Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

SWALI: Naomba kujua tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi ?, kama tunavyosoma katika 2Wakorintho  7:1

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na UCHAFU WOTE WA MWILI NA ROHO, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.


JIBU: Ili tuwe wakamilifu kwa kiwango cha  kuweza kuzikaribia ahadi za Mungu, Tujue kuwa Mungu anataka tuwe watakatifu kote kote yaani Mwilini na rohoni.

Sasa hapo anaposema tujitakase na Uchafu wote wa mwilini. Anamaanisha kuwa tujiweke mbali na dhambi zote zinazozalika katika miili yetu. Mfano wa dhambi hizi ni kama vile, uzinzi, ulevi, wizi, uvutaji sigara, utukanaji, uvaaji mbovu, kama vile vimini na suruali kwa wanawake, kujichubua, kujipaka make-up, kutoa mimba, kuvaa milegezo,  kujichoraji tattoo, na ushoga, utumiaji wa madawa ya kulevya na mambo mengine yote yanayofanana na hayo, ambayo asili yake ni mwilini.

Na pale aliposema tuweke kando Uchafu wa rohoni, Anamaanisha dhambi zote zinazotoka ndani ya mtu, ambazo hazihusiani na mwili moja kwa moja, mfano wa dhambi hizi ni kama vile, wivu, hasira, tamaa, mawazo mabaya, unafki, uchoyo, husuda, fitna, majigambo, kiburi, ibada za sanamu, uongo. Hizi ni dhambi ambazo zinazalika ndani, na Mungu anazichukia sana, kama vile tu anavyozichukia zile zinazozalika katika mwili.

Hivyo tujue kuwa Mungu anaangalia kote kote, Kuna watu wanadhani kuwa Mungu anaangalia roho tu, hatazami mwili. Ndugu, mwili wako unathamani sawa na roho yako mbele za Mungu, kwasababu siku ile ya mwisho si roho yako tu itaokolewa, bali hata na mwili wako pia (kasome biblia utalithibitisha hilo). Hivyo mtukuze Mungu katika mwili wako, usidanganywe na mafundisho ya manabii wa Uongo,  wanaokuambia Mungu anatazama roho haangalii mwili. Hizi ni nyakati za mwisho, Tii Neno la Mungu Zaidi ya maneno ya mwanadamu. Kwasababu hilo ndilo litakalokutetea siku ile, na hilo ndilo litakalokuhumu siku ile. Neno la Mungu ni upanga. Liogope sana.

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Neno Buruji lina maana gani katika biblia?

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

Jaa ni nini katika biblia?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
2 Comments
Newest
Oldest Most Voted
Inline Feedbacks
View all comments
Mercy ndunge
Mercy ndunge
4 months ago

Nimependanzwa na mafudisho yenu mungu wa mbinguni walinde