Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?

Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?

Swali 1: Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?..Roho inaweza kuelewa, kutambua, kuona bila ubongo?.. Swali 2: Adamu na Hawa walimwona Mungu?.. Swali 3: Na je! Mungu anazidi kujificha kwetu au kujidhihirisha kadiri muda unavyozidi kwenda?.


Swali 1: Mungu anaweza kuongea wakati yeye ni Roho?..

Jibu: Kabla ya kwenda kwa Mungu, tuanze kwanza kwa mtu.  Mtu anapozungumza, kuzungumza kwake kunaanzia rohoni..katika roho yake ndio anazungumza..Mwili ni kama kipazia sauti cha roho katika mazingira ya kidunia… Ili kuelewa vizuri tafakari mfano ufuatao.

Umechukua simu yako na ukampigia ndugu yako (video-call) ambaye yupo mkoa mwingine au nchi nyingine..mkawa mnazungumza huku mnaonana kabisa kupitia simu…ukawa unamwona yule ndugu yako kupitia simu ile na kuisikia sauti yake…Sasa yule ndugu yako aliyeko mkoa mwingine, je anaweza kusema pasipo simu wewe huwezi kuzungumza naye?..Jibu ni hapana…unaweza kuzungumza naye hata pasipo simu, endapo akisafiri akakufuata mahali ulipo au ukimfuata mahali alipo bado mnaweza kuzungumza tu tena vizuri sana Zaidi hata ya kutumia simu…

Sasa simu ni kiunganishi tu, ambacho ili kiweze kutuunganisha na watu walioko mbali nasi kinahitaji kiwe na chaji, kiwe na betri, kiwe na network, kiwe na spika, na kiwe na jicho la kamera ili kiweze kumrekodi yule aliyeko mbali.

Na miili yetu ndio hivyo hivyo, ni kama simu tu! Ili iweze kuziunganisha roho zetu na mazingira ya kimwili Inahitaji ubongo, inahitaji moyo unaosukuma damu, inahitaji, macho mawili kurekodi matukio ya nje na kuyatuma katika roho zetu, inahitaji pua kuchukua taarifa za mwili kuzipeleka rohoni, n.k

 Lakini pia pasipo hii miili tunaweza kuongea, kutazama, kuzungumza tena vizuri sana pasipo hata kuwa na miili.. Kama vile ilivyomubashara Zaidi mtu kuzungumza uso kwa uso na mwenzake Zaidi kuliko kuzungumza naye kwenye simu. Tukitoka katika huu mwili bado tunauwezo wa kuona, kusikia, kuzungumza n.k Mwili si kitu cha lazima sana kama vile simu isivyokuwa ya lazima.

Kwahiyo mwili ni njia tu, lakini mambo yote yanaanzia katika utu wa ndani. Na kama sisi tupo hivyo basi Mungu uwezo wake ni mkubwa Zaidi na mpana sana..upeo wake ni mkuu Zaidi ya huo na anaweza kufanya zaidi ya hayo. Ndio maana utaona mara kadhaa sauti ilisikika kutoka mbinguni ikisema huyu ni mwanangu mpendwa wangu.

Swali 2: Adamu na Hawa walimwona Mungu?

Jibu: Biblia haijasema moja kwa moja walikuwa wanamwona kwa namna gani, lakini kulingana na habari ile ni wazi kuwa walikuwa wanamwona kabisa wazi.

Swali 3: Kadiri muda unavyozidi kwenda, Mungu anazidi kujificha kwetu au kujidhihirisha?

Jibu: Mungu yupo karibu na sisi siku zote…hana wakati ambao alishawahi kuwa karibu nasi sana kuliko wakati mwingine wowote, wala hana wana wakati ambao alijitenga nasi. kamwe yeye yupo pale pale.  Kinachotufanya sisi tumwona yupo mbali nasi au karibu nasi ni kiwango cha maovu yetu na utakatifu wetu.

Isaya 59: 1 “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”.

Yakobo 4: 8  “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.

Anatushauri haya..

Kumbukumbu 30: 11 “Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.

  12 Si mbinguni, hata useme, Ni nani atakayetupandia mbinguni akatuletee, aje atuambie tusikie, tupate kuyafanya?

  13 Wala si ng’ambo ya pili ya bahari, hata useme, Ni nani atakayetuvukia bahari, akatuletee, aje atuambie, tusikie, tupate kuyafanya?

 14 Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya.

15 Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya”

Ubarikiwe.

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

WEWE SI MALI YAKO MWENYEWE!

HISTORIA YA ISRAELI.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

ALIJARIBIWA SAWASAWA NA SISI KATIKA MAMBO YOTE.

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

JINSI YA KUJIWEKA KARIBU NA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments