Mathayo 20:6
[6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Bwana Yesu alizungumza mfano ambao unagusia kabisa uhalisia wa kiroho uliopo sasa katika kazi ya Mungu (Ushuhudiaji).
Mfano huo unahusu mtu mmoja aliyetoka asubuhi sana kuajiri wafanyakazi ili kwenda kulilima shamba lake ambalo lilihitaji watu wengi kulihudumia.
Hivyo akatoka alfajiri sana, kuwatafuta na kwa bahati nzuri akawakuta, akawapeleka shambani mwake, akatoka tena saa tatu, akawakuta wengine wamekaa bila kazi, akawatuma shambani, akaenda tena saa sita na saa tisa vivyo hivyo akafanya…Mpaka ilipofika saa kumi na moja akatoka na kuwakuta watu wengine wamesimama tu toka asubuhi mpaka jioni…hawafanyi chochote wapo “Idle”
akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Mathayo 20:1-7
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. [2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. [3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; [4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda. [5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. [6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? [7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
[2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
[3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
[4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
[5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.
[7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
Embu jiulize swali moja.. Je! Unadhani watu hawa wa saa kumi na moja hawapo leo?
Kukaa bila kufanya kazi ya Mungu, wakati Kazi ipo kubwa kwa kisingizio kuwa hakuna wa kukuajiri ni ulegevu kiroho… yule Bwana hakuwa na muda wa kusikiliza sababu zao, kwamba waendelee kukaa na kumalizia tu siku kwasababu muda umeenda, bali aliwatuma haraka sana shambani.
1) Hofu ya kutumika
Kusema mimi siwezi, Mimi bado mchanga kiroho, sijui biblia vizuri, Mimi bado mdogo kiumri, mimi siwezi Kuongea nina aibu, nina kigugumizi..sina fedha, sina elimu n.k…haya ndio mambo yanayowakawiisha watu wengi wasimtumikie Mungu..
Ndugu fahamu kuwa Mungu hategemei ukamilifu wetu, kutimiza kusudi lake kamilifu, bali hututumia katika hali zetu hizi hizi, hivyo usingojee siku fulani utakuwa mzoefu ndio umtumikie Mungu..haitafika, anzia na hali yako hiyo hiyo.(1Wakoritho1:26-29)
2) Kungojea muda fulani sahihi.
Kudhani Kuwa upo muda fulani maalumu utaitwa na Bwana rasmi umtumikie, hilo pia limewafanya wengi, kungoja muda mrefu na hatimaye kutoona mafanikio.. saa ya kutumika ni sasa..tayari Wote tulishaitwa tumtumikie yeye tangu siku tulipookoka..ukishaokoka umepewa na vibali vyote na mamlaka ya kumtumikia Bwana..usingoje utokewe na Yesu kama Paulo Dameski, Usingoje usikie sauti fulani ikikwambia nenda kawafundishe watu. Anza sasa na Bwana ataungana na wewe mbele ya safari.
3) Masumbufu ya maisha
Mizigo mingi ya kimaisha, utakula nini, utavaa nini, utaishije, linawapunguza watu kasi ya kufikiria kwamba wanahitaji kwanza kuyaandaa maisha yao yawe safi ndipo waamke kwenda kumuhubiri Kristo.
Ndicho walichokifanya wayahudi walipokuwa wanajenga hekalu la pili, ilifika wakati wakaacha ujenzi kila mmoja akaenda kwenye mambo yake, Kwasababu tu, ya kujiangalia hali zao.
Hagai 1:2-4
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA. [3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, [4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA.
[3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,
[4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
Usingoje ufanikiwe, uoe, uwe na maisha ndio sasa uanze kuifanya kazi ya Mungu, ukijitazama Sana, hutamtumikia Mungu ndugu.. fahamu kuwa wengi wanaokuletea wewe habari njema sio wenye mafanikio, lakini Bwana hawaachi.
4) Ulegevu.
Kupendelea mambo ya kirahisi rahisi, zaidi ya kujitoa..wakati mwingine kukataa kutaabika kwa ajili ya injili..kutaka ijiendeshe Yenyewe, bila kuwa mfuatiliaji na mwombaji, pia hukawiisha utendaji kazi wa injili.
Hivyo, ndugu muda ni mfupi sana, tupo katika saa la kumi na moja yetu, usihudhurie tu kanisani, kuwa sehemu ya utumishi kanisani, usisikilize / kusoma tu mahubiri, hubiri na kwa wengine unachojifunza, Shamba la Bwana linatuhitaji wote.
Ni wakati wa kuamka usingizini, bado hatujachelewa, ikiwa tutatimiza kusudi la Mungu vema, basi tutalipwa sawasawa tu na wale waliowahi..Hivyo amka sasa.. anza kushuhudia.
Shiriki injili kwa kushea na wengine habari hizi
Bwana akubariki
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Print this post
Siku moja nilikuwa nakatiza eneo fulani la biashara ambalo limechangamka sana, Ni eneo ambalo watu wengi wanapishana..ghafla kwa mbele nikamwona kijana mmoja ameinama, baada ya muda kidogo akachuchumaa, na mara akaanza kutapika matapishi mengi sana.. Uso wake ulionekana kuumwa, hivyo moja kwa moja nilipomwangalia moyoni mwangu, niliguswa sana na ile hali aliyokuwa anapitia..
Kikawaida zipo hali ambazo ukiumwa Unaweza kuzivumilika mpaka ufike mahali fulani pa matibabu..lakini kuumwa mpaka kutapika Hakuzuiliki, na kama ulishawahi kutapika unaelewa nguvu inayotumika, hali unayoisikia wakati huo.. ni kama nusu ya kufa..
Sasa sisi ndivyo tunavyomfanya Mungu, ajisikie muda wote tunapokuwa Na aina ya mwenendo wa uvuguvugu maishani mwetu, .alisema hivi;
Ufunuo wa Yohana 3:15-19
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. [16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. [17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. [18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. [19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
[16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Uvuguvugu ni ile hali ya kuwa mtu wa kidini na sio wa kiroho, unahudhuria ibada lakini mabadiliko huna, unavaa vizuri kanisani lakini ukiwa nje unavaa nguo zisizo na adabu, unaimba kwaya, lakini wakati huo huo unasikiliza nyimbo za kidunia, ni mtumishi mzuri wa kanisani lakini bado unaishi na mume wa mtu..
Maisha ya uvuguvugu, yanamtesa Kristo isivyo kawaida..Ikiwa wewe hupendi kutapika- tapika Kwanini wewe umfanye Mungu kuwa na hali hiyo?
Ukristo ni mwendelezo sio tukio…eti mimi nimeshamkiri Yesu kwa Kinywa..inatosha nimeokoka, hapana…bali ni ukuaji wa kiroho.. ni lazima uonyeshe ukuaji…kitu chochote kilicho hai kinakua…lakini kuwa mtu yule yule kila siku wewe ni vuguvugu.
Kanisa La Laodikia, lilikuwa na sifa ya kujiona ni tajiri Kisa Lina vyombo vizuri vya miziki, lina Makongamano makubwa ya nje, lina mwonekano wa kuvutia, lina umaarufu, Lakini Yesu aliliona si la kiroho hata kidogo..Linamheshimu Mungu kwa nje tu, lakini ndani limepoa zaidi ya barafu..
Hizi ni nyakati ambazo watu wengi wanazisahau ibada za kweli, wanatafuta fedha na Midundo inayovutia masikio ya watu lakini hawajali ujumbe wa rohoni au ‘uzuri Wa utakatifu’.
Na watu ambao wakiwaona wengine wamesimama kikamilifu mbele za Mungu wanawaita “walokole” …
Embu tubu, rafiki…uzuri wako, mwonekano wako, Sifa zako, udunia wako, havina ushirika na Kristo, hizo status zisizo na staha na elimu, unampostia nani mitandaoni? Hiyo mitandao ya kizinzi unayoitembelea kila siku, na kujichua unakoendelea nako kwa siri na wakati huo huo unasema umeokoka, nini unakiunda kama sio kumfanya Bwana atapike?…maanisha kumpokea Kristo. Simama katika imani, ili umwone Mungu wa kweli na sio sanamu.
Kumbuka hizi ni nyakati za kusimama kikamilifu, kwasababu mwisho umekaribia..Unyakuo Ukipita watakaokwenda na Bwana ni walio moto tu, na sio vuguvugu.
Kutubu ni kugeuka…Geuka tu leo kwa kumaanisha na Bwana atakusamehe kabisa na kuanza na wewe..Ikiwa hujaokoka na upo tayari leo kufanya hivyo…Basi wasiliana nasi kwa mwongozo wa sala ya Toba..
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?
Mtambo kwenye biblia ni neno linalomaanisha aidha kifaa kinachonasa kitu, au kinachorahisisha kazi Fulani.
Kwamfano tukisoma
Ayubu 18:9
[9]Tanzi litamshika kisigino chake, Na mtambo utamgwia.
Hapo ni Bildadi rafiki yake Ayubu anaeleza hatma ya mtu mwovu, anasema ni sawa na mtu atembeaye katika njia ya mitego, na ghafla hunaswa asiweze kunasuka ndio mtu mwovu katika njia zake mbaya hukumbwa na hayo.
Anasema mtambo utamgwia, maana yake kitu kinasacho Kitamkamata.
Neno hilo pia utalisoma…kwenye mistari ya juu yake..Bildadi anasema..
Ayubu 18:2
[2]Je! Hata lini utayategea maneno mitambo? Fikiri, kisha baadaye tutanena.
Akitumia lugha ya picha…
akimaanisha hata lini utayanasa maneno yako? (yaani utaacha kuongea?).
Lakini sehemu nyingine Inayolitaja Neno hili Ni..
2 Mambo ya Nyakati 26:14-15
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo. [15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo.
[15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
Inazungumzia nguvu za kijeshi alizokuwa nazo mfalme Uzia, hata kufikia kubuni mitambo mikubwa ya kivita.. ya kufyatulia silaha kwa maadui zake.
Je umeokoka?
Kumbuka saa Tulizopo ni za majeruhi, siku yoyote wakati wowote Kristo anarudi jiulize umejiandaaje ndugu?. Unyakuo wa kanisa ukipita leo utakuwa wapi mpendwa…
Jitathmini maisha yako? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote na mambo yake halafu upate Hasara ya nafsi yako. Tubu mgeukie Kristo uoshwe dhambi zako, upokee uzima wa milele.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo.. basi fungua hapa kwa mwongozo Wa Sala ya Toba.. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
WhatsApp
Haya ni mafundisho maalumu kwa viongozi aidha wachungaji, au wasimamizi ndani ya kanisa..Maadamu una kundi la watu aidha 2-3 au zaidi la kuwasimamia, basi mafunzo haya yatakusaidia sana.
Kutoka 32:9-10
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu [10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
[10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
Mungu alipomuita Musa kwenda kuwaokoa watu wake, alijua asili ya hao watu watakuwa ni wa namna gani. Pengine Musa alidhani anawaokoa watu ambao ni wema sana, watulivu, na wapole.
Lakini mambo hayakuwa kama hivyo, licha ya kuona miujiza mikubwa namna ile, bahari kupasuka, mana kushuka Mbinguni, miamba kutoa maji, nguzo ya moto kuwaongoza usiku kila siku…
Bado walitengeneza sanamu za ndama na kusema hii ndio miungu yetu iliyotutoa Misri tuiabudu..walinung’unika, walimsengenya kiongozi wao, waliasi na kujiundia Makundi..Ni watu ambao walikuwa ni wagumu kuongoza, wazito kutii na wapesi kulalamika.
Ni vema kujua kuwa kila kiongozi wa kweli kuna siku atapitia kama Musa alivyopitia..
Ikifikia hatua hii wengi wanasema kama utumishi ndio huu ni heri niache, kama naonyesha fadhila zote hizi kinyume chake narudishiwa masengenyo na uasi, ni heri niache…
Ukifikiria hivyo bado hujawa kiongozi, Mungu alijua asili yao kwamba ni watu wenye shingo ngumu..alijua Yuda ni msaliti lakini bado alimpatia mwanae, amchunge.
Hao hao bado aliwaokoa na akataka wachungwe..
Shingo ngumu ni mtu wa namna gani?. Ni mtu anayefananishwa na ng’ombe ambaye hataki kufungwa Nira na Bwana wake…shingo inakuwa ngumu kuvishwa nira..
Hii ni aina ya watu ambao Hawana utii, hawachungiki, hata waone miujiza mikubwa namna Gani, hata wasaidiweje, si rahisi kuacha tabia zao za usengenyaji, wizi, uasi. Kiburi N.k.
Lakini bado Mungu anawaacha chini ya mchungaji waangaliwe..
Musa alikutana na waabudu sanamu, wanung’unikaji, Na wasahaulifu wa fadhili za Mungu…
Lakini alifanyaje?
Hata pale ambapo Mungu alitaka kuwaangamiza Musa aliwaombea. Alisimama kufanya upatanisho kwa ajili yao.
Ni ujumbe gani tunapewa?
Kiongozi wa kweli badala ya kughahiri kumchunga kondoo wake humwombea kwa bidii ili Bwana amponye asipotee kabisa kwenye dhambi.
Kiongozi wa kweli, huwa tayari hata kupoteza maisha yake kwa kondoo wake.. Musa alisema..
Kutoka 32: 32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.
Uongozi sahihi sio Kuongoza Watu wakamilifu, lakini kuongozo Watu dhaifu Kwa Mungu mkamilifu.
Uongozi Sahihi huweka katika uwiano sahihi “neema na kweli”
Ni vema kufahamu pia si kila wakati Musa alikuwa anasimama kuwatetea Waovu, hapana wakati mwingine aliruhusu upanga wa Mungu upite, Ili dhambi iogopwe…utakumbuka wakati ule walipotengeneza Sanamu ya ndama, na hasira Ya ki-Mungu ilimvaa Musa, ndipo Akazivunja zile mbao mbili, kisha akawaita watu walio upande wa Bwana wamfuate, Na wale waliosalia waliadhibiwa vikali kwa mauti.
Dhambi iwapo kanisani, haipaswi kuvumiliwa..Kutoa adhabu na wakati mwingine kuwaondoa wale wabaya ndani ya kundi ili lisiendelee kuharibiwa..
Lakini katika yote wewe kama kiongozi, huna budi kujifunza Uvumilivu, kuwaombea kondoo wako, na kuwa mpole, lakini pia kushughulika na dhambi Vikali katika nyumba ya Bwana.
Lakini kumbuka ijapokuwa Ni kazi, yenye mapito mengi ya masumbufu na maumivu Lakini thawabu yake na faida yake haifananishwi na gharama ulizoingia.. Hivyo penda kuchunga watu wa Mungu…Ndio heshima ya juu ya upendo kwa Mungu wako.
Mithali 14:4
[4]Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe; Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.
MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.
Jina la Mwokozi YESU, Ngome Imara libarikiwe (Mithali 18:10).
Hatujaitwa kujipenda tu wenyewe, au kuwapenda wale wenye imani moja na sisi au watu wa familia zetu tu!, bali tumeitwa kuwapenda hata watu walio mbali na imani zetu, tamaduni zetu, na hata itikadi zetu (hao ndio Biblia imewatafsiri kama majirani zetu).
Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? 47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Katika Agano la kale ilizoeleka kufahamika kuwa Jirani wa mtu ni Yule wa jamii moja naye, itikadi moja naye, na hata Taifa moja naye, jambo lililowafanya wana wa Israeli wasiwe na ushirika na mtu mwingine yoyote kutoka katika Taifa lingine, na wala wasiwe na upendo na mtu wa Taifa lingine lolote na kuwaona wote maadui (Na kwa wakati huo hawakufanya kosa kwasababu hawakuujua ukweli wote wa Upendo wa Mungu).
Lakini alipokuja Bwana YESU, (mjumbe wa Agano jipya sawasawa na Waebrania 12:24) yeye alitukamilishia kweli yote..na kuwafundisha kuwa majirani zao si tu watu wa Taifa lao, au wanaowajua…
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? 47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? 48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
Jambo hili Bwana Yesu aliliweka vizuri tena, wakati alipojiwa na yule mwanasheria ambaye alitaka kujionyesha yeye ni mwenye haki (kwamba anawapenda majirani zake) pasipo kujua jirani yake ni nani,
Huyu alipokuja alimwuliza Bwana je! Jirani yangu ni nani?.. kuna jibu Bwana alilompa, tusome..
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje? 27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. 28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi. 29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani? 30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa. 31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando. 32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando. 33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia, 34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza. 35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa. 36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni YUPI ALIYEKUWA JIRANI YAKE yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi? 37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?
30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni YUPI ALIYEKUWA JIRANI YAKE yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?
37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.
Kufuatana na mfano huu.. ni wazi kuwa huyu Mwanasheria alijiona kuwa yeye hana upendo kabisa!… Kwasababu hapo Bwana alikuwa anaonyesha kuwa Kuhani na Mlawi ambao walikuwa ni wayahudi, walishindwa kumsaidia myahudi mwenzao, aliyeangukia katika mikono ya wanyang’anyi, na badala yake anakuja kusaidiwa na Msamaria (mtu asiye wa imani yao wala Taifa lao).
Maana yake Yule Msamaria kafanya Ujirani mwema kwa myahudi aliyeangukia kwenye mikono ya wanyang’anyi zaidi hata ya wayahudi wenyewe… Hiyo Ikifunua kuwa ujirani sio tu kwa mtu wa imani moja na wewe, au wa Taifa moja na wewe, au rangi moja na wewe.. hata mtu mwenye itikadi tofauti kabisa na zetu, huyo tumeamriwa tumpende na hata kumfadhili pale inapobidi.
Na ndicho Bwana YESU alichokuwa anajaribu kukipanda kwa wayahudi kwamba kama vile Mungu aliyemtakatifu anavyowanyeshea mvua yake wenye haki na wasio haki, na sisi pia hatuna budi kunyesha mvua zetu za upendo na Baraka kwa wanaofanana nasi na wasiofanana nasi, kama vile Mungu anavyowaangazia Jua lake waovu na wema, na sisi hatuna budi kuangaza fadhili zetu kwa watu wote (wenye haki na wasio haki), huo ndio ujirani mwema.
Lakini tukijifunga kwa imani zetu, jamii zetu, itikadi zetu na kuwadharau wengine wote na hata kutoonyesha upendo, basi tufahamu kuwa tumejifungia wenyewe fadhili za MUNGU.
Bwana Yesu atasaidie sana, kwasababu kwa nguvu zetu hatutaweza.. pale tunapoambiwa “tumpende adui”.. ni jambo zito sana… Lakini kwasababu yupo Roho Mtakatifu aliyewekwa kutusaidia udhaifu wetu, basi tutaweza na kushinda na zaidi ya kushinda..
Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.
Maran atha!a
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe.
Jenga utamaduni wa kusoma Biblia, siku za mwisho ibilisi anazidi kuwekeza nguvu nyingi kwa watu wasisome wala kulielewa Neno, badala yake wapende tu kusikiliza mahubiri au kufanyiwa maombezi, lakini si Kusoma.
Lakini ukweli ni kwamba tukitaka kuisikia sauti ya Mungu ya wazi kabisa, njia ni kusoma Neno, tukitaka kumwona Mungu suluhisho ni kusoma Neno, tukitaka kumwelewa Mungu katika viwango vingine jawabu ni kusoma Biblia, tukitaka kuishi maisha ya kumpendaza Mungu,ni kusoma tu maandiko. Usipuuzie kamwe kusoma maandiko.
Hebu tujifunze kwa Bwana YESU wakati ule alipokutana na Yule mwanasheria ni maneno gani alimwambia…
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE? 27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako. 28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”.
26 Akamwambia, IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI? WASOMAJE?
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi”.
Zingatia hayo maneno katika mstari wa 26, ….IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?
Najiuliza kwanini Bwana Yesu hakumpa jibu la moja kwa moja, lakini badala yake anamrudishia swali.. “IMEANDIKWA NINI KATIKA TORATI?…. WASOMAJE?” maana yake kama angesema siju, ni wazi kabisa Bwana YESU asingempa jibu lolote, badala yake angemwambia akasome maandiko (akatafute katika maandiko)..Na leo hii wengi tunamwuliza sana Bwana maswali ambayo majibu yake yapo kwenye maandiko…..
Tukimwuliza Bwana swali ambalo jibu lake lipo katika biblia, anaweza kutujibu kama tu alivyomjibu huyu mwana sheria…. IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. WASOMAJE?
Hatuwezi kumlazimisha MUNGU azungumze kitu ambacho tayari alishakizungumza katika maandiko…tukimwuliza kitu ambacho tayari kipo ndani ya Biblia tunaweza tukapokea jibu kama hilo hilo tu… IMEANDIKWA NINI KATIKA BIBLIA?…. TWASOMAJE?
Na kitu pekee anachohakikisha shetani tusikijue ni UWEZA WA MUNGU pamoja na UWEZA WA MUNGU katika hayo maandiko.. kwa namna gani?
Marko 12:24 “Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?”
Weka ratiba ya kujifunza Biblia mtu wa Mungu, usiishie tu kusikiliza mahubiri, usiishie tu kusikiliza maombi.. bali soma soma soma.. Wakati mwingine unaweza ukawa unapitia vipindi ambavyo hujui nini cha kufanya, huo ni wakati wa kusoma Biblia utapokea ni nini cha kufanya huo wakati..
Unaweza kupitia wakati ambapo hujui uombe nini, soma Biblia utapata nini cha kuombea n.k
Nabii Danieli alikuwa sana kimaarifa na hata kujua nini cha kuomba kwa kusoma maandiko na si tu kutegemea maono yake na njozi zake.
Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. 3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. 4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.
3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.
4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”
Na zingatia: Kusoma Biblia si tu kutafuta neno moja la siku na kutembea nalo hilo, acha hiyo desturi!. Neno la Siku liwe ni ufupisho wa kingi ulichokisoma.
Bwana atusaidie.
Kwanini biblia ni neno la Mungu?
Kitabu kifupi katika biblia ni kipi, na ujumbe wake ni upi?
Je biblia inatufundisha tuwe wapole kiasi? (Wagalatia 5:22-23)
Je kuna haja gani ya kuamini biblia iliyoandikwa na watu?
Mistari ya biblia kuhusu sadaka