Category Archive Uncategorized @sw-tz

LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.

1 Samweli 30:6

[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake. 

Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.

Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe, 

Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe, 

Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..

Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.

Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.  

Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu. 

Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.

Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.

Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

KATIKA UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA

1Wakorintho 14:20 “Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika UOVU MGEUZWE WATOTO WACHANGA, bali katika akili zenu mkawe watu wazima”.

Biblia inatufundisha kuwa “Watu wazima” katika Akili, lakini tuwe watoto wachanga katika uovu, sasa ni nini maana ya kuwa watoto wachanga katika uovu?

Tukiwatazama watoto wachanga tunajifunza mengi, lakini jambo kuu tunaloweza kujifunza ni “Ukamilifu” watoto wadogo wanyonyao wanakuwa hawana hatia, sio waongo, si waasi, si walevi, si wazinzi, si wauaji, si wadhalimu, si wahuni, si waasi na mambo mengine maovu hayapo kwao, Na ndio maana Bwana YESU alisema kuwa ni lazima na sisi tugeuzwe kitabia na kuwa kama watoto wachanga..

Mathayo 18:3 “akasema, Amin, nawaambia, MSIPOONGOKA NA KUWA KAMA VITOTO, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.

4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni”.

Lakini haishii tu kusema tuwe “watoto katika uovu” bali pia tuwe “watu wazima katika akili”.. Mtu mzima katika akili ni Yule aliyeyabatilisha mambo mabaya, ya kale… mtoto anayechezea matope na kupenda kula peremende kila siku anapokuwa mtu mzima, ndipo anapoyabatilisha mambo ya kitoto na kuwa mtu mzima (hapo tunasema ameimarika kiakili).

Vile vile mtu ambaye alikuwa katika machafu ya dunia (ambayo ndio mfano wa uchafu wote wa utotoni), anapompokea YESU basi ya kale yanakuwa yamepita na sasa amekuwa kiumbe kipya.

2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Lakini mtu aliye nje ya imani, na kuendelea na machafu yote ya dunia, kibiblia anakuwa hana akili, na anafananishwa na mnyama.

Zaburi 49:20 “Mwanadamu mwenye heshima, IWAPO HANA AKILI, Amefanana na wanyama wapoteao”.

Ndio kwani biblia imesema mtu aziniye hana akili kabisa (soma Mithali 6:32, Mithali 7:7), na mtu anayemdharau mwenzake pia hana akili (Mithali 11:12).

Kwahiyo ni lazima tuache mambo ya kale, na kumgeukia Kristo, ili tupate akili, na mwenye uwezo wa kutubadilisha ni YESU tu peke yake, lakini wanadamu wengine wote hawawezi kutusaidia kitu, je umempokea huyu YESU?.. Je unauhakika Kristo akija leo unakwenda naye?.

Kama bado haujampokea YESU unangoja nini?.. maisha ya dhambi na anasa yamekusaidia nini?.. je ukifa leo utaenda wapi?

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?

Print this post

UFANYE BIDII KATIKA KUSOMA.

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika KUSOMA, Kuonya na Kufundisha”.

Wakristo wengi hawapendi “KUSOMA” wanapenda “kusomewa”.. hawapendi “Kujifunza” wanapenda “Kufundishwa” hawapendi “Kujiaminisha” wanapendwa “kuaminishwa”… Kwaufupi wanapenda kutafuniwa na kusaidiwa kila kitu na wanadamu.

Ni kweli MUNGU anatumia watu, lakini “hategemei watu”.. Ukitegemea kusaidiwa kila kitu katika mambo ya rohoni, imani yako itakuwa imesimama juu ya watu, kiasi kwamba Yule mtu unayemtegemea akisomee maandiko, au akufundishe akirudi nyuma wewe nawe ni lazima utarudi nyuma tu.

Akibadilika wewe nawe utabadilika tu, akifa kiroho wewe nawe huna siku nyingi za kuwa hai kiroho.. iko hivyo, kwasababu imani  yako ipo kwake hata kama hukiri hilo.

Lakini Biblia inatufundisha kila mtu “KUSOMA” tena kwa bidii.. sio kusoma Geografia, au hisabati au siasa.. bali KUSOMA NENO LA MUNGU.

ZIFUATAZO NI FAIDA CHACHE ZA KUSOMA NENO LA MUNGU, badala ya kusubiri kufundishwa.

   1. UNAMPA ROHO MTAKATIFU NAFASI YA KUSEMA NAWE.

Unaposoma Biblia binafsi, katika utulivu… kunakuwa kuna “tafakari” za kiMungu zinapita ndani ya kichwa chako, hizo tafakari nyingi zinakuwa ni sauti ya Roho Mtakatifu, kukufundisha kwa kile unachokisoma.

Sasa unaposikiliza mhubiri akihubiri, yeye anazunguza kile Roho alichokiweka ndani yake, na anaposema hawezi kurudia mara mbili, alichokisema kinakuwa kimepita, hivyo huna nafasi ya kutosha wewe kukichakata kile ulichokipokea, labda upate nafasi ya kurudia kusikiliza tena mafundisho yake katika utulivu..

Lakini unapokuwa msomaji wa Biblia, unayo nafasi ya kwenda kituo baada ya kituo huna haraka hivyo inakuwa unampa nafasi nzuri Roho Mtakatifu kusema nawe.

   2. UNAPATA UHAKIKA WA MAMBO.

Ukiwa msomaji wa Biblia binafsi, unakuwa unapata uhakika wa mambo uliyowahi kuyasikia au kufundiswa, kama ni ya kweli au si  ya kweli, lakini usipokuwa msomaji ni ngumu kuhakiki mambo.

   3. UWEZO WA KUUNGANISHA MAANDIKO UNAONGEZEKA.

Unapokuwa msomaji mzuri wa Neno ule uwezo wa kuyaunganisha maandiko, kwamba andiko hili linaladnana na andiko lingine, unapanda!.. hiyo itakusaidia sana kumwelewa MUNGU.

   4. HAMASA YA KUMJUA MUNGU ZAIDI INAONGEZEKA.

Unaposoma mwenyewe Biblia zaidi ya kufundishwa, ile hamasa ya kutaka kumjua MUNGU zaidi inaongezeka, kila mstari unaoumaliza unakupa hamasa ya kuendelea mbele kusoma mwingine, na hiyo ni faida kubwa kwani utajikuta inaipenda Biblia na inakuwa ni kitabu chako.

    5. UNAONGEZA UZOEFU WA KUIJUA BIBLIA.

Unapokuwa msomaji wa Neno uzoefu wako wa kulisoma Neno unaongezeka, ninaposema uzoefu, simaanishi kulizoelea Neno, La!.. bali ile namna ya kujua mpangilio mzuri wa Maandiko na mistari unapanda, hiyo inakuongezea urahisi wa kujifunza Neno la kulielewa.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

WOKOVU UKIHARAKISHA USIUZUIE.

Wokovu ni kama farasi ambaye ana uwezo wa kusafiri kwa mwendo wa kasi sana au kwa mwendo wa taratibu sana, inategemea tu, nia ya mwendeshaji.

Halikadhalika Ikiwa wewe ni mshuhudiaji,(mhubiri wa injili) ni vema kufahamu tabia hizi, mara nyingi wokovu mpaka ukamilike ndani ya mtu, yaani kukubali toba, kuamini, kikiri, kubatizwa, kujazwa Roho, huweza kuchukua muda fulani wa wastani au mrefu kidogo, ambao huusisha kushawishi, kufuatilia, kufundisha madarasa mbalimbali imani, ya ubatizo na Roho Mtakatifu, n.k. ndipo aamini na kukamilishwa.

Lakini tembea pia ukijua kuwa si wakati wote hili litakuwa hivyo…

Zipo nyakati Mungu anabadili gia, atataka kukamilisha mambo yote hata kwa siku moja tu…yaani kumwokoa, kumbatiza na leo leo kumjaza Roho…Ukiona jambo hilo kamwe usijaribu kupunguza mwendo huo..Ni Mungu kaamua kuongeza kasi ya usafiri wake.

Je hili lipo kibiblia?

Ndio…wakati fulani Paulo na Sila walikamatwa na kutupwa gerezani, wakiwa kule usiku ule tunaona walianza kumwimbia Mungu na kumsifu sana…na mara vifungo vya gereza vikafunguka..yule askari msimamizi alipoona tukio lile aliogopa sana na kutetemeka…akasema nifanye nini ili niokoke? Wakawaambia wamwamini Bwana Yesu utaokoka. Na usiku ule ule walitubu, na kubatizwa nyumba yote, na kisha wakajazwa furaha ya Roho Mtakatifu yeye na nyumba yake yote..

Yaani kitendo cha usiku mmoja…familia nzima inaokoka, inabatizwa, inapokea tunda la Roho..

Matendo ya Mitume 16:27-34

[27]Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia. 

[28]Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. 

[29]Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; 

[30]kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? 

[31]Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. 

[32]Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake. 

[33]Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo. 

[34]Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu. 

Kama ni mchakato, wengine humaliza hata wiki au miezi mpaka nyumba nzima kuamini na kubatizwa, ..lakini hapa ilikuwa ni masaa machache sana…tena ya usiku..

Utaona jambo kama hili lilijirudia kwa Kornelio..Petro alipoenda kwake, hata kabla hajamaliza mazungumzo yake, akidhani kuwa inahitaji madarasa marefu, inahitaji vyuo vya kuufafanua msalaba…pale pale katikati ya mazungumzo watu wakashukiwa na Roho Mtakatifu wakajazwa, wakapewa ile hatua ya mwisho kabisa ya wokovu ndipo wakaenda kubatizwa…(Matendo 10).

Mambo ambayo yamkini yangechukua madarasa ya muda na maombezi ya kuwekewa mikono ya kipindi kirefu..

 Na yule mkushi aliyekutana na Filipo gaza naye vivyo hivyo hakusubiri kwanza alike kushi, pale pale njiani alibatizwa.

Matendo ya Mitume 8:36-39

[36]Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe? 

[37]Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.] 

[38]Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza. 

[39]Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi. 

Vivyo hivyo, fahamu kuwa kuna nyakati Mungu anaisukuma mioyo ya watu kwa nguvu sana..tena sana kiasi kwamba mioyo yao hufunguka na kutamani kukamilishwa katika yote…

Ukiona hivyo, msaidie haraka, usifikiri kwamba inahitaji maarifa mengi ili mtu kuokolewa…bali moyo uliowazi..hilo tu..

Pengine wewe ni kiongozi..unaona mtu ameamini…usingoje ratiba za mwisho wa mwaka za ubatizo kanisa kwako…ndipo ambatize huyo mtu, angalia tu mwitikio wake…Ndio lipo pia kundi lingine ambalo litahitaji mafundisho kwanza…kutokana na viwango vyao vya upokeaji, ila usilisahau hili pia.

Jifunze kwenda na kasi zote za injili.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

Biblia inaposema watu wakali hushika mali sikuzote, ina maana gani? (Mithali 11:16)

Print this post

SHUKURU, ITA NA JULISHA.

Labda unaweza kujiuliza maana yake nini maneno haya, tusome Zab.105:1

Zaburi 105:1 “Haleluya. Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake, Wajulisheni watu matendo yake”.

“Kumshukuru Mungu” na “Kuliitia jina lake” na “ Kuwajulisha watu matendo yake” Ni mambo ya msingi sana kuyafanya.

Haya ni mambo makuu matatu (03) yaliyo ya muhimu na msingi sana, hebu tuyasome tena mahali pengine katika maandiko..

Isaya 12:4 “Na katika siku hiyo mtasema, Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake; Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, Litajeni jina lake kuwa limetukuka”.

Soma pia 1Nyakati 16:8.

   1. MSHUKURU MUNGU

Kumshukuru Mungu ni agizo la Mungu!.. Kumshukuru Mungu kwaajili ya uzima aliokupa, pumzi, ulinzi, Rehema, Fadhili na mambo mengine yote ni jambo linalompendeza MUNGU sana.

     2. LIITE JINA LA YESU

Vivyo hivyo, KULIITIA JINA LA MUNGU ni agizo!.. Tunapopitia vitisho, majaribu au mapito mengine yoyote ni lazima tuliitie jina la Mungu wetu, kwasababu hata waabuduo miungu huita majina ya miungu yao, ndivyo maandiko yanavyotuonesha..

1 Wafalme 18:25 “Eliya akawaambia manabii wa Baali, Jichagulieni ng’ombe mmoja, mkamtengeze kwanza; maana ninyi ndio wengi; mkaliitie jina la mungu wenu, wala msitie moto chini”

Nasi tunapaswa tuliitie kila wakati jina la YESU, ambalo ndilo pekee lituokoalo ( Matendo 4:12).

Watu wa MUNGU tunapoliita jina la YESU, vifungo vinakatika na mbingu na nchi zinatetemeka, tangu Siku za Sethi mpaka leo jina la MUNGU lina nguvu ile ile ya kuokoa.

Mwanzo 4:26 “Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la BWANA”.

Soma pia Mwanzo 12:8, Mwanzo 13:4, Mwanzo 21:33,  Mwanzo 26:25,  Utaona ilikuwa ni desturi ya watu wote wa Mungu enzi za Biblia.

Na tunapoliitia jina la Bwana, anaitika.

Zaburi 99:6 “Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake, Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake, Walipomwita Bwana aliwaitikia”

Lakini pia kama hatujamaanisha kumfuata Mungu na tukaliitia jina lake tunajiletea matatizo badala ya msaada, soma ile habari ya wana  watano wa Skewa utaelewa vizuri. (Matendo 19:13-15).

Kwahiyo ili tujidhi vigezo vya kuliita jina la MUNGU, ni lazima tumaanishe kumfuata MUNGU na kuacha dhambi (huo ndio Msingi).

2 Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu”.

         3.WAJULISHE WATU MATENDO YA MUNGU.

Kumshuhudia Mungu mbele za watu, kwa kazi zake ni nguzo ya tatu ya msingi…

Na ushuhuda wa kwanza tunaopaswa kushuhudia ni kufufuka kwa YESU, Hilo ni tendo kuu la kwanza Mungu alilolifanya, kumfufua YESU kutoka katika mautini… na kwa kupitia huyo tunapata ondoleo la dhambi.

Shuhuda nyingine kama kuponywa magonjwa, kuokoka na ajali na majanga na kubarikiwa zinasimama kuthibitisha ushuhuda mmoja mkuu wa kufufuka kwa YESU na ondoleo la dhambi kwa wote wanaomwamini.

1 Yohana 5:11 “Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe”.

Je wewe uliyempokea YESU kama mwokozi, je unafanya hayo?…je Una Desturi ya kumshukuru MUNGU kila wakati, au mambo yote anayokutendea wewe unaona ni kawaida tu?.

Na je una desturi ya kuliitia jina la MUNGU, kama huna desturi hiyo anza sasa utaona matokeo yake..

Na mwisho unayo desturi ya kushuhudia matendo makuu ya MUNGU?..Kama bado anza leo.

Kwa mambo hayo matatu, tutaweza kuangusha Ngome na kumpendeza MUNGU.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

WATU HAWA WALIOUPINDUA ULIMWENGU WAMEFIKA HUKU NAKO

Kama tunavyofahamu katika maandiko Mitume walipofika mji wa Thesalonike kwa ajili ya injili, na kukutana na wenyeji wa mji ule, na kusikia walichokihubiri maandiko yanatuambia walipiga kelele sana na kusema maneno haya;

“Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako”

Matendo ya Mitume 17:6

[6]na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Ulishawahi kutafakari kwa ukaribu maneno hayo walichokimaanisha?

Wanasema;

Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, 

Maana yake ni kuwa ulimwengu na wao, ni kama vitu viwili tofauti…

Wamefika na huku pia….yaani wameshaushinda ulimwengu wanakuja na huko kwao kumalizia walichokifanya kule..

Hii ikiwa na maana…mitume walishapata ushindi kabla hata ya kufika maeneo yote…

Kuna mahali pajulikanapo ulimwenguni ambapo tayari walishapashinda.

Sasa huo ulimwengu ni upi?

Chukulia mfano wa dunia ya sasa.. kuna usemi wasemao nchi za Afrika ni dunia ya tatu.. ijapokuwa wote tupo kwenye sayari moja, ujulikano dunia, lakini uhalisia dunia zipo tatu…Zile nchi zilizoendelea sana…Kama vile Marekani, urusi, China, ufaransa..ni dunia ya kwanza… na zile zilizo katika uchumi wa kati ni dunia ya pili na hizi maskini ni dunia ya tatu..

Sasa ikitokea mtu akayapiga hayo mataifa makubwa na kuyateka, maana yake huyo mtu ameiteka dunia, ameipindua dunia…..hata kama hajapigana na haya mengine madogo..lakini ikiwa nguvu zake zimewashinda wale basi hawa wengine ni maji tu.

Vivyo hivyo waamini wa wakati ule walionekana, wanamapinduzi wakubwa sana..kwasababu ushindi wao ulianzia kwenye vichwa.

Sasa huu ulimwengu ni upi?

JIBU: Ulimwengu wa Roho.

Zamani zile dini zilijulikana kama msingi mikubwa sana inayosukuma mielekeo ya mataifa.. hivyo Kristo alipokuja aliweza kuvunja misingi ya imani potofu na dhaifu kuanzia pale pale Israeli mpaka miisho ya dunia. Alileta Nuru duniani ambayo giza lolote halikuweza kulishinda..

Yohana 1:4-5

[4]Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 

[5]Nayo nuru yang’aa gizani, wala giza halikuiweza. 

Ndio maana kipindi cha injili utaona Wayahudi wengi waliokoka, wapagani wengi wakaacha miungu yao..wakaichoma moto, utaona hata kule Efeso mungu mke aliyeabudiwa ulimwenguni kote (Matendo 19:27), mitume walipofika habari yake ikaishia pale pale, tofauti na zamani manabii walishindana sana na mabaali lakini hawakuweza kuyashinda..kwasababu hakukuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mkuu wa ulimwengu huu(shetani)

Yohana 16:11

[11]kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa. 

Hivyo ulimwengu wa roho uligeuzwa juu chini, mapepo yaliwakimbia wengi, watu walifunguliwa kwenye vifungo vya giza..makaburi waliwaachia wafu..kila siku watu waliongozeka kumjua Mungu…na kuachana na dhambi.

Matendo 19:19-20

[19]Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. 

[20]Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. 

Huu ndio ulimwengu sugu uliopata tiba…ulimwengu wa giza, kama kichwa cha mifumo yote mibovu ya dunia…uliwekwa chini…

Hivyo wale watu walipoona imani za watu zinageuzwa kwa kasi hata za maakida wakubwa,(Matendo 13:7-12) majemedari, watu wenye vyeo, wake kwa waume, nao pia wanaigeukia imani..wakatambua ya kuwa kila kitu kimekwisha sasa, sisi ni masalia..tu.

Walijiona kama mapanzi, ni sawa na wana wa Israeli walipoweza kuliangusha taifa la Misri, hata kabla ya kufika Yeriko, Wale watu wenyewe walishajiona kama mapanzi..Kwasababu kichwa cha ulimwengu kimeshaangushwa.

Vivyo hivyo hata sasa, ni lazima tujue kuwa sisi tuliomwamini Yesu…tayari tumeshaupindua ulimwengu kwa Injili iliyokwisha fika kuzimu kwenye kiti cha enzi wa shetani…

Hakuna chenye nguvu ya kutuzuia sisi tena, sisi ni watawala wa dunia.

Wanasiasi, hawawezi kutuzuia, wanadamu hawawezi kutusimamisha..wao ni kama mapanzi tu kwetu…

Hatuna budi kuuinua ujasiri wetu wote…tufikie mataifa yote kuhubiri injili kwasababu ulimwengu tayari tumeshaupindua…hatuhitaji kwenda tena kuupindua..sisi ni kumalizia tu masalia. Unasubiri nini usiamke kuihubiri injili? Amka sasa…

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NI INJILI GANI UNAHUBIRI?

PELEKA INJILI KOTE KOTE KWA SADAKA YAKO.

KWANINI KILA MWAMINI ANAPASWA AWE MHUBIRI WA INJILI

Print this post

MPE MUNGU MAJUTO YAKO.

Kila mwanadamu maadamu amezaliwa na kuishi duniani, ndani yake lazima kuna kiwango tu cha majuto..

Wengine wana majuto makubwa sana, wengine kiasi.

Majuto ni hali ya kuhuzunishwa na matokeo ya machaguzi au maamuzi yaliyofanyika katika maisha.

Kwamfano kijana anaweza kuchagua kukatisha masomo kisha aende mtaani, kuuza peremende, sasa hayo ni maamuzi yake, lakini baadaye anapoona haoni matokeo makubwa, kinyume chake anawaona wenzake waliosoma wamepiga hatua kubwa anaanza kuingiwa na huzuni ya kujishitaki mwenyewe, sasa hayo ndio majuto.

Mwingine amechagua kuishi na mtu bila kufunga naye ndoa, hatimaye akazalishwa, watoto wengi na kuachwa..baadaye umri umeenda anataka kuoelewa, inakuwa shida…anaingiwa na majuto.

Mwingine amepoteza miaka mingi duniani kumtumikia shetani, sasa ameshakuwa mzee anajisikitikiza miaka yake ya ujana aliyoipoteza yenye nguvu alikuwa wapi asimtumikie Mungu…

Majuto yapo ya namna nyingi, na kila mtu kwa sehemu yake anayo majuto fulani, haijalishi unaishi wapi, au umefanikiwa vipi…kuna mahali ulikosea na yakaingia..

Kimsingi majuto sio dhambi, ni hali ya ki-Mungu kabisa ambayo mwanadamu ameumbiwa ndani yake..

Lakini ni vema kujua namna ya kuyaweka mahali pake..kwasababu yasipoweza kutenganishwa ipasavyo hupelekea hasara kubwa mno ndani ya maisha ya mtu.

Katika biblia kulikuwa na watu wawili ambao walihuzunishwa na maamuzi walillyoyafanya …mmoja ni Petro, mwingine ni Yuda.

 Yuda alihuzunishwa lakini huzuni yake ilimpelekea kujinyonga…Petro alihuzunishwa lakini huzuni yake ilipelekea kulilia msaada wa Mungu..(badiliko)

Petro aliruhusu majuto yake yabebwe na Mungu, Yuda aliruhusu yabebwe na shetani.

Lakini majuto yalikuwa yale yale…Yuda hakukosea kujuta hadi kurudisha pesa

2 Wakorintho 7:8-11

[8]Kwa sababu, ijapokuwa naliwahuzunisha kwa waraka ule, sijuti; hata ikiwa nalijuta, naona ya kwamba waraka ule uliwahuzunisha, ingawa ni kwa kitambo tu. 

[9]Sasa nafurahi, si kwa sababu ya ninyi kuhuzunishwa, bali kwa sababu mlihuzunishwa, hata mkatubu. Maana mlihuzunishwa kwa jinsi ya Mungu, ili msipate hasara kwa tendo letu katika neno lo lote. 

[10]Maana huzuni iliyo kwa jinsi ya Mungu hufanya toba liletalo wokovu lisilo na majuto; bali huzuni ya dunia hufanya mauti. 

[11]Maana, angalieni, kuhuzunishwa kuko huko kwa jinsi ya Mungu kulitenda bidii kama nini ndani yenu; naam, na kujitetea, naam, na kukasirika, naam, na hofu, naam, na shauku, naam, na kujitahidi, naam, na kisasi! Kwa kila njia mmejionyesha wenyewe kuwa safi katika jambo hilo. 

Umeona Majuto ya ki-Mungu huleta toba.. lakini majuto ya shetani hupelekea mauti..

Ukishaanza kujiona kama wewe huwezi tena, Mungu kakuacha, hufai, huna maana, hustahili, ujue shetani yupo nyuma ya juto hilo, ambalo anataka kukusababishia usiinuke tena, ujitenge, ujiue, uache kwenda kanisani, aache maombi, uache kumtafuta Mungu, uache uchungaji …

Kinyume chake unapokosea jione kama ulikuwa unapitishwa katika funzo ambalo sasa unapewa nafasi nyingine usiitmie vibaya…

Watu wengi, unaowaona wamekata tamaa, wamepoa, hawana mabadiliko tena, wamejitenga, lakini hapo zamani walikuwa vizuri, wana mashaka na hofu ya ndani kwa ndani, asilimia kubwa ni majuto mabaya yanawasonga ndani yao.

Daudi alipoanguka katika dhambi ya uzinzi, alimrudia Bwana kwelikweli, ijapokuwa ilimgharimu pakubwa…hakwenda kujificha na uso wa Mungu kama Adamu.

Lakini ya ki-Mungu huturudisha kumtazama Mungu…Rudi umwangalie Mungu wako kisha chukua hatua nyingine, kwani hiyo huwa na nguvu na matokeo ya haraka zaidi ya mwanzo.

Petro baada ya pale alikuwa na ujasiri mkubwa wa kumshuhudia Kristo, zaidi ya mitume wengine wote, ikiwa umefeli mahali fulani embu amka tena kwa nguvu, usikubali kunyong’onyea kama Yuda na mfalme Sauli ambaye alijiua..

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

KUWA MWOMBOLEZAJI.

NI KIPI KINAKULEWESHA?

TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA

Print this post

Hasimu ni nani? (Isaya 50:8).

Jibu: Turejee..

Isaya 50:8 “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye HASIMU yangu? Na anikaribie basi”.

“Hasimu” maana yake ni “mpinzani”…Kwahiyo andiko hilo kwa lugha nyingine laweza kusomeka hivi…

 Isaya 50:8 “Yeye anipatiaye haki yangu yu karibu; ni nani atakayeshindana nami? Na tusimame pamoja; ni nani aliye MPINZANI WANGU? Na anikaribie basi”.

Andiko hili linaelezea nguvu wanayotembea nayo watu wa MUNGU, kwamba wanao ulinzi mkubwa zaidi ya wote na wanao utetezi mkubwa zaidi ya wenngine wote, kwasababu mbingu inawatetea daima.

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?”.

Je na wewe umezungukwa na Mahasimu? Je mtetezi wako ni nani katikati ya hao?.

Ni heri Mtetezi wako akawa YESU leo, kwasababu wanadamu wala mashetani hayawezi kukutetea wakati wa matatizo bali yatakuwa Mahasimu wako tu siku zote.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

NI KIPI KINAKULEWESHA?.

Je Mkristo, anapaswa KULEWA?..

Jibu ni NDIO! Anapaswa alewe lakini si kwa MVINYO (yaani kwa pombe)… bali kwa ROHO MTAKATIFU.

Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”

Roho Mtakatifu ni Kilevi cha Mkristo, ni lazima sote tujae Roho Mtakatifu katika kiwango cha KULEWA KABISA!!.

Ndio maana ile siku ya Pentekoste watu walipopokea ujazo Roho Mtakatifu na kuanza kunena kwa lugha mpya walisomeka kama “Walevi wa mvinyo mpya” mbele ya waliowasikia.

Matendo 2:12 “Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?

13 Wengine walidhihaki, wakisema, WAMELEWA KWA MVINYO MPYA.

14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.

15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;

16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,

17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote ROHO YANGU, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.

18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake ROHO YANGU, NAO WATATABIRI”.

Umeona?…Mitume walipopokea ujazo wa Roho Mtakatifu walionekana ni walevi.

Ni kweli kabisa walilewa lakini si kwa mvinyo bali Roho Mtakatifu.

Na maandiko yanazidi kutuonyesha kuwa Roho Mtakatifu, TUNAMNYWA!!.. Ni kinywaji tunachokinywa, na kila kilevi lakini si cha kidunia bali cha kimbinguni.

1 Wakorintho 12:13 “Kwa maana katika ROHO MMOJA  sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote TULINYWESHWA ROHO MMOJA”.

Sasa sifa za Mlevi ni zipi?

     1. UJASIRI.

Mlevi anapolewa huwa kiwango chake cha ujasiri kinapanda..utaona mtu akishakunywa basi atakuwa anaongea neno lolote linakuja kinywani mwake bila haya, hiyo ni sifa mojawapo ya mlevi.

Na halikadhalika mtu aliyejazwa Roho Mtakatifu, huwa anakuwa ana ujasiri mkuu kuzungumza lolote kuhusu ufalme wa MUNGU aoni aibu, ndivyo tunavyosoma pia katika maandiko..

Matendo 4:31 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri”

Hivyo kama umelewa na Roho Mtakatifu basi utaona ujasiri wa kuzungumza habari za Ufalme wa MUNGU pia unaongezeka, ujasiri wa kukemea dhambi unaongezeka, ujasiri wa kusifia mema pia unaongezeka.

      2. GANZI

Mtu mlevi, akishalewa anaweza kulala popote hata mtaroni, wala hasikii baridi na wala wadudu kama mbu hawamsogelei, kwanini?..ni kwasababu mwili wake umepata ganzi.

Hali kadhalika mtu aliyejawa na Roho Mtakatifu huwa anapata ganzi katika utumishi, maana yake mazingira yoyote anaweza kwenda katika utumishi wake bali kuona shida mfano wa mtumishi wa Mhngu Mtume Paulo.

2 Wakorintho 11:23 “Wao ni wahudumu wa Kristo? (Nanena kiwazimu), mimi ni zaidi; katika taabu kuzidi sana; katika vifungo kuzidi sana; katika mapigo kupita kiasi; katika mauti mara nyingi.

24 Kwa Wayahudi mara tano nalipata mapigo arobaini kasoro moja.

25 Mara tatu nalipigwa kwa bakora; mara moja nalipigwa kwa mawe; mara tatu nalivunjikiwa jahazi; kuchwa kucha nimepata kukaa kilindini;

26 katika kusafiri mara nyingi; hatari za mito; hatari za wanyang’anyi; hatari kwa taifa langu; hatari kwa mataifa mengine; hatari za mjini; hatari za jangwani; hatari za baharini; hatari kwa ndugu za uongo;

27 katika taabu na masumbufu; katika kukesha mara nyingi; katika njaa na kiu; katika kufunga mara nyingi; katika baridi na kuwa uchi”.

Nasi ni lazima tufe ganzi katika mwili wakati wa kuhubiri injili.

2 Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.

     3.KUNYWA KILA SIKU.

Mlevi halisi haiwezi kupita wiki bila kulewa, atahisi kuumwa!…ni lazima ajaze tanki lake karibia kila siku ili ajisikie vizuri..

Vile vile Mlevi wa Roho Mtakatifu ni lazima ajazwe Roho Mtakatifu karibu kila siku na Roho Mtakatifu anajaa ndani ya watu kwa njia ya maombi na kumsifu MUNGU.

Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Hivyo maisha ya maombi kwa mtu aliyejaa Roho mtakatifu, yanapaswa yawe sehemu yake daima.

Swali ni je na wewe umeleweshwa na kiti gani??..Ni dhambi? Au Roho Mtakatifu??….Fahamu kuwa ulevi wa pombe matokeo yake ni ufisadi sawasawa na Waefeso 5:18 na hivyo ni upotevu.

Mpokee leo YESU kama bado haujampokea na Ujazwe Roho mtakatifu.

Bwana YESU akubariki sanWashirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

TUNASHINDA NA ZAIDI YA KUSHINDA

Warumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda”

Upo ushindi, lakini pia Upo “Ushindi ulio zaidi ya ushindi”

Unaposhindana na Mtu/Watu na kuwashinda hapo unahesabika kuwa ni “Mshindi”.

Hali kadhalika unaposhindana na mashetani/mapepo na kuyashinda hapo unahesabika kuwa ni “Mshindi”.

Lakini unaposhindana na “MUNGU WA MBINGU NA NCHI” na kumshinda huo ni “Zaidi ya ushindi”

Utauliza kivipi?. Je mtu anaweza kushindana na MUNGU aliyemwumba na kumshinda?..jibu ni ndio!.

Yakobo alishindana na watu na MUNGU na kumshinda..

Mwanzo 32:27 “Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.

Tafsiri ya jina “Israeli” ni “Mshindi”..

Yakobo alizishindani baraka za MUNGU na kuziteka, alishavuka viwango vya kupambana na watu, sasa yupo viwango vya kupambana na MUNGU na kushinda…huyo huwezi kumwita tena mshindi, ni zaidi ya Mshindi.

Kadhalika walio ndani ya YESU kikwelikweli ni “Zaidi ya Washindi” Ni Israeli kwelikweli…wamevuka viwango vya kupambana na watu, wapo viwango vya kupambana na MUNGU na kuteka baraka zao.

Waefeso 3:20 “Basi atukuzwe yeye awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadiri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu”

Waliookoka kweli kweli hawana muda na wachawi, kwasababu hao tayari wamewashinda..

Hawana muda na wanadamu wabaya, kwasababu tayari wameshawashinda katika ulimwengu wa roho, lakini wenyewe wana muda na MUNGU na baraka zake, wanazishindania hizo, na wanaposhinda hawaitwi tena washindi, bali Zaidi ya washindi! Haleluya.

Na kumbuka ushindi huu usio na maelezo upo ndani ya mmoja tu ambaye ni YESU KRISTO, na si kwa mwingine..

1 Wakorintho 15:57 “Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo”

Hiyo ndio faida ya kuwa ndani ya YESU…

Wachawi hawawezi kukushinda ukiwa ndani ya YESU, Mapepo hayawezi kukushinda ukiwa ndani ya YESU, Watu wanaoshindana nawe hawawezi kukushinda ukiwa ndani ya YESU.

Dhambi haiwezi kukushinda ukiwa ndani ya YESU, Zaidi sana na (mashetani, watu na viumbe vingine vyote), ambavyo vinafanya vita nawe pasipo wewe kujua haviwezi kukushinda, kwasababu wewe ni mshindi na zaidi ya Mshindi.

Unaingiaje katika huu Ushindi?..Kwanza kwa kumwamini Bwana YESU, na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa kisha kupokea ujazo wa Roho Mtakatifu.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post