SWALI: Kwanini Yesu akubali ombi la mapepo, na si kuyaamulia adhabu yake mwenyewe, au kuyafukuza kabla hata hayajaongea?
Luka 8:31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. 32 Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.
JIBU: Maneno hayo aliyasema baada ya kukutana na mtu yule aliyekuwa amevamiwa na jeshi la mapepo, yaliyomfanya akae makaburini muda mrefu, bila nguo. Hivyo kama tunavyosoma yale mapepo yalipomwona tu Yesu, kabla ya tamko lolote yenyewe yakamfuata na kuwasilisha ombi lao kwa kusihi sana. Kwamba yawaingie wale nguruwe waliokuwa jirani wakichungwa. Yesu akasiliza ombi lao, akayapa ruhusa. Yakamtoka Yule mtu, na kuwaelekea wale nguruwe, na saa ile ile Yule mtu akawa mzima.
Zipo sababu mbili.
Ni wazi kuwa Bwana alilitafakari wazo lao, na kuona kama lingeweza kuleta madhara yoyote au uharibifu wowote wa mpango wa Mungu. Na akaona kinyume chake ni kuwa kusudi la Mungu litaendelea kuthibitika hata katika ombi lao, kwasababu kutoka kwao na kuwaingia wale nguruwe kisha kwenda kujitupa ziwani. Ilikuwa ni udhihirisho wa wazi kwa watu kuwa mapepo ni halisi, lakini pia yanatabia ya uuaji. Kwamfano kama angemponya tu, bila ishara yoyote, pengine wengine wangesema “aah huyu akili zilimruka tu!” alikuwa na stress zake, au maisha yalimtinga sana, akachizika, hivyo amekutana na mwanasaikolojia mzuri amemweka sawa… Lakini kuona mapepo yale yameruhuisiwa kwenda kuingia viumbe vingine, halafu yakawaendesha ziwani kuwaua, ilikuwa ni ishara bora zaidi ya kazi za Mungu.
Utakumbuka mapepo yenyewe yalimwambia Yesu ‘tuna nini nawe, je umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?’
Mathayo 8:29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Maana yake ni kuwa mapepo yalijua kuwa walishawekewa wakati wao wa mateso baadaye kule shimboni na atakayekuja kuwapeleka huko ni Kristo. Hivyo hapa yanamkumbusha Bwana asibatilishe mpango huo, na kuwaadhibu mapema.
Pengine hiyo ndio sababu nyingine ya Bwana kutotoa adhabu kali kwao, ni kuwa mpango wa hukumu ungebatilika.
Kitendo cha mapepo kujisalimisha yenyewe kuomba kupunguziwa adhabu, ni kuonyesha mamlaka kuu iliyo ndani ya Kristo. Ambayo hata sasa ipo ndani yetu. Hatufundishwi kuongea na mapepo, bali kuyakemea kwa mamlaka yote. Ambayo yaweza tokea mengine hata kabla ya kukemewa yakaomba yenyewe nafasi ya kupunguziwa adhabu. Hilo linawezekana!
Tumia mamlaka uliyopewa ndani yako. Fukuza pepo wote.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Gengeni ni wapi, wale nguruwe walipoteremkia? (Marko 5:13)
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
Je mapepo au majini yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai?
Katika agano la kale dhambi ilitokea na kuhesabiwa katika maeneo mbalimbali.
Kwamfano
> Kulikuwa na makosa ya jamii nzima. Yaani taifa zima kuasi. (Kutoka 32,)
> Makosa ya mtu binafsi. Mfano kutenda uzinzi, Wizi, uuaji n.k.
> Makosa ya kuwatendea vibaya wanyonge: Mfano maskini, wageni, mayatima na wajane (Amosi 5:11-12),
> Makosa ya kukaidi sherehe za kidini (Walawi 11-15),
> Makosa ya kuvunja maagano (Yeremia 17:21-23),
> Makosa ya kuabudu miungu mingine (sanamu).
Lakini pia kulikuwa na aina nyingine mbili za makosa..
> Aina ya kwanza ni makosa ya kukusudia
> Aina pili ni yale ya kutokusudia.
Ikiwa mtu alitenda dhambi kwa kutojua, alihesabika kuwa ni dhambi, hivyo alilazimika atoe sadaka ya dhambi. Lakini kama alitenda dhambi ya makusudi kinyume na mwenzake, ili kuondoa kosa Ilipasa atoe sadaka ya hatia.
Aina ya sadaka hizi zinaelezwa kwa urefu kwenye kitabu cha Walawi 4:1 – 5:13
Dhambi za kutokusudia Mfano wake ilikuwa ni kama kuvunja amri bila kujua au kutojua Sheria ya vitu safi au najisi ilivyo. Hivyo mtu alijikuta tu anatenda kwa kukosa ufahamu.
Walawi 4:1-3
[1]BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
[2]Haya, nena na wana wa Israeli, uwaambie, Kama mtu ye yote akifanya dhambi pasipo kukusudia, katika neno lo lote ambalo BWANA amelizuilia lisifanywe, na kutenda neno lo lote la maneno hayo;
[3]kama kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa BWANA ng’ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi.
Dhambi za kukusudia ni zote ambazo zilitendwa kinyume na mtu mwingine au mambo matukufu mfano wa hizi ni kama kuiba, kusema uongo, viapo Vya uongo, hivyo iliambatana pia na kutoa fidia ya vitu hivyo.
Sio tu kusamehewa bali pia kuweka mambo sawasawa kwa kulipia fidia.
Mfano wa tendo hili, tunaona kwa Zakayo, alipofikiwa na wokovu, alitubu kwa kurejesha mara nne ya vyote alivyodhulumu. (Luka 19:8) huo ni mfano wa sadaka ya hatia.
Katika agano jipya dhambi Zote Za kukusudia na kutokusudia na nyingine zote zinaondolewa na sadaka moja tu ya daima nayo ni DAMU YA YESU (Waebr 9:26, Isaya 53:10, 1Petro 2:24). Hiyo tu ndio inafuta hatia zote.
Lakini pamoja na hayo, sadaka hizi hutukumbusha pia kila tuombapo rehema, (kwa unajisi tunaojitia kila siku), hatuna budi kuomba sio tu kwa dhambi tuzijuazo bali pia kwa zile tusizozijua.
Kwasasa dhambi tusizokusudia ni kama vile kumkwaza mwenzako bila kufahamu, Kutowaombea wengine(2Samweli 12:23), kuwaza vibaya, kutotumiza nadhiri zetu, au wajibu wetu N.k.
Bwana akubariki.
Je umesamehewa na kuondolewa dhambi zako? Kama ni la! basi wakati ndio sasa, unapomgeukia Bwana Yesu, anakuondolea kumbukumbu lote la makosa. Hivyo fungua hapa kwa msaada huo wa kumpokea yeye >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ndio kipi? (Matendo 21:25).
Nini maana ya dhabihu na matoleo hukutaka? (Waebrania 10:5).
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Ili kuelewa maana ya ndoto yako, jambo la kwanza ni kujiuliza ni kwanini awe mchungaji, na si mwalimu wako, au boss wako, au rafiki yako, au ndugu yako au mtu mwingine yoyote?
Ukiwaza hivyo, tendo linalofuata ni kujua kazi ya mchungaji hasa ni nini?
Mchungaji ni mwakilishi wa Mungu na hivyo anafanya kazi ya kutoa mashauri bora ya kiroho kwa mafundisho sahihi (Tito 1:7-9): Kuonyesha kuwa maisha yako yanahitaji hekima ya ki-Mungu kukuongoza, zaidi ya hekima yako mwenyewe. Kila jambo au uamuzi unaojitokeza kwenye maisha yako, mshirikishe kwanza Mungu kimaombi, kisha angalia kwenye biblia jambo hilo Mungu analiagizaje, ikiwa si rahisi kutatulika, basi ni vema ukamshirikisha kiongozi wako wa kiroho kukusaidia.
Wachungaji pia wamepewa mamlaka ya kutoa maonyo kwa kondoo wao.
2Timotheo 4:2 lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho
Angalia pengine katika maisha yako Mungu anakuonya / anakutahadharisha katika jambo Fulani, ambalo sio sawa unalotaka kulifanya. Hivyo zingatia sana pia hilo.
Kazi ya wachungaji ni kuwalinda, kuwafariji na kuwainua waliokata tamaa. Mfano wa Yesu kristo mwokozi wetu, na faraja yetu, aliyemchungaji mkuu (Mathayo 11:28, Zab 23). Hivyo Mungu anakuonyesha kuwa yupo na wewe katika safari yako, kukuchunga, usiogope.
Lakini sababu nyingine ya mwisho (ambayo si kubwa): Yaweza kuwa ni wazo la ki-akili. Kwasababu kumbuka si ndoto zote hutoka kwa Mungu au kwa shetani, nyingine ni wazo la bongo zetu, kufuatana na mazingira yanayotuzunguka (Mhubiri 5:3). Kwamfano ikiwa mara nyingi unakuwa karibu na mchungaji wako, kuota unaongea naye mara kwa mara, itakuwa ni jambo la kawaida. Au mtu ni mpishi, kujiona yupo jikoni mara kwa mara anapika litakuwa ni jambo kawaida kabisa kwake.
Hivyo kwa ufupi ni kuwa kuota unaongea na mchungaji wako, si ndoto mbaya, bali kwa asilimia kubwa ni ya ki-Mungu. Inategemea zaidi na maudhui yake. Hakikisha tu unapiga magoti na kuomba Bwana akufunulie ni eneo lipi hasaa, ndoto yako imeegemea ukilinganisha na maisha yako, na lile eneo ambalo unaona lina uzito zaidi basi ujue hapo ndipo Mungu anasema nawe hapo. Chukua hatua.
Je! Umeokoka?
Unafahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu amekaribia sana kurudi? Ikiwa ni la! Basi muda ndio huu, mgeukie Kristo akuoshe dhambi zako, akupe uzima wa milele bure. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo sasa, fungua hapa kwa msaada wa kuongozwa sala ya toba >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Isaya 6:1
[1]Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu.
Je unayajua makao hasaa ya Mungu?
Ni kweli tunafahamu Mungu anaketi katika kiti chake cha enzi, lakini ni kiti kilicho wapi hasaa?
Je! handakini? Mabondeni? Mapangoni? Kichakani? hasha!
Maandiko yanatueleza “Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana”
Kwahiyo na sisi lazima tuyajue makao hayo, ili tumfikie, vinginevyo tutajikuta tunaabudu Mungu mahali Ambapo kiti chake hakipo.
Katika biblia sehemu yoyote unapokutana na hili Neno “mahali pa juu”, Moja kwa moja utaona palihusishwa Na ibada..Yaani madhahabu zilijengwa pale ili kumtolea Mungu dhabihu. (1Samweli 9:12-13, 1Wafalme 3:2)
Yalikuwa ni maeneo yote yaliyoinuka mfano milimani. Kwasababu huko ndiko Mungu alikuchagua kujidhihirisha, na sio mabondeni, au mapangoni.
Ni kwanini?
Kwasababu Mungu anakaa sehemu Bora kuliko zote, sehemu iliyozidi vyote, sehemu ya juu ya juu kuliko zote. Hakai penginepo, Mungu hawekwi chini, haabudiwi mabondeni..kamwe hiyo sio sifa yake.
Hivyo ni vema ukafahamu sifa yake hii, ili tujue namna sahihi ya kumwendea.
1). Makazi:
(Mbinguni)
Kimakazi Mungu anaketi mbinguni.. Kwasababu Mbingu ni bora kuliko dunia hii.
Isaya 66:1
[1]BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?
Ndio maana tuna ujasiri na Mungu, akatie sehemu Bora zaidi ya hii, ambayo alisema atatukaribisha katika makao hayo baadaye.
Bwana Yesu alituambia tukisali tuseme Baba yetu uliye mbinguni.. (Mathayo 6:9). Hata alipoomba aliinua macho yake juu(Yoh 17:1), na sisi tumtakaripo Mungu, tuiweke picha hiyo akilini mwetu. Kwamba Baba yetu yupo mbinguni.
Na kutoka huko ndio tunatarajia mema yetu yaje, Na wenyeji wetu kushuka.(Yerusalemu mpya).
2) Viumbe.
(Mwanadamu).
Mwanadamu ametukuka kuliko viumbe vyote, amemvika uwezo na mamlaka (Zab 8:4-6). ndio maana amechagua kuketi ndani ya moyo wa mwanadamu na sio kiumbe kingine chochote. Mungu hakai ndani ya swala, au sungura, au simba.. amechagua makao yake kuwa ndani ya mwanadamu tu.
Na aliyetufungulia lango hilo ni Yesu Kristo mwokozi wetu, kama mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alikaa ndani yake kikamilifu. Pasipo yeye kamwe Mungu asingekaa ndani ya moyo wa mwanadamu.
Ukimkosa Kristo umemkosa Mungu ndani yako.
Hivyo wewe uliyeokoka, fahamu kuwa Mungu anakaa ndani yako, hivyo wajibu wa kujichunga sana na kumpa Mungu ibada ya kweli( Warumi 12:1)
Ndio maana anapouheshimu mwili wako umemuheshimu Mungu. Kama mwanadamu ogopa sana kujiharibu kwasababu wewe ni mahali pa juu sana palipoinuka pa Mungu.
1 Wakorintho 3:16-17
[16]Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
[17]Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi.
3) Tabia
(Utakatifu)
Mungu ni mtakatifu, hivyo amechagua usafi zaidi ya uchafu, yeye ni Nuru si giza, ni mkamilifu si mwenye kasoro.
Hivyo tufahamu kuwa, tukimwendea yeye? kwa kupenda usafi? Lazima tutamwona.Lakini tukisema tunamtafuta na huku ni wachafu, hapo bado hatujamfikia Mahali pake pa juu anapoketi.
Isaya 57:15
[15]Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.
Sehemu nyingine anasema..
Zaburi 24:3-4
[3]Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
[4]Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.
Soma pia, Zab 15
4) Uweza:
(Imani)
Mungu si dhaifu, hivyo jambo lolote linaloonekana lina Nguvu, lililotukuka, lipitalo uwezo au ufahamu wa kibinadamu ni lake.
Ndio maana mtu anayemwendea Mungu kuomba yasiyowezekana kibinadamu, amemfikia Mungu.
Anaitwa Mungu wa miungu, Ibrahimu alimwamini Mungu kwa yasiyowezekana akawa rafiki wa Mungu, watu wote walio wa Imani ndio wanaomwona Mungu, Akiwatendea miujiza. Fahamu kuwa Mungu anavutiwa zaidi na yale yasiyowezekana Kibinadamu kuliko yale yanayowezekana..Jifunze kuishi kwa Imani, maana hapo ni mahali pake pa juu.. ondoa mashaka Ndani yako. Utamfikia Bwana hakika.
5) Ibada:
(Heshima)
Katika eneo la ibada, Mungu hafanyiwi Ibada ilimradi ibada. akiabudiwa ni lazima iwe katika Roho na kweli. Tunamtolea ibada ya juu sana..ikiwa ni sadaka Hatumpelekei kilema, bali ile ya juu zaidi, ikiwa ni sifa tunamsifu kwa nguvu zetu zote, kama Daudi,bila kujali kitu, kama ni kumtukuza Basi tunamtukuza sana na kumwadhimisha kwa viwango vyote.
Kwasababu yeye ndiye Mungu wetu astahiliye sifa zote.
Hivyo yatupasa maeneo yote hayo, tuyatambue, kisha tumwabudu kiufasaha Mahali pake pa Juu palipoinuka.
Zaburi 113:5-6
[5]Ni nani aliye mfano wa BWANA, Mungu wetu aketiye juu; [6]Anyenyekeaye kutazama, Mbinguni na duniani?
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Katika kanisa, Mungu aliweka huduma mbalimbali, karama mbalimbali, na utendaji kazi tofauti tofauti, ili kulikamilisha kanisa lake na kuupanda ufalme wake duniani kama alivyokusudia.
Sasa katika upande wa huduma, Mungu aliziweka huduma kuu tano, ambazo zenyewe zinasimama kama kuliongoza kanisa, kulikuza, kulichunga, ni kama nguzo za kanisa ambazo husimama wakati wote, Nao ni;
Mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. (Waefeso 4:10-12)
Kwa urefu wa maelezo ya huduma hizo jinsi zinavyotenda kazi basi bofya hapa upitie >>> TOFAUTI YA MITUME, MANABII, WAINJILISTI, WACHUNGAJI NA WAALIMU NI IPI?
Lakini sambamba na hizo aliweka wengine katika kanisa, wanaoshirikiana na hawa watano (5).
Ambao ni WAZEE WA KANISA, MAASKOFU na MASHEMASI
Tuangalie kazi ya kila mmoja;
Tamaduni za kiyahudi tangu zamani walikuwa na desturi ya kuteuwa wazee (watu waliokomaa kiumri), wenye hekima na busara na uzoefu wa Kidini kufanya maamuzi na Kutoa hukumu mbalimbali katikati ya jamii ya wayahudi Soma (Kutoka 3:16, Kumbukumbu 1:9-18)
Hata baadaye kanisa lilipokuja kuanza, nyakati za mitume, tunaona bado walirithi utaratibu huo katika nafasi za kiuongozi ndani ya kanisa. Isipokuwa haikuhitaji awe ni lazima mzee Kiumri, lakini ni lazima Awe amekomaa Kiroho.
Nafasi hii hasaa iliwahusu wanaume, Kwasababu katika nyaraka za mitume hatuoni mahali popote kama kuna mfano wa mwanamke aliyeteuliwa kuwa mzee wa kanisa.
Ukisoma Tito 1:6, inaeleza sifa zao, anasema wazee wawe waume wa mke mmoja..
Tito 1:5-6
[5]Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;
[6]ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni wafisadi wala wasiotii.
(Matendo 14:23)
Zingatia: Hii haiwafanyi wanawake wasiwe na kazi yoyote katika kanisa hapana, wanaweza kusimama kama huduma-kivuli ambazo zaweza Kuonekana kama za wazee wa kanisa, waalimu, mashemasi, kama wasaidizi wenye huduma hizo, lakini sio rasmi kwao. Mfano wa hawa kwenye biblia walikuwa ni akina Fibi, prisila,
KAZI ZA WAZEE WA KANISA:
1). Kulichunga kundi,
Matendo 20:28
Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe.
(Soma pia 1Petro 5:1-4)
ii) Kufundisha vema watu.
1 Timotheo 5:17
[17]Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.
Tito 1:9
[9]akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.
iii) Kutatua migogoro ya kiimani ndani ya kanisa.
Utakumbuka wakati ule makanisa ya mataifa yalikuwa yakitaabishwa, na wayahudi juu ya kushika torati, hivyo kukatokea mkanganyiko mkubwa, na kuwalazimu wawafuate wazee kule Yerusalemu ili walitatue tatizo hilo, na kama tunavyosoma baada ya hoja nyingi, walifikia hitimisho sahihi la Roho Mtakatifu.
Matendo 15:6 Mitume na wazee wakakusanyika wapate kulifikiri neno hilo.
7 Na baada ya hoja nyingi Petro akasimama, akawaambia, Ndugu zangu, ninyi mnajua ya kuwa tangu siku za kwanza Mungu alichagua miongoni mwenu ya kwamba Mataifa walisikie neno la Injili kwa kinywa changu, na kuliamini
iv) Kuwaombea wagonjwa.
Yakobo 5:14-15
[14]Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana.
[15]Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
2) MAASKOFU.
Maana ya Askofu ni mwangalizi.
Kazi yake kubwa ni kuliangalia kanisa,/ kulisimamia, mfano kusimamia malengo ya kikanisa, kulinda fundisho, na kusimamia uchungaji ulio bora.
Japokuwa mahali pengine maaskofu wanatajwa kama wazee wa kanisa. (Tito 1:5-9).
Lakini tofauti yao hasaa ni kwamba wazee wanayasimamia makanisa madogo madogo, lakini maaskofu ni waangalizi wa makanisa (yote/baadhi), Wazee wanaweza kuwa wengi, lakini maaskofu ni cheo, cha uangalizi hivyo aweza kuwa mmoja au wachache, wazee wanaweza kuwa na wajibu wa kufundisha, na kuchunga, lakini maaskofu hasaa katika kuongoza. Vilevile kwenye maandiko hatuoni mahali popote nafasi hii ikihusisha wanawake.
Sifa za maaskofu na wazee, wa kanisa zinafanana.
Sifa za mtu kuwa mzee wa kanisa. (Tito 1:5-9, 1Timotheo 3:1-7)
3) MASHEMASI.
Mashemasi ni mtumishi wa kanisa. Huduma hii ilitokea katika kanisa kwa mara ya kwanza, mitume walipokuwa wanahudumu na kuona kuwa baadhi ya mapungufu kwamba wajane wanasahaulika katika huduma ya kila siku, ndipo ikalazimika wateue watu saba, ndani ya kanisa watakaoweza kusimamia mambo yote ya kimahitaji ya kundi. (Matendo 6:1-7), mmojawapo alikuwa ni Stefano.
Kazi za mashemasi:
i) Kulihudumia kundi katika masuala ya mahitaji ya mwilini ya kundi:
Hususani kwa maskini, wajane, wenye mahitaji, mayatima.
ii) Kuongoza kwa mifano:
Lazima wawe kipaumbele kitabia, uaminifu, na nidhamu Na kuonyesha roho ya kiutumishi
iii) Kusimamia shughuli za kikanisa:
Ujenzi, taratibu za kiibada na mikutano, kusimamia hazina na mali za kanisa.
Sifa za mtu kuwa shemasi:
Zinatajwa kwenye 1Timotheo 3:8
1Timotheo 3:8 Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana,si watu wanaotamani fedha ya aibu.
9 wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. 10 Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.
11 Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.
12 Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.
13 Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu
Hivyo wazee, maaskofu na mashemasi, ni nguzo muhimu za kulifanya kanisa kusimama, katika nidhamu ya kitabia na kimapokeo, pamoja na kihuduma.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Zaburi 22:1 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati.
Maneno haya ukiyatafakari, utagundua ni ya mtu aliyefikia hatua mbaya sana ya kukaribia kukata tamaa kwasababu ya aidha magumu, au huzuni, au mateso yasiyoelekeza anayoyapitia, akiangalia kulia, haoni tumaini lolote, akiangalia kushoto haoni mkono wowote wa Mungu ukimsaidia licha ya kuomba na kulia sana, kwa muda mrefu.
Sehemu nyingine anasema, amekataliwa kila kona, amekuwa kama msikwao kwa ndugu zake.
Zaburi 69:10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.
11 Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao. 12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki. 13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako.
14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji. 15 Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu.
16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. 17 Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi.
Mwandishi huyu alikuwa ni Daudi, alipitia kipindi kirefu sana cha kujiona kama vile Mungu kamtupa, hadi kuna wakati akaona heri aende kuomba hifadhi kwa maadui zake wafilisti ambao hapo mwanzo aliwafukuza na kuwaita makafiri (wasio tahiriwa), lakini safari hii kwa unyenyekevu wote, anaenda kuwa mmoja wa askari wao, ili tu apate hifadhi, asiangamie kabisa. Huyo ni mtu ambaye maji ya shingo yalimfikia kwelikweli.
Sio kwamba alikuwa haombi, au hamlili Mungu?. Au kwamba ana dhambi kuliko wengine, mpaka awe mtu wa bahati mbaya hivyo Hapana, nyakati zote alikuwa mwombaji, lakini akafika mahali katika uhalisia wa kibinadamu aliona kama Mungu amemwacha kabisa.
Lakini kwasababu huruma za Mungu zilikuwa nyingi juu yake alimpa moyo mkuu, wa kuendelea kumngoja Bwana. Ndio maana sehemu nyingi katika Zaburi anasisitiza sana Neno hili ‘mngojeeni Bwana’ (Zaburi 37:7, 25:3, 31:24,38:15, 40:1).
Sasa moja ya maneno machache ya Daudi yaliyonikuliwa na Bwana Yesu lilikuwa ni hili.
Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Mathayo 27: 45 Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.
46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Je! Unadhani kauli hiyo Yesu aliyoitoa alimaanisha kweli ameachwa?
Hapana, tangu mwanzo alikuwa anajua Mungu yupo pamoja naye, na kwamba saa yake imekaribia, muda si mrefu anakwenda kuinuliwa na kutukuzwa, tena sehemu nyingine anasema alishangalia pale msalabani (Wakolosai 2:15). Lakini kuinukuu kauli ile ni kuonyesha ubinadamu wetu, unavyoweza kutuhubiria tuwapo katikati ya shida, kwamba Mungu ametuacha hususani pale tunapopitia shida, na mateso.
Yesu alinukuu ubinadamu wetu kukumbuka mfano wa yale aliyoyapitia Daudi..
Lakini tunaona dakika chache baada ya pale, pindi tu alipokata roho, makaburi yakapasuka, wafu wakatoka makaburini, pazia la hekalu likapasuka, na baada ya siku tatu akafufuka, ukombozi wetu mkuu ukapatikana, ‘Lakini ni kwa maneno ya kudhaniwa kuwa Mungu amemwacha’.
Mathayo 27:50 Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka;
miamba ikapasuka; 52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala; 53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.
Ndugu, upitiapo hatua hizo ambazo mawazo yako yanakufundisha kuwa Mungu hayupo na wewe tena, amekuacha, kwasababu ya shida unazozipitia muda mrefu, magonjwa yasiyokoma, umeomba mpaka umechoka, umelia hadi ukomo,wewe ona ni kawaida,…. Piga moyo konde Mngojee Bwana. Daudi alistahimili hatimaye akathibitishwa kwenye ufalme ambao ulidumu pamoja na vizazi vyake vingi tofauti na wafalme wengine wa Israeli. Mngojee Bwana, kimaombi, kwasababu baada ya joto huja mvua.
Shalom.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nzi wa Misri, na Nyuki wa Ashuru vilimaanisha nini? (Isaya 7:18-20).
JIBU: Swali la kwanza la kujiuliza, je! mkristo ni mtu gani?..Mkristo ni mtu aliyemwamini,Yesu Kristo, kisha akapokea msamaha wa dhambi,kwa toba ya kweli, ubatizo na kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu.
Mtu wa namna hiyo anakuwa na Kristo ndani yake. Na mtu mwenye Kristo Hawezi kuwa na mapepo, kwasababu Yesu hana pepo.
Vifungu hivi vinatuthibitishia kuwa hilo jambo haliwezekani;
1 Yohana 4:4
[4]Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia.
2 Wakorintho 6:14
[14]Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Kuonyesha kuwa giza na nuru haviwezi kuwepo sehemu moja, wakati mmoja.
Lakini swali linakuja inakuwaje kuna baadhi ya watu waliokoka wanaonekana kuwa na mapepo ndani yao?
Kama tulivyoona mkristo hawezi kuwa na mapepo, lakini ni vema kufahamu kuwa kuna tofauti kati ya kukaliwa na mapepo, na kushambuliwa na kipepo.
Mtu aliyeokoka hawezi kukaliwa na mapepo, lakini anaweza akashambuliwa au kusumbuliwa na uwepo wa mapepo, hicho ndicho kinachoweza kumtokea, lakini sio kwamba ana mapepo ndani yake.
Sababu zinazoweza mpelekea asumbuliwe nayo, ni hizi kuu tatu;
Tukianza na sababu ya kwanza.
Kukosa kujua nafasi na mamlaka uliyo nayo ndani ya Kristo, shetani anaweza kukusumbua kwelikweli. Na wakati mwingine kukutesa. mapepo yanaweza kuwasumbua watu kifikra na kwa kuwawekea mawazo machafu akilini mwao, kuwashitaki, kwa kuwatupia ndoto mbaya, au kuwakaba usiku, au kuwaletea majaribu mbalimbali, lakini huyu mtu akijua kuwa ameshakabidhiwa mamlaka yote ya kukanyaga nge na nyoka na nguvu zote za yule mwovu,(Luka 9:1), akaitumia vema, shetani atamwogopa kumsogelea kwasababu anajua nguvu ya kimamlaka iliyo ndani yake ni thabiti haitoki mdomoni bali inasukumwa na ufalme wa Mungu ulio nyuma yake.. Ni sawa na mtu anayetoa amri kwa kinywa chake mwenyewe na yule anayetoa kwa agizo la raisi watu watamwogopa yule anayetoa kwa mamlaka aliyopewa na raisi. Hivyo ni muhimu sana kuitafakari na kuiamini mamlaka uliyopewa na Kristo ndani yako ili hayo maroho unapoona dalili ya kutaka kukusumbua unatamka jina la Yesu mara moja tu yanatetemeka na kukimbia. Mamlaka hiyo amepewa mkristo yoyote aliyeokoka, haijaishi ni mchanga au mkomavu.
Ukiokolewa, kwasababu ya kutoondoka mara moja kwa baadhi ya tabia, au msingi au mienendo ya kale, hivyo tabia hizo mara nyingine zinakuwa ni upenyo wa uwepo wa kipepo kuzunguka zunguka karibu yako. Vitu vichanga sikuzote hushambulika kirahisi, unyasi ukiwa mdogo hutikiswa sana na upepo, Ndio maana ni lazima uanze kuukulia wokovu, kwa kujifunza Neno, kujizoesha utakatifu, maombi, ibada, mambo ambayo adui hapendi kwasababu ni kama moto kwao. Mtu asipokuwa mkristo wa vitendo, sikuzote atasumbuliwa na roho za kidunia, na hatimaye atajiona kama ni ana mapepo kabisa, na akiendelea kuishi hivyo, mpaka kurudi nyuma atakufa kiroho, na Roho Mtakatifu kuondoka ndani yake, na mapepo ndio yatapata nafasi ya kumtawala kabisa. (2Petro 1:5-10)
Mtu aliyeokoka, akaanza kutenda dhambi za makusudi, anarudia yale yale kila siku, jambo hilo ni upenyo mwingine wa mapepo kumsumbua, kwasababu anakuwa ameyapa nafasi, na maandiko yanasema tumsimpe ibilisi nafasi. (Waefeso 4:27).
Kwamfano umeacha ulevi, baada ya kuokoka, na umekuwa hivyo kwa muda mrefu sasa, halafu ghafla unaanza tena kuwa mlevi, Mungu anakuonya uache hutaki, unaendelea kunywa pombe..kitendo hicho kinaweza kukupelekea kusumbuliwa sana na mapepo. Mfano tu wa Yule ambaye anatawaliwa nayo.
Mathayo 12:43 Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika,asipate.
44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na
kupambwa.
45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye
mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya.
Hivyo kwa hitimisho, ni kuwa mtu aliyeokoka, hawezi kukaliwa na mapepo, yaani kutawaliwa au kupagawishwa, au kuendeshwa nayo.. Isipokuwa anaweza kushambuliwa, kusababishiwa madhara, lakini kuvamiwa na uwepo wao. Ndio maana tumeambiwa tuvae silaha zote za haki, ili tuweze kumpinga shetani (Waefeso 6:10). Kwa kulijua Neno, utakatifu, maombi, na ibada.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mbona ni maskini tu huwa ndio wanaolipuka mapepo, na sio matajiri?
DALILI TISA (9) ZA PEPO KUWEPO NDANI YA MTU.
Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka,
Katika biblia wapo watu wanne Wanatajwa Kwa jina la Filipo.
Huyu ndiye anayetambulika sana, ambaye alikuwa ni mmoja wa mitume wa Yesu Kristo
Yohana 1:43-44
[43]Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.
[44]Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.
Soma pia (Marko 13:18)
Huyu ni moja ya wale watu saba (mashemasi), waliochaguliwa na mitume wasimamie shughuli za kanisa. Habari yake tunaisoma Katika..
Matendo ya Mitume 6:2-5
[2]Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani.
[3]Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;
[4]na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.
[5]Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;
Huyu ndiye alikwenda kumbatiza yule towashi mkushi, na baadaye Kunyakuliwa na kupelekwa sehemu nyingine kwa ajili ya injili (Matendo 8).
Lakini pia anaonekana kuja kuishi Kaisaria ambapo alikuwa na mabinti wake wanne waliokuwa wanatabiri (Matendo 21: 8-9)
Huyu alikuwa mtoto wa Herode Mkuu.
Luka 3:1
[1]Mwaka wa kumi na tano wa kutawala kwake Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alipokuwa liwali wa Uyahudi, na Herode mfalme wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania mfalme wa Abilene,
Kulingana na historia Huyu hakuonekana na sifa za chuki au ukatili bali mtenda haki, ndiye Aliyekuja kujenga mji wa Kaisari-Filipi, ulioitwa kwa jina lake (Mathayo 16:13).
Alikuwa mtoto mwingine wa herode mkuu, wengine humchanganya na Filipo mfalme wa Iturea. Herode mkuu alikuwa na watoto.wawili walioitwa Filipo. Huyu hakuwa mfalme kama ndugu zake, ndiye aliyekuwa mume wa Hedoria, Ambaye alimwacha na kwenda kuolewa na kaka yake Herode, kitendo ambacho kilikemewa Na Yohana mbatizaji? Ikampelekewa yeye kufungwa na baadaye kukatwa kichwa. (Marko 6:17-19).
Nini tunaweza kumulika katika Filipo hawa wote.
Ijapokuwa walifanana majina Lakini tabia zao zilikuwa tofauti, Filipo wawili Wa kwanza walikuwa wakristo, lakini wawili wa mwisho hawakuwa wakristo.
Kuonyesha kuwa majina sio yanayowageuza watu. Bali Ni mwitikio wa injili. Ni vema kuwa na majina mazuri, Lakini ikiwa hakuna mwitikio wa kweli haiwezekani kubadilika hata tupewe majina mazuri namna gani.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii.>>>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Je! ile habari ya Herode kutaka kumwua Yohana mbatizaji inajichanganya?(Mathayo 14:5 na Marko 6:20).
Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mithali 29:9 Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu; Akikasirika au akicheka, pia hapana raha.
Mstari huo kwa lugha rahisi tunaweza kuuweka kwa namna hii. “Mwenye hekima akijadiliana na mpumbavu, akijibu kwa kicheko au kwa hasira, matokeo ni yaleyale tu hakuna amani au suluhisho”
Unafunua sifa za mpumbavu, kwamba sikuzote mwitikio wake wowote hauwezi kuleta mabadiliko. Kwamfano labda hoja imetolewa na ikamuumiza kiasi cha kumfanya ajibu kwa hasira. Sasa wewe waweza tarajia pengine jambo hilo limemgusa kweli moyo, litambadilisha lakini matokeo yake ni kwamba anakuwa vilevile, Halikadhalika waweza kutoa hoja ikamfanya acheke ukitarajia kitaambatana na badiliko lolote ndani yake lakini hakuna.
Maana yake mpumbavu, haguswi kwa ukali au kwa wepesi wa maneno ya aina yoyote…Na hivyo ni kuachana naye Tu.
Tukiachia wapumbavu wa kawaida tunaowafahamu..Mpumbavu hasaa ni yule mtu anayeikataa kweli ya Mungu mfano wa wale waandishi na mafarisayo wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 23:17), mtu wa namna hii unapomuhubiri injili, hata imchomeje au imchekesheje hawezi kufikiri hata chembe kubadilika, kinyume Chake ni mapambano tu.
Bwana Yesu alitufundisha na kutuambia kuwa si kila mtu ni wa kumtupia lulu zetu, maana yake wanaweza kutugeukia na Kuturarua. Ukiona mtu anaishia kwenye ubishi tu na mashindano, ni kuachana naye na kugeukia waliotayari kupokea.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)
Elewa tafsiri ya Mithali 27:22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwa mchi kinuni.