Category Archive Home

HIVI UNAMTESA MWOKOZI WAKO?

Sauli, Sauli, mbona waniudhi? 

Kuna mambo unaweza ukayafanya ukadhani ni sawa machoni pako. Lakini kumbe hujui kama unaleta huzuni kubwa kwa Kristo.

Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo aliitwa Sauli, alikuwa akishindana na mawazo,  na jamii ya watu waliomwabudu Mungu akidhani anashindana na ubaya kumbe anashindana na Kristo mwenyewe.

 mpaka alipokutana  na Kristo mwenyewe njiani alipokuwa anakwenda Dameski..akaambiwa maneno haya..Sauli, Sauli, mbona waniudhi? 

Matendo 9:4-5

[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? 

[5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe. 

Hilo Neno waniudhi, kwenye tafsiri ya asili linamaanisha hasaa “wanitesa”?  Biblia ya kiingereza inaeleza vizuri zaidi inatumia neno “persecutest”…yaani kutesa..

Sasa haya ni Makundi mawili yanayomtesa Kristo.

  1. Wasioamini
  2. Waamini wanao-rudi nyuma

Paulo alikuwa mfano wa wapagani  waliomtesa Kristo, pale alipokuwa anawaburuta watakatifu, anawafunga, anawapinga, na kuwatukana…hakujua kuwa anamtesa Kristo mwenyewe..Leo hii makundi ya watu wanaowapinga watakatifu, wanaoyapinga makanisa ya kweli, wanaowatukana watumishi wa Mungu, wanaowapiga na kuwaua wafahamu kuwa wanamtesa Kristo.

Ikiwa wewe ni mmojawapo kuwa makini, uache mara moja, ni heri utubu leo umpe Yesu maisha yako. Akuokoe.

Lakini  kundi la pili ni wale waamini- waliorudi nyuma. Mtu ambaye ameshaokoka, Halafu anaiacha Njia kwa makusudi anayafanya yale machafu aliyoyaacha nyuma huyo anamtesa Kristo, tena yale mateso ya msalabani kabisa.

Waebrania 6:4-8

[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, 

[5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, 

[6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri. 

[7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; 

[8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa. 

Acha tabia ya kuzoelea dhambi, ukishaokoka ukitenda dhambi, haihesabiki kama kosa kama la wapagani bali uasi.  

Kama Ulimpokea Kristo ili umtese, kuokoka kwako kuna maana gani? Ulishawahi ona mtoto anampiga Baba yake?  Hiyo si laana?

Ndivyo ilivyo kwako unapozini na huku umeokoka, unapokunywa pombe na kufanya anasa.. Tubu haraka sana umrudie Kristo

Penda utakatifu, Ishi maisha matakatifu..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)

Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; 

Print this post

UMEITWA KWANZA KUWA SHAHIDI, SIO MHUBIRI

Matendo 1:8

Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.

Ipo tofauti kati Mhubiri na Shahidi

Kwa lugha rahisi kuna tofauti ya kuhubiri na kushuhudia.
Yesu alituita tuwe mashahidi duniani.. Na hiyo ni kazi ya kila mmoja, Wito wa kumtangaza Yesu, sio wa kimahubiri, bali ni wa kiushuhudiaji.

Mhubiri ni nani?

Mhubiri ni mtu anayesimama na biblia, anayefundisha maandiko, anayefafanua, hadithi mbalimbali na mafunzo katika biblia kisha kutarajia watu kugeuka kwa mafundisho hayo. Huyu anaweza akawa mchungaji, mwinjilisti, mtume, Askofu, shemasi n..k

Shahidi ni nani?

Lakini shahidi ni mtu aliyeona ukweli wa jambo Fulani, kisha akasimama kama mteteaji au mthibitishaji wa ukweli huo.
Ndio kazi tuliyopewa sisi sote kufanya kuhusu Kristo, kuwa mashahidi wake ulimwenguni kote. Wa yale yote aliyotutendea sisi katika maisha yetu. Yaani yale aliyoyasema tukayathibitisha sisi wenyewe kuwa ni kweli katika maisha yetu.

Kwamfano pale aliposema njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha (Mathayo 11:28). Ulipokwenda kwake ukaona mzigo huo umetuliwa, Hivyo tukio hilo huna budi kusimama na kulithibitisha kwa wengine, na wao pia waamini, ili watendewe jambo hilo hilo.

Pale Yesu aliposema tukiamini tukabatizwa, tutapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.(Matendo 2:38) Na wewe sasa umepokea Roho Mtakatifu, umejua ni ukweli, sasa hapo ndipo unapokwenda kuwashuhudia kwa wengine ukweli huo.

Pale ulipoponywa, ulipofunguliwa, ulipoonyeshwa ishara, ulipopewa nguvu ya kushinda dhambi fulani.. Hapo ndipo unapopashuhudia..Na kwa kupitia ushuhuda huo, mwingine atajengwa Imani na kumwamini Yesu kama wewe ulivyoamini hatimaye kuokoka.

Ushuhuda hauhitaji theolojia

Sasa kazi hii haihitaji theolojia ya biblia, haihitaji ukomavu wa kiroho, haihitaji mifungo na maombi, inahitaji tu kufungua kinywa chako na kuanza kueleza uzuri ulioupata ndani ya Kristo, na kwa njia hiyo ndio Mungu atamshawishi mtu na kuokoka.

Mfano wa Paulo – Matendo 9

Ukiwa kama mkristo umeokoka labda tuseme leo, Kumbuka tayari una deni la kuanza kushuhudia uzuri wa Kristo kwa maneno hayo hayo machache uliyonayo kinywani mwako.. Ndicho alichokifanya Paulo baada tu ya kubatizwa..

Matendo 9:
17 Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu.
Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;
19 akala chakula, na kupata nguvu. Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski.
20 Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.
21 Na wote waliosikia wakashangaa, wakasema, Siye huyu aliyewaharibu walioliitia Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuwa amekuja kwa kusudi hilo, awafunge na kuwapeleka kwa wakuu wa makuhani?
22 Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.
23 Hata siku nyingi zilipopita, Wayahudi wakafanya shauri ili wamwue.

Tatizo la kimtazamo juu ya kazi ya injili

Tatizo linatokea pale ambao tunaona kazi ya injili ni ya watu maalumu na ni nzito . Hapana, kumbuka anayeshawishi watu mioyo ni Mungu, sio kwa wingi wa vifungu vya maandiko au kwa uzoefu wa kuhubiri, bali kwa Roho Mtakatifu tu. Maneno mawili, tu yenye kumshuhudia Yesu, yana nguvu ya kugeuza mtu zaidi hata ya maneno elfu ya vifungu vya biblia.

Unapokwenda kushuhudia usifikiri fikiri ni nini utasema, wewe anzia pale ambapo ulitendewa na Yesu ikawa sababu ya wewe kuokoka.. muhadhithie huyo mtu Habari hiyo kwa taratibu. Utashangaa tu, huko huko Katikati Mungu anakupa hekima na kinywa cha kumhubiria mpaka utashangaa hekima hiyo umeitolea wapi. Pengine mtu atakuuliza swali umsaidie, lile jibu linalokuja kwenye kinywa chako liseme, wala usijidharau au usiogope, anayemshawi mtu ni Mungu, yeye kuelewa au kutokuelewa hiyo sio kazi yako ni ya Mungu, uwe tu na ujasiri, kwasababu hakuna Habari yoyote yenye maudhui ya Kristo ndani yake haina matokeo.

Anza sasa kumshuhudia Yesu, Na kwa Pamoja tuujenge ufalme wa Kristo. Anza na marafiki zako, familia, wafanyakazi wenzako, majirani zako kabla ya Kwenda hata mwisho wa nchi.

Mungu akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI

YESU KATIKA KUCHOKA KWAKE.

Enendeni ulimwenguni mwote

Print this post

Na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. 

SWALI: nini maana ya Yohana 17:20

[20]Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.

Ni akina nani hao ambao wataamini Kwasababu ya Neno lao, Bwana Yesu aliotaka kuwaombea?

JIBU: Sura hiyo ya 17 ni sura iliyoelezea kwa kina dua ambayo Bwana Yesu aliifanya kwa mitume wake kwa Baba.

Ambapo aliwaombea mambo kadha wa kadha ikiwemo walindwe katika umoja wa Roho, walindwe na yule mwovu, watakaswe na ile kweli.. Lakini pia Bwana Yesu hakuishia kuwaombea wao tu, bali na wengine ambao mitume wake watawahubiria injili na kuamini baadaye. Na hao pia maombi yake yalikuwa ni yaleyale kwao.

Maana yake ni kuwa watu wote walioamini kwa injili ya mitume walishiriki dua hiyo ya Kristo, Na hao si wengine zaidi ya wale watakatifu wa kanisa la kwanza, hadi sisi tuliopo sasa, hadi na wale watakaokuja baadaye.. sisi wote ni washirika wa dua ile (Yohana 17), kwasababu tumeamini katika injili moja ya mitume..

Ndio sababu kwanini maandiko yanasema Kristo anatuombea…maana yake ni kuwa sasa anatuombea kwa yule Roho Mtakatifu auguaye ndani yetu, lakini pia analituombea alipokuwa duniani ambapo sala hiyo tunaona matokeo yake hata sasa.

Waebrania 7:25

[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.

Hii ni kututhibitishia Kuwa pale tunapomwamini Kristo upo ulinzi usioelezeka unawekwa juu yetu, kiasi kwamba malango ya adui hayawezi Kushinda..kinachohitajika ni kutii tu.

Warumi 8:34

[34]Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.

Je na wewe ni mshirika wa sala hiyo ya Bwana? Kwa kumpokea Bwana Yesu? Kama ni la! Basi nafasi ni sasa mwamini Yesu upokee uzima wa milele.

Lakini pia Bwana anatufundisha namna sahihi ya kuomba..hatupaswi tu kuyaombea yale matunda tunaoyaona..bali hata na yale yatakayokuja baadaye..wale watakaokoka baadaye kwasababu ya Neno letu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.

MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.

“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).

Print this post

Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana

Mariamu alipotokewa na Malaika na kuelezwa habari ya mambo ambayo hayawezekaniki kibinadamu, alionyesha tabia ya kitofauti sana…hakuanza kubisha, Hakuanza kukinzana na kusudi na mpango wa Mungu juu yake, ulio juu ya upeo wa ufahamu wake, kinyume chake aliukubali, tena si Kwa maneno ya juu juu tu, bali kwa ukiri wa utumwa…akasema

“Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema.”

Maana yake ni kuwa ikiwa jambo hilo linanilazimu kulitumikia mimi nitafanya hivyo kama Mtumwa..

Luka 1:34-35,38

[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?

[35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu…

[38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Mariamu ni kielelezo kamili cha mwanamke thabiti wa kikristo, lakini sio tu mwanamke bali bali kwa kanisa la Kristo kwa ujumla.

Utii wa namna hii ndio Bwana anaoutaka kwa watu wote wamchao yeye..

Ijapokuwa kibinadamu haikuwezekana, akijua pia ikishatokea itamletea aibu katika jamii, atakaposadikika amepata ujauzito, kimiujiza hakuna atakaye mwelewa, watasema ni mzinzi, akijua pia kuna majukumu mengine mazito yatafuata..bado alilipokea kusudi la Mungu..lililo juu ya uwezo wake.

Hakukubali kuingia kwenye kosa kama la Musa, kusema mtume mwingine, hakulimbikia kusudi la Mungu kama Yona kukimbilia Tarshishi…bali alilipokea zaidi ya mtumwa.

Si ajabu kwanini Bwana alimpa neema kubwa namna ile…

Ndugu/kaka Bwana anatazama Utayari wako zaidi ya uwezo wako, anatazama utii wako zaidi ya umri wako.

Kila mmoja wetu leo, aliyeamini katika agano jipya ameitwa kufanya MAKUBWA mfano tu wa Mariamu…Hakuna hata mmoja ambaye hajaitwa kwa ajili ya mambo makubwa ya Mungu… kwasababu Mungu ni Mungu wa miujiza na yaliyoshindikana.

Isipokuwa Imani zetu ni haba Kwa Mungu ndio maana hatuoni matokeo makubwa. Kinachohitajika ni kujiachilia tu kwake..kisha kumwacha yeye atende kazi zake ndani yetu.

Haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke, mzee au kijana, una elimu au huna elimu, tajiri au maskini.. kubali kujiachia kama Mariamu katika kusudi lolote la Mungu.. unapoona una nafasi ya kuombea wagonjwa Fanya hivyo, una nafasi ya kuwashuhudia watu mitaani, masokoni, viwanjani fanya hivyo, huko huko Bwana atajifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida. Na Utukufu utamrudia yeye.

Kumbuka tu Mungu amechagua kutumia vyombo Dhaifu kukamilisha kusudi lake timilifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?

JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?

USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!

Print this post

Je Ayubu alitoka kwenye ukoo gani?

Tofauti na Ibrahimu, Isaka na Yakobo ambao chimbiko lao linaonekana katika mtiririko wake tokea Adamu mpaka Nuru hadi wao wenyewe..

Ayubu yeye ni tofauti, kwani kitabu kinaanza kwa kumweleza yeye, na mahali tu alipokuwa ambapo ni Usi.

Usi ni nchi ambayo ilikuwa nje ya Israeli, maeneo ya aidha Arabia, Syria au Yordani..lakini eneo sahihi kwa uhakika halijulikani hivyo  hakuwa na chimbuko lolote la kiyahudi ndani yake.

Maandiko yanamtaja tu kama “Mtu”, wala sio nabii, au kuhani bali mtu aliyekuwa mkamilifu na mwelekezo aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu.

Ayubu 1:1

[1]Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.

kwanini Mungu aruhusu, watu kama hawa ambao hawakuwa katika mtiririko wa kifamilia waandikwe kwenye biblia na zaidi hata wawe na sehemu kubwa katika ufalme wa Mungu…

Ni kuonyesha kuwa Mungu hana upendeleo, yeyote yule amchaye yeye hukubaliwa naye..ndicho Petro alichokiona kwa Kornelio akasema..

Matendo ya Mitume 10:34-35
[34]Petro akafumbua kinywa chake, akasema, Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo;

[35]bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.

Mwanamke Ruthu hakuwa myahudi, lakini Bwana alimkubali.

Hata na wewe kitendo cha kutozaliwa familia ya kikristo au kichungaji haimaanishi kuwa wewe huna neema ya kumtumikia Mungu. Hapana..ukionyesha bidii ile ile wanayoonyesha wengine Mungu hukujalizilisha neema Izidiyo haijalishi ukoo wenu wote ni wa kiganga. Kila mmoja wetu ana nafasi sawa mbele za Mungu, haijalishi kama ni myahudi au mwarabu, kama ni mzungu au mwafika wote kwa Mungu wanayo neema sawa kwasababu yeye haangalii chimbuko wala sura ya mtu.

Je unamcha Mungu?

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.


Print this post

MKUU WA ULIMWENGU AMEKWISHA HUKUMIWA.

Je unafahamu kuwa “Hukumu ya ibilisi” ilishapitishwa?.. Ni muhimu kulifahamu hili ili tusipumbazwe na dhambi.

Awali turejee maandiko..

Yohana 16:11 “kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa”.

Haya ni maneno aliyoyasema Bwana YESU kuhusiana na hukumu ya ibilisi kwamba imeshapita, na hana wakati tena wa kusimama mbele ya kiti cha hukumu kuhumiwa tena, tayari kashahukumiwa..

Fahamu kuwa kosa kubwa lililomfanya ibilisi kutupwa katika ziwa la moto si kumdanganya mwanadamu, wala hakuna adhabu yoyote anayojiongezea katika kumdanganya mwanadamu… kwanini?, kwasababu tayari alishahukumiwa na hiko ndicho kinachomfanya afanye kazi yake kwa bidii sana ya kudanganya watu na kuwapoteza..

Kosa kubwa ibilisi alilolifanya ni KUASI HUKO MBINGUNI, na akapimiwa kipimo cha adhabu ya juu kikubwa cha kumstahili ambacho ni ZIWA LA MOTO (yenye makali kuliko jua) yeye pamoja na malaika walioasi pamoja naye, kwa ufupi ni kwamba ziwa la moto lilikwisha kuwepo kabla hata ya mwanadamu kuumbwa, kwasababu biblia inatuambia hilo kuwa lilitengenezwa kwaajili ya shetani na malaika zake na si mwanadamu.

Mathayo 25:41 “Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, ALIOWEKEWA TAYARI IBILISI NA MALAIKA ZAKE

Umeona?.. moto uliwekwa tayari kwa shetani na malaika zake na si wanadamu, lakini kwasababu wapo wanadamu watakaomfuata ibilisi na kumkataa Mungu, ndipo wataungana na jeshi hilo la ibilisi katika moto huo.

Kwahiyo kamwe tusijidanye kuwa ibilisi ataenda kuulizwa kwanini katupoteza, au kwanini alisababisha wewe uzini, au kwanini alishababisha ajali na watu wakafa, au kwanini aliwatesa watu duniani?..hana hukumu yoyote kwasababu ya kuudanganya ulimwengu, adhabu aliyopewa ni kuasi kule juu, na hiyo adhabu yake ni kubwa sana na ya kutosha..

Siku ile mbele ya kiti cha hukumu ni wanadamu ndio watakaosimamishwa  wenyewe kuhukumiwa kwa kadiri ya matendo yao.

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.

Kwahiyo dada usimlaumu shetani kana kwamba siku ile ataulizwa kwa kukudanganya wewe, yeye hana maswali tena ya kuulizwa, yeye hana hoja tena za kujibu, yeye tayari adhabu yake imeshapitishwa, na hilo ndilo linalomfanya aendelee kufanya uharibifu kwa kasi sana, kwasababu hakuna anachoongeza wala kupunguza katika adhabu yake.

Hata akiua watu elfu kikatili, hakuna kinachoongezeka kwenye adhabu yake kwasababu amekwisha hukumiwa, ule moto ni mkuu sana ibilisi alioandaliwa.

Kwahiyo dada maisha yako ya uchafu yatafakari sana, kaka maisha yako ya uzinzi yatafakari sana, ndugu maisha yako ya uvuguvugu yatafakari sana, usikae umsingizie shetani kana kwamba shetani ataulizwa siku ile kwaajili yako, siku ile utasimama peke yako, nitasimama peke yangu, futa kale kausemi “shetani kanipitia”

Ni heri ukatubu leo na kumpa Yesu maisha yako kabla hizo siku za hatari hazijafika, kabla siku zako za kuishi hazijafika.

Neno la Mungu linasema, mkumbuke muumba wako kabla roho haijamrudia aliyeitoa (yaani Mungu,

Mhubiri 12:7 “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Shetani alitoka wapi?

NIFANYE NINI NIMSHINDE SHETANI?

Nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.

HIZO NDIZO ROHO ZA MASHETANI.

NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?

Print this post

ZINGATIA MOYONI MWAKO.

Jina la Bwana YESU libarikiwe.

Mungu huwa anasema nasi mara nyingi mioyoni mwetu, lakini huwa hatuzingatii na mwisho wake tunaingia katika matatizo.

Matokeo ya kutozingatia sauti ya Mungu ni makubwa, hebu tujifunze kwa mwana mpotevu, aliyeomba urithi kwa Baba yake.

Luka 15:11 “Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; 

12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. 

13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati”. 

14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. 

15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. 

16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. 

17 ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 

18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako”

Nataka tuone huo mstari wa 17, unaosema.. “ALIPOZINGATIA MOYONI MWAKE”.

Maana yake tayari sauti ya MUNGU ilikuwa imeshaanza kumsemesha muda mrefu sana moyoni mwake, kwamba njia anayoiendea sio sahihi, mambo anayoyafanya ni mabaya na hivyo ageuke, lakini hakuwa ANAZINGATIA hiyo sauti.

Na kwa kadiri alivyokuwa anaipuuzia ndivyo mambo yalivyozidi kuwa mabaya, mpaka siku alipoamua kuizingatia.

Inawezekana sauti ya MUNGU inasema nawe moyoni mwako muda mrefu (dhamiri inakushuhudia), usiiendee hiyo njia, usiendelee kufanya hayo unayoyafanya, lakini huzingatii, leo anza kuzingatia sauti ya MUNGU, na geuka acha hiyo njia, mrudie Baba yako, mpe Mungu moyo wako…

Mithali 23:26 “Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu”.

Zingatia sauti inayokuambia UOMBE, zingatia sauti inayokuambia ufunge, Zingatia sauti inayokuambia usome Neno, zingatia sauti inayokuambia Usamehe, zingatia sauti inayokuambia mtumikie MUNGU, wakati mwingine zingatia hata sauti unayokuambia uhame hapo ulipo…

Matokeo ya kuikaidi hiyo sauti ni mabaya, ni kama hayo ya Mwana mpotevu na yale ya Yona.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Print this post

Beliari ni nini? (2Wakorintho 6:15)

Jibu: Turejee…

2Wakorintho 6:15 “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na BELIARI? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?”

Neno Beliari ni muunganiko wa maneno mawili ya kiebrania, ambayo ni “Beliy-ya’al” lenye maana ya “Asiyefaa kitu” na Neno lingine la “Baradhuli”

Sasa hapo kwenye 2Wakorintho 6:15 inaweza kusoma hivi kwa Kiswahili kirahisi… “Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na mtu asiye na maana? ”

Kibiblia mtu asiyefaa kitu ni mtu asije mcha Mungu, asiye na hofu ya Mungu, mwenye roho ya ibilisi ndani yake, kwaufupi ni Baradhuli, mfano wa Beliari/baradhuli ni wale tunaowasoma katika 2Nyakati 13:7..

2Nyakati 13:7 “Wakamkusanyikia watu mabaradhuli, WASIOFAA KITU, waliojitia nguvu juu ya Rehoboamu mwana wa Sulemani, Rehoboamu alipokuwa kijana na wa moyo mwororo, asiweze kuwazuia”.

Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu mabaradhuli wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.

Soma pia Kumbukumbu 13:13, Waamuzi 11:3,  Waamuzi 20:13, 2Samweli 6:20 na Ayubu 11:11.

Na kama maandiko yanavyosema hakuna mapatano au ulinganifu kati ya Kristo na Beliari, maana yake Kristo hawezi kuchanganywa na uchafu, wala hawazi kutembea na Mabeliari au Mabaradhuli, hivyo hatuna budi kujitakasa na uchafu wote wa mwilini na rohoni, ili tutembee na Kristo.

2Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu”.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

WATU WASIOJIZUIA.

HII NDIO TABIA YA WATU WA KEILA, USIIGE

Watu wenye kuvunja maagano ndio watu wa namna gani? (Warumi 1:31)

Kwanini Herode aliwakasirikia watu wa Tiro na Sidoni? (Matendo 12:20)

Print this post

Uchimbueni udongo wa mashamba yenu.

Hosea 10:12

[12]Jipandieni katika haki, vuneni kwa fadhili; uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA, hata atakapokuja na kuwanyeshea haki.

Tunaishi katika majira ambayo kumtafuta Mungu hakupaswi kuwe kwa juu juu tu… kumbuka Neno la Mungu linatufananisha sisi na wakulima wapandao na wenye malengo ya kuvuna kwa vile tuvipandavyo…

Na sikuzote mkulima yoyote labda tuseme yule wa nafaka hatupi mbegu zake tu juu ya ardhi akitarajia ziote, bali utamkuta Na jembe, tena lile imara analikita chini ardhini kwa nguvu, huku jasho likimtoka.

Kimsingi kupiga jembe chini ndio kazi aliyonayo mkulima, haijalishi ardhi itakuwa ngumu kiasi gani hana budi kuichimba kwa nguvu, ili mbegu izame aone matokeo… vinginevyo hatavuna chochote.

Bwana anasema…

Uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA,

Kumtafuta BWANA…ni kuchimba chini…

Yaani kama ni maombi basi ni Maombi ya masafa marefu sio yale mfano wa kuombea chai ya asubuhi, kama ni kusoma na kujifunza Neno, basi ni kufanya hivyo vya kutosha kila siku sio kuamka na mstari mmoja, au kusubiri Tu kuhubiriwa YouTube halafu basi..

Kama ni ibada, kujifunza Kudumu uweponi mwa Mungu kwa nyakati ndefu…huko ndiko kuchimba chini ambako Bwana anakutaka…

Tusipende mambo ya juu juu, yatatugharimu vibaya sana, na tutajikuta tunapata hasara ya mbegu zetu kuliwa na ndege..

Fahamu kuwa Yesu amekaribia kurudi.. Je umezama Kweli ndani yake? Je unamtafuta kwa bidii, je umejiweka tayari kumpokea? Kama ni hapana basi anza sasa..

Kwasababu mbinguni hakitaingia kinyonge.

Chimba ardhi yako.

Neema ya Bwana akufunike.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Print this post

Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)

Swali: Kwanini Nabii Yeremia ailaani siku aliyozaliwa?, na je ni sahihi kulaani siku tulizozaliwa?

Jibu: Turejee maandiko hayo kuanzia ule mstari wa 14 hadi wa 17..

Yeremia 20:14 “Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu.

15 Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha.

16 Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri;

17 kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito”.

Utaona sababu kuu ya Nabii Yeremia kuzungumza maneno yale ni “mateso aliyokuwa anayapitia katika huduma yake”.. kwani alipitia mapigo na  vifungo vingi na aliwindwa kila mahali kwasababu ya maneno ya Mungu (Soma Yeremia 20:1-2, Yeremia 37:15-16, Yeremia 38:6, Yeremia 15:5)…kama mstari wa 18 unavyoelezea.

“..18 Nalitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?”

Na si tu Nabii Yeremia aliyeilaani siku yake aliyozaliwa, bali tunaona pia Ayubu naye alisema hayo hayo..

Ayubu 3:1 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake.

2 Ayubu akajibu, na kusema;

3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.

4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.

5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe.

6 Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi”.

Sasa swali ni je! Walifanya sahihi kuzilaani siku zao?, na sisi je tunapopitia dhiki zilizozidi ni sahihi kuzilaani siku tulizozaliwa na watu waliotuzaa, na matumbo yaliyotuzaa?.

Jibu ni La! Si sahihi kabisa kuzilaani siku tulizozaliwa, wala kulaani matumbo yaliyotuzaa, hata tupitie dhiki kiasi gani?..

Nabii Yeremia na Ayubu walisema maneno yale kwakuwa yalionekana kama ni mambo mapya kwao, kwamba inawezekanaje uwe Nabii uliyetumwa na Mungu, unayesema maneno ya kweli, au inakuwaje uwe mtu wa Mungu, mwelekevu na mkamilifu halafu unakubwa na mambo mazito kama yale?.

Kwahiyo yale yaliyowapata yalikuwa ni mambo mapya kwao, hawakuwa na mifano ya waliowatangulia waliopitia kama hayo katika kiwango hiko, hivyo walisema yale kwa udhaifu wa kibinadamu, lakini hawakuwa sahihi, ndio maana baadaye utaona Ayubu anakuja kutubu, kwa kusema “amesema maneno yazidiyo”

Ayubu 42:3 “Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? Kwa maana, nimesema maneno nisiyoyafahamu, Mambo ya ajabu ya kunishinda mimi, nisiyoyajua.

4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.

5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.

6 Kwasababu hiyo NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU Katika mavumbi na majivu”.

Umeona? Hapa Ayubu anakuja kutubia maneno yake, baada ya kumjua Mungu zaidi, na ni hivyo ivyo Yeremia alikuja kuona makosa yake, soma Yeremia 15:18-19.

Na hatuoni tena Ayubu baada ya kuponywa msiba wake wala Yeremia baada ya kustahereshwa wakirudia kusema hayo maneno, hivyo wao walipitishwa katika mapito hayo ili iwe darasa kwetu sisi, kwamba ukiwa mtumishi wa Mungu, au mtu mkamilifu mbele za MUNGU, sio tiketi ya kutopitia majaribu!, LA! Majaribu yanawapata watu wote (wakamilifu na wasio wakamilifu), hivyo hatupaswi kulalamika wala kulaani yanapokuja bali kuomba na kumngoja BWANA.

Na hiyo ndio sababu ya Bwana wetu YESU kuwatahadharisha wanafunzi wake, na hivyo anatutahadharisha hata sasa kwamba tutakapopitia dhiki kwaajili ya Imani tunapaswa tuwe wapole kama hua na wenye busara kama nyoka.

Mathayo 10:16 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.

17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba si sahihi kuzilaani siku za kuzaliwa au siku nyingine yoyote, wakati wote tunapaswa tuwe watu wenye busara, na watulivu..hakuna faida yoyote katika kunung’unika wala kulalamika.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Laana ya torati maana yake ni nini?

JE NI LAANA KULELEWA NA BABA AU MAMA WA KAMBO?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

NAKUJUA JINA LAKO!

Print this post