Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

Ratili ni kipimo cha uzito kilichotumika enzi za kale..chenye uzito sawa na Gramu 500 hivi. Karibia na nusu kilo.

Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi kwenye biblia..

Yohana 19:39

[39]Akaenda Nikodemo naye, (yule aliyemwendea usiku hapo kwanza), akaleta machanganyiko ya manemane na uudi, yapata ratli mia.

Pia..

Yohana 12:3

[3]Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.

Unaweza kupata picha Mariamu alibeba manukato yaliyokuwa na uzito wa karibia nusu kilo..na yote akammwagia Bwana Yesu..manukato ambayo ingetosha tu kuchukua kidogo na kumpaka lakini yeye aliyamimina kwake kama maji.

Kwasasa mafuta hayo kwa wingi wake ni thamani isiyo pungua milioni 6 kwa fedha za kitanzania..kufunua ni jinsi gani Mariamu alimthaminisha Yesu kuliko mtu mwingine yeyote au mfalme yeyote duniani..

Si ajabu kwanini matendo ya watu kama hawa tunayasoma hadi leo katika maandiko..Ni kutufundisha kuwa na sisi pia tukitoa vitu vyetu vya thamani nyingi sana kwa ajili ya Mungu..

Mungu naye ni lazima arudishe fadhila kwetu kwa kutupa kumbukumbu la daima..ndivyo alivyofanya kwa yule mwanamke pale watu walipomng’unikia kwa upotevu wote ule..Bwana alisema..

Marko 14:8-9

[8]Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko.

[9]Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake.

Swali ni je na sisi tunaweza kumthamini Bwana kwa namna hiyo? Bwana atupe macho hayo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Panda/ Sauti ya panda ni nini kibiblia?(Danieli 3:5)

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments