MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

Mwisho wa dunia utakuwaje?

Mwisho wa dunia maana yake ni hatua ambayo ustaarabu wa dunia utaifkia mwisho…Na mwisho wa dunia utahitimishwa na tukio moja kuu la vita vya HARMAGEDONI. Vita hivyo vitamaliza ustaarabu wote wa wanadamu…zitakuwepo vita ndogo ndogo zitakazotangulia, lakini vita hii kubwa ya mwisho ujulikanayo kama Harmagedon ndiyo itakayomaliza ustaarabu wote wa wanadamu.

Vita hii Biblia inaitaja kuwa ni vita kati ya Mungu mwenyezi na Wafalme wa Dunia..

Ufunuo 16:14  “Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)

16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni”

Vita hiyo Mwanakondoo yaani Yesu Kristo ataimaliza ndani ya muda mfupi sana kwa ushindi mnono..kwasababu  yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme.

Siku hiyo pia kutakuwa na tetemeko kubwa la nchi ambalo mfano wake haujawahi kutokea na visiwa vitahama na ustaarabu wa dunia ndio utakuwa umefikia mwisho.

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?

Biblia inasema wasemapo amani! amani! ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla

1Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”

Kwahivyo tunaonywa tusidanganyike na amani hii ya dunia inayodanganya…Amani ya kweli ipo kwa Yesu tu!..nchi inaweza kutangaza kuwa tupo katika kipindi cha amani lakini kumbe ndio tupo mwishoni kabisa mwa nyakati.

Mkabidhi Yesu maisha yako kama hujafanya hivyo, kwasababu yeye ndiye njia ya kufika mbinguni na kuepukana na ghadhabu ya Mungu inayokaribia kumwangwa duniani kote katika siku hizi za mwisho, zinazoonekana zenye amani tele.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USINIPITE MWOKOZI

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?

NINI MAANA YA KUSAGA MENO?

NINI MAANA YA KUKUA KIROHO

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
acrey
acrey
6 days ago

nahitaji kujifunza zaidi kwa email na whatsapp acreymathias01@gmail.com

acrey
acrey
6 days ago
Reply to  acrey

0783658080 whatsapp