Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 16:33

[33]Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

JIBU: Kura zilipigwa kwa namna mbalimbali zamani, njia iliyokuwa nyepesi ndio hiyo ambayo kipande cha shuka, au nguo, iliyofumwa vilitumiwa kukusanya kura za watu mbalimbali ambazo ziliandikwa katika vipande vya vibao vidogo vidogo, au mawe kisha hukorogwa, na lile litakalotoka la kwanza au kuchukiliwa humo basi ndio kilichosahihi..

Wengine walitumia makopo, wengine kofia, kisha kuzikoroga kura na ile itakayotoka au kuchaguliwa cha kwanza huko ndio huaminika kuwa chaguo sahihi

Hivyo, zipo nyakati ambazo Mungu aliruhusu baadhi ya mambo yaamuliwe kwa kura kama vile kugawanya nchi n.k.Soma(Hesabu 26:55, Yoshua 18:6-10)Lakini si kila jambo, mengi Mungu alitoa majibu kwa njia ya moja kwa moja, kwa kufunuliwa aidha kwa kupitia manabii au maono au ndoto.

Sasa tukirudi katika mstari huo..

Anaposema..

Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.

Maana yake ni kuwa Japo kuwa kupiga kura ni tendo linaloonekana la kibinadamu lakini ikiwa linafanyika katika Bwana, majibu ya kweli hutoka kwake.

Yule atakayechaguliwa, au kile kitakachopendekezwa, ndio jibu sahihi kutoka kwa Bwana.

Katika Biblia tunaona mtume Mathiya alichaguliwa kwa kura, lakini kabla ya kupiga kura ile, mitume walimtanguliza kwanza Mungu katika uchaguzi wao,waliomba na kumsihi Bwana aingilie uchaguzi wao..kisha kila mmoja akaandika pendekezo lake na jawabu likatoka na ndio likawa kweli jibu sahihi la Mungu.

Matendo 1:23-26

[23]Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.

[24]Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,

[25]ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.

[26]Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

Wakati mwingine tunaweza kulaumu, viongozi tuliowachagua, tukasema waliiba kura n.k. lakini kama Mungu asingetaka wawepo pale wasingekuwepo tu, kwasababu yeye ndio anayewamilikisha watawala haijalishi watakuwa ni waovu au wema..

Danieli 2:21

[21]Yeye hubadili majira na nyakati; huuzulu wafalme na kuwamilikisha wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa;

Hii ni kuonyesha uhuru wa Mungu wa kuchagua, yapo mambo kwetu tutaona kama tumeamua sisi, au yametokea kwa bahati, lakini kumbe ni Mungu kapanga..kwake yeye vitu havitokei kwa bahati, bali vyote chini ya makusudi yake.Mungu ndiye ayaruhusuyo yote..

Utukufu una yeye milele na milele.

Amina.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP-GROUP

Mada Nyinginezo:

Je ni halali kupiga kura kanisani kuchagua viongozi?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

HAKUVAA NGUO SIKU NYINGI.

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

NI WAPI UTAKUTANA NA MALAIKA WA BWANA?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments