SWALI: Sheria ya uhuru ni ipi inayozungumziwa na mtume Yakobo kulingana na maandiko?
Yakobo 2:11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. 12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.
Neno hili pia utaliona likitajwa na mtume Yakobo katika vifungu vingine vya juu.
Yakobo 1:25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.
Katika biblia zipo sheria kuu mbili
Sheria ya dhambi na mauti ndio ile ya torati, ambayo kazi yake kubwa ni kufichua uovu, kushtaki makosa, lakini haimfanyi mtu kuwa huru, kwa mfano sheria inasema usizini, mtu atakataa kuzini, sio kwasababu hapendi uzinzi, lakini kwasababu sheria imesema tu hivyo, anaogopa adhabu atakapotenda hiyo dhambi atauawa.
Lakini sheria ya Roho wa uzima, ni sheria ya Mungu, isipokuwa hii mtu anavuviwa na Roho Mtakatifu, nguvu ya kuisha sawasawa na matwaka ya Mungu, bila shuruti Fulani, ni ya uhuru. Mfano labda sheria inasema usiue, mtu haui sio kwasababu sheria imesema, lakini kwasababu moyoni mwake hiyo nia, tamaa, au kiu ya kuua haipo, hivyo hata kama sheria isingesema hilo jambo lisingekubalika ndani yake, Hivyo mtu kama huyu tunasema ni huru na sheria, hayupo ki-sheria, sheria haimtawali ijapokuwa sheria yenyewe ipo.
Mtu ukishaokoka, anakutana na sheria mpya ya Mungu, ambayo hiyo ni lazima ifuatwe na ishikwe, lakini inakuwa ya uhuru, sio tena ya kifungo, kwasababu Roho Mtakatifu anamsaidia huyo mtu kuuishi..
Ndio hiyo inayoitwa sheria ya uhuru, kwenye kitabu cha Yakobo.
Maana yake ni nini? Sisi kama waamini, Mungu anatarajia tuonyeshe matunda ya Imani yetu katika upendo, huruma, na matendo mema, kwasababu tunaye Roho.
Hivyo inapotokea, hayo hayaonekani, sheria itatuwajibisha, kutuhukumu, au vinginevyo hatukipokea sheria hiyo ya uhuru.. Ni sawa, na mtu aende kuua watu ovyo bila sababu yoyote,
Mtu huyu atahukumiwa, sawa tu na yule ambaye amesukumwa na sababu fulani, labda kisasi, hasira, wivu, chuki n.k.,
Hivyo sisi waamini, tulipokuwa huru na dhambi, hatupaswi kufikiri kuwa ndio tuna uhalali wa Kutenda dhambi. Kinyume chake, tujue kuwa ipo sheria yetu ya uhuru, itakayotuhukumu, kama tu vile wale wengine walivyohukumiwa kwa sheria ya dhambi na mauti (torati).
Ndicho alichokisema mtume Yakobo..
Kwa hitimisho ni kuwa sheria ya uhuru, ni sheria tunayoitimiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Ambayo hiyo pia itatuhukumu. Hivyo wewe kama mwamini, hakikisha wokovu wako unathibitika kwa kazi zake njema, chini ya upendo
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29)
Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?
Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)
Print this post
Kitabu cha Waraka wa kwanza wa Yohana ni kitabu ambacho kilielekezwa mahususi kwa makundi matatu (3) ya watu, Watoto, vijana, na Wababa. Sasa sio Watoto au vijana au wababa kimwili, Hapana, bali alikuwa anazungumzia ngazi hizo katika roho, yaani Kundi la Watoto kiroho, vijana kiroho na wababa kiroho.
1Yohana 2:12-14
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
Na kila mmoja wao ameelezwa sifa zao, zinazowafanya wawe vile. Kwamfano Watoto kiroho, anasema ni kwasababu wamesahewa dhambi, lakini pia wamemjua Baba, tafsiri yake ni nini? Kwa mtu ambaye ni mchanga kiroho, anapokuja kwa Kristo, jambo la kwanza, ambalo atalipitia kwenye maisha yake, ni kutuliwa mizigo, mizito ambayo alikuwa anasumbuka nayo, ambayo asili yake ni dhambi. Ndio hapo ataanza kujiona mwepesi, anapokuja kwa Kristo, anajiona huru, katika kifungoni, anajiona na amani ambayo hajui chanzo chake ni nini, anajiona anapendwa,..Na ndivyo ilivyo upendo wa Mungu kwa huyu mtu unakuwa wa kipekee sana, ndio sababu kwanini anasema nimewaandikia nyinyi Watoto wadogo kwasababu mmesamehewa dhambi zenu, na mmemjua Baba. Hayo ni mambo mawili ambayo walio wa changa kiroho hujapitia.
Lakini kwa vijana, anasema nimewaandikia kwasababu mmemshinda yule mwovu. Hatua hii ya ujana ni ya kipindi cha ukuaji kiroho, hapa mara nyingi mwamini hukutana sana na majaribu ya shetani, mapingamizi makubwa, vita vya kiimani, misukosuko kwa sababu ya Kristo. Kiroho mtu kama huyu huitwa kijana, kwasababu wakati huu, ijapokuwa atasongwa lakini huwa haachi kumng’ang’ania Mungu, moto wake hauzimiki, hata kidogo, kama ni maombi, kasi huwa ni ile ile,usomaji Neno haupungui, hata akiumwa haiwi vyepesi kumwacha Mungu, kwasababu ni wakati wa Nguvu za Mungu nyingi Kutenda kazi ndani yake, na kumshinda mwovu kotekote.
Lakini Wababa kiroho, sifa yao pia ni tofauti na hao wengine, Sifa yao ni kuwa “ wamemjua yeye aliye tangu mwanzo”.
Maana yake ni nini? Kwanini hasemi kwasababu mmehubiri sana?, au kwasababu mmedumu sana ndani ya Kristo? Bali kwasababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo?
Kumfahamu Mungu, tangu mbali, ni kigezo kikuu sana cha ukomavu rohoni. Mpaka mitume kuitwa baba zetu, ni kwasababu walipewa kumwona Mungu kutokea mbali, tofauti na waandishi na makuhani..Ndio maana waraka tu huu ulipoanza anasema..
1Yohana 1:1 Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima;
Hili lilikuja kudhihirika pale Yesu alipoanza kuwaeleza mambo yake mwenyewe aliyoandikiwa tangu, Torati ya Musa, Zaburi na Manabii, jinsi alivyokuwepo na watu wake, jangwani, kupitia ule mwamba, Mana, nyoka wa shaba, jinsi alivyo mtokea Ibrahimu kama Melkizedeki, jinsi alivyojidhihirisha kwao kwa namna mbalimbali kupitia tumbo la Samaki kwa Yona n.k. lakini hawakumwelewa.
Luka 24:44
44 Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. 45 Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko.
Sasa, mtu akishamwona Mungu kwa namna hiyo, basi Mungu kwake hawi wa “matukio” bali wa wakati wote. Yaani alikuwa nasi jana, yupo nasi leo, na atakuwa nasi hata milele.. Watoto wachanga kiroho, hawawezi kumwona Mungu jana, wenyewe Mungu wao, ni wa matukio ya leo.
Maeneo matatu ambayo macho yako yanapaswa yafunguke kuhusu, kumjua Mungu tangu mwanzo.
Hivyo ile uwe Baba, ni lazima umjue Mungu aliyekuwepo tangu Mwanzo, usiwe mtu wa matukio ya leo leo, kama mtu uliyeokoka jana, Kaa chini, tafakari sana, hatua moja baada ya nyingine ya maisha yako, anzia kwenye maandiko uone jinsi Mungu alivyokuwa na watu wake tangu zamani, ambao wengine kwa kukosa kumjua wakawa wanalalamika tu, wanaishi kiwepesi wepesi, na hatimaye kumsulibisha, lakini wale waliomjua waligeuzwa na kuwa mitume wake,
Kuwa baba rohoni.
Mungu akubariki.
Shalom.
Je umewaonea utungu watoto wako?
Kwa jina lake Ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.
LAKINI SISI HATUKUIPOKEA ROHO YA DUNIA.
SWALI:Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.mfano “We kenge njoo hapa”, kama YESU alivyo tumia mbweha katika
luka 13:32.
JIBU: Katika biblia tunaona watu wakiitwa kwa majina mbalimbali ya wanyama mfano mbwa mwitu (Mathayo 7:15), kondoo(Yohana10:27), nyoka(Mathayo 13:34). Lakini pia mbweha, Njiwa, nguruwe, Simba, mbuzi.
Sasa ni vema kufahamu makusudio ya watu/jamii kuitwa hivyo yalikuwa ni nini, hayakuwa kwa lengo la kutukana, au kukejeli, au kudharau..
Hapana Bali kwa lengo la kuonyesha tabia ya mtu, jinsi ilivyo hilo tu.
Kwamfano Yesu alipomuitwa Herode Mbweha, hakuwa na kusudi la kumtukana, au kumdharau, bali alikuwa Anaeleza tabia zake zilizo mfano wa mbweha, ambaye anatabia ya kuvizia na kurarua wanyama wadogo na kuwaua. Maana hivyo ndivyo Herode alivyokuwa, jambo lililoonekana Hata kwa baba zake Kipindi Yesu anazaliwa walimwinda ili wamuue.
Sasa Ikiwa mtu atajulikana kwa namna kama hiyo, kibiblia sio tusi.
Lakini kinyume chake watu hutumia Majina ya wanyama kuwatukana Wengine, au kuwaabisha, au kuonyesha dharau kinyume chao, chuki au hasira, hayo biblia imekataza…na ni dhambi
Kusema “wewe kenge njoo hapa”..Moja kwa moja kauli hiyo inaonyesha chanzo chake ni hasira, dharau au chuki.
Waefeso 4:29
[29]Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.
Wakolosai 3:8
[8]Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.
Mathayo 5:22
[22]Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.
Hivyo chunga kinywa chako. Kila Neno ulisemalo pima makusudi yaliyo nyuma yake.
VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.
JAWA SANA MOTO ULAO
USIWAOGOPE WAZAMZUMI
SWALI: Naomba kufahamu tunaposema Bwana Yesu asifiwe tunamaanisha nini? Na ni nani anayepaswa kuisema hiyo salamu, na kwanini wengine wanasema ‘shalom’ badala yake?
JIBU
‘Bwana Yesu asifiwe’ ni kauli inayotangaza kustahili kwa Yesu sifa kwa ile kazi njema aliyoifanya Hapa duniani.
Yesu ndiye Mtu pekee ambaye alikubali kuingia gharama ya kuacha enzi na mamlaka Mbinguni, na kuja kuishi hapa duniani kwa kusudi moja tu la kutukomboa sisi,katika dhambi zetu, akateswa na kujaribiwa sana, akafa baadaye akafufuka na hata sasa yupo hai ameketi kama mpatanishi wa sisi na Mungu,..
Kiasi kwamba kwa kupitia Yeye tunapokea msamaha wa dhambi, tunaponywa magojwa, tunamseta shetani, tunabarikiwa, tunawasiliana na Mungu moja kwa moja bila vikwazo vyovyote kwa damu yake.
Mtu Kama huyu ni lazima astahili kusifiwa..ndio maana inakuwa ni salamu ya Wakati wote BWANA YESU ASIFIWE..
Kwasababu ya nuru tuliyo ipata kwa kazi yake njema ya ukombozi.
Je ni nani anayepaswa kuisema?
Hakuna mtu anayekatazwa kuisema, lakini mtu asipojua kwanini Yesu asifiwe basi anaisema kwa unafki, Na Mungu hapendi unafiki. Kwamfano mtu ambaye hajaokoka, halafu anasema Bwana Yesu asifiwe, ni sharti ajiulize asifiwe kwa lipi wakati hakuna chochote kilichofanya na yeye katika maisha yake..
Ni sawa na mtu aliyeokoka aseme shetani asifiwe.. atasifiwa kwa jambo gani hapo wakati hakuna ushirika wowote alio nao na shetani. Lakini mganga wa kienyeji Akisema hivyo hiyo ni kweli kwasababu kuna faida amezipata Kwa shetani.
Salamu hii pia, au kauli hii, ni sahihi kutumika katika matamshi ya kiibada..mfano kwenye mahubiri, mafundisho, nyimbo, maombezi N.k. kwasababu katika Maeneo haya kazi za Yesu hudhihirishwa.
Lakini shalom Ni neno la kiyahudi linalomaanisha ‘Amani’. Ni Neno ambalo mtu yeyote anaweza kulitumia awe ameokoka au hajaokoka kwasababu ni Neno la kilugha zaidi kuliko kiimani. Ni sawasawa na sisi tunavyosema, ‘habari yako’. Mtu yeyote anaweza kutumia hilo neno. Lakini Bwana Yesu asifiwe ni Neno la kiimani ambalo anayestahili kulitamka ni mtu aliyemwamini Yesu tu.
WhatsApp
Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.
Sasa Makosa kama haya,(ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.
Tutakwenda kuona aina tano (5) vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. [2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. [3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. [4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. [6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’
Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).
Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…
Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.
Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.
Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.
Mwanzo 4:10-13
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. [11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; [12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. [13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia
Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao
Kutoka 3:7-9
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; [8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. [9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.
Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.
Ufunuo 6:9-10
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. [10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.
Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.
5) Kilio (Shangwe) cha waovu.
Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kubwe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.
Mwanzo 18:20-21
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, [21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.
Je! Umemwamini Yesu?
Je una uhakika kubwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.
Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)
ENDELEZA UPONDAJI.
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
Swali: Tunasoma katika Yohana 1:29 kuwa Yohana anamshuhudia Bwana YESU kuwa yeye “mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu”.. Lakini tukirudi katika Mathayo11:3 tunasoma tofauti, Yohana anawatuma wanafunzi wake wamwulize kama yeye ndiye Kristo au wamtazamie mwingine, sasa swali ni je Yohana alimtilia shaka Bwana Yesu au hakumwamini tangu mwazo?.
Jibu: Ni ngumu imani ya Yohana kutikisika kirahisi lakini hebu kwanza turejee kitabu cha Mathayo…
Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza, 3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine? 4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; 5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 6 Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami”.
Ni kweli Masihi ajaye alikuwa ametabiriwa kuwa atakuja na nguvu kuwaokoa Israeli na utumwa wa maadui zao, na Israeli wote walitazamia kabisa kuwa Kristo atakayekuja atawafungua na utumwa mgumu wa warumi.. lakini haikuwa hivyo kwa YESU KRISTO, kwani alianza kushughulika na dhambi za wana wa Israeli, zaidi ya Taifa.. Hiyo ikawafanya baadhi ya watu kumtilia mashaka YESU kama yeye ndiye KRISTO (Yaani Masihi).
Na bila shaka Yohana hakuwa na wasiwasi wa YESU kuwa Masihi, kwani tayari alishaonyeshwa wakati anambatiza YESU kuwa Yule atakayembatiza na ishara ya hua ikionekana juu yake basi huyo ndiye Masihi, na ni wazi kabisa Yohana alijua kuwa wakati wake aliokuwa anaishi duniani, Kristo naye alikuwa anaishi, ila hakumjua ni nani mpaka wakati wa ubatizo, Roho kama Hua aliposhuka juu ya Bwana, na mbingu kufunguka. (Mathayo 3:16-17).
Sasa kama ni hivyo ni kitu gani kilichomfanya Yohana Mbatizaji atume wanafunzi wake kwa YESU na kumwuliza swali ambalo tayari alikuwa na jibu lake?.
Jibu ni kwamba baadhi ya watu ikiwemo wanafunzi wake Yohana bado hawakuwa na uhakika wa moja kwa moja kama YESU ndiye KRISTO, kwahivyo kwa kusikia Neno linalotoka moja kwa moja kinywani mwa YESU, ingeweza kuwafanya waamini zaidi, hivyo Yohana lengo lake huu ni wanafunzi wakasikie na kujihakikishia wenyewe, kwamaana muda wake wa kuishi ulikuwa umekaribia kuisha na watakayebaki naye ni YESU. Na walipokwenda walipata majibu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Yohana hakuwa na mashaka na Bwana YESU, bali wanafunzi wake na baadhi ya watu, na hiyo ni kutokana na kwamba Bwana YESU hakuwa anajitangaza hadharani kuwa yeye ni KRISTO.
Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi”.
Soma pia Luka 22:77..
Je umempokea YESU?.. Una uhakika kwamba YESU akirudi leo utakwenda naye?.. kama bado upo nje ya Imani fahamu kuwa upo hatarini sana, hivyo mkaribie YESU leo usamehewe dhambi zako na upokee ujazo wa Roho Mtakatifu. Shalom.
Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)
NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?
“Hakuna aniulizaye unakwenda wapi”, maana yake nini? (Yohana 16:5).
Nini maana ya “manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana” (Mathayo 11:13)
Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?
Turejee..
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi; 21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi;
21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Wazamzumi walikuwa ni watu warefu na wakubwa na wenye nguvu walioishi nyakati za kale, mfano wa hao ni akina Goliathi..
Watu hawa katika enzi za kale ndio watu waliokuwa wanatisha na kuogopeka sana.. walikuwa ni hodari wa vita na wenye maendeleo makubwa, walijenga miji mikubwa na walikuwa na silaha zenye nguvu, hakuna Taifa lililowaweza kwa uhodari wao.
Lakini pamoja na kusifika kuwa na nguvu nyingi za mwili, na uhodari mkubwa, bado mbele za MUNGU mazamzumi wote si kitu, Goliathi aliangushwa na kijana Daudi aliyekuwa mtumishi wa MUNGU, Mazamzumi waliokuwepo Yeriko waliangushwa na vijana walionekana dhaifu wa kiisraeli, na zaidi sana Mazamzumi wote waliangamizwa na Bwana wakati wa gharika ya Nuhu (Mwanzo 6:4).
Kama Zamzumi wako ni “dhambi” mwambie Bwana amwangushe..kwa nguvu zako hutaweza.. kama Zamzumi wako ni kikundi cha watu fulani wabaya.. mwambie Bwana akuondolee hao watu, haijalishi ni hodari kiasi gani au wana uwezo kiasi gani, bado MUNGU ana uwezo wa kuwaondoa.
Unachopaswa kufanya ili Mazamzumi yote yaondoke ndani yako nan je yako, ni wewe kumwamini Bwana YESU na kukubali kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na pia kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia maishani mwako na kukutakasa kabisa kabisa.
Ikiwa bado haujabatizwa na unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu.
Bwana YESU akubariki.
Simoni Mkirene aliubeba msalaba wa Bwana Yesu au la?
Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.
Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”
MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.
Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?
Luka 15:20
[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..
Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..
Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..
Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..
Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..
Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…
Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…
Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?
Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.
Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.
Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?
Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU
JAWA SANA MOTO ULAO.
TENGENEZA NJIA YAKO.
Marko 9:24
[24]Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Habari ya yule mzee ambaye kijana wake alivamiwa na mapepo sugu ya kumtupa motoni tangu utoto wake, na baada ya kuhangaika sana kwa madaktari na kila aina ya matabibu, hadi mitume nao kushindwa kumponya, hatimaye akakutana na Bwana Yesu..
Akamwambia ‘Ukiweza’ Bwana neno utuhurumie na kutusaidia… lakini saa hiyo Hiyo Yesu akamjibu….Ukiweza?..
Mimi unaniambia ukiweza?
Marko 9:23
[23]Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Kuonyesha kuwa Imani yake, haikuwa kamili, lakini, saa hiyo hiyo akaweka tegemeo lake lote kwa Yesu na kumwamini..’Naamini’…lakini pia nisaidie ‘kutokuamini kwangu’..
Hiki ni Moja ya ombi ya uwazi na la ukweli kabisa ambalo tunaweza kulisoma kwenye biblia…
Ni kweli ameamini, lakini imani yake si timilifu, anapambana sana kuifanya iwe sawa.. hivyo pamoja na hilo akamwona na Bwana amsaidie…kuonyesha tabia ya kujiachia kikamilifu kwa Bwana…kwamba sio tu kutendewa muujiza lakini pia kusaidiwa..
Saa hiyo hiyo Yesu hakumfukuza, wala kumkemea, wala kumwambia kafanye hivi au vile kwanza… bali akamkemea yule pepo Na hatimaye kijana akawa mzima saa ile ile.
Imani, ya kweli haimaanishi kwamba mashaka yatapotea…bali ni kuchagua kujimimina kwa Bwana na kuweka tegemeo lako lote kwake tu, hata kama moyo wako utakuambia wewe mbona unamashaka mashaka, mbona huna imani, mbona maneno yako mwenyewe yanathibitisha umekata tamaa..
Hakika hapo usiache kuomba na kukiri, ukiulilia pia msaada wa Bwana akusaidie imani yako iwe Kamilifu, kwa kujimimina tu hivyo hatimaye utayaona mambo makubwa akikutendea..
Usianze kujilaumu kwa mashaka mia uliyoonyesha, wewe egemea tu kwa Yesu bila kuondoa mguu wako hapo…atakujenga..Yule baba hakuondoka kwa Yesu, kwasababu ya madhaifu yake bali aliendelea kukaa pale pale. Kwasababu imani inajengwa kwa mahusiano sio kwa utimilifu wetu.
neema ya Mungu hizidi mapungufu yetu..kiri.udhaifu wako kwake, lakini onyesha kumtegemea yeye, hapo nguvu za Mungu utaziona.
Shetani atataka ujilaumu, katika shida yoyte lakini sema…
“Naamini, Bwana, nisaidie kutokuamini kwangu.
MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?
Waebrania 12:29
[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.
Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa
Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)
Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…
Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.
Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;
Isaya 33:14
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele? [15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..
Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.
Hii ndio mbio yetu wote…
Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.
Shalom
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.