Yeremia alikuwa ni nabii aliyezaliwa Israeli (Kwa asili alikuwa ni Myahudi)..na alitokea nyakati za mwisho mwisho kabisa, karibia na wakati wa Israeli kuchukuliwa mateka Babeli. Ni nabii aliyetabiri na kushuhudia kuteketezwa kwa mji wa Yerusalemu na watu kuchinjwa na baadhi kuchukuliwa mateka. Tafsiri ya jina lake ni “Yehova atapandisha au atanyanyua” .Unaweza kutazama tafsiri za baadhi ya majina hapa >>>Maana ya majina na tafsiri zake
Kama jina lake lilivyo, Yeremia alitabiri Israeli kunyanyuliwa tena na Mungu baada ya kushushwa chini..alisema..Bwana atawarudia tena watu wake baada ya kukaa ugenini miaka 70.
Yeremia 25:11 “Na nchi hii yote pia itakuwa ukiwa, na kitu cha kushangaza; nayo mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli miaka sabini. 12 Na itakuwa miaka hiyo sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na taifa lile, asema Bwana, kwa sababu ya uovu wao, nayo nchi ya Wakaldayo pia; nami nitaifanya kuwa ukiwa wa milele”.
Yeremia 25:11 “Na nchi hii yote pia itakuwa ukiwa, na kitu cha kushangaza; nayo mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli miaka sabini.
12 Na itakuwa miaka hiyo sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na taifa lile, asema Bwana, kwa sababu ya uovu wao, nayo nchi ya Wakaldayo pia; nami nitaifanya kuwa ukiwa wa milele”.
Yeremia tofauti na manabii wengine, yeye aliitwa na Mungu katika utumishi akiwa na umri mdogo na ni moja ya manabii waliopitia mateso mengi sana katika huduma zao, lakini Mungu hawaacha!..na Mungu alimtuma kwa mataifa mbali mbali…Manabii wengine wa Israeli kama Samweli, Ezekieli,Musa, Malaki na wengineo hawakutumwa kwa watu wa Mataifa, isipokuwa kwa watu wa jamii yao tu (yaani kwa wasraeli wenzao!). Yeremia na wengine wachache ndio pekee waliotumwa watoke nje ya mipaka ya Israeli kusema na watu wa Mataifa ya mbali.
Yeremia 1:4 “Neno la Bwana lilinijia, kusema, 5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. 6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto. 7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. ”
Yeremia 1:4 “Neno la Bwana lilinijia, kusema,
5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.
7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. ”
Mungu alimtuma Yeremia kwa mataifa mengi ulimwenguni, kuyatangazia hukumu…kwamba yote yatawekwa chini ya utawala mgumu wa Nebukadneza kama yasipotubu na kuacha njia zao mbaya…na mataifa hayo yote hayakuisikiliza sauti ya Yeremia nabii na yote kuishia kuwekwa chini ya mikono ya Nebukadneza (kasome Yeremia 25:15-28) ikianza na Yuda. (Na Yeremia aliifanya kazi hiyo ya Mungu kwa uaminifu mpaka alipokuwa mzee.)
Kwa maelezo ya urefu kuhusu Nabii huyu, vitabu alivyoandika, na huduma yake ilivyokuwa kwa mapana fungua hapa >> Vitabu vya Biblia (sehemu ya 7)
Wito wa Mungu hauna mipaka, Mungu anaweza kukuita na kukutuma katika umri mdogo kama Yeremia, na vile vile anaweza kukuita na kukutumia katika umri mkubwa, kama Elisha. Kwa wito wowote ule tutakaoitwa na Mungu, tunapaswa tuwe waaminifu.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4
MAOMBI YA TOBA.
Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?
PARAPANDA ITALIA.
Rudi Nyumbani:
Print this post