Turejee..
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi; 21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi;
21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Wazamzumi walikuwa ni watu warefu na wakubwa na wenye nguvu walioishi nyakati za kale, mfano wa hao ni akina Goliathi..
Watu hawa katika enzi za kale ndio watu waliokuwa wanatisha na kuogopeka sana.. walikuwa ni hodari wa vita na wenye maendeleo makubwa, walijenga miji mikubwa na walikuwa na silaha zenye nguvu, hakuna Taifa lililowaweza kwa uhodari wao.
Lakini pamoja na kusifika kuwa na nguvu nyingi za mwili, na uhodari mkubwa, bado mbele za MUNGU mazamzumi wote si kitu, Goliathi aliangushwa na kijana Daudi aliyekuwa mtumishi wa MUNGU, Mazamzumi waliokuwepo Yeriko waliangushwa na vijana walionekana dhaifu wa kiisraeli, na zaidi sana Mazamzumi wote waliangamizwa na Bwana wakati wa gharika ya Nuhu (Mwanzo 6:4).
Kama Zamzumi wako ni “dhambi” mwambie Bwana amwangushe..kwa nguvu zako hutaweza.. kama Zamzumi wako ni kikundi cha watu fulani wabaya.. mwambie Bwana akuondolee hao watu, haijalishi ni hodari kiasi gani au wana uwezo kiasi gani, bado MUNGU ana uwezo wa kuwaondoa.
Unachopaswa kufanya ili Mazamzumi yote yaondoke ndani yako nan je yako, ni wewe kumwamini Bwana YESU na kukubali kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na pia kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia maishani mwako na kukutakasa kabisa kabisa.
Ikiwa bado haujabatizwa na unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu.
Bwana YESU akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Simoni Mkirene aliubeba msalaba wa Bwana Yesu au la?
Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.
Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”
MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.
Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?
Print this post
Luka 15:20
[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..
Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..
Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..
Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..
Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..
Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…
Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…
Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?
Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.
Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.
Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?
Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU
JAWA SANA MOTO ULAO.
TENGENEZA NJIA YAKO.
Marko 9:24
[24]Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Habari ya yule mzee ambaye kijana wake alivamiwa na mapepo sugu ya kumtupa motoni tangu utoto wake, na baada ya kuhangaika sana kwa madaktari na kila aina ya matabibu, hadi mitume nao kushindwa kumponya, hatimaye akakutana na Bwana Yesu..
Akamwambia ‘Ukiweza’ Bwana neno utuhurumie na kutusaidia… lakini saa hiyo Hiyo Yesu akamjibu….Ukiweza?..
Mimi unaniambia ukiweza?
Marko 9:23
[23]Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Kuonyesha kuwa Imani yake, haikuwa kamili, lakini, saa hiyo hiyo akaweka tegemeo lake lote kwa Yesu na kumwamini..’Naamini’…lakini pia nisaidie ‘kutokuamini kwangu’..
Hiki ni Moja ya ombi ya uwazi na la ukweli kabisa ambalo tunaweza kulisoma kwenye biblia…
Ni kweli ameamini, lakini imani yake si timilifu, anapambana sana kuifanya iwe sawa.. hivyo pamoja na hilo akamwona na Bwana amsaidie…kuonyesha tabia ya kujiachia kikamilifu kwa Bwana…kwamba sio tu kutendewa muujiza lakini pia kusaidiwa..
Saa hiyo hiyo Yesu hakumfukuza, wala kumkemea, wala kumwambia kafanye hivi au vile kwanza… bali akamkemea yule pepo Na hatimaye kijana akawa mzima saa ile ile.
Imani, ya kweli haimaanishi kwamba mashaka yatapotea…bali ni kuchagua kujimimina kwa Bwana na kuweka tegemeo lako lote kwake tu, hata kama moyo wako utakuambia wewe mbona unamashaka mashaka, mbona huna imani, mbona maneno yako mwenyewe yanathibitisha umekata tamaa..
Hakika hapo usiache kuomba na kukiri, ukiulilia pia msaada wa Bwana akusaidie imani yako iwe Kamilifu, kwa kujimimina tu hivyo hatimaye utayaona mambo makubwa akikutendea..
Usianze kujilaumu kwa mashaka mia uliyoonyesha, wewe egemea tu kwa Yesu bila kuondoa mguu wako hapo…atakujenga..Yule baba hakuondoka kwa Yesu, kwasababu ya madhaifu yake bali aliendelea kukaa pale pale. Kwasababu imani inajengwa kwa mahusiano sio kwa utimilifu wetu.
neema ya Mungu hizidi mapungufu yetu..kiri.udhaifu wako kwake, lakini onyesha kumtegemea yeye, hapo nguvu za Mungu utaziona.
Shetani atataka ujilaumu, katika shida yoyte lakini sema…
“Naamini, Bwana, nisaidie kutokuamini kwangu.
ENDELEZA UPONDAJI.
MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?
WhatsApp
Waebrania 12:29
[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.
Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa
Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)
Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…
Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.
Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;
Isaya 33:14
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele? [15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..
Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.
Hii ndio mbio yetu wote…
Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.
Shalom
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)
Mwanzo 3:15
[15]nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa..
Kitu pekee Ambacho kilitabiriwa kuweza kuvunja vichwa vya majoka(shetani), ni uzao wa mwanamke tu. Aliyetabiriwa kwenye (Mwanzo 3:15)
Uzao huu wa mwanamke ni Yesu Kristo.. kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyezaliwa Bila mwanamume, sisi wote ni uzao wa mwanamume…kwasababu mbegu yetu imetoka kwa Baba zetu, lakini Kristo ni mbegu iliyoshuka Kutoka mbinguni, ndio maana hapo anatajwa Kama uzao wa mwanamke.
Yeye kwa ushindi alioupata dhidi ya nguvu za giza kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu na kupaa mbinguni..ni pigo Kubwa sana kwa shetani, ambalo lilimlenga moja kwa moja katika kichwa chake.
Kwasababu kwa njia hiyo wanadamu tumevuka kutoka mautini kwenda uzimani…
Lakini habari njema ni kuwa yeyote amwaminiye, anakuwa sehemu ya uzao huo kwa imani. Na hivyo anapokea mamlaka ile ile ya kuvunja mafuvu ya majoka…mpaka ufalme wa giza kutokomea kabisa katika uso wa ulimwengu..
Wagalatia 3:29
[29]Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
Luka 10:19
[19]Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Kumbuka uwezo huu, hakuna uzao mwingine wowote unaoweza kumuharibu shetani, waafrika hawawezi, wazungu hawawezi, wachina hawawezi, waarabu hawawezi, ukoo wa kiyahudi hauwezi, familia za kichifu, haiwezi, wanadamu wote hawawezi kuponda majoka, hata waungane kwa vifaru vyao na makombora ya nyuklia, bado hawawezi kinyume chake wao ndio watafanyika chakula cha hao majoka.Ni uzao mmoja tu wa Yesu Kristo ndio wenye nguvu hizo..
Swali ni je! Tunapondaje vichwa vya majoka.
Ni kwa kuendelea kuhubiri. Ukikaa tu bila kushuhudia habari za Kristo kwa wenye dhambi, kukaa bila kujishughulisha na shamba la Bwana..Fahamu kuwa ‘mabuti’ yako uliyopewa huko miguuni huyatendei Haki..yapo tu!
Unamridhia shetani, unafurahishwa na uwepo wake shambani mwa Bwana, ndugu njia pekee inayomdosha shetani kwa wepesi ni wewe kukutana na mwenye dhambi mmoja na kumshuhudia habari za wokovu.
Mitume walipoenda kuhubiri baada ya kutumwa na Yesu, waliporudi na ushindi, Yesu aliwaambia nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..
Luka 10:18
[18]Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
Simama tumia mabuti yako vizuri, endeleza kuponda, ponda kweli kweli, haribu kisawasawa, kwa njia ya injili.
Sio kwa kuimba “nakuponda shetani” au
Kusema “toka shetani” bali kwa injili
Kuponda kwingine ni maombi na kuishi maisha ya utakatifu, huku nako kunahubiri injili ya Kristo na hivyo shetani anaumizwa vibaya sana.
Amka tumia buti zako, kila kichaka katika shamba la Bwana ambacho majoka yamejificha Ni kwenda kuponda tu, mpaka habari njema za ufalme zifike ulimwenguni kote.
Bwana awe nawe.
Amen.
IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.
INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.
Ni vema kufahamu Kanisa ni nini?
Kanisa sio jengo, au mahali, bali ni watu, walioitwa Na Mungu, waliookolewa wanakusanyika pamoja katika nia moja kumwabudu na kumtumikia yeye.
Hivyo watu hawa wanaweza kukusanyika maeneo yaliyo rasmi, lakini pia maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli zao za kiibada..maadamu tu wamekidhi vigezo hivyo vya kiroho.
Kanisa la kwanza lilikusanyika Hekaluni (mahali rasmi kwa shughuli za kiibada tu). Lakini pia lilikusanyika majumbani…wakati mwingi pembezoni Mwa mito na kwenye madarasa..
Matendo ya Mitume 2:46
[46]Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,
Matendo ya Mitume 5:42
[42]Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.
Kama tunavyojua majumbani mahali ambapo, pana shughuli nyingi wakimaliza ibada huwenda sherehe zinafanyika hapo, au vikao vya kijamii, lakini hilo halikuwazuia kutimiza makusudi ya Mungu yaliyoyakusudia.
Hivyo yaweza kuwa ni sahihi endapo, hakuna mahali rasmi bado, ibada zinaweza kufanyika kwenye majengo ya shule, kwenye mabwalo, kwenye kumbi,.viwanjani, hata chini ya miti maadamu tu umoja huo upo na nia ni Kristo..hata hivyo yapo makanisa makubwa na yamefanikiwa lakini bado hayana maeneo yao rasmi ya kukutanikia…lakini kanisa Limesimama.
Mambo tu ya kuzingatia, ni nidhani yenu, adabu na utulivu wa mazingira ya kiroho kwa wakati huo,..ikiwa haya yapo hapo Mnapokusanyikia basi Mungu yupo nanyi..wala si dhambi.
Lakini ni busara na vema zaidi kanisa likatafuta eneo rasmi la kukusanyikia litakalokuwa ni kwa shughuli zao tu za kiibada.
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
1Petro 1:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Siku ya kujiliwa ni wakati ambao, Mungu anashuka ulimwenguni, aidha kwa kuokoa au kuhukumu.
Zote mbili ni siku za kujiliwa.
Kwa mfano kwa lengo la kuokoa. Upo wakati ambao neema ya Mungu humjia mtu, au taifa, na hivyo wakati huo mara nyingi uamsho mkubwa huwa unapita, Kwamfano, kipindi cha Kristo, kilikuwa ni kipindi maalumu cha Israeli kujiliwa lakini hawakukubali ..isipokuwa wachache..(Luka 19:41-44)
Lakini kwa lengo la hukumu ni siku ambayo kila mmoja wetu atahukumiwa kulingana na matendo yake.
Hivyo tukirudi kwenye 1 Petro 1:12, inayosema ‘Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa’.
Maana yake, matendo mema ya mwamini, hupelekea watu kuupokea wokovu na kumtukuza Mungu,siku neema yao inapowafikia, kwamfano wapo watu ambapo kwa kukuangalia, kwa kipindi kirefu, siku ya kujiliwa inapowafikia inakuwa ni rahisi kuamini na kumtukuza Mungu, kwasababu walishawahi kuona watu waliokoka walivyo na sifa zao njema, mfano upendo, amani, uadilifu..Lakini ukiwa na mwenendo mbovu, siku yao ya kujiliwa inapowafikia, wakikumbuka mwenendo mbovu waliouna kwako , ni ngumu sana kumtukuza Mungu,
Ndicho ambacho mtume Petro alikuwa anakieleza hata mbeleni kidogo, kuhusiana na Wanandoa, kwa upande wa wanawake, akasema, ikiwa mtu ana mume asiyeamini, anao uwezo wa kumvuta ndani ya Kristo kwa mwenendo wake tu.. (1Petro 3:1).
Kwa ufupi ni kuwa mwenendo wako mwema hulainisha njia ya neema ya Kristo Kutenda kazi vema juu ya mtu.
Mungu akubariki.
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
MILANGO YA KUZIMU.
Jibu: Turejee..
Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao WALIOUDHIWA NA PEPO WACHAFU; nao wote wakaponywa”.
Katika Biblia, neno “Kuchukizwa” au “Kuchukiza” limekuwa na maana zaidi mbili, maana ya kwanza ya kuchukizwa ni ile hali/hisia ya “Kutopendezwa na jambo” inayozaa huzuri, au hasira mfano wa hiyo ni ile iliyompata Bwana Yesu alipokutana na Sauli alipokuwa anaenda Dameski kuwafunga wakristo..
Matendo 9:3 “Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni. 4 Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, SAULI, SAULI, MBONA WANIUDHI? 5 Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, MIMI NDIMI YESU UNAYENIUDHI WEWE. 6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda”.
Matendo 9:3 “Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.
4 Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, SAULI, SAULI, MBONA WANIUDHI?
5 Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, MIMI NDIMI YESU UNAYENIUDHI WEWE.
6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda”.
Hapa inaonyesha ni jinsi gani matendo ya Sauli ya kikatili yalivyokuwa yanamwudhi Bwana.. Lakini pia tunaona mahali pengine pakionyesha Wayahudi walikuwa wakimwudhi Bwana YESU kwasababu alikuwa anafanya miujiza siku ya sabato..
Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi. 15 Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima. 16 Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato. 17 Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi”
Yohana 5:14 “Baada ya hayo Yesu akamkuta ndani ya hekalu, akamwambia, Angalia, umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi.
15 Yule mtu akaenda zake, akawapasha habari Wayahudi ya kwamba ni Yesu aliyemfanya kuwa mzima.
16 Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.
17 Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi”
Sasa si mahali pote katika Biblia neno hilo “kuudhi/kuudhiwa” limemaanisha “kukwazwa au kutopendezwa na jambo fulani” bali sehemu nyingine limemaanisha “KUTESWA”
Mfano wa sehemu hizo ni hapa katika kitabu cha Matendo ya Mitume..
Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao WALIOUDHIWA NA PEPO WACHAFU; nao wote wakaponywa”
Kuudhiwa kunakomaanishwa hapo ni ile hali ya “Kuteswa na Kuonewa” Hivyo hapo Biblia imemaanisha kuwa waliokuwa wanateswa na pepo wachafu walifunguliwa, hali kadhalika mahali pengine panapoonesha kuwa kuudhiwa kunakomaanisha kuteswa ni katika kitabu kile cha Ufunuo 12:13.
Ufunuo 12:13 “Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume”.
Na katika Mathayo 5:10-12 ni Maudhi ya Mateso yanayozungumziwa hapo..
Mathayo 5:10 “Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. 11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. 12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu”
Mathayo 5:10 “Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.
12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu”
Je na wewe unaudhiwa kwaajili ya haki au kwaajili ya Mabaya?…Kama ni kwaajili ya Kristo basi fahamu kuwa thawabu yako ni kubwa mbinguni, lakini kama ni kwaajili ya mabaya, basi tubu leo na mpokee YESU akutoe katika hizo dhiki ambazo hazina faida yoyote bali mwisho wake ni hasara mara mbili katika siku ile ya mwisho.
Je unajua sababu nyingine ya MUNGU kuigharikisha dunia ya wakati wa Nuhu?
Mwanzo 6:12 “Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; MAANA KILA MWENYE MWILI AMEJIHARIBIA NJIA YAKE DUNIANI 13 Mungu akamwambia Nuhu, MWISHO WA KILA MWENYE MWILI UMEKUJA MBELE ZANGU; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.
Mwanzo 6:12 “Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; MAANA KILA MWENYE MWILI AMEJIHARIBIA NJIA YAKE DUNIANI
13 Mungu akamwambia Nuhu, MWISHO WA KILA MWENYE MWILI UMEKUJA MBELE ZANGU; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.
Umeona? Kumbe sababu nyingine ya Mungu kuigharikisha dunia ni “WATU KUHARIBU NJIA ZAO DUNIANI”.
Njia yako ina maana sana kwako na kwa MUNGU, ukiiharibu au mwingine akakuharibia basi na uwepo wako duniani utakuwa hauna maana..
Sasa Kila mtu anayo njia ya MAISHA YAKE duniani, na NJIA kila mmoja haifanani na ya Mwingine..lakini haijalishi njia ya mtu ipoje mwisho wake inapaswa imfikishe mtu katika Amani, Furaha, Utulivu, Ushindi, uchaji wa Mungu na mwisho Uzima wa Milele.
Lakini mtu aliyepoteza uelekeo wa njia yake, basi anakuwa anaishi katika tamaa za ulimwengu, dhambi, maasi na mwisho wake ni hukumu ya Mungu.
Lakini habari njema ni kwamba, haijalishi MTU kapoteza uelekeo kiasi gani, au njia yake imeharibika kiasi gani, maadamu anaishi bado anao uwezo wa kuitengeneza na mapito yake yakawa yamenyooka kabla ya kifo, au hukumu ya Mungu kufika..
Mfano wa mtu katika Biblia aliyetengeneza njia zake kabla ya kufa kwake ni Mfalme Yothamu..
2Nyakati 27:6 “BASI YOTHAMU AKAWA NA NGUVU, KWA KUWA ALIZITENGENEZA NJIA ZAKE MBELE ZA BWANA, MUNGU WAKE. 7 Na mambo yote ya Yothamu yaliyosalia, na vita vyake vyote, na njia zake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda. 8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita huko Yerusalemu. 9 Yothamu akalala na babaze, wakamzika katika mji wa Daudi; na Ahazi mwanawe akatawala mahali pake”.
2Nyakati 27:6 “BASI YOTHAMU AKAWA NA NGUVU, KWA KUWA ALIZITENGENEZA NJIA ZAKE MBELE ZA BWANA, MUNGU WAKE.
7 Na mambo yote ya Yothamu yaliyosalia, na vita vyake vyote, na njia zake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka kumi na sita huko Yerusalemu.
9 Yothamu akalala na babaze, wakamzika katika mji wa Daudi; na Ahazi mwanawe akatawala mahali pake”.
SASA TUNATENGENEZAJE NJIA ZETU?
1. Kwa kulitii Neno la Mungu
Zaburi 119:9 “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? KWA KUTII, akilifuata neno lako”.
Neno la Mungu (kwa ufupi Biblia) ndio taa na mwanga wa njia yetu (soma Zab. 119:105), maana yake tukitaka uelekeo wa maisha tunaupata ndani ya Biblia.
Biblia ni kitabu ambacho kimeelezea kwa ufasaha wote wa rohoni na mwilini namna ya kutembea Duniani, na mtu anayesoma Biblia kwa ufunuo kamwe hawezi kupoteza uelekeo wa Maisha, kwani ndani ya Biblia kuna kanuni za namna ya kupata amani, furaha, utulivu, uvumilivu, ushindi, mafanikio na zaidi sana UZIMA WA MILELE.
Mtu anayeikwepa Biblia na maonyo yake tayari kashajiweka katika hatari ya kuharibu njia yake Duniani, na mabaya yatamfikia tu kwasababu njia yake imeharibika..
Yeremia 26:13 “Basi sasa, tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, mkaisikilize sauti ya Bwana, Mungu wenu; naye Bwana atayaghairi mabaya aliyoyanena juu yenu”.
Ukitaka kufikia Amani ya maisha yako, lisome na kulitii Neno la Mungu, Biblia inaposema usifanye jambo fulani basi usifanye, vile vile inaposema fanya jambo fulani basi tii na kufanya..njia yako ya Amani utakuwa umeinyoosha, vile vile njia yako ya furaha utakuwa umeinyoosha, vile vile njia yako ya mafanikio yako ya rohoni na pia UZIMA WA MILELE, zipo ndani ya Biblia.
Yeremia 7:3 “Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tengenezeni njia zenu, na matendo yenu, nami nitawakalisha ninyi mahali hapa”.
Bwana atusaidie.
Mwanzo 6:11 “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia IKAJAA DHULUMA. 12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani. 13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.
Mwanzo 6:11 “Dunia ikaharibika mbele za Mungu, dunia IKAJAA DHULUMA.
12 Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.
13 Mungu akamwambia Nuhu, Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia”.
Kwa tafsiri ya Kawaida Dhuluma/kudhulumu ni kitendo cha kumnyima au kumpokonya mtu haki yake kwamfano kwamfano umeazimwa pesa na haujairudisha na unao uwezo wa kufanya hivyo, hiyo ni dhuluma.
Au mtu ana haki ya kupata huduma fulani kutoka kwako na humpatii kwasababu binafsi hapo unakuwa unamdhulumu haki yake.. Na dhuluma ya namna hii ni dhambi..
Lakini katika Biblia neno hili Dhulumu limeenda mbali zaidi likijumuisha mambo mengi zaidi ya “kumnyima tu mtu haki yake” bali limejumisha pia “vurugu, uonevu, ubaya na uasi”.
Hivyo Neno dhuluma linapotajwa kwenye Biblia linabeba maana pana zaidi ya tunayoifahamu na kuitumia sasa.. Kwamfano hapo katika Mwanzo 6:11-13 inapotajwa Dhuluma, imemaanisha vitendo vyote vya vurugu, uonevu, maasi, na kuwanyima watu haki zao, na hiyo ndio ikawa sababu ya Mungu kuigharikisha Dunia ya kwanza..
Maandiko mengine yanayotaja dhuluma ni pamoja na Zaburi 55:9-11, Zaburi 82:2, Zaburi 119:78, Zaburi 119:134, Warumi 2:8 na Ufunuo 22:11.
Je umempokea YESU?.. au upo bado unatanga tanga na dhuluma za huu ulimwengu?.. Kumbuka maandiko yanasema Dunia ya kwanza iligharikishwa kwa maji lakini hii ya sasa imewekwa akiba kwa moto, kwasababu zile zile zilizoigharikisha Dunia ya kwanza (yaani ya kipindi cha Nuhu).
2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule ILIGHARIKISHWA NA MAJI, ikaangamia. 7 Lakini mbingu za sasa na nchi ZIMEWEKWA AKIBA KWA MOTO, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.
2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule ILIGHARIKISHWA NA MAJI, ikaangamia.
7 Lakini mbingu za sasa na nchi ZIMEWEKWA AKIBA KWA MOTO, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.
Bwana YESU mkuu wa haki (Zaburi 45:7) ANARUDI!
Maran atha!