Jina la Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze pamoja Biblia.
Bwana alipokutana na Petro aliambiwa “TANGU SASA UTAKUWA UKIVUA WATU”. Hii ni kauli pana, ambayo ni muhimu tuijadili kwa kina kidogo..
Luka 5:10 “na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu akamwambia SIMONI, USIOGOPE, TANGU SASA UTAKUWA UKIVUA WATU”.
Luka 5:10 “na kadhalika Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, waliokuwa washirika wa Simoni. Yesu
akamwambia SIMONI, USIOGOPE, TANGU SASA UTAKUWA UKIVUA WATU”.
Hapa Bwana YESU alifananisha “Uvuvi wa Samaki” na “Uvunaji wa watu” . Kwa ufupi Bwana YESU alifananisha watu na “Samaki”… Kama vile samaki wanavyovuliwa kutoka majini hali kadhalika watu wanavuliwa kutoka upotevuni.
Sasa kama maji yanavyohusika katika “Uvuvi wa samaki” vile vile maji pia yatahusika “uvuvi wa watu” kama ishara.. na hapa ndio tunakuja kuona umuhimu wa UBATIZO.
Wengi hatuoni umuhimu wa Ubatizo katika kukamilisha wokovu, lakini Ubatizo wa maji mengi unasimama kama muhuri wa kukamilisha wokovu wa mtu (Soma Marko 16:16).
Unapobatizwa kwa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU ni ishara ya kwamba umevuliwa kutoka katika ulimwengu..
Sasa jiulize, Umeona wapi samaki anavuliwa kutoka katika nchi kavu?.. Vile vile wewe na mimi kama samaki tuliovuliwa ni lazima tuwe na ishara ya kutoka majini, ndio hapa linakuja agizo la ubatizo.
Na samaki akishatoka majini anapoteza uhai wa maisha yake ya kwanza, na vile vile baada ya ubatizo mtu anapoteza uhai wa maisha yake ya kwanza ya dhambi (maana yake yale maisha ya dhambi anayafia, anakuwa kiumbe kipya).
Je umeshabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO (sawasawa na Matendo 2:38, Matendo 10:48 na Matendo 19:5).. Kama bado unasubiri nini?.. je bado unaendelea kushikilia mapokeo ya dini na dhehebu hata baada ya kuujua ukweli wa Biblia?
Siku ile hatutahukumiwa kulingana na Mapokeo tuliyopokea bali kulingana na maneno yaliyoandikwa katika vitabu vyote sitini na sita vya kwenye Biblia..
Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.
Maneno ya Mungu ndani ya Biblia ndio yatakayotuhukumu siku ya mwisho, maana yake siku ile tutaulizwa kwa yale yaliyoandikwa kwenye biblia sio kwa yale tuliyoyapokea kwenye dini zetu..
Kwa namna gani?.. Hebu tuingie ndani kidogo kulifafanua hili..
Mtu mmoja alimfuata Bwana YESU na kumwuliza tiketi ya kuurithi uzima wa milele, hebu tusome jibu la Bwana YESU Mkuu.
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele? 26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?”
Luka 10:25 “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?”
Tazama jibu la Bwana hapa?.. hakumwambia “umerithishwa nini na wazazi, au umefundishwa nini kwenye dini yako”.. Lakini alimwambia “Imeandikwa nini” lakini sio tu imeandikwa nini, bali pia “Unasomaje”
Ikimaanisha kuwa wakati wa Mwisho, watu watahukumiwa kwa yaliyoandikwa katika Biblia..Na moja wapo ya jambo lililoandikwa katika maandiko ni ubatizo. Sasa kupuuzia agizo la msingi namna hii ni hatari sana, hatutakuwa na la kujibu siku ile, ikiwa tulijua kweli na hatukuifanyia kazi.
shetani amepofusha fikra za watu wengi katika siku hizi za mwisho, na kuwafanya wasijue wala kuona umuhimu wa ubatizo pamoja na baadhi ya mambo mengine ya msingi katika Biblia.
2Wakorintho 4:4 “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu”.
Bwana atusaidie sisi tusiwe miongoni mwao wanapofushwa fikra na ibilisi.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
AGIZO LA TOBA LINAENDANA NA UBATIZO!.
TOFAUTI YA UBATIZO WA YOHANA NA UBATIZO WA BWANA YESU
Ni sahihi kusema sikuitiwa kuhubiri ubatizo kama Paulo alivyosema (1Wakorintho 1:17)?.
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
WOKOVU UKIHARAKISHA USIUZUIE.
Print this post
Kuishi ni tufoauti na kuwa na uhai. Hata mti ni hai, lakini hauishi. Kuishi ni maisha, yaani unasifa ya kuwa na mfumo au ustaarabu Fulani ambao unatembea nao, unaweza kuchagua mahali pa kukaa, unafanya kazi, unapumzika, unajenga, unapanda, unajichagulia burudani mfano miziki, michezo, vyakula, unafanya ibada, unauza, unanunua.. mambo kama hayo kiumbe kikitenda tunasema kinaishi.
Lakini kuwa kifungoni, ndani ya gereza huoni jua wala mwezi siku zako zote uwapo duniani, hatuwezi kusema unaishi, tunasema wewe upo hai, lakini hauishi.. Au unapokaa kwenye kitanda cha wagonjwa mauti-uti, umepooza, huwezi kuongea wala kutembea, umekata kauli, kwa sikuzote uwapo duniani, hayo si maisha ijapokuwa upo hai.
Sasa kuna maneno Yesu aliyasema, ambayo si wengi hujaelewa kwa undani na upana.. Tusome;
Yohana 11:25-26
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Hii kauli ukiisoma vizuri, unaweza ukasema inajichanganya, Embu tafakari, jambo la kwanza Yesu anasema, tukimwamini tukifa tutakuwa tunaishi, lakini pia tukiwa hai na kuamini hatutakufa kabisa hata milele.
Je! Sisi tuliomwamini hatufi?
Jibu ni Ndio hatufi kabisa, bali tunahamishwa makao. Hicho kinachoitwa kifo, ni macho ya wanadamu yanaona hivyo, lakini sisi tunakuwa kama tumefumba macho, kisha tukafumbua na kujikuta katika ulimwengu mwingine kabisa, Ndio maana lugha ambayo hutumika kueleza hali hiyo kwa watakatifu ni kulala (Matendo 7:54-60, 1Kor 15:51-58, Yohana 11:11-19)
Sisi tuliomwamini Yesu hatutaona kitu kinachoitwa kaburi, wala hatutajikuta kwenye gereza Fulani , bali kwenye ulimwengu mwingine mzuri sana uitwao pepo, sio tukiwa hai, bali tukiwa tunaishi kabisa huru.
Maana yake, tunaendeleza maisha, ikiwa kuna kutembea, huku na huko au kushughulika kwa vitu vya kimbingu, kufanya hivi, kufanya vile..Tutakuwa tunayafanya. Hayo ndio maisha anayosema mtu akimwamini yeye, ajapokufa (lala), atakuwa anaishi.. Si atakuwa na uhai
Tutakaa huko pepo, kwa kipindi chote, ambacho tunamsubiria Yesu, kulikamilisha kusudi la watakatifu wote, kisha baadaye,(mwisho ukifika), atakuja mwenyewe kuwachukua walio hai Pamoja na miili yetu tuliyoiacha duniani, na sote kwa Pamoja tutaanza ziara mpya ya kuelekea mbingu ya tatu. Makao yetu ya milele yalipo (2Wakorintho 12:2-4)
Lakini waovu wanapokufa, wenyewe watajiona kwanza wakiingia makaburini, kisha wakishuka kuzimu, Uhai wao ukitunzwa kwenye vifungo vya giza wasijue chochote, wala wasitende kazi yoyote, mpaka siku ya hukumu itakapofika, ambapo watatolewa huko kisha watasimama kwenye kiti cha enzi cheupe cha mwana-kondoo kwa ajili ya hukumu, (Ufunuo 20) baada ya kuhukumiwa ndipo watakapotupwa kwenye ziwa la moto, na kuangamia milele.
Sasa wakiwa huko kuzimu, ambapo kwa jina lingine kunaitwa Jehanamu, ni mahali pa shida, dhiki nyingi na mateso yasiyoelezeka, huko hakuna maisha, ni mateso tu vifungoni.
Hivyo ndugu, unapomwamini Yesu ipo faida kubwa zaidi ya unavyofikiri, unapokea MAISHA YA MILELE, Tangu ukiwa hapa duniani, ndani yako hakuna kitu kinachoitwa kifo, wala hutakihisi hata kidogo. Kwanini leo usimkaribishe maishani mwako? Ikiwa upo tayari basi wasiliana nasi kwa namba hizi kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba, bure.
Au sema sala hii kwa Imani, na Moja kwa moja Yesu ataingia moyoni mwako.
Bwana akubariki
AINA ZA FARAJA BWANA AZIACHILIAZO KWA WATUMISHI WAKE.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
ASIYEMPENDA BWANA NA AWE AMELAANIWA.
WhatsApp
Maisha ya Imani, hayafuti dhiki, hayafuti hisia za kibinadamu, haijalishi mtu atakuwa na ukomavu mkubwa kiasi gani, bado mahangaiko ya ndani na nje, zipo nyakati atakutana nayo.
Mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo, pamoja na kuwa walitumiwa na Mungu kipekee sana na neema ya Mungu kubwa kukaa juu yao. Bado walikiri kwa wazi kabisa bila maficho dhiki ziliwasonga kote kote,
2 Wakorintho 7:5
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu.
Paulo anasema nje kulikuwa na vita, maana yake maadui, walioshindana naye, kuipinga imani, kutaka kumuua, kumfunga walikuwa ni wengi sana…lakini pia ndani anasema kulikuwa na hofu si nje tu,..akiwa na maana hofu ya kwenye nafsi..mfano wa hizi ni kama vile hofu za majukumu, hofu za kusalitiwa, hofu za kuvunjwa moyo, kuachwa peke yako, za kuvamiwa na wezi, mashaka ya ugenini, kushtakiwa, hofu za mwili kudhoofika, kuugua n.k. ambazo kimsingi kazi yake ni kukufanya ukate tamaa, usisonge mbele, usizae matunda.
Ndivyo ilivyo hata kwa watumishi wa Mungu wa kweli leo, mbele ya macho ya watu wanaweza kuonekana ni watu walio- mbali na mateso, lakini kwa mujibu wa kibiblia mioyoni mwao, vipo vita vingi na hofu kote kote…
Sasa swali ni je! Wanaweza kuishi na kuendelea na imani au huduma bila kukata tamaa wakiwa katika viwango vilevile ilihali nje vita ndani hofu?
Jibu ni kuwa Bwana..huwatumia faraja kwa njia mbalimbali, na faraja hizo ni kama zifuatazo;
Paulo katika dhiki zake anasema;..Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
2 Wakorintho 7:5-7
[5]Kwa maana hata tulipokuwa tumefika Makedonia miili yetu haikupata nafuu; bali tulidhikika kote kote; nje palikuwa na vita, ndani hofu. [6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito. [7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
[6]Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.
[7]Wala si kwa kuja kwake tu, bali kwa zile faraja nazo alizofarijiwa kwenu, akituarifuhabari ya shauku yenu, na maombolezo yenu, na bidii yenu kwa ajili yangu, hata nikazidi kufurahi.
Ni ukweli usiopingika zipo nyakati ambazo unajihisi kama kuishiwa nguvu ya kuendelea aidha na wokovu au huduma, kwasababu ya hali fulani ngumu zinazokuzunguka..
Majira kama haya, Mungu hufanya njia, habari njema za faraja zinaweza kukufikia na kukutia nguvu na hatimaye kuendelea mbele kwa hamasa mpya.
Kwamfano Paulo alikuwa katika nyakati hizo mbaya, akiona kama taabu yake kwa Mungu ni bure, hakuna matunda, lakini ghafla analetewa taarifa na Tito ya wanafunzi wake huko Korintho wamebadilika, wamesimama imara zaidi sana wana shauku naye. Hilo lilimtia nguvu tena hata kujiona tena hayupo katika dhiki.
Kwamfano unaweza ukawa unafanya huduma kwa muda mrefu, na pengine huoni matokeo uliyoyategemea, lakini ghafla unakutana na mtu anakuambia nimebadilishwa sana na huduma yako au mafundisho yako. Wakati ule unafanya maombezi nilipona ile ugonjwa, ulipokuwa unahubiri niliguswa moyoni na sasa nimeokoka.
Hiyo ni faraja kubwa sana, na kama ulikuwa umelegea unaamka tena unasema…oh! Kumbe Bwana yupo pamoja nami.
Nyakati za uzito, nyakati za dhiki, Bwana huachilia mafunuo kwa njia mbalimbali ili kukufariji katika wokovu wako au huduma yako aidha anaweza kutumia ndoto au maono, au Neno, au hata fundisho fulani kama hili unalolisoma sasa…
Paulo alipokuwa kama mfungwa anaelekea Rumi, njiani Meli ilipata shida mpaka wakakata tamaa ya kuishi..lakini Mungu alimtokea na kumtia nguvu kwa maono.
Matendo ya Mitume 27:23-24
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, [24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
[23]Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
[24]akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
Ni kawaida ya Mungu, kutufariji kwa njia za mafunuo, wewe ni mchungaji Bwana kukuonyesha ukichunga watu wengi, litakuwa ni jambo la kawaida, au anaweza kukupa andiko ambalo, litakupa sababu ya kusimama au kuendelea mbele. Au wakati mwingine hata kutumia mtumishi wake kukufundisha, na lile fundisho likawa ni nanga kubwa sana kwako, kutembea katika aina yoyote ya mapito.
Hii ni namna nyingine ambayo Mungu huwafariji watumishi wake, huwafungulia milango ya kifedha, aidha kusaidiwa na watu wa amani mahali fulani kimahitaji.
2 Wakorintho 11:9
[9]Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu; nami katika mambo yote najilinda nafsi yangu nisiwalemee hata kidogo; tena najilinda.
Ni kawaida ya Mungu, nyakati fulani kufungua milango ya kupokea vitu kwa watu wake, lengo lake ni kukufariji, kukutia moyo ili usonge mbele katika kazi yake.
Hii ni njia nyingine ambayo Bwana huitumia sana, kutukumbusha mioyoni mwetu kuwa hizi taabu ni za kitambo, Bwana wetu ametuandalia makao na siku moja atarudi, nasi tutaishi naye milele na milele mbinguni.. katika maisha ya milele yasiyokuwa na fujo..Bwana anataka tuyakumbuke hayo, tufarijike.
1 Wathesalonike 4:16-18
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. [17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. [18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
[16]Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.
[17]Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.
[18]Basi, farijianeni kwa maneno hayo.
Sikuzote kumbuka kuwa furaha yetu, urithi wetu, utajiri wetu upo kule ng’ambo unatungoja, hapa duniani ni wasafiri, hivyo hatutaona shida tuwapo katika dhiki za muda mfupi…Ni sawa na umeingia katika nyumba ya wageni, halafu ukaona mazingira si safi, aidha ya choo au vyumba..huwezi kulalamika na kuanza kusoneneka na kutaabika sana, kana kwamba umeingia kwenye matatizo makubwa…hapana utavumilia tu.kwasababu unajua hapo sio kwako, unapita tu utalala siku moja kesho yake utaondoka..na kurudi kwako palipo pasafi..hivyo utavumilia.
Bwana akutie nguvu. Songa mbele katika imani.
Amen.
MAANA HUYAWAZI YALIYO YA MUNGU, BALI YA WANADAMU
WALAKINI MIMI SI PEKE YANGU.
LAKINI DAUDI ALIJITIA NGUVU KATIKA BWANA, MUNGU WAKE.
Je unajua “Kumpenda Mungu sio Ombi bali ni Amri”?..Tofauti na inavyodhaniwa leo kuwa kumpenda Mungu ni jambo ambalo ni “Ombi”.. Kwamba tunaombwa kumpenda Mungu.. Lakini Biblia haitufundishi hivyo.
Biblia inatufundisha kuwa kumpenda Mungu ni Amri, (maana yake tunaagizwa kumpenda Bwana Mungu wetu kwa roho zetu zote) na pasipo kufanya hivyo ni makosa..
Mathayo 22:35 “Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu; 36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? 37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. 38 HII NDIYO AMRI ILIYO KUU, TENA NI YA KWANZA”
Mathayo 22:35 “Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
38 HII NDIYO AMRI ILIYO KUU, TENA NI YA KWANZA”
Ni madhara gani yanayoweza kumpata Mtu, anapoivunja hii amri na kumpenda miungu mingine?
Madhara yapo mengi ikiwemo kuukosa uzima wa milele katika siku ya mwisho, lakini katika maisha haya dhara lake kubwa kuliko yote ni LAANA!.
Mtu asiyempenda Bwana MUNGU wake, anajiletea laana juu yake, na uzao wake na vyote alivyonavyo..
1Wakorintho 16:22 “Mtu awaye yote asiyempenda Bwana, na awe amelaaniwa. Maran atha”.
Jifunze kumpenda Mungu kwakuwa yeye ndiye aliyekuumba.
Ukimpenda utamkaribisha YESU maishani mwako,
> Ukimpenda utaacha hizo dhambi unazozifanya (Zaburi 97:10)
> Ukimpenda utatafuta kujua kusudi lako kuja duniani ni lipi
> Ukimpenda hutaendelea na maisha ya uvuguvugu
> Ukimpenda hutafanya matambiko na mila
> Ukimpenda hutaabudu sanamu wala kudharau maagizo yake.
Ukimpenda utafanya yote yaliyoandikwa katika Biblia.
Kwa mapana kuhusiana na jinsi ya kumpenda Bwana kwa moyo wote, roho yote, nguvu zote na akili zote, fungua link hii hapa chini. >>
Nini maana ya kumpenda Bwana kwa moyo,roho, akili na nguvu zetu zote?
Zaburi 145:20 “Bwana huwahifadhi wote wampendao, Na wote wasio haki atawaangamiza”.
MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.
UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.
NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?
UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA;
JE UNAO UHAKIKA BWANA YESU AKIRUDI LEO UNAKWENDA NAYE?.
Je ni mafuta gani umepakwa?.
1 Yohana 2:26 “Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27 Nanyi, MAFUTA YALE MLIYOYAPATA KWAKE YANAKAA NDANI YENU, wala HAMNA HAJA YA MTU KUWAFUNDISHA; lakini kama mafuta yake YANAVYOWAFUNDISHA HABARI ZA MAMBO YOTE, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake”
1 Yohana 2:26 “Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.
27 Nanyi, MAFUTA YALE MLIYOYAPATA KWAKE YANAKAA NDANI YENU, wala HAMNA HAJA YA MTU KUWAFUNDISHA; lakini kama mafuta yake YANAVYOWAFUNDISHA HABARI ZA MAMBO YOTE, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake”
Awali ya yote hebu tuangalie haya mafuta ya kweli ni ya namna gani kabla ya kujihoji kama yamo ndani yetu au la!.
Kama tunavyosoma hapo juu sifa za mafuta hayo Matakatifu ni “kutufundisha”..Na sio tu kutufundisha, bali “kutufundisha mambo yote”..
Hiyo ndio sifa ya kwanza, lakini sifa nyingine ya pili “YANAKAA NDANI YETU” (yaani moyoni).. Na si nje yetu (kwenye ngozi).. Mpaka kufikia hapo tumeshajua kuwa sio mafuta ya chupa au ya upako yanayozungumziwa hapo..bali ni mafuta mengine tofauti kabisa..
Hebu tusogee mbele zaidi kuangalia kimaadiko haya mafuta ni kitu gani na ni kwa namna gani “yanatufundisha habari za mambo yote”..
Kupitia maandiko yafuatayo tutapata majibu…
Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, ATAWAFUNDISHA YOTE, na kuwakumbusha yote niliyowaambia”.
Kumbe kitu peke pekee chenye uwezo wa kutufundisha mambo yote ni Roho Mtakatifu?.
Bila shaka Yale mafuta yanayotajwa na Mtume Yohana katika 1Yohana 2:27 si mengine zaidi ya “Roho Mtakatifu”.
Na tunazidi kulithibitishaje hilo?.
Kwa kuvichunguza vitabu hivi viwili (1Yohana 2:27 na Yohana 14:26). Tunaona vyote vimeandikwa na mtu mmoja ambaye ni Mtume Yohana kwa uongozo wa Roho Mtakatifu.
Sasa isingewezekana kwa Yohana kumaanisha vitu viwili tofauti katika maandiko hayo mawili…bali alimaanisha kitu kile kile kimoja ambacho ni Roho Mtakatifu.
Na Roho Mtakatifu pekee ndiye anayekaa ndani yetu mandiko yanasema hivyo..
1 Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?”.
Soma pia..
2 Timotheo 1:14 “Ilinde ile amana nzuri kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu”.
Na ni kwa namna gani “Ajapo Roho Mtakatifu, hamna haja ya mtu kutufundisha”?..
Turejee Waebrania 8:10-12.
Waebrania 8:10 “Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu. 11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao. 12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena”.
Waebrania 8:10 “Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; Nitawapa sheria zangu katika nia zao, Na katika mioyo yao nitaziandika; Nami nitakuwa Mungu kwao, Nao watakuwa watu wangu.
11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.
12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena”.
Roho Mtakatifu ambaye ndiye “Mafuta ya Mungu ndani yetu” anapoingia ndanj ya mtu, yule mtu anakuwa na shauku ndani ya noyo wake wa kumtafuta Mungu mwenyewe, hahitaji kusukumwa na mtu,
Vile vile yule Roho Mtakatifu anakuwa anamfundisha kwa mafunuo ambayo hawezi kuyapata kutoka kwa watu..
Je umepakwa mafuta na Bwana? Ambaye ni Roho Mtakatifu wake?..Kumbuka wote wasio na Roho Mtakatifu hao sio wake kulingana na Biblia (Warumi 8:9).
Na pia huwezi kujua yote pasipo Roho Mtakatifu..
1 Yohana 2:20 “Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote”
Kanuni ya kupokea Roho Mtakatifu, kwa mujibu wa Biblia ni ile iliyotajwa katika Matendo 2:38.
Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.
Epuka elimu za uongo za kutumia mafuta ya kupikia au ya mizeituni kuvuta au kuimarisha ukaribu wako na MUNGU, ni hatari kubwa sana.
Mafuta mabichi ni mafuta ya aina gani? (Zaburi 92:10)
Zaburi ya Pili ni nini? (Matendo 13:33).
Je tunajazwaje maarifa ya mapenzi yake? (Wakolosai 1:9)
Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)
Swali: Biblia inasema kuwa Bwana Yesu atawahukumu walio hai, na waliokufa (2Timotheo 4:1)
Jibu: Turejee..
2Timotheo 4:1 “Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, ATAKAYEWAHUKUMU WALIO HAI NA WALIOKUFA; kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake”..
Maneno kama haya yanarudiwa tena katika kitabu cha 1Petro 4:5
1Petro 4:5 “Nao watatoa hesabu kwake yeye aliye tayari kuwahukumu WALIO HAI NA WALIOKUFA”.
Zamani na hata sasa, ipo imani ya kwamba mtu akishakufa ndio tayari “kashahukumiwa” hakuna tena hukumu huko aendako.. maana yake mitihani aliyopitia akiwa duniani tayari ni hukumu tosha, hakuna tena hukumu baada ya kifo.
Lakini Biblia inatufudisha jambo jingine tofauti na hilo, kwamba watu wote ambao wamekufa pasipo kujalisha wamekufaje siku ya mwisho watafufuliwa na Bwana YESU na kuhukumiwa..
Yohana 5:25 “Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai. 26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake. 27 Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu. 28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. 29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Yohana 5:25 “Amin, amin, nawaambia, Saa inakuja, na sasa ipo, wafu watakapoisikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale waisikiao watakuwa hai.
26 Maana kama vile Baba alivyo na uzima nafsini mwake, vivyo hivyo alimpa na Mwana kuwa na uzima nafsini mwake.
27 Naye akampa amri ya kufanya hukumu kwa sababu ni Mwana wa Adamu.
28 Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Soma pia Mathayo 11:24 utaona kuwa hata baada ya hukumu ya moto ya Sodoma na Gomora bado watu wa miji hiyo watasimama tena kuhukumiwa katika siku ya mwisho..
Kwahiyo hukumu si ya walio hai tu, bali watu wote, (walio hai na waliokufa)..
Je umempokea YESU?.. Kumbuka sasa anasema nasi kama Mwanakondoo, lakini siku ya mwisho atakuwa ni Mhukumu.. wakati mlango wa Neema utakapofungwa, hakutakuwa na nafasi nyingine ya kutubu wala kupokea wokovu, bali kitakachokuwa kimesalia na hukumu..
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao”.
Mpokee YESU leo, kama bado hujafanya hivyo.
Fahamu maana ya Mithali 21:3 Kutenda haki na hukumu Humpendeza BWANA kuliko kutoa sadaka.
Nini maana ya Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma?
ITAFAKARI SIKU YA HUKUMU.
NIFANYE NINI ILI NIIKWEPE HUKUMU.
Kuna hukumu za aina ngapi?
Swali: Kughofiri ni kufanya nini kama tunavyosoma katika Zaburi 79:9?.
Zaburi 79:9 “Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, UTUGHOFIRI dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako”.
Maana ya “Kughofiri” ni “kuondoa”.
Neno hilo limeonekana mara moj tu kwenye Biblia…na maana yake ni ile ile na ya kusamehe..
Lakini Biblia inazidi kutufundisha kuwa Bwana anatuokoa na kutusamehe pia makosa yetu kwaajili ya jina lake.
Maana yake pia kwa utukufu wa jina lake, anapotusamehe makosa basi pia jina lake linatukuzwa zaidi, hivyo ni fahari ya Mungu pia kutusamehe sisi.
Isaya 43:25 “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako”
Sasa swali kama Mungu anafurahia kutusamehe makosa yetu kwanini tusitumie hiyo fursa kuungama?.
Je umempokea YESU?.. Umetubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha?kama bado je unasubiri nini?…
Tubu leo upate msamaha wa dhambi, na upate ondoleo la dhambi pia.
Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; 47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.
Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;
47 na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu”.
Shalom
NGUVU YA MSAMAHA
UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.
KAMA NISIPOKUTAWADHA, HUNA SHIRIKA NAMI
NINI MAANA YA UKOMBOZI?
ZIFAHAMU ALAMA KUU NNE ZA KRISTO NDANI YAKO.
Biblia inasema watakatifu waliopo duniani ndio Bwana wanaompendeza.
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
Lakini swali ni je! anaposema “Watakatifu”..anamaanisha ni watu wasiokosea kabisa?…kwamba hawawezi kabisa kufanya makosa na kwamba wamekamilika kwa asilimia zote?.
Jibu ni Ndio! … watu wote waliompokea YESU na kupokea Roho Mtakatifu wamekamilika kwa asilimia zote katika vigezo vya “Kuokolewa”, mbele za Mungu lakini si katika vigezo vya kutokosea kabisa (Yaani kufanya mistakes).
Kukosea kusoma maandiko wakati wa mahubiri hayo ni makosa (mistakes), kusahau kutimiza ahadi uliyoitoa kwa mtu ni makosa..
Sasa makosa ya namna hiyo hayawezi kumpokonya mtu haki ya kuwa “MTAKATIFU” mbele za MUNGU.
Vile vile ikiwa mtu kampokea YESU leo na bado hajajua kuwa “anapaswa akabatizwe” ili akamilishe wokovu wake (sawasawa na Marko 16:16).
Na akawa katika hali hiyo hiyo ya kutobatizwa lakini bado anafanya mengine ya imani yaliyo sahihi bado hiyo haimwondolei sifa ya kuwa MTAKATIFU MBELE ZA MUNGU…yupo miongoni mwa watakatifu wa Bwana waliopo ulimwenguni.
Halikadhalika na mambo mengine yote ambayo mtu hajayajua wala kuyasikia kama ni makosa katika hatua zake za awali za wokovu, hayawezi kumpokonya haki ya kuwa mtakatifu mbele za MUNGU.
Lakini anaposikia au kuujua ukweli na kuupinga au kukataa mabadiliko anapoteza moja kwa moja sifa ya kuwa MTAKATIFU mbele za MUNGU.
Kwa namna gani?
Hebu tusome
Ufunuo 22:1″Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA“
Nataka tuone hapo…“NA MTAKATIFU NA AZIDI KUTAKASWA”..
Kama MTAKATIFU ameshakamilika hafanyi makosa kwanini tena hapo maandiko yaseme…“NA AZIDI KUTAKASWA”..
Kumbe MTAKATIFU bado anaweza KUTAKASWA.
Maana yake ni kwamba hakuna kipimo fulani maalumu kwamba hapa mtu kashafikia UTAKATIFU wa mwisho…
UTAKATIFU ni jambo endelevu, kwamba kila siku tunajiona kasoro zetu na kufanya mabadiliko.
Unaweza kujiona leo upo sawa kabisa kiimani na kiutakatifu..lakini baada ya mwezi mmoja uliposoma Neno ukajigundua kuna mambo ulikuwa unakosea hivyo ukajirekebisha,….hapo maana yake “umejitakasa”.
Sasa kipindi ambacho hukuwa unajua makosa, haimaanishi kwamba haukuwa mtakatifu..La! Ulikuwa mtakatifu…
Lakini siku ulipojua jambo fulani ni kosa na kubadilika..hapo “ulizidi kuwa mtakatifu”…na siku utakapojua jambo jingine ambalo leo hii hulijui. Na jambo hilo ukaliacha “hapo utazidi kuwa mtakatifu mara mbili zaidi”.
Kwahiyo ili tuweze kuhesabika ni watakatifu ni lazima “TUJITAKASE”.
Je na wewe ni Mtakatifu?..Je na wewe unajitakasa?.
Swali unajitakasaje?.
Unajitakasa kwa kukaa mbali na kila aina ya vichocheo vya dhambi, na kwa kusoma Neno na maombi pamoja na kukusanyika na wengine (kufanya ibada).
Kuna mambo hutaweza kujua kuwa ni makosa pasipo kusoma Neno, kuna mambo huwezi kujua kuwa ni makosa usipokuwa mwombaji n.k
Bwana akubariki na kuzidi kutusaidia..
Swali: Katika kitabu cha Matendo 13:33 tunasoma pakitajwa “Zaburi ya Pili” je hii zaburi ya Pili ni ipi, nay a kwanza ni ipi na ya mwisho ni ipi?
Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari ule wa 32..
Matendo 13:32 “Na sisi tunawahubiri habari njema ya ahadi ile waliyopewa mababa, 33 ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika ZABURI YA PILI, Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa”.
Matendo 13:32 “Na sisi tunawahubiri habari njema ya ahadi ile waliyopewa mababa,
33 ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika ZABURI YA PILI, Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa”.
Andiko hilo ni Mtume Paulo alikuwa akilirejea kutoka katika kitabu cha Zaburi ule mlango wa Pili, ambapo ndipo tunaposoma maandiko hayo..
Zaburi 2:7 “Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa”.
Kwahiyo tafsiri rahisi ya “Zaburi ya Pili” anayoizungumzia Mtume Paulo katika hiyo Matendo 13:33 ni “Zaburi Mlango wa PIli au Zaburi sura ya Pili”.. ndipo unabii huo unapotokea.. Na Zaburi ya Tatu ni Zaburi mlango wa tatu… na Zaburi ya mia na hamsini ni Zaburi mlango wa mia na hamsini (150).
Lakini pia tunasoma mahali pengine, mwandishi wa kitabu cha Wabrania akinukuu Zaburi hiyo ya Pili..
Waebrania 1:5 “Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, NDIWE MWANANGU, MIMI LEO NIMEKUZAA? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?”
Na tena akarudia katika ule mlango wa tano.
Waebrania 5:5 “Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa.”
Je umempokea YESU?.. kama bado unasubiri nini?. Fahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na YESU amekaribia sana kurudi.
Fahamu mana ya Zaburi 48:14 Yeye ndiye atakayetuongoza
Fahamu maana ya Zaburi 125:3 “ Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki.
Uele ni nini katika biblia? (Zaburi 91:6)
Nini maana ya neno kumwamba (Zaburi 78:19)
Mathayo 8:29
[29]Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Mashetani yanajua kila jambo lipo katika mpangilio wa muda wake, yanajua kuwa tayari hukumu ilishatolewa ya wao kutupwa katika ziwa la moto lililo hatma yao ya milele..
Lakini utekelezaje wake, utakuja baadaye, ambao utakuwa ni mwisho wa dunia, utakao asisiwa na Bwana Yesu Kristo mwenyewe.(Mathayo 25:41)
Wengi tunadhani mapepo, hushindana na sisi, kwa kutuonea wivu, hilo ni kweli kwa sehemu, lakini sababu kubwa ya mapepo na shetani kushindana na sisi…ni wao kujilinda…na adhabu ijayo.
Na wanajua mwanadamu ndiye anayeweza kuiharakisha hiyo siku au kuikawiisha hiyo siku. Ndio maana yanafanya kazi kubwa sana kuwaharibu wanadamu ili siku hiyo isifike upesi.
Hizi ni njia tatu mapepo, hufanya kwa watu ili kukawiisha muhula wao usiwafikie haraka.
1) Kuchochea maovu.
2) Kukengeusha Imani za watu
3) Kukawisha injili
Maovu mengi, humsukuma Mungu kuwa mvumilivu na wanadamu, ili wafikie toba wasiangukie hukumu ya mapepo..Kama wanadamu wasingekuwa na shingo ngumu, mwisho wa dunia na hukumu yao ingeshafika zamani sana.. hivyo mapepo wanabuni kazi mbalimbali ili kuwafanya wanadamu wazidi kupotoka.
2 Petro 3:9-11
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba. [10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea. [11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
[9]Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.
[10]Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
[11]Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,
Luka 18:8
[8]Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?
Kristo anatarajia kanisa lake kusimama katika msingi wa imani kamili ambayo haijaharibiwa wala kuvurugwa na mapokeo na mafundisho ya uongo.. hii ndio sababu ya shetani kuinua makundi ya manabii wa uongo, kufundisha injili nyingine ambayo Kristo hajaileta duniani. Matokeo yake ndio kuwa na kundi kubwa la wakristo lakini dhaifu wasio tayari kumlaki Bwana mawinguni.
Mathayo 24:14
[14]Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Injili ya kweli adui huipiga vita vikubwa..Na wanajua ikihubiriwa ulimwenguni kote, basi ushuhuda wa Mungu utakuwa umefika na hakuna atakayekuwa na udhuru.
Sasa mimi na wewe hatuna budi kusimama katika utakatifu lakini pia imani na injili kuisambaza ili watu waokolewe…
Kumbuka tayari tupo kwenye siku za mwisho, Amka simama na Bwana.
MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.
Je mkristo anaweza akawa na mapepo?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?