Baraka za Mungu.

Baraka za Mungu.

Baraka za Mungu zinakujaje?


Ni vizuri kufahamu kuwa mafanikio sio Baraka, lakini Baraka zinaweza kupelekea mafanikio.

Unaweza ukawa ni tajiri na ukafanikiwa na mali zako zikawa ni nyingi sana, lakini ukawa bado hujabarikiwa na Mungu. Kwasababu mafanikio hata shetani naye anayatoa.

Hilo utalithibitisha katika kitabu cha Mathayo, siku ile ambayo shetani alipotaka kumtajirisha  Yesu kwa mapatano ya kumsujudia..Soma

Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,

9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia”.

Unaona, utajiri, na mali hatoi tu Mungu peke yake kama wengi wanavyodhani, bali shetani pia anatoa  tena anatoa kweli kweli, Lakini Baraka huwa Baraka huwa zinatoka kwa Mungu tu peke yake.

Tukilijua hilo sasa turudi, ili kujifunza Baraka za Mungu ni zipi.

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

14 ili kwamba BARAKA YA IBRAHIMU iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, TUPATE KUPOKEA AHADI YA ROHO kwa njia ya imani”.

Unaona, hapo Baraka ambayo Mungu aliiachia kwanza kwa Ibrahimu tunamjua kuwa alibarikiwa na Mungu, iliachiliwa hata na kwetu sisi kwa njia Yesu Kristo, Na Baraka yenyewe tuliyoipokea ni Roho Mtakatifu.

Leo hii hakuna Baraka kubwa kutoka kwa Mungu zaidi ya Roho Mtakatifu kuwa ndani ya mtu. Ukimkosa Roho Mtakatifu, wewe ni mlaaniwa. Lakini ukimpata Roho Mtakatifu basi umepata vitu vyote. Na mafanikio juu.

Huwezi kumpendeza Mungu kama huna Roho Mtakatifu yeye mwenyewe alisema..

Warumi 8:9 “……..Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Sasa Roho Mtakatifu tunampataje?

Tunampata kwanza kwa kutubu dhambi zetu  kwa kumaanisha, kisha tunakwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamwishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, ili tupate ondoleo la dhambi zetu, na baada ya hapo sasa Mungu atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ndani yetu. Sawasawa na Matendo 2:38

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Sasa ukishakuwa na uhakika kuwa umeyafuata hayo maagizo yote kwa bidii, na umemaanisha kweli kutubu dhambi zako, na sio nusu nusu, yaani mguu mmoja nje, mwingine ndani, basi wakati huo huo Roho wa Mungu atashushwa ndani yako..(Wengi wanadhani Roho Mtakatifu ni mpaka unene kwa Lugha, hapana yeye ni zaidi ya hapo, kunena kwa lugha ni moja ya njia zake, lakini unapotubu na kubatizwa wakati huo huo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako.) .

Na baada ya hapo sasa ndipo na mafanikio mengine yote yataambatana nawe kwa wakati wake, kwa kuwa umeyashika maagizo yake kwa bidii. Sawasawa na Kumbukumbu la Torati 28

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. 7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.

9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.

10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.

11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.

12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.

13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;”

Hivyo Baraka ya Mungu ni Roho Mtakatifu.Ukimpata huyo basi umepata kila kitu.

Lakini usidanganyike na kumwona kila mtu mwenye mafanikio na huku yupo mbali na Mungu ukadhani amebarikiwa…Huyo ni mlaaniwa tu mbele za macho ya Mungu.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

USIFIKIRI FIKIRI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments