Wana kumi na mbili wa Yakobo ndio waliozaa makabila 12 ya Israeli. Majina yao ni kama yafuatavyo;
Zipo kazi au majukumu ambayo makabila yote yaliwajibika kuyatekeleza mfano wa hayo ni kama kumwabudu Mungu, kuihudumia hema, ambayo baadaye ikawa hekalu, ulinzi kwa taifa (msaada wa kijeshi), kuendeleza Sheria ya Mungu kwa vizazi vyote.
Lakini pamoja na hayo, yapo majukumu ambayo yalitekelezwa Zaidi na kabila husuka kuliko mengine. ambapo mengine yaliagizwa na Mungu Moja kwa moja na mengine yalikuja Kama kipawa, walichokirimiwa . Na hatimaye yakawa ni majukumu yao.
Reubeni alipaswa kuwa na jukumu la kiuongozi, kama mzaliwa wa kwanza, lile kusudi lote la ukuhani lingepaswa liwe la lake lakini kwasababu alizini na mke wa Baba yake, akapoteza haki ya mzaliwa wa kwanza akaondolewa nafasi hiyo (mwanzo 35:22, 49:3-4).
Ijapokuwa alishushwa daraja lake. Bado alibakia kutimiza kusudi la kiulinzi upande wa mashariki mwa Israeli kwani jeshi lake, lilikiwa na watu hodari, lakini hawakuwa viongozi wa kijeshi.
Kabila la Simeoni nalo lingepaswa lichukue nafasi kuu katika Israeli, lakini lilishushwa chini kwasababu ya ukatili wao pamoja na Lawi, walipokwenda kuwaua wale washekemu ambao hawakustahili Kufanyiwa mauaji yale, kwa kosa la kumnajisi dada yao.(Mwanzo 34)
Hivyo kabila hili halikuwa na uongozi wowote wa kiroho katika Israeli, zaidi lilimezwa katika kabila la Yuda, kutimiza unabii wa Baba yao (Mwanzo 49:5-7), likabakia kuwa mchango kwenye eneo la kijeshi Israeli.
Lawi lilichukua nafasi ya kikuhani, lilihudumu katika hema na Hekalu, kufanya Upatanisho kwa wana wa Israeli, kwa sadaka mbalimbali pamoja Kufundisha Torati. (Kutoka 32:26-29).
Lawi hawakuwa urithi Israeli, bali walisambazwa katika makabila yote ya Israeli, kama Simeoni, kutimiza unabii wa Baba yao juu ya hasira walioionyesha Isiyo na huruma.(Mwanzo 49:5-7)
Kabila la Yuda lilisimama Kama kabila la Kifalme, na la kikuhani halisi wa milele (2Samuel 7:16)
Ndilo lililoandaa njia ya masihi kuja Duniani,(Mwanzo 49:10).Yuda lilichukua nafasi zote za juu, kutokana na kuwa Reubeni, Lawi na Simeoni kupoteza uwezo wa kuzishika, kwa matendo yao yasiyofaa.
Kabila Hili lilikuwa pia na askari hodari wa vita, na likasimama Kama kitovu cha kiutalawa, kivita na kiibada katika Israeli. Halikadhalika Yuda ilisimama kutunza urithi wa Israeli kwa vizazi vingi baada ya kutawanywa Kwenye mataifa yote, ndio lenyewe tu lililoweza kurudi Israeli.(Mwanzo 49:9-12)
Kabila la Dani lilikuwa na jukumu la kimahakama katika Israeli, (Mwanzo 49:16-18). Lilikuwa ninasimama katika nafasi ya maamuzi. Kuhakikisha Sheria na taratibu zake zinafuatwa ipasavyo.
Lakini pia lilisimama kusaidia Israeli, mahali popote walipoweka marago na kuondoka lilihusika kukusanya vitu vyote muhimu, na kuhakikisha watu wasiojiweza wanatembea Na kundi. (Hesabu 10:25).
Pamoja na hilo lilisimama kama mashujaa wa nyuma wa jeshi la Israeli, pale linapokwenda vitani lilisimama kulinda dhidi ya wavamizi wa nyuma.
lakini baadaye lilikuja kupoteza sifa yake ya kiuamuzi, kwasababu ya kwenda kusimamisha miungu ya kigeni na kuiabudu (Waamuzi 18).
Kabila la hekima na nguvu.
Ni kabila Ambalo lilikuwa na mchango mkubwa Katika eneo la kivita. Tunaweza kuona katika kipindi cha waamuzi kabila hili kwa uongozi wa Debora na Baraka (Waamuzi 4:6), lilimshinda Sisera.
Lakini lilisimama Kama washauri wa kiroho kwa Israeli.
Mwanzo 49:21
[21]Naftali ni ayala aliyefunguliwa; Anatoa maneno mazuri.
Katika wakati wa Kristo, eneo La wanaftali ambalo lilikuwa sehemu ya Galilaya lilidharauliwa sana, na kuonekana nyonge,(Yohana 1:46,7:52) si tu kimaendeleo lakini pia kuwa na wapagani wengi, lakini ndio mahali Ambapo palikuwa mji wa makazi ya Masihi Yesu Kristo, sawasawa na unabii alioutoa Isaya.(Mathayo 4:13-16).
Gadi lilikuwa hodari katika vita, lisilojisalimisha kirahisi kwa maadui, lilisimama Kama Walinzi wa lango la mashariki la taifa la Israeli, pembezoni mwa Reubeni.
Mwanzo 49:19
[19]Gadi, jeshi litamsonga, Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
Ni kabila ambalo halikujikita Sana katika mchango Wa kijeshi. Bali Lilikuwa ni kabila la kibiashara Tajiri, lenye kulinda uchumi wa nchi.
Mwanzo 49:20
[20]Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.
Ni kabila Lilipewa neema katika kutambua Nyakati na kutoa mashauri sahihi ya kufanya. lilisimama kama washauri Wa taifa.
1 Mambo ya Nyakati 12:32
[32]Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Walichangia maaskari wa vita, kwasababu walikaa katika fukwe, iliwafanya wawe hodari katika biashara na uchuuzi.
Mwanzo 49:13 Zabuloni atakaa pwani ya bahari, Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu, Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.
Ni kabila lililopewa nguvu, kiutawala na kijeshi , lilitimiza kusudi la kulisimamisha taifa la Israeli, hata wakati Israeli ilipogawanyika, makao makuu ya kabila zile 10, yalikuwa Ni samaria mji wa Efraimu. (Mwanzo 49: 22-26)
Ni kabila Lililokirimiwa watu hodari wa vita watumiao mashoto (Waamuzi 20:16), ambao walisimama vema katika vita, ijapokuwa lilikuwa dogo, lililojichanganya katika kabila la Yuda ndio kabila la kwanza kutoa mfano Israeli (Sauli), na baadaye mtume Paulo.
La kujifunza: Kuwa mdogo haimaanishi kuwa utakuwa wa mwisho. Bwana anasema walio wa mwisho Watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wamwisho.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Biblia imeandikwa na watu, (kama Paulo, Petro, Musa, Daudi na wengineo) je tutaamini vipi kitu kilichoandikwa na wanadamu kuwa ni kweli,? vipi kama wametoa tu kwenye akili zao, kwanini tukiamini kitabu cha namna hiyo, chenye mikono ya wanadamu?
Jibu: Kabla ya kujibu swali hili, tusome kwanza maandiko yafuatayo…
Yohana 14:11 “Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, SADIKINI KWA SABABU YA KAZI ZENYEWE”
Hapa Bwana YESU anatoa njia za sisi kumwamini yeye, kwamba kama hatutamwamini kwa yeye kutuambia kwa mdomo wake mwenyewe, basi tumwamini kupitia zile kazi anazozifanya ambazo ni ishara na miujiza.
Hiyo hakika ni hekima kuu sana!… kwamba kama sisi ni kazi sana kumwamini yeye kwa maneno ya kinywa chake, basi tuzipime zile kazi anazozifanya ikiwa ni halisi na za kweli, basi tumwamini kwahizo pasipo hata maneno yake.
Vile vile na hata kuhusiana na waandishi wa Biblia, kama hatuwaamini kuwa wameandika mambo waliyovuviwa na MUNGU, basi kupitia matokeo ya kazi hizo, (jinsi yanavyobadilisha watu wengi leo, na kuponya watu wengi) basi tuamini.
Labda hujaelewa vizuri, tafakari tena mfano huu.
Umeletewa kitabu cha Fizikia, ambacho kimsingi kimeandikwa na watu wengi, ambapo ndani ya kitabu hiko waandishi wameeleza kanuni/fomula za kuunda ndege inayoruka juu sana, sasa kitabu kama kitabu kinakuambia kuwa kwa kupitia kanuni hii inawezekana kutengeneza chombo na kuruka juu mawinguni..(hayo ni maneno ya waandishi wa kitabu, ambao ni wanasayansi).
Sasa kwa maneno yao hivyo tu, hatuwezi kuamini, au tuseme ni ngumu kuamini!, kwamba huwenda yakawa ni maneno ya kutunga tu, au ya watu waliorukwa na akili… lakini anapotokea mtu na kutengeneza chombo kinachoruka angani kupitia kanuni za wanasayansi hao walizoziandika kwenye kitabu chao hiko, basi ndipo tunaweza kuamini kuwa waliyokuwa wanayasema ndani ya kitabu ni kweli, kwani tumeona kabisa ndege ikiruka kupitia kanuni walizoziandika kupitia kile kitabu.
Vile vile tunaweza tusiyaamini maneno ya Paulo, au ya Petro au ya Daudi au ya Mtume mwingine yoyote ndani ya biblia, lakini tutakapoyaona yametumiwa na wengine na kuleta matokeo kama waliyoyasema ndani ya kitabu cha biblia tutawaamini.
Sasa maneno yao (Paulo, Petro, Daudi na wengineo) yamewekwa katika matendo na majaribio ya mamilioni ya watu, na yameleta matokeo yale yale waliyoyasema hao Mitume ndani ya biblia, hicho ndicho kinachotufanya tuwaamini kuwa waliyokuwa waliyoyaandika ni kweli, na uzuri ni kwamba hata mimi na wewe tumepewa nafasi ya kuyatafiti maneno hayo kama ni kweli au uongo..
Walisema na kuandika ndani ya kitabu (biblia) kuwa kwa jina la YESU pepo wanatoka, leo tumejaribu na tumeona ni kweli, na maelfu ya watu wamejaribu na kuona ni kweli, hivyo basi maneno yao ndani ya biblia ni kweli!.
Mitume waliandika kuwa Aminiye na kubatizwa atapokea zawadi ya Roho Mtakatifu (Matendo 2:38), jambo hilo tumelihakiki wenyewe kuwa ni kweli, na wewe unaweza kulihakiki kuwa ni kweli, sasa kuna sababu gani ya kutoaiamini biblia, ijapokuwa imeandikwa na watu?.. kama watu wanaishuhudia kweli, basi kinachofuatwa ni ile kweli wanaousema na si watu.
Ukiona mtu anasema mwanasayansi aliyetoa kanuni ya kuunda ndege ni mwongo na katunga, na huku ndege zinaonekana zikiruka, basi mtu huyo anayepinga huwenda anamatatizo ya afya ya akili, na anahitaji msaada, vile vile ukiona mtu anapinga elimu inayotolewa na mitume wa kwenye biblia na huku matokeo ya elimu hiyo yanaonekana wazi kwa macho, basi mtu huyo huwenda anayo matatizo pia ya afya ya akili za rohoni au hata ya mwilini, anahitaji msaada.
2Petro 1:20 “Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu.
21 Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, WAKIONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU”.
Biblia si kitabu kilichoandikwa kwa fikra za watu, kama ulikuwa unafikiri hivyo, basi leo hii anza kubadili mtazamo wako na fikra zao, anza kuisoma Biblia kwa mtazamo mwingine na utamwona MUNGU na si Mtu, kwa msaada wa njia bora ya kusoma biblia tutafute inbox.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Jibu: Mpaka kufikia mwaka 2024 biblia imetafsiriwa kwa lugha 756, hivyo kuna tafsiri Zaidi ya 756 mpaka sasa duniani kote.
Sasa kwa asili biblia iliandikwa kwa lugha kuu tatu, ambazo ni KIEBRANIA (Agano la Kale), lugha ya KIARAMU (Sehemu za Agano la kale na jipya) pamoja na lugha ya KIYUNANI AU KIGIRIKI (Agano jipya), Hizo ndizo lugha kuu tatu zilizoandikia biblia ya kwanza, na haikuandikwa kwa lugha ya kiingereza wala Kiswahili, wala lugha nyingine yoyote tofauti na hizo tatu.
Sasa kuna tafsiri nyingi za biblia siku hizi za leo kwasababu kadhaa, na sababu hizo zipo tatu (3)..
1)Tofauti za lugha, 2) Maendeleo ya Lugha 3) Mitazamo ya kidhehebu.
Hizo ndizo sababu kuu tatu,.. hebu tutatame moja baada ya nyingine.
1. Tofauti za Lugha
Kwasababu biblia kwa asili iliandikwa kwa lugha ya Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Zipo jamii za watu zisizozungumza lugha hizo, na kwasababu ni lazima watu wote, ulimwenguni kote walisikie Neno la Mungu, ni lazima tafsiri iwepo,….na watalisikiaje na kulielewa wasipolisikia kwa lugha yao na kulisoma kwa lugha yao?..
Hiyo ndiyo ikawa sababu ya Biblia ya kwanza yenye lugha hizo tatu, kutafsiriwa kwa lugha nyingine mbali mbali ikiwemo lugha yetu ya Kiswahili, Hebu tafakari laiti isingetafsiriwa kwa lugha yetu, biblia kwetu ingekuwa ngumu kiasi gani leo?.. Hivi ilivyo tu tayari ni ngumu!… vipi kama tungekuwa tunaisoma kwa lugha nyingine?? Si hali ingekuwa mbaya Zaidi??…kwasababu ingetupasa tukajifunze kwanza lugha hizo tatu, jambo ambalo lingekuwa gumu sana kwa wengi!.
Kwasababu ya shida hiyo, ndipo Bwana MUNGU wetu kupitia Roho wake Mtakatifu alitangulia kuachilia uwezo wa lugha na tafsiri zake ile siku ya Pentekoste, (soma Matendo 2) kuonyesha kuwa sasa Neno linapaswa lihubiriwe kwa watu wote na lugha zote, na ndipo zikaja tafsiri hizo.
2. Maendeleo ya Lugha.
Hii ni sababu ya pili ya uwepo wa tafsiri nyingi, utaona tayari kuna tafsiri moja ya lugha husika, tuchukue mfano lugha ya Kiswahili, halafu baada ya muda unaona kuna tafsiri nyingine zinaongezeka tofauti na hiyo ya kwanza na tena kwa lugha hiyo hiyo ya Kiswahili.
Sasa hiyo inatokana na kukua kwa lugha, kwani lugha siku zote inakuwa (inaongezeka misemo na maneno), na kwasababu hiyo basi tafsiri nyingi zinatokea na bado zitaendelea kutokea,
3. Mitazamo ya Kidhehebu na Theolojia
Kutokana na ongezeko la Madhehebu mengi yenye itikadi zinazotofautiana, imechangia pakubwa kutokea kwa tafsiri mpya kila siku kulingana na misimamo ya dhehebu husika. Kwani tafsiri nyingine zinaegemea mapokeo ya dhehebu hilo, kwamfano utaona dhehebu la katoliki linatumia biblia yenye vitabu vingine vya Deuterokanoni, ambavyo vinafanya jumla ya vitabu 72, tofauti na Biblia ya asili yenye vitabu 66.
Zipo na sababu nyingine ndogo ndogo ikiwemo mbinu za kutafsiri, kwamba wengine wanatafsiri neno kwa neno, na wengine wanatafsiri sentensi nzima na kuleta maana ya ujumla, na sababu nyingine ni mapendekezo ya lugha laini kwaajili ya watoto, zenye kutumia tafsida na zisizotumia lugha za ukali na kuogopesha. Hizi zote ndizo zinazochangia ongezeko la tafsiri za biblia kila siku.
Lakini swali je! Ni tafsiri ipi iliyo sahihi na isiyo na sumu kwa mkristo?
Mara nyingi kitu cha asili kinakuwa ni bora kuliko kile kilichochujwa Zaidi.. Tafsiri iliyo bora na yenye kufaa kuliko zote ni ile yenye lugha tatu (Kiebrania, Kiaramu na kiyunani), lakini kwasababu ni ngumu sisi kukijua kiyunani, na kiebrania kifasaha, basi tafsiri inayofuata kwa Ubora ni ile ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa katika yetu lugha husika, kwamfano kwa sisi tunaozungumza Kiswahili, tafsiri ya kwanza kabisa na bora kwa lugha yetu ni ile ya SWAHILI UNION VERSION (SUV), ambayo ndiyo inayotumika sasa kwa wingi, inayoanza na…
Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”
Hiyo ndiyo tafsiri iliyo bora, tafsiri nyingine zinazofuata baada ya hapo faida yake inakuwa ni ndogo ukilinganisha na hasara…kwani zinabadilishwa maana na zinatengenezwa kwa kuegemea dini Fulani, na katika lugha nyingine ni hivyo hivyo, ile ya kwanza ni bora Zaidi kuliko zilizoendelea kufuata.
Kwahiyo kwa hitimisho, Tafsiri sahihi yenye kumfaa mtu ni ile ya kwanza (yenye kiebrania, kiyunani na kigiriki) ikiwa mtu atakuwa ana uwezo wa kuzielewa lugha hizo, lakini kama hana uwezo basi ile tafsiri ya kwanza kabisa iliyotafsiriwa kwa lugha yake, ni bora Zaidi.
Je umempokea Bwana YESU kikweli kweli?
Je unajua kuwa tunaishi katika siku za kurudi kwa pili kwa Bwana YESU na unyakuo upo karibu?, Je unajua kuwa kama huna Roho Mtakatifu huwezi kuiona mbingu (Warumi 8:9).. sasa kama bado hujaokoka unasubiri nini?,
Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini
12 Usiku umeendelea sana, mchana umekaribia, basi na tuyavue matendo ya giza, na kuzivaa silaha za nuru.
13 Kama ilivyohusika na mchana na tuenende kwa adabu; si kwa ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.
14 Bali mvaeni Bwana Yesu Kristo, wala msiuangalie mwili, hata kuwasha tamaa zake”.
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
SWALI: Naomba kufahamu Biblia unapozungumzia kuhusu kupewa jina jipya inamaanisha nini?
JIBU: Kazi ya jina sio tu kumtambulisha au kumtofautisha mtu mmoja na mwingine. Bali jina linasimama pia kueleza Wasifa wa mtu,
Hivyo jina la mtu linapobadilika, aidha Wasifa pia hubadilika.
Kwamfano Ibrahimu alipobadilishwa jina kutoka Abramu na Kuwa Ibrahimu ni kwasababu alikuwa anaenda kuwa Baba wa mataifa mengi.(Mwanzo 17:5)
Vilevile Sarai kuitwa Sara. Ni kwasababu anaenda kuwa mama wa mataifa mengi..(Mwanzo 17:15)
Sauli kuwa Paulo kwasababu anaenda kuwa mtume kwa mataifa.(Matendo 13:9)
Vivyo hivyo tunaona Mungu katika maandiko Akijitambulisha kwa majina mbalimbali, lengo sio kuonyesha uzuri au upekee wa majina yake hapana bali kutambulisha wasifa wake.
Kwamfano alipojitambulisha kama Yehova rafa, alisimama kama Mungu mponyaji..Yehova yire Mungu atupaye, Yeshua(Yesu), kama Mungu atuokoaye.
Tukirudi kwa wakati wa sasa Biblia Inatuonyesha kuwa Kristo atakaporudi mara ya pili atakuja na jina lingine jipya. Ambalo ndio tunangojea kuona utukufu wake, mamlaka yake na nguvu zake.
Ufunuo wa Yohana 3:12
[12]Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.
Jina hili halitakuwa Yesu,tulitumialo sasa ambalo linawasifa wa wokovu, lililojikita katika kiwakomboa na kuwafungua wanadamu katika mauti na vifungo vya kila namna.
Lakini hilo linalokuja litakuwa ni jina lenye uweza Mwingi, la kifalme, la kiutawala zaidi. Wakati huo Kristo hataonekana tena kama mwanakondoo mpole, asimamaye kutuombea kwa Baba N.k..hapana ataonekana katika taswira mpya kabisa ya kifalme, na zaidi ya hapo (Ufunuo 19:11-16), sawasawa na hilo jina lake litakavyokuwa.
Ndio maana kuna umuhimu sana kuokoka sasa, angali neema na msamaha upo katika jina la YESU, kwasababu atakaporudi mara ya pili,na jina jipya hatajua kusamehe ni nini, bali mambo mengine mapya yatakuwa wanaendelea..Usipookoka leo hakuna wokovu siku ya mwisho.
Vilevile wale watakaoshinda Kristo ana ahidi kuwapa majina mapya ya kipekee, ambayo yatawanafisisha kipekee mbele ya Kristo.
Ufunuo wa Yohana 2:17
[17]Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.
Ndugu Utukufu Unaokuja wa Kristo ni mkuu sana, ni heri ukose vyote sasa, lakini usikose mbingu Mpya na nchi mpya na ile Yerusalemu mpya ishukayo kutoka kwa Baba mbinguni.
Siku hizi ni za mwisho, unyakuo umekaribia sana. Mambo ya umilele yanakaribia kuanza. Bado unaendelea kung’ang’ana na ya kidunia? tubu leo mgeukie Kristo.
Bwana akubariki.
Amen.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.
JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?
Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?
SWALI: Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka, na pia mtu anaweza akawa ameokoka akaombea mtu na pepo lisitoke ?
JIBU: Kuhusu swali la kwanza linalosema je mtu anaweza akawa hajaokoka kisha akaenda kuombea mtu mwenye pepo na hatimaye likamtoka?
Jibu ni la!, haiwezekani mtu ambaye hajaokoka, akawa na uwezo wa kutoa pepo, kwasababu pale alipo yupo chini ya vifungo vya ibilisi, haiwezekani akaenda kumfungua mtu ambaye ni mfungwa mwenzake, inahitaji mtu aliye huru ndio aweze kufanya hivyo.
Bwana Yesu alisema…
Marko 3:23-27
[23]Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
[24]Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
[25]na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
[26]Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.
[27]Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.
Ni hatari huyo mtu akijaribu kufanya hivyo, kwasababu anaweza kukutana na madhara kama yaliyowakuta wale wana wa Skewa.(Matendo 19:13-16).
Kuhusu swali la pili linalouliza Je mtu ambaye ameokoka anaweza akaombea na pepo lisitoke?
Jibu ni ndio Ikiwa mtu huyo anakiwango kidogo cha imani, si mapepo yote yanaweza yakatoka, kwasababu mashetani yanatofautiana kimadaraja (Mathayo 12:43-45), yapo yenye nguvu kubwa ya ukinzani, mengine huitwa wakuu wa giza, mengine wafalme na wenye mamlaka. (Waefeso 6:12)
Hivyo inahitaji nguvu zaidi za kiimani ambazo zinakuja kwa njia ya mifungo na maombi.
Ndio maana mitume kuna mahali walitoa kweli pepo wengi lakini kuna mahali hawakuweza kwasababu ya uhaba wa maombi. (Mathayo 17:14-21)
Lakini uhalisia ni kuwa mtu yeyote aliyeokoka, haijalishi amedumu sana katika wokovu au ni mchanga. Anayo mamlaka ndani yake ya kutoa pepo lolote lile, isipokuwa anahitaji pia na maombi ile mengine yasishindikane kwake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Maana ya Madhali ni nini kama ilivyotumika hapo katika Zaburi 21:11
Jibu: Turejee…
Zaburi 21:11 “Madhali walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Neno “Madhali” limeonekana mara moja tu kwenye biblia yote, na maana yake ni “Ingawa” Hivyo Kiswahili kingine cha neno “Ingawa” ni “Madhali” …
Kwahiyo maandiko hayo yanaweza kuweleweka pia hivi…“Ingawa walinuia kukutenda mabaya, Waliwaza hila wasipate kuitimiza”.
Madhara yanayonuiwa na watu wabaya, ikiwa tupo ndani ya Kristo, hayataweza kushinda juu yetu, haijalishi yataonekana yamekomaa kiasi gani.
Je umempokea BWANA YESU?..
Unao wokovu ndani yako?
Waebrania 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.
Maran atha
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Tunasoma Simeoni alipomwona mtoto YESU, Alikiri kuuona Wokovu wa MUNGU, sasa swali ni Wokovu gani huo alioupata?
Jibu: Tuanzie ule mstari wa 25 ili tuweze kuelewa vyema…
Luka 2:25 “Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana.
27 Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria,
28 yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema,
29 Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;
30 KWA KUWA MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU WAKO,
31 Uliouweka tayari machoni pa watu wote;
32 Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli”
Sasa hapo hajasema AMEUPATA WOKOVU..La! bali anasema “MACHO YANGU YAMEUONA WOKOVU”.. kuuona wokovu na kuupata wokovu ni vitu viwili tofauti…
Wokovu wa Mungu unapatikana kupitia mmoja tu, naye ni YESU KRISTO (Matendo 4:12),..Baada ya YESU kusulibiwa ndipo watu wakaanza kuupata wokovu, lakini kabla ya hapo waliusikia na kuuona tu,…waliousikia ni manabii wa kale na watu wote wa agano la kale, na waliouona ni watu waliokuwepo kipindi BWANA YESU anazaliwa, na walioupata ni wote waliomwamini baada ya kufufuka kwake.
Sasa utauliza vipi waliokufa katika haki wakati wa agano la kale, je hawakupata wokovu kabisa katika kipindi chao?… Jibu ni kwamba baada ya kufa kwao wokovu wao ulikuwa haujakamilika, lakini KRISTO aliposhuka kuzimu na kuchukua mamlaka yote ya walio hai na waliokufa, ndipo wokovu wao ukakamilika (maana yake wakaupata wokovu).
1Petro 1:10 “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi.
11 Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.
12 Wakafunuliwa ya kuwa si kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yenu walihudumu katika mambo hayo, ambayo sasa yamehubiriwa kwenu na wale waliowahubiri ninyi Injili kwa Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni. Mambo hayo malaika wanatamani kuyachungulia”.
Kwahiyo Simoni aliuona Wokovu, kwakuwa anayebeba wokovu (YESU KRISTO) yupo pale.
Na wote tunaomwamini sasa, tunapokea wokovu wa roho zetu.
Je umempokea YESU?… Je umeoshwa dhambi zako kwa damu yake?
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Maran atha.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
FAHAMU KANUNI ZA KUZISUBIRIA AHADI ZA MUNGU?
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
UKIAMINI NA UKIMKIRI YESU KWA KINYWA CHAKO, UTAOKOKA.
Musa alikuwa na sababu kadha wa kadha za yeye kufanye vile, ikiwemo
Kutoka 3:11
[11]Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?
Musa aliogopa, kwenda kuwahubiria watu juu ya Mungu Ambaye hakulijua jina lake, kwani zamani zile, miungu yote ilifahamika kwa majina, hivyo alijiona kama kwenda kuwaambia watu habari za Mungu asiyejulikana jina lake, ni kama anawafedhehi.
Kutoka 3:13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
Kutoka 4:1
[1]Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.
Kwasababu alikuwa hana ishara yoyote ya ki-Mungu ndani yake.
Kutoka 4:10
[10]Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.
Pamoja na Mungu kumwakikishia kuwa atakuwa naye na kumsaidia lakini Musa bado akakataa, ndipo Mungu akaghadhibika na kumletea nduguye Haruni, kama msaidizi wake.
Jambo ambalo halikuwa mpango wa awali wa Mungu, kwani uongozi wa Haruni hakuwa kusudi kamilifu la Bwana. Sababu kadha wa kadha zilizowapelekea wana wa Israeli kupata adhabu, zilikuwa ni pamoja na uongozi dhaifu wa Haruni. Utakumbuka wakati Musa amepanda juu mlimani kuchukua zile mbao mbili za amri 10, Haruni aliachiwa uongozi kwa muda, watu walipomfuata Kwa ajili ya hatma zao, akasikiliza mapendekezo yao akawaundia sanamu ya ndama ili waiabudu, ikapelekea Mungu kuwaangamiza wana wa Israeli wengi sana, (Kutoka 32:1-6) mzizi huo ni kutokana na kutokutii kwa Musa, halikadhalika sababu ya Musa kutoiona nchi ya ahadi ilichangiwa pia na uongozi hafifu wa Haruni, kwani kule Meriba kosa alilofinya Musa la kuchukua utukufu wa Mungu, alihusika na Haruni pia. (Hesabu 20:10-12)
Hivyo ni wazi kama angekuwa na imani na Mungu, mengi yasingetokea mbeleni. Hata wakati huu wa sasa, wengi wetu tumejikuta katika machaguzi ya pili ya Mungu kwasababu tu, ya kumpotezea imani, kuwa anaweza kutenda kusudi lake lote hata katika Madhaifu yetu.
Mwamini Mungu mtegemee yeye tu.
Shikilia vifungu hivi vikusaidie.
Mithali 3:5
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Isaya 6:8
[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
2 Timotheo 1:7
[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?
Je ni sala gani inahitajika kabla ya kumchinja mnyama katika ukristo?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
Mungu hakumchagua Musa kwasababu ya wema, au kipawa, au ujuzi fulani aliokuwa nao tofauti na wengine. Hapana almchagua ili ‘kutumiza kusudi lake la kuchagua’ ambalo tunalisoma kwa urefu katika (Warumi 9:11-17). Linalomaanisha Mungu humchagua mtu na kumfanya awe kama anavyotaka mwenyewe, na sio kwa jinsi Yule mtu atakavyo. Kwamfano alimchagua Farao, kisha akamwekea moyo mgumu,ili atimize kusudi lake mwenyewe, kujichotea utukufu kwa mapigo yale kumi,aliyoyaachia kwa wamisri, vivyo hivyo na kwa Musa alimchagua na kumpa neema ile kubwa ya hofu ya Ki-Mungu na upole ili atimize kusudi lake la kuwakomboa wana wa Israeli.
Lakini hakuwa na tendo lolote jema alilowahi kutenda lililomshawishi Mungu amchague yeye tofauti na wengine.
Na ndivyo anavyofanya hata sasa kwa wanadamu wote. Tunaokolewa na kutumiwa na Mungu kwa neema tu, na si kwasababu ya matendo Fulani mema tuliyowahi kumtendea Mungu.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nini tofauti ya Majira na Wakati?
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
NAAM, HATA WABAYA KWA SIKU YA UBAYA.