Category Archive Home

WATU HAWA WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA HUKU NAKO

Kama tunavyofahamu katika maandiko Mitume walipofika mji wa Thesalonike kwa ajili ya injili, na kukutana na wenyeji wa mji ule, na kusikia walichokihubiri maandiko yanatuambia walipiga kelele sana na kusema maneno haya;

“Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako”

Matendo ya Mitume 17:6

[6]na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Ulishawahi kutafakari kwa ukaribu maneno hayo walichokimaanisha?

Wanasema;

Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Maana yake ni kuwa ulimwengu na wao, ni kama vitu viwili tofauti…

Wamefika na huku pia….yaani wameshaushinda ulimwengu wanakuja na huko kwao kumalizia walichokifanya kule..

Hii ikiwa na maana…mitume walishapata ushindi kabla hata ya kufika maeneo yote…

Kuna mahali pajulikanapo ulimwenguni ambapo tayari walishapashinda.

Sasa huo ulimwengu ni upi?

Chukulia mfano wa dunia ya sasa.. kuna usemi wasemao nchi za Afrika ni dunia ya tatu.. ijapokuwa wote tupo kwenye sayari moja, ujulikano dunia, lakini uhalisia dunia zipo tatu…Zile nchi zilizoendelea sana…Kama vile Marekani, urusi, China, ufaransa..ni dunia ya kwanza… na zile zilizo katika uchumi wa kati ni dunia ya pili na hizi maskini ni dunia ya tatu..

Sasa ikitokea mtu akayapiga hayo mataifa makubwa na kuyateka, maana yake huyo mtu ameiteka dunia, ameipindua dunia…..hata kama hajapigana na haya mengine madogo..lakini ikiwa nguvu zake zimewashinda wale basi hawa wengine ni maji tu.

Vivyo hivyo waamini wa wakati ule walionekana, wanamapinduzi wakubwa sana..kwasababu ushindi wao ulianzia kwenye vichwa.

Sasa huu ulimwengu ni upi?

JIBU: Ulimwengu wa Roho.

Zamani zile dini zilijulikana kama msingi mikubwa sana inayosukuma mielekeo ya mataifa.. hivyo Kristo alipokuja aliweza kuvunja misingi ya imani potofu na dhaifu kuanzia pale pale Israeli mpaka miisho ya dunia. Alileta Nuru duniani ambayo giza lolote halikuweza kulishinda..

Yohana 1:4-5

[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 

[5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. 

Ndio maana kipindi cha injili utaona Wayahudi wengi waliokoka, wapagani wengi wakaacha miungu yao..wakaichoma moto, utaona hata kule Efeso mungu mke aliyeabudiwa ulimwenguni kote (Matendo 19:27), mitume walipofika habari yake ikaishia pale pale, tofauti na zamani manabii walishindana sana na mabaali lakini hawakuweza kuyashinda..kwasababu hakukuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mkuu wa ulimwengu huu(shetani)

Yohana 16:11

[11]kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 

Hivyo ulimwengu wa roho uligeuzwa juu chini, mapepo yaliwakimbia wengi, watu walifunguliwa kwenye vifungo vya giza..makaburi waliwaachia wafu..kila siku watu waliongozeka kumjua Mungu…na kuachana na dhambi.

Matendo 19:19-20

[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. 

[20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. 

Huu ndio ulimwengu sugu uliopata tiba…ulimwengu wa giza, kama kichwa cha mifumo yote mibovu ya dunia…uliwekwa chini…

Hivyo wale watu walipoona imani za watu zinageuzwa kwa kasi hata za maakida wakubwa,(Matendo 13:7-12) majemedari, watu wenye vyeo, wake kwa waume, nao pia wanaigeukia imani..wakatambua ya kuwa kila kitu kimekwisha sasa, sisi ni masalia..tu.

Walijiona kama mapanzi, ni sawa na wana wa Israeli walipoweza kuliangusha taifa la Misri, hata kabla ya kufika Yeriko, Wale watu wenyewe walishajiona kama mapanzi..Kwasababu kichwa cha ulimwengu kimeshaangushwa.

Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tujue kuwa sisi tuliomwamini Yesu…tayari tumeshaupindua ulimwengu kwa Injili iliyokwisha fika kuzimu kwenye kiti cha enzi wa shetani…

Hakuna chenye nguvu ya kutuzuia sisi tena, sisi ni watawala wa dunia.

Wanasiasi, hawawezi kutuzuia, wanadamu hawawezi kutusimamisha..wao ni kama mapanzi tu kwetu…

Hatuna budi kuuinua ujasiri wetu wote…tufikie mataifa yote kuhubiri injili kwasababu ulimwengu tayari tumeshaupindua…hatuhitaji kwenda tena kuupindua..sisi ni kumalizia tu masalia. Unasubiri nini usiamke kuihubiri injili? Amka sasa…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Print this post

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

Kila mwanadamu maadamu amezaliwa na kuishi duniani, ndani yake lazima kuna kiwango tu cha majuto..

Wengine wana majuto makubwa sana, wengine kiasi.

Majuto ni hali ya kuhuzunishwa na matokeo ya machaguzi au maamuzi yaliyofanyika katika maisha.

Kwamfano kijana anaweza kuchagua kukatisha masomo kisha aende mtaani, kuuza peremende, sasa hayo ni maamuzi yake, lakini baadaye anapoona haoni matokeo makubwa, kinyume chake anawaona wenzake waliosoma wamepiga hatua kubwa anaanza kuingiwa na huzuni ya kujishitaki mwenyewe, sasa hayo ndio majuto.

Mwingine amechagua kuishi na mtu bila kufunga naye ndoa, hatimaye akazalishwa, watoto wengi na kuachwa..baadaye umri umeenda anataka kuoelewa, inakuwa shida…anaingiwa na majuto.

Mwingine amepoteza miaka mingi duniani kumtumikia shetani, sasa ameshakuwa mzee anajisikitikiza miaka yake ya ujana aliyoipoteza yenye nguvu alikuwa wapi asimtumikie Mungu…

Majuto yapo ya namna nyingi, na kila mtu kwa sehemu yake anayo majuto fulani, haijalishi unaishi wapi, au umefanikiwa vipi…kuna mahali ulikosea na yakaingia..

Kimsingi majuto sio dhambi, ni hali ya ki-Mungu kabisa ambayo mwanadamu ameumbiwa ndani yake..

Lakini ni vema kujua namna ya kuyaweka mahali pake..kwasababu yasipoweza kutenganishwa ipasavyo hupelekea hasara kubwa mno ndani ya maisha ya mtu.

Katika biblia kulikuwa na watu wawili ambao walihuzunishwa na maamuzi walillyoyafanya …mmoja ni Petro, mwingine ni Yuda.

 Yuda alihuzunishwa lakini huzuni yake ilimpelekea kujinyonga…Petro alihuzunishwa lakini huzuni yake ilipelekea kulilia msaada wa Mungu..(badiliko)

Petro aliruhusu majuto yake yabebwe na Mungu, Yuda aliruhusu yabebwe na shetani.

Lakini majuto yalikuwa yale yale…Yuda hakukosea kujuta hadi kurudisha pesa

2 Wakorintho 7:8-11

[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu. 

[9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. 

[10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. 

[11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo. 

Umeona Majuto ya ki-Mungu huleta toba.. lakini majuto ya shetani hupelekea mauti..

Ukishaanza kujiona kama wewe huwezi tena, Mungu kakuacha, hufai, huna maana, hustahili, ujue shetani yupo nyuma ya juto hilo, ambalo anataka kukusababishia usiinuke tena, ujitenge, ujiue, uache kwenda kanisani, aache maombi, uache kumtafuta Mungu, uache uchungaji …

Kinyume chake unapokosea jione kama ulikuwa unapitishwa katika funzo ambalo sasa unapewa nafasi nyingine usiitmie vibaya…

Watu wengi, unaowaona wamekata tamaa, wamepoa, hawana mabadiliko tena, wamejitenga, lakini hapo zamani walikuwa vizuri, wana mashaka na hofu ya ndani kwa ndani, asilimia kubwa ni majuto mabaya yanawasonga ndani yao.

Daudi alipoanguka katika dhambi ya uzinzi, alimrudia Bwana kwelikweli, ijapokuwa ilimgharimu pakubwa…hakwenda kujificha na uso wa Mungu kama Adamu.

Lakini ya ki-Mungu huturudisha kumtazama Mungu…Rudi umwangalie Mungu wako kisha chukua hatua nyingine, kwani hiyo huwa na nguvu na matokeo ya haraka zaidi ya mwanzo.

Petro baada ya pale alikuwa na ujasiri mkubwa wa kumshuhudia Kristo, zaidi ya mitume wengine wote, ikiwa umefeli mahali fulani embu amka tena kwa nguvu, usikubali kunyong’onyea kama Yuda na mfalme Sauli ambaye alijiua..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MWOMBOLEZAJI.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA

Print this post

IPO NJIA YA MKATO YA KUFIKA KIWANGO VYA MBALI VYA KIROHO.

Maisha ya mwilini mara nyingi hubeba mafundisho ya rohoni, ndio maana Bwana Yesu alitumia sana mifano ya kidunia kuwafundisha siri za ufalme wa mbinguni.

Katika jamii ili mtu aitwe profesa au daktari(kitaaluma) anapaswa awe ni msomi wa kukaa darasani kwa muda mrefu, awe na ujuzi lakini pia na uzoefu wa tafiti nyingi..yaani kwa ufupi haiwezekani ukaitwa daktari(kitaaluma) halafu usiwe msomi wa elimu za juu.

Lakini kuna udaktari ambao mtu anaweza kupewa kwa kutunikiwa, na mara nyingi huu huja pale mtu anapotoa mchango fulani mkubwa katika jamii…mtu kama huyu anaweza kutunukiwa udaktari hata kama yale mafunzo ya ndani ya kitaaluma hana.

Sasa kiroho ni vivyo hivyo unaweza pia ukawa mkufunzi, mwenye ukomavu mkubwa, zaidi ya mababa zako wa kiroho, hata zaidi ya wachungaji wako, au maaskofu wako, au wazee wako wa kiimani, kwa namna gani?

Mstari ufuatao unatupa jibu;

Zaburi 119:99-100

[99]Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote,

Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo. Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.

Ukitafakari huo mistari, utaona ni mwanafunzi anayejisifia kuwa ana akili zaidi ya waalimu wake…sio kwamba ameshahitimu, hapana bado yupo chini ya waalimu wake lakini akili zake zimewapita, bado ni kijana lakini ufahamu wake umeshawazidi wazee wake.

Imewezekanikaje?

JE anasoma sana? Au ana kiwapa cha asili tofauti na wengine? Hapana…anasema kwasababu shuhuda za Mungu ndizo anazozitafakari, lakini pia anayashika mahusia ya Mungu .

Hiyo ndio siri yake, usiku na mchana ni kufikiri juu ya “KWELI”, Yaani Neno la Mungu, na na namna ya kulifanya kuwa sehemu ya maisha yake..(kujiepusha na dhambi.)

Hiyo ndio namna inayomkomaza mtu kiroho kwa haraka sana kuliko hata maarifa mengi ambayo wengi hudhani, au mafunuo mengi, au kuhubiri kwingi, au kufundisha kwingi…

Mtu mmoja anaweza akawa na uelewa mkubwa, mwalimu mzuri, mtume mwenye ushawishi mkubwa, lakini bado asimkute mwanafunzi wake ambaye maisha yake anajitahidi kuliishi Neno la Mungu.

Hivyo ndivyo Mungu anavyowatambua wakufunzi wake (kiroho), uwezo wa “kumcha Mungu” haijalishi utapoteza sifa nyingine zote za maarifa,mafunuo, lakini akiwa na hiyo huyo amefika mbali sana.

Kwasababu Biblia inasema hakuna mwisho wa usomi, (kujua maarifa), ila mtu akizingatia kumcha Mungu na kuziishika amri zake, ni zaidi ya usomi wa vitabu vyote.

Mhubiri 12:12-13

[12]Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili.

[13]Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa;

Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

Tuwekeze nguvu zetu zote katika kuliishi Neno na neema ya Mungu itusaidie..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JE! UNATAKA UITWE MSOMI NA MUNGU?

USIKWEPE CHUO CHA UTAKATIFU.

HAWEZI KUWA MWANAFUNZI WANGU.

Print this post

KAMA NISIPOKUTAWADHA, HUNA SHIRIKA NAMI

Nakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima

Tengeneza picha Mungu amekutokea amesimama mbele yako, wakati ukiwa na mawazo ya kumwangukia chini umsujudie, unashangaa yeye moja kwa moja anakuwa wa kwanza kuinama na kukusafisha miguu yako…

Hivi utajisikiaje? Ukweli ni kwamba hutajisikia huru hata kidogo, kwa ufupi hutakubali kitendo hicho kifanywe na yeye kutoka na ukuu wake, na heshima yake iliyozidi vyote, ni sawa na uone baba amemnunulia mtoto wake zawadi halafu yeye ndio anayekuwa wa kwanza kumshukuru mtoto, tena kwa kumwinamia..ni wazi kuwa hilo halijakaa sawa, au mtu aliyeibiwa mali zake nyingi, halafu amekutana na aliyemwibia badala ya mwenye mali kungojea kuombwa msamaha, yeye ndio anajionyesha kama ni mkosaji kwake…unaona ni jambo ambalo halina uhalisia, halikubaliki kifikra hata kidogo…

Kwa namna ya kawaida hali kama hizi akitendewa mtu hawezi kuridhia…lakini Mungu anatutendea sisi na anasema kama hutakubali kutendewa naye hivyo kamwe hutuna ushirika naye.

Ndicho kilichotokea kwa mitume na Petro. Wakati ule walipomwona Bwana Yesu, anashika kitambaa na maji kisha akaanza kuwaosha na kuwapangusa miguu yao…Petro hakuweza kuridhia akasema Bwana hutanitawadha miguu kamwe. Lakini Yesu akamwambia usipokubali huna ushirika nami.

Yohana 13:8

[8]Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami. 

Hii ni kufunua nini…

Ni lazima tumjue Kristo, ni kweli anasimama kwetu kama mfalme, kama Bwana, kama Mungu…tunamwabudu…lakini pia anasimama kama mtumishi wetu..Ni jambo ambalo hatuwezi kuingia akilini  lakini ndivyo alivyo, amependa yeye kuwa hivyo kwetu.

Ni mfalme mwenye taji la kifalme lakini wakati huo huo pia mfalme aliyebeba kitambaa cha kuwasafisha watu miguu.

Hiyo ndio sifa ya ufalme wake. Amesimama kama muumba wetu tumwabuduye, lakini pia anatutumikia, katika kutuponya magonjwa yetu, kutulisha, kutuvisha, kutuombea, kutulinda, kutufuta machozi, na kuchukua mizigo yetu mfano wa punda na hata kufanya mambo ambayo sisi hatuwezi stahimili akitufunulia yote kwa jinsi anavyojishusha na kujishughulisha sana na mambo yetu…. Na mfano tukitataa yeye asituhudumie hivyo anasema wazi kuwa hatuna ushirika naye.

Maana yake ni fahari yake kututendea hayo, wala yeye hayahesabu kuwa ni kitu.

Anatufundisha nini?

Tuwe watumishi pia wa wengine kwa namna hiyo, kama yeye alivyo kwetu…kujitoa kwake sio kutimiza wajibu bali ni fahari yake ambayo isipokubaliwa inaharibu moja kwa moja mahusiano.

Kumsaidia mpendwa mwenzako iwe ni furaha..kujinyenyekeza kwake isiwe ni sababu za umri au cheo bali fahari..Kumwombea iwe ni fahari yako, kumsikiliza iwe ni furaha yako…hivyo ndivyo Bwana anavyotaka.. na ndivyo alivyomwambia Petro.

Yohana 13:12-17

[12]Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea? 

[13]Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo. 

[14]Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi. 

[15]Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo. 

[16]Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka. 

[17]Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda. 

Neema ya Bwana itusaidie.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WEWE NI ZAO LA MAHUSIANO NA USHIRIKA.

USHIRIKA WA ROHO MTAKATIFU UKAE NANYI NYOTE.

WENGINE WANAKESHA KWAAJILI YAKO.

Print this post

Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu.

Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu

Wimbo ulio bora 2:15

15 : Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.

Kitabu cha wimbo ulio Bora ni kitabu kinachoeleza asili ya upendo wa Kristo kwetu na jinsi tunavyopaswa kuuitikia.

Kuwa urefu wa masomo yaliyo nyuma ya kitabu hiki fungua hapa >>> NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

Lakini kwenye mstari huu, tunaona ni kama vile mtu kwa lugha ya picha anaona mbweha “ Wadogo” wamevamia shamba lake la mizabibu inayochanua na hivyo hawapuuzii kwasababu ya udogo wao, bali anatoa tamko la kukamatwa na kuondolewa…ili shamba lake linalochanua liwe salama.

Kimsingi mbweha si mnyama anayekula nyama tu, bali hula pia mizazibu, na mingine kuiharibu.

Hii ni kufunua nini katika hali zetu za rohoni.. 

Adui akishaona mahusiano Yetu na Kristo yanazaa matunda, huinua vitu Vidogo vidogo ili kuharibu mahusiano wakati mwingine unaweza usione kama vina madhara sana au vina nguvu sana, lakini katika eneo la kiroho kitu kidogo kina nguvu sawa na kitu kikubwa…

Hivi ndio vinavyoitwa mbweha wadogo..

Mambo Kama haya ni kama vile kuendekeza vishawishi vya dhambi kwenye maisha yako.

Kwa mfano wewe ni binti halafu kila siku unaona wanaume wanazungumza na wewe maneno ya mizaha, sasa kama usipokemea tabia hiyo, ukaona ni kawaida, tabia hizo ndogo ndogo ndizo zinazopelekea mtu baadaye kuanguka kwenye dhambi za uzinzi.

Samsoni, alipoona ushawishi wa delila unaendelea, badala aukatishe yeye akapuuzia mwisho wa siku akatekwa..

Hao ni mbweha wadogo wanaoharibu shamba lako, kila kichocheo na kishawishi kiwe kidogo kiasi gani usikipuuzie.

Wakati mwingine kuendekeza uvivu wa kiroho, yaani kupuuzia maombi, kupuuzia ibada, kidogo kidogo hupelekea kupoa kiroho, na hatimaye unajikuta kabisa umerudi duniani..mpaka unajiuliza nimefikaje hapa? Ni kwasababu uliendekeza uvivu wa kiroho..ulisema. nitaomba kesho, nikesha kesho, nitamtumikia Mungu mwezi ujao..mwishowe ukawa hivyo ulivyo leo…

Angalia ni eneo lipi la maisha yako limevamiwa na hawa mbweha wadogo, kisha chukua hatua za haraka kurekebisha.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Mwandishi wa kitabu cha wimbo uliobora.

Nini maana ya Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, (Wimbo 2:7)

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?


 

Print this post

Kuba ni nini kibiblia?

Kuba ni kitu chenye umbo la duara kinachofunika kwa juu, ni kama paa lililopinda. Lenye mwonekano unaofanana na nusu ya mpira au bakuli lililogeuzwa juu chini.

Mifano ya kuba:

unaweza kuona kwenye ujenzi wa Misikiti mingi na baadhi ya Makanisa na majengo ya kale

Tukirudi kwenye biblia Enzi za kale, ilidhaniwa kuwa dunia ina kuba kwa juu, yaani kifuniko. Ambao ndani yake jua, mwezi na nyota hutembea..

Neno hilo utalisoma katikq vifungu hivi; 

Ayubu 22:14

[14]Mawingu mazito ni kifuniko chake, hata asione; 

Naye yuatembea juu ya kuba ya mbingu. 

Amosi 9:6

[6]Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; BWANA ndilo jina lake. 

Kumbuka, ujumbe unaowasilishwa hapo ni kueleza ukuu uliozidi wa Mungu, katika uumbaji wake na mamlaka yake.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya Israeli?

Binti za Yerusalemu wanaotajwa katika kitabu cha Wimbo ulio Bora 1:5 ni akina nani?

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

UNAJISIKIAJE, KUTEMBEA NA SANDA?

Print this post

Nini maana ya Israeli?

JIBU: Maana yake ni “yeye ashindanaye na Bwana”

Siku ile Yakobo alipotokwa na Mungu, kisha akashindana naye usiku kucha bila kumwacha, ndipo yule mtu akamuuliza jina lako nani, akasema Yakobo, akaambiwa hutaitwa tena hilo jina Yakobo, bali Israeli.

Mwanzo 32:28

[28]Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.

Au kwa namna nyingine tafsiri yake ni

“mtu anayeng’ang’ana na Mungu mpaka kuona matokeo”

Ndio jina ambalo kabila zake zote ziliitwa. Leo hii tunaposema taifa la Israeli, tunamaanisha taifa la washindanaji.

Lakini Israeli kwa agano jipya si hii ya mwilini tu.. bali ile ya rohoni ambayo imeundwa na Yesu Kristo mwenyewe..

Warumi 2:28-29

[28]Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;

[29]bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.

Maana yake ikiwa umempokea Kristo, wewe tayari ni mwisraeli/myahudi.

Na kama ni mwisraeli, jua asili ya jina lako..kuwa wewe ni mtu wa kung’ng’ana na Mungu…sio mtu mwepesi mwepesi…

Usimrajie Mungu katika vitu virahisi rahisi, huyo ndio sababu kwanini tunakuwa na mifungo na mikesha, kudumu uweponi mwa Bwana wakati mwingi, kumtafuta Bwana, sio kwamba yeye ni mgumu kupatikana hapana, bali kwa asili hataki wana walioitwa kwa jina hilo wawe walegevu,

Wengi hulalamika, mbona sioni uwepo wa Mungu, mbona sioni amani ya kutosha ndani, siono furaha ya wokovu, ukiwauliza vipi juhudi yako rohoni…mmoja atasema ratiba yangu huwa ni maombi ya dk 10 kwa siku, kusoma Neno dk 10.. Sasa mtu kama huyu hawezi kuhudumiwa vema na Mungu ikiwa ameokoka…

Ndugu jitambue wewe ni nani! Ikiwa ni mwisraeli, simama kama mtu shupavu kung’ang’ana na Mungu wako, nje ya hapo, tafuta jina lingine na mungu mwingine mwenye vigezo vyake vya kukuhudumia, lakini kama ni waisraeli wa Kristo, basi ni watu wa kuliitia jina la Bwana bila kukoma (Luka 18)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA UKOMBOZI?

Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?

PALE MAOMBI YANAPOGEUKA KUWA MAPAMBANO.

Print this post

Njumu ni nini? (Wimbo 3:10)

Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa urujuani, GARI LAKE LIMENAKISHIWA NJUMU, Hiba ya binti za Yerusalemu”.

Neno hili pia tunalisoma katika 1Nyakati 29:2..

1Nyakati 29:2 “Basi kwa uwezo wangu wote nimeiwekea akiba nyumba ya Mungu wangu, dhahabu kwa vitu vya dhahabu, na fedha kwa vitu vya fedha, na shaba kwa vitu vya shaba, na chuma kwa vitu vya chuma, na miti kwa vitu vya miti; vito vya shohamu, na vya kujazia, VITO VYA NJUMU, na vya rangi mbalimbali, na mawe ya thamani ya kila namna, na marimari tele.

“Njumu” ni malighafi za “kung’ara ng’ara/ kuwaka-waka” Tazama picha juu, mfano wa vazi lililonakshiwa na Njumu..

Na gari la Mfalme Sulemani kulingana na maandiko hayo ya Wimbo 3:10, lilikuwa limenakshiwa na malighafi hizo za kung’ara ng’ara, hivyo lilikuwa linavutia sana, lakini pamoja na kunakshiwa kwa vito hivo vyote vya thamani lakini bado sifa za binti Yerusalemu zilikuwa bora zaidi.

Kufahamu kwa kina Gari/Machela ya Sulemani jinsi ilivyokuwa na rangi ya Urujuani ilikuwaje fungua masomo chini ya somo hili, Bwana akubariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Print this post

Binti za Yerusalemu wanaotajwa katika kitabu cha Wimbo ulio Bora 1:5 ni akina nani?

Swali: Katika kitabu karibia chote cha Wimbo uliobora tunaona wakitajwa sana Binti za Yerusalemu je, hawa walikuwa ni mabinti wa aina gani?..au ni wa mji wa Yerusalemu kama Biblia inavyosema hapo?

Jibu: Turejee..

Wimbo 1:5 “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, ENYI BINTI ZA YERUSALEMU, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.”

Sehemu nyingine Biblia inawaasa hawa Binti za Yerusalemu kutoyachochea mapenzi ..

Wimbo 2:7 “Nawasihi, enyi BINTI ZA YERUSALEMU, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Sasa swali hawa Binti za Yerusalemu ni akina nani?

“Binti za Yerusalemu” au kwa lugha nyingine “Binti Sayuni” ni lugha ya mithali inayowakilisha “Jamii nzima ya watu wa Israeli”… na si Mabinti waliopo Yerusalemu tu peke yao..la! bali jamii yote ya wana wa Israeli.

Turejee maandiko yafuatayo ili tuweze kulielewa hili vizuri…

Zekaria 9:9 “Furahi sana, EE BINTI SAYUNI; piga kelele, EE BINTI YERUSALEMU; Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda, Naam, mwana-punda, mtoto wa punda.”

Unabii huu ulimuhusu Bwana YESU kipindi anaingia Yerusalemu, ambapo jamii ya watu wote walipomwona walikata majani ya mitende na kutandaza njiani ili apite..

Yohana 12:15 “Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;

13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, HOSANA! NDIYE MBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA, MFALME WA ISRAELI!

14 Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,

15 Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.

16 Mambo hayo wanafunzi wake hawakuyafahamu hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kwamba ameandikiwa hayo, na ya kwamba walimtendea hayo”.

Umeona hapo?.. waliooimba Hosana! Hosana! si tu mabinti waliokuwepo Yerusalemu bali “ni jamii yote na marika yote!”.. ikifunua kuwa Binti za Yerusalemu ni jamii nzima wa Israeli, kuzidi kulithibitisha hilo soma pia Mika 4:8, 2Wafalme 19:20-21, Isaya 37:22, na Isaya 62:1.

Na sisi kama wakristo (wakike na kiume) tunahesabika kama Israeli ya Rohoni, hivyo sisi sote pasipo kujalisha jinsia zetu, marika yetu wala nafasi zetu, maadamu tu tumempokea YESU tunafahamika kama Binti Sayuni, au Binti za Yerusalemu.

Na Biblia inatuonya Binti za Yerusalemu, mji wa Mungu tujiepushe na dhambi, hususani Uasherati wa rohoni na mwilini.

Uasherati wa rohoni ni ibada zote za sanamu.. Je umempokea BWANA YESU KRISTO?.

Fahamu kuwa hizi ni siku za Mwisho na YESU amekaribia sana kurudi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DANIELI: Mlango wa 2

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

JE UMEJIFUNZA ULE WIMBO MPYA?

Print this post

WEWE NI NANI PALE AMBAPO WATU HAWAKUONI?

Tunasahau sana maisha yetu ya sirini, na kuweka nguvu kubwa, katika kuonekana kwetu kwa  nje mbele za watu, hatujui kuwa Darasa kubwa la Mungu kwa mwanadamu lipo katika maisha yake ya sirini.  Na Mungu humlipa mtu kwa hayo na si mengine.

Mathayo 6:4….na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Kujazi maana yake ni kulipa.

Ikiwa na maana, unayoyatenda sasa iwe ni mema au mabaya kwa siri, malipo yake utayaona baadaye kwa wazi.

Yusufu, kabla ya kuwekwa kuwa msimamizi wa mali yote ya Farao, alitumika kama wakili mwaminifu katika nyumba ya potifa, kwa muda mrefu. Baadaye Mungu akamlipa kwa kumpa Misri yote.

Yuda mpaka kuingiwa na shetani, hadi kumuuza Bwana wake, ni matokeo ya wizi aliokuwa anaufanya kwa siri kwa muda mrefu.

Daudi kabla ya kujazwa mafuta ya kumwangusha Goliathi, ni maisha ya sirini ya Imani aliyokuwa anayadhihirisha kule maporini kwa Mungu wake, mbele ya simba na dubu walipokuwa wanakuja kulishambulia Kundi. 1 Samweli 17:34-37)

Vilevile, kwa mtu yeyote yule, kupata kibali, kutumiwa na Mungu, kuinuliwa viwango vya kiroho..hutegemea sana hali zetu za sirini zinazoendelea sasa, Kwamfano utakuta labda huyu ni mwanakwaya, au mtumishi wa Mungu, lakini katika maisha yake ya sirini, anajichua, ni mzinzi, anakunywa pombe, Lakini kwa nje, anajionyesha kuwa ni mwema, anautunza ushuhuda wake, anavaa mavazi ya kujisitiri, anaongea kwa staha, ana juhudi katika utumishi, akidhani kuwa hilo ndio litamshawishi Mungu kumwongezea neema.

Ukweli ni kwamba hapo anapoteza nguvu, kwasababu tusipokuwa waaminifu katika madogo ya sirini, Bwana Yesu hawezi kutuaminisha katika makubwa.. Tabia mbaya za sirini, zinaharibu huduma zetu, utumishi wetu wa baadaye.

Mtu anataka apandishwe labda cheo kazini, lakini katika nafasi hiyo hiyo ya chini, anaiba,  mwingine anataka apewe cheo lakini pale pale alipo hawajali watu walio chini yake, ni mwenye wivu, . Unategemea vipi Mungu amlipe mtu kama huyu?

Kabla hujalipwa na Mungu, unakuguliwa kwanza na Mungu.

Shughulika na maisha yako ya binafsi ya sirini, kwasababu hayo ndiyo yanayokueleza utakuwa nani mbele za watu baadaye.

Nini cha kufanya..

Mwalike Bwana, akuchunguze, sirini mwako, Mawazo yako, tabia zako, matendo yako. Kisha mwombe akuponye, na baada ya hapo anza kutendea kazi uliyoyaomba.

Simamia andiko hili;

Zaburi 139:23-24

23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu;
24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.

NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

Print this post