Danieli 12:3 “Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele.”
Yuda 1:12 “Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachukuliwayo na upepo; ni miti iliyopukutika, isiyo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa kabisa;
13 ni mawimbi ya bahari yasiyozuilika, yakitoa aibu yao wenyewe kama povu; NI NYOTA ZIPOTEAZO, AMBAO WEUSI WA GIZA NDIO AKIBA YAO WALIOWEKEWA MILELE”.
Amosi 5: 8 “mtafuteni YEYE AFANYAYE KILIMIA NA ORIONI, NA KUKIGEUZA KIVULI CHA MAUTI KUWA ASUBUHI, NA KUUFANYA MCHANA KUWA giza kwa usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; Bwana, ndilo jina lake;”
Ayubu 9:7 “Aliamuruye jua, nalo halichomozi; Nazo nyota huzipiga muhuri.
8 Ambaye peke yake ni mwenye kuzitandika mbingu, Na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.
9 Yeye afanyaye hizo NYOTA ZA DUBU, na ORIONI, na hicho KILIMIA, Na makundi ya nyota ya kusini”.
Ayubu 38: 31 “Je! Waweza kuufunga mnyororo wa KILIMIA, Au kuvilegeza vifungo vya ORIONI?
32 Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake?….”
Mada Nyinginezo:
INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA.
HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).
MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.
SIRI YA KUASI KATIKA KANISA LA MUNGU.
About the author