwangu mimi nia yangu ilikuwa kujenga nyumba kwa ajili ya jina la BWANA, Mungu wangu.
[8]Lakini neno la BWANA likanijia, kusema, Wewe umemwaga damu nyingi, na vita vikubwa umevifanya; wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu;
Jiweke katika hiyo hali unatamani ufanye kitu fulani chema, lakini Mungu anakuambia (aidha kwa maneno au vitendo) hapana wewe hustahili kufanya au kuchukua nafasi hiyo, kwasababu hii na hii na hii, bali ataichukua kijakazi wako, mtumwa wako, rafiki yako, mpendwa mwenzako…Sasa Kibinadamu hilo linaweza likaleta ukakasi lisikuvutie Masikioni mwako…kwasababu unajua litampa cheo mwezako.
Pengine ndivyo angeweza kufikiri Daudi… Lakini alijifunza kunyenyekea, na kumtii Mungu na kuachilia kijiti kwa mwingine…
matokeo yake ikiwa ujenzi ule ukadumishwa na jina lililodumishwa halikuwa lingine bali la Daudi kwa vizazi vyote vijavyo..aliyejenga alikuwa ni Sulemani, lakini utukufu ulikuja kwa jina la Daudi mpaka leo linatajwa.
Hii ni kutufundishia kukubali kunyenyekea Katika mapenzi yote ya Mungu..Zipo nyakati hutafanya wewe, hata kama umeomba na kuitamani hiyo nafasi yakupasa ukubali wengine wafanye, upo wakati hutatukuzwa wewe kubali wengine watukuzwe kupitia wewe, hutaheshimiwa wewe lakini fanya bidii wengine waheshimiwe kupitia wewe…kwasababu hiyo ndio ngazi ya kuinuliwa na Mungu, na matokeo yake utayaona..
Makatazo ya Mungu ni fursa ya mafanikio, unaweza ukawa hujapewa uzao, lakini ukamlea mtoto wa mwingine, Mungu akaja kumfanya raisi wa nchi, ukaitwa mama wa Taifa. Hivyo maadamu unatembea katika njia za Bwana na umeomba, amini kuwa Mungu amekupa zaidi ya kile ukiwazacho.
Kamwe Using’ang’anie jambo, bali jifunze kuachilia neema ya Mungu yenyewe kuamua, kwasababu hutapoteza chochote..
Waefeso 3:20
[20]Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu;
Bwana awe nawe…
Swali: Uzao wa mwanamke utampondaye kichwa nyoka, na nyoka ataupondanye mguu uzao wa mwanamke?
Jibu: Turejee..
Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; 15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; HUO UTAKUPONDA KICHWA, NA WEWE UTAMPONDA KISIGINO”.
Mwanzo 3:14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;
15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; HUO UTAKUPONDA KICHWA, NA WEWE UTAMPONDA KISIGINO”.
Andiko hili lina maana mbili (02) ya mwilini na rohoni.. tuzitazame zote.
1. MWILINI
Kiumbe cha kwanza kinachoogopeka zaidi na mwanadamu ni nyoka vingine ni simba na mamba, lakini nyoka ndiye anayeshika namba moja..
Na mwanadamu anapokutana na nyoka mara nyingi anakimbilia kuponda kichwa!… hata pasipo kufundishwa na mtu, kichwa cha nyoka ni shabaha ya kwanza ya mtu, na hiyo haiji tu kwa bahati mbaya bali ni kwasababu tayari tangu mwanzo Mungu alishasema hayo.. “HUO UTAKUPONDA KICHWA”.
Lakini pia sehemu ya kwanza sehemu ya kwanza ya nyoka kuuma/kugonga ni mguu wa mtu/kisigino, kwasababu ndio sehemu ya chini kabisa ya mwili wa mwanadamu na ndio sehemu rahisi nyoka kuifikia kwasababu yeye mwenyewe anatambaa kwa tumbo..
Ni ngumu nyoka kukimbilia kung’ata mkono wa mtu au goti la mtu, lakini ni rahisi sana kisigino kwasababu ndio kipo chini na karibu sana na yeye.. Sasa hiyo ni maana ya kimwili, yenye uhalisia hebu tutazame maana ya pili ya kiroho.
2. ROHONI.
Kiroho “Uzao wa mwanamke” ni “Uzao wa YESU KRISTO”.. sasa si kwamba Yesu ni mwanamke la!. Bali kwasababu alizaliwa na mwanamke pasipo mbegu ya mwanaume kuhusika… Kwahiyo Yesu alikuwa na mama wa kibinadamu, lakini hakuwa na Baba wa kibinadamu (Isaya 7:14)..ndio maana anajulikana kama Uzao wa mwanamke.
Na wote wanaomwamini Yesu wanaingia katika uzao huo, (wa mwanamke).. Na uzao wa mwanamke una nguvu kwasababu ndio uzao wa MUNGU.
Sasa kama uzao wa mwanamke ni Yesu pamoja na wote wanaomwamini, vipi kuhusu uzao wa nyoka. Uzao wa nyoka ni wote ambao hawaitaki kweli, lakini wanamwabudu ibilisi.. kwanini wote wanaomwabudu ibilisi wanaitwa uzao wa nyoka?.
Ni kwasababu Biblia inamtaja “Nyoka” kama Ibilisi (Soma Ufunuo 20:2).. Na tena Bwana Yesu akasema “ninyi ni wa baba yenu ibilisi”.
Yohana 8:43 “Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu. 44 Ninyi ni wa BABA YENU, IBILISI, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.
Yohana 8:43 “Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu.
44 Ninyi ni wa BABA YENU, IBILISI, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake”.
Hapo anasema “Ninyi ni wa BABA YENU, IBILISI” sasa badala ya kusema “ibilisi” weka “nyoka” kulingana na Ufunuo 20:2, kwahiyo ni sahihi kabisa kusema “nyinyi ni wa baba yenu joka/nyoka” hivyo wao ni uzao wa nyoka.
Ndio maana Yohana akawataja kama wazao wa nyoka..
Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?”
Soma tena Mathayo 12:34, Bwana Yesu anautaja uzao wa nyoka.. Kwahiyo kumbe tumejua! Mtu yeyote anayeikataa kweli na kumwabudu ibilisi ni uzao wa nyoka!..
Sasa hebu turejee pale maandiko yanaposema “uzao wa mwanamke utamponda kichwa uzao wa nyoka, na uzao wa nyoka utaponda kisigino uzao wa mwanamke.”
Hapa anazungumzia uwezo wa kimamlaka.. Kwamba uzao wa mwanamke (yaani watu walio ndani ya Imani ya Yesu Kristo) watakuwa na mamlaka juu ya uzao wa ibilisi, na hawa watakuwa na uadui, ndio maana utaona ijapokuwa watu wa MUNGU siku zote ni washindi lakini bado wanakutana na majaribu ya watu wanaomwabudu ibilisi, na wakati mwingine wanaumizwa nao.
Kwahiyo upo uadui wa asili kati ya watu wa Mungu (walio na imani ya YESU) na wale wanaomwabudu ibilisi.. Watu wa Mungu wanaponda vichwa (yaani Uongozi na mamlaka) za falme za watu wa ibilisi, ndivyo maandiko yanavyosema..
Habakuki 3:13 “Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako, Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako; UKAKIPONDA KICHWA CHA NYUMBA YA WAOVU, Ukiuweka wazi msingi hata mwambani”.
Na kinyume chake, watu wa ufalme wa giza (wa ibilisi) wanasumbua miguu (sehemu za mwisho mwisho) za watu wa Mungu… ndio maana utaona ijapokuwa Kristo aliziponda mamlaka za giza pale Kalvari kupitia kifo chake lakini miguu yake ilikuwa na alama za misumari, kutimiza unabii wa uzao wa nyoka kuponda miguu uzao wa mwanamke.
Na Ukitaka kuthibitisha zaidi kuwa “Uzao wa Nyoka” unaweza kuwakilisha watu Fulani.. rejea maandiko yafuatayo..
Mwanzo 49:17 “Dani atakuwa NYOKA barabarani, BAFE katika njia, Aumaye VISIGINO vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali”.
Kwahiyo tunaona kuna faida kubwa ya kuwa upande wa Bwana zaidi ya ule wa ibilisi.. kwasababu upande wa ibilisi utapondwa kichwa na uzao wa mwanamke..Na hata sasa matukio ya nyoka kuuawa na mwanadamu ni mengi kuliko nyoka kuua wanadamu.. kiroho inatakangaza jambo hilo hilo, kuwa uzao wa Mungu una nguvu nyingi.
Je upo upande gani?.. je wewe ni uzao wa nyoka au wa mwanamke??.. Kama hujaokoka huna haja ya kutafuta kujua upo upande gani, ni moja kwa moja upo ule wa nyoka, “wa kupondwa kichwa” kwasababu ibilisi ni nyoka.. Mpokee leo YESU na ugeuzwe asili yako, kama bado hujampokea, na uwe mtu mwenye mamlaka ya kuponda vichwa vya majoka..
1Samweli 2:10 “Washindanao na Bwana watapondwa kabisa; Toka mbinguni yeye atawapigia radi; Bwana ataihukumu miisho ya dunia; Naye atampa mfalme wake nguvu, Na kuitukuza pembe ya masihi wake”.
Wale Nyoka wa Moto jangwani, walikuwa ni wa namna gani?
TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.
KUOTA NYOKA.
Huu ni mwongozo wa maombi yetu ya kambi July 30 – Aug 2.
Kanisa la Nuru ya Upendo
Daresalaam Tegeta. Bofya hapa
👇 📥
Miongozo mingine.
MWONGOZO WA MAOMBI YA KUJIKUZA KIROHO.
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
MWONGOZO WA MAOMBI YA FAMILIA