Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

SWALI: Biblia inamaanisha nini inaposema “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?(Yuda 1:23)


JIBU: Maneno hayo utayasoma katika vifungu hivi;

 Yuda 1:22 “Wahurumieni wengine walio na shaka,

23 na wengine waokoeni kwa kuwanyakua katika moto; na wengine wahurumieni kwa hofu, MKILICHUKIA HATA VAZI LILILOTIWA UCHAFU NA MWILI.

24 Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu”;

Kama tunavyosoma vifungu hivyo, vinaeleza wajibu wa kila aliyeokoka katika kuwavuta wengine katika Imani. Mtume Yuda anaeleza yapo makundi mbalimbali ya watu waonaopaswa kuokolewa, lipo kundi la watu  ambalo linapaswa lihurumiwe kwa hofu, yaani lichukuliwe katika uchanga, na utulivu, livutwe kwa upendo wa Mungu tokea mbali, kundi hili ni la watu wote ambao hawamjui Mungu, wanaoishi duniani leo hii. Walevi, wezi, wazinzi, waoabudu sanamu, n.k.

Lakini lipo kundi lingine linalopaswa kuokolewa kwa kunyakuliwa katika moto. Unajua mpaka mtu awe  ndani ya moto, huhitaji kumbembeleza bembeleza, ili kumtoa, unachopaswa kufanya ni kumnyakua  tu atoke kule kwa gharama zozote zile, kwasababu akiendelea kubaki kule muda si mrefu atakufa. wapo watu ambao unaona kabisa wanakwenda kuangamia kwa mienendo yao ya dhambi, wapo wengine unaona kabisa wapo katika dakika za mwisho wamalizie mwendo wao hapa duniani, na bado hawajaokoka, wapo watu ambao wameshakata tamaa kiasi cha kwamba kilichobakia kwao ni kujiua tu siku yoyote, wapo watu ambao wamefungwa katika minyororo na mateso ya ibilisi, wao wenyewe hawawezi tena kufanya chochote juu ya maisha yao , n.k. Sasa watu kama hawa wanapaswa waokolewe kwa nguvu ya ziada. Kwa kuwafungua na kuwaombea sana, na kuwafuatialia kwa ukaribu sana, na wengine kwa kuwahubiria injili ya Jehanamu ili wajue huko wanapoelekea ni wapi, waogope wageuke kabla kifo hakijawakuta..

Sasa katika kazi hiyo yote ya uokoaji, mwandishi anasema.. “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”. Yaani kujilinda nafsi zenu, na nyinyi msije mkachukuliwa katika dhambi zao. Na ndio maana hapo anatumia mfano wa vazi lililotiwa unajisi kwa uchafu. Katika agano la kale vazi lililotiwa unajisi ni vazi lililovaliwa na mtu mwenye ukoma. Ambalo lilikuwa ni rahisi kumuambikaza mtu mwingine ukoma huo endapo atalishika au kulivaa.  Yaani kwa ufupi Nguo zote zilizokuwa zinatiwa unajisi wa aina yoyote ile, uwe ni ule unaotoka mwilini au vyovyote vile uliweza kumtia unajisi hata mtu mwingine asiyestahili endapo tu atazigusa au kuzivaa. (Walawi 21:11, Hesabu 6:6).

Yapo matendo ambayo, ni rahisi kutiwa na watu wengine unajisi kwayo, unapokwenda kumubuhiria mzinzi, hakikisha na wewe huna uzinzi ndani yako, unapokwenda kumuhubiria mlevi hakikisha na wewe vimelea vya ulevi havipo ndani yako, vivyo hivyo na kila mtu unayekwenda kumshuhudia.  Unapaswa ujichunge wewe mwenyewe kwanza. Kwasababu shetani naye anatenda kazi.

Wagalatia 6:1” Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, UKIJIANGALIA NAFSI YAKO USIJE UKAJARIBIWA WEWE MWENYEWE”.

Hiyo ndio maana ya kulichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

MAMA UNALILIA NINI?

Je mtu anayeua anabeba dhambi zote za yule aliyemuua?

Herode aliliwa na chango, Je, chango ni nini kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments