Siku moja Yesu alipokuwa anahubiri katika nyumba fulani, watu wengi walikusanyika mahali pale, na ghafla wakamletea mtu aliyepooza mwili mzima hawezi kufanya lolote, wakamweka Mbele yake ili amponye. Lakini tunaona mwitikio wa Yesu ulikuwa ni tofauti na matarajio yao. Bwana Yesu hakumwekea mikono na kumwambia simama uende, bali alimwambia..
Rafiki, umesamehewa dhambi zako.
Luka 5:17-20
[17]Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya. [18]Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake. [19]Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu. [20]Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.
[17]Ikawa siku zile mojawapo alikuwa akifundisha, na Mafarisayo na waalimu wa torati walikuwa wameketi hapo, waliotoka katika kila kijiji cha Galilaya, na Uyahudi, na Yerusalemu; na uweza wa Bwana ulikuwapo apate kuponya.
[18]Na tazama, wakaja watu wanamchukua kitandani mtu mwenye kupooza; wakataka kumpeleka ndani na kumweka mbele yake.
[19]Hata walipokosa nafasi ya kumpeleka ndani kwa ajili ya lile kundi la watu, walipanda juu ya dari wakampisha katika matofali ya juu, wakamshusha yeye na kitanda chake katikati mbele ya Yesu.
[20]Naye alipoiona imani yao, alimwambia, Ee rafiki, umesamehewa dhambi zako.
Jicho la mwanadamu linaona uponyaji ni kutendewa muujiza wa nje, lakini kwa Mungu Uponyaji hasaa ni kusamehewa dhambi. Mtu akishasamehewa dhambi, mengine yote hufuata..
Tunasamehewaje dhambi?
Kwa kumwamini Bwana Yesu na kumaanisha kumfuata kwa toba ya kweli. Hapo ndipo tunapopokea Msamaha Wa dhambi zetu, na hatimaye uponyaji Wa mambo yetu mengine yote.
Wakolosai 1:13-14
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; [14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
[13]Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;
[14]ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;
Matendo ya Mitume 26:18
[18]uwafumbue macho yao, na kuwageuza waiache giza na kuielekea nuru, waziache na nguvu za Shetani na kumwelekea Mungu; kisha wapate msamaha wa dhambi zao, na urithi miongoni mwao waliotakaswa kwa imani iliyo kwangu mimi.
Ni ajabu Kuona, watu wanakwenda kwa Yesu na mapooza Yao, wengine katika afya zao kama huyu, wengine mapooza ya shughuli zao, wengine katika familia Zao n.k. wakitarajia Yesu awaponye kwa njia zao.
Lakini wanapokutana Na injili za wokovu na kuacha dhambi.. wanazikwepa wanakimbilia kwenye maombezi na mafuta Ya upako.
Ndugu fahamu kuwa asili ya kila tatizo ni dhambi..Mahali ambapo maisha yako yanawekwa wazi, yanamulikwa hapo ndipo uponyaji wako halisi upo. Usikimbie, usitange-tange.
Pokea kwanza msamaha wa dhambi mengine yafuate…kubali wokovu, kubali uzima, uponywe. Itakufaidia nini upate ulimwengu wote, afya yote, amani yote kisha akateketee tena jehanamu milele baadaye?
Ikiwa bado hujaokolewa (yaani hujapata msamaha wa dhambi zako) basi wakati ndio huu.. wasiliana nasi kwa namba hizi kwa mwongozo wa kumpokea Yesu.
Bwana akubariki.
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
NITAACHAJE DHAMBI?
MAFUNZO YA BIBLIA KWA WATOTO
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
Print this post
Swali: Kwanini MUNGU aliufanya mkono wa Musa kuwa na ukoma kama ishara kwa wana wa Israeli? (Kutoka 4:6).
Jibu: Turejee..
Kutoka 4:6 “Bwana akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama theluji. 7 Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake. 8 Basi itakuwa, wasipokusadiki, wala kuisikiliza sauti ya ishara ya kwanza, wataisikiliza sauti ya ishara ya pili”.
Kutoka 4:6 “Bwana akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama theluji.
7 Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake.
8 Basi itakuwa, wasipokusadiki, wala kuisikiliza sauti ya ishara ya kwanza, wataisikiliza sauti ya ishara ya pili”.
Sababu kuu ya BWANA MUNGU, kuutia mkono wa Musa ukoma na kisha kuuponya ni kutoa ujumbe kwa wana wa Israeli kuwa yeye ni Mungu awaponyaye.. Kwa hivyo wana wa Israeli walipoiona ile ishara walitambua kuwa Mungu wao ni Mungu anayeponya na kuondoa maradhi, misiba, mateso na hata utumwa..
Jambo hilo tunalithibitisha mbele kidogo katika ile sura ya 15 alipowaambia jambo hilo pale alipoyaponya maji yaliyokuwa machungu..
Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji. 23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara. 24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini? 25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko; 26 akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE. 26 kawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, MIMI SITATIA JUU YAKO MARADHI YO YOTE NILIYOWATIA WAMISRI; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE”.
Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji.
23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo jina lake likaitwa Mara.
24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?
25 Naye akamlilia Bwana; Bwana akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na hukumu huko, akawaonja huko;
26 akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE.
26 kawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, MIMI SITATIA JUU YAKO MARADHI YO YOTE NILIYOWATIA WAMISRI; KWA KUWA MIMI NDIMI BWANA NIKUPONYAYE”.
Na hata sasa bado MUNGU wetu ana sifa hiyo hiyo, “YEYE NI MUNGU ATUPONYAYE”… Ikiwa tutasikiliza kwa bidii sauti yake na kufanya yale anayotuelekeza.. Magonjwa yote hayatakuwa sehemu yetu, mateso yote hayatakuwa sehemu yetu na kila aina ya mabaya ya ibilisi hayatatutawala.
Je umempokea YESU KRISTO kama Bwana na Mwokozi pekee wa maisha yako?
Kama bado unasubiri nini?.. mwamini leo uokolewe na kuponywa.
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
FIMBO YA HARUNI!
MAMBO SITA, AMBAYO MUNGU HUTUMIA KUONDOA UOVU NDANI YA MTU.
Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?
NABII MUSA.
Mathayo 20:6
[6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Bwana Yesu alizungumza mfano ambao unagusia kabisa uhalisia wa kiroho uliopo sasa katika kazi ya Mungu (Ushuhudiaji).
Mfano huo unahusu mtu mmoja aliyetoka asubuhi sana kuajiri wafanyakazi ili kwenda kulilima shamba lake ambalo lilihitaji watu wengi kulihudumia.
Hivyo akatoka alfajiri sana, kuwatafuta na kwa bahati nzuri akawakuta, akawapeleka shambani mwake, akatoka tena saa tatu, akawakuta wengine wamekaa bila kazi, akawatuma shambani, akaenda tena saa sita na saa tisa vivyo hivyo akafanya…Mpaka ilipofika saa kumi na moja akatoka na kuwakuta watu wengine wamesimama tu toka asubuhi mpaka jioni…hawafanyi chochote wapo “Idle”
akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?
Mathayo 20:1-7
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu. [2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu. [3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; [4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda. [5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. [6]Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? [7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
[1]Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
[2]Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
[3]Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
[4]na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
[5]Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.
[7]Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.
Embu jiulize swali moja.. Je! Unadhani watu hawa wa saa kumi na moja hawapo leo?
Kukaa bila kufanya kazi ya Mungu, wakati Kazi ipo kubwa kwa kisingizio kuwa hakuna wa kukuajiri ni ulegevu kiroho… yule Bwana hakuwa na muda wa kusikiliza sababu zao, kwamba waendelee kukaa na kumalizia tu siku kwasababu muda umeenda, bali aliwatuma haraka sana shambani.
1) Hofu ya kutumika
Kusema mimi siwezi, Mimi bado mchanga kiroho, sijui biblia vizuri, Mimi bado mdogo kiumri, mimi siwezi Kuongea nina aibu, nina kigugumizi..sina fedha, sina elimu n.k…haya ndio mambo yanayowakawiisha watu wengi wasimtumikie Mungu..
Ndugu fahamu kuwa Mungu hategemei ukamilifu wetu, kutimiza kusudi lake kamilifu, bali hututumia katika hali zetu hizi hizi, hivyo usingojee siku fulani utakuwa mzoefu ndio umtumikie Mungu..haitafika, anzia na hali yako hiyo hiyo.(1Wakoritho1:26-29)
2) Kungojea muda fulani sahihi.
Kudhani Kuwa upo muda fulani maalimu utaitwa na Bwana rasmi umtumikie, hilo pia limewafanya wengi, kungoja muda mrefu na hatimaye kutoona mafanikio.. saa ya kutumika ni sasa..tayari Wote tulishaitwa tumtumikie yeye tangu siku tulipookoka..ukishaokoka umepewa na vibali vyote na mamlaka ya kumtumikia Bwana..usiongoje utokewe na Yesu kama Paulo Dameski, Usiongoje usikie sauti fulani ikikwambia nenda kawafundishe watu. Anza sasa na Bwana ataungana na wewe mbele ya safari.
3) Masumbufu ya maisha
Mizigo mingi ya kimaisha, utakula nini, utavaa nini, utaishije, linawapunguza watu kasi ya kufikiria kwamba wanahitaji kwanza kuyaandaa maisha yao yawe safi ndipo waamke kwenda kumuhubiri Kristo.
Ndicho walichokifanya wayahudi walipokuwa wanajenga hekalu la pili, ilifika wakati wakaacha ujenzi kila mmoja akaenda kwenye mambo yake, Kwasababu tu, ya kujiangalia hali zao.
Hagai 1:2-4
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA. [3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, [4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
[2]BWANA wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya BWANA.
[3]Ndipo neno la BWANA lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema,
[4]Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika?
Usingoje ufanikiwe, uoe, uwe na maisha ndio sasa uanze kuifanya kazi ya Mungu, ukijitazama Sana, hutamtumikia Mungu ndugu.. fahamu kuwa wengi wa wanaokuletea wewe habari njema sio wenye mafanikio, lakini Bwana hawaachi.
4) Ulegevu.
Kupendelea mambo ya kirahisi rahisi, zaidi ya kujitoa..wakati mwingine kukataa kutaabika kwa ajili ya injili..kutaka ijiendeshe Yenyewe, bila kuwa mfuatiliaji na mwombaji, pia hukawiisha utendaji kazi wa injili.
Hivyo, ndugu muda ni mfupi sana, tupo katika saa la kumi na moja yetu, usihudhurie tu kanisani, kuwa sehemu ya utumishi kanisani, usisikilize / kusoma tu mahubiri, hubiri na kwa wengine unachojifunza, Shamba la Bwana linatuhitaji wote.
Ni wakati wa kuamka usingizini, bado hatujachelewa, ikiwa tutatimiza kusudi la Mungu vema, basi tutalipwa sawasawa tu na wale waliowahi..Hivyo amka sasa.. anza kushuhudia.
Shiriki injili kwa kushea na wengine habari hizi
Bwana akubariki
WhatsApp
Siku moja nilikuwa nakatiza eneo fulani la biashara ambalo limechangamka sana, Ni e neo ambalo watu wengi wanapishana..ghafla kwa mbele nikamwona kijana mmoja ameinama, baada ya muda kidogo akachuchumaa, na mara akaanza kutapika matapishi mengi sana.. Uso wake ulionekana kuumwa, hivyo moja kwa moja nilipomwangalia moyoni mwangu, niliguswa sana na ile hali aliyokuwa anapitia..
Kikawaida zipo hali ambazo ukiumwa Unaweza kuzivumilika mpaka ufike mahali fulani pa matibabu..lakini kuumwa mpaka kutapika Hakuzuiliki, na kama ulishawahi kutapika unaelewa nguvu inayotumika, hali unayouisikia wakati huo.. ni kama nusu ya kufa..
Sasa sisi ndivyo tunavyomfanya Mungu, ajisikie muda wote tunapokuwa Na aina ya mwenendo wa uvuguvugu maishani mwetu, .alisema hivi;
Ufunuo wa Yohana 3:15-19
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. [16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. [17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. [18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. [19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
[15]Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
[16]Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
[17]Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
[18]Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
[19]Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Uvuguvugu ni ile hali ya kuwa mtu wa kidini na sio wa kiroho, unahudhuria ibada lakini mabadiliko huna, unavaa vizuri kanisa lakini ukiwa nje unavaa nguo zisizo na adabu, unaimba kwaya, lakini wakati huo huo unasikiliza nyimbo za kidunia, ni mtumishi mzuri wa kanisani lakini bado unaishi na mume wa mtu..
Maisha ya uvuguvu, yanamtesa Kristo isivyo kawaida..Ikiwa wewe hupendi kutapika- tapika Kwanini wewe umfanye Mungu kuwa na hali hiyo?
Ukristo ni mwendelezo sio tukio…eti mimi nimeshamkiri Yesu kwa Kinywa..inatosha nimeokoka, hapana…bali ni ukuaji wa kiroho.. ni lazima uonyeshe ukuaji…kitu chochote kilicho hai kinakua…lakini kuwa mtu yule yule kila siku wewe ni vuguvvugu.
Kanisa La Laodikia, lilikuwa na sifa ya kujiona ni tajiri Kisa Lina vyombo vizuri vya miziki, lina Makongamano makubwa ya nje, lina mwonekano wa kuvutia, lina umaarufu, Lakini Yesu aliliona si la kiroho hata kidogo..Linamheshimu Mungu kwa nje tu, lakini ndani limepoa zaidi ya barafu..
Hizi ni nyakati ambazo watu wengi wanazisahau ibada za kweli, wanatafuta fedha na Midundo inayovutia masikio ya watu lakini hawajali ujumbe wa rohoni au ‘uzuri Wa utakatifu’.
Na watu ambao wakiwaona wengine wamesimama kikamilifu mbele za Mungu wanawaita “walokole” …
Embu tubu, rafiki…uzuri wako, mwonekano wako, Sifa zako, udunia wako, havina ushirika na Kristo, hizo status zisizo na staha na elimu, unampostia nani mitandaoni? Hiyo mitandao ya kizinzi unayoitembelea kila siku, na kujichua unakoendelea nako kwa siri na wakati huo huo unasema umeokoka, nini unakiunda kama sio kumfanya Bwana atapike?…maanisha kumpokea Kristo. Simama katika imani, ili umwone Mungu wa kweli na sio sanamu.
Kumbuka hizi ni nyakati za kusimama kikamilifu, kwasababu mwisho umekaribia..Unyakuo Ukipita watakaokwenda na Bwana ni walio moto tu, na sio vuguvugu.
Kutubu ni kugeuka…Geuka tu leo kwa kumaanisha na Bwana atakusamehe kabisa na kuanza na wewe..Ikiwa hujaokoka na upo tayari leo kufanya hivyo…Basi wasiliana nasi kwa mwongozo sala sala ya Toba..
NAYAJUA MATENDO YAKO.
Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.
Nini maana ya kumwabudu Bwana katika uzuri wa utakatifu?
Mtambo kwenye biblia ni neno linalomaanisha aidha kifaa kinachonasa kitu, au kinachorahisisha kazi Fulani.
Kwamfano tukisoma
Ayubu 18:9
[9]Tanzi litamshika kisigino chake, Na mtambo utamgwia.
Hapo ni Bildadi rafiki yake Ayubu anaeleza hatma ya mtu mwovu, anasema ni sawa na mtu atembeaye katika njia ya mitego, na ghafla hunaswa asiweze kunasuka ndio mtu mwovu katika njia zake mbaya hukumbwa na hayo.
Anasema mtambo utamgwia, maana yake kitu kinasacho Kitamkamata.
Neno hilo pia utalisoma…kwenye mistari ya juu yake..Bildadi anasema..
Ayubu 18:2
[2]Je! Hata lini utayategea maneno mitambo? Fikiri, kisha baadaye tutanena.
Akitumia lugha ya picha…
akimaanisha hata lini utayanasa maneno yako? (yaani utaacha kuongea?).
Lakini sehemu nyingine Inayolitaja Neno hili Ni..
2 Mambo ya Nyakati 26:14-15
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo. [15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
[14]Uzia akawafanyizia jeshi lote ngao na mikuki, na chapeo, na deraya za madini, na nyuta, na mawe ya kupiga kwa teo.
[15]Akafanya katika Yerusalemu mitambo ya vita, iliyobuniwa na watu wastadi, iwekwe juu ya minara na juu ya buruji, ili kutupa mishale na mawe makubwa. Jina lake likaenea mbali sana; kwa kuwa alisaidiwa mno ajabu, hata akapata nguvu.
Inazungumzia nguvu za kijeshi alizokuwa nazo mfalme Uzia, hata kufikia kubuni mitambo mikubwa ya kivita.. ya kufyatulia silaha kwa maadui zake.
Je umeokoka?
Kumbuka saa Tulizopo ni za majeruhi, siku yoyote wakati wowote Kristo anarudi jiulize umejiandaaje ndugu?. Unyakuo wa kanisa ukipita leo utakuwa wapi mpendwa…
Jitathmini maisha yako? Itakufaidia nini uupate ulimwengu wote na mambo yake halafu upate Hasara ya nafsi yako. Tubu mgeukie Kristo uoshwe dhambi zako, upokee uzima wa milele.
Ikiwa upo tayari kumpokea Yesu leo.. basi fungua hapa kwa mwongozo Wa Sala ya Toba.. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Haya ni mafundisho maalumu kwa viongozi aidha wachungaji, au wasimamizi ndani ya kanisa..Maadamu una kundi la watu aidha 2-3 au zaidi la kuwasimamia, basi mafunzo haya yatakusaidia sana.
Kutoka 32:9-10
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu [10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
[9]Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu
[10]basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu.
Mungu alipomuita Musa kwenda kuwaokoa watu wake, alijua asili Ya hao watu watakuwa ni wa namna gani. Pengine Musa alidhani anawaokoa watu ambao ni wema sana, watulivu, na wapole.
Lakini mambo hayakuwa kama hivyo, licha ya kuona miujiza mikubwa namna ile, bahari kupasuka, mana kushuka Mbinguni, miamba kutoa maji, nguzo ya moto kuwaongoza usiku kila siku…
Bado walitengeneza sanamu za ndama na kusema hii ndio miungu yetu iliyotutoa Misri tuiabudu..walinung’unika, walimsengenya kiongozi wao, waliasi na kujiundia Makundi..Ni watu ambao walikuwa ni wagumu kuongoza, wazito kutii na wapesi kulalamika.
Ni vema kujua kuwa kila kiongozi wa kweli kuna siku atapitia kama Musa alivyopitia..
Ikifikia hatua hii wengi wanasema kama utumishi ndio huu ni heri niache, kama naonyesha fadhila zote hizi kinyume chake narudishiwa masengenyo na uasi, ni heri niache…
Ukifikiri hivyo bado hujawa kiongozi, Mungu alijua asili yao kwamba ni watu wenye shingo ngumu..alijua Yuda ni msaliti lakini bado alimpatia mwanae, amchunge.
Hao hao bado aliwaokoa na akataka wachungwe..
Shingo ngumu ni mtu wa namna gani?. Ni mtu anayefananishwa na ng’ombe ambaye hataki kufungwa Nira na Bwana wake…shingo inakuwa ngumu kuvishwa nira..
Hii ni aina ya watu ambao Hawana utii, hawachungiki, hata waone miujiza mikubwa namna Gani, hata wasaidiweje, si rahisi kuacha tabia zao za usengenyaji, wizi, uasi. Kiburi N.k.
Lakini bado Mungu anawaacha chini ya mchungaji waangaliwe..
Musa alikutana na waabudu sanamu, wanung’unikaji, Na wasahaulifu wa fadhili za Mungu…
Lakini alifanyaje?
Hata pale ambapo Mungu alitaka kuwaangamiza Musa aliwaombea. Alisimama kufanya upatanisho kwa ajili yao.
Ni ujumbe gani tunapewa?
Kiongozi wa kweli badala ya kughahiri kumchunga kondoo wake humwombea kwa bidii ili Bwana amponye asipotee kabisa kwenye dhambi.
Kiongozi wa kweli, huwa tayari hata kupoteza maisha yake kwa kondoo wake.. Musa alisema..
Kutoka 32: 32 Walakini sasa, ikiwa utawasamehe dhambi yao – na kama sivyo, unifute, nakusihi, katika kitabu chako ulichoandika.
Uongozi sahihi sio Kuongoza Watu wakamilifu, lakini kuongozo Watu dhaifu Kwa Mungu mkamilifu.
Uongozi Sahihi huweka katika uwiano sahihi “neema na kweli”
Ni vema kufahamu pia si kila wakati Musa alikuwa anasimama kuwatetea Waovu, hapana wakati mwingine aliruhusu upanga wa Mungu upite, Ili dhambi iogopwe…utakumbuka wakati ule walipotengeneza Sanamu ya ndama, na hasira Ya ki-Mungu ilimvaa Musa, ndipo Akazivunja zile mbao mbili, kisha awaita watu walio upande wa Bwana wamfuate, Na wale waliosalia waliadhibiwa vikali kwa mauti.
Dhambi iwapo kanisani, haipaswi kuvumiliwa..Kutoa adhabu na wakati mwingine kuwaondoa wale wabaya ndani ya kundi ili lisiendelee kuharibiwa..
Lakini katika yote wewe kama kiongozi, huna budi kujifunza Uvumilivu, kuwaombea kondoo wako, na kuwa mpole, lakini pia kushughulika na dhambi Vikali katika nyumba ya Bwana.
Lakini kumbuka ijapokuwa Ni kazi, yenye mapito mengi ya masumbufu na maumivu Lakini thawabu yake na faida yake haifananishwi na gharama ulizoingia.. Hivyo penda kuchunga watu wa Mungu…Ndio heshima ya juu ya upendo kwa Mungu wako.
Mithali 14:4
[4]Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe; Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.
TEMBEA NDANI YA SUKOTHI YAKO.-Maafundisho maalumu kwa watumishi
TOFAUTISHA KATI YA MAFUNDISHO YA YESU, NA YA WAANDISHI.
MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.
Huu ni mfufulizo wa mafunzo maalumu ya wazazi kwa watoto..
Ukiwa kama mzazi, Njia bora ya malezi, sio kumjali mtoto wako, kwa kila kitu sasa.. Hata kama ni haki yake kukipata, Usiwe mwepesi kumfanyia kila jambo leo hata kama una uwezo wa kumfanyia, Usimjali sasa, mjali kwa baadaye. Tumia nguvu hizo kumwekezea kwa baadaye lakini sasa shughulika naye kitabia, kinidhani, ki-utu..Acha hiyo tabia ya kujali-jali utamuharibu mtoto.
Wengi wetu tunashindwa kujua, kuwa ni kanuni ya ki- Mungu mtoto aishi kama mtumwa, hata kama yeye ndio mrithi wa yote.
Wagalatia 4:1 Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote; 2 bali yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba
Mzazi mwenye Akili na maono bora kwa wanawe, haangalii mali zake anazitumiaje kwa mwanawe sasa, bali huangalia tabia gani anamjengea leo, ili kesho aweze simama vema maisha yake, au mali zake.
Embu fikiria vema, yule Baba Tajiri aliyekuwa na wana wawili, ambao kwa siku nyingi waliishi na baba yao bila kuona faida ya utajiri wa baba yao. Mpaka siku moja mmojawao (yule mdogo) uzalendo ukamshinda, akamwambia baba yake nipe sehemu ya mali yangu inayoniangukia, hatimaye akapewa akaondoka, lakini maisha yaliyopo-mgeukia hali ikawa mbaya, mwishowe akazingatia kurudi kwa baba yake. Na baba yake akampokea akamfanyia karamu kubwa. Lakini yule mwana mwingine aliporudi mashambani, na kuona sherehe kubwa kwa ndugu yake, akachukizwa, ndipo akamwambia baba yake “Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wo wote, Lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu;”
Tusome;
Luka 15:11-31
11 Akasema, Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; 12 yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. 13 Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati. 14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. 15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. 16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. 17 Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. 18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; 19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. 20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. 22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; 23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi; 24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia. 25 Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. 26 Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? 27 Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. 28 Akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi babaye alitoka nje, akamsihi. 29 AKAMJIBU BABA YAKE, AKASEMA, TAZAMA, MIMI NIMEKUTUMIKIA MIAKA MINGAPI HII, WALA SIJAKOSA AMRI YAKO WAKATI WO WOTE, LAKINI HUJANIPA MIMI MWANA-MBUZI, NIFANYE FURAHA NA RAFIKI ZANGU; 30 lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona. 31 Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami sikuzote, na vyote nilivyo navyo ni vyako.
Nataka uone sifa ya huyo baba, kwa wanawe, ijapokuwa alikuwa na mali, lakini hakutaka Watoto wake, waishi kwa mali zake, bali waishi kama watumwa wengine. Sio kwamba alikuwa anawatesa, Hapana, alikuwa anawatengeneza ili baadaye wakishajua maisha hasaa ni nini kivitendo, ndipo awaache huru, wapewe vyote na baba yao, wafurahie maisha wayapendayo.
Leo hii imekuwa kinyume chake, utaona mtu ndiye anayetumia nguvu zake, na mali zake, kumdekeza mtoto, kama yai, kumletea wafanyakazi ndani, wawapikie, wawafulie, wawapigie deki, na pasi, wenyewe wakae wakitazama muvi Netflix, na kucheza magemu, kwenye Ipad, na computa,
Akidhani anamlea mtoto, kumbe anamlea mwana-mpotevu. Mtoto akikosea tu, hawezi kuadhibiwa, mzazi anasema sitaki mtoto wangu ateseke kama mimi nilivyoteseka, kwani ni nani kakwambia mtoto akiadhibiwa ni lengo la kuteswa? Watoto hawafundishwi kufunga, hata kwa sehemu (nusu siku), au kupelekwa mikesha mara moja moja wajifunze kanuni za kiroho, wazazi wanasema hawa bado wadogo. Hivi ni kazazi gani tunakilea??
Si lazima kila siku ale mboga saba, si lazima umpe chakula anachokitaka yeye, siku nyingine fululiza ugali maharage, wiki mbili nyumbani, mwache alie, mpaka azoee..Mambo kama hayo unaweza kuona unamtesa mtoto, lakini ndio njia sahihi ya maleza..unamtengeneza mtu imara sio lege-lege.
Likizo inapofika, kuliko kumpeleka beach kwenye mapembea, na masherehe, mpeleke kijijini kwenu, aone mazingira ya asili, ale vyakula vya kule, atumie vyoo vya kule ambavyo sio vya kuflash, aende akakatie ng’ombe majani, aende na wafungaji machungaji akae huko mpaka likizo iishe, ndipo arudi..
Lakini wewe mwenyewe huku nyuma unajua ni nini unafanya, ukimwandalia akiba, nzuri, ili baadaye atakapoelimika kiroho na kimwili, ukimpa vya kwako, au ukimdekeza atakavyo, ataweza kujisimamia mwenyewe, na kuwa mtu mkakamavu thabiti, na Jasiri, mwenye utu na kiongozi awezaye kuishi katika jamii, na kuwajali na walio wanyonge na wenye shida.
Hayo ndio malezi bora ya mtoto. Mfanye leo mtumwa ili kesho awe mfalme, lakini ukichagua kumfanya leo mfalme, jiandae kesho kuwa mtumwa mfano wa mwana- mpotevu.
Mithali 22:6 Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee
NI NINI KINATOKA KINYWANI MWA MTOTO WAKO?
MRUDI MWANAO NAYE ATAKUSTAREHESHA
NAFASI YAKO WEWE MAMA KWA MTOTO NA WAJUKUU WAKO NI IPI?.
SWALI: Tumekuwa tukisikia kuwa mtu akifa, huko aendako anakutana na mateso makali ya jehanamu. Sasa napenda kufahamu je ni roho ndio itakayoteketezwa au na miili pia?
JIBU: Maandiko yanatueleza siku ya mwisho ya hukumu, wafu wote watafufuliwa. (Iwe ni wema au waovu), wote watairudia miili yao ya asili yaliyokuwa nayo duniani.
Yohana 5:28
28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu
Ufunuo 20: 12-13
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake
Waliokufa katika Kristo (Watakatifu) watavikwa miili mipya ya utukufu, isiyoharibika (1Wakorintho 15:42-54) lakini waovu watakuwa na miili yao ya asili. Ambayo katika hiyo watahukumiwa na kutupwa katika lile ziwa la moto, lililo maalumu kwa mateso ya mtu milele.
Hivyo ni vizuri ifahamike, kuwa kitakachoteketezwa sio roho tu, bali na mwili pia, Bwana Yesu aliliweka hilo wazi katika maneno haya;
Mathayo10:28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Umeona hapo?.. Awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum. Kuonyesha kuwa mwili nao utashiriki mateso ya milele.
Tukishayajua hayo, tunapaswa tufanyaje?
Je! Umemwamini Bwana Yesu ndugu? Wokovu ni sasa, mgeukie akuponye, uwe salama, hata ukifa uwe na uhakika wa kuurithi uzima wa milele, Itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima, kisha upate hasara ya nafsi yako? Fanya uamuzi wa busara.
Okoka, leo uponywe. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya Toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA
MWOMBENI BWANA WA MAVUNO APELEKE WATENDA KAZI.
MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE.
Mtume Paulo, alipokamatwa kule Yerusalemu na kupelekwa mbele ya wafalme kuhukumiwa, tunaona ujasiri wake ulikuwa wa ajabu, badala atumie nafasi ile kujitetea, kimahakama, kinyume chake alitumia nafasi ile kuhubiri injili, kiasi cha kumfanya mfalme Agripa kushawishwa kwa muda mfupi kuiamini injili.. Ujasiri wa namna hiyo hakika, ni wa kuigwa sana.
Matendo 26:28
25 Lakini Paulo akasema, Sina wazimu, Ee Festo mtukufu, bali nanena maneno ya kweli na ya akili kamili. 26 Kwa maana mfalme anajua habari za mambo haya, nami naweza kusema naye kwa ujasiri, kwa sababu najua sana ya kuwa hapana neno moja katika hayo asilolijua; kwa maana jambo hilo halikutendeka pembeni. 27 Mfalme Agripa, je! Wawaamini manabii? Najua ya kuwa wawaamini. 28 AGRIPA AKAMWAMBIA PAULO, KWA MANENO MACHACHE WADHANI KUNIFANYA MIMI KUWA MKRISTO. 29 Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe kama mimi, isipokuwa vifungo hivi.
Lakini Tunaona jambo moja, huyu mfalme Agripa alichomwa sana na maneno ya mtume Paulo, alishawishwa ipasavyo na injili ile, lakini hakuwa tayari kugueka moja kwa moja kwa Kristo, aliishia tu kushawishwa.. Ukweli ni kwamba mtu katika hatua hiyo bado hujaokolewa..
Ni sawa na leo hii, watu wengi wanapoisikia injili, ni kweli wanashawishwa, wanaiheshimu, wanaifurahia, wanachomwa mioyo yao, wengine wanaomboleza na kuhuzunika juu ya dhambi zao, lakini je! Wameikubali na kutii?
Utaona wataishia tu kusema, nimebarikiwa!, wataishia kusema Neno zuri linaonya!, wataishia kusema, Mungu nisaidie, nimeguswa leo, ndugu hiyo haimaanishi kuwa umeokoka, huna tofauti na Agripa.
Watu walioshawishwa kwelikweli, waliochomwa mioyo, ni lazima utaona kuna kitu cha ziada watafanya watauliza “Tufanyeje ndugu zetu?”
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Umeona?, hawakuishia tu kusema “asante Petro kwa Neno” hawakuishia kusema “ubarikiwe mtumishi” ..“Umetujenga mchungaji”. Walisema, tutendeje ndugu zetu?..Tuchukue hatua gani?
Utaona Wakabatizwa, wote siku ileile, wajazwa Roho, Wakadumu katika fundisho la mitume, kila siku. Ndio hao walioisambaza injili ulimwenguni kote.
Leo ndio tunahitaji kuona Kundi la watu wa namna hii, ambao wanachukua hatua ya kumpokea Yesu kikamilifu na kumfuata kwa mioyo yao yote, kimatendo. Na sio kama akina Agripa, ambaye hakuwa na matunda ya kuitii injili.
Saa ya wokovu ni sasa, usiseme kesho nitaokoka, hakuna wokovu wa kesho, acha kujidanganya, bali ni leo. Aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi usifurahie mafundisho, usifurahie miguso ya ki-mahubiri swali ni je umeokoka? Kristo leo akirudi utaenda naye?
Na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
WOKOVU NI SASA
Sauli (Mtume Paulo) alipokuwa anaelekea Dameski kwa lengo la kuwafunga na kuwatesa watakatifu, kama tunavyoifahamu habari alitokewa na Yesu njiani, mwanga Mkali ulimpiga machoni, akashindwa kuona, Wakamchukua mpaka ndani ya mji akiwa kipofu.
Lakini tunaona alipokuwa kule, hakuwa katika hali ya kawaida, bali katika maombolezo makubwa rohoni, hakula chakula chochote, wala maji..(maana Yake alikuwa katika mfungo), lakini si hilo tu zaidi sana alikuwa akiomba dua.
Baada ya hapo tunaona jambo lingine likitokea mtu mmoja aliyeitwa Anania anatokewa na Yesu, kisha anaagizwa amfuate Paulo. Lakini eneo analoagizwa ni katika njia iliyoitwa NYOFU…
Maana Yake “njia iliyonyoka”.
Matendo 9:8-12
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. [9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi. [10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. [11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; [12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
[9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.
[10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.
[11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;
[12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Unaweza kujiuliza kwanini apelekwe njia ile ..tena iitwe kwa jina la NYOFU na si lingine labda “njia kuu”, au “nzuri” au “panda” bali nyofu?
Ni kwasababu rohoni, Kristo huwaweka watu wake Katika hiyo njia. Njia iliyonyoka.
Hapo mwanzo Paulo alikuwa katika njia iliyoharibika, mbovu, ya kuupinga ukristo, ya uuaji, ya utukanaji, ya dhambi, ya mauti.
Lakini alipokutana na YESU, akatolewa huko akawekwa katika njia iliyonyooka ya utumishi wake.
Ni ajabu kuona watu wengi leo wanampinga Kristo, hawataki kuokoka, wakidhani udini ndio utawanyooshea mapito yao, fedha ndio zitawasawazishia mabonde Yao, elimu ndio zitaangusha milima yao.
Kumbe hawajui kuwa njia iliyonyooka ni maisha ndani ya Kristo tu!. Kwingine kote ni mabonde, milima Na mwishowe shimoni na mauti. Hakuna pumziko Nje ya Kristo.
Yohana mbatizaji aliliona hilo akapaza sauti yake kwa nguvu Akisema..
Yohana 1:23
[23]Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
Kumwamini Yesu ndio kuinyoshe njia ya Bwana..
Je upo katika njia ya nyofu.
Okoka leo, uponywe kila kitu ndugu, kumbuka Umepotea nje ya Kristo,hakuna mjadala na huo ndio ukweli, hakuna tegemeo kama Yesu hajakuokoa. Fanya haraka utubu, leo uiamini kazi ya Kristo ya ukombozi iliyokamilishwa kwa ajili yako pale msalabani. Muda ni mchache mlango wa neema hautadumu Milele.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Yesu maisha yako. Basi bofya bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Jehanamu ni nini?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.