JE UNAMTUMIKIAJE BWANA?

JE UNAMTUMIKIAJE BWANA?

Mafunzo maalumu kwa Wanawake.

Karibu tujifunze Biblia,

Je Bwana alishakufanyia muujiza wowote katika maisha yako?..Na ukaufurahia?.. Je baada ya hapo ulimfanyia nini Bwana?.. Je uliishia kushukuru tu na kuendelea na mambo yako? Au kuna lingine la ziada ulilifanya?, kama hukufanya chochote au hukujua nini cha kufanya basi leo fahamu yakupasayo kufanya!

Hebu tujifunze kwa baadhi ya wanawake katika biblia ambao hawakuwa Mitume, wala Waalimu, wala Maaskofu wala wachungaji lakini walikuwa wakimtumikia Bwana Yesu.. na kisha tutazame walikuwa wakimtumikia kwa namna gani?

Mathayo 27:55  “Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, HAO NDIO WALIOMFUATA YESU TOKA GALILAYA, NA KUMTUMIKIA.

56  Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo”.

Hawa wanawake walikuwa wakifuatana na Bwana Yesu kila mahali.. Lakini je! Walikuwa wanafuata naye kumtazama uso?, au kumsikiliza tu anayoyahubiri?..Jibu ni La! Biblia inatuambia walikuwa pia WAKIMTUMIKIA!!.. Sasa swali wakimtumikia kwa nini?..tusome mistari ifuatayo..

Luka 8:1  “Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,

NA WANAWAKE KADHA WA KADHA ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,

3  na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, WALIOKUWA WAKIMHUDUMIA KWA MALI ZAO”.

Umeona hapo?.. Walikuwa wakimhudumia kwa MALI ZAO!. Ikiwa na maana kuwa gharama kubwa za kuipeleka Injili zilikuwa zinabebwa na hawa WANAWAKE!..  hata ule mkoba ambao Yuda alikuwa anaushika, huenda sehemu kubwa ilijazwa na hawa wanawake!.

Na kwanini wanawake hawa walipata msukumo huo mkuu wa kumhudumia Bwana kwa mali zao?.. Jibu ni kwasababu walitendewa miujiza na Bwana, walitolewa pepo waliokuwa wanawatesa, waliponywa magonjwa  yao yaliyokuwa yanawatesa, walipewa wokovu ndani yao ambao uliwapa Amani na tumaini la maisha..Hivyo wakaona si sawa kumtazama Yesu kwa uso tu na kumshukuru kwa maneno tu!, bali pia kwa vitendo.

Ndipo wakaona wavunje vibweta vyao ili Bwana akaende miji mingi Zaidi kuhubiri, wakaona watoe hazina zao ili wanafunzi wa Bwana wasipungukiwe wanapokwenda kuhubiri miji na miji. Na hivyo wakawa mashujaa wa Imani ambao mpaka leo tunawasoma.

Na sio hao tu, bali pia tunamwona na Mkwe wake Petro, (Mama yake mkewe) ambaye alikuwa anaumwa homa, biblia inasema baada ya Bwana kumponya, alinyanyuka na kuanza KUMTUMIKIA BWANA!.

Mathayo 8:14 “Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.

15  Akamgusa mkono, homa ikamwacha; NAYE AKAONDOKA, AKAWATUMIKIA”

Je na wewe Mama unamtumikia nani?, Na wewe binti unamtumikia nani?…Je umemtumikia Bwana kwa kipi tangu alipokuponya?, tangu alipokufungua?, tangu alipokuinua?, tangu alipokupa wokovu bure?.. Je unamtumikia kwa maneno tu, au pia na vitendo?.

Ni kweli wewe sio Mchungaji, wala Mwalimu, wala Mhubiri, wewe ni kama tu Mariamu Magdalena, au Susana..basi fanya kama hao!.. Na kumbukumbu lako litadumu kama la hao wanawake lilivyodumu, Bwana atakuheshimu na kukuona wewe ni mtumishi wake kama tu walivyo Mitume kwasababu na wewe pia unamtumikia kwa mali zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

Katika (Mathayo 25:8 na Marko 16:8) Wale wanawake walitangaza kufufuka kwa Bwana au walikaa kimya?

WANNE WALIO WAONGO.

JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Emmanuel kulwa
Emmanuel kulwa
1 year ago

Napenda kujifunza neno la Mungu