PETE YA DHAHABU PUANI MWA NGURUWE.

Nini maana ya “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”


Jibu: Turejee..

Mithali 11:22 “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”

Kabla ya kujua kwa undani maana ya mstari huu, hebu tujifunze kidogo juu ya Nguruwe, na pete inayowekwa puani mwake.

Nguruwe ni mnyama mwenye sifa ya uchafu, na asiyekuwa na ustaarabu, anaweza kuoshwa na baada tu ya kumaliza kuoshwa akarudi kwenye matope..Biblia inatuthibitishia hilo..

2Petro 2:22 “Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”

Sasa pamoja na tabia hiyo ya uchafu na kukosa ustaarabu nguruwe waliyonayo, bado wana tabia nyingine ya kuchimba chimba chini ya ardhi, au kwenye mashamba na kwenye zio kwa kutumia “pua zao” kwa lengo la kutafuta chakula, au utofauti wa mazingira.

Tabia hiyo ya kuchimba chimba kwa kutumia pua, inawafanya kubeba tabia nyingine ya uharibifu usiokuwa wa kawaida,

Sasa wafugaji wa nguruwe ili kulidhibiti hilo, huwa wanaweka pete katika pua zao lengo ni ili wanapojaribu kuchimba chimba kwa kutumia pua zao, basi ile pete iliyowekwa puani iwaumize na waache au kupunguza tabia hiyo ya uharibifu.

Sasa hizi pete si za urembo, bali zinakuwa kama Hereni kwenye pua ya nguruwe, na zinakuwa ni za chuma..tazama picha juu..

Sasa inapotokea Mfugaji anamwekea nguruwe pete ya dhahabu badala ya chuma isiyo na thamani..itakuwa ni jambo la ajabu sana na la kushangaza..kwani nguruwe kamwe hajawahi kuthamini kitu cha thamani, na hata yeye mwenyewe hajithamini soma Mathayo 7:6

Sasa anapowekewa kitu cha thamani puani mwake, ni kitu cha ajabu na kinachoshangaza..

Kwa mantiki hiyo hiyo Biblia inajaribu kuufananisha uzuri wa mwanamke na PETE YA DHAHABU, na mwanamke asiye na busara inamfananisha na NGURUWE.

Kwamba Mwanamke aliye na uzuri wa uso halafu akakosa busara ni sawa na kitu cha thamani kilichowekwa mahali pasipostahili.

Mwanamke mzuri wa uso/wa nje halafu hana heshima kimwonekano ni sawa na pete puani mwa nguruwe,

“Uzuri” na “Busara” ni lazima viende pamoja, lakini ukiwa ni mzuri halafu huna busara ya kiMungu, unafananishwa na nguruwe.

Sasa swali ni je hii busara inapatikana wapi?

Chanzo cha Busara halisi ni YESU KRISTO, kwamba unapompokea YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, basi hapo tayari umeshafungua mlango wa busara kuumbika nakuanza kufanya kazi ndani yako.

Na kazi hiyo ya kujaza  busara ndani yako ni ya Roho wa Mungu atakayeingia ndani yako baada ya wewe kuokoka….Utaanza kuona  kiwango chako cha hekima kinaongezeka, na ueledi katika masuala ya kiroho na kimwili.. na hiyo busara itaulinda uzuri wako wa nje na ule wa ndani kama maandiko yanavyosema..

Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;

11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi”

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Kwanini Mungu aliwazuia walemavu wasimtumikie madhabahuni kwake?(Walawi 21:16-24)

Maana ya Mithali 29:20 Je! umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno?

Mithali 29:20

Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye

Mtu mwenye kuhamaki.

Ni mtu anayezungumza maneno kwa haraka, yaani anayezungumza bila kufikiri, au kujizuia.

Vitu kama mizaha, ugomvi, hasira, uongo, na mafarakano, huzaliwa na tabia kama hii ya watu kunena bila kufiriki.

Kwamfano, mtu anaweza kukutukana, na wakati huo huo hasira ikawaka ndani, sasa kwasababu huwezi kujizuia, unajikuta unarudisha majibizano, hatimaye na wewe unafungua kinywa chako unatukana.

Au labda unatambua jambo Fulani ambalo si jema, na pengine ukilisema linaweza lisiwe na maana yoyote, kinyume chake likazua ugomvi, au kumuabisha mwingine, au sintofahamu, lakini wewe kwasababu huwezi jizuia unalisema, mwishowe matatizo yanazuka makubwa yasiyokuwa na lazima.

Watu wanaoapa, ni matokeo ya kunena bila kufikiri, mafarisayo ambao walitenda dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni kwasababu ya maneno ambayo hayana hekima nyuma yake.

Mathayo 12:36  Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.

Mpaka hapo unaweza kuona ni kwanini mpumbavu anaweza kuonekana ana afadhali kuliko mtu mwenye kuhamaki.

Mstari huu unatukumbusha nguvu iliyopo katika maneno, biblia inasema ulimi ni kama moto ni kiungo kidogo lakini kinawasha misitu, hivyo hatuna budi kuwa wazito katika kunena,  tukifiri kwanza ndipo tuseme. Yakobo 1:19

19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;

Maneno yana nguvu, kila siku yatupaswa tujifunze kudhibiti vinywa vyetu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

 

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

 

 

 

 

Je wana wa Israeli waliofia jangwani, walienda mbinguni au jehanamu?

JIBU: Wakiwa jangwani wana wa Israeli walitenda  makosa  ya aina mbili.

  1. Makosa yaliyopoteza Ahadi
  2. Makosa yaliyopoteza Uzima wa milele.

Makosa yaliyopoteza Ahadi ndio yalikuwa yale ya kutokuamini. Mfano Mungu alipowatoa jangwani, na kuwavusha, mara nyingi walionyesha hali ya kutoamini, Kosa ambalo liliwafanya Mungu aghahiri kuwafikisha kule alipowaahidia, ambapo ni nchi ya Kaanani ibubujikayo maziwa na asali, Na kilele cha kosa hilo kilikuja  pale wale wapelelezi waliporudi katika kuichunguza nchi, na kutoa ripoti za kule, kwamba wao wanaonekana kama mapanzi, hivyo wote wakaanza kulia na kutaka kurudi Misri, Ndipo Mungu akakasirika sana na kuapa kuwa wote  hawataiona hiyo nchi ya Kaanani isipokuwa Kalebu na Yoshua, kwasababu wao hawakuonyesha kutokuamini.

Hesabu 14:21-24

21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana;
22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;
23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona;
24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki

Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hawatakwenda mbinguni, kwasababu wapo waliotubu,hata wakati ule ule

Kwahiyo kusema adhabu ile ndio iliwapelekea moja kwa moja kupoteza mbingu si sahihi.

Kwasababu Mungu aliendelea kutembea nao kwa wingu lake, baadaye akawainua viongozi, wa kuwaaamua na Pamoja na wazee, akawamwagia  Roho wake, (Hesabu 11:25). Hivyo kama Mungu kasingekuwa nao, basi hayo yote yasingefanyika, kwasababu Mungu hawezi kuwaongoza wafu.

Lakini yapo makosa ambayo yaliwagharimu adhabu ya kupoteza kabisa uzima wa milele. Na makosa kama hayo ndio yale ya makusudi kabisa, mfano wa hayo ni yale ya kuvunja amri za Mungu, kama vile kutengeneza sanamu ya ndama  na kuiabudu, Kuzini, kuwa na miungu mingine, na kuhalifu sabato za Mungu .

Makosa kama hayo ndio yaliyopelekea  kupoteza uzima wa milele, ndio maana ukichunguza utaona watu kama hawa walipokea adhabu za moja kwa moja.     Hivyo ni kuwa makini sana na neema ya Mungu.

Hata sasa, zipo dhambi za aina mbili zinazozungumziwa kwenye maandiko, dhambi za mauti, na dhambi zisizo za mauti.

Kwa urefu wa maelezo yake, pitia hapa>>> DHAMBI YA MAUTI

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?

Kwanini Roho Mtakatifu amzuie Paulo kuipeleka injili Asia? (Matendo 16:6-7).

KUMBUKA NI AMRI MPYA!

Yohana 13:34

[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 

Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..

Ni amri ipi hiyo mpya?

Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?

Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana

Mambo ya Walawi 19:18

[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA. 

Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…

“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”

Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.

Je upendo wa Yesu ulikuwa upi?

Upendo wa upeo.

Yohana 13:1

[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo. 

Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..

Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..

Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo

Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.

Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.

Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)

Je amri hii mpya tunayo?

2 Yohana 1:5

Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane. 

Bwana awe nawe.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.

JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.

1 Samweli 30:6

[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake. 

Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.

Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe, 

Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe, 

Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..

Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.

Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.  

Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu. 

Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.

Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.

Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KATIKA UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA

1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”.

Biblia inatufundisha kuwa “Watu wazima” katika Akili, lakini tuwe watoto wachanga katika uovu, sasa ni nini maana ya kuwa watoto wachanga katika uovu?

Tukiwatazama watoto wachanga tunajifunza mengi, lakini jambo kuu tunaloweza kujifunza ni “Ukamilifu” watoto wadogo wanyonyao wanakuwa hawana hatia, sio waongo, si waasi, si walevi, si wazinzi, si wauaji, si wadhalimu, si wahuni, si waasi na mambo mengine maovu hayapo kwao, Na ndio maana Bwana YESU alisema kuwa ni lazima na sisi tugeuzwe kitabia na kuwa kama watoto wachanga..

Mathayo 18:3 “akasema, Amin, nawaambia, MSIPOONGOKA NA KUWA KAMA VITOTO, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni”.

Lakini haishii tu kusema tuwe “watoto katika uovu” bali pia tuwe “watu wazima katika akili”.. Mtu mzima katika akili ni Yule aliyeyabatilisha mambo mabaya, ya kale… mtoto anayechezea matope na kupenda kula peremende kila siku anapokuwa mtu mzima, ndipo anapoyabatilisha mambo ya kitoto na kuwa mtu mzima (hapo tunasema ameimarika kiakili).

Vile vile mtu ambaye alikuwa katika machafu ya dunia (ambayo ndio mfano wa uchafu wote wa utotoni), anapompokea YESU basi ya kale yanakuwa yamepita na sasa amekuwa kiumbe kipya.

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Lakini mtu aliye nje ya imani, na kuendelea na machafu yote ya dunia, kibiblia anakuwa hana akili, na anafananishwa na mnyama.

Zaburi 49:20 “Mwanadamu mwenye heshima, IWAPO HANA AKILI, Amefanana na wanyama wapoteao”.

Ndio kwani biblia imesema mtu aziniye hana akili kabisa (soma Mithali 6:32, Mithali 7:7), na mtu anayemdharau mwenzake pia hana akili (Mithali 11:12).

Kwahiyo ni lazima tuache mambo ya kale, na kumgeukia Kristo, ili tupate akili, na mwenye uwezo wa kutubadilisha ni YESU tu peke yake, lakini wanadamu wengine wote hawawezi kutusaidia kitu, je umempokea huyu YESU?.. Je unauhakika Kristo akija leo unakwenda naye?.

Kama bado haujampokea YESU unangoja nini?.. maisha ya dhambi na anasa yamekusaidia nini?.. je ukifa leo utaenda wapi?

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

UFANYE BIDII KATIKA KUSOMA.

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika KUSOMA, Kuonya na Kufundisha”.

Wakristo wengi hawapendi “KUSOMA” wanapenda “kusomewa”.. hawapendi “Kujifunza” wanapenda “Kufundishwa” hawapendi “Kujiaminisha” wanapendwa “kuaminishwa”… Kwaufupi wanapenda kutafuniwa na kusaidiwa kila kitu na wanadamu.

Ni kweli MUNGU anatumia watu, lakini “hategemei watu”.. Ukitegemea kusaidiwa kila kitu katika mambo ya rohoni, imani yako itakuwa imesimama juu ya watu, kiasi kwamba Yule mtu unayemtegemea akisomee maandiko, au akufundishe akirudi nyuma wewe nawe ni lazima utarudi nyuma tu.

Akibadilika wewe nawe utabadilika tu, akifa kiroho wewe nawe huna siku nyingi za kuwa hai kiroho.. iko hivyo, kwasababu imani  yako ipo kwake hata kama hukiri hilo.

Lakini Biblia inatufundisha kila mtu “KUSOMA” tena kwa bidii.. sio kusoma Geografia, au hisabati au siasa.. bali KUSOMA NENO LA MUNGU.

ZIFUATAZO NI FAIDA CHACHE ZA KUSOMA NENO LA MUNGU, badala ya kusubiri kufundishwa.

   1. UNAMPA ROHO MTAKATIFU NAFASI YA KUSEMA NAWE.

Unaposoma Biblia binafsi, katika utulivu… kunakuwa kuna “tafakari” za kiMungu zinapita ndani ya kichwa chako, hizo tafakari nyingi zinakuwa ni sauti ya Roho Mtakatifu, kukufundisha kwa kile unachokisoma.

Sasa unaposikiliza mhubiri akihubiri, yeye anazunguza kile Roho alichokiweka ndani yake, na anaposema hawezi kurudia mara mbili, alichokisema kinakuwa kimepita, hivyo huna nafasi ya kutosha wewe kukichakata kile ulichokipokea, labda upate nafasi ya kurudia kusikiliza tena mafundisho yake katika utulivu..

Lakini unapokuwa msomaji wa Biblia, unayo nafasi ya kwenda kituo baada ya kituo huna haraka hivyo inakuwa unampa nafasi nzuri Roho Mtakatifu kusema nawe.

   2. UNAPATA UHAKIKA WA MAMBO.

Ukiwa msomaji wa Biblia binafsi, unakuwa unapata uhakika wa mambo uliyowahi kuyasikia au kufundiswa, kama ni ya kweli au si  ya kweli, lakini usipokuwa msomaji ni ngumu kuhakiki mambo.

   3. UWEZO WA KUUNGANISHA MAANDIKO UNAONGEZEKA.

Unapokuwa msomaji mzuri wa Neno ule uwezo wa kuyaunganisha maandiko, kwamba andiko hili linaladnana na andiko lingine, unapanda!.. hiyo itakusaidia sana kumwelewa MUNGU.

   4. HAMASA YA KUMJUA MUNGU ZAIDI INAONGEZEKA.

Unaposoma mwenyewe Biblia zaidi ya kufundishwa, ile hamasa ya kutaka kumjua MUNGU zaidi inaongezeka, kila mstari unaoumaliza unakupa hamasa ya kuendelea mbele kusoma mwingine, na hiyo ni faida kubwa kwani utajikuta inaipenda Biblia na inakuwa ni kitabu chako.

    5. UNAONGEZA UZOEFU WA KUIJUA BIBLIA.

Unapokuwa msomaji wa Neno uzoefu wako wa kulisoma Neno unaongezeka, ninaposema uzoefu, simaanishi kulizoelea Neno, La!.. bali ile namna ya kujua mpangilio mzuri wa Maandiko na mistari unapanda, hiyo inakuongezea urahisi wa kujifunza Neno la kulielewa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WOKOVU UKIHARAKISHA USIUZUIE.

Wokovu ni kama farasi ambaye ana uwezo wa kusafiri kwa mwendo wa kasi sana au kwa mwendo wa taratibu sana, inategemea tu, nia ya mwendeshaji.

Halikadhalika Ikiwa wewe ni mshuhudiaji,(mhubiri wa injili) ni vema kufahamu tabia hizi, mara nyingi wokovu mpaka ukamilike ndani ya mtu, yaani kukubali toba, kuamini, kikiri, kubatizwa, kujazwa Roho, huweza kuchukua muda fulani wa wastani au mrefu kidogo, ambao huusisha kushawishi, kufuatilia, kufundisha madarasa mbalimbali imani, ya ubatizo na Roho Mtakatifu, n.k. ndipo aamini na kukamilishwa.

Lakini tembea pia ukijua kuwa si wakati wote hili litakuwa hivyo…

Zipo nyakati Mungu anabadili gia, atataka kukamilisha mambo yote hata kwa siku moja tu…yaani kumwokoa, kumbatiza na leo leo kumjaza Roho…Ukiona jambo hilo kamwe usijaribu kupunguza mwendo huo..Ni Mungu kaamua kuongeza kasi ya usafiri wake.

Je hili lipo kibiblia?

Ndio…wakati fulani Paulo na Sila walikamatwa na kutupwa gerezani, wakiwa kule usiku ule tunaona walianza kumwimbia Mungu na kumsifu sana…na mara vifungo vya gereza vikafunguka..yule askari msimamizi alipoona tukio lile aliogopa sana na kutetemeka…akasema nifanye nini ili niokoke? Wakawaambia wamwamini Bwana Yesu utaokoka. Na usiku ule ule walitubu, na kubatizwa nyumba yote, na kisha wakajazwa furaha ya Roho Mtakatifu yeye na nyumba yake yote..

Yaani kitendo cha usiku mmoja…familia nzima inaokoka, inabatizwa, inapokea tunda la Roho..

Matendo ya Mitume 16:27-34

[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. 

[28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. 

[29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; 

[30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? 

[31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. 

[32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. 

[33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo. 

[34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu. 

Kama ni mchakato, wengine humaliza hata wiki au miezi mpaka nyumba nzima kuamini na kubatizwa, ..lakini hapa ilikuwa ni masaa machache sana…tena ya usiku..

Utaona jambo kama hili lilijirudia kwa Kornelio..Petro alipoenda kwake, hata kabla hajamaliza mazungumzo yake, akidhani kuwa inahitaji madarasa marefu, inahitaji vyuo vya kuufafanua msalaba…pale pale katikati ya mazungumzo watu wakashukiwa na Roho Mtakatifu wakajazwa, wakapewa ile hatua ya mwisho kabisa ya wokovu ndipo wakaenda kubatizwa…(Matendo 10).

Mambo ambayo yamkini yangechukua madarasa ya muda na maombezi ya kuwekewa mikono ya kipindi kirefu..

 Na yule mkushi aliyekutana na Filipo gaza naye vivyo hivyo hakusubiri kwanza alike kushi, pale pale njiani alibatizwa.

Matendo ya Mitume 8:36-39

[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? 

[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.] 

[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. 

[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi. 

Vivyo hivyo, fahamu kuwa kuna nyakati Mungu anaisukuma mioyo ya watu kwa nguvu sana..tena sana kiasi kwamba mioyo yao hufunguka na kutamani kukamilishwa katika yote…

Ukiona hivyo, msaidie haraka, usifikiri kwamba inahitaji maarifa mengi ili mtu kuokolewa…bali moyo uliowazi..hilo tu..

Pengine wewe ni kiongozi..unaona mtu ameamini…usingoje ratiba za mwisho wa mwaka za ubatizo kanisa kwako…ndipo ambatize huyo mtu, angalia tu mwitikio wake…Ndio lipo pia kundi lingine ambalo litahitaji mafundisho kwanza…kutokana na viwango vyao vya upokeaji, ila usilisahau hili pia.

Jifunze kwenda na kasi zote za injili.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

Biblia inaposema watu wakali hushika mali sikuzote, ina maana gani? (Mithali 11:16)

SHUKURU, ITA NA JULISHA.

Labda unaweza kujiuliza maana yake nini maneno haya, tusome Zab.105:1

Zaburi 105:1 “Haleluya. Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake, Wajulisheni watu matendo yake”.

“Kumshukuru Mungu” na “Kuliitia jina lake” na “ Kuwajulisha watu matendo yake” Ni mambo ya msingi sana kuyafanya.

Haya ni mambo makuu matatu (03) yaliyo ya muhimu na msingi sana, hebu tuyasome tena mahali pengine katika maandiko..

Isaya 12:4 “Na katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake; Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, Litajeni jina lake kuwa limetukuka”.

Soma pia 1Nyakati 16:8.

   1. MSHUKURU MUNGU

Kumshukuru Mungu ni agizo la Mungu!.. Kumshukuru Mungu kwaajili ya uzima aliokupa, pumzi, ulinzi, Rehema, Fadhili na mambo mengine yote ni jambo linalompendeza MUNGU sana.

     2. LIITE JINA LA YESU

Vivyo hivyo, KULIITIA JINA LA MUNGU ni agizo!.. Tunapopitia vitisho, majaribu au mapito mengine yoyote ni lazima tuliitie jina la Mungu wetu, kwasababu hata waabuduo miungu huita majina ya miungu yao, ndivyo maandiko yanavyotuonesha..

1 Wafalme 18:25 “Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng’ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini”

Nasi tunapaswa tuliitie kila wakati jina la YESU, ambalo ndilo pekee lituokoalo ( Matendo 4:12).

Watu wa MUNGU tunapoliita jina la YESU, vifungo vinakatika na mbingu na nchi zinatetemeka, tangu Siku za Sethi mpaka leo jina la MUNGU lina nguvu ile ile ya kuokoa.

Mwanzo 4:26 “Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la BWANA”.

Soma pia Mwanzo 12:8, Mwanzo 13:4, Mwanzo 21:33,  Mwanzo 26:25,  Utaona ilikuwa ni desturi ya watu wote wa Mungu enzi za Biblia.

Na tunapoliitia jina la Bwana, anaitika.

Zaburi 99:6 “Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake, Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake, Walipomwita Bwana aliwaitikia”

Lakini pia kama hatujamaanisha kumfuata Mungu na tukaliitia jina lake tunajiletea matatizo badala ya msaada, soma ile habari ya wana  watano wa Skewa utaelewa vizuri. (Matendo 19:13-15).

Kwahiyo ili tujidhi vigezo vya kuliita jina la MUNGU, ni lazima tumaanishe kumfuata MUNGU na kuacha dhambi (huo ndio Msingi).

2 Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”.

         3.WAJULISHE WATU MATENDO YA MUNGU.

Kumshuhudia Mungu mbele za watu, kwa kazi zake ni nguzo ya tatu ya msingi…

Na ushuhuda wa kwanza tunaopaswa kushuhudia ni kufufuka kwa YESU, Hilo ni tendo kuu la kwanza Mungu alilolifanya, kumfufua YESU kutoka katika mautini… na kwa kupitia huyo tunapata ondoleo la dhambi.

Shuhuda nyingine kama kuponywa magonjwa, kuokoka na ajali na majanga na kubarikiwa zinasimama kuthibitisha ushuhuda mmoja mkuu wa kufufuka kwa YESU na ondoleo la dhambi kwa wote wanaomwamini.

1 Yohana 5:11 “Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe”.

Je wewe uliyempokea YESU kama mwokozi, je unafanya hayo?…je Una Desturi ya kumshukuru MUNGU kila wakati, au mambo yote anayokutendea wewe unaona ni kawaida tu?.

Na je una desturi ya kuliitia jina la MUNGU, kama huna desturi hiyo anza sasa utaona matokeo yake..

Na mwisho unayo desturi ya kushuhudia matendo makuu ya MUNGU?..Kama bado anza leo.

Kwa mambo hayo matatu, tutaweza kuangusha Ngome na kumpendeza MUNGU.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WATU HAWA WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA HUKU NAKO

Kama tunavyofahamu katika maandiko Mitume walipofika mji wa Thesalonike kwa ajili ya injili, na kukutana na wenyeji wa mji ule, na kusikia walichokihubiri maandiko yanatuambia walipiga kelele sana na kusema maneno haya;

“Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako”

Matendo ya Mitume 17:6

[6]na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Ulishawahi kutafakari kwa ukaribu maneno hayo walichokimaanisha?

Wanasema;

Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Maana yake ni kuwa ulimwengu na wao, ni kama vitu viwili tofauti…

Wamefika na huku pia….yaani wameshaushinda ulimwengu wanakuja na huko kwao kumalizia walichokifanya kule..

Hii ikiwa na maana…mitume walishapata ushindi kabla hata ya kufika maeneo yote…

Kuna mahali pajulikanapo ulimwenguni ambapo tayari walishapashinda.

Sasa huo ulimwengu ni upi?

Chukulia mfano wa dunia ya sasa.. kuna usemi wasemao nchi za Afrika ni dunia ya tatu.. ijapokuwa wote tupo kwenye sayari moja, ujulikano dunia, lakini uhalisia dunia zipo tatu…Zile nchi zilizoendelea sana…Kama vile Marekani, urusi, China, ufaransa..ni dunia ya kwanza… na zile zilizo katika uchumi wa kati ni dunia ya pili na hizi maskini ni dunia ya tatu..

Sasa ikitokea mtu akayapiga hayo mataifa makubwa na kuyateka, maana yake huyo mtu ameiteka dunia, ameipindua dunia…..hata kama hajapigana na haya mengine madogo..lakini ikiwa nguvu zake zimewashinda wale basi hawa wengine ni maji tu.

Vivyo hivyo waamini wa wakati ule walionekana, wanamapinduzi wakubwa sana..kwasababu ushindi wao ulianzia kwenye vichwa.

Sasa huu ulimwengu ni upi?

JIBU: Ulimwengu wa Roho.

Zamani zile dini zilijulikana kama msingi mikubwa sana inayosukuma mielekeo ya mataifa.. hivyo Kristo alipokuja aliweza kuvunja misingi ya imani potofu na dhaifu kuanzia pale pale Israeli mpaka miisho ya dunia. Alileta Nuru duniani ambayo giza lolote halikuweza kulishinda..

Yohana 1:4-5

[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 

[5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. 

Ndio maana kipindi cha injili utaona Wayahudi wengi waliokoka, wapagani wengi wakaacha miungu yao..wakaichoma moto, utaona hata kule Efeso mungu mke aliyeabudiwa ulimwenguni kote (Matendo 19:27), mitume walipofika habari yake ikaishia pale pale, tofauti na zamani manabii walishindana sana na mabaali lakini hawakuweza kuyashinda..kwasababu hakukuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mkuu wa ulimwengu huu(shetani)

Yohana 16:11

[11]kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 

Hivyo ulimwengu wa roho uligeuzwa juu chini, mapepo yaliwakimbia wengi, watu walifunguliwa kwenye vifungo vya giza..makaburi waliwaachia wafu..kila siku watu waliongozeka kumjua Mungu…na kuachana na dhambi.

Matendo 19:19-20

[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. 

[20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. 

Huu ndio ulimwengu sugu uliopata tiba…ulimwengu wa giza, kama kichwa cha mifumo yote mibovu ya dunia…uliwekwa chini…

Hivyo wale watu walipoona imani za watu zinageuzwa kwa kasi hata za maakida wakubwa,(Matendo 13:7-12) majemedari, watu wenye vyeo, wake kwa waume, nao pia wanaigeukia imani..wakatambua ya kuwa kila kitu kimekwisha sasa, sisi ni masalia..tu.

Walijiona kama mapanzi, ni sawa na wana wa Israeli walipoweza kuliangusha taifa la Misri, hata kabla ya kufika Yeriko, Wale watu wenyewe walishajiona kama mapanzi..Kwasababu kichwa cha ulimwengu kimeshaangushwa.

Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tujue kuwa sisi tuliomwamini Yesu…tayari tumeshaupindua ulimwengu kwa Injili iliyokwisha fika kuzimu kwenye kiti cha enzi wa shetani…

Hakuna chenye nguvu ya kutuzuia sisi tena, sisi ni watawala wa dunia.

Wanasiasi, hawawezi kutuzuia, wanadamu hawawezi kutusimamisha..wao ni kama mapanzi tu kwetu…

Hatuna budi kuuinua ujasiri wetu wote…tufikie mataifa yote kuhubiri injili kwasababu ulimwengu tayari tumeshaupindua…hatuhitaji kwenda tena kuupindua..sisi ni kumalizia tu masalia. Unasubiri nini usiamke kuihubiri injili? Amka sasa…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI