ORODHA YA WAANDISHI WA BIBLIA.

ORODHA YA WAANDISHI WA BIBLIA.

Biblia kitabu kikamilifu, na kitakatifu kimeandikwa na waandishi Zaidi ya 40 kwa Uvuvio wa Roho Mtakatifu. Ndani ya biblia kuna taarifa zinazohusu maisha ya watu zilizobeba sauti ya Mungu nyuma yake, pia kuna taarifa za Mataifa mbalimbali pia zenye kubeba sauti ya Mungu nyuma yake, lakini Zaidi sana kuna Nabii za wakati ujao.

Ifuatayo ni orodha ya waandishi 40 wa Biblia kuanzia Agano la kale hadi Agano jipya.

Agano la kale.

  1. Amosi – Mwandishi wa kitabu cha Amosi
  2. Danieli – Mwandishi wa kitabu cha Danieli.
  3. Daudi- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi, kwa baadhi ya Zaburi.
  4. Ezekieli- Mwandishi wa kitabu cha Ezekieli.
  5. Ezra- Mwandishi wa kitabu cha Ezra.
  6. Habakuki – Mwandishi wa kitabu cha Habakuki.
  7. Hagai – Mwandishi wa kitabu cha Hagai.
  8. Hosea- Mwandishi wa kitabu cha Hosea.
  9. Isaya- Mwandishi wa kitabu cha Isaya.
  10. Yeremia – Mwandishi wa kitabu cha Yeremia
  11. Yoeli – Mwandishi wa kitabu cha Yoeli
  12. Yona- Mwandishi wa kitabu cha Yona.
  13. Yoshua- Mwandishi wa kitabu cha Yoshua.
  14. Malaki- Mwandishi wa kitabu cha Malaki.
  15. Mika- Mwandishi wa kitabu cha Mika.
  16. – Mwandishi wa kitabu cha Esta.
  17. Musa – Mwandishi wa kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Kumbukumbu la Torati, Hesabu, Ayubu na Zaburi 90.
  18. Nathani (Nabii) – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  19. Nabii Gadi- – Mwandishi wa kitabu cha 1Samweli na 2Samweli (sehemu baadhi)
  20. Nahumu- Mwandishi wa kitabu cha Nahumu.
  21. Nehemia- Mwandishi wa kitabu cha Nehemia.
  22. Obadia- Mwandishi wa kitabu cha Obadia.
  23. Samweli- Mwandishi wa kitabu cha Samweli (Sehemu baadhi)
  24. Sulemani- Mwandishi wa kitabu cha Mithali, Mhubiri na Wimbo ulio bora.
  25. Sefania -Mwandishi wa kitabu cha Sefania.
  26. Zekaria-Mwandishi wa kitabu cha Zekaria.
  27. Wana wa Kora-Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 42, Zaburi 44-49, Zaburi 84-85, na Zaburi 87-88.
  28. Asafu- Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 50, na Zaburi 73-83.
  29. Ethani – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  30. Heman – Mwandishi wa kitabu cha Zaburi 89 (sehemu).
  31. Aguri – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 30.
  32. Lemueli – Mwandishi wa kitabu cha Mithali 31.

Agano Jipya.

  1. Mathayo – Mwandishi wa kitabu cha Mathayo.
  2. Marko – Mwandishi wa kitabu cha Marko.
  3. Luka – Mwandishi wa kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume.
  4. Yohana – Mwandishi wa kitabu cha Yohana Mtakatifu na 1 na 2Yohana pamoja na Ufunuo.
  5. Yakobo – Mwandishi wa kitabu cha Yakobo.
  6. Yuda – Mwandishi wa kitabu cha Yuda.
  7. Paulo- Mwandishi wa kitabu cha Warumi, 1 na 2Wakorintho, Wagalatia, Waefeso, Wakolosai, Wafilipi, 1 na 2Wathesalonike, 1na 2Timotheo, Tito na Filemoni.
  8. Petro – Mwandishi wa kitabu cha 1 na 2Petro.

Kwanini waandishi wapo Zaidi ya 40 na si 40 kamili?.. Ni kwasababu biblia pia imewataja wana wa Kora, ambao hatujui walikuwa ni wangapi, zaidi sana yupo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, ambaye hajatajwa ni nani, huenda akawa ni Mtume Paulo, lakini kama si yeye bali ni mwingine, basi ataongezeka katika idadi ya walioiandika biblia.

Kumbuka tena, biblia ni kitabu cha Mungu kilichoandikwa na WATU, kwa uvuvio wa ROHO MTAKATIFU, Hivyo maneno yaliyoandikwa ndani ya Biblia, yana uzima.

2Timotheo 3:16  “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema”.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KALAMU YENYE UONGO YA WAANDISHI IMEIFANYA KUWA UONGO.

Mwandishi wa kitabu cha Matendo ya mitume.

Je ni Mungu au Malaika?

Mwandishi wa kitabu cha Mithali ni nani?

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Rudi Nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest

0 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments