Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?

Je! Watoto wa Ibrahimu/Wana wa Ibrahimu walikuwa ni wangapi?


Jumla ya wana wa Ibrahimu walikuwa ni nane (8). Kulingana na Biblia.

Mwana wa kwanza alikuwa ni Ishmaeli, ambaye alizaliwa na kijazi wa mke wake Sara aliyeitwa Hajiri (Mwanzo 16:1-4).

Mwana wa Pili, alikuwa ni Isaka,(Ndiye mwana wa Ahadi) ambaye alizaliwa miaka 14 baada ya Ishmaeli kuzaliwa.

Mwanzo 21:1 “Bwana akamjia Sara kama alivyonena, na Bwana akamfanyia kama alivyosema.

2 Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. 3 Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia”.

Sara alipofariki, Ibrahimu akaoa mke mwingine, aliyeitwa Ketura. (Mwanzo 25:1-2)

Huyu Ketura ndiye aliyemzaliwa Ibrahimu wana wengine 6. Kufanya jumla ya watoto wote wa Ibrahimu kuwa 8, Biblia haielezi kuwa alikuwa na wana wengine wa kike.

Lakini katika wana hao wote, ni mmoja tu, aliyekuwa mrithi wa Ibrahimu, naye ni Isaka. Na siri moja ni kuwa wale wana wengine Ibrahimu aliwapa zawadi nyingi, lakini Isaka alipewa vyote, zawadi pamoja na urithi, kwasababu yeye ndiye aliyekuwa mwana wa Ahadi kutoka kwa Mungu.

Mwanzo 25:5 “Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo.

6 Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu”.

Vivyo hivyo na sisi, tunaweza sote tukawa ni watu wa Mungu, tulioumbwa na Mungu, lakini si sote tukawa wana wa ahadi wa Mungu mfano wa Isaka. Wana wa ahadi ni wale waliozaliwa mara ya pili (yaani waliokoka). Na hao ndio Mungu kawaandalia vyote, thawabu pamoja na urithi wa ufalme wa mbinguni.

Ambapo Yesu alikwenda kuwaandalia waliompokea, Na siku atakaporudi, atawagawia urithi huo ambao alikuwa akiwaandalia kwa miaka 2000. Mambo ambayo jicho halijawahi kuoa wala sikio kusikia.

Swali la kujiuliza  Ni je!  na wewe ni mmojawapo wa wana wa Ahadi? Kama hujaokoka na kusimama, bado hujawa mwana wa ahadi, Lakini habari njema ni kuwa nafasi bado ipo lakini haitakuwepo siku zote ya wewe kufanyika hivyo.. Kama upo tayari leo hii kufanyika mtoto wa Mungu, na kuachana na dunia, na kutaka Yesu akuokoe, basi uaumuzi huo ni wa busara kwako, unachopaswa kufanya ni kufungua hapa ili upate maelekezo ya sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tazama chini kwa masomo mengine ya rohoni.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp yako mara kwa mara tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WATOTO WA YESE KATIKA BIBLIA.

Wafilisti ni watu gani.

Israeli ipo bara gani?

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
4 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Doreen
Doreen
1 year ago

Mtoto wa ibrahimu wakwanza inaitwa ishimaile

Doreen
Doreen
1 year ago

Bwana yesu asifiwe

Doreen
Doreen
1 year ago

Amen

Modester stanslaus
Modester stanslaus
2 years ago

Ibraim alikuwa na watoto nane