Sauli (Mtume Paulo) alipokuwa anaelekea Dameski kwa lengo la kuwafunga na kuwatesa watakatifu, kama tunavyoifahamu habari alitokewa na Yesu njiani, mwanga Mkali ulimpiga machoni, akashindwa kuona, Wakamchukua mpaka ndani ya mji akiwa kipofu.
Lakini tunaona alipokuwa kule, hakuwa katika hali ya kawaida, bali katika maombolezo makubwa rohoni, hakula chakula chochote, wala maji..(maana Yake alikuwa katika mfungo), lakini si hilo tu zaidi sana alikuwa akiomba dua.
Baada ya hapo tunaona jambo lingine likitokea mtu mmoja aliyeitwa Anania anatokewa na Yesu, kisha anaagizwa amfuate Paulo. Lakini eneo analoagizwa ni katika njia iliyoitwa NYOFU…
Maana Yake “njia iliyonyoka”.
Matendo 9:8-12
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. [9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi. [10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. [11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; [12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
[9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.
[10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.
[11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;
[12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Unaweza kujiuliza kwanini apelekwe njia ile ..tena iitwe kwa jina la NYOFU na si lingine labda “njia kuu”, au “nzuri” au “panda” bali nyofu?
Ni kwasababu rohoni, Kristo huwaweka watu wake Katika hiyo njia. Njia iliyonyoka.
Hapo mwanzo Paulo alikuwa katika njia iliyoharibika, mbovu, ya kuupinga ukristo, ya uuaji, ya utukanaji, ya dhambi, ya mauti.
Lakini alipokutana na YESU, akatolewa huko akawekwa katika njia iliyonyooka ya utumishi wake.
Ni ajabu kuona watu wengi leo wanampinga Kristo, hawataki kuokoka, wakidhani udini ndio utawanyooshea mapito yao, fedha ndio zitawasawazishia mabonde Yao, elimu ndio zitaangusha milima yao.
Kumbe hawajui kuwa njia iliyonyooka ni maisha ndani ya Kristo tu!. Kwingine kote ni mabonde, milima Na mwishowe shimoni na mauti. Hakuna pumziko Nje ya Kristo.
Yohana mbatizaji aliliona hilo akapaza sauti yake kwa nguvu Akisema..
Yohana 1:23
[23]Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
Kumwamini Yesu ndio kuinyoshe njia ya Bwana..
Je upo katika njia ya nyofu.
Okoka leo, uponywe kila kitu ndugu, kumbuka Umepotea nje ya Kristo,hakuna mjadala na huo ndio ukweli, hakuna tegemeo kama Yesu hajakuokoa. Fanya haraka utubu, leo uiamini kazi ya Kristo ya ukombozi iliyokamilishwa kwa ajili yako pale msalabani. Muda ni mchache mlango wa neema hautadumu Milele.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Yesu maisha yako. Basi bofya bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Jehanamu ni nini?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Print this post
Awali tufahamu nini maana ya kumwabudu Mungu, Kumwambudu Mungu si kumwimbia tu Mungu nyimbo ya kuabudu tulizozizoea, Neno kuabudu limetokana na neno “ibada” hivyo kumwabudu Mungu ni “kumfanyia ibada”
Sasa ibada imebeba mambo mengi ikiwemo kuomba, kumwimbia Mungu, kumtolea Mungu, kujifunza Biblia, kushiriki meza ya Bwana n.k
Sasa ni kwa namna gani tutamwabudu Mungu?.. si kwa njia nyingine zaidi ya hizo, ambazo ni kuomba ambako kunaweza kuhusisha kwa kupiga magoti au kusujudu, pia kumwimbia nyimbo za kumshukuru na kumsifu, na kumtolea matoleo yetu, na kujifunza maneno yake na kuyaishi na mambo mengine yanayoendana na hayo..
Maana yake tukiyafanya mambo hayo katika ukweli wote na katika roho bila kupunja chochote tutakuwa tunamwabudu Mungu..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kumwabudu Mungu ni kumfanyia Mungu ibada katika ukweli wote na katika roho, kwanini ni katika kweli yote na katika roho??..Turejee maandiko yafuatayo..
Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.
Hivyo mpendwa kama unataka kumwabudu Mungu kweli kweli usikwepe kukusanyika kanisani, na hakikisha unakusanyika katika usafi na utakatifu, pia usikwepe ushirikia wa meza ya Bwana, pia usikwepe maombi binafsi na ya pamoja, usikwepe kumtolea Mungu (ni jambo la msingi sana), pia usikwepe kumshukuru Mungu na kumsifu kwa njia ya nyimbo na tenzi za rohoni.
Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
EPUKA KUCHELEWA IBADA.
NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.
NAWAAMBIA MAPEMA!
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
Je unafahamu asili ya kanisa la Kristo? Ni vema wewe kama mwamini ufahamu mapito ya Imani yako.
Mpaka leo hii injili iliyotokea Yerusalemu (Israeli) kunifikia mimi na wewe, fahamu kuwa kuna mapito ambayo waliyapitia , ambayo na sisi tunapaswa tuyafahamu ili tuweze kuifikisha injili hiyo kila mahali, duniani kote na kwa vizazi vyote bila kuwa na deni.
Mwanzoni kabisa kanisa lilikuwa mahali pamoja pale Yerusalemu, Lakini dhiki ilipotokea na kuwa kubwa, mpaka watakatifu kuuliwa hadharani mfano Stefano, iliwagharimu wengi wa wakristo wakimbie Israeli na kwenda mbali kwenye mataifa mageni.
Lakini kuondoka kwao haikuwa mwisho wa safari, kwenda kuanza maisha mapya ya utulivu..hapana kinyume chake kule walipofika ugenini waliendelea kulihubiri lile Neno, kama tu vile walivyokuwa nyumbani.
Matendo ya Mitume 8:1,4
[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume… [4]Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume…
[4]Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
Umeona asili ya kanisa la Kristo.. Ni sawa na leo, kuhama-hama kwa watu, pengine kwasababu za kikazi, kivita, kimasomo, kijamii n.k. unajikuta unaenda kijiji jirani, mkoa mwingine, au taifa lingine geni. Jiulize Je! Unalihubiri Neno kama kule nyumbani ulipokuwepo au ndio unabadilika tabia.
Kanisa la kwanza halikupoteza ubora mahali popote ugenini..Kwamfano utaona mtume Petro Aliendelea kuandika nyaraka zake kwa watakatifu waliotawanyika..mataifa mbalimbali, akijua kuwa injili ya Kristo inaendelea,
1 Petro 1:1
[1]Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia;
Mazingira hayapaswi kuwa kizuizi cha ushuhudiaji wako, kwasababu kanisa halizuiwi na mazingira..Shuhudia Kristo popote ulipo kwasababu popote walipo watu, Mungu yupo hapo. Usipumbazwe na fikra za kusema mimi nilipo nashindwa kushuhudia afadhali kule nilipotoka, hii kazi mpya niliyoipata siwezi kuwashuhudia watu, ndugu hilo si wazo la Mungu. Fikiri Mungu akupe hekima, na hakika utaona upenyo.
Shalom.
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.
TUTAFUTE KWA BIDII KUKAA NDANI YA YESU.
Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Kuna mambo unaweza ukayafanya ukadhani ni sawa machoni pako. Lakini kumbe hujui kama unaleta huzuni kubwa kwa Kristo.
Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo aliitwa Sauli, alikuwa akishindana na mawazo, na jamii ya watu waliomwabudu Mungu akidhani anashindana na ubaya kumbe anashindana na Kristo mwenyewe.
mpaka alipokutana na Kristo mwenyewe njiani alipokuwa anakwenda Dameski..akaambiwa maneno haya..Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Matendo 9:4-5
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? [5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
[5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
Hilo Neno waniudhi, kwenye tafsiri ya asili linamaanisha hasaa “wanitesa”? Biblia ya kiingereza inaeleza vizuri zaidi inatumia neno “persecutest”…yaani kutesa..
Paulo alikuwa mfano wa wapagani waliomtesa Kristo, pale alipokuwa anawaburuta watakatifu, anawafunga, anawapinga, na kuwatukana…hakujua kuwa anamtesa Kristo mwenyewe..Leo hii makundi ya watu wanaowapinga watakatifu, wanaoyapinga makanisa ya kweli, wanaowatukana watumishi wa Mungu, wanaowapiga na kuwaua wafahamu kuwa wanamtesa Kristo.
Ikiwa wewe ni mmojawapo kuwa makini, uache mara moja, ni heri utubu leo umpe Yesu maisha yako. Akuokoe.
Lakini kundi la pili ni wale waamini- waliorudi nyuma. Mtu ambaye ameshaokoka, Halafu anaiacha Njia kwa makusudi anayafanya yale machafu aliyoyaacha nyuma huyo anamtesa Kristo, tena yale mateso ya msalabani kabisa.
Waebrania 6:4-8
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, [5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, [6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri. [7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; [8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
[5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
[6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
[7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
[8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
Acha tabia ya kuzoelea dhambi, ukishaokoka ukitenda dhambi, haihesabiki kama kosa kama la wapagani bali uasi.
Kama Ulimpokea Kristo ili umtese, kuokoka kwako kuna maana gani? Ulishawahi ona mtoto anampiga Baba yake? Hiyo si laana?
Ndivyo ilivyo kwako unapozini na huku umeokoka, unapokunywa pombe na kufanya anasa.. Tubu haraka sana umrudie Kristo
Penda utakatifu, Ishi maisha matakatifu..
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
WhatsApp
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Kwa lugha rahisi kuna tofauti ya kuhubiri na kushuhudia.Yesu alituita tuwe mashahidi duniani.. Na hiyo ni kazi ya kila mmoja, Wito wa kumtangaza Yesu, sio wa kimahubiri, bali ni wa kiushuhudiaji.
Mhubiri ni mtu anayesimama na biblia, anayefundisha maandiko, anayefafanua, hadithi mbalimbali na mafunzo katika biblia kisha kutarajia watu kugeuka kwa mafundisho hayo. Huyu anaweza akawa mchungaji, mwinjilisti, mtume, Askofu, shemasi n..k
Lakini shahidi ni mtu aliyeona ukweli wa jambo Fulani, kisha akasimama kama mteteaji au mthibitishaji wa ukweli huo.Ndio kazi tuliyopewa sisi sote kufanya kuhusu Kristo, kuwa mashahidi wake ulimwenguni kote. Wa yale yote aliyotutendea sisi katika maisha yetu. Yaani yale aliyoyasema tukayathibitisha sisi wenyewe kuwa ni kweli katika maisha yetu.
Kwamfano pale aliposema njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha (Mathayo 11:28). Ulipokwenda kwake ukaona mzigo huo umetuliwa, Hivyo tukio hilo huna budi kusimama na kulithibitisha kwa wengine, na wao pia waamini, ili watendewe jambo hilo hilo.
Pale Yesu aliposema tukiamini tukabatizwa, tutapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.(Matendo 2:38) Na wewe sasa umepokea Roho Mtakatifu, umejua ni ukweli, sasa hapo ndipo unapokwenda kuwashuhudia wengine ukweli huo.
Pale ulipoponywa, ulipofunguliwa, ulipoonyeshwa ishara, ulipopewa nguvu ya kushinda dhambi fulani.. Hapo ndipo unapopashuhudia..Na kwa kupitia ushuhuda huo, mwingine atajengwa Imani na kumwamini Yesu kama wewe ulivyoamini hatimaye kuokoka.
Sasa kazi hii haihitaji theolojia ya biblia, haihitaji ukomavu wa kiroho, haihitaji mifungo na maombi, inahitaji tu kufungua kinywa chako na kuanza kueleza uzuri ulioupata ndani ya Kristo, na kwa njia hiyo ndio Mungu atamshawishi mtu na kuokoka.
Ukiwa kama mkristo umeokoka labda tuseme leo, Kumbuka tayari una deni la kuanza kushuhudia uzuri wa Kristo kwa maneno hayo hayo machache uliyonayo kinywani mwako.. Ndicho alichokifanya Paulo baada tu ya kubatizwa..
Matendo 9:17 Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu.Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;19 akala chakula, na kupata nguvu. Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski.20 Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.21 Na wote waliosikia wakashangaa, wakasema, Siye huyu aliyewaharibu walioliitia Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuwa amekuja kwa kusudi hilo, awafunge na kuwapeleka kwa wakuu wa makuhani?22 Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.23 Hata siku nyingi zilipopita, Wayahudi wakafanya shauri ili wamwue.
Tatizo linatokea pale ambapo tunaona kazi ya injili ni ya watu maalumu na ni nzito . Hapana, kumbuka anayeshawishi watu mioyo ni Mungu, sio kwa wingi wa vifungu vya maandiko au kwa uzoefu wa kuhubiri, bali kwa Roho Mtakatifu tu. Maneno mawili, tu yenye kumshuhudia Yesu, yana nguvu ya kugeuza mtu zaidi hata ya maneno elfu ya vifungu vya biblia.
Unapokwenda kushuhudia usifikiri fikiri ni nini utasema, wewe anzia pale ambapo ulitendewa na Yesu ikawa sababu ya wewe kuokoka.. muhadhithie huyo mtu Habari hiyo kwa taratibu. Utashangaa tu, huko huko Katikati Mungu anakupa hekima na kinywa cha kumhubiria mpaka utashangaa hekima hiyo umeitolea wapi. Pengine mtu atakuuliza swali umsaidie, lile jibu linalokuja kwenye kinywa chako liseme, wala usijidharau au usiogope, anayemshawi mtu ni Mungu, yeye kuelewa au kutokuelewa hiyo sio kazi yako ni ya Mungu, uwe tu na ujasiri, kwasababu hakuna Habari yoyote yenye maudhui ya Kristo ndani yake haina matokeo.
Anza sasa kumshuhudia Yesu, Na kwa Pamoja tuujenge ufalme wa Kristo. Anza na marafiki zako, familia, wafanyakazi wenzako, majirani zako kabla ya Kwenda hata mwisho wa nchi.
Mungu akubariki
JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI
YESU KATIKA KUCHOKA KWAKE.
Enendeni ulimwenguni mwote
SWALI: nini maana ya Yohana 17:20
[20]Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Ni akina nani hao ambao wataamini Kwasababu ya Neno lao, Bwana Yesu aliotaka kuwaombea?
JIBU: Sura hiyo ya 17 ni sura iliyoelezea kwa kina dua ambayo Bwana Yesu aliifanya kwa mitume wake kwa Baba.
Ambapo aliwaombea mambo kadha wa kadha ikiwemo walindwe katika umoja wa Roho, walindwe na yule mwovu, watakaswe na ile kweli.. Lakini pia Bwana Yesu hakuishia kuwaombea wao tu, bali na wengine ambao mitume wake watawahubiria injili na kuamini baadaye. Na hao pia maombi yake yalikuwa ni yaleyale kwao.
Maana yake ni kuwa watu wote walioamini kwa injili ya mitume walishiriki dua hiyo ya Kristo, Na hao si wengine zaidi ya wale watakatifu wa kanisa la kwanza, hadi sisi tuliopo sasa, hadi na wale watakaokuja baadaye.. sisi wote ni washirika wa dua ile (Yohana 17), kwasababu tumeamini katika injili moja ya mitume..
Ndio sababu kwanini maandiko yanasema Kristo anatuombea…maana yake ni kuwa sasa anatuombea kwa yule Roho Mtakatifu auguaye ndani yetu, lakini pia analituombea alipokuwa duniani ambapo sala hiyo tunaona matokeo yake hata sasa.
Waebrania 7:25
[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Hii ni kututhibitishia Kuwa pale tunapomwamini Kristo upo ulinzi usioelezeka unawekwa juu yetu, kiasi kwamba malango ya adui hayawezi Kushinda..kinachohitajika ni kutii tu.
Warumi 8:34
[34]Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
Je na wewe ni mshirika wa sala hiyo ya Bwana? Kwa kumpokea Bwana Yesu? Kama ni la! Basi nafasi ni sasa mwamini Yesu upokee uzima wa milele.
Lakini pia Bwana anatufundisha namna sahihi ya kuomba..hatupaswi tu kuyaombea yale matunda tunaoyaona..bali hata na yale yatakayokuja baadaye..wale watakaokoka baadaye kwasababu ya Neno letu.
WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.
MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.
“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).
Mariamu alipotokewa na Malaika na kuelezwa habari ya mambo ambayo hayawezekaniki kibinadamu, alionyesha tabia ya kitofauti sana…hakuanza kubisha, Hakuanza kukinzana na kusudi na mpango wa Mungu juu yake, ulio juu ya upeo wa ufahamu wake, kinyume chake aliukubali, tena si Kwa maneno ya juu juu tu, bali kwa ukiri wa utumwa…akasema
“Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema.”
Maana yake ni kuwa ikiwa jambo hilo linanilazimu kulitumikia mimi nitafanya hivyo kama Mtumwa..
Luka 1:34-35,38
[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? [35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu… [38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
[35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu…
[38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
Mariamu ni kielelezo kamili cha mwanamke thabiti wa kikristo, lakini sio tu mwanamke bali bali kwa kanisa la Kristo kwa ujumla.
Utii wa namna hii ndio Bwana anaoutaka kwa watu wote wamchao yeye..
Ijapokuwa kibinadamu haikuwezekana, akijua pia ikishatokea itamletea aibu katika jamii, atakaposadikika amepata ujauzito, kimiujiza hakuna atakaye mwelewa, watasema ni mzinzi, akijua pia kuna majukumu mengine mazito yatafuata..bado alilipokea kusudi la Mungu..lililo juu ya uwezo wake.
Hakukubali kuingia kwenye kosa kama la Musa, kusema mtume mwingine, hakulimbikia kusudi la Mungu kama Yona kukimbilia Tarshishi…bali alilipokea zaidi ya mtumwa.
Si ajabu kwanini Bwana alimpa neema kubwa namna ile…
Ndugu/kaka Bwana anatazama Utayari wako zaidi ya uwezo wako, anatazama utii wako zaidi ya umri wako.
Kila mmoja wetu leo, aliyeamini katika agano jipya ameitwa kufanya MAKUBWA mfano tu wa Mariamu…Hakuna hata mmoja ambaye hajaitwa kwa ajili ya mambo makubwa ya Mungu… kwasababu Mungu ni Mungu wa miujiza na yaliyoshindikana.
Isipokuwa Imani zetu ni haba Kwa Mungu ndio maana hatuoni matokeo makubwa. Kinachohitajika ni kujiachilia tu kwake..kisha kumwacha yeye atende kazi zake ndani yetu.
Haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke, mzee au kijana, una elimu au huna elimu, tajiri au maskini.. kubali kujiachia kama Mariamu katika kusudi lolote la Mungu.. unapoona una nafasi ya kuombea wagonjwa Fanya hivyo, una nafasi ya kuwashuhudia watu mitaani, masokoni, viwanjani fanya hivyo, huko huko Bwana atajifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida. Na Utukufu utamrudia yeye.
Kumbuka tu Mungu amechagua kutumia vyombo Dhaifu kukamilisha kusudi lake timilifu.
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?
USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!
Tofauti na Ibrahimu, Isaka na Yakobo ambao chimbiko lao linaonekana katika mtiririko wake tokea Adamu mpaka Nuru hadi wao wenyewe..
Ayubu yeye ni tofauti, kwani kitabu kinaanza kwa kumweleza yeye, na mahali tu alipokuwa ambapo ni Usi.
Usi ni nchi ambayo ilikuwa nje ya Israeli, maeneo ya aidha Arabia, Syria au Yordani..lakini eneo sahihi kwa uhakika halijulikani hivyo hakuwa na chimbuko lolote la kiyahudi ndani yake.
Maandiko yanamtaja tu kama “Mtu”, wala sio nabii, au kuhani bali mtu aliyekuwa mkamilifu na mwelekezo aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu.
Ayubu 1:1
[1]Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.
kwanini Mungu aruhusu, watu kama hawa ambao hawakuwa katika mtiririko wa kifamilia waandikwe kwenye biblia na zaidi hata wawe na sehemu kubwa katika ufalme wa Mungu…
Ni kuonyesha kuwa Mungu hana upendeleo, yeyote yule amchaye yeye hukubaliwa naye..ndicho Petro alichokiona kwa Kornelio akasema..
Matendo ya Mitume 10:34-35 [34]Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo;
[35]bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.
Mwanamke Ruthu hakuwa myahudi, lakini Bwana alimkubali.
Hata na wewe kitendo cha kutozaliwa familia ya kikristo au kichungaji haimaanishi kuwa wewe huna neema ya kumtumikia Mungu. Hapana..ukionyesha bidii ile ile wanayoonyesha wengine Mungu hukujalizilisha neema Izidiyo haijalishi ukoo wenu wote ni wa kiganga. Kila mmoja wetu ana nafasi sawa mbele za Mungu, haijalishi kama ni myahudi au mwarabu, kama ni mzungu au mwafika wote kwa Mungu wanayo neema sawa kwasababu yeye haangalii chimbuko wala sura ya mtu.
Je unamcha Mungu?
Je unafahamu kuwa “Hukumu ya ibilisi” ilishapitishwa?.. Ni muhimu kulifahamu hili ili tusipumbazwe na dhambi.
Awali turejee maandiko..
Yohana 16:11 “kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa”.
Haya ni maneno aliyoyasema Bwana YESU kuhusiana na hukumu ya ibilisi kwamba imeshapita, na hana wakati tena wa kusimama mbele ya kiti cha hukumu kuhukumiwa tena, tayari kashahukumiwa..
Fahamu kuwa kosa kubwa lililomfanya ibilisi kutupwa katika ziwa la moto si kumdanganya mwanadamu, wala hakuna adhabu yoyote anayojiongezea katika kumdanganya mwanadamu… kwanini?, kwasababu tayari alishahukumiwa na hiko ndicho kinachomfanya afanye kazi yake kwa bidii sana ya kudanganya watu na kuwapoteza..
Kosa kubwa ibilisi alilolifanya ni KUASI HUKO MBINGUNI, na akapimiwa kipimo cha adhabu ya juu kikubwa cha kumstahili ambacho ni ZIWA LA MOTO (yenye makali kuliko jua) yeye pamoja na malaika walioasi pamoja naye, kwa ufupi ni kwamba ziwa la moto lilikwisha kuwepo kabla hata ya mwanadamu kuumbwa, kwasababu biblia inatuambia hilo kuwa lilitengenezwa kwaajili ya shetani na malaika zake na si mwanadamu.
Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, ALIOWEKEWA TAYARI IBILISI NA MALAIKA ZAKE”
Umeona?.. moto uliwekwa tayari kwa shetani na malaika zake na si wanadamu, lakini kwasababu wapo wanadamu watakaomfuata ibilisi na kumkataa Mungu, ndipo wataungana na jeshi hilo la ibilisi katika moto huo.
Kwahiyo kamwe tusijidanye kuwa ibilisi ataenda kuulizwa kwanini katupoteza, au kwanini alisababisha wewe uzini, au kwanini alisababisha ajali na watu wakafa, au kwanini aliwatesa watu duniani?..hana hukumu yoyote kwasababu ya kuudanganya ulimwengu, adhabu aliyopewa ni kuasi kule juu, na hiyo adhabu yake ni kubwa sana na ya kutosha..
Siku ile mbele ya kiti cha hukumu ni wanadamu ndio watakaosimamishwa wenyewe kuhukumiwa kwa kadiri ya matendo yao.
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Kwahiyo dada usimlaumu shetani kana kwamba siku ile ataulizwa kwa kukudanganya wewe, yeye hana maswali tena ya kuulizwa, yeye hana hoja tena za kujibu, yeye tayari adhabu yake imeshapitishwa, na hilo ndilo linalomfanya aendelee kufanya uharibifu kwa kasi sana, kwasababu hakuna anachoongeza wala kupunguza katika adhabu yake.
Hata akiua watu elfu kikatili, hakuna kinachoongezeka kwenye adhabu yake kwasababu amekwisha hukumiwa, ule moto ni mkuu sana ibilisi alioandaliwa.
Kwahiyo dada maisha yako ya uchafu yatafakari sana, kaka maisha yako ya uzinzi yatafakari sana, ndugu maisha yako ya uvuguvugu yatafakari sana, usikae umsingizie shetani kana kwamba shetani ataulizwa siku ile kwaajili yako, siku ile utasimama peke yako, nitasimama peke yangu, futa kale kausemi “shetani kanipitia”
Ni heri ukatubu leo na kumpa Yesu maisha yako kabla hizo siku za hatari hazijafika, kabla siku zako za kuishi hazijafika.
Neno la Mungu linasema, mkumbuke muumba wako kabla roho haijamrudia aliyeitoa (yaani Mungu,
Mhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa”.
Bwana atusaidie.
Shetani alitoka wapi?
NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?
Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.
NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?
SWALI: Kwanini Anasi na Kayafa walihudumu pamoja? Je Mungu aliruhusu makuhani wakuu wawili kuhudumu kwa wakati mmoja?
Luka 3:2
[2]wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, neno la Mungu lilimfikia Yohana, mwana wa Zakaria, jangwani.
JIBU: Ni kweli kipindi cha Bwana Yesu tunaonyeshwa makuhani wawili walihudumu katika nafasi ya ukuhani mkuu. Jambo ambalo ni kinyume na agizo la Bwana kuhusu nafasi hiyo..Kwani kuhani mkuu alipaswa awe mmoja tu, mpaka atakapokufa ndio asimamishwe mwingine..Lakini kwanini ilikuwa vile.
Uhalisia ni kuwa Ukuhani ulikuwa kwanza kwa Anasi, lakini kwasababu za kisiasa ambazo zilikuwa zikisimamiwa na dola ya Warumi wakati ule.. walimteua ndugu yake ( yaaani mkwe wake) ambaye ni Kayafa asimame kwa awamu nyingine…
Ni kwanini iwe vile..
Kwa warumi nafasi za kikuhani zilikuwa ni moja ya nafasi nyeti, zenye nguvu kubwa ambazo zisipodhibitiwa walihisi uasi unaweza kutokea, na kuhatarisha ufalme, hivyo kupungumza nguvu zao hawakuwa wanawaacha makuhani wamalize muhula wao wote, mpaka kifo.kwasababu sheria ya kikuhani ilikuwa kifo ndio mwisho wa ukuhani, hivyo wenyewe waliwastaafisha makuhani…
Ndicho kilichotokea kwa Anasi, alikatizwa ukuhani wake na warumi akapewa mkwewe Kayafa. Jambo ambalo ni kosa kwa agizo la Mungu.
Yohana 18:13
[13]Wakamchukua kwa Anasi kwanza; maana alikuwa mkwewe Kayafa, yule aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule.
Japo kwa wayahudi waliendelea kumheshimu Anasi zaidi ya Kayafa kama ni kuhani sahihi kwa Bwana…lakini Kayafa pia walimpokea maana ndiye aliyekuwa anaendesha shughuli zote za kikuhani.
Ndio maana hata wakati Bwana Yesu anakamatwa, wayahudi walimpeleka kwanza kwa Anasi kabla ya Kayafa. Hiyo kuonyesha walimtambua Anasa hata baada ya kuondolewa ukuhani
Hivyo wote waliheshimika ndio maana wanatajwa kama makuhani.
Ni nini tunafunzwa katika habari zao?
Mkanganyiko.
Si ajabu kwanini nyakati zile mifumo ya kidini haikuweza kumtambua Kristo ijapokuwa alijidhihirisha kwao kwa namna zote..
Wayahudi walivunjika vunjia kwanza kiiamani licha ya kuwepo makuhani wawili…walikuwepo pia mafarisayo na waandishi.. na madhehebu mengine kadha wa kadha.
Mfano tu wasasa uwepo wa madhehebu mengi..ikidhaniwa kuwa Mungu yupo huko.
Leo hii kila mtu ana lake..Lakini je Kristo ni hayo?
Embu tuwazie kwa wakati ule…
Kuhani mkuu halisi (Yesu Kristo), alikuwa akizunguka huku na huko akiwahubiria maskini wa roho habari njema, akiwafanya huru waliosetwa na shetani, akiwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao (Luka 4), sio kuunda dini, au dhehebu au taasisi, fulani, Sio mashindano, n.k.
Sio kwamba taasisi Haziifai, zinafaa sana lakini je, Kazi za msingi za Kristo zinapewa kipaumbele?
Makuhani wakuu wa tatu waliokuwepo.. Kati ya hao Kristo ndiye aliyekubaliwa, hivyo mfuate yeye.
Amen