Title June 2019

JE! UNA MASIKIO YANAYOSIKIA?

Yohana 2:13 ‘’Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu.

14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng’ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi.

15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng’ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao;

16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara.

17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.

18 Basi Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya? 19 Yesu akajibu, akawaambia, Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.

20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.

22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu.’’

Tukisoma kisa hichi ni rahisi kuwahukumu Makuhani na Mafarisayo na Wayahudi kuwa walikuwa watu wasiofikiri…watu wanaoona miujiza lakini hawaamini…ni kweli kuna mambo ya kulaumiwa lakini si yote…. hebu leo kwa sehemu tuchunguze kama ni kweli walikuwa hawafikiri wakati wote..

Jaribu kuchukua mfano wewe ni mtumishi wa Serikali, labda unatumika kwenye shirika fulani la Umma..halafu siku moja anatokea mtu usiyemjua anaingia mahali mnapofanyia kazi na kuanza kuvuruga vuruga nyaraka na hati muhimu..huku anawapazia sauti na kuwaambia…msigeuze serikali ya Raisi wangu kuwa pango la mafisadi….na mnapojaribu kumzuia na kumwuliza yeye ni nani na nani kamtuma kufanya vile, anawajibu…jiuzuluni wote na mwachie ngazi leo na baada ya siku tatu nitalinyanyua hili shirika upya.

Unafikiri ni kitu gani..kitagonga kwenye akili…Moja kwa moja aidha utajua huyo mtu karukwa na akili..Na pili jambo litakalofuata ni kutafuta njia ya kwenda kumshitaki haraka…Kwasababu anakuja kuharibu kazi na kuzungumza vitu visivyoeleweka…eti atalinyanyua shirika ndani ya siku tatu!!…Shirika hili mpaka kulifikisha hapa tumetumia miaka Zaidi ya 20 wewe unataka kulinyanyua ndani ya siku tatu!..

Hebu fikiria huyo mtu hata akienda mahakamani atashindaje kesi?..kwasababu amesikiwa na watu wote kwa kinywa chake akisema atalinyanyua shirika kwa siku tatu.

Na ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu mahali Fulani, alipowakuta wayahudi wanafanya biashara kule Hekaluni,aliwaambia wasigeuze nyumba ya Baba yake kuwa pango la wanyang’anyi lakini walipomuhoji kwa ishara gani unafanya haya? Akawaambia libomoeni hekalu hili na ndani ya siku tatu nitalisimamisha.

Sasa wayahudi walidhani wamemsikia vizuri na kumwelewa…kumbe hawajamwelewa ingawa wamemsikia,..ndio maana Neno linasema ‘kusikia mtasikia lakini hamtaelewa..Kutazama mtatazama lakini hamtaona (Mathayo 13:14)’…Walidhani hekalu litakalobomolewa na kusimamishwa ndani ya siku tatu ni hilo la mawe wanaloliona mbele yao..kumbe kulikuwa na hekalu lingine ambalo lilikuwa ni mwili wa Bwana Yesu.

Na waliendelea na huo upofu mpaka siku ya mwisho, pale walipomsulibisha

Walisema maneno haya:

Mathayo 27:40 ‘’Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani’’.

Lakini tunaona waliokuja kumwelewa ni wanafanzi wake tu! Tena dakika za mwisho, Wale waliokuwa wanatembea naye kila siku. Ndio waliopewa neema ya kumwelewa Bwana Yesu alikuwa anamaanisha nini katika maneno yake. Sio kila mtu tu alikuwa anamwelewa Bwana Yesu.

Ndugu huo upofu mpaka leo upo! Unaendelea kwa watu wengi wasio wanafunzi wa Yesu Kristo..Bwana hana wanafunzi 12..alianza na wanafunzi 12, lakini sasa anao wanafunzi wengi…Na hao ndio anaowafunua macho ya kuyaelewa maneno yake…wengine walio nje maneno ya Yesu yatakuwa ni mafumbo kwao…wataona wanamwelewa sana Bwana Yesu lakini kumbe hawamwelewi..

Watadhani kwasababu Bwana aliyageuza maji kuwa divai basi alihalalisha unywaji wa pombe, lakini hawaelewi kuwa Pia kitendo cha Bwana kula na makahaba na wenye dhambi lengo lake halikuwa kuhalalalisha ukahaba wao wala dhambi zao…Alifanya vile ili kutafuta njia ya kuwavuta watubu kwa upendo wake….Na watu walipomwita kuwa mlevi haikumaanisha kuwa yeye kweli ni mlevi..wewe unaweza kuitwa mlevi na maadui zako lakini isiwe ni mlevi kweli…kadhalika walipomwita yeye ni mlafi haikumaanisha Bwana Yesu alikuwa ni mlafi kweli…

Alipomwita Herode Mbweha!..hakumaanisha kumtukana!!…ingekuwa ndio hivyo, basi yeye mwenyewe amejitukana sana…alipokuwa anajiita mwanakondoo?..au anapowafananisha watu wake na kondoo..kwa wale wafugaji wanaelewa ni afadhali mtu akuite mbwa kuliko kondoo.

Kadhalika aliposema mkawabatize watu wote kwa jina la Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu hakumaanisha hivyo vyeo bali alimaanisha ni jina moja ambalo ndio la Baba, na ndio hilo hilo la Mwana na ndio hilo hilo la Roho Mtakatifu na hilo sio lingine Zaidi ya Jina la YESU (Matendo 2:38).

Na aliposema…’’aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele’’..hakumaanisha tukamkamate na kumchinjwa na kunywa damu yake kama simba…bali alimaanisha kuula katika roho na kuinywa damu yake katika roho..Na chakula cha Roho zetu ni Maneno tunayosikia…Yakiwa ni Maneno ya Mungu, basi ni chakula bora cha uzima wa milele, na yakiwa maneno ya yule mwovu basi ni chakula kisichofaa cha mauti.

Kwahiyo Biblia inatufundisha tuwe na masikio yanayosikia, na macho yanayoona..ili kwamba tunaposoma Biblia tuielewe…Na hayo tutayapata kwa kuwa wanafunzi wa Yesu tu!..kwasababu hao ndio Bwana alikuwa anawapa kuelewa maneno yake…

Na vigezo vya kuwa mwanafunzi ni hivi..

Luka 14:25 ‘’Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 MTU YE YOTE ASIYEUCHUKUA MSALABA WAKE NA KUJA NYUMA YANGU, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

28 Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia?

29 Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki,

30 wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza.

31 Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini?

32 Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.

33 Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu’’.

Je! Umeuchukua msalaba wako?..je! umewachukia ndugu zako, baba yako na mama yako?…kuchukia kunakozungumziwa hapo sio kuchukia mtu kwa hasira au chuki ya moyo…hapana! Bali ni kitendo cha kuyakataa na kuyachukia maamuzi ya wazazi wako au ndugu zako yanayopingana na mapenzi ya Mungu kwako, na kuamua kuyafuata yale mapenzi ya Mungu tu!..Huko ndio kuwachukia kunakozungumziwa hapo juu!!…kama baba yako ni mlevi na anakutaka na wewe uwe kama yeye…hapo unayachukia hayo maamuzi na kusema hapana!..kama ni msengenyaji hivyo hivyo..kama ni mlarushwa na wewe anataka uwe kama yeye unasema No! kama ni mchawi au Mwenda kwa waganga..na anataka kukufundisha na wewe uwe kama yeye..hapo unasema hapana! N.k. 

Na pia ili uwe mwanafunzi biblia inasema unapiga gharama!! Ukristo sio jambo la kujaribu na kutoka! Biblia inasema utachekwa….Ukiamua kumfuata Bwana Yesu, hesabu kuwa kuna kuonekana mpumbavu, kuonekana mshamba…wakati mwingine kuonekana umerukwa na akili…Na pia ukristo sio mteremko muda wote…piga hesabu kuwa kuna wakati Bwana anaweza kukuacha kwa kipindi Fulani kirefu pasipo kuzungumza na wewe kwa njia unayotaka! Je! Utaendelea kuwa naye!…utakapopitia shida, dhiki na wakati mwingine misiba utamwacha?

Pia piga gharama! Je asipokupa vile vitu unavyohitaji! Utaendelea kuwa naye?.

Na mwisho anasema ‘mtu yeyote asiyeacha vyote alivyo navyo hawezi kuwa mwanafunzi wangu’..Kuacha vyote ulivyonavyo ni mfano wa wakina Petro…waliacha vyote walivyo navyo na kumfuata Bwana…Kuacha vyote ulivyo navyo sio lazima kwenda kuuza mali zako au hazina yako…bali ni kuishi kana kwamba hivyo vitu sio vya kwako…kiasi kwamba hata ikitokea kimepotea hakipo kwenye akili yako…umeshakiacha siku nyingi…akili yako imetawaliwa na kutenda mapenzi ya Mungu na kuyaishi…hakina chochote katika moyo wako…kiwepo au kisiwepo vyote kwako ni sawa sawa tu.

Ukishapiga hizo gharama, na kujitwika msalaba wako, biblia inasema umekuwa mwanafunzi wake…ambao wamepewa Neema ya kuzijua siri za ufalme wa mbinguni…

Hivyo kama hujampa Kristo Yesu Maisha yako, ni vizuri ukafanya hivyo leo… Na ili uwe mwanafunzi wake piga gharama za kumfuata…na Bwana akusaidie katika hilo.

Mungu akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

NINI MAANA YA KUISHI KWA KUUKOMBOA WAKATI?.

Shalom mwana wa Mungu, ikiwa Mungu amekupa neema ya kuiona siku hii ya leo, basi usipuuze kujifunza ni kitu gani anataka kutoka kwako leo?, Kukutana na ujumbe huu si kwa bahati mbaya bali Mungu anakusudi na wewe juu ya wakati aliokupa hapa duniani.

Tukisoma Waefeso 5:15-18 biblia inatuambia hivi.. “15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 MKIUKOMBOA WAKATI kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”.

Nataka leo tujifunze nini maana ya kuukomboa wakati kimaandiko. Tunajua tafsiri rahisi ya hili neno kuukomboa wakati ni “kuutumia muda vizuri”, tulipokuwa shuleni moja ya vitu ambavyo vilikuwa vinawachukiza sana walimu,ni pale walipokuwa wanaona wanafunzi wanautumia muda wao vibaya (hawaukomboi wakati), Hususani pale mwalimu anapotazama muda aliobakiwa nao mbeleni jinsi ulivyo mchache, topics bado ni nyingi za kusoma, halafu mwanafunzi, anaruka ruka hajisomei, anapiga kelele darasani, hazingatii masomo, haudhurii darasani, inawatia sana hasira waalimu pamoja na wazazi. Vivyo hivyo na katika mambo mengine.

Lakini pia katika upande wa maandiko, tunafundishwa tuukomboe wakati, kwasababu biblia imeweka wazi kabisa kuwa zamani hizi ni za UOVU, na tunauokomboa wakati kwa namna gani? Biblia inasema ni kwa kutaka kufahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Mungu kwetu.Huko ndiko kuukomboa wakati kuliko na maana mbele za Mungu.

Ndugu huu ulimwengu una mambo mengi na mahangaiko mengi, Ni kweli tunafahamu kwa sehemu moja au nyingine hatuwezi kuepuka mihangaiko kama ipo lakini tunaonywa tuishi kama watu wenye hekima, na sio wajinga, tukijua kuwa sisi ni wapitaji tu hapa duniani, na siku zetu zinakimbia kwa kasi sana, biblia inasema sisi ni kama MVUKE uonekanao kwa kitambo kisha kutoweka (Yakobo 4:14), Mvuke sio kama moshi ambao unaweza walau ukauona ukipaa mawinguni, mvuke wenyewe hata kwenye dari haufiki umeshapotea, ndivyo maisha yetu yalivyo. Biblia inasema na mwanadamu ni kama maua ambayo hayo hayana maisha marefu,(Zaburi 103:15 ”Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo).

Hata kama tutaishi miaka 60 tu au miaka 120 bado siku zetu zitabakia kuwa ni chache sana. Hivyo swali tunalopaswa kujiuliza tukifa leo huko tunapokwenda ni kitu gani cha maana kitaoneka tumekifanya hapa duniani?. Kwasababu kule hatutaulizwa tulikuwa na majumba mangapi, au magari mangapi, au biashara ngapi, au watoto wangapi,wala hatutaulizwa tulikuwa maskini kiasi gani LA! Tutaulizwa ni kitu gani tumeongeza katika ufalme wa mbinguni..Tukiliweka hilo akilini basi itatusaidia sana kuishi kwa uangalifu.

Tunamwona Bwana wetu Yesu alijua nini maana ya kuukomboa wakati, angalia alichowaambia wanafunzi wake..Yohana 9:4 ”Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi…”

Unaona Japo alikuwa ni Mungu katika mwili alijua nini maana ya muda, kuwa kuna kipindi kinachoitwa usiku (KIFO) ambacho mtu yoyote atatamani kufanya kazi ya Mungu asiweze, Na tunamwona Bwana wetu japo aliishi miaka 33 tu lakini kazi aliyoifanya ina matunda makubwa mpaka sasa tunayafaidi. Hiyo ni kwasababu aliukomboa muda wake vizuri hapa duniani ipasavyo. Wakati mwingine hakuwa na muda hata wa kula. Alipoletewa chakula.

NA SISI JE! TUNAWEZAJE KUUMBOA WAKATI WETU?

Tujijengee utaratibu wa kila siku mpya inapoanza tumwombe Mungu atusaidie tufanya kitu ambacho kitakuwa na manufaa katika ufalme wa mbinguni na katika maisha yetu ya rohoni… tuzitazame siku zetu ikiwa inaweza kupita siku nzima, wiki, mwezi bila kuona kitu chochote cha maana tulichokifanya kwa ajili ya maisha yetu ya rohoni au kwa ajili ya ufalme wa Mungu, basi tujue hatuukomboi muda haijalishi tunatengeneza mabilioni pa pesa kiasi gani kwa siku. Ndugu huu ndio wakati wa kuanza kuitengeneza njia yako upya mbele za Mungu, kabla ya siku ile kufika.

Muda ambao unautumia kuchati kwenye magroup ya whatsapp, au kusoma habari zisizokuwa na maana mitandaoni, komboa wakati kwa kutumia muda huo kujifunza Neno la Mungu, au kusoma mahubiri au mafundisho ya Neno la Mungu. hayo ndio mapenzi ya Mungu kwako, au tumia muda huo kukaa katika utulivu kumsifu na kumwimbia Mungu wako..peke yako au pamoja na wakristo wengine..

Tukiwa makazini kwetu, tumwombe Mungu atusaidie, sio wakati wote, tutakuwa buzy na shughuli, au kuongea na wafanyakazi wenzetu mambo ya kikazi, tutumie muda wetu wakati mwingine kuwashirikisha habari za Yesu, huku tukiwaelekeza katika vyanzo vizuri vya kupata habari za Mungu, kwa kufanya hivyo pia tutakuwa tumeukomboa wakati na siku yetu kuwa na maana mbele za Mungu.

Muda ambao tumekaa hatuna shughuli yoyote, tunaweza tumia muda huo kwenda kuomba, hata kama hatutakuwa na mahitaji wakati huo mbele za Mungu, lakini pia tumeagizwa kuwaombea wengine, hivyo tumia muda huo kuwaombea watu wengine, kuna ndugu zako, rafiki zako, jamaa zako, taifa lako, kanisa n.k..Kwa kufanya hivyo utakuwa umeukomboa wakati. Na pia maombi yanasaidia kuepukana na majaribu.

Kama biblia inavyosema Mungu utusaidie kuzihesabu siku zetu tupate mioyo ya hekima (Zab 90:12). Hivyo na sisi tupate leo hekima ya kujua kuwa muda unakwenda sana, na jukumu bado ni kubwa mbele yetu na mtihani ulio mbele yetu bado hatujauvuka. Basi tusiwe kama wajinga, tukaze mwendo, tuanze kutumia muda wetu sasa kwa vitendo kujifunza kwa bidii Neno la Mungu kuliko jana, tuombe, na tuifanye kazi yake pia kana kwamba hatuna tena mwaka mbele. Maana usiku waja asioweza mtu kuitenda kazi. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 


Mada Zinazoendana:

MIISHO YA ZAMANI.

SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

MWEZI NI ISHARA GANI KWETU?


Rudi Nyumbani

 

Print this post

CHANZO CHA MAMBO.

Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. karibu tujifunze Neno la Mungu ambalo ndio taa iongozayo njia zetu. Biblia inasema “Mjue sana Mungu ili uwe na Amani (Ayubu 22:21)”..Siku zote ukijua sababu ya jambo Fulani basi unapata amani. Amani inakuja baada ya kujua sababu ya jambo Fulani.

Leo tutajifunza juu ya vyanzo vya matatizo, na namna ya kuyatatua. Kama tunavyojua wengi wetu vyanzo vya matatizo mengi ni shetani..huo ni ukweli usiopingika. Lakini je! Shetani analetaje matatizo?.

Tukijifunza Mfano wa Ayubu, tunaweza kupata majibu baadhi, tunaona shetani alimshambulia Ayubu baada ya kupata kibali maalumu kutoka kwa Mungu, hiyo ikifunua kwamba shetani hawezi kumgusa mtu yeyote wa Mungu pasipo ruhusa yeyote kwa Mungu..

Hivyo Mungu anaporuhusu mtu ajaribiwe…anachokifanya ni kutoa ulinzi wake juu ya Yule mtu, na akishatoa ulinzi wake maana yake shetani anapata nafasi ya kumwingia. Hivyo anamshambulia.

Na shetani huwa ana njia kuu mbili za kuwashambulia watu.

1) Anatumia mapepo…Katika njia hii mtu atajikuta tu ameingia matatizoni pasipo kujua chanzo ni nini. Kumbe ni majeshi ya mapepo wabaya yamemvamia.

2) Na njia ya pili anatumia watu..(Na watu atakaowatumia ni aidha watumishi wake wa uongo wanaovaa mavazi ya kondoo lakini ndani ni mbwa-mwitu wakali…au atatumia wachawi na waganga)….atatumia watumishi wa uongo kuwajaribu wale wanaomjua Mungu, na atatumia wachawi na waganga kuwajaribu wale wasiomjua Mungu…au wakati mwingine atatumia vyote viwili kuwajaribu wale watu wanaomjua Mungu.

Sasa tukirudi kwenye mfano wa Ayubu..baada ya ulinzi wa kiMungu kuondoka juu yake…shetani alimletea majaribu wengi… Kama haikuwa ni kazi ya mapepo moja kwa moja basi kuna uwezekano mkubwa sana shetani alitumia watu Fulani kumfanyia Ayubu yale mambo…Alichofanya shetani baada ya kuona ukingo wa kiMungu umeondoka juu ya Ayubu ni pengine aliwatupia roho ya wivu watu baadhi waliokuwa wanamzunguka…na ile roho ilipowaingia pengine ikawasukuma kumwendea hata kwa waganga… labda walikwenda kwa mganga fulani maarufu kwa kipindi hicho mwenye nguvu, wakaenda na picha yake na za watoto wake..na nyayo zake labda..Na wakiwa kule wakaona wanafanikiwa kumwona kwenye kioo chao cha kichawi, na pengine huyo mganga akafanya mambo yake na kutuma kimbunga cha kichawi juu ya watoto wake wakiwa karamuni, na kwasababu ulinzi wa kiMungu umeondoka juu ya Ayubu jambo lile likafanikiwa na Kuwaua watoto wake wote. Na magonjwa ni hivyo hivyo ni kikundi Fulani cha maadui zake Ayubu kilihusika kumletea yale magonjwa.

Sasa labda baada ya tukio hilo pengine Ayubu aliona tabia Fulani za watu wanaomzunguka kufurahi..na pengine walisema vimaneno Fulani kuonyesha kuwa wao ndio walifanya vile. Sasa kwa jicho la haraka haraka kama Ayubu angekuwa sio mtu wa rohoni…angesema maadui zake wamemfanyia visa..Lakini Bwana alimpa jicho la Mbali kujua mwanzo wa Matatizo yake hayakuwa ni wale watu..bali alijua yalikuwa ni Mungu mwenyewe…kutoa ulinzi juu yake. Ndio maana aliishia kusema “Bwana alitoa na Bwana alitwaa, jina lake libarikiwe”…Alijua maisha yake ni makamilifu isipokuwa ni Mungu tu katoa ulinzi juu yake kwa makusudi Fulani. Angalia jinsi alivyouamini uhusiano wake na Mungu, kiasi cha kwamba hakuweza kuyumbishwa ni kitu chochote, na sisi je! tunaweza tukawa hivyo?.

Na mambo hayo hayo yanaendelea leo hii, watu wanatumiwa na shetani kukuharibu, pengine ni wachawi au waganga…na kushindwa kuelewa chanzo cha mambo yote ni nini?…chanzo cha mambo yote sio watu kukuonea wivu, au wachawi kukuchukia hapana!..chanzo cha matatizo yote ni Ulinzi wa kiMungu kuondoka juu yako..Usianze kupambana na watu wanaokuchukia, anza kutafuta mzizi wa tatizo ni wapi..kama Ayubu.

Ayubu alijua chanzo cha matatizo yake, kuwa ni Bwana ndiye kayaruhusu hayo lakini njia zake ni kamilifu…alijua sio dhambi ndani yake iliyosababisha ulinzi wa kiMungu uondoke juu yake.

Kadhalika na sasa tunapaswa tujitathmini, kama kuna jambo Fulani limetokea ambalo halipo sawa…chanzo chake ni nini?..Je! ni kama Ayubu? (Njia zetu ni kamilifu isipokuwa ni Bwana anatujaribu tu) au ni kwasababu ya dhambi zetu, kwasababu kitu pekee kinachotoa ulinzi wa kiMungu juu ya mtu ni dhambi…

Ukiwa mwasherati magonjwa yatakusumbua na wachawi watakusumbua sana, mapepo yatakusumbua sana hakuna namna utaweza kuwashinda, hata uombewe kiasi gani hakuna namna utaweza kuchomoka mikononi mwao…ukiwa mtazamaji wa pornography na mfanyaji wa masturbation ni hivyo hivyo…ukiwa ni mzinzi, ni shoga ni msagaji ni hivyo hivyo, watakusumbua na hakuna namna utaweza kuwashinda…Usidanganywe kuwa kuna mchungaji yeyote duniani mwenye uwezo wa kukuombea wachawi au mapepo yasikufikie wala kukudhuru, wala usidanganyike kuwa kuna maji yoyote au mafuta yoyote ya upako yanayowazuia wachawi wasiweze kufika nyumbani kwako…Usidanganyike kabisa ndugu…

Kitu pekee kinachoweza kufukuza na kuzishinda nguvu za giza juu ya maisha yako ni MAISHA YA UTAKATIFU katika Kristo Yesu, Uhusiano wako na Mungu ni wa kiwango gani, hicho tu! Wala hakuna kingine….Maisha unayoishi ndio yanayoamua ulinzi wa kiMungu uwe juu yako au uondoke.

Fanya uamuzi sahihi leo, usitazame wachawi, wala waganga, kama ndio chanzo cha matatizo yako…wala usiende kutafuta suluhisho kwa kuombewa, wala kupakwa mafuta..Suluhisho lipo kwako ambalo ndio chanzo cha mambo yote…suluhisho ni KUBADILIKA na kuishi maisha ya utakatifu, ambayo hayo yanakuja kwa kutubu kwanza dhambi zako zote, na kudhamiria kuziacha kabisa kuanzia sasa na kuendelea na kwenda kubatizwa na kisha kupokea Kipawa cha Roho Mtakatifu ambaye atakusaidia kushinda dhambi.

Ukifanya hivyo, ulinzi wa kiMungu utakuwa juu yako, haihitaji wewe kwenda kuombewa wala kupakwa mafuta, wala kuwaogopa wachawi…Utaishi kwa Amani sana, na wala hakuna chochote kitakachokugusa. Kwasababu nguvu iliyopo ndani yako ni kubwa kuliko ya kwao..Bwana Yesu alisema..

Luka 6.17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio;…… watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa;…”

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

HUDUMA YA (ELIFAZI, BILDADI, NA SOFARI).

JE! MUNGU ANASABABISHA AJALI?


Rudi Nyumbani

Print this post

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA;

Jina Bwana wetuYesu libarikiwe. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema kuiona hivyo nakukaribisha ndugu popote pale ulipo tushiriki pamoja Baraka Bwana alizotuandalia leo.

Tukisoma Zekaria 12:9-14, inasema. 

“ 9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu. 

10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Watu wanaozungumziwa hapo ni wayahudi (yaani Waisraeli) , Embu leo jiulize tu Israeli ni Taifa dogo sana kama mkoa wa njombe, ni taifa ambalo huwezi hata ukaenda na kukutana na vitu vya kuvutia huko au vya kushangaza kama mataifa mengine makubwa, lakini ni kwanini leo hii imekuwa ni JICHO LA DUNIA?. Wapo mbali na Mungu lakini ni watu wenye akili na wenye mafanikio makubwa duniani, jiulize siku wakiwa karibu na Mungu itakuwaje?

Hayo maandiko hapo juu ni lazima yatime, utafika wakati biblia inasema Roho ya neema itaachiliwa juu yao na watamwamini huyu Yesu ambaye sasa hawamwamini, Siku hiyo Watalia na kuomboleza baada ya kugundua makosa yao kuwa Yule waliyemsulibisha na KUMCHOMA MKUKI miaka 2000 iliyopita kumbe ndiye Masiya waliokuwa wanamsubiria kwa miaka mingi..Ile roho ya ufarisayo na usadukayo itaondoka juu yao.

Kama vile biblia inavyotabiri kutakuwa na maombolezo makubwa sana huko Yerusalemu wakitubu makosa yao.

Sasa hicho ndio kile kipindi ambacho mtume Paulo alikiandika katika

 Warumi 11:25 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili [anasema na sisi watu wa mataifa]; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.

27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao”.

Unaona hapo unabii huo utatimia katika hiyo siku?, Huo wakati wa Israeli kurudiwa na kutengwa na maovu yao upo karibuni sana, na utakapoanza tu basi ujue utimilifu wetu sisi mataifa utakuwa umeshawasili yaani kwa lugha nyingine neema kwetu itakuwa imeshaondoka na kurudi tena Israeli, na hiyo itaambatana na tendo KUU la UNYAKUO.

Sasa wayahudi ambao leo hii utawaona wanalia usiku na mchana pale kwenye ule Ukuta wa maombolezo (wailing wall). wakimwomba Mungu wa Ibrahimu baba yao aje kuwaokoa na maadui zao na kuleta utawala wa masihi duniani, ipo siku hayo maombolezo yatakoma, na ndipo Mungu atawarudia kwa kuwafumbua macho na kumwona YESU, Kumbuka Mungu aliwapofusha kwa makusudi kabisa wasimwamini Kristo ili sisi mataifa tuipate neema vinginevyo huyu Yesu wa thamani ambaye leo hii tunaifurahia neema yake, tungemsikilizia tu kwa wayahudi, sisi tungeendelea kuwa waabudu miti,vinyago, na wachawi. Na hata hivyo dunia ungekuta imeshakwisha siku nyingi, wakati ule ule tu Yesu aliokuwa ndio ungepaswa uwe ni wakati wa wao kurejeshewa ufalme wa dunia na Yesu.

Unakumbuka mitume walimuuliza Yesu baada ya kufufuka je! Huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme? Yesu akawaambia, sio kazi yenu kujua nyakati wala majira.(Matendo 1:6), Hii ikiwa na maana kuna wakati utafika watarudishiwa na huyu huyu masihi Yesu Kristo.

Hivyo huo wakati unafika, Pale Mungu atakaposimama tena upande wa Israeli na kuwashindania kwa nguvu nyingi kama alivyokuwa anafanya zamani, pale mataifa yote ulimwenguni yatakapoungana ili yaje kujaribu kuisambaratisha Israeli katika ile vita ya Harmagedoni ndipo hapo Kristo atakawapigania toka juu kwa nguvu na uweza mwingi…damu nyingi itamwagika sana, maadui wote wa Israeli watakufa kama kuku waliochinjwa wakaachwa, wakati huo Bwana atakapolipigania Taifa lake…. Tunalisoma hilo katika..

Zekaria 14:1 “Tazama, siku moja ya Bwana inakuja, ambayo mateka yatagawanyika kati yako.

2 Kwa maana nitawakusanya mataifa yote walete vita juu ya Yerusalemu; na huo mji utapigwa, nazo nyumba zitatekwa, nao wanawake watatendwa jeuri; na nusu ya watu wa mji watatoka kwenda utumwani; ila mabaki ya watu wa mji hawatakatiliwa mbali.

3 Hapo ndipo ATAKAPOTOKEA BWANA, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita.

4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.

5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu; kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku zaUzia, mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye.

Kwahiyo tusifurahie tu kuona leo hii Israeli inazidi kufanikiwa lakini badala yake tuogope na tujiulize maswali je! Wewe tumejiandaaje sasa?, neema ndio hivyo inaondoka kwetu, tazama hata hali ya ukristo sasa hivi duniani sio kama ile ya zamani, tazama mataifa ya ulaya ambayo ndio yalikuwa ya kwanza kutuleta injili lakini sasa jinsi yanavyozidi kujitenga na ukristo kwa kasi, hiyo ni dalili kuwa neema inaondoka kwa mataifa, inakimbilia Israeli..Itafika wakati mataifa yote yataenda kinyume na taifa teule la Mungu hata hili taifa letu vilevile litaungana na yule mpinga-Kristo ili kuiangamiza Israeli.

Zekaria 12: 3 “Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake”.

Ndugu wakati huo sio wa kuutamani kwanini tusubirie mpaka hayo yote yatukute kwa ghafla wakati tunayo nafasi sasa? Neema inamalizikia AFRIKA, usiiche ikupite, chukua hatua ya kumwamini Yesu ayasafishe maisha yako, ili uwe tayari kwa unyakuo ulio karibuni kutokea.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

“WOKOVU WETU U KARIBU NASI KULIKO TULIPOANZA KUAMINI”

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani

Print this post

Neema ya Bwana.

[print_responsive_video_grid]

Print this post

WATAMTAZAMA YEYE AMBAYE WALIMCHOMA;

Jina Bwana wetu Yesu libarikiwe. Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema kuiona hivyo nakukaribisha ndugu popote pale ulipo tushiriki pamoja Baraka Bwana alizotuandalia leo.

Tukisoma Zekaria 12:9-14, inasema. 

“ 9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu. 

10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.

12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;

13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.

14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao”.

Watu wanaozungumziwa hapo ni wayahudi (yaani Waisraeli) , Embu leo jiulize tu Israeli ni Taifa dogo sana kama mkoa wa njombe, ni taifa ambalo huwezi hata ukaenda na kukutana na vitu vya kuvutia huko au vya kushangaza kama mataifa mengine makubwa, lakini ni kwanini leo hii imekuwa ni JICHO LA DUNIA?. Wapo mbali na Mungu lakini ni watu wenye akili na wenye mafanikio makubwa duniani, jiulize siku wakiwa karibu na Mungu itakuwaje?

Hayo maandiko hapo juu ni lazima yatime, utafika wakati biblia inasema Roho ya neema itaachiliwa juu yao na watamwamini huyu Yesu ambaye sasa hawamwamini, Siku hiyo Watalia na kuomboleza baada ya kugundua makosa yao kuwa Yule waliyemsulibisha na KUMCHOMA MKUKI miaka 2000 iliyopita kumbe ndiye Masiya waliokuwa wanamsubiria kwa miaka mingi..Ile roho ya ufarisayo na usadukayo itaondoka juu yao.

Kama vile biblia inavyotabiri kutakuwa na maombolezo makubwa sana huko Yerusalemu wakitubu makosa yao.

Sasa hicho ndio kile kipindi ambacho mtume Paulo alikiandika katika

Warumi 11:25 “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili [anasema na sisi watu wa mataifa]; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26 Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake.

27 Na hili ndilo agano langu nao, Nitakapowaondolea dhambi zao”.

Unaona hapo unabii huo utatimia katika hiyo siku?, Huo wakati wa Israeli kurudiwa na kutengwa na maovu yao upo karibuni sana, na utakapoanza tu basi ujue utimilifu wetu sisi mataifa utakuwa umeshawasili yaani kwa lugha nyingine neema kwetu itakuwa imeshaondoka na kurudi tena Israeli, na hiyo itaambatana na tendo KUU la UNYAKUO.

Sasa wayahudi ambao leo hii utawaona wanalia usiku na mchana pale kwenye ule Ukuta wa maombolezo (wailing wall). wakimwomba Mungu wa Ibrahimu baba yao aje kuwaokoa na maadui zao na kuleta utawala wa masihi duniani, ipo siku hayo maombolezo yatakoma, na ndipo Mungu atawarudia kwa kuwafumbua macho na kumwona YESU, Kumbuka Mungu aliwapofusha kwa makusudi kabisa wasimwamini Kristo ili sisi mataifa tuipate neema vinginevyo huyu Yesu wa thamani ambaye leo hii tunaifurahia neema yake, tungemsikilizia tu kwa wayahudi, sisi tungeendelea kuwa waabudu miti,vinyago, na wachawi. Na hata hivyo dunia ungekuta imeshakwisha siku nyingi, wakati ule ule tu Yesu aliokuwa ndio ungepaswa uwe ni wakati wa wao kurejeshewa ufalme wa dunia na Yesu.

Unakumbuka mitume walimuuliza Yesu baada ya kufufuka je! Huu ndio wakati wa kuwarudishia Israeli ufalme? Yesu akawaambia, sio kazi yenu kujua nyakati wala majira.(Matendo 1:6), Hii ikiwa na maana kuna wakati utafika watarudishiwa na huyu huyu masihi Yesu Kristo.

Hivyo huo wakati unafika, Pale Mungu atakaposimama tena upande wa Israeli na kuwashindania kwa nguvu nyingi kama alivyokuwa anafanya zamani, pale mataifa yote ulimwenguni yatakapoungana ili yaje kujaribu kuisambaratisha Israeli katika ile vita ya Harmagedoni ndipo hapo Kristo atakawapigania toka juu kwa nguvu na uweza mwingi…damu nyingi itamwagika sana, maadui wote wa Israeli watakufa kama kuku waliochinjwa wakaachwa, wakati huo Bwana atakapolipigania Taifa lake…. Tunalisoma hilo katika..

Zekaria 14:1 “Tazama, siku moja ya Bwana inakuja, ambayo mateka yatagawanyika kati yako.

2 Kwa maana nitawakusanya mataifa yote walete vita juu ya Yerusalemu; na huo mji utapigwa, nazo nyumba zitatekwa, nao wanawake watatendwa jeuri; na nusu ya watu wa mji watatoka kwenda utumwani; ila mabaki ya watu wa mji hawatakatiliwa mbali.

3 Hapo ndipo ATAKAPOTOKEA BWANA, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita.

4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.

5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu; kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku zaUzia, mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye.

Kwahiyo tusifurahie tu kuona leo hii Israeli inazidi kufanikiwa lakini badala yake tuogope na tujiulize maswali je! Wewe tumejiandaaje sasa?, neema ndio hivyo inaondoka kwetu, tazama hata hali ya ukristo sasa hivi duniani sio kama ile ya zamani, tazama mataifa ya ulaya ambayo ndio yalikuwa ya kwanza kutuleta injili lakini sasa jinsi yanavyozidi kujitenga na ukristo kwa kasi, hiyo ni dalili kuwa neema inaondoka kwa mataifa, inakimbilia Israeli..Itafika wakati mataifa yote yataenda kinyume na taifa teule la Mungu hata hili taifa letu vilevile litaungana na yule mpinga-Kristo ili kuiangamiza Israeli.

Zekaria 12: 3 “Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake”.

Ndugu wakati huo sio wa kuutamani kwanini tusubirie mpaka hayo yote yatukute kwa ghafla wakati tunayo nafasi sasa? Neema inamalizikia AFRIKA, usiiche ikupite, chukua hatua ya kumwamini Yesu ayasafishe maisha yako, ili uwe tayari kwa unyakuo ulio karibuni kutokea.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Print this post

MAANDALIZI YA UJENZI WA HEKALU LA TATU YAPO TAYARI.

Jicho la Mungu kidogo kidogo linaanza kuondoka kwa mataifa na kurejea Israeli. Wakati wowote Hekalu la tatu nitaanza kujengwa pale Yerusalemu kwani maandalizi yote yapo tayari.Kilichobaki ni amri tu kutolewa, Na kumbuka ujenzi wa sasa hivi sio kama ule wa zamani, haitachukua tena miaka 7 au 20 kukamilika, itakuwa ni kitendo cha wiki kadhaa tu, au miezi kadhaa tu, kila kitu kitakuwa kimeshakamilika. Na tunafahamu likishakamilika tu, Mungu ataliweka JINA LAKE HAPO kama alivyomwahidia mtumishi wake Daudi na Sulemani zamani (1Wafalme 9:3), na mahali popote jina la Mungu lilipo basi WIVU wake utakuwepo pia.

Na biblia inatuambia mpinga-kristo akishaliona hilo ataondoka moja kwa moja na kwenda kutaka kuketi pale kama Mungu kupatia unajisi ili Mungu atiwe wivu alete uharibifu duniani kote ndio maana kimaandiko huyu mpinga-kristo anajulikana kama (CHUKIZO LA UHARIBIFU), Yeye ndio atakayeleta dhiki kuu, wakati huo unyakuo wa kanisa utakuwa umeshapita.

2Wathesalonike 2:3 “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;

4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.

5 Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

Unadhani muda tuliobakiwa nao sasa ni mwingi?.Uzuri ni kwamba hatuna haja ya kuelezeana kila kitu kwani mambo yote yapo wazi kwenye TV na Internet siku hizo zitakapofika.. Huu ni wakati wa kujifunga mkanda UNYAKUO upo mbioni.

Maran Atha.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UFUNUO: Mlango wa 11

UNYAKUO. 

CHUKIZO LA UHARIBIFU NI NINI?

MPINGA-KRISTO AU YULE MWANA WA KUASI NI NANI?


Rudi Nyumbani

Print this post

NGUVU YA UPOTEVU.

Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO litukuzwe mpendwa, karibu tujifunze habari za uzima.

Wapo wengi wanaojifariji kuwa baada ya unyakuo watakuwa na nafasi ya pili. Ndugu Kama hutataka kuitii nguvu ya Roho Mtakatifu itokayo kwa Mungu inayokushawishi leo hii umgeukie Mungu, basi fahamu kuwa hutakuwa na tumaini lolote huko mbele baada ya unyakuo biblia imeweka wazi kabisa kuna NGUVU nyingine itakayoachiwa kutoka kwa Mungu juu ya watu waliosalia kuwafanya wauamini uongo wa mpinga-kristo. Nguvu hiyo biblia inaiita nguvu ya upotevu.

Jiulize ni kitu gani kitakachomfanya mpinga-Kristo apate nguvu dunia nzima kwa muda mfupi sana kama huo, Unadhani ni jambo rahisi tu mtu mmoja atokee ateke dunia nzima, halafu ishikamane naye? Ni wazi kuwa kuna nguvu nyingine itaachiliwa hapo ndani ya mioyo ya watu wamwamini yeye, wazikubali sera zake na ustaarabu wake, na mfumo wake bandia, na ishara zake na ajabu zake za uongo.

Ndugu ukiwepo wakati huo hakuna namna utaweza kumchukia, utaungana naye tu, hatakuwa mtu mkatili kama wewe unavyomfikiria, kwamba atakuwa anaua watu ovyo ovyo tu barabarani, hilo halitawezekana ufalme wake utasimamaje sasa, sharti mataifa yamkubali , apendwe na watu wote na serikali zote na majeshi yote duniani..yafanye kazi pamoja na yeye, ili baadaye apate nafasi ya kuwaangamiza wayahudi na baadhi ya watu wachache watakoanekana huku kwenda kinyume na ustaarabu wake mpya.

Ikiwa leo hii bado hauuoni etendaji kazi wake, unatazamia vipi siku ile umtambue, kwasababu biblia inasema tangu kipindi cha mitume SIRI ya kuasi inatenda kazi, bado tu mwasisi wa hiyo ASI kufunuliwa tu, ambaye ndio mpinga-kristo mwenyewe.na hilo sio jambo kubwa kutokea, kama mipango yake yote imeshakita mizizi kinachongojewa ni nini kama sio kufunuliwa.

2Wathesalonike2:3 “Mtu awaye yote asiwadanganye kwa njia yo yote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu;

4 yule mpingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa; hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu.

5 Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 MAANA ILE SIRI YA KUASI HIVI SASA INATENDA KAZI; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutendakwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;

10 na katika madanganyo yote yaudhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;

12 ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.

Unaona hapo? Sasa Mpinga-Kristo huyu atatokea katika utawala wa RUMI biblia imelithibitisha hilo, ndani ya dini yenye wafuasi wengi leo hii duniani, na kiongozi wake anapata sifa na kukubalika sasa na dini zote duniani na mataifa yote, Na katika kiti hicho anachokalia huko VATICAN ndicho hicho hicho mpinga-kristo atakaponyanyukia..

Ndugu, ulimwengu huu upo ukingoni sana, bado unayachezea maisha yako mpaka siku nguvu ya upotevu itokayo kwa Mungu ikuingie, ili uamini uongo uende kuzimu?. Ni jambo la kuogopesha sana. Geuza NIA yao mtazame YESU, UNYAKUO wa kanisa upo karibu.

Mungu akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana:

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

SIRI YA MUNGU.

ALAMA KATIKA VIPAJI VYA NYUSO.


Rudi Nyumbani

Print this post

UFUNUO: Mlango wa 16.

Jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe…Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Ufunuo, ambapo leo tutaitazama ile sura ya 16, ya kitabu hichi, Ni vizuri kama hujapita sura za nyuma ungeanza kwanza kuzipita hizo ili uweke msingi mzuri wa kuzielewa sura zinazofuata.

Katika sura hii ya 16, habari kuu tunayoina ni juu ya vitasa 7, “Vitasa ni VIBAKULI kwa lugha ya sasa”..Na hasira ya Mungu sehemu nyingine imefananishwa na mfano wa kimiminika fulani kinachojaa katika chombo, ambacho kwa jinsi hasira ya Mungu inavyozidi kuongezeka juu ya mtu au watu ndivyo kimiminika kile kinavyozidi kujaa ndani ya hicho kikombe au kibakuli…Na kikiisha kujaa kukaribia kumiminika, ndipo mtu au watu wanapewa wakinywe..na kunywa kunaashiria “kuipokea ghadhabu ya hasira ya Mungu (yaani kuadhibiwa)”.

Ndio maana ukisoma kwenye biblia wakati wana wa Israeli walipomkosa Mungu hata Mungu akadhamiria kuwapeleka Babeli, Nabii Yeremia alipewa maono ya kuwanywesha wana wa Yuda kikombe cha ghadhabu ya Mungu…Na wakati ulipofika wa Neno hilo kutimia Mfalme wa Babeli alishuka juu yao akawachinja chinja  wanawake na watoto,  na wale waliosalia akawachukua mpaka Babeli utumwani..Na utaona kikombe hicho cha ghadhabu ya Mungu hawakunywesha tu wana wa Yuda bali mataifa mengi duniani pia walinyweshwa.

Yeremia 25: 15 “Maana Bwana, Mungu wa Israeli, aniambia hivi, Pokea kikombe cha divai ya ghadhabu hii mkononi mwangu, ukawanyweshe mataifa yote, ambao nitakupeleka kwao;

16 nao watakunywa, na kulewalewa, na kufanya wazimu, kwa sababu ya upanga nitakaoupeleka kati yao.

17 Ndipo nikakipokea kikombe kile mkononi mwa Bwana, nikawanywesha mataifa yote, ambao Bwana alinipeleka kwao;

18 yaani, Yerusalemu, na miji ya Yuda, na wafalme wake, na wakuu wake, ili kuwafanya kuwa ukiwa, na ajabu, na mazomeo, na laana; vile vile kama ilivyo leo;

19 Farao, mfalme wa Misri, na watumishi wake na wakuu wake na watu wake wote;

20 na watu wote waliochanganyika pamoja, na wafalme wote wa nchi ya Uzi, na wafalme wote wa nchi ya Wafilisti, na Ashkeloni, na Gaza, na Ekroni, na mabaki ya Ashdodi;

21 Edomu, na Moabu, na wana wa Amoni;

22 na wafalme wote wa Tiro, na wafalme wote wa Sidoni, na wafalme wote wa kisiwa kilicho ng’ambo ya pili ya bahari; 23 Dedani, na Tema, na Buzi, na watu wote wakatao denge;”

Na pia tutakuja kumwona jinsi Yule mwanamke(Babeli mkuu,Mama wa makahaba) akipewa kikombe hiki cha ghadhabu ya Mungu katika ufu. 16:19.

Lakini katika sura hii, tunaona Malaika saba wakiwa na VIBAKULI saba. Hivi sasa ni vibakuli vya ghadhabu ya Mungu juu ya dunia nzima sio tena juu ya mataifa Fulani baadhi au watu Fulani wachache, ghadhabu ya Mungu juu ya watu wachache haihitaji kibakuli, kikombe tu kingeweza kutosha..lakni hapa ni maovu ya dunia nzima..Maovu ya wanadamu ndio yamevijaza vibakuli hivyo..Kimoja baada ya kingine kimejaa..Bwana hakukiweka kimoja kwa sababu yeye ni wa rehema bali aliviweka saba ingekuwa ni kimoja tayari siku nyingi sana tungeshaangamizwa kwasababu kingekuwa kimeshajaa..lakini wanadamu wamevijaza vyote saba…Na hivyo vitakwenda kumiminwa juu ya dunia nzima, kumbuka hawatanyweshwa watu bali watamiminiwa..hiyo ni hatari sana.

Lakini kabla ya kuviangalia hivi vitasa kuna vitu vichache vya utangulizi vya kufahamu..

Hii neema tulionayo leo itafika mwisho, kuna baadhi ya misemo imekuwa ikisemwa kuwa Mungu wa agano la kale leo hii hayupo, kama yupo zile ishara alizokuwa anatenda agano la kale ziko wapi leo?. Lakini SIKU YA BWANA inakuja ndugu usitamani uwepo! USITAMANI UWEPO! ni mambo ya kuogopesha ambayo usingetamani hata adui yako yampate, Mungu kuzuia ghadhabu yake ni kwa ajili yetu sisi ili tutubu lakini tusipotubu hukumu itatukuta wakati tusioutazamia.

Kuna vitu vitatu vya kutisha ambavyo vipo mbele yetu sasa, 

1) DHIKI KUU, 

2) SIKU YA BWANA, 

3) ZIWA LA MOTO.   

Leo tutaitazama hii SIKU YA BWANA ni ipi, itakuja lini na itakuwa inamuhusu nani.

Kwa ufupi ndugu, DHIKI KUU itakuja na tunafahamu itakuwa kwa wakristo watakaokataa kuipokea ile alama/chapa ya mnyama. Hii itamuhusu mpinga-kristo akiwatesa wakristo wale waliokataa kuipokea ile chapa ya mnyama, Ambapo mwishoni mpinga-kristo atafanikiwa kuwaua kikatili wote wasioipokea chapa. Na hii dhiki itadumu kwa muda wa miaka mitatu na nusu, ni wakati wa kutisha sana unakuja mbeleni. Kwahiyo wakati wakristo wachache wanapitia dhiki kuu, wengine wote waliosalia watakuwa wanaendelea kujifurahisha na mambo yao ya dunia wakimfurahia mpinga kristo na utawala wake.

Sasa SIKU YA BWANA itaanza mara tu baada ya DHIKI KUU kuisha ambapo watakatifu wote wakati huo watakuwa wameshaondoka,(wameuliwa na mpingakristo) na unyakuo utakuwa umeshapita wakati huo, lakini hao waliobakia walioipokea chapa ya mnyama itawapasa waingie kwenye adhabu kali sana ya Mungu mwenyewe, Kwasababu wameshirikiana na mpinga kristo kuwaua watu wa Mungu na kwasababu wamekataa kumcha Mungu na kuzishika amri zake, ndugu Hii SIKU YA BWANA usitamani uwepo. Kumbuka haitakuwa jehanamu ya moto, bali itakuwa ni adhabu ya hapa hapa duniani.

maandiko yanasema:

Amosi 5:18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani SIKU YA BWANA; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma.

20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga.

Pia tukisoma…

Isaya 13:6″ Pigeni kelele za hofu; maana SIKU YA BWANA i karibu; itanyesha kama maangamizi yatokayo kwa Mwenyezi Mungu.

7 Kwa sababu hiyo mikono yote italegea, na moyo wa kila mtu utayeyuka.

8 Nao watafadhaika; watashikwa na utungu na maumivu; watakuwa na utungu kama mwanamke aliye karibu na kuzaa; watakodoleana macho; nyuso zao zitakuwa ni nyuso za moto.

9 Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahariyao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri.”

Maandiko yanaposema SIKU YA BWANA hayamanishi ni siku kama siku moja, bali inamaanisha ni kipindi fulani cha WAKATI ambacho Bwana amekitenga kwa kusudi fulani. Kama maandiko yanavyotueleza ni kipindi ambacho kimetengwa cha GHADHABU NA HASIRA ya Mungu kulipiza kisasi kwa wanadamu wote wasiomcha Mungu. Kipindi Hichi cha SIKU YA BWANA kitadumu kwa muda wa siku 75, Hizi zimepatikana kutoka katika kitabu cha Nabii Danieli 12:12, ambapo tunaona kipindi cha ile dhiki kuu kitadumu kwa muda wa siku 1260(sawa na miaka 3 na nusu), na hapo zimeongezeka siku nyingine kutoka siku 1260 mpaka kufikia siku 1335, kwahiyo ukichukua hizo siku 1335-1260=75. Kwahiyo hizi siku 75 zilizoongezwa ni mahususi kwa ajili ya BWANA kujilipizia kisasi kwa wanadamu wote waliosalia juu ya uso wa nchi.

Kabla ya SIKU hiyo ya BWANA kuanza Kutakuwa na baragumu saba zitakazopigwa kuitangulia , Hizi Zitabeba hukumu kwa watu wote, kama onyo watu watubu kumgeukia Mungu, Dunia itapigwa kwa mapigo mengi ya ajabu ukisoma Ufunuo 8 ikiwemo, theluthi moja ya maji kuwa damu, theluthi ya maji duniani kutiwa uchungu,theluthi ya mwezi na jua na nyota kupigwa,hebu tafakari kutakuwaje duniani wakati huo mchana kutakuwa kama jioni, giza litakuwa nene usiku na baridi kali sana, nzige wa ajabu watapandishwa kutoka kuzimu, maumivu yao ni kama ya kung’wata na nge, na meno yao ni kama meno ya simba, n.k. Biblia inasema watu watakitamani kifo lakini hawatakiona, kumbuka hapo bado SIKU YA BWANA haijaanza huo ni mwanzo wa utungu tu, unatangaza hukumu KUU ya Bwana inayokuja mbeleni kwa urefu soma ufunuo sura ya 8 na ya 9. inaelezea haya mapigo ya baragumu saba za Mungu.

Lakini pamoja na mapigo yote hayo ya baragumu biblia inasema watu watakaokuwa juu ya uso wa nchi hawatatubu maovu yao kwasababu roho ya uovu imeshakaa juu yao kwa kuwa wote wamekwisha ipokea ile chapa ya mnyama neema ya Mungu imeondoka juu yao hawawezi kutubu tena.

Kwahiyo mara baada ya dhiki kuu kuisha wakristo kuuliwa na unyakuo kupita, Sasa Hawa wanadamu waliobaki ndio watakaoingia katika SIKU YA BWANA inayotisha, ile inayowaka kama moto yenye vile vitasa saba ambayo ndiyo yale mapigo saba ya mwisho ya Mungu, katika hayo ghadhabu ya Mungu imetimia : Hebu tutazame vitasa hivi kimoja baada ya kingine.

KITASA CHA KWANZA:

Ufunuo 16:1 ” Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi.

2 Akaenda huyo wa kwanza, akakimimina kitasa chake juu ya nchi; pakawa na JIPU BAYA, BOVU, juu ya wale watu wenye chapa ya huyo mnyama, na wale wenye kuisujudia sanamu yake.”

Sasa adhabu hizi zitakuwa ni kwa Dunia nzima na sio theluthi tena ya dunia kama ilivyokuwa kwa zile baragumu saba. Majipu haya tunaona ni mfano wa yale yale waliopigwa wamisri, Kutakuwa na majipu ya ajabu usidhani ni haya ya kuwaida uliyoyazoea, biblia imeyaita ni MAJIPU MABOVU bado hajatokea kabisa duniani, huo ugonjwa bado haujazuka, Tuna magonjwa mengi ya hatari duniani lakini biblia haijayataja yote hayo, lakini ni huu ugonjwa wa MAJIPU tena jipu bovu ndio umetabiriwa utakuja, homa yake itakuwa sio kama hizi za kawaida tulizozizoea, na utakuwa na vidonda vikubwa sana, utampata kila mtu aliyekaa juu ya nchi, pamoja na wanyama Ndugu usitamani kuwepo huko wewe unayesema Mungu wa agano la kale haishi, siku hiyo utayaona haya wazi wazi.

KITASA CHA PILI:

Ufunuo 16:3 “Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.”

Duniani kutakuwa na harufu kama ya damu ya mtu aliyekwisha kufa, damu ya mtu aliyekufa ni tofauti na ya aliye hai, damu ya mtu aliyekufa inakuwa kama mgando Fulani mweusi hivi…ndivyo bahari itakavyokuwa.. hakutakuwa na kiumbe chochote baharini chakula kitapungua duniani, maji yataisha, shughuli za usafirishaji baharini vitakwama, mvua zitaacha kunyesha duniani kutakuwa sio sehemu ya kuishi tena mwanadamu, taabu itaongezeka duniani, hofu kuu itawaingia watu wakitazama ni mambo gani haya yameipata dunia?..nini kinaendelea?.. lakini bado mapigo yatakuwa yanaendelea,

KITASA CHA TATU:

Ufunuo 16:4 ” Na huyo wa tatu akakimimina kitasa chake juu ya mito na chemchemi za maji; zikawa damu.

5 Nami nikamsikia malaika wa maji akisema, Wewe u mwenye haki, uliyeko na uliyekuwako, Mtakatifu, kwa kuwa umehukumu hivi;

6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu na ya manabii, nawe umewapa damu wainywe; nao wamestahili.

7 Nikaisikia hiyo madhabahu ikisema, Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, ni za kweli, na za haki, hukumu zako”. 

Baada ya bahari kugeuzwa kuwa damu ya mizoga, watu wote tunajua wangekimbilia kutafuta maji katika mito na kwenye chemchemi za maji, kutokana na kiu kali, lakini Bwana atayapiga pia maji ya mitoni na kwenye chemchemi, wakati huo fedha itakuwa haifanyi kazi tena, Mtu tajiri atakuwa ni mwenye kikombe cha maji safi mkononi mwake na sio fedha, Kwahiyo Bwana atawalazimisha kuyanywa hayo maji ya DAMU kwasababu walishirikiana na yule mnyama kumwaga damu ya watakatifu wa Mungu, hivyo nao Bwana amewapa wainywe. Na kwasababu ya kiu kali watakunywa hiyo damu, na wanadamu wengi wataangamia na kufa kwa pigo hilo.

KITASA CHA NNE:

Ufunuo 16:8 “Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.

9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.”

Baada ya pigo la maji kuwa damu, jua litashushwa chini, maunguzo yatakuwa ni makubwa sana, joto litaongezeka duniani kwa nyuzi joto kubwa kuliko kiwango cha kawaida. Mimea yote itakauka ghafla, dunia itafanana na jangwa ndani ya muda mfupi sana, jaribu kutafakari majipu ya ajabu yanawapata watu wakati huo huo maji yote damu..na bado jua kali linapiga na hakuna maji hata kidogo ya kujipooza,ni dhiki kiasi gani? ni mambo ambayo huwezi dhania yatatokea lakini yapo mbioni kutokea. Lakini pamoja na hayo mapigo yote biblia inasema watu watamtukana Mungu hawatatubu…watalia kwa uchungu wa maumivu hayo watasema kama Mungu yupo kwanini anatufanyia hivi…na kwasababu hawataona majibu yoyote wakati wanateseka watakasirika na kuishia kumtukana Mungu.. Mfano tu wa kizazi chetu hichi watu wanapopatwa na majanga badala wageuke na kumuuliza Mungu ni kwanini na kutubu, wao wanalaani na kutoa maneno ya makufuru.

KITASA CHA TANO:

Ufunuo 16:10 “Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,

11 wakamtukana Mungu wa mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala hawakuyatubia matendo yao. “

Sasa pigo hili linamuhusu sana sana yule mnyama aliyewakosesha wanadamu wote kuipokea ile chapa, mahali kiti chake cha enzi kilipo ambapo ni VATICAN, Roma, Mungu ataachilia laana kwa mataifa ya ulaya ambayo ndio zile pembe kumi, zitamchukia na kumwangamiza yule mwanamke kahaba (Kanisa Katoliki) ambalo makao yake makuu ni VATICAN. Hii ni kutokana na kwamba yale mataifa ambayo yalimtumaini mpinga kristo ayaletee amani duniani, hayajaletewa zaidi ya yote mpingakristo (PAPA) ameiongezea dunia matatizo hivyo basi watamchukia na kumwangamiza, tangu wakati huo utawala wa Roma, pamoja na mpinga kristo (PAPA) na Vatican yake hawatakuwepo tena ufalme wao umekwishatiwa giza. Wakati huo bado wataona bahari ipo vile vile damu, hakuna maji wala umande, jua limegeuka kuwa moto, na majipu yanazidi kuwaharibu…wataona hakuna sababu ya kuwepo na kiongozi mwongo kama asiyekuwa na msaada na mwongo.. hivyo wakiwa katikati ya huo msiba mkubwa ulioikumba dunia watamgeuka Papa na kumwangamiza.

Soma ufunuo 17:16” Na zile pembe kumi ulizoziona, na huyo mnyama, hao watamchukia yule kahaba, nao watamfanya kuwa mkiwa na uchi, watamla nyama yake, watamteketeza kabisa kwa moto. ”

KITASA CHA SITA:

Ufunuo 16:12 “Na huyo wa sita akakimimina kitasa chake juu ya mto ule mkubwa Frati; maji yake yakakauka, ili njia itengenezwe kwa wafalme watokao katika maawio ya jua.

13 Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.

14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.

15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)

16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni.”

Kitasa hichi kunazungumzia ile vita kuu ya HAR MAGEDONI ambayo itakuwa ni vita kati ya Mungu mwenyezi akilipigania taifa la Izraeli dhidi ya wafalme wote wa dunia. karibu kila taifa litaunga mkono vita hii wakiongozwa na mataifa kutoka mawio ya jua. Haya mataifa ya mawio ya jua ni mataifa ya mashariki, nayo ni CHINA,JAPAN, KOREA na machaache baadhi. Wakati huo Vatican itakuwa haipo, Marekani itakuwa haipo, Urusi itakuwa haipo yatatoweshwa katika vita vilivyoelezwa katika Ezekieli 38 & 39, Kwahiyo zile roho chafu ambazo zilikuwa zinaendesha Vatican na Marekani zitahamia kwenye haya mataifa ya mashariki yaliyosalia kwa ajili ya vita dhidi ya Izraeli. Wakati huo ndio Bwana YESU atakapotokea kuwapigania watu wake Izraeli. Ndugu wakati huo dunia itakuwa mfano wa sayari ya Zebaki, hakutakuwa na maji, chakula, magonjwa, joto litakuwa juu sana,maji yote damu, machafuko pamoja na vita, itakuwa ni vilio na kusaga meno, siku hiyo watu watatamani siku hizi za neema tulizonazo leo hawataziona.

KITASA CHA SABA:

Ufunuo 16:17 ” Na huyo wa saba akakimimina kitasa chake juu ya anga. Sauti kuu ikatoka katika hekalu, katika kile kiti cha enzi, ikisema, Imekwisha kuwa.

18 Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.

19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno.”

Hili ni pigo la mwisho, na katika hili ghadhabu ya Mungu imetimia tukisoma pale muhuri wa sita ulipofunguliwa ulitoa picha halisi jinsi hii siku itakavyokuwa soma Mathayo 24:30-31 na pia Ufunuo 6:12-17

Ufunuo 6:12-17 ” Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu, 

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi. 

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake. 

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo. 

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?”

Pigo la saba la mwisho kama tunavyosoma ni baya kuliko yote yaliyotangulia maana jua linaondolewa, mwezi utakuwa damu, nyota zitatoweka, unaweza kuona kutakuwa na giza kiasi gani duniani, na baridi kiasi gani (wakati huu sasa jua litakuwa limeondolewa),kutakuwaa ni giza zito sana, hakutakuwa na chanzo chochote cha umeme, wala nishati…shughuli zote za kimaendeleo zilishamalizwa katika mapigo yaliyotanguliwa, hadi kufikia hapa watu wachache sana watakuwa wamesalia duniani, kumbuka hapo bado ziwa la moto linasubiri watu, Hichi ni kisasi tu cha hapa hapa duniani.

Mvua ya mawe kubwa sana itanyesha, mawe kama talanta,(Talanta 1 ni kama kg 34), Huwezi kujificha kwenye nyumba yako ya bati au ya kigae, kg 34 ni uzani mkubwa sana ambayo yatashuka kwa kasi kubwa sana kutoka juu…itaambana na tetemeko ambalo halijawahi kutokea, kiasi cha kwamba visiwa vitahama, kisiwa cha zanzibar kitapotea siku hizo, Milima itatapika volkano, kumbuka hayo yote yatafanyika katikati ya giza nene, hakuna mawasiliano, kutakuwa hakuna kuonana wala kupigiana simu.. hapo hakuna mfalme wala mtumwa, raisi wala mwananchi wote waliosalia watatamani wafe kuliko kuishi, watatamani milima iwaangukie waikwepe ghadhabu ya Mungu, Hapo ndipo itakapoonekana ishara ya mwana wa Adamu mawinguni.

Soma Mathayo 24:29 “Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika; 

30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi. “

Rafiki haya mambo ni kweli yatatokea, ndivyo yatakavyokuja kuupata ulimwengu na dalili zote zinaonyesha kuwa yatatokea katika kizazi chetu tunachoishi mimi na wewe, Bwana amekwisha kutuonya mbele, Nia yake ni sisi tuiepuke hiyo ghadhabu na ndio maana kuna mahali alisema alipokuwa katikati ya kitasa cha sita (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake). Kwahiyo ametuonya tukeshe na kuyatunza mavazi yetu, maana hii siku ya ghadhabu itakuja ghafla.

Ndugu kimbia injili ambazo zinakufanya usifikiri hatma ya maisha yako ya milele badala yake inakupeleka kutazama mambo ya ulimwengu huu tu!. Hii ni roho ya shetani inayowapumbaza wengi wafikiri mambo hayo yatakuja kutokea baada ya miaka 2,000 mbele, usidanganyike ni uongo wa shetani, ndugu dalili zote zinaonyesha, unabii wote umetimia kwamba tunaishi katika kizazi cha hatari sana. Chunguza maisha yako na maandiko angali neema ipo, mambo hayatakuwa hivi siku zote, pale mlango wa neema utakapofungwa kutakuwa hakuna kurudi nyuma itakuwa ni vilio na maombolezo, kimbilia kalvari sasa tubu dhambi zako, uoshwe kwa damu ya Yesu, na Upokee Roho Mtakatifu kabla ya huo wakati kufika. Kumbuka adhabu ya hii SIKU YA BWANA, sio jehanamu ya moto, baada ya mapigo hayo ndipo ziwa la moto ziwa la moto litafuata, wote waliokufa katika hii siku ya Bwana ambao ndio wale wote walioipokea chapa ya mnyama…baada ya ule utawala wa miaka 1000 watafufuliwa na kuhukumiwa katika kiti cheupe cha hukumu na kisha watatupwa katika lile ziwa la moto.

Ikiwa unataka kumpa Bwana Yesu maisha yako na kugeuka leo tubu mwenyewe moyoni mwako au fuatiliza sala hii kwa imani:


⏩ SEMA: “Bwana Yesu, Leo hii nasogea mbele zako nikiwa mwenye dhambi, natubu makosa yangu yote niliyokukosea, naomba unisamehe, nimeamua kugeuka leo, nisaidie Bwana Yesu, neema yako iwe juu yangu, nikuishie wewe, siku zote za maisha yangu, asante Bwana Yesu kwa kunisikia na kunisamehe. AMEN! “.

Baada ya kutubu na kudhamiria kutokufanya tena dhambi unahitaji kubatizwa, Hivyo basi tafuta kanisa linalobatiza ubatizo sahihi nao ni kwa kuzamishwa kwenye maji mengi na ni kwa jina la YESU KRISTO, Kwa kufanya hivyo Bwana atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu na utakuwa umekamilisha wokovu wako.

MUNGU AKUBARIKI.

Kwa Mwendelezo >> UFUNUO: Mlango wa 17

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara,  kwa njia ya whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255789001312. Na kama utapenda kwa njia ya E-mail basi tuandikie email yako katika boksi la maoni chini.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Zinazoendana..


DANIELI: Mlango wa 12.

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

SIKU YA HASIRA YA BWANA.


Rudi Nyumbani

Print this post