Category Archive Home

Nini maana ya Israeli?

JIBU: Maana yake ni “yeye ashindanaye na Bwana”

Siku ile Yakobo alipotokwa na Mungu, kisha akashindana naye usiku kucha bila kumwacha, ndipo yule mtu akamuuliza jina lako nani, akasema Yakobo, akaambiwa hutaitwa tena hilo jina Yakobo, bali Israeli.

Mwanzo 32:28

[28]Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.

Au kwa namna nyingine tafsiri yake ni

“mtu anayeng’ang’ana na Mungu mpaka kuona matokeo”

Ndio jina ambalo kabila zake zote ziliitwa. Leo hii tunaposema taifa la Israeli, tunamaanisha taifa la washindanaji.

Lakini Israeli kwa agano jipya si hii ya mwilini tu.. bali ile ya rohoni ambayo imeundwa na Yesu Kristo mwenyewe..

Warumi 2:28-29

[28]Maana yeye si Myahudi aliye Myahudi kwa nje tu, wala tohara siyo ile ya nje tu katika mwili;

[29]bali yeye ni Myahudi aliye Myahudi kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko; ambaye sifa yake haitoki kwa wanadamu bali kwa Mungu.

Maana yake ikiwa umempokea Kristo, wewe tayari ni mwisraeli/myahudi.

Na kama ni mwisraeli, jua asili ya jina lako..kuwa wewe ni mtu wa kung’ng’ana na Mungu…sio mtu mwepesi mwepesi…

Usimrajie Mungu katika vitu virahisi rahisi, huyo ndio sababu kwanini tunakuwa na mifungo na mikesha, kudumu uweponi mwa Bwana wakati mwingi, kumtafuta Bwana, sio kwamba yeye ni mgumu kupatikana hapana, bali kwa asili hataki wana walioitwa kwa jina hilo wawe walegevu,

Wengi hulalamika, mbona sioni uwepo wa Mungu, mbona sioni amani ya kutosha ndani, siono furaha ya wokovu, ukiwauliza vipi juhudi yako rohoni…mmoja atasema ratiba yangu huwa ni maombi ya dk 10 kwa siku, kusoma Neno dk 10.. Sasa mtu kama huyu hawezi kuhudumiwa vema na Mungu ikiwa ameokoka…

Ndugu jitambue wewe ni nani! Ikiwa ni mwisraeli, simama kama mtu shupavu kung’ang’ana na Mungu wako, nje ya hapo, tafuta jina lingine na mungu mwingine mwenye vigezo vyake vya kukuhudumia, lakini kama ni waisraeli wa Kristo, basi ni watu wa kuliitia jina la Bwana bila kukoma (Luka 18)

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NINI MAANA YA UKOMBOZI?

Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?

PALE MAOMBI YANAPOGEUKA KUWA MAPAMBANO.

Print this post

Njumu ni nini? (Wimbo 3:10)

Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa urujuani, GARI LAKE LIMENAKISHIWA NJUMU, Hiba ya binti za Yerusalemu”.

Neno hili pia tunalisoma katika 1Nyakati 29:2..

1Nyakati 29:2 “Basi kwa uwezo wangu wote nimeiwekea akiba nyumba ya Mungu wangu, dhahabu kwa vitu vya dhahabu, na fedha kwa vitu vya fedha, na shaba kwa vitu vya shaba, na chuma kwa vitu vya chuma, na miti kwa vitu vya miti; vito vya shohamu, na vya kujazia, VITO VYA NJUMU, na vya rangi mbalimbali, na mawe ya thamani ya kila namna, na marimari tele.

“Njumu” ni malighafi za “kung’ara ng’ara/ kuwaka-waka” Tazama picha juu, mfano wa vazi lililonakshiwa na Njumu..

Na gari la Mfalme Sulemani kulingana na maandiko hayo ya Wimbo 3:10, lilikuwa limenakshiwa na malighafi hizo za kung’ara ng’ara, hivyo lilikuwa linavutia sana, lakini pamoja na kunakshiwa kwa vito hivo vyote vya thamani lakini bado sifa za binti Yerusalemu zilikuwa bora zaidi.

Kufahamu kwa kina Gari/Machela ya Sulemani jinsi ilivyokuwa na rangi ya Urujuani ilikuwaje fungua masomo chini ya somo hili, Bwana akubariki..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Urujuani ni nini? (Wimbo 3:10)?

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

MAANA YA KUISHI NA MKE KWA AKILI.

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

Print this post

Binti za Yerusalemu wanaotajwa katika kitabu cha Wimbo ulio Bora 1:5 ni akina nani?

Swali: Katika kitabu karibia chote cha Wimbo uliobora tunaona wakitajwa sana Binti za Yerusalemu je, hawa walikuwa ni mabinti wa aina gani?..au ni wa mji wa Yerusalemu kama Biblia inavyosema hapo?

Jibu: Turejee..

Wimbo 1:5 “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, ENYI BINTI ZA YERUSALEMU, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.”

Sehemu nyingine Biblia inawaasa hawa Binti za Yerusalemu kutoyachochea mapenzi ..

Wimbo 2:7 “Nawasihi, enyi BINTI ZA YERUSALEMU, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe”.

Sasa swali hawa Binti za Yerusalemu ni akina nani?

“Binti za Yerusalemu” au kwa lugha nyingine “Binti Sayuni” ni lugha ya mithali inayowakilisha “Jamii nzima ya watu wa Israeli”… na si Mabinti waliopo Yerusalemu tu peke yao..la! bali jamii yote ya wana wa Israeli.

Turejee maandiko yafuatayo ili tuweze kulielewa hili vizuri…

Zekaria 9:9 “Furahi sana, EE BINTI SAYUNI; piga kelele, EE BINTI YERUSALEMU; Tazama, mfalme wako anakuja kwako; Ni mwenye haki, naye ana wokovu; Ni mnyenyekevu, amepanda punda, Naam, mwana-punda, mtoto wa punda.”

Unabii huu ulimuhusu Bwana YESU kipindi anaingia Yerusalemu, ambapo jamii ya watu wote walipomwona walikata majani ya mitende na kutandaza njiani ili apite..

Yohana 12:15 “Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;

13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, HOSANA! NDIYE MBARIKIWA AJAYE KWA JINA LA BWANA, MFALME WA ISRAELI!

14 Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,

15 Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.

16 Mambo hayo wanafunzi wake hawakuyafahamu hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kwamba ameandikiwa hayo, na ya kwamba walimtendea hayo”.

Umeona hapo?.. waliooimba Hosana! Hosana! si tu mabinti waliokuwepo Yerusalemu bali “ni jamii yote na marika yote!”.. ikifunua kuwa Binti za Yerusalemu ni jamii nzima wa Israeli, kuzidi kulithibitisha hilo soma pia Mika 4:8, 2Wafalme 19:20-21, Isaya 37:22, na Isaya 62:1.

Na sisi kama wakristo (wakike na kiume) tunahesabika kama Israeli ya Rohoni, hivyo sisi sote pasipo kujalisha jinsia zetu, marika yetu wala nafasi zetu, maadamu tu tumempokea YESU tunafahamika kama Binti Sayuni, au Binti za Yerusalemu.

Na Biblia inatuonya Binti za Yerusalemu, mji wa Mungu tujiepushe na dhambi, hususani Uasherati wa rohoni na mwilini.

Uasherati wa rohoni ni ibada zote za sanamu.. Je umempokea BWANA YESU KRISTO?.

Fahamu kuwa hizi ni siku za Mwisho na YESU amekaribia sana kurudi.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

DANIELI: Mlango wa 2

Machela ni nini (Wimbo ulio bora 3:7)

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?

MAAJABU YA AGANO LA UPENDO WA KRISTO.

JE UMEJIFUNZA ULE WIMBO MPYA?

Print this post

WEWE NI NANI PALE AMBAPO WATU HAWAKUONI?

Tunasahau sana maisha yetu ya sirini, na kuweka nguvu kubwa, katika kuonekana kwetu kwa  nje mbele za watu, hatujui kuwa Darasa kubwa la Mungu kwa mwanadamu lipo katika maisha yake ya sirini.  Na Mungu humlipa mtu kwa hayo na si mengine.

Mathayo 6:4….na Baba yako aonaye sirini atakujazi.

Kujazi maana yake ni kulipa.

Ikiwa na maana, unayoyatenda sasa iwe ni mema au mabaya kwa siri, malipo yake utayaona baadaye kwa wazi.

Yusufu, kabla ya kuwekwa kuwa msimamizi wa mali yote ya Farao, alitumika kama wakili mwaminifu katika nyumba ya potifa, kwa muda mrefu. Baadaye Mungu akamlipa kwa kumpa Misri yote.

Yuda mpaka kuingiwa na shetani, hadi kumuuza Bwana wake, ni matokeo ya wizi aliokuwa anaufanya kwa siri kwa muda mrefu.

Daudi kabla ya kujazwa mafuta ya kumwangusha Goliathi, ni maisha ya sirini ya Imani aliyokuwa anayadhihirisha kule maporini kwa Mungu wake, mbele ya simba na dubu walipokuwa wanakuja kulishambulia Kundi. 1 Samweli 17:34-37)

Vilevile, kwa mtu yeyote yule, kupata kibali, kutumiwa na Mungu, kuinuliwa viwango vya kiroho..hutegemea sana hali zetu za sirini zinazoendelea sasa, Kwamfano utakuta labda huyu ni mwanakwaya, au mtumishi wa Mungu, lakini katika maisha yake ya sirini, anajichua, ni mzinzi, anakunywa pombe, Lakini kwa nje, anajionyesha kuwa ni mwema, anautunza ushuhuda wake, anavaa mavazi ya kujisitiri, anaongea kwa staha, ana juhudi katika utumishi, akidhani kuwa hilo ndio litamshawishi Mungu kumwongezea neema.

Ukweli ni kwamba hapo anapoteza nguvu, kwasababu tusipokuwa waaminifu katika madogo ya sirini, Bwana Yesu hawezi kutuaminisha katika makubwa.. Tabia mbaya za sirini, zinaharibu huduma zetu, utumishi wetu wa baadaye.

Mtu anataka apandishwe labda cheo kazini, lakini katika nafasi hiyo hiyo ya chini, anaiba,  mwingine anataka apewe cheo lakini pale pale alipo hawajali watu walio chini yake, ni mwenye wivu, . Unategemea vipi Mungu amlipe mtu kama huyu?

Kabla hujalipwa na Mungu, unakuguliwa kwanza na Mungu.

Shughulika na maisha yako ya binafsi ya sirini, kwasababu hayo ndiyo yanayokueleza utakuwa nani mbele za watu baadaye.

Nini cha kufanya..

Mwalike Bwana, akuchunguze, sirini mwako, Mawazo yako, tabia zako, matendo yako. Kisha mwombe akuponye, na baada ya hapo anza kutendea kazi uliyoyaomba.

Simamia andiko hili;

Zaburi 139:23-24

23 Ee Mungu, unichunguze, uujue moyo wangu, Unijaribu, uyajue mawazo yangu;
24 Uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu, Ukaniongoze katika njia ya milele

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

USIIHARIBU TABIA YAKO KWA MAZUNGUMZO YAKO.

NIONYESHE MARAFIKI ZAKO, NIKUAMBIE TABIA ZAKO.

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

Print this post

Hiba ni nini? (Wimbo 3:10)

Swali: Neno Hiba linamaanisha nini kwenye Biblia kwa mujibu wa andiko hili, Wimbo 3:10.

Jibu: Turejee..

Wimbo 3:10 “Nguzo zake alizifanyiza za fedha, Na mgongo wake wa dhahabu, Kiti chake kimepambwa urujuani, Gari lake limenakishiwa njumu, HIBA ya binti za Yerusalemu”.

“Hiba” kama ilivyotumika hapo inamaanisha “Mapenzi ya Kina (yale yaliyozama kabisa)”

Kwahiyo hapo kwa Kiswahili chepesi kabisa mstari huo unaweza kusomeka hivi.. “..Gari lake limenakishiwa njumu, MAPENZI YA DHATI ya binti za Yerusalemu”

Mstari huu unaelezea Machela ya Mfalme Sulemani (yaani kiti chake kinachotumika kumbebea, anaposafiri) jinsi kilivyopambwa vizuri, na jinsi kilivyo na ufahari, lakini hayo yote si kitu zaidi ya Upendo wa dhati.

Hivyo Upendo wa dhati unaotoka kwa hadhira ya binti za Yerusalemu ni bora kuliko fedha na dhahabu, na huo unaeleza zaidi uthamani wa kitu kuliko mapambo mengine yote.

Je umempa YESU maisha yako?

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je kunena kwa Lugha mpya kukoje?

UWEZO WA KIPEKEE.

TUNALINDWA NA NGUVU ZA MUNGU.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

NAO WAKAMSHINDA KWA DAMU YA MWANA-KONDOO.

Print this post

WEWE NI ZAO LA MAHUSIANO NA USHIRIKA.

Ulishawahi kujiuliza, kwanini Mungu atumie  namna ya “wingi”, alipomuumba mwanadamu, na sio, “umoja”, kama alivyokuwa anafanya kwenye uumbaji wa vitu vingine?

Mwanzo 1:26-28

26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba

Anasema na “tumfanye” mtu kwa mfano wetu, na si “nimfanye mtu”? Ni kuonyesha hali ya asili ya anaye muumba, kwamba si wa kibinafsi, bali ya kimjumuiko..asili yake ni jumuiya. Ijapokuwa ni Mungu mwenyewe ndio aliyemuumba mwanadamu, lakini wazo lake aliwashirikisha Malaika zake, ambao walikuwepo kabla yetu sisi..Ndio maana ya hiyo “na tumfanye mtu”

Ni kufunua kuwa sisi ni zao la muunganiko, na ushirika, na ndivyo ambavyo tunaweza pia kuzaa, au kufanikiwa katika namna hiyo hiyo.. Ndio maana, hata sisi tukitaka kumleta mwanadamu mwenye asili yetu, sio jambo la mtu binafsi kujitakia pekee yake, ni lazima mwanamume, atakutana na mwanamke, kila mmoja atachangia alichonacho, na mwishowe, anatokea kiumbe kama wao. Hiyo ni kanuni..sisi  kuwepo ni kazi ya “mchango” iliofanywa na watu wawili.

Hata katika maendeleo yetu, na mafanikio yetu. Jambo lolote tukitaka lifanikiwe, ni sharti tukubali michango.. Haiwezekani mtu kusimama mwenyewe mwenyewe kufanikisha kila jambo., Ukuaji wa kiroho, unahitaji kanisa,  ukutanapo na watakatifu wenzako,(wawili, watatu, mia) ndipo unajengwa na kukua, tofauti na kujisukuma mwenyewe mwenyewe, hakuna mafanikio .

Vilevile na katika maendeleo ya mambo mengine yote ya mwilini na rohoni, wanaofanikiwa, ni watu wenye kuruhusu, michango, kusaidiwa, kujihusianisha, kujishusha, kujengwa, kufundishwa, kushauriwa, kuwezeshwa, na wengine..Na hatimaye kufanikiwa..Mafanikio ya moyoni yaani furaha, amani, utulivu, ni mahusiano mazuri na mema uliyonayo na wengine, katika ushirika wa Roho Mtakatifu.

Mwanadamu kamili, huishi kwa mahusiano. Kuanzia sasa usipuuzie mahusiano, Jenga mizizi yako vema, tafuta kwa bidii kuishi kwa amani na watu wote (Waebrania 12:14). Kwasababu wewe ni zao la Mahusiano, tangu mwanzo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

ENYI WAJINGA, ACHENI UJINGA, MKAISHI

Mithali 9:6 “Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi, Mkaende katika NJIA YA UFAHAMU”.

Kibiblia mtu asiye na Ufahamu ni “Mjinga”..Na hapa Neno la MUNGU linasema… “Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi, Mkaende katika NJIA YA UFAHAMU”..

Sasa hiyo sio Kejeli wala Tusi, bali ni onyo, kwamba mtu akiendelea kuishi katika Ujinga atapoteza maisha yake, kwasababu ya kukosa ufahamu.

Sasa swali ni je! Ufahamu ni nini na njia ya ufahamu ni nini?.. Biblia hii hii imetupa majibu ya nini maana ya ufahamu.

Ayubu 28:28 ”Kisha akamwambia mwanadamu, Tazama, kumcha Bwana ndiyo hekima,  NA KUJITENGA NA UOVU NDIO UFAHAMU”.

Kumbe mtu anayejitenga na Uovu kwa mujibu wa Biblia ndio mwenye Ufahamu!.

Mtu anayejitenga na zinaa, ulevi, ibada za sanamu, uuaji, uvaaji mbaya n.k ana UFAHAMU!!..

Nilifikiri Biblia ingesema mtu mwenye ufahamu ni yule mwenye elimu kubwa, au mwenye uwezo wa kutafuta Pesa..Lakini kumbe ni kinyume chake.

Mtu awe na elimu kubwa au cheo kikubwa, elimu kubwa au uwezo mwingine wowote wa kimaisha na huku dhambo bado inamshinda ni MJINGA kulingana na Biblia.

Na Biblia imesema “Mjinga aache ujinga wake akaishi”.

Je wewe ni Mjinga au mwerevu?.

Kama bado upo chini ya utumwa wa dhambi, basi kuna ujinga unakusumbua ambao YESU KRISTO anaweza kukusaidia ukatokana nao na ukapata Ufahamu.

Kinachohitajika ni wewe tu kudhamiria kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa katika ubatizo sahihi na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

Kuanzia huo wakati Ufahamu wa KiMungu utaingia ndani yako.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

TUNAFAHAMU KWA SEHEMU, TUNAFANYA UNABII PIA KWA SEHEMU.

1 Wakorintho 13:9-10

[9]Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;

[10]lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.

Biblia inatupa dira kamili wa maisha yetu, na namna ambavyo tunapaswa kumwelewa Mungu na utendaji kazi wake kwetu sisi. Ni vizuri wewe kama mtoto wa Mungu, kujua ni kipi umewezeshwa kujua na kipi hujawezeshwa..

Watu wengi tunapopitia hili andiko, tunashindwa kulitafakari kwa ndani zaidi, na matokeo yake yanakuwa ni kuishi maisha ya kuhangaika na kutaabika tukidhani kuwa Mungu hasemi au Mungu hajibu.

Roho Mtakatifu anatufundisha kuwa katika eneo la kujua mambo yote, sisi hatujakusudiwa kwa sasa. Hujakusudiwa kuishi duniani ujue kila kitu.

Bali kwa sehemu ndogo tu.. kwa mfano wa sasa tunasema unapewa vidokezo(trailer) vya filamu. Lakini picha nzima ya filamu yote hutaijua sasa, mpaka utakapovuka ng’ambo.

Ndivyo ilivyo katika mambo yote, kwamfano ikiwa mtu unamwomba Mungu akupe kujua jambo Fulani, au akufunulie kila kitu kinachoendelea au kitakachoendelea, au akufunulie kila kitu kinachohusu maisha yako ya sasa au ya baadaye…usitarajie utaonyeshwa taswira yote, kwamba leo itakuwa hivi, kesho vile, mwaka vile, wiki ijayo vile n.k. ndugu haiwi hivyo Mungu atakugusia kwa sehemu tu..ndogo ndogo ambazo hizo zitakupa picha fulani…lakini si taswira yote, kwasababu tumepewa kujua kwa sehemu.

Ikiwa wewe ni nabii, Mungu amekuonyesha jambo, toa unabii kama ulivyoonyeshwa usianze kuweka matukio yako ambayo hujaonyeshwa ..mwisho wa siku utajichanganya mwenyewe au jamii unayoitabiria..kwasababu hata iweje huwezi jua kila kitu, huwezi funuliwa kila jambo hata ulieje.

Ndio yaliyomkuta Yohana Mbatizaji.. aliweka matarajio yake, fikra zake, na kuziamini sana mwisho wa siku akamwona hata Kristo siye…ilihali alimshuhudia mwenyewe ndiye.

Kwamfano leo utaenda kwa nabii, kisha akaonyeshwa kwenye maono umebeba mtoto wa kiume, sasa kwasababu atataka kujifanya yeye ni nabii mwenye viwango vya juu ataanza kutoa simulizi zake za uongo…Bwana ananionyesha utabeba mtoto wa kiume hivi karibuni, hivyo andaa nguo zake, pia mwombee, mwandalie na sadaka ya shukrani.

Lakini kumbe Mungu hakumaanisha atampa mtoto, alimaanisha atamfanikisha na kumfanya mlezi wa mayatima.. kwa taswira ile ya mwanamke aliyembeba mtoto.

Matokeo yake yule mwanamke anaweka matarajio yake hapo, miaka inapita hapati mtoto, baadaye yule nabii anaonekana mwongo. Kumbe sio..ni kwasababu alijaribu kuvuka kipimo cha unabii alichopimiwa.

Angesema Bwana amenionyesha hivi na hivi.. zaidi ya hapo sijui, Mungu atakufunulia mwenyewe, ingetosha kumpa yule mama wigo wa kutafakari maono yake, na yatakapotimia atajua kuwa kumbe tafsiri yake ndio ile.

Vivyo hivyo hata wewe mwenyewe..utamwomba Mungu akuthibitishie jambo Fulani, utagundua mara nyingi hupewi taarifa za kujitosheleza juu ya hilo jambo, utapewa ishara tu, wakati mwingine alama Fulani, .

Ukiona hivyo usihangaike sana kupata picha yote ya kila kitu, bali chukua hatua na Bwana atakuwa na wewe..

Ikiwa ndio hivyo tufanyaje?

Kuishi kwa Imani.

Jambo kuu tuliloumbiwa na Mungu, ni kuishi kwa imani sio kwa kuona.

Jambo lolote lifanye kwa imani, kwasababu hujapewa kujua kila kitu kwa ufasaha wote sasa..

Ikiwa na kushuhudia huwezi kungoja kwanza Mungu akuonyeshe jina la mtaa, aina ya mtu utakayekutana naye, nguo aliyovaa na jina lake ndipo uende…hapo ndugu utangoja sana..

Lakini unaenda kwa imani,.ukiamini lile Neno kwamba “nitakuwa pamoja nanyi mpaka ukamilifu wa dahari,” na matokeo yake unakutana na yule mtu ambaye Mungu amemkusudia kati ya wengi.

Hivyo ndugu fahamu kuwa tunajua kwa sehemu, tunatoa unabii kwa sehemu..

Ndio maana anamalizia kwa kusema;

1 Wakorintho 13:12

[12]Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.

Tembea kwa Imani. Unabii, maelekezo, taarifa, vinapokuja machache, ni wakati sasa wa kuchukua hatua ya kutenda kuliko kusubiri hapo muda mrefu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

HEKIMA NANE(8) ZA KIUINJILISTI, KATIKA KUWAVUA WATU KWA KRISTO.

KUSUDI LA KWANZA LA KUCHAGULIWA NA MUNGU NI LIPI?

PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.

Print this post

 Buu/ Mabuu humaanisha nini kwenye biblia?

Kibiblia ni neno lenye maana ya wale funza, ambapo hutokea palipo na mzoga, au uozo. Hivyo popote ukutanapo na Neno hilo, huashiria/humaanisha, uharibifu au maiti, au kaburi,

Kwamfano ukisoma;

Ayubu 17:14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;

Buu kama lilivyotumika hapo ni kaburi, Ayubu akimaanisha katika hatua aliyofikia, kaburi, na uharibifu ni kama familia yake (baba yake, mama yake na dada yake), kama tunavyojua familia ni kitu cha karibu sana na mtu, ndivyo Ayubu alivyojiona katika hali aliyokuwa amepitia.

Maana yake, kifo kilikuwa karibu na yeye zaidi hata ya familia yake.

Sehemu nyingine inasema;

Ayubu 25:6 iuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!

Mwandishi akimaanisha mwanadamu ni sawa na mzoga, (yaani mwili wenye uharibifu usio na umilele).

Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;

Kutoka 16:20,24, Kumbukumbu 28:39, Ayubu 7:5.

Katika maeneo mengine kwenye biblia linatajwa moja kwa moja kama  funza. (Isaya 66:24)

Hii ni hatma ya kila mwanadamu asiye na Mungu, yeye ni buu, haijalishi atakuwa na afya leo, anapesa zote ulimwenguni, anacheo kikubwa au elimu, maisha yake bila Yesu Kristo kumwokoa, ni buu tu (maiti, kaburi, )..atakufa na kuishia jehanam ya moto. Lakini  akiokoka, hata ajapokufa, ataishi, siku ya ufufuo ikifika, atafufuliwa na kubadilishwa mwili wake na kupewa mwili mwingine wa utukufu, kisha Kwenda kuishi na Kristo milele na milele mbinguni.

Ikiwa haujaokoka, bado na upo tayari kufanya hivyo leo, basi basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba upokee msamaha wa dhambi leo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).

Jehanamu ni nini?

Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?

Print this post

Ni umeme gani Bwana anaouzungumzia katika (Mathayo 24:27)?

Swali: Katika Mathayo 24:27, tunaona “UMEME” ukitajwa, Je kipindi cha Bwana YESU umeme ulikuwepo?


Jibu:  Turejee..

Mathayo 24:27 “Kwa maana kama vile UMEME utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu”.

Umeme unaozungumziwa hapo ni ule “MWANGA WA RADI” unaoonekana nyakati za Mvua… Kwaasili “Radi” ni “Umeme” na si Moto. Na tangu Uumbaji Radi zipo,

Ayubu 28:26 “Hapo alipoiwekea mvua amri, Na njia kwa UMEME WA RADI”.

Soma pia Ayubu 37:15, Zaburi 77:18, Zaburi 135:7, Yeremia 10:13, Yeremia 51:6, Danieli 10:6 na Nahumu 2:4 na Luka 10:18.

kwahiyo hapo maandiko yamemaanisha kuwa kama vile Radi imulikavyo kutoka mashariki hata magharibi ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake mwana wa Adamu.

Na kwanini Umeme umetumika kufunua ujio wa YESU?.. Ni kwasababu ya Nguvu ya Umeme, na kasi ya Umeme.. Kikawaida Radi huwa inapiga sehemu ya juu iliyoinuka nan a inaweza kupasua mti wa Mbuyu ulio mkubwa vipande viwili chini ya dakika moja..

Na YESU KRISTO atarudi kwa nguvu hizo hizo, na kupakanyaga mahali pa juu pa dunia palipoinuka (Amosi 4:13)

Isaya 22:5 “Kwa maana siku ya kutaabika, SIKU YA KUKANYAGWA, SIKU YA FUJO INAKUJA, itokayo kwa Bwana, Bwana wa majeshi, katika bonde la Maono; inabomoa kuta; na kuililia milima”.

Je umempokea YESU?.. na kumfanya Bwana na Mwokozi wa maisha yako? Na kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza yeye?.. Kama bado unasubiri nini?.. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwa YESU leo, kwamaana siku hizi tuishizo ni siku za hatari na dakika yoyote ule mwisho unafika.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAUTI NA UZIMA HUWA KATIKA UWEZO WA ULIMI.

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).

FUNGUO ZA UZIMA, MAUTI NA KUZIMU.

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

Print this post