ORODHA YA WAANDISHI WA BIBLIA.

ORODHA YA WAANDISHI WA BIBLIA.

Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.

Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.

Agano la kale.

  1. Amosi – Mwandishi wa kitabu cha Amosi
  2. Danieli – Mwandishi wa kitabu cha Danieli.
  3. Daudi- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi, kwa baadhi ya Zaburi.
  4. Ezekieli- Mwandishi wa kitabu cha Ezekieli.
  5. Ezra- Mwandishi wa kitabu cha Ezra.
  6. Habakuki – Mwandishi wa kitabu cha Habakuki.
  7. Hagai – Mwandishi wa kitabu cha Hagai.
  8. Hosea- Mwandishi wa kitabu cha Hosea.
  9. Isaya- Mwandishi wa kitabu cha Isaya.
  10. Yeremia – Mwandishi wa kitabu cha Yeremia
  11. Yoeli – Mwandishi wa kitabu cha Yoeli
  12. Yona- Mwandishi wa kitabu cha Yona.
  13. Yoshua- Mwandishi wa kitabu cha Yoshua.
  14. Malaki- Mwandishi wa kitabu cha Malaki.
  15. Mika- Mwandishi wa kitabu cha Mika.
  16. – Mwandishi wa kitabu cha Esta.
  17. Musa – Mwandishi wa kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Kumbukumbu la Torati, Hesabu, Ayubu na Zaburi 90.
  18. Nathani (Nabii) – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  19. Nabii Gadi- – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  20. Nahumu- Mwandishi wa kitabu cha Nahumu.
  21. Nehemia- Mwandishi wa kitabu cha Nehemia.
  22. Obadia- Mwandishi wa kitabu cha Obadia.
  23. Samweli- Mwandishi wa kitabu cha Samweli (Sehemu baadhi)
  24. Sulemani- Mwandishi wa kitabu cha Mithali, Mhubiri na Wimbo ulio bora.
  25. Sefania -Mwandishi wa kitabu cha Sefania.
  26. Zekaria-Mwandishi wa kitabu cha Zekaria.
  27. Wana wa Kora-Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 42, Zaburi 44-49, Zaburi 84-85, na Zaburi 87-88.
  28. Asafu- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 50, na Zaburi 73-83.
  29. Ethani – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  30. Heman – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  31. Aguri – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 30.
  32. Lemueli – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 31.

Agano Jipya.

  1. Mathayo – Mwandishi wa kitabu cha Mathayo.
  2. Marko – Mwandishi wa kitabu cha Marko.
  3. Luka – Mwandishi wa kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume.
  4. Yohana – Mwandishi wa kitabu cha Yohana Mtakatifu na 1 na 2Yohana pamoja na Ufunuo.
  5. Yakobo – Mwandishi wa kitabu cha Yakobo.
  6. Yuda – Mwandishi wa kitabu cha Yuda.
  7. Paulo- Mwandishi wa kitabu cha Warumi, 1 na 2Wakorintho, Wagalatia, Waefeso, Wakolosai, Wafilipi, 1 na 2Wathesalonike, 1na 2Timotheo, Tito na Filemoni.
  8. Petro – Mwandishi wa kitabu cha 1 na 2Petro.

Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.

Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.

2Timotheo 3:16  “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Je ni Mungu au Malaika?

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi Nyumbani

Print this post

Je kweli Abramu alikuwa hajui aendako kulingana na Waebrania 11:8?.

Swali: Je kipindi Ibrahimu anatoka Uru ya Ukaldayo, hakuwa anajua anakokwenda kwamba ni Kaanani? au alikuwa anaongozwa na Roho Mtakatifu mpaka pale alipofika, ndipo Bwana akamwambia hapo hapo atulie?…na mbona tukisoma Mwanzo 12:5 tunaona kama Abramu alikuwa anajua kabisa anakoelekea, au je biblia inajichanganya?


Jibu: Biblia, Neno la Mungu halijichanganyi kamwe..

Turejee …

Waebrania 11:8 “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka ASIJUE AENDAKO”.

Hapa ni kweli panaonesha kuwa Ibrahimu alikuwa hajui aendako, lakini hebu tusome maandiko mengine ndipo tutapata kuelewa zaidi..

Mwanzo 12:1 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka………………

5 Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani”

Hapa panaonyesha kuwa Abramu alikuwa anajua anakokwenda, kuwa ni Kaanani, Je lipi ni sahihi?

Jibu ni kwamba Abrahamu alikuwa anajua anakokwenda isipokuwa alikuwa hajui kama nchi hiyo aiendeayo (yaani ya Kaanani) kama ndio itakuwa ya ahadi..

Hivyo alienda mpaka alipofika na alipofika ndipo Mungu akamtokea na kumwambia kuwa nchi hiyo aliyopo ndiyo itakuwa milki yake (ya ahadi).

Mwanzo 12:5 “Abramu akamchukua Sarai mkewe, na Lutu mwana wa nduguye, na vitu vyao vyote walivyokuwa wamejipatia na hao watu waliowapata huko Harani, wakatoka ili kwenda nchi ya Kanaani; nao wakaingia katika nchi ya Kanaani.

6 Abramu akapita katikati ya nchi mpaka mahali patakatifu pa Shekemu; mpaka mwaloni wa More. Na Wakanaani siku zile walikaa katika nchi hiyo.

7 BWANA akamtokea Abramu, akasema, Uzao wako nitawapa nchi hii. Naye huko akamjengea madhabahu BWANA aliyemtokea”

Sasa swali linakuja, je ni kitu gani kilichomwelekeza Abramu aende nchi ya Kanaani na si nchi nyingine?

Tulirejea ule mlango wa 11 wa kitabu cha Mwanzo, tunasoma kuwa wazo la kuhama Uru wa Wakaldayo na kuelekea Kanaani halikuanzia kwa Abramu, bali lilianzia kwa baba yake aliyeitwa Tera, huyo ndiye aliyefikiri kuhama Ukadayo na hata kuchukua hatua ya kuhama pamoja na watoto wake wote ikiwemo Abramu.

Mwanzo 11:31 “Tera akamtwaa Abramu mwanawe, na Lutu mwana wa Harani, mwana wa mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka wote katika Uru wa Wakaldayo, waende nchi ya Kanaani, wakafika mpaka Harani wakakaa huko”.

Umeona hapo?..sio Abramu aliyekuwa na wazo la kuondoka Ukaldayo bali ni Tera, na sababu za kuwaondoa kule hazijulikani, kwani biblia haijaweka wazi, labda huenda ni maasi ya nchi hiyo, au sababu nyingine za kijamii au kibiashara.

Lakini katika wazo hilo la kuhama, lilikuwepo pia kusudi la Mungu ndani yake, kwamba Abramu afike Kanaani.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu alijua anakoenda, lakini hakujua nchi atakayopewa mpaka alipofika.

Nini tunajifunza hapo?

Wakati mwingine Bwana anaweza kutumia wazo la mtu mwingine kukupeleka wewe mahali Mungu anapotaka uwe.

Hivyo wakati mwingine usinung’unike unapoona unahamishwa mahali ulipo, kwani pengine Mungu anakupeleka mahali anapotaka wewe uwe, na ukishafika ndipo atakuonyesha.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).

Swali: Je Mungu hapendezwi na dhabihu na matoleo, kulingana na mstari huo?


Jibu: Turejee..

Waebrania 10:5 “Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema,

Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari”.

Andiko hili limerejewa kutoka katika Zaburi 40:6, tusome ili tupate maana kamili.

Zaburi 40:6 “Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo,

Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka”.

Hapo imewekwa vizuri kuwa ni kafara na sadaka zinazotolewa kwaajili ya DHAMBI!! ndizo asizozitaka…

Sasa Dhabihu ni sadaka za kuteketezwa (ambazo ni kafara za wanyama) zilizokuwa zinatolewa kipindi cha agano la kale kwaajili ya kufunika dhambi..

Na kasoro ya dhabihu za wanyama ndio hiyo, ilikuwa haiondoi dhambi bali inafunika tu..

Kwahiyo hapo anaposema “Dhabihu na matoleo hukutaka”.. alimaanisha kuwa hizo dhabihu za wanyama hazifai katika kumwondolea mtu makosa yake na kumtakasa bali mwili wa Yesu na damu yake ndio iwezayo kumtakasa mtu na kumwondolea kabisa dhambi zake.

Ndivyo maandiko yasemavyo kuwa damu za mbuzi na mafahali haziwezi kuondoa dhambi na kumtakasa mtu bali zilikuwa zinafunika tu.

Waebrania 10:3 “Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.

4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi”

Lakini dhabihu ya mwili wa YESU, kupitia kumwagika kwa damu yake, unaondoa kabisa dhambi… Na hiyo ndio sadaka Mungu aliyoihitaji na sio dhabihu za kondoo na mbuzi na mafahali.

Waebrania 10:10 “Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.

Lakini kuhusiana na utoaji wa sadaka ni kwaajili ya shukrani, au kwaajili ya kazi ya ufalme wa mbinguni ni jambo linalompendeza Mungu na lenye baraka.

Lakini kama ni kwaajili ya dhambi (hakuna sadaka inayoweza kuondoa dhambi)..isipokuwa damu ya YESU ambayo tayari tumeshalipiwa bureee… tunachopaswa kufanya ili sadaka hiyo ifanye kazi juu yetu ni KUTUBU TU kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi!.

Tukiweza kutubu kwa kumaanisha basi tunapata msamaha na ondoleo la dhambi bure.

Je unaye YESU maishani?.

Kumbuka daima kuwa mwisho wa dunia upo, kama tu vile mwisho wa maisha ulivyo, ikiwa leo hii damu ya YESU si kitu cha thamani kwako, utasimamaje siku ile ya mwisho mbele zake?..Tafakari mara mbili.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je maji na giza viliumbwa siku ya ngapi?

Swali: Je vitu kama giza, na maji viliumbwa siku ya ngapi, maana tunaona wakitajwa tu wanyama na mimea, je hivi vingine viliumbwa lini?


Jibu: Ni kweli katika kitabu cha Mwanzo tunaona uumbaji unaanza kwa kusema “giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”, lakini haitaji ni lini giza liliumbwa wala ni lini maji yaliumbwa, badala yake tunaona uumbaji unaendelea na vitu vingine kama mimea pamoja na wanyama na wanadamu?..

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.

2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji”.

Jibu la swali hili lipo katika mstari huo wa kwanza..

Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi”.

Neno “hapo mwanzo”… halimaanishi kile kipindi cha siku saba (7) bali linamaanisha mwanzo kabisa wa uumbaji kabla ya kitu kingine chochote, Mungu aliumba mbingu (hii yenye mawingu na sayari) pamoja na mbingu ile yenye Malaika watakatifu.

Na vile vile aliumba “NCHI” Au kwa lugha nyingine ARDHI/DUNIA. Na ili ardhi iweze kukamilika ni lazima iwe na malighafi zake zote kama udongo, mchanga, mawe, milima, mabonde, chuma, madini, moto na maji na mengineyo.

Vile vile ili mbingu ikamilike lazima iwe na nyota na mwanga uwepo na giza liwepo, kwahiyo vitu hivi vyote viliumbwa Hapo Mwanzo, kabla ya zile siku sita za uumbaji.

Na baada ya Mungu kuumba Mbingu na nchi, hatujui ni kitu gani kilitokea kikaifanya nchi/dunia yenye milima na mawe na madini na mabonde na maji kuwa UKIWA! Au kwamba Mungu ndio aliiumba ikae hivyo ukiwa kwa kipindi Fulani cha muda..hatujui!, labda tutakuja kujua tutakapomaliza maisha haya na kufika huko kwake, tutamwuliza, lakini tunajua kuwa alisema hakuiumba ukiwa, bali ikaliwe na watu.

Isaya 45:18 “Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine”

Hivyo kama hakuiumba ikae ukiwa bali ili ikaliwe na watu, basi hana budi kuiikarabati na kumweka mwanadamu humo, na ndipo hapo siku sita za uumbaji wa wanyama na wanadamu na miti zilipoanza..

Lakini kiuhalisia tayari mbingu na nchi zilikuwa zimeshaumbwa hapo kabla, na malighafi zake zote (kama maji, udongo, mawe, madini, giza, hewa n.k)..na ndio maana hatuoni vikitajwa katika uumbaji.

Lakini pamoja na hayo, upo unabii unaoonyesha kuwa dunia itakuja kuwa tena ukiwa siku za mwisho, kipindi ambacho ghadhabu ya Bwana MUNGU itakapokuja kumwagwa juu wa wanadamu wote wakosaji, ambayo hata mmoja wetu hapaswi kuwepo..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze”.

Isaya 24:1 “Tazama, Bwana ameifanya dunia kuwa tupu, aifanya ukiwa, aipindua, na kuwatawanya wakaao ndani yake”.

Jambo litakalotokea siku hiyo ni lile tunalolisoma katika kitabu cha 2Petro 3:10-12 na Isaya 34:4.

Lakini wateule, waliomwamini Bwana na kuoshwa kwa damu yake, hawatakuwepo katika siku hiyo ya ghadhabu yake, kwani watakuwa mbinguni pamoja na Bwana.

Bwana atubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Je kuna pepo wazuri kulingana na Waefeso 6:12?

Swali: Biblia inasema kushindana kwetu ni dhidi ya pepo wachafu, je kulingana na mstari huo, wapo pepo wazuri?


Jibu: Turejee…

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHI YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”

Biblia iliposema kuwa kushindana kwetu ni dhidi ya “pepo wabaya” haijamaanisha kuwa wapo pepo wazuri, bali inaelezea tu sifa ya hizo roho (mapepo) kwamba ni mbaya na chafu.

Ni sawa na biblia inapotaja Malaika watakatifu, (soma Mathayo 25:31, Marko 8:38 na Ufunuo 14:10) haimaanishi kuwa wapo Malaika wasio watakatifu, na kama wapo wasio watakatifu basi hawaitwi tena Malaika bali ni mapepo, vile vile hakuna mapepo wasafi na kama zipo hizo roho safi basi haziwezi kuitwa tena mapepo, bali zitaitwa Malaika.

Hivyo uzuri na usafi unaotajwa juu ya Malaika au Mapepo, ni kuelezea tu sifa zao na kazi zao, kwamba Malaika wote walioko mbinguni ni wasafi na watakatifu, na mapepo yote yaliyotupwa ulimwenguni ni machafu na mabaya.

Na kumbuka pia “Pepo na jini” ni kitu kimoja, isipokuwa ni lugha mbili tofuati tu!… Na hakuna jini wala pepo mzuri, wote ni wabaya na wachafu. Zipo dini zinazofundisha kuwa wapo majini (mapepo) wazuri, na kwamba watu wanaweza kuwa nao na wakawaletea mafanikio na hata kuwalinda.

Huo ni uongo wa shetani asilimia mia, kwani shetani ndiye baba wa uongo..

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; KWA SABABU YEYE NI MWONGO, NA BABA WA HUO”.

Shetani hajawahi kuwa na urafiki wa kweli na mwanadamu, wala hajawahi kuwa na mapenzi na mwanadamu, kitu anachokipenda kutoka kwa mwanadamu ni utukufu tu!.. lakini hajawahi kumpenda mwanadamu, na hakuna unabii ya kwamba atakuja siku moja kumpenda mwanadamu, yeye ni adui wa mwanadamu wa milele.

Na Kama tu shetani asivyopendwa kuitwa shetani, bali anapendwa aitwe mungu, kadhalika hawezi kuruhusu mapepo yake yaitwe vibaya, kwa sifa mbaya?..atawatakasa tu!.. na anawatakasaje?..si kwa njia nyingine bali kwa njia za dini za uongo, zinazohubiri na kufundisha kuwa wapo mapepo wazuri.

Kwa urefu kuhusiana na pepo wachafu(majini) fungua hapa >>

MAJINI WAZURI WAPO?

Je umempokea YESU?.. kama bado ni nini kinakungojesha?

Bwana anarudi.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Naliupata wenyeji huu kwa mali nyingi, maana yake nini (Matendo 22:28)

Jibu: Habari hii inamhusu Mtume Paulo, kipindi aliposhikwa na kufungwa akiwa Yerusalemu.. sasa ili tuelewe vizuri tuanze kusoma ule mstari wa 25

Matendo 22:25 “Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?

26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi

27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.

28 Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA WENYEJI HUU KWA MALI NYINGI. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa”.

Wenyeji unaozungumziwa hapo ni “URAIA”.. Kwahiyo hapo kiswahili kingine cha andiko hili ni hiki .. “Jemadari akajibu, MIMI NALIPATA URAIA HUU KWA MALI NYINGI”.

Zamani za kanisa la karne ya kwanza, ufalme uliokuwa na nguvu duniani, ulikuwa ni ufalme wa Rumi, na ndio uliokuwa unatawala dunia chini ya Kaisari. Hivyo kutokana na nguvu ya ufalme huo, basi hata raia wake walikuwa na nguvu, na heshima.

Raia wa kirumi (yaani Mrumi) alikuwa hawezi kuadhibiwa bila kushitakiwa, na haki zake zilikuwa zinalindwa sana kuliko raia wa Taifa lingine lolote duniani,..ilikuwa ni kosa kubwa kumhukumu Mrumi kabla ya kumsikiliza.

Sasa hapa Paulo alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa lakini kwaasili ni Mwebrania (yaani muisraeli), na hapa alikuwa amevunjiwa haki yake kama raia wa kirumi, na hivyo akida pamoja na jemedari wakaogopa, kwasababu ni kosa kumhukumu Mrumi kabla ya kumpandisha kizimbani na kumsikiliza.

Sasa swali la Msingi kwanini, Jemedari aseme Uraia wake kaupata kwa mali nyingi?

Zamani ili uwe Raia wa kirumi ni aidha uwe mzawa (yaani umezaliwa katika Taifa la Rumi) au Umeununua uraia.

Sasa kitendo cha kuununua Uraia hakikuwa rasmi, bali kilikuwa ni kwa njia ya rushwa, na waliopata uraia huo waliupata wakati wa sense, ambapo majina yako yaliongezwa katika orodha ya warumi kinyume cha sheria, baada ya kulipa pesa nyingi,

Na hapa huyu Jemedari aliyeitwa Klaudio Lisia (Matendo 23:26) anaonekana kumwambia Paulo kuwa Uraia wake “Aliununua” maana yake kwa asili hakuwa mrumi, bali alikuwa kuwa mtu wa Taifa lingine, huenda Ugiriki, kwasababu hilo jina la Pili la LISIA ni jina la kigiriki, lakini Paulo yeye alikuwa ni Mrumi kwa kuzaliwa na si kwa kununua uraia.

Upo uraia mwingine ambao ni wa Mbinguni…huo haupatikani kwa fedha, wala mtu haupati kwa rushwa bali bali kwa kuzaliwa mara ya pili.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.”

Je umeupata uraia huu wa mbinguni kwa kuzaliwa mara ya pili?.. kama bado ni nini kinachokusubirisha??

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

USIVAE HERENI

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa PETE MASIKIONI MWAKE, na kwa vito asema Bwana”.

Kabla ya kuvaa kitu, au kuiga mtindo fulani, hebu tenga muda kwanza kufuatilia asili ya kitu hiko kibiblia, kwasababu kuna vitu vingine asili yake ni mbaya, na isiyo na baraka kwa Mungu.

Hebu jiulize swali hili.. Mungu akuumbe na masikio yaliyo kamili, halafu akwambie au akuruhusu ukayatoboe masikio hayo, eti ili tu upendeze?..hivi jambo hilo ni kweli Mungu kaliagiza au kaliruhusu??.. au ni ujanja tu wa akili za watu! (walionyanyuliwa na ibilisi, Waefeso 4:14).

Sasa sikuhukumu wewe uliyetobolewa masikio, huenda si wewe kwa hiari ulifanya hivyo, bali walikutoboa tu ukiwa mchanga..na pia waliokutoboa huenda nao pia walipokea tu kwa waliotangulia, hivyo huenda kosa si lako wala la wazazi, bali la yule wa kwanza kuanzisha makosa hayo..

Lakini sasa baada ya kuelewa, si sawa kuendeleza hayo makosa kwa vizazi vyako, vile vile si sawa kuweka chuma au dhahabu katika matundu ya masikio yaliyotobolewa, kwani kwa kufanya hivyo bado utakuwa unaendeleza desturi hiyo.

Hebu tusome tena…

Hosea 2:13 “Nami nitamwadhibu kwa sababu ya siku za Mabaali, aliowafukizia uvumba; hapo alipojipamba kwa pete masikioni mwake, na kwa vito asema Bwana”.

Asili ya kujipamba kwa pete za masikioni (yaani kuweka hereni) ilikuwa NI KUJIWEKA TAYARI KWA KUVUKIZA UVUMBA KWA MABAALI… na baali si mwingine zaidi ya shetani mwenyewe/kusifa katika kinyago chake kingine.

Kwahiyo zamani mtu akijipamba kwa kutoboa masikio na kuweka hereni alikuwa aidha ametoka kuvukiza uvumba kwa baali au ndio anaenda kuvukiza uvumba kwa baali, na hereni zamani hazikuwa zinavaliwa tu na wanawake, bali hata na wanaume, na lengo lilikuwa ni hilo hilo kumvukizia uvumba baali.

Labda utauliza ni wapi tena pengine panapoonyesha hereni, zinahusishwa na ibada za miungu..

Mwanzo 35:2 “Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake, na wote waliokuwa pamoja naye, ONDOENI MIUNGU MIGENI ILIYOKO KWENU, mjisafishe mkabadili nguo zenu. .

4 NAO WAKAMPA YAKOBO MIUNGU MIGENI YOTE ILIYOKUWA MIKONONI MWAO, NA PETE ZILIZOKUWA MASIKIONI MWAO, naye Yakobo akazificha chini ya mwaloni ulioko Shekemu”.

Sasa shetani ni yule yule, na ibada zake ni zile zile, hazijabadilika……kama bado yupo kwenye makafara ya mang’ombe mpaka leo, na mambuzi, na bado waganga wake ni wale wale, na mavazi yao ni yale yale, na uchawi wake ni ule ule, unadhani uchawi wake katika HERENI (pete za masikioni) utakuwa umebadilika??.. Jibu ni la! Utakuwa ni ule ule tu.

Tafakari, tafakari mama, tafakari dada, tafakari kaka unayevaa hereni, kuambiwa usivae hereni sio kwamba unawekwa chini ya sheria, hapana!.. bali kinyume chake ndio UNAKUWA HURU… Lakini kuvaa hereni ndio sheria, kwani itakulazimu kila siku kuivaa kabla ya kutoka nje, na kubadilisha aina ya hereni leo hii kesho ile, sasa huoni kama hiyo ndio SHERIA???, na kutokuvaa hereni ndio uhuru??.

Ni kweli ukiacha kuzivaa utaonekana si mrembo kwa baadhi ya watu, lakini utakuwa umejiepusha na ibada za sanamu, ambazo zitakuzalia madhara mengine makubwa kiroho.

Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, sawasawa na 1Wakorintho 3:16, na 1Wakorintho 6:19.

Kwa jinsi tunavyozidi kuiweka kuwa mitakatifu, ndivyo Roho Mtakatifu anavyokaa ndani yetu, na ndivyo tunavyomfaidi Roho Mtakatifu kwa matunda yake yaliyotajwa katika Wagalatia 5:22.

Bwana akubariki sana.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

                          Rudi Nyumbani.

Print this post

Kwanini Mungu auweke Mti wa Mema na Mabaya katikati ya bustani?

Swali: Kulikuwa na sababu gani ya Bwana MUNGU kuuweka mti wa mema na mabaya katikati ya bustani ili hali anajua kuwa mti huo ndio utakaowakosesha Adamu na Hawa, kwanini Mungu asingeondoa, na kuubakisha tu ule mmoja wa uzima katikati ya bustani?


Jibu: Ni kweli inaweza kuonekana ni busara mti mmoja tu kuwepo pale bustanini lakini ukweli ni kwamba endapo Mti mmoja tu ungekuwepo pale bado MTI WA UZIMA, usingeeleweka na wala maana yake isingekuwepo..

Kwani ili kuuthibitisha wema lazima uwepo ubaya mahali fulani… kwasababu wema hauwezi kujilikana kama ubaya haujadhihirishwa, vinginevyo ule wema utaonekana ni kitu cha kawaida, lakini ukifunuliwa ubaya ndipo wema unapopata kujulikana na kueleweka.

Nuru haiwezi kujulikana kama ni njema na kitu kizuri, kama giza halipo.. lakini ili Nuru ipate sifa, na kuheshimika ni lazima giza liwepo mahali ili nuru ilishinde giza.

Vile vile Mungu aliuweka ule mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambao matunda yake ni MAUTI, ili kuuthibitsha MTI WA UZIMA ambao matunda yake ni UZIMA.

Adamu na Hawa wasingeweza kuelewa nini maana ya UZIMA kama kisingekuwepo kingine kinachoelezea/kuhubiri MAUTI, vile vile hata sisi leo tusingejua Uzima ni nini kama MAUTI isingekuwepo, vile vile hatuwezi kujua Amani ni nini, kama hatujawahi kusikia kuhusu vita, au kupitia vita..

Hatuwezi kujua umaskini ni nini kama hatujawahi kuona utajiri, vile vile hatuwezi kujua utajiri ni nini kama hatuwahi kuona au kupitia umasikini,.. hatuwezi kujua kuwa tuna afya kama hatujawahi kuona wagonjwa, wala hatuwezi kujijua kuwa tuna ugonjwa kama hatujawahi kuona wenye afya, au sisi wenyewe kuwa na afya, huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakipo, wala huwezi kujua hiki ni kirefu kama kifupi hakijawekwa mahali kama mfano.

Hivyo utaona kuwa uwepo wa vibaya au vyenye kasoro ni ili kuvithibithisha vile vilivyo vizuri na visivyo na kasoro.. Na lengo la Mungu kuuweka mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya lilikuwa ni kuwapa kuelewa Adamu na Hawa Uzima ni nini, na thamani yake, na ili wauthamini na kuushika… na wala lengo lake si kuwatega!.

Hebu pia tengeneza picha miili yetu isingekuwa na maumivu, je unadhani ni nini kingetokea?…bila shaka hakuna mtu ambaye angehangaika kuutunza… hakuna mtu angeogopa kujikata na kisu, au kutembea peku kwenye miiba, au kunywa maji ya moto yale yanayotokota… lakini maumivu yamewekwa ili tujue na kutamani kuwa katika hali ya kutokuwa na maumivu na vile vile kuitunza miili yetu na kuushikilia uzima vizuri .

Hali kadhalika uwepo wa mti ule wa ujuzi wa mema na mabaya ni ili kuuthaminisha mti wa UZIMA. Ili mtu ajue umuhimu wa UZIMA, na RAHA ya Uzima, faida za uzima.

Je wewe umempokea YESU, na kuoshwa dhambi zako? Kumbuka YESU ndiye njia ya Mti wa UZIMA, na yeyote anayempokea humpa matunda hayo na kuishi milele, ndani yake.

Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.

Ufunuo 2:7 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu”

Bwana akubariki.

Kujua kwanini BWANA MUNGU awazuie wasile matunda ya Mti wa Uzima baada ya kula ya ujuzi wa mema na mabaya fungua hapa >>>

Kwanini Bwana MUNGU aliwazuia Adamu na Hawa wasile matunda ya Mti wa uzima waishi milele?

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

YESU MNAZARETI,  ANWANI YA MSALABA.

Je unaijua anwani ya msalaba?…na je unajua nguvu yake? Kama bado hujaifahamu basi leo ifahamu na anza kuitumia katika maombi yako, badala ya vitendea kazi vingine kama maji, chumvi na mafuta.

Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.

20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani”

Jina la YESU WA NAZARETI ndio ANWANI ya maombi ya kila Mkristo.

Umewahi kujiuliza kwanini haijaandikwa YESU MGALILAYA, au YESU MBETHLEHEMU mji ule aliozaliwa, badala yake imeandikwa YESU MNAZARETI?..na tena kwa lugha zote tatu (3), zilizokuu za dunia.

Kuna nini katika Nazareti?

Nazareti ndio mji uliotabiriwa na manabii kubeba utambulisho wa Masihi Mkuu ajaye… hivyo huo ni mji wa UTAMBULISHO KIBIBLIA.

Mathayo 2:23 “akaenda, akakaa katika mji ulioitwa Nazareti; ili litimie neno lililonenwa na manabii, Ataitwa Mnazorayo”.

Kwahiyo tunapotaja jina la YESU na kuelekeza yule wa NAZARETI tumelenga kwenye shabaha yenyewe hivyo mashetani yanaondoka, magonjwa yanaondoka, dhambi inaisha nguvu, kwasababu ndiye Masihi halisi aliyetajwa.

Hebu tulione hili zaidi…

Wakati Bwana YESU anamtokea Sauli alipokuwa anaenda Dameski kwa ajili ya kuwaua wakristo, utaona hakujitambulisha kama YESU wa Galilaya, au YESU aliye mbinguni, badala yake alijitambulisha kama YESU Mnazaeti ijapokuwa yupo mbinguni.

Matendo 22:6 “Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.

7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?

8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, MIMI NI YESU MNAZARETI, ambaye wewe unaniudhi”.

Utaona pia Mitume wa Bwana YESU waliitumia hii anwani popote walipokwenda katika huduma zao.

Petro aliitumia alipokutana na yule kiwete aliyezaliwa katika hali ile..

Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.

7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.

8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.

9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu”.

Soma pia Matendo 2:22, Matendo 3:6, Matendo 4:10, Matendo 10:38, Matendo 26:9, Marko 1:24, Marko 16:6, Marko 10:47, Luka 24:9, Yohana 1:45, utazidi kuona jambo hilo.

Na hiyo pia ndio sababu Mungu aliruhusu Pilato aandike anwani ile juu ya msalaba… “YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI”. Kwa lugha zote kuu, ikimaanisha kuwa anwani ya wokovu wa msalaba kwa mataifa yote na lugha zote ni jina la YESU WA NAZARETI.

Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

Maana yake njili inayohubiri msalaba pasipo kuhusisha anwani ya jina la YESU ni uchawi, maombi yoyote yasiyohusisha anwani ya jina la YESU ni unashiri na ibada za sanamu.

Kama anwani hiyo ya jina la YESU WA NAZARETI hata baada ya Bwana kupaa bado anaitumia akiwa mbinguni, sisi ni akina nani tuifanye iieshe matumizi katika zama zetu?, na kuweka mafuta, chumvi, maji au majina yetu kama mbadala??.

Tumia jina la YESU, liamini jina la YESU WA NAZARETI epuka matapeli, na jina la YESU HALIUZWI, EPUKA MATAPELI!.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post

Biblia inaposema ndugu wa kunyonya inamaanisha nini (Matendo 13:1)?

Swali: Katika kitabu cha Matendo 13:1, tunamsoma mtu mmoja akitajwa kama ndugu wa kunyonya wa Herode, je maana yake nini?.


Jibu: Maana ya “Ndugu wa kunyonya” ni “mtu aliyelelewa katika familia fulani, tangu utotoni, alipokuwa akinyonya” kwa lugha nyingine amekuwa “adopted” tangu utotoni, (katika umri wa kunyonya).

Hivyo mtu kama huyu anahesabika kuwa kama mwanafamilia, na watoto wa familia hiyo watamhesabu kama ndugu yao wa kunyonya, kwani amekulia katika familia yao.

Hivyo huyu Manaeni alilelewa pamoja na Mfalme Herode, katika familia moja, ingawa hawakuwa ndugu wa damu, lakini tangu utoto walikuwa pamoja.

Matendo 13:1 “Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na MANAENI ALIYEKUWA NDUGU WA KUNYONYA WA MFALME HERODE, na Sauli”.

Lakini kulikuwa na kusudi kwanini habari zake ziandikwe katika biblia, ukizingatia ya kuwa ndugu yake, ambaye alikuwa ni Herode pamoja na maherode wote walikuwa ni wakatili sana, waliwaua wakristo na kuwapiga vita vikali, lakini huyu Manaeni ambaye ni ndugu ya Herode, yeye alikuwa wa tofauti, kwani alikuwa ni miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kugeuka na kuifuata Imani ya Kikristo, na kuwa miongoni mwa wasimamizi wa Imani katika kanisa la kwanza la watu wa mataifa, huko Antiokia.

Na kumbuka Antiokia ndiko jina la Ukristo lilikozaliwa, kwani hapo kabla waliomfuata YESU walikuwa wanaitwa wanafunzi tu.

Matendo 11: 26 “hata alipokwisha kumwona akamleta Antiokia. Ikawa kwa muda wa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi waliitwa Wakristo kwanza hapo Antiokia”

Sasa kufahamu kwa urefu ushuhuda alilolibeba Mtumishi huyu wa Mungu (Manaeni) na ujumbe tuupatao watu wa sasa katika Kanisa, fuatilia somo linalofuata…

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Rudi Nyumbani

Print this post