Kabla ya Bwana wetu YESU KRISTO, Mkuu wa Uzima, Mfalme mwenye Nguvu, Mwamba Mgumu, na Mkombozi, na Mfalme wa wafalme, kuutoa uhai wake, ili baadaye aurudishe tena (Yohana 10:17), yapo maneno saba (7) aliyasema pale msalabani, ambayo tunayapata katika zote nne (yaani Mathayo, Marko, Luka na Yohana), na maneno hayo ni kama yafuatayo.
1. BABA UWASAMEHE, KWA KUWA HAWAJUI WATENDALO.
Luka 13:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura”.
Hili ndilo Neno la Kwanza Bwana YESU kulisema akiwa pale msalabani, kuonyesha upendo wa hali ya juu na huruma kwetu, ijapokuwa yeye tayari alishawasamehe, lakini alijua pia umuhimu wa kuwaombea msamaha kwa Baba, kwani si kila msamaha unaoweza kutoa wewe ukawa pia umetolewa na MUNGU, waweza kumsamehe mtu lakini Baba wa mbinguni akawa hajamsamehe huyo mtu bado, hivyo tunajifunza hata sisi kuwaombea wengine msamaha kwa Baba yetu wa mbinguni, kama alivyofanya Bwana wetu YESU KRISTO.
2. AMIN, NAKUAMBIA LEO UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI.
Luka 13:42 “Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.
Hili ni neno la Pili Bwana kuzungumza msalabani, kuonyesha huruma za Bwana YESU hata katika hatua za mwisho kabisa za maisha ya mtu.
3. MAMA TAZAMA MWANAO, NA KISHA AKAMWAMBIA YULE MWANAFUNZI TAZAMA MAMA YAKO.
Yohana 19:26 “Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao.
27 Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake”.
Hili ni neno la tatu, lenye ujumbe wa kuangaliana sisi kwa sisi, kwani kwa kufanya hivyo tunaitimiza amri ya Kristo la upendo.
4. MUNGU WANGU, MUNGU WANGU MBONA UMENIACHA?
Mathayo 27:46 “Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”
Hili ni neno la nne, lenye kuonyesha Uzito wa dhambi Bwana wetu alizozibeba kwaajili yetu, zilikuwa ni nyingi kiasi cha kuuzima uwepo wa MUNGU mbele zake pale msalabani.
5. NAONA KIU.
Yohana 19:28 “Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu”.
Hili ni neno la tano, lenye kuonyesha uzito wa mateso ya Bwana YESU kuwa yalikuwa ni makuu.
6. IMEKWISHA
Yohana 19:30 “Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake”.
Hili ni neno la sita, lenye kutangaza mwisho wa utumwa wa dhambi.. na kuanza kwa majira mapya, hakuna tena mateso, wala kilio wala uchungu kwake YESU, na kwa wote watakaokuwa ndani yake.
7. BABA MIKONONI MWAKO NAIWEKA ROHO YANGU.
Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu”.
Hili ni neno la mwisho, kabla ya kukata roho.
Maneno haya yalifunga kauli ya Bwana duniani na baada ya siku tatu, alitoka kaburini, Mauti ilimwachia, na akaja na ushindi MKUU, Wokovu kwetu, Haleluyaa!…
Je bado upo dhambini?.. bado huoni ni gharama gani aliyoiingia YESU kwaajili yako?.. Tubu leo na kumkaribisha maishani mwako kabla ya nyakati mbaya na hatari zinazoikaribia dunia kufika.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini tarehe ya pasaka inabadilika kila mwaka?
PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?
Nini tofauti kati ya kileo na divai?
Je kibiblia ni sahihi kuadhimisha jumapili ya mitende?
Ipi tofauti kati ya Sheria na kanuni kibiblia.
Swali: Inakuwaje manabii wa uongo wanakuwa na uwezo wa kutoa pepo kwa jina la YESU?, na ilihali hawana mahusiano na Mungu wa kweli? je ni nguvu gani wanazitumia? Za Mungu au shetani?.
Jibu: Zipo aina mbili za manabii wa uongo. Aina ya kwanza ni ile inayotumia nguvu za giza asilimia mia moja (100%), kundi hili halihusishi kabisa jina la YESU katika huduma zake, wala halimhubiri YESU wa kweli bali shetani.
Hawa wanakuwa ni wachawi waliovaa suti na kushika biblia, na Neno la MUNGU linasema tutawatambua kwa matunda yao, na si mwonekano wao wa nje.
Kundi la Pili: la manabii wa Uongo, ni wale ambao sio wachawi lakini halina mahusiano na MUNGU, maana yake aidha wanamtumikia MUNGU kwa faida za matumbo yao, au walishamwacha MUNGU na kufuata akili zao, kundi hili ndio hatari zaidi kwasababu bado linaweza kutumia jina la YESU na miujiza ikatendeka.
Mtu anakuwa kashapoteza mahusiano na MUNGU lakini bado upako anao!.. utauliza hilo linawezekanaje?.. Mkumbuke MUSA!.. Bwana MUNGU alimwambia auambie mwamba utoe maji, lakini yeye pamoja na ndugu yake Haruni, hawakumsikiliza MUNGU wakaenda kufanya kinyume na walivyoagizwa, na jambo la ajabu ni kwamba ijapokuwa walikuwa wameenda kinyume na agizo la MUNGU (wapo nje na mpango wa Mungu) lakini walipouchapa mwamba ulitoa maji, binafsi ningetegemea maji yasitoke mwambani kwasababu walikuwa nje na agizo la MUNGU, lakini haikuwa hivyo.
Hesabu 20:6 “Musa na Haruni wakatoka pale palipokuwa mkutano, wakaenda hata mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka kifudifudi; utukufu wa Bwana ukawatokea.
7 Bwana akasema na Musa, akinena,
8 Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao.
9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za Bwana kama alivyomwamuru.
10 Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu?
11 Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.
12 Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa”.
Umeona hapo?.. ijapokuwa Musa alikuwa anatembea nje ya agizo la MUNGU, lakini bado upako alikuwa nao, na manabii wa uongo ni hivyo hivyo, wanaweza kuwa wanatembea na upako wa MUNGU wa kweli lakini hawana MUNGU maishani mwao, na mwisho wao ni mbaya…na hawa tumeambiwa tutawatambua kwa matunda yao na si upako wao, wala mwonekano wao.
Mfano mwingine ni Yule nabii mzee tunayemsoma katika biblia, aliyemwambia uongo nabii mwenzake, na badala nguvu za MUNGU zimwondoke baada ya kusema kwake uongo, kinyume chake ndio kwanza anapokea unabii mwingine kumhusu mwenzie. Soma habari hiyo katika 1Wafalme 12:11-30.
Ikifunua kuwa unabii, au muujiza au upako mtu/mtumishi alionao sio kipimo cha kwanza cha kumtambua nabii/mtumishi wa Mungu wa kweli, bali ni mtu kuwa na mahusiano mazuri na MUNGU, kwani maandiko yanasema Yohana Mbatizaji hakufanya ishara wala muujiza hata mmoja lakini mbinguni alihesabika kuwa mkuu kuliko manabii wote na watu wote wa agano la kale (Yohana 10:41 na Mathayo 11:11).
Na tena Bwana YESU alisema wengi watakuja siku ile wakisema, hatukutoa pepo na kufanya unabii kwa jina lako?.. na yeye atasema siwajui mtokako! (Mathayo 7:21-22).
Ili kumtambua kuwa huyu ni Nabii wa kweli na si wa uongo, ni matunda anayoyatoa.. Maana yake Matunda ya maisha yake, na matunda ya kazi yake.
Matunda ya maisha yake ni jinsi anavyoishi, je anazaa matunda ya Roho mtakatifu tunayoyasoma katika Wagalatia 5:22?.. au ni mtu wa namna gani?..kama maisha yake si kulingana na Neno la MUNGU bali ni mtenda dhambi, basi huyo hata kama anauwezo wa kusimamisha jua, bado hatupaswi kudanganyika kwake.
Vile vile kama matunda anayoyazaa kutokana na kazi yake (maana yake watu anao wahubiria) hawawi wasafi mwilini na rohoni, hiyo ni ishara nyingine ya kumtambua nabii huyo kuwa si wa MUNGU. Kwani kama watu anaowatengeneza hawana tofauti na wa ulimwengu, maana yake matunda yake si matunda ya kiMungu bali ya adui.
Hiyo ndio namna pekee ya kuwapima manabii au wachungaji au waalimu au mitume wa kweli na wale wa uongo, na tunapowafahamu biblia imetuonya tujihadhari nao.
Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.
18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.
19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.
20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.
21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)
SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.
SADAKA INAHARIBU NGUVU ZA MADHABAHU ZA MASHETANI.
Swali: Je! tunaweza kuthibitisha vipi kuwa Yule malaika aliyekuwa anashuka na kuyatibua maji alikuwa ni malaika wa MUNGU na si wa shetani, kwasababu maandiko yanasema kuwa shetani naye anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa nuru (2Wakorintho 11:14).
JIbu: Turejee..
Yohana 5:1 “Baada ya hayo palikuwa na sikukuu ya Wayahudi; naye Yesu akakwea kwenda Yerusalemu. 2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano.
3 Ndani ya hayo jamii kubwa ya wagonjwa walikuwa wamelala, vipofu, viwete, nao waliopooza, [wakingoja maji yachemke.
4 Kwa maana kuna wakati ambapo MALAIKA HUSHUKA, AKAINGIA KATIKA ILE BIRIKA, AKAYATIBUA MAJI. Basi yeye aliyeingia wa kwanza baada ya maji kutibuliwa, AKAPONA UGONJWA WOTE ULIOKUWA UMEMPATA.]”
Ni kweli Biblia inasema shetani anaweza kujigeuza na kuwa mfano wa Malaika wa Nuru, lakini haisemi kuwa anaweza kujigeuza na kuwa Malaika wa Nuru, bali mfano wa..
Kwahiyo huyu tunayemsoma hapa katika Yohana 5:4 hakuwa malaika wa giza, kwasababu matunda yake si ya giza kwani Maandiko yanasema “shetani hawezi kumtoa shetani mwenzake”.
Mathayo 12:25 “Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.
26 Na SHETANI AKIMTOA SHETANI, AMEFITINIKA JUU YA NAFSI YAKE; basi ufalme wake utasimamaje?”
Sasa wote waliokuwa wamelala pale walikuwa wanasumbuliwa na magonjwa yaliyoletwa na mapepo, kwasababu asilimia kubwa ya magonjwa yanasababishwa na mapepo (soma Mathayo 9:32 na Mathayo 12:22).
Sasa kwa mantiki hiyo haiwezekani malaika wa giza kushuka na kuwatoa malaika wenzake wa giza (yaani mapepo) wenzao ndani ya watu, ni jambo ambalo haliwezekani!, vinginevyo ufalme wa giza usingesimama, kwahiyo Yule malaika alikuwa anashuka kuyatibua maji ni malaika wa Nuru na si wa giza.
Jambo la ziada la kujifunza ni kwamba watu wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji kwaajili ya kutatuliwa shida zao au magonjwa yao na baada ya kupiga ramli wanaona kama wamepona..
Kiuhalisia ni kwamba hawajatatuliwa matatizo yao bali ndio yameongezwa, kwamfano mtu ataenda kwa mganga akiwa na tatizo la homa, na anaaguliwa na kujiona amepona kabisa, na kuambiwa kuwa majini yamefukuzwa ndani yake.
Sasa kiuhalisia kulingana na biblia yale mapepo hayajaondoka!, bali yamehamishwa kutoka sehemu moja ya mwili kwenda nyingine, au kutoka sehemu moja ya maisha kwenda nyingine, lakini si kwamba yamefukuzwa/kuondolewa kabisa kutoka katika maisha yake,
Maana yake sasa huyu mtu atapata unafuu kwenye kifua kilichokuwa kinamshumbua, au kwenye mguu, lakini lile pepo limehamia kwenye tumbo, au miguu, au limepelekwa kusababisha matatizo mengine katika maisha ya Yule mtu, na tena mtu anayeenda kwa mganga anakuwa anaongezewa mapepo mengine kwa ajili ya matatizo mengine yatakayotokea wakati huo huo au wakati mwingine huko mbeleni, kwasababu shetani kamwe hawezi kumtoa shetani mwenzake.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?.
JE BADO UNASUBIRIA MAJI YACHEMKE?
AKAWAPONYA WALE WENYE HAJA YA KUPONYWA
Theofania ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno ya mawili “theos (Mungu)” na “faino (kuonekana)”. Hivyo ukiunganisha linazalika neno “kuonekana kwa Mungu”
Theofania sio kuonekana kwa Mungu katika ule utimilifu wake wote, hapana, kwasababu maandiko yanasema hakuna mtu awezayo kumwona Mungu akaishi (Kutoka 33:20). Hivyo Theofania ni njia mbadala (isiyo ya moja kwa moja) ambayo Mungu aliitumia kujitokeza na kuongea na watu, kuthibitisha agano lake, au kuwapa maagizo.
Mfano wa njia hizo,
> Ni kijiti cha moto, alichotumia kuzungumza na Musa kule jangwani. (Kutoka 3)
> Mtu Yule aliyeshindana na Yakobo mweleka (Mwanzo 32:24-30)
> Melkizedeki (Mwanzo 14: 18-20)
> Yule mtu wanne aliyewatokea Shedraka, Meshaki na Abednego ndani ya moto (Danieli 3)
> Nguzo ya moto na wingu jangwani (Kutoka 13:21-22)
> Mungu kumtokea Samweli (1Samweli 3:10)
> Maono ya Ezekieli (Ezekieli 1)
Yesu Kristo alipozaliwa katika mwili, sio tena theofania, Bali ni utimilifu wote wa Mungu katika mwili.
Wakolosai 2:9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.
Hapo mwanzo watu hawakumwona Mungu katika utimilifu huo, kwasababu kama wangemwona Mungu wangekufa kwasababu ya dhambi. Lakini Kristo alipokuja kuondoa dhambi kwa damu yake, wanadamu wote tunamwona Mungu katika utilimilifu wote, kwa Roho Mtakatifu aliyemweka ndani yetu.
Tunakikaribia kiti cha rehema, na neema kwa ujasiri bila kufa kama kule mwanzo, kwasababu damu ya Yesu inanguvu ya kuzificha dhambi zetu zote. Ukimwona Kristo(moyoni) umemwona Mungu (Yohana 14:6-11)
Ndio maana ni kwanini leo hii mtu huwezi kumfikia Mungu bila Yesu Kristo.
Okoka leo upokee neema hii, ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Wanethini ni kundi la watu ambao walitumika katika hekalu, ambao sio asili ya wayahudi. Wanatajwa sana kwenye kitabu cha Nehemia na Ezra. Maana ya neno ‘Nethini’ kwa kiyahudi linamaanisha “waliotolewa”. Wakimaanisha watu waliotelewa kuwasaidia walawi katika shughuli za hekaluni.
Hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowataja;
Ezra 8:20 na katika Wanethini, ambao Daudi, na wakuu, walikuwa wamewaweka kwa ajili ya utumishi wa Walawi, Wanethini mia mbili na ishirini; wote wametajwa kwa majina yao.
Nehemia 7:73 Hivyo makuhani, na Walawi, na mabawabu, na waimbaji, na baadhi ya watu, na Wanethini, na Israeli wote, wakakaa mijini mwao. Hata ulipowadia mwezi wa saba, wana wa Israeli walikuwa wakikaa katika miji yao.
Soma pia, (Ezra 2:43, 2:58, 7:24)
Biblia haituonyeshi moja kwa moja asili yao ni wapi, lakini wanazuoni wengi huamini walitokea katika chimbuko la wale wagibeoni waliowadanganya Israeli wakati ule mpaka wakafanya nao maagano, Ambao Yoshua aliwapa kazi ya kupasua kuni, na kuteka maji.
Yoshua 9:27 Siku iyo hiyo Yoshua akawafanya kuwa ni wenye kupasua kuni, na wenye kuteka maji, kwa ajili ya mkutano, na kwa ajili ya madhabahu ya Bwana, hata siku hii ya leo, katika mahali hapo atakapopachagua
Mbali na hawa wagibeoni wengine wanaweza wakawa ni wageni au mateka., ambao baadaye wakaja kuwekwa kwenye utumishi wa hekaluni.
Wanethini hawakufanya kazi zozote za kikuhani, ikumbukwe kuwa ilikuwa ni kosa, mtu ambaye sio myahudi tena wa kabila la Lawi kufanya shughuli zozote za kihekalu, Hawa walikuwa wanafanya kazi za usaidizi ule wa nje, kama vile kutweka maji, kukusanya kuni, usafi, na kazi nyingine zilizohitaji msaada wa pembeni.,Ili kuwaruhusu walawi wasilemewe wajikite zaidi katika kazi za hekaluni.
Maandiko yanaonyesha walikuwa na makao yao maalumu palipoitwa Ofeli kule Yerusalemu karibu na hekalu (Nehemia 3:26)
Hata Baadaya ya uhamisho wa Babeli, tunaona mabaki yaliyorudi Israeli kufanya shughuli za kihekalu, hawa wanethini pia walirejea
Kwa ufupi wanethini walikuwa ni la watu (wasio-wayahudi) waliowekwa kwa ajili ya kusaidia shughuli za hekaluni.
Licha ya kwamba Mungu ameliita kanisa lake na amelitenga, limtumikie lenyewe katika shughuli zote za kimadhabahu. Lakini Bado Bwana anaweza kunyanyua watu wengine nje ya kanisa, kusaidia kanisa kusonga mbele. Mfano wa hawa ni Yule akida wa kirumi ambaye alilipenda taifa la Israeli na kulijengea sinagogi (Luka 7:1-5). Hakuwa myahudi lakini aliwasaidia wayahudi.
Hata sasa wanethini wapo wengi, hawapaswi kuzuiliwa, endapo wanasaidia kanisa au kazi ya Mungu, kwasababu ni Bwana ndiye aliyewavuta.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Swali: Je ni vema sisi tuliookoka kushika matawi siku ya jumapili na kuingia nayo kanisani au kutembea nayo?
Jibu: Jumapili ya mitende ni jumapili moja kabla ya jumapili ya pasaka, ambapo katika historia ni siku ambayo KRISTO aliingia YERUSALEMU, na watu wakakata matawi ya mitende na kuyatandaza njiani ili Bwana YESU apite. (kumbuka, mtende ni mti unaozaa matunda ya tende).
Mathayo 21:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,
2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana punda pamoja naye; wafungueni mniletee.
3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.
6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; NA WENGINE WAKAKATA MATAWI YA MITI, WAKAYATANDAZA NJIANI.
9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.
10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?
11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya”.
Sasa swali ni je! Na sisi ni sahihi/ruksa kuisheherekea/kuiadhimisha hii siku?
Jibu: Hatujapewa agizo lolote kwenye Biblia la kuiadhimisha jumapili ya mitende, wala jumapili ya pasaka. Isipokuwa kutokana na umuhimu wa hizo siku katika historia ya Ukristo, si vibaya kuzifanya hizo siku/tarehe kuwa za ibada ya kutafakari mambo yaliyotokea wakati huo.
Kwamfano katika jumapili ya mitende, ni wakati ambao watu walimsifu YESU kwa kumwimbia Hosana Hosana (yaani Okoa). Nasi kwa kutafakari jambo hilo twaweza kutengeneza kama igizo la wakati huo, na kumwimbia Bwana kwa furaha tukisema Hosana amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la BWANA, kwa kufanya hivyo huku tumeshika matawi ya mitende sio kosa wala dhambi kwani ni sehemu ya sifa tu kama sifa nyingine zinazohusisha shangwe za kurusha rusha leso juu au matawi ya miti.
Lakini matawi yale yakifanyika kama ni vitu vitakatifu, (kwamba vimebeba nguvu Fulani ya kiungu, kama vile sanamu zinazowekwa kwenye baadhi ya makanisa) hilo ni kosa, kwani tayari hizo ni ibada za sanamu, na si tena kwa lengo la sifa za kumtukuza MUNGU.
Utakuta mtu anatembea na tawi lile si kwa lengo la sifa, wala tafakari ya mambo yaliyotokea miaka elfu mbili iliyopita, bali kama kisaidizi cha kuondoa mikosi, au matatizo, au cha kufukuzia wachawi n.k Huyu mtu anakuwa anafanya ibada za sanamu, na inaweza isiwe ni kosa lake bali la waliomfundisha.
Kwahiyo jumapili ya mitende si vibaya kuadhimishwa ikiwa itafanyika kwa ufunuo na maarifa namna hiyo, lakini kama itafanyika kidini na kidesturi, inageuka kuwa ibada ya sanamu, jambo ambalo ni machukizo kwa BWANA.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
AKAUKAZA USO WAKE KWENDA YERUSALEMU.
MUNGU AKETIYE MAHALI PA JUU PALIPOINUKA.
Ni mji gani mtakatifu shetani aliomchukua Bwana YESU? (Mathayo 4:5)
SWALI: Kwanini Yesu akubali ombi la mapepo, na si kuyaamulia adhabu yake mwenyewe, au kuyafukuza kabla hata hayajaongea?
Luka 8:31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. 32 Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.
JIBU: Maneno hayo aliyasema baada ya kukutana na mtu yule aliyekuwa amevamiwa na jeshi la mapepo, yaliyomfanya akae makaburini muda mrefu, bila nguo. Hivyo kama tunavyosoma yale mapepo yalipomwona tu Yesu, kabla ya tamko lolote yenyewe yakamfuata na kuwasilisha ombi lao kwa kusihi sana. Kwamba yawaingie wale nguruwe waliokuwa jirani wakichungwa. Yesu akasiliza ombi lao, akayapa ruhusa. Yakamtoka Yule mtu, na kuwaelekea wale nguruwe, na saa ile ile Yule mtu akawa mzima.
Zipo sababu mbili.
Ni wazi kuwa Bwana alilitafakari wazo lao, na kuona kama lingeweza kuleta madhara yoyote au uharibifu wowote wa mpango wa Mungu. Na akaona kinyume chake ni kuwa kusudi la Mungu litaendelea kuthibitika hata katika ombi lao, kwasababu kutoka kwao na kuwaingia wale nguruwe kisha kwenda kujitupa ziwani. Ilikuwa ni udhihirisho wa wazi kwa watu kuwa mapepo ni halisi, lakini pia yanatabia ya uuaji. Kwamfano kama angemponya tu, bila ishara yoyote, pengine wengine wangesema “aah huyu akili zilimruka tu!” alikuwa na stress zake, au maisha yalimtinga sana, akachizika, hivyo amekutana na mwanasaikolojia mzuri amemweka sawa… Lakini kuona mapepo yale yameruhuisiwa kwenda kuingia viumbe vingine, halafu yakawaendesha ziwani kuwaua, ilikuwa ni ishara bora zaidi ya kazi za Mungu.
Utakumbuka mapepo yenyewe yalimwambia Yesu ‘tuna nini nawe, je umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?’
Mathayo 8:29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Maana yake ni kuwa mapepo yalijua kuwa walishawekewa wakati wao wa mateso baadaye kule shimboni na atakayekuja kuwapeleka huko ni Kristo. Hivyo hapa yanamkumbusha Bwana asibatilishe mpango huo, na kuwaadhibu mapema.
Pengine hiyo ndio sababu nyingine ya Bwana kutotoa adhabu kali kwao, ni kuwa mpango wa hukumu ungebatilika.
Kitendo cha mapepo kujisalimisha yenyewe kuomba kupunguziwa adhabu, ni kuonyesha mamlaka kuu iliyo ndani ya Kristo. Ambayo hata sasa ipo ndani yetu. Hatufundishwi kuongea na mapepo, bali kuyakemea kwa mamlaka yote. Ambayo yaweza tokea mengine hata kabla ya kukemewa yakaomba yenyewe nafasi ya kupunguziwa adhabu. Hilo linawezekana!
Tumia mamlaka uliyopewa ndani yako. Fukuza pepo wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Gengeni ni wapi, wale nguruwe walipoteremkia? (Marko 5:13)
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Marko 4:35-36
[35]Siku ile kulipokuwa jioni, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo.
[36]Wakauacha mkutano, wakamchukua vile vile alivyo katika chombo. Na vyombo vingine vilikuwako pamoja naye.
Vifungu hivi vinazidi kutueleza tabia ya Bwana wetu Yesu Kristo na huduma yake jinsi ilivyokuwa ya kitofauti sana hapa dunia.
Kujitoa kwake kulikuwa ni kwa gharama sana tofauti na sisi tunavyoweza kufikiri, embu fikiria kisa kile cha pale kisimani alipokutana na yule mwanamke msamaria, na kuanza kumshuhudia habari zake mpaka kupelekea wimbi kubwa la watu Samaria kumfuata.
Kwa jicho la kawaida unaweza kudhani ilikuwa ni huduma ya kawaida lakini kiuhalisia haikuwa ni jambo lililomruhusu sana kimwili. Kwani maandiko yanatuambia alichoka sana kwasababu alikuwa katika safari ndefu kutoka uyahudi Kwenye Galilaya.
Tunasoma akiwa na njaa na kuchoka ‘alijibwaga’ hivyo hivyo pale kisimani, akawaruhusu wanafunzi wake kwenda mjini kutafuta chakula..
Lakini Mwanamke yule alipokuja kisimani hakusema ngoja nipumzike kwanza, nivute pumzi, kinyume chake alianza muda ule ule kusema naye..hata baadaye alipoletewa chakula ale hamu yake ya kula ilikatwa na ile kazi ya Mungu Aliyokuwa anaifanya.
Yohana 4:6-8,30-33
[6]Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
[7]Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
[8]Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula…..
[30]Basi wakatoka mjini, wakamwendea.
[31]Huko nyuma wanafunzi wakamsihi wakisema, Rabi, ule.
[32]Akawaambia, Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi.
[33]Basi wanafunzi wake wakasemezana, Je! Mtu amemletea chakula?
Vivyo Hivyo tena wakati mwingine alikuwa anawahubiria Makutano mchana kutwa, mpaka ilipofika jioni ambapo alipaswa aende kupumzika kidogo, ili kesho aendelee na huduma. Maandiko yanatuambia akawaambia wanafunzi wake “Tuvuke Ng’ambo”.
Kibinadamu jambo kama hilo la safari Nyingine mpya lingetemea kwanza maandalizi fulani labda ya chakula, au mavazi, au kushughulikia mahitaji mengine…lakini kwakua kusudi la Mungu lilimsukuma kwa nguvu wakamchukua Vilevile alivyo katika chombo Mpaka ng’ambo..hakuna kuoga, wala kupumzika, wala kuwatembelea marafiki na ndugu, ni kuunganisha ziara nyingine, sio kwamba alikuwa hachoki hapana alichoka sana, kuthibitisha hilo utaona akiwa katikati Ya safari ile alipitiwa na usingizi kwa sababu ya uchovu (4:38)
Hii inatuonyesha wazi utayari wa Kristo ambao uliathiri mpaka hali zake za kimwili.
Kwasababu yeye ni yule yule jana na leo na hata Milele, utayari ule ule aliokuwa nao zamani anao hata leo.
Kristo haitaji maandalizi wala hali ya kimazingira, katika kutumika Na sisi. Ni rahisi Kudhani mpaka Bwana atende miujiza tunahitaji kwanza maandalizi ya Maombi na mifungo na mikesha, au mpaka Bwana amwokoe mtu tunahitaji tuwe na elimu nyingi ya biblia, au uzoefu kumbe si lazima..
Ni kweli mambo hayo ni muhimu katika baadhi ya mazingira lakini si yote. Anataka tuwe wepesi wa kumchukua yeye vilevile kama alivyo katika mazingira yoyote?
Yupo tayari kwenda na sisi popote, maadamu tu sisi tunakuwa tayari kumchukua katika safari zetu kwa imani. Hatupaswi kujali tutatolea Wapi fedha za huduma kumuhubiri Kristo.
Ikiwa umeokoka, ni nini unasubiri Usimtumikie Mungu wako?. Unataka uwe kama Martha ambaye alijisumbua na maandalizi mengi wakati lililohitajika ni moja tu, kumsikiliza Kristo? Kumchukua vilevile kama alivyo.
Yesu alipowaacha mitume hakuwapa mitaji ya maspika, au vyuo vya kusoma au majengo ya kuabudia…aliwaambia enendeni nami nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari. Msibebe fimbo wala mkoba, wala pesa kibindoni, wala kanzu mbili.(Mathayo 10:5-10)
Kwa tafsiri nyingine anasema nichukueni hivi hivi nilivyo, msijali hali yangu, nanyi mtaona Maajabu mbeleni.
Bwana atujalie kujua matamanio yake, ili tusizuiliwe kuhudumu naye popote, kwenye mazingira yoyote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Masomo mengine:
RABI, UNAKAA WAPI?
Yesu alipopanda kuomba kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine?
SAUTI NYUMA YA ISHARA.
Swali: Neno la MUNGU linamaanisha nini linaposema “mtu atachukua dhambi yake au uovu wake”?
Jibu: Turejee andiko hilo..
Walawi 5:17 “Na kama mtu akifanya dhambi, na kutenda mambo hayo mojawapo ambayo Bwana alizuilia yasifanywe, ajapokuwa hakuyajua, ni mwenye hatia vivyo, NAYE ATACHUKUA UOVU WAKE”
Tusome tena..
Walawi 24:5 “Nawe nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake ATACHUKUA DHAMBI YAKE”.
Utalisoma tena neno kama hilo katika Walawi 7:18, Hesabu 9:13, Ezekieli 44:10-12..
Katika Agano la kale Bwana MUNGU aliruhusu mtu kulipizwa kisasi endapo amefanya jambo la kusudi lililo baya.. kwamba UHAI kwa UHAI.. jino kwa jino..jicho kwa jicho..
Maana yake kama mtu amemkata mwenzake mkono naye pia ni lazima akatwe mkono, kama mtu amemwua mwenzake sharti naye pia auawe..
Walawi 24:17 “Na mtu ampigaye mtu hata akafa, lazima atauawa;
18 na atakayempiga mnyama hata akafa atalipa; uhai kwa uhai.
19 Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;
20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo”.
Lakini yapo matukio ambayo yalikuwa yakifanyika yanakuwa HAYANA KISASI!, kwamfano mtu aliyesikika kamtukana MUNGU au kulilaani jina la MUNGU, mtu huyo sheria ilikuwa ni kuuawa kwa kupigwa mawe, sasa wale watu waliomwua kwa kumpiga mawe baada ya kuthibitika uasi wa Yule mtu, hao hawawezi kulipwa kisasi kwamba nao wauawe kwasababu sheria imesema uhai kwa uhai.
La! Bali wataachwa hai,.. sasa hiko kitendo cha hawa wauaji kuachwa Hai na kutokulipwa kisasi ndio tafsiri yake kwamba “Yule aliyekufa kauchukua uovu/dhambi yake mwenyewe”.. maana yake hajaacha dhambi kwa waliomwua!.
Lakini laiti kama atauawa pasipo hatia na ikathibitika hivyo, basi wauaji wale watabeba dhambi ya mauaji hivyo nao pia watauawa, kama sheria isemavyo kwamba uhai kwa uhai na jino kwa jino. Sasa kitendo hiko cha kuuawa kwa kosa la mauaji yasiyo na hatia, ndicho kinachoitwa kubeba dhambi ya aliyekufa.
(kumbuka si kwamba watabeba makosa ya Yule mtu, la!, Yule mtu atabaki na dhambi zake alizozifanya.. bali hawa wauaji watabeba lile kosa moja tu la mauaji ya mtu asiye na hatia), hivyo watahukumiwa tu kama wauaji waliomwua mtu asiye na hatia.
Na lugha nyingine ya kubeba dhambi ya mtu ni kubeba damu ya mtu. Hivyo mahali popote katika biblia Bwana MUNGU anaposema kuwa “nitaitaka damu mikononi mwa mtu” maana yake ni hiyohiyo kwamba “kwamba atamhukumu muuaji kwa kosa la kumwua asiye na hatia”.. na anaposema damu yake itakuwa juu yake mwenyewe aliyefanya kosa, maana yake ni kwamba aliyeuawa hatalipiwa kisasi kwa waliomwua.
Zifuatazo ni baadhi ya dhambi ambazo mtu akizitenda basi alibeba dhambi zake mwenyewe, wala waliomwua hawakuwa na hatia ya kulipwa kisasi wala kushtakiwa.
Je hata sasa (Agano jipya) sheria hizi zipo?.
Katika Agano jipya hatuna sheria yoyote ya kisasi, Bwana YESU alitufundisha hilo katika Mathayo 5:38-41, ikiwa na maana kuwa hatujapewa ruhusa ya kumwua mtu au kulipiza kisasi bali kisasi ni juu ya Bwana (soma Warumi 12:19).
Kwahiyo kama hatujapewa ruhusa ya kulipa kisasi, au kutoa hukumu ya aina yoyote kama katika kipindi cha agano la kwanza, basi maana yake ni kwamba mtu yoyote Yule alipaye kisasi atakuwa na hatia pasipo kujalisha makosa aliyoyafanya ndugu yake!..
Muuaji wa aina yoyote ile, atabeba kosa la mauaji, (Bwana ataitaka damu ya aliyemwua mikononi mwake).. hata kama amemwua mtu aliyemlaani MUNGU, bado ni kosa!..katika agano la kale haikuwa makosa lakini agano jipya ni kosa!.
Kwahiyo hatujapewa ruhusa ya kuua kwa kosa lolote lile, tukifanya hivyo tutakuwa na hatia na Bwana ataitaka damu ya aliyekufa mikononi mwetu.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Orodha ya majina ya Miji ya Biblia (Agano la kale) na Sasa
Agano la Chumvi ni nini? (2Nyakati 13:5)
Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?
Jibu: Turejee maandiko machache..
“Uhai” ni hali ya kuwa “HAI” (yaani kuishi) ili kiumbe kiwe kinaishi ni lazima kipumue, kile, kikue na hata kijongee. Hizo ndizo tabia chache za viumbe HAI, Wanadamu, wanyama na mimea vyote vina uhai kwasababu vinapumua, vinaongezeka na pia kujongea.
Lakini “UZIMA” Umeenda mbali zaidi kuelezea UHAI wa kiroho ambao unapatikana kwa mtu kuwa na mahusiano na MUNGU.
Uhai unaelezea mwili lakini Uzima unaelezea roho. Mimea haina UZIMA bali ina UHAI.. wanyama hawana UZIMA bali wana UHAI maandiko yanaonyesha hivyo…
Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri UHAI WA MNYAMA WAKE; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.
Na UZIMA unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO,
Yohana 10:10 “Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, kisha wawe nao tele”.
ikiwa na maana kuwa wanadamu yoyote aliye nje ya YESU KRISTO anao “Uhai” tu kama wanyama lakini hawana “Uzima”… anapumua, anakula, anatembea lakini akisha kufa hana UZIMA tena.. Lakini aliye ndani ya KRISTO, hata akiwa amekufa ataendelea kwasababu anao UZIMA wa MILELE alioupokea kutoka kwa YESU.
Je unao uzima wa milele ndani yako?…Je YESU ni sehemu ya maisha yako?
Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape UZIMA WA MILELE.
3 Na UZIMA WA MILELE ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.
Maran atha!
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
JE! UPO KATIKA MAJI YA UTULIVU?
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Kwanini pawekwe MITI pale bustanini na si kitu kingine?.