Leo hii watu watashangaa inawezekanikaje mtu kuishi bila kuzini, mtu kuishi bila kutazama pornography, kuishi bila pombe, kuishi bila sigara, kuishi bila kuongoa matusi, inawezekanikaje mtu kuishi maisha ya furaha wakati huna pesa, inawezekanikaje unapitia shida zote hizo lakini bado tumaini lako lote lipo kwa Kristo, inawezekanikaje katika kizazi hiki cha Sodoma na Gomora, kutokuvaa suruali kwa mwanamke, na kuweka mawigi na ma-lipstick na marangi usoni, wala kupaka uwanja kama Yezebeli, inawezekanikaje unadumu katika imani bila kutetereka…