SWALI: Naomba kufahamu tunaposema Bwana Yesu asifiwe tunamaanisha nini? Na ni nani anayepaswa kuisema hiyo salamu, na kwanini wengine wanasema ‘shalom’ badala yake?
JIBU
‘Bwana Yesu asifiwe’ ni kauli inayotangaza kustahili kwa Yesu sifa kwa ile kazi njema aliyoifanya Hapa duniani.
Yesu ndiye Mtu pekee ambaye alikubali kuingia gharama ya kuacha enzi na mamlaka Mbinguni, na kuja kuishi hapa duniani kwa kusudi moja tu la kutukomboa sisi,katika dhambi zetu, akateswa na kujaribiwa sana, akafa baadaye akafufuka na hata sasa yupo hai ameketi kama mpatanishi wa sisi na Mungu,..
Kiasi kwamba kwa kupitia Yeye tunapokea msamaha wa dhambi, tunaponywa magojwa, tunamseta shetani, tunabarikiwa, tunawasiliana na Mungu moja kwa moja bila vikwazo vyovyote kwa damu yake.
Mtu Kama huyu ni lazima astahili kusifiwa..ndio maana inakuwa ni salamu ya Wakati wote BWANA YESU ASIFIWE..
Kwasababu ya nuru tuliyo ipata kwa kazi yake njema ya ukombozi.
Je ni nani anayepaswa kuisema?
Hakuna mtu anayekatazwa kuisema, lakini mtu asipojua kwanini Yesu asifiwe basi anaisema kwa unafki, Na Mungu hapendi unafiki. Kwamfano mtu ambaye hajaokoka, halafu anasema Bwana Yesu asifiwe, ni sharti ajiulize asifiwe kwa lipi wakati hakuna chochote kilichofanya na yeye katika maisha yake..
Ni sawa na mtu aliyeokoka aseme shetani asifiwe.. atasifiwa kwa jambo gani hapo wakati hakuna ushirika wowote alio nao na shetani. Lakini mganga wa kienyeji Akisema hivyo hiyo ni kweli kwasababu kuna faida amezipata Kwa shetani.
Salamu hii pia, au kauli hii, ni sahihi kutumika katika matamshi ya kiibada..mfano kwenye mahubiri, mafundisho, nyimbo, maombezi N.k. kwasababu katika Maeneo haya kazi za Yesu hudhihirishwa.
Lakini shalom Ni neno la kiyahudi linalomaanisha ‘Amani’. Ni Neno ambalo mtu yeyote anaweza kulitumia awe ameokoka au hajaokoka kwasababu ni Neno la kilugha zaidi kuliko kiimani. Ni sawasawa na sisi tunavyosema, ‘habari yako’. Mtu yeyote anaweza kutumia hilo neno. Lakini Bwana Yesu asifiwe ni Neno la kiimani ambalo anayestahili kulitamka ni mtu aliyemwamini Yesu tu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Print this post
Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.
Sasa Makosa kama haya,(ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.
Tutakwenda kuona aina tano (5) vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. [2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. [3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. [4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. [6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’
Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).
Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…
Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.
Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.
Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.
Mwanzo 4:10-13
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. [11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; [12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. [13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia
Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao
Kutoka 3:7-9
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; [8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. [9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.
Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.
Ufunuo 6:9-10
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. [10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.
Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.
5) Kilio (Shangwe) cha waovu.
Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kubwe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.
Mwanzo 18:20-21
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, [21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.
Je! Umemwamini Yesu?
Je una uhakika kubwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.
Mafundisho mengine:
Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)
ENDELEZA UPONDAJI.
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
Swali: Unakuta mtu anapitia tatizo fulani, halafu anasema.. ndio nimeandikiwa hivyo! Na siwezi kubadilisha.. sasa je mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya yampate na mwingine mema?
Jibu: Kifungu cha Biblia kinachosapoti kuwa mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya au mema ni kutoka katika kitabu cha Yeremia..
Yeremia 15:2 “Kisha itakuwa, hapo watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi, WALIOANDIKIWA KUFA, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa upanga; AU KUFA KWA NJAA, WATAKUFA KWA NJAA, au kutekwa nyara, watakuwa mateka”.
Kwa haraka andiko hilo laweza kueleweka kwamba wapo watu walioandikwa na MUNGU matatizo tangu mwanzo, lakini kiuhalisia haiko hivo.. hakuna mtu aliyeandikiwa na MUNGU matatizo, au shida..
Sasa kama hivyo ndivyo, nini maana ya andiko hilo ya kwamba “waliondikiwa kufa watakufa? (Yeremia 15:2)”
Mantiki ya “kuandikiwa hapo” inarejea sheria za Mungu huko nyuma.. kwamba iliandikwa “Mtu asiyeishi kwa sheria za Mungu atadhibiwa kwa sheria”… Kwamfano iliandikwa hivi katika Kumbukumbu 28:15-18..
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. 17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia. 18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.
17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.
18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Sasa kulingana na andiko hilo, mtu Yule ambaye ataacha kusikiliza sauti ya Bwana na atafanya mabaya… basi maandiko hayo ya laana yatampata, na hapo ni sawa na kusema kwamba “ameandikiwa laana”…
Lakini si kwamba Mungu anamchagua mtu na kumwandikia laana na mwingine anamchagua na kumwandikia Baraka!… La!..Bali laana zake na Baraka zake zinakuja juu ya mtu kwasababu ya matendo ya mtu.
Kwahiyo mtu aliyekufa kwa upanga huwenda ni kwasababu aliua kwa upanga, na hivyo andiko hili ndio aliloandikiwa na limetimia kwake..
Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga….”
Na makosa mengine yote ni hivyo hivyo, yameshaandikiwa adhabu yake.. kwahiyo mtu akiyatenda atakuwa anapokea malipo ya yaliyoandikwa na kuichukua hiyo nafasi.
Bwana atusaidie, tusitimize maandiko ya Laana, bali tutimize maandiko ya Baraka ili tuwe miongoni mwa waliondikiwa Baraka.
Je umempokea YESU, Umebatizwa kwa Roho Mtakatifu?.. kama bado unasubiri nini?…fahamu ya kuwa unyakuo wa kanisa umekaribia sana na siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu wanafufuliwa.
Maran atha!
UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.
ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?
LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia yetu (Zab. 119:105).
“Maneno” yanafaa kuthibitisha jambo, lakini “matendo” ni bora zaidi.. Hebu tujifunze kwa Bwana YESU ambaye alitumia matendo zaidi kuliko maneno.
Kipindi ambacho Yohana Mbatizaji anawatuma wanafunzi wake kwa YESU kumwuliza kama yeye ndiye au wamtazamie mwingine, jibu la YESU halikuwa “Ndio mimi ndiye”.. bali aliwaambia wale watu wamrudie Yohana wamwambie wanayoyaona, viwete wanatembea, vipofu wanaona..
Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza, 3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine? 4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; 5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema”.
Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,
3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;
5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema”.
Umeona hapo KRISTO hakutumia maneno kujieleza yeye ni nani bali matendo.. Kwa ufupi kazi zake zilimshuhudia yeye ni nani, na sio hapo tu bali kila mahali ilikuwa ni hivyo hivyo..
Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi. 25 Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia”.
Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.
25 Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia”.
Umeona, kumbe kazi (yaani matendo) ya YESU ndio yaliyomshuhudia??… Je na sisi tutumie kipi kutangaza ushuhuda wetu?.. maneno yetu au kazi zetu?..Bila shaka Matendo yetu yanafaa zaidi kuliko maneno.
Tutatambulika kuwa sisi ni wakristo kwa matendo na si maneno tu.. tutatambulika sisi ni watumishi kwa matendo na si maneno matupu tu!, tutatambulika sisi ni wakweli kwa matendo na si kwa maneno tu.
Ukisema umepata badiliko moyoni, uthibitisho wa badiliko hilo ni matendo ya mwilini, kwamba kama umebadilishwa tabia basi huwezi kuendelea kuiba, au kutukana au kuvaa vibaya au kufanya uzinzi, uthibitisho wa badiliko la ndani ni matendo ya nje, na si maneno tu..
Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.
Hivyo tutie bidii kutengeneza matendo yetu zaidi ya maneno yetu.
Bwana YESU atusaidie..
MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU
USHUHUDA WA RICKY:
MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?
Swali: Tunasoma katika Yohana 1:29 kuwa Yohana anamshuhudia Bwana YESU kuwa yeye “mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu”.. Lakini tukirudi katika Mathayo11:3 tunasoma tofauti, Yohana anawatuma wanafunzi wake wamwulize kama yeye ndiye Kristo au wamtazamie mwingine, sasa swali ni je Yohana alimtilia shaka Bwana Yesu au hakumwamini tangu mwazo?.
Jibu: Ni ngumu imani ya Yohana kutikisika kirahisi lakini hebu kwanza turejee kitabu cha Mathayo…
Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza, 3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine? 4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona; 5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema. 6 Naye heri awaye yote asiyechukizwa nami”.
Ni kweli Masihi ajaye alikuwa ametabiriwa kuwa atakuja na nguvu kuwaokoa Israeli na utumwa wa maadui zao, na Israeli wote walitazamia kabisa kuwa Kristo atakayekuja atawafungua na utumwa mgumu wa warumi.. lakini haikuwa hivyo kwa YESU KRISTO, kwani alianza kushughulika na dhambi za wana wa Israeli, zaidi ya Taifa.. Hiyo ikawafanya baadhi ya watu kumtilia mashaka YESU kama yeye ndiye KRISTO (Yaani Masihi).
Na bila shaka Yohana hakuwa na wasiwasi wa YESU kuwa Masihi, kwani tayari alishaonyeshwa wakati anambatiza YESU kuwa Yule atakayembatiza na ishara ya hua ikionekana juu yake basi huyo ndiye Masihi, na ni wazi kabisa Yohana alijua kuwa wakati wake aliokuwa anaishi duniani, Kristo naye alikuwa anaishi, ila hakumjua ni nani mpaka wakati wa ubatizo, Roho kama Hua aliposhuka juu ya Bwana, na mbingu kufunguka. (Mathayo 3:16-17).
Sasa kama ni hivyo ni kitu gani kilichomfanya Yohana Mbatizaji atume wanafunzi wake kwa YESU na kumwuliza swali ambalo tayari alikuwa na jibu lake?.
Jibu ni kwamba baadhi ya watu ikiwemo wanafunzi wake Yohana bado hawakuwa na uhakika wa moja kwa moja kama YESU ndiye KRISTO, kwahivyo kwa kusikia Neno linalotoka moja kwa moja kinywani mwa YESU, ingeweza kuwafanya waamini zaidi, hivyo Yohana lengo lake huu ni wanafunzi wakasikie na kujihakikishia wenyewe, kwamaana muda wake wa kuishi ulikuwa umekaribia kuisha na watakayebaki naye ni YESU. Na walipokwenda walipata majibu.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Yohana hakuwa na mashaka na Bwana YESU, bali wanafunzi wake na baadhi ya watu, na hiyo ni kutokana na kwamba Bwana YESU hakuwa anajitangaza hadharani kuwa yeye ni KRISTO.
Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi”.
Soma pia Luka 22:77..
Je umempokea YESU?.. Una uhakika kwamba YESU akirudi leo utakwenda naye?.. kama bado upo nje ya Imani fahamu kuwa upo hatarini sana, hivyo mkaribie YESU leo usamehewe dhambi zako na upokee ujazo wa Roho Mtakatifu. Shalom.
Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)
NI NINI TUNAJIFUNZA KWA YOANA NA MANAENI?
“Hakuna aniulizaye unakwenda wapi”, maana yake nini? (Yohana 16:5).
Nini maana ya “manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana” (Mathayo 11:13)
Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?
Turejee..
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi; 21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Kumbukumbu 2:20 “(Nchi hiyo nayo yadhaniwa kuwa ni nchi ya Warefai, hapo kale Warefai walikaa humo; lakini Waamoni huwaita Wazamzumi;
21 nao ni watu wengi, WAKUBWA, WAREFU, KAMA WAANAKI; lakini Bwana aliwaangamiza mbele yao; wakawafuata wakakaa badala yao”
Wazamzumi walikuwa ni watu warefu na wakubwa na wenye nguvu walioishi nyakati za kale, mfano wa hao ni akina Goliathi..
Watu hawa katika enzi za kale ndio watu waliokuwa wanatisha na kuogopeka sana.. walikuwa ni hodari wa vita na wenye maendeleo makubwa, walijenga miji mikubwa na walikuwa na silaha zenye nguvu, hakuna Taifa lililowaweza kwa uhodari wao.
Lakini pamoja na kusifika kuwa na nguvu nyingi za mwili, na uhodari mkubwa, bado mbele za MUNGU mazamzumi wote si kitu, Goliathi aliangushwa na kijana Daudi aliyekuwa mtumishi wa MUNGU, Mazamzumi waliokuwepo Yeriko waliangushwa na vijana walionekana dhaifu wa kiisraeli, na zaidi sana Mazamzumi wote waliangamizwa na Bwana wakati wa gharika ya Nuhu (Mwanzo 6:4).
Kama Zamzumi wako ni “dhambi” mwambie Bwana amwangushe..kwa nguvu zako hutaweza.. kama Zamzumi wako ni kikundi cha watu fulani wabaya.. mwambie Bwana akuondolee hao watu, haijalishi ni hodari kiasi gani au wana uwezo kiasi gani, bado MUNGU ana uwezo wa kuwaondoa.
Unachopaswa kufanya ili Mazamzumi yote yaondoke ndani yako nan je yako, ni wewe kumwamini Bwana YESU na kukubali kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na pia kutafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia maishani mwako na kukutakasa kabisa kabisa.
Ikiwa bado haujabatizwa na unahitaji msaada huo basi wasiliana nasi kwa namba zetu.
Bwana YESU akubariki.
Simoni Mkirene aliubeba msalaba wa Bwana Yesu au la?
Je! aliyemwua Goliathi ni Daudi au Elhanani.
Maana ya Mithali 29:21 “Amtunduiaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe”
MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.
Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?
Luka 15:20
[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..
Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..
Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..
Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..
Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..
Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…
Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…
Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?
Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.
Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.
Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?
Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.
Shalom.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU
JAWA SANA MOTO ULAO.
TENGENEZA NJIA YAKO.
Marko 9:24
[24]Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Habari ya yule mzee ambaye kijana wake alivamiwa na mapepo sugu ya kumtupa motoni tangu utoto wake, na baada ya kuhangaika sana kwa madaktari na kila aina ya matabibu, hadi mitume nao kushindwa kumponya, hatimaye akakutana na Bwana Yesu..
Akamwambia ‘Ukiweza’ Bwana neno utuhurumie na kutusaidia… lakini saa hiyo Hiyo Yesu akamjibu….Ukiweza?..
Mimi unaniambia ukiweza?
Marko 9:23
[23]Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Kuonyesha kuwa Imani yake, haikuwa kamili, lakini, saa hiyo hiyo akaweka tegemeo lake lote kwa Yesu na kumwamini..’Naamini’…lakini pia nisaidie ‘kutokuamini kwangu’..
Hiki ni Moja ya ombi ya uwazi na la ukweli kabisa ambalo tunaweza kulisoma kwenye biblia…
Ni kweli ameamini, lakini imani yake si timilifu, anapambana sana kuifanya iwe sawa.. hivyo pamoja na hilo akamwona na Bwana amsaidie…kuonyesha tabia ya kujiachia kikamilifu kwa Bwana…kwamba sio tu kutendewa muujiza lakini pia kusaidiwa..
Saa hiyo hiyo Yesu hakumfukuza, wala kumkemea, wala kumwambia kafanye hivi au vile kwanza… bali akamkemea yule pepo Na hatimaye kijana akawa mzima saa ile ile.
Imani, ya kweli haimaanishi kwamba mashaka yatapotea…bali ni kuchagua kujimimina kwa Bwana na kuweka tegemeo lako lote kwake tu, hata kama moyo wako utakuambia wewe mbona unamashaka mashaka, mbona huna imani, mbona maneno yako mwenyewe yanathibitisha umekata tamaa..
Hakika hapo usiache kuomba na kukiri, ukiulilia pia msaada wa Bwana akusaidie imani yako iwe Kamilifu, kwa kujimimina tu hivyo hatimaye utayaona mambo makubwa akikutendea..
Usianze kujilaumu kwa mashaka mia uliyoonyesha, wewe egemea tu kwa Yesu bila kuondoa mguu wako hapo…atakujenga..Yule baba hakuondoka kwa Yesu, kwasababu ya madhaifu yake bali aliendelea kukaa pale pale. Kwasababu imani inajengwa kwa mahusiano sio kwa utimilifu wetu.
neema ya Mungu hizidi mapungufu yetu..kiri.udhaifu wako kwake, lakini onyesha kumtegemea yeye, hapo nguvu za Mungu utaziona.
Shetani atataka ujilaumu, katika shida yoyte lakini sema…
“Naamini, Bwana, nisaidie kutokuamini kwangu.
WhatsApp
Waebrania 12:29
[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.
Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa
Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)
Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…
Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.
Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;
Isaya 33:14
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele? [15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?
[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.
Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..
Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.
Hii ndio mbio yetu wote…
Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.
Shalom
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.
Swali: Kutawa kwa Elisabeti miezi mitano maana yake nini?
Jibu: Turejee..
Luka 1:24 “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKATAWA miezi mitano, akisema, 25 Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana katika siku zile alizoniangalia ili kuniondolea aibu yangu mbele ya watu”.
Luka 1:24 “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKATAWA miezi mitano, akisema,
25 Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana katika siku zile alizoniangalia ili kuniondolea aibu yangu mbele ya watu”.
Tafsiri ya “Kutawa” ni “kujitenga”.. hivyo Kiswahili kingine cha mstari huo ni hiki… “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKAJITENGA miezi mitano”
Hivyo Elisabeti alijitenga na jamii ya watu pengine kwasababu za kumshukuru MUNGU kwa muujiza aliomtendea wa kubeba mimba uzeeni, au kwa nia ya kuepusha uadui kutoka kwa watu ambao ungetokana na wivu, au pengine kwasababu nyingine za kupumzika na kumtafakari MUNGU kwa faragha!. Mojawapo ya hizo au zote zaweza kuwa sababu za kujitenga kwake.
Na tunaona lilikuwa ni jambo jema kwa Elisabeti kwani baadaye alipokutana na Mariamu ndugu yangu, alijazwa Roho Mtakatifu na kuzungumza kiusahihi habari za Mariamu na Bwana Yesu aliye tumboni mwa Mariamu.
Hiyo inatufundisha nini?
Si kila Baraka kutoka kwa MUNGU inapokuja ni wakati wa kutangaza na kushuhudia wakati huo huo, wakati mwingine ni vizuri kujitenga/kutawa kwa muda ili kutumia kumshukuru MUNGU, na kuomba ulinzi wa Baraka ile,..kuwahi kutangaza Baraka za MUNGU au mlango MUNGU aliokufungulia kabla ya kupata utulivu ni hatari kwako na kwa utakaoenda kuwaambia.
Hivyo ni vizuri kutokuwa mwepesi wa kuzungumza bali ni vizuri kuwa mwepesi wa kupata faragha na MUNGU na kutafakari fadhili zake kabla ya kuzungumza au kushuhudia.
Bwana atusaidie.
MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?