Category Archive Home

Maana ya Mithali 29:20 Je! umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?

Mithali 29:20

Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye

Mtu mwenye kuhamaki.

Ni mtu anayezungumza maneno kwa haraka, yaani anayezungumza bila kufikiri, au kujizuia.

Vitu kama mizaha, ugomvi, hasira, uongo, na mafarakano, huzaliwa na tabia kama hii ya watu kunena bila kufiriki.

Kwamfano, mtu anaweza kukutukana, na wakati huo huo hasira ikawaka ndani, sasa kwasababu huwezi kujizuia, unajikuta unarudisha majibizano, hatimaye na wewe unafungua kinywa chako unatukana.

Au labda unatambua jambo Fulani ambalo si jema, na pengine ukilisema linaweza lisiwe na maana yoyote, kinyume chake likazua ugomvi, au kumuabisha mwingine, au sintofahamu, lakini wewe kwasababu huwezi jizuia unalisema, mwishowe matatizo yanazuka makubwa yasiyokuwa na lazima.

Watu wanaoapa, ni matokeo ya kunena bila kufikiri, mafarisayo ambao walitenda dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni kwasababu ya maneno ambayo hayana hekima nyuma yake.

Mathayo 12:36  Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.

Mpaka hapo unaweza kuona ni kwanini mpumbavu anaweza kuonekana ana afadhali kuliko mtu mwenye kuhamaki.

Mstari huu unatukumbusha nguvu iliyopo katika maneno, biblia inasema ulimi ni kama moto ni kiungo kidogo lakini kinawasha misitu, hivyo hatuna budi kuwa wazito katika kunena,  tukifiri kwanza ndipo tuseme. Yakobo 1:19

19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Maneno yana nguvu, kila siku yatupaswa tujifunze kudhibiti vinywa vyetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

 

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

 

 

 

 

Print this post

Je wana wa Israeli waliofia jangwani, walienda mbinguni au jehanamu?

JIBU: Wakiwa jangwani wana wa Israeli walitenda  makosa  ya aina mbili.

  1. Makosa yaliyopoteza Ahadi
  2. Makosa yaliyopoteza Uzima wa milele.

Makosa yaliyopoteza Ahadi ndio yalikuwa yale ya kutokuamini. Mfano Mungu alipowatoa jangwani, na kuwavusha, mara nyingi walionyesha hali ya kutoamini, Kosa ambalo liliwafanya Mungu aghahiri kuwafikisha kule alipowaahidia, ambapo ni nchi ya Kaanani ibubujikayo maziwa na asali, Na kilele cha kosa hilo kilikuja  pale wale wapelelezi waliporudi katika kuichunguza nchi, na kutoa ripoti za kule, kwamba wao wanaonekana kama mapanzi, hivyo wote wakaanza kulia na kutaka kurudi Misri, Ndipo Mungu akakasirika sana na kuapa kuwa wote  hawataiona hiyo nchi ya Kaanani isipokuwa Kalebu na Yoshua, kwasababu wao hawakuonyesha kutokuamini.

Hesabu 14:21-24

21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana;
22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;
23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona;
24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki

Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hawatakwenda mbinguni, kwasababu wapo waliotubu,hata wakati ule ule

Kwahiyo kusema adhabu ile ndio iliwapelekea moja kwa moja kupoteza mbingu si sahihi.

Kwasababu Mungu aliendelea kutembea nao kwa wingu lake, baadaye akawainua viongozi, wa kuwaaamua na Pamoja na wazee, akawamwagia  Roho wake, (Hesabu 11:25). Hivyo kama Mungu kasingekuwa nao, basi hayo yote yasingefanyika, kwasababu Mungu hawezi kuwaongoza wafu.

Lakini yapo makosa ambayo yaliwagharimu adhabu ya kupoteza kabisa uzima wa milele. Na makosa kama hayo ndio yale ya makusudi kabisa, mfano wa hayo ni yale ya kuvunja amri za Mungu, kama vile kutengeneza sanamu ya ndama  na kuiabudu, Kuzini, kuwa na miungu mingine, na kuhalifu sabato za Mungu .

Makosa kama hayo ndio yaliyopelekea  kupoteza uzima wa milele, ndio maana ukichunguza utaona watu kama hawa walipokea adhabu za moja kwa moja.     Hivyo ni kuwa makini sana na neema ya Mungu.

Hata sasa, zipo dhambi za aina mbili zinazozungumziwa kwenye maandiko, dhambi za mauti, na dhambi zisizo za mauti.

Kwa urefu wa maelezo yake, pitia hapa>>> DHAMBI YA MAUTI

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?

Kwanini Roho Mtakatifu amzuie Paulo kuipeleka injili Asia? (Matendo 16:6-7).

Print this post

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

Yohana 13:34

[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 

Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..

Ni amri ipi hiyo mpya?

Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?

Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana

Mambo ya Walawi 19:18

[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA. 

Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…

“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”

Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.

Je upendo wa Yesu ulikuwa upi?

Upendo wa upeo.

Yohana 13:1

[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. 

Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..

Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..

Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo

Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.

Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.

Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)

Je amri hii mpya tunayo?

2 Yohana 1:5

Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane. 

Bwana awe nawe.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Print this post

LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.

1 Samweli 30:6

[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake. 

Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.

Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe, 

Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe, 

Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..

Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.

Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.  

Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu. 

Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.

Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.

Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

WATU HAWA WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA HUKU NAKO

Kama tunavyofahamu katika maandiko Mitume walipofika mji wa Thesalonike kwa ajili ya injili, na kukutana na wenyeji wa mji ule, na kusikia walichokihubiri maandiko yanatuambia walipiga kelele sana na kusema maneno haya;

“Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako”

Matendo ya Mitume 17:6

[6]na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Ulishawahi kutafakari kwa ukaribu maneno hayo walichokimaanisha?

Wanasema;

Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Maana yake ni kuwa ulimwengu na wao, ni kama vitu viwili tofauti…

Wamefika na huku pia….yaani wameshaushinda ulimwengu wanakuja na huko kwao kumalizia walichokifanya kule..

Hii ikiwa na maana…mitume walishapata ushindi kabla hata ya kufika maeneo yote…

Kuna mahali pajulikanapo ulimwenguni ambapo tayari walishapashinda.

Sasa huo ulimwengu ni upi?

Chukulia mfano wa dunia ya sasa.. kuna usemi wasemao nchi za Afrika ni dunia ya tatu.. ijapokuwa wote tupo kwenye sayari moja, ujulikano dunia, lakini uhalisia dunia zipo tatu…Zile nchi zilizoendelea sana…Kama vile Marekani, urusi, China, ufaransa..ni dunia ya kwanza… na zile zilizo katika uchumi wa kati ni dunia ya pili na hizi maskini ni dunia ya tatu..

Sasa ikitokea mtu akayapiga hayo mataifa makubwa na kuyateka, maana yake huyo mtu ameiteka dunia, ameipindua dunia…..hata kama hajapigana na haya mengine madogo..lakini ikiwa nguvu zake zimewashinda wale basi hawa wengine ni maji tu.

Vivyo hivyo waamini wa wakati ule walionekana, wanamapinduzi wakubwa sana..kwasababu ushindi wao ulianzia kwenye vichwa.

Sasa huu ulimwengu ni upi?

JIBU: Ulimwengu wa Roho.

Zamani zile dini zilijulikana kama msingi mikubwa sana inayosukuma mielekeo ya mataifa.. hivyo Kristo alipokuja aliweza kuvunja misingi ya imani potofu na dhaifu kuanzia pale pale Israeli mpaka miisho ya dunia. Alileta Nuru duniani ambayo giza lolote halikuweza kulishinda..

Yohana 1:4-5

[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 

[5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. 

Ndio maana kipindi cha injili utaona Wayahudi wengi waliokoka, wapagani wengi wakaacha miungu yao..wakaichoma moto, utaona hata kule Efeso mungu mke aliyeabudiwa ulimwenguni kote (Matendo 19:27), mitume walipofika habari yake ikaishia pale pale, tofauti na zamani manabii walishindana sana na mabaali lakini hawakuweza kuyashinda..kwasababu hakukuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mkuu wa ulimwengu huu(shetani)

Yohana 16:11

[11]kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 

Hivyo ulimwengu wa roho uligeuzwa juu chini, mapepo yaliwakimbia wengi, watu walifunguliwa kwenye vifungo vya giza..makaburi waliwaachia wafu..kila siku watu waliongozeka kumjua Mungu…na kuachana na dhambi.

Matendo 19:19-20

[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. 

[20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. 

Huu ndio ulimwengu sugu uliopata tiba…ulimwengu wa giza, kama kichwa cha mifumo yote mibovu ya dunia…uliwekwa chini…

Hivyo wale watu walipoona imani za watu zinageuzwa kwa kasi hata za maakida wakubwa,(Matendo 13:7-12) majemedari, watu wenye vyeo, wake kwa waume, nao pia wanaigeukia imani..wakatambua ya kuwa kila kitu kimekwisha sasa, sisi ni masalia..tu.

Walijiona kama mapanzi, ni sawa na wana wa Israeli walipoweza kuliangusha taifa la Misri, hata kabla ya kufika Yeriko, Wale watu wenyewe walishajiona kama mapanzi..Kwasababu kichwa cha ulimwengu kimeshaangushwa.

Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tujue kuwa sisi tuliomwamini Yesu…tayari tumeshaupindua ulimwengu kwa Injili iliyokwisha fika kuzimu kwenye kiti cha enzi wa shetani…

Hakuna chenye nguvu ya kutuzuia sisi tena, sisi ni watawala wa dunia.

Wanasiasi, hawawezi kutuzuia, wanadamu hawawezi kutusimamisha..wao ni kama mapanzi tu kwetu…

Hatuna budi kuuinua ujasiri wetu wote…tufikie mataifa yote kuhubiri injili kwasababu ulimwengu tayari tumeshaupindua…hatuhitaji kwenda tena kuupindua..sisi ni kumalizia tu masalia. Unasubiri nini usiamke kuihubiri injili? Amka sasa…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Print this post

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

Kila mwanadamu maadamu amezaliwa na kuishi duniani, ndani yake lazima kuna kiwango tu cha majuto..

Wengine wana majuto makubwa sana, wengine kiasi.

Majuto ni hali ya kuhuzunishwa na matokeo ya machaguzi au maamuzi yaliyofanyika katika maisha.

Kwamfano kijana anaweza kuchagua kukatisha masomo kisha aende mtaani, kuuza peremende, sasa hayo ni maamuzi yake, lakini baadaye anapoona haoni matokeo makubwa, kinyume chake anawaona wenzake waliosoma wamepiga hatua kubwa anaanza kuingiwa na huzuni ya kujishitaki mwenyewe, sasa hayo ndio majuto.

Mwingine amechagua kuishi na mtu bila kufunga naye ndoa, hatimaye akazalishwa, watoto wengi na kuachwa..baadaye umri umeenda anataka kuoelewa, inakuwa shida…anaingiwa na majuto.

Mwingine amepoteza miaka mingi duniani kumtumikia shetani, sasa ameshakuwa mzee anajisikitikiza miaka yake ya ujana aliyoipoteza yenye nguvu alikuwa wapi asimtumikie Mungu…

Majuto yapo ya namna nyingi, na kila mtu kwa sehemu yake anayo majuto fulani, haijalishi unaishi wapi, au umefanikiwa vipi…kuna mahali ulikosea na yakaingia..

Kimsingi majuto sio dhambi, ni hali ya ki-Mungu kabisa ambayo mwanadamu ameumbiwa ndani yake..

Lakini ni vema kujua namna ya kuyaweka mahali pake..kwasababu yasipoweza kutenganishwa ipasavyo hupelekea hasara kubwa mno ndani ya maisha ya mtu.

Katika biblia kulikuwa na watu wawili ambao walihuzunishwa na maamuzi walillyoyafanya …mmoja ni Petro, mwingine ni Yuda.

 Yuda alihuzunishwa lakini huzuni yake ilimpelekea kujinyonga…Petro alihuzunishwa lakini huzuni yake ilipelekea kulilia msaada wa Mungu..(badiliko)

Petro aliruhusu majuto yake yabebwe na Mungu, Yuda aliruhusu yabebwe na shetani.

Lakini majuto yalikuwa yale yale…Yuda hakukosea kujuta hadi kurudisha pesa

2 Wakorintho 7:8-11

[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu. 

[9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. 

[10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. 

[11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo. 

Umeona Majuto ya ki-Mungu huleta toba.. lakini majuto ya shetani hupelekea mauti..

Ukishaanza kujiona kama wewe huwezi tena, Mungu kakuacha, hufai, huna maana, hustahili, ujue shetani yupo nyuma ya juto hilo, ambalo anataka kukusababishia usiinuke tena, ujitenge, ujiue, uache kwenda kanisani, aache maombi, uache kumtafuta Mungu, uache uchungaji …

Kinyume chake unapokosea jione kama ulikuwa unapitishwa katika funzo ambalo sasa unapewa nafasi nyingine usiitmie vibaya…

Watu wengi, unaowaona wamekata tamaa, wamepoa, hawana mabadiliko tena, wamejitenga, lakini hapo zamani walikuwa vizuri, wana mashaka na hofu ya ndani kwa ndani, asilimia kubwa ni majuto mabaya yanawasonga ndani yao.

Daudi alipoanguka katika dhambi ya uzinzi, alimrudia Bwana kwelikweli, ijapokuwa ilimgharimu pakubwa…hakwenda kujificha na uso wa Mungu kama Adamu.

Lakini ya ki-Mungu huturudisha kumtazama Mungu…Rudi umwangalie Mungu wako kisha chukua hatua nyingine, kwani hiyo huwa na nguvu na matokeo ya haraka zaidi ya mwanzo.

Petro baada ya pale alikuwa na ujasiri mkubwa wa kumshuhudia Kristo, zaidi ya mitume wengine wote, ikiwa umefeli mahali fulani embu amka tena kwa nguvu, usikubali kunyong’onyea kama Yuda na mfalme Sauli ambaye alijiua..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MWOMBOLEZAJI.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA

Print this post

IPO NJIA YA MKATO YA KUFIKA KIWANGO VYA MBALI VYA KIROHO.

Maisha ya mwilini mara nyingi hubeba mafundisho ya rohoni, ndio maana Bwana Yesu alitumia sana mifano ya kidunia kuwafundisha siri za ufalme wa mbinguni.

Katika jamii ili mtu aitwe profesa au daktari(kitaaluma) anapaswa awe ni msomi wa kukaa darasani kwa muda mrefu, awe na ujuzi lakini pia na uzoefu wa tafiti nyingi..yaani kwa ufupi haiwezekani ukaitwa daktari(kitaaluma) halafu usiwe msomi wa elimu za juu.

Lakini kuna udaktari ambao mtu anaweza kupewa kwa kutunikiwa, na mara nyingi huu huja pale mtu anapotoa mchango fulani mkubwa katika jamii…mtu kama huyu anaweza kutunukiwa udaktari hata kama yale mafunzo ya ndani ya kitaaluma hana.

Sasa kiroho ni vivyo hivyo unaweza pia ukawa mkufunzi, mwenye ukomavu mkubwa, zaidi ya mababa zako wa kiroho, hata zaidi ya wachungaji wako, au maaskofu wako, au wazee wako wa kiimani, kwa namna gani?

Mstari ufuatao unatupa jibu;

Zaburi 119:99-100

[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote,

Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.

Ukitafakari huo mistari, utaona ni mwanafunzi anayejisifia kuwa ana akili zaidi ya waalimu wake…sio kwamba ameshahitimu, hapana bado yupo chini ya waalimu wake lakini akili zake zimewapita, bado ni kijana lakini ufahamu wake umeshawazidi wazee wake.

Imewezekanikaje?

JE anasoma sana? Au ana kiwapa cha asili tofauti na wengine? Hapana…anasema kwasababu shuhuda za Mungu ndizo anazozitafakari, lakini pia anayashika mahusia ya Mungu .

Hiyo ndio siri yake, usiku na mchana ni kufikiri juu ya “KWELI”, Yaani Neno la Mungu, na na namna ya kulifanya kuwa sehemu ya maisha yake..(kujiepusha na dhambi.)

Hiyo ndio namna inayomkomaza mtu kiroho kwa haraka sana kuliko hata maarifa mengi ambayo wengi hudhani, au mafunuo mengi, au kuhubiri kwingi, au kufundisha kwingi…

Mtu mmoja anaweza akawa na uelewa mkubwa, mwalimu mzuri, mtume mwenye ushawishi mkubwa, lakini bado asimkute mwanafunzi wake ambaye maisha yake anajitahidi kuliishi Neno la Mungu.

Hivyo ndivyo Mungu anavyowatambua wakufunzi wake (kiroho), uwezo wa “kumcha Mungu” haijalishi utapoteza sifa nyingine zote za maarifa,mafunuo, lakini akiwa na hiyo huyo amefika mbali sana.

Kwasababu Biblia inasema hakuna mwisho wa usomi, (kujua maarifa), ila mtu akizingatia kumcha Mungu na kuziishika amri zake, ni zaidi ya usomi wa vitabu vyote.

Mhubiri 12:12-13

[12]Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.

[13]Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa;

Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

Tuwekeze nguvu zetu zote katika kuliishi Neno na neema ya Mungu itusaidie..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?

USIKWEPE CHUO CHA UTAKATIFU.

HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

Print this post

KAMA NISIPOKUTAWADHA, HUNA SHIRIKA NAMI

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima

Tengeneza picha Mungu amekutokea amesimama mbele yako, wakati ukiwa na mawazo ya kumwangukia chini umsujudie, unashangaa yeye moja kwa moja anakuwa wa kwanza kuinama na kukusafisha miguu yako…

Hivi utajisikiaje? Ukweli ni kwamba hutajisikia huru hata kidogo, kwa ufupi hutakubali kitendo hicho kifanywe na yeye kutoka na ukuu wake, na heshima yake iliyozidi vyote, ni sawa na uone baba amemnunulia mtoto wake zawadi halafu yeye ndio anayekuwa wa kwanza kumshukuru mtoto, tena kwa kumwinamia..ni wazi kuwa hilo halijakaa sawa, au mtu aliyeibiwa mali zake nyingi, halafu amekutana na aliyemwibia badala ya mwenye mali kungojea kuombwa msamaha, yeye ndio anajionyesha kama ni mkosaji kwake…unaona ni jambo ambalo halina uhalisia, halikubaliki kifikra hata kidogo…

Kwa namna ya kawaida hali kama hizi akitendewa mtu hawezi kuridhia…lakini Mungu anatutendea sisi na anasema kama hutakubali kutendewa naye hivyo kamwe hutuna ushirika naye.

Ndicho kilichotokea kwa mitume na Petro. Wakati ule walipomwona Bwana Yesu, anashika kitambaa na maji kisha akaanza kuwaosha na kuwapangusa miguu yao…Petro hakuweza kuridhia akasema Bwana hutanitawadha miguu kamwe. Lakini Yesu akamwambia usipokubali huna ushirika nami.

Yohana 13:8

[8]Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami. 

Hii ni kufunua nini…

Ni lazima tumjue Kristo, ni kweli anasimama kwetu kama mfalme, kama Bwana, kama Mungu…tunamwabudu…lakini pia anasimama kama mtumishi wetu..Ni jambo ambalo hatuwezi kuingia akilini  lakini ndivyo alivyo, amependa yeye kuwa hivyo kwetu.

Ni mfalme mwenye taji la kifalme lakini wakati huo huo pia mfalme aliyebeba kitambaa cha kuwasafisha watu miguu.

Hiyo ndio sifa ya ufalme wake. Amesimama kama muumba wetu tumwabuduye, lakini pia anatutumikia, katika kutuponya magonjwa yetu, kutulisha, kutuvisha, kutuombea, kutulinda, kutufuta machozi, na kuchukua mizigo yetu mfano wa punda na hata kufanya mambo ambayo sisi hatuwezi stahimili akitufunulia yote kwa jinsi anavyojishusha na kujishughulisha sana na mambo yetu…. Na mfano tukitataa yeye asituhudumie hivyo anasema wazi kuwa hatuna ushirika naye.

Maana yake ni fahari yake kututendea hayo, wala yeye hayahesabu kuwa ni kitu.

Anatufundisha nini?

Tuwe watumishi pia wa wengine kwa namna hiyo, kama yeye alivyo kwetu…kujitoa kwake sio kutimiza wajibu bali ni fahari yake ambayo isipokubaliwa inaharibu moja kwa moja mahusiano.

Kumsaidia mpendwa mwenzako iwe ni furaha..kujinyenyekeza kwake isiwe ni sababu za umri au cheo bali fahari..Kumwombea iwe ni fahari yako, kumsikiliza iwe ni furaha yako…hivyo ndivyo Bwana anavyotaka.. na ndivyo alivyomwambia Petro.

Yohana 13:12-17

[12]Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? 

[13]Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. 

[14]Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. 

[15]Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. 

[16]Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka. 

[17]Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda. 

Neema ya Bwana itusaidie.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WEWE NI ZAO LA MAHUSIANO NA USHIRIKA.

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Print this post

Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu.

Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu

Wimbo ulio bora 2:15

15 : Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.

Kitabu cha wimbo ulio Bora ni kitabu kinachoeleza asili ya upendo wa Kristo kwetu na jinsi tunavyopaswa kuuitikia.

Kuwa urefu wa masomo yaliyo nyuma ya kitabu hiki fungua hapa >>> NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

Lakini kwenye mstari huu, tunaona ni kama vile mtu kwa lugha ya picha anaona mbweha “ Wadogo” wamevamia shamba lake la mizabibu inayochanua na hivyo hawapuuzii kwasababu ya udogo wao, bali anatoa tamko la kukamatwa na kuondolewa…ili shamba lake linalochanua liwe salama.

Kimsingi mbweha si mnyama anayekula nyama tu, bali hula pia mizazibu, na mingine kuiharibu.

Hii ni kufunua nini katika hali zetu za rohoni.. 

Adui akishaona mahusiano Yetu na Kristo yanazaa matunda, huinua vitu Vidogo vidogo ili kuharibu mahusiano wakati mwingine unaweza usione kama vina madhara sana au vina nguvu sana, lakini katika eneo la kiroho kitu kidogo kina nguvu sawa na kitu kikubwa…

Hivi ndio vinavyoitwa mbweha wadogo..

Mambo Kama haya ni kama vile kuendekeza vishawishi vya dhambi kwenye maisha yako.

Kwa mfano wewe ni binti halafu kila siku unaona wanaume wanazungumza na wewe maneno ya mizaha, sasa kama usipokemea tabia hiyo, ukaona ni kawaida, tabia hizo ndogo ndogo ndizo zinazopelekea mtu baadaye kuanguka kwenye dhambi za uzinzi.

Samsoni, alipoona ushawishi wa delila unaendelea, badala aukatishe yeye akapuuzia mwisho wa siku akatekwa..

Hao ni mbweha wadogo wanaoharibu shamba lako, kila kichocheo na kishawishi kiwe kidogo kiasi gani usikipuuzie.

Wakati mwingine kuendekeza uvivu wa kiroho, yaani kupuuzia maombi, kupuuzia ibada, kidogo kidogo hupelekea kupoa kiroho, na hatimaye unajikuta kabisa umerudi duniani..mpaka unajiuliza nimefikaje hapa? Ni kwasababu uliendekeza uvivu wa kiroho..ulisema. nitaomba kesho, nikesha kesho, nitamtumikia Mungu mwezi ujao..mwishowe ukawa hivyo ulivyo leo…

Angalia ni eneo lipi la maisha yako limevamiwa na hawa mbweha wadogo, kisha chukua hatua za haraka kurekebisha.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.

Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?


 

Print this post

Kuba ni nini kibiblia?

Kuba ni kitu chenye umbo la duara kinachofunika kwa juu, ni kama paa lililopinda. Lenye mwonekano unaofanana na nusu ya mpira au bakuli lililogeuzwa juu chini.

Mifano ya kuba:

unaweza kuona kwenye ujenzi wa Misikiti mingi na baadhi ya Makanisa na majengo ya kale

Tukirudi kwenye biblia Enzi za kale, ilidhaniwa kuwa dunia ina kuba kwa juu, yaani kifuniko. Ambao ndani yake jua, mwezi na nyota hutembea..

Neno hilo utalisoma katikq vifungu hivi; 

Ayubu 22:14

[14]Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; 

Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu. 

Amosi 9:6

[6]Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA ndilo jina lake. 

Kumbuka, ujumbe unaowasilishwa hapo ni kueleza ukuu uliozidi wa Mungu, katika uumbaji wake na mamlaka yake.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Israeli?

Binti za Yerusalemu wanaotajwa katika kitabu cha Wimbo ulio Bora 1:5 ni akina nani?

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

UNAJISIKIAJE, KUTEMBEA NA SANDA?

Print this post