UTOE MWILI WAKO KWA BWANA KWASABABU SI MALI YAKO.

UTOE MWILI WAKO KWA BWANA KWASABABU SI MALI YAKO.

Jambo linalotupa wengi kiburi ni kufikiri kwamba miili hii tuliyonayo ni mali yetu wenyewe..Lakini kama mtu ukitenga muda na kutafakari kwa kina utakuja kugundua kuwa mwili ulionao hauna mamlaka nao asilimia mia, na hivyo huo ni uthibitisho kwamba si mali yako kabisa..

Kama mwili ungekuwa ni mali yako ungekuwa na uwezo wa kujichagulia kimo, au rangi au jinsia…ungekuwa pia na uwezo wa kuyazuia mapigo ya moyo yasidunde pindi unapotaka, au ungekuwa na uwezo wa kuzuia damu isizunguke mwilini au mwili usitoe jasho wakati wa joto linapozidi kuwa kali. Lakini kama mojawapo ya mambo hayo huwezi basi ni uthibitisho kwamba huo mwili ni mali ya mtu mwingine ambaye wewe humjui. Kwa ujumla sio milki yako binafsi…Kama biblia inavyosema..

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE”

Kwasababu hiyo basi ndio maana ni lazima tuishi chini ya amri za mwenye miili hii…akisema miili hii haipaswi kufanywa kituo cha dhambi..basi tunatii kwasababu sio mali yetu..akisema hatupaswi kuitumia kwa zinaa, au ulevi, au uasherati basi ni lazima tutii kwasababu sio ya kwetu ni yake yeye. Sisi ni wageni waalikwa au wapangaji tu ndani ya hii miili yake..Hatuna uhuru asilimia 100 wa kuiweka tunavyotaka sisi. Akisema hatupaswi kuivisha mavazi yapasayo jinsia nyingine, hatupaswi kuhoji kwanini au kwasababu gani.

Sasa hebu tujifunze Zaidi juu Mmiliki wa hii miili tuliyonayo.

Kuna wakati Bwana wetu Yesu aliulizwa swali lifuatalo na Mafarisayo…

Mathayo 22:17 “Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?

18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?

19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.

20 Akawaambia, NI YA NANI SANAMU HII, NA ANWANI HII?

21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, NA MUNGU YALIYO YA MUNGU”

Ukisoma mstari huo wa 20 utaona Bwana anawauliza maswali mawili..1).Ni ya nani sanamu hii? Maana yake ile sura juu ya ile sarafu ni sura ya nani?…2).Na ni ya nani anwani hii?. Na wote wakajibu ni ya Kaisari..na yeye Bwana akawaambia vya Kaisari mpeni Kaisari na vya Mungu mpeni Mungu..

Sasa swali linakuja, vya Mungu ni vipi hapo?…Ndio vinaweza kuwa navyo pia ni fedha, (kama sadaka, zaka au malimbuko)..lakini hebu leo tuingie ndani Zaidi kujifunza vilivyo vya Mungu ni vipi.

Turudi kusoma kitabu cha Mwanzo..

Mwanzo 1: 26 “Mungu akasema, Na tumfanye MTU KWA MFANO WETU, KWA SURA YETU; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Mpaka hapo utakuwa umeona vya Mungu ni vipi?…Miili yetu ndio vya Mungu tunavyopaswa tumpe..kwasababu miili yetu ndio imebeba SURA na MFANO wa Mungu…Kwahiyo kama Bwana alivyowaambia watu wampe kodi Kaisari kwasababu tu sarafu ile imebeba sura yake na anwani yake..zaidi sana tunapaswa tumpe Kristo miili yetu kwasababu imebeba sura na mfano wa Mungu..

Kwahiyo tunapaswa tujipime kila siku je hii miili yetu tunaiweka jinsi Mungu anavyotaka?…Je tunaiweka katika utakatifu, je tunaishughulisha katika kufunga na kuomba na kuifikisha kwenye nyumba za Ibada?..Kama hufanyi hivyo, kila ukifika muda wa kuomba unasema umechoka!..ukifika muda wa kufunga unasema unaumwa, ikifika siku ya kwenda kwenye ibada unasema unapumzika…Kumbuka utatoa hesabu siku ile kwa mwenye huo mwili.

Kama unautumia mwili huo kuufanyia uzinzi, au uasherati…jitafakari sana, kama unafikiri ni mali yako hiyo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri una uhuru wa kuitembeza bila mavazi au kuichubua, au kuiweka kila aina ya matangazo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri ni ya kupokea mimba na kutoa tu jinsi utakavyo hilo nalo lifikirie…

Bwana atusaidie daima..

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”,(Mwanzo 1:26)?

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

CHAPA YA MNYAMA

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.

Kwanini kabila la Dani limeondolewa kwenye Ufunuo 7?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Patrick kahinga lumande - Elie
Patrick kahinga lumande - Elie
8 months ago

Nami salimu sana
Nafurai kabisa juu ya mafundisho mina penda nyanze kuyapokeya
Aksanti.
Mungu amibariki