Jibu: Tureje..
Waefeso 1:5 “Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe WANAWE kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na URADHI WA MAPENZI YAKE”.
Maana rahisi ya “Uradhi wa Mapenzi” ni “Mapenzi ya Hiari”..
Mtu anayefanya kazi fulani kwa Hiari yake mwenyewe na kwa mapenzi yake yote bila kusukumwa, kulazimishwa wala kuhamasishwa mtu huyo ni sahihi kusema amefanya kazi ile kwa “Uradhi wa Mapenzi”.
Na Mungu ametupenda alituchagua sisi tuwe “Watoto wake”.. Kwa mapenzi yake ya Hiari.. na kwa furaha ya Moyo wake, Maana yake ni jambo linalompa raha na furaha sisi kuwa watoto wake, sio uamuzi wa majuto kwake..
1Yohana 3:1 “Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, KWAMBA TUITWE WANA WA MUNGU; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye”.
Kwahiyo ni bahati na upendo mkubwa sana MUNGU kutufanya sisi kuwa watoto wake, na Kuwa Mtoto wa Mungu maana yake ni lazima utabeba tabia za Uungu, na ndio maana wana wa MUNGU wanaitwa miungu..
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, NDINYI MIUNGU? 35 Ikiwa ALIWAITA MIUNGU wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.
Yohana 10:34 “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, NDINYI MIUNGU?
35 Ikiwa ALIWAITA MIUNGU wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka)”.
Ni hii ni kweli kabisa mwana ni lazima afanane na Baba, hata mtoto wa Mtu ni Mtu, mtoto wa kondoo ni kondoo, na mtoto wa simba ni simba..vivyo hiyo ni mtoto/watoto wa MUNGU ni miungu.
Je umefanyika mtoto wa MUNGU?.. Na je unaijua kanuni ya kufanyika kuwa mtoto wa MUNGU?.. Si nyingine zaidi ya ile tunayoisoma katika Yohana 1:12..
Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”
Mpokee leo YESU nawe utapata uwezo huu mkuu wa kuwa mwana wa Mungu na mrithi wa ahadi za MUNGU… kwasababu ni Uradhi wa mapenzi yake tuwe hivyo.
Waefeso 1:9 “akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo”.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?
JE! UMEFIKIA VIGEZO VYA KUWA BABA ROHONI?
Siku ya kujiliwa inayozungumziwa katika 1Petro 1:12, ni ipi?
HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?
NIFANYE NINI ILI NIPENDWE NA MUNGU?
Print this post
Kibiblia ni neno lenye maana ya wale funza, ambapo hutokea palipo na mzoga, au uozo. Hivyo popote ukutanapo na Neno hilo, huashiria/humaanisha, uharibifu au maiti, au kaburi,
Kwamfano ukisoma;
Ayubu 17:14 Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu; Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;
Buu kama lilivyotumika hapo ni kaburi, Ayubu akimaanisha katika hatua aliyofikia, kaburi, na uharibifu ni kama familia yake (baba yake, mama yake na dada yake), kama tunavyojua familia ni kitu cha karibu sana na mtu, ndivyo Ayubu alivyojiona katika hali aliyokuwa amepitia.
Maana yake, kifo kilikuwa karibu na yeye zaidi hata ya familia yake.
Sehemu nyingine inasema;
Ayubu 25:6 iuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!
Mwandishi akimaanisha mwanadamu ni sawa na mzoga, (yaani mwili wenye uharibifu usio na umilele).
Neno hili utalisoma pia katika vifungu hivi;
Kutoka 16:20,24, Kumbukumbu 28:39, Ayubu 7:5.
Katika maeneo mengine kwenye biblia linatajwa moja kwa moja kama funza. (Isaya 66:24)
Hii ni hatma ya kila mwanadamu asiye na Mungu, yeye ni buu, haijalishi atakuwa na afya leo, anapesa zote ulimwenguni, anacheo kikubwa au elimu, maisha yake bila Yesu Kristo kumwokoa, ni buu tu (maiti, kaburi, )..atakufa na kuishia jehanam ya moto. Lakini akiokoka, hata ajapokufa, ataishi, siku ya ufufuo ikifika, atafufuliwa na kubadilishwa mwili wake na kupewa mwili mwingine wa utukufu, kisha Kwenda kuishi na Kristo milele na milele mbinguni.
Ikiwa haujaokoka, bado na upo tayari kufanya hivyo leo, basi basi fungua hapa kwa mwongozo wa sala ya toba upokee msamaha wa dhambi leo >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Msikwao ni mtu gani Na nini tunajifunza katika neno hilo? (Zaburi 69:8).
Jehanamu ni nini?
Shetani anaishi wapi, Je! Amefungwa au yupo kuzimu?
Shalom, karibu katika kuyatafakari maandiko..
Inafahamika kuwa Kristo alimwaga Damu yake pale Golgotha, pale ambapo misumari ilipopita katikati ya mikono yake na miguu yake, pamoja na mapigo mengine mwili mzima. Kwa damu ile iliyomawagika tulipata ondoleo la dhambi na ukombozi wa Roho zetu,
Lakini Damu hiyo hiyo, tunasoma haikuanza kumwagika saa hiyo ya Mateso ya msalaba…Bali ilitangulia kumwagwa wakati Bwana akiwa anaomba pale kwenye mlima wa Mizeituni pamoja na wanafunzi wake,
Sasa ilimwagika kwa jinsi gani?.. si kwa jinsi nyingine bali kwa jinsi ya JASHO LAKE
Luka 22:44 “Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; HARI YAKE IKAWA KAMA MATONE YA DAMU YAKIDONDOKA NCHINI.]”
Sasa swali la msingi ni kwanini, itoke wakati akiwa katika MAOMBI?.. Ni kwasababu maneno pekee hayatoshi kufikisha maombi kwa Baba, bali Damu inanena zaidi kuliko maneno, na Hivyo ile damu iliyokuwa inamwagika wakati wa maombi ilinena zaidi kuliko maneno tu.. Kwa namna gani tunalithibitisha hilo??..Turejee habari ya Habili.
Biblia inasema Damu ya Habili ilinena ardhini baada ya kuuawa kwake..ijapokuwa alikufa lakini ile damu ililia na kuomboleza mbele za Mungu.. (soma Mwanzo 4:10) na Mungu akaisikia, na ikaleta kisasi kwa Kaini aliyemwua..
Vile vile maombi ya Bwana YESU pamoja na Damu yake inayomwagika ardhini kabla ya mateso ya msalaba.. ilinena zaidi na ndio maana baada ya pale, walitumwa Malaika kumtia Nguvu..na tena Damu ya YESU inanena mema kuliko ile ya Habili..
Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.
Na wakati huu tunapoomba kwa kufahamu Ufunuo huo uliopo katika Damu ya YESU, tutapenda MAOMBI!.. tukijua na kuamini kuwa ipo damu ya YESU inayochuruzika sasa kwaajili yetu tunapoomba.. na hiyo damu inanena mema zaidi ya maneno yetu.
Lakini kama tupo nje ya Imani ya kumwamini Bwana YESU KRISTO, damu yake hiyo haiwezi kunena mema kwaajili yetu, ili iweze kunena mema na kumshinda Yule Mwovu, na hata kuvuta majibu ya maombi, ni sharti kwanza kumwamini Bwana YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kubatizwa ubatizo wa maji na Roho, kuanzia huo wakati na kuendelea ile damu inakuwa inanena mema kwaajili yako na utakuwa unazo nguvu za kumshinda shetani.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.
11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa”.
NA SISI TUTOKE TUMWENDEE NJE YA KAMBI.
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.
ZIJUE TABIA ZA AHADI ZA MUNGU KWA MWAMINIO.
Konstantino mkuu ni nani, na je anaumuhimu wowote katika ukristo?
Biblia inatufundisha kumfahamu sana MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO)..
Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na KUMFAHAMU SANA MWANA WA MUNGU, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo”
Tukimjua vizuri mwana wa Mungu tutaweza kutembea naye vema, tutaweza kumpendeza vema na vile vile tutaweza kumheshimu zaidi.
Leo tutazame jinsi MWANA WA MUNGU (YESU KRISTO) alivyojitambulisha mwenyewe mara saba (07) kama “MIMI NDIMI”.
1. MIMI NDIMI MKATE WA UZIMA.
Yohana 6:35 “Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe”.
Maneno haya ameyarudia tena katika mstari wa 48 na 51 ya mlango huo huo wa sita (06).. Ikiwa na maana kuwa tukimpata YESU maishani ni zaidi ya chakula cha damu na nyama.. chakula cha damu na nyama kinatoa uzima wa masaa machache tu, au siku chache tu, na baadaye mtu atasikia tena njaa, na asipokula anakufa, lakini YESU ndiye chakula cha UZIMA, ambacho mtu akila hatasikia tena njaa.. bali atakuwa na uzima wa milele.
2. MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU.
Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, MIMI NDIMI NURU YA ULIMWENGU, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima”.
Kwa kumwamini YESU na kuyaishi maneno yake, maisha yetu yatakuwa na Mwanga, kila mahali tutakapokwenda na kila tutakachofanya kitakuwa na mwelekeo kama vile mtu anavyotembea katika Nuru..
3. MIMI NDIMI MLANGO WA KONDOO
Yohana 10:7 “Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo”.
Yeye ndiye mchungaji mwema, na kama vile Mchungaji anavyowahesabu kondoo wake wanaoingia na kutoka zizini, na kwamba hakuna hata mmoja atakayepotea mkononi mwake, kadhalika na YESU ndiye Mchungaji wetu, atulindaye na kutuongoza zizini, kuingia kwetu na kutoka kwetu, wala mkononi mwake hatutapote.
4. MIMI NDIMI MCHUNGAJI MWEMA.
Yohana 10:11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo”.
Mchungaji mwema ni Yule anayejitoa hata uhai wake kwaajili ya kondoo, na Kristo aliutoa uhai wake kwaajili yetu, kuonesha upendo wake mkuu kwetu.
5. MIMI NDIMI UFUFUO NA UZIMA.
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”
Kwa kumwamini YESU tunalo tumaini la kufufuliwa siku ya mwisho, hakuna mwanadamu yoyote wala malaika aliyewahi kumwahidia mwanadamu yoyote ahadi kama hii inayotoa tumaini baada ya kifo.
6. MIMI NDIMI NJIA, KWELI NA UZIMA.
Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi”.
Hakuna njia ya mkato ya kufika mbinguni, isipokuwa kupitia YESU KRISTO, tukilijua hili tutamwangalia kwa bidii ili tuwe warithi wa uzima wa milele.
7. MIMI NDIMI MZABIBU WA KWELI.
Yohana 15:1 “Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima”.
Tunapokaa ndani ya YESU ni kama matawi katika shina la mzabibu, ambalo linazaa sana, na sisi tutazaa sana kama tukikaa ndani ya YESU KRISTO.
Je umemkaribisha huyu YESU (Mkuu wa Uzima) maishani mwako?.. au bado unatanga-tanga na dunia tu!.. badilisha uelekeo leo, anza kutembea na YESU aliyejaa heshima.
MANENO SABA YA YESU MSALABANI.
ELOI ELOI LAMA SABAKTHANI?
MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.
ZIFAHAMU ALAMA KUU NNE ZA KRISTO NDANI YAKO.
JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.
Yohana 11:44
[44]Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.
Nakusalimu Katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo. Nataka tujifunze jambo moja Kwa Lazaro aliyefufuliwa…
Kama tunavyojua mtu huyu alikufa, akazikwa na akaoza pia..lakini Bwana Yesu alipofika kaburini Alifanya muujiza mkubwa wa kumfufua.
Na kweli Lazaro alitoka kaburini akiwa mzima kabisa bila shida yoyote…Lakini wengi wetu tunaishia hapo, na kusema Bwana Ametenda muujiza…Lakini Yesu alipomwangalia aliona bado akatoa agizo akisema mfungueni mkamwache aende zake.. Maana yake ni kuwa ufufuo, ulimpa uzima kweli lakini sio uhuru..
Ilihitaji afunguliwe, maana kaburi lilimfunga mikono yake, miguu yake pamoja na uso wake…hata alipofufuka bado liliacha mizizi yake kwa mtu.
Ufufuo unafananishwa na wokovu, Mtu anapomwamini Yesu anakuwa tayari amefufuka kutoka katika wafu…lakini hilo peke yake halitoshi, bado Anakuwa na kamba za makaburini (maisha ya kale), hivyo anapaswa afunguliwe…
Ukiokoka haimaanishi, tabia za kale zote zitaondoka siku hiyo hiyo, unahitaji kukubali kufunguliwa, ili uwe huru kwelikweli..
Sanda, zilizomzinga Lazaro, uso wake, miguu, mikono, kama wavu wa bui-bui, hutembei, Hushiki wala huoni…ndio maisha Ya wakristo wengi baada ya kuokoka yalivyo..
Zile tabia za kale wanaendelea nazo, uchungu, wivu, hasira, uadui, maumivu, vinyongo, hofu, wasiwasi, wanashindwa kuendelea mbele kwasababu hawatoi nafasi ya kufunguliwa…
Angalia hapo Bwana Yesu anasema..”Mfungueni, mkamwache aende zake…”
Hasemi jifungue…bali mfungueni…yapo mambo huna budi kukubali kusaidiwa ili upone..
Ndio hapo Mungu akaweka…Kanisa.
Ambapo..
Utakutana na wachungaji.. kukusimamia na kukulisha mpaka utakapokomaa Na kukua vizuri kiroho…kuishi bila kanisa yaani mwenyewe mwenyewe tu, ni sawa na kutembea na sanda lako,
Kumbuka Bwana anatarajia umzalie matunda mara baada ya wokovu wako…yapo majukumu ya kufanya baada ya kuokoka..lakini ikiwa miguu na mikono na uso umefungwa unatarajia nini hapo?
Kubali kufundishika, Kubali kuchungwa, kubali mashauri na kuonywa, kubali kuombewa, kubali kuishi na ndugu (katika Bwana), kubali kusoma Neno, kuomba na wenzako utafunguliwa sana.. zaidi ya kuridhika tu na wokovu ulioupokea ukidhani utazalisha chochote katika hali hiyo hiyo ya kiroho ambayo upo peke yako peke yako.
Mara nyingine hata maono yako huwezi kuyafikia kwasababu umefungwa miguu yako. usisonge mbele.. Ogopa sanda, kama vile unavyoogopa mauti.
Ukijiona una tabia ambazo haziendani Na hali mpya ya wokovu ulioupokea basi ndio wakati wa kushughulika na sanda lako, kwa kutii na kufuata hayo maagizo. Jiwajibishe, tendea kazi wokovu Wako, kwasababu kila mtu anawajibu wa kufanya hivyo.
Hofu ya Bwana ni nini? (2Wakorintho 5:11)
Sheria ya uhuru ni ipi? (Yakobo 2:12)
Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24
WhatsApp
SWALI: Sheria ya uhuru ni ipi inayozungumziwa na mtume Yakobo kulingana na maandiko?
Yakobo 2:11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria. 12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.
Neno hili pia utaliona likitajwa na mtume Yakobo katika vifungu vingine vya juu.
Yakobo 1:25 Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.
Katika biblia zipo sheria kuu mbili
Sheria ya dhambi na mauti ndio ile ya torati, ambayo kazi yake kubwa ni kufichua uovu, kushtaki makosa, lakini haimfanyi mtu kuwa huru, kwa mfano sheria inasema usizini, mtu atakataa kuzini, sio kwasababu hapendi uzinzi, lakini kwasababu sheria imesema tu hivyo, anaogopa adhabu atakapotenda hiyo dhambi atauawa.
Lakini sheria ya Roho wa uzima, ni sheria ya Mungu, isipokuwa hii mtu anavuviwa na Roho Mtakatifu, nguvu ya kuisha sawasawa na matwaka ya Mungu, bila shuruti Fulani, ni ya uhuru. Mfano labda sheria inasema usiue, mtu haui sio kwasababu sheria imesema, lakini kwasababu moyoni mwake hiyo nia, tamaa, au kiu ya kuua haipo, hivyo hata kama sheria isingesema hilo jambo lisingekubalika ndani yake, Hivyo mtu kama huyu tunasema ni huru na sheria, hayupo ki-sheria, sheria haimtawali ijapokuwa sheria yenyewe ipo.
Mtu ukishaokoka, anakutana na sheria mpya ya Mungu, ambayo hiyo ni lazima ifuatwe na ishikwe, lakini inakuwa ya uhuru, sio tena ya kifungo, kwasababu Roho Mtakatifu anamsaidia huyo mtu kuuishi..
Ndio hiyo inayoitwa sheria ya uhuru, kwenye kitabu cha Yakobo.
Maana yake ni nini? Sisi kama waamini, Mungu anatarajia tuonyeshe matunda ya Imani yetu katika upendo, huruma, na matendo mema, kwasababu tunaye Roho.
Hivyo inapotokea, hayo hayaonekani, sheria itatuwajibisha, kutuhukumu, au vinginevyo hatukipokea sheria hiyo ya uhuru.. Ni sawa, na mtu aende kuua watu ovyo bila sababu yoyote,
Mtu huyu atahukumiwa, sawa tu na yule ambaye amesukumwa na sababu fulani, labda kisasi, hasira, wivu, chuki n.k.,
Hivyo sisi waamini, tulipokuwa huru na dhambi, hatupaswi kufikiri kuwa ndio tuna uhalali wa Kutenda dhambi. Kinyume chake, tujue kuwa ipo sheria yetu ya uhuru, itakayotuhukumu, kama tu vile wale wengine walivyohukumiwa kwa sheria ya dhambi na mauti (torati).
Ndicho alichokisema mtume Yakobo..
Kwa hitimisho ni kuwa sheria ya uhuru, ni sheria tunayoitimiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Ambayo hiyo pia itatuhukumu. Hivyo wewe kama mwamini, hakikisha wokovu wako unathibitika kwa kazi zake njema, chini ya upendo
Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29)
Fahamu maana ya Warumi 7:25 je tunatumikia sheria ya dhambi?
Silaha za Nuru ni zipi? (Warumi 13:12)
Swali: Kwasasa tunatumia kifaa kinachoitwa saa (iwe na ukutani, mkononi au kwenye simu) kujua sekunde, dakika na saa.. Je watu wa zamani walijuaje sekunde, dakika na saa?
Jibu: Nyakati za Biblia siku iligawanywa katika masaa 12 ya mchana na masaa 12 ya usiku, tunalithibitisha hilo katika Yohana 11:19-20.
Yohana 11:9 “Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu. 10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.
Yohana 11:9 “Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake”.
Hii ikimaanisha kuwa ni kweli enzi za Bwana YESU akiwa duniani, siku ilikuwa ikigawanywa katika mgawanyo wa masaa.. Lakini kuhusiana na mgawanyo wa sekunde Biblia haituonyeshi mahali popote kwamba watu wa kale waligawanya saa katika sekunde, hivyo hakukuwa na mgawanyo wa sekunde katika kila saa.
Sasa swali walijuaje kuwa lisaa limoja limekwisha na limeingia lingine, na hatimaye kumaliza yote 12 ya mchana na usiku? Na ilihali hawakuwa na saa kama za kwetu zinazohesabu masaa?
Watu wa kale hawakutumia saa za mkononi kama za kwetu, katika kuigawanya siku katika masaa, bali walitumia njia za asili kuigawanya siku katika masaa 12, na njia hizo ni kutazama Jua, kutumia kivuli cha jua, kipimo cha maji, na saa ya mchanga, kipimo cha nyota tutazamame kimoja baada ya kingine kwa ufupi.
1. Kipimo cha kutazama jua.
Asuhuni kulipopambazuka walijua ni saa moja, na Jua lilipofika la utosini waliweza kujua ndio nusu ya siku, yaani saa sita mchana, na lilipozama waliweza kujua ni saa 12 jioni, hivyo wakati jua likiwa katikati ya moja na saa sita mchana waliweza kukadiria masaa hayo ya katikati, vivyo hivyo na jioni, na njia hii ndio iliyotumika sana na wayahudi katika kujua masaa.
2. Saa ya kivuli cha Jua (Sundial).
Hii ni njia iliyotumika kwa kutazama mwelekeo wa kivuli cha jua, na ndio ile iliyotajwa katika Isaya 38:8, wakati wa mfalme Ahazi.
3. Saa ya Maji.
Hii ilitumika zaidi wakati wa usiku, ambapo kiwango cha maji kilidondoka kidogo kidogo katika kifaa husika, na njia hii ilitumiwa sana na watu wa Babeli.
4. Saa ya Mchanga.
Mchanga uliwekwa katika kifaa maalum, na baadaye kuachiwa kudondoka kidogo kidogo.
5. Kipimo cha Nyota.
Kipimo hiki kilitumika nyakati za usiku ambapo waliangalia nafasi za makundi ya nyota kama vile Orioni, na Kilimia.
Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba enzi za Biblia walitumia zaidi kipimo cha jua na kivuli cha jua kujua mgawanyo wa masaa.
Sasa kwa urefu kwanini Bwana YESU asema saa za mchana si 12, fungua hapa >>>NI SAA KUMI NA MBILI (12) TU, ZA KRISTO KWAKO.
JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.
FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.
FUNGUA KINYWA CHA ROHO MTAKATIFU KIHUDUMU.
USIKAWIE- KAWIE KUUFUNGUA MOYO WAKO
SWALI:Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.mfano “We kenge njoo hapa”, kama YESU alivyo tumia mbweha katika
luka 13:32.
JIBU: Katika biblia tunaona watu wakiitwa kwa majina mbalimbali ya wanyama mfano mbwa mwitu (Mathayo 7:15), kondoo(Yohana10:27), nyoka(Mathayo 13:34). Lakini pia mbweha, Njiwa, nguruwe, Simba, mbuzi.
Sasa ni vema kufahamu makusudio ya watu/jamii kuitwa hivyo yalikuwa ni nini, hayakuwa kwa lengo la kutukana, au kukejeli, au kudharau..
Hapana Bali kwa lengo la kuonyesha tabia ya mtu, jinsi ilivyo hilo tu.
Kwamfano Yesu alipomuitwa Herode Mbweha, hakuwa na kusudi la kumtukana, au kumdharau, bali alikuwa Anaeleza tabia zake zilizo mfano wa mbweha, ambaye anatabia ya kuvizia na kurarua wanyama wadogo na kuwaua. Maana hivyo ndivyo Herode alivyokuwa, jambo lililoonekana Hata kwa baba zake Kipindi Yesu anazaliwa walimwinda ili wamuue.
Sasa Ikiwa mtu atajulikana kwa namna kama hiyo, kibiblia sio tusi.
Lakini kinyume chake watu hutumia Majina ya wanyama kuwatukana Wengine, au kuwaabisha, au kuonyesha dharau kinyume chao, chuki au hasira, hayo biblia imekataza…na ni dhambi
Kusema “wewe kenge njoo hapa”..Moja kwa moja kauli hiyo inaonyesha chanzo chake ni hasira, dharau au chuki.
Waefeso 4:29
[29]Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.
Wakolosai 3:8
[8]Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.
Mathayo 5:22
[22]Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.
Hivyo chunga kinywa chako. Kila Neno ulisemalo pima makusudi yaliyo nyuma yake.
VILIO VINAVYOUFIKIA MOYO WANGU.
JAWA SANA MOTO ULAO
USIWAOGOPE WAZAMZUMI
Kilio kibiblia ni mafadhaiko, machozi, au maonezi yanayoendelea kwa muda mrefu, bila kuchukuliwa hatua, au kupatiwa utatuzi stahiki, Lakini sio tu machozi bali pia shangwe ovu..zinazoendelezwa kwa muda mrefu mbele za Mungu bila kuachwa nazo pia huitwa vilio.
Sasa Makosa kama haya,(ambayo huzaa vilio) ni tofauti na makosa mengine, kwasababu haya hujilimbikiza mpaka kuzama moyoni mwa Mungu, Na adhabu zake huwa ni nzito sana, kulingana na matukio kadha wa kadha tunayoyasoma katika maandiko.
Tutakwenda kuona aina tano (5) vilio ambavyo vinatajwa katika biblia. Na yamkini pengine umekuwa mmojawapo uliyesababisha hivyo, Basi utubu mapema ili mabaya yasije kukukuta wakati wowote
Yakobo 5:1-6
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia. [2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo. [3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho. [4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi. [5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo. [6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
[1]Haya basi, enyi matajiri! Lieni, mkapige yowe kwa sababu ya mashaka yenu yanayowajia.
[2]Mali zenu zimeoza, na mavazi yenu yameliwa na nondo.
[3]Dhahabu yenu na fedha yenu zimeingia kutu, na kutu yake itawashuhudia, nayo itakula miili yenu kama moto. Mmejiwekea akiba katika siku za mwisho.
[4]Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna vimeingia masikioni mwa Bwana wa majeshi.
[5]Mmefanya anasa katika dunia, na kujifurahisha kwa tamaa; mmejilisha mioyo yenu kama siku ya machinjo.
[6]Mmehukumu mwenye haki mkamwua; wala hashindani nanyi.
Mstari wa nne anasema. ‘Angalieni, ujira wa wakulima waliovuna mashamba yenu, ninyi mliouzuia kwa hila, unapiga kelele, na vilio vyao waliovuna’
Hii ni aina ya kilio cha wafanyakazi Wote wa chini (humaanisha pia waajiriwa wote).
Ukweli Ni kwamba asilimia kubwa ya waajiri, huwadhulumu wafanyakazi wao mishahara au wanawatumikisha kupita kiasi na kuwapa mishahara midogo, Lengo ni ili wajilimbikizie mali, kwa manufaa yao wenyewe…
Sasa hilo ni jambo baya sana, kwasababu huku chini Mungu anasikia kilio chao hata kama hawasemi au hawaoni…mwisho wake utakuwa mbaya, hizo mali zitakutafuna kama yule tajiri wa Lazaro.
Hakikisha kuwa yule unayemwajiri, mpe stahiki zake, si tu kwenye ngazi za mashirika au makampuni lakini pia hata nyumbani kwako ikiwa umemwajiri msaidizi wa kazi, mpalilia bustani, msafisha choo, hakikisha iliyo haki yake unampa kwa wakati ili Bwana asiharibu ulivyo navyo. Vilio vyao vina nguvu sana mbele za Mungu.
Tunaona Kaini alipomuua ndugu yake, alidhani kila kitu kimekwisha…lakini Mungu akamweleza kinachoendelea katika ulimwengu Wa roho, kuwa damu yake inamlilia..Na adhabu yake ikawa ni mbaya sana…kulaaniwa na kukataliwa na nchi.
Mwanzo 4:10-13
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. [11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; [12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani. [13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
[10]Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.
[11]Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako;
[12]utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.
[13]Kaini akamwambia BWANA, Adhabu yangu imenikulia kubwa, haichukuliki.
Kamwe usiue mtu. Au kuchochea mauaji Yasiyo na hatia
Wana wa Israeli, walipokuwa Misri walitumikishwa na kuteswa na kunyanyaswa na Farao..wakamlilia Mungu, Bwana akasikia kilio chao
Kutoka 3:7-9
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; [8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. [9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
[7]BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
[8]nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
[9]Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
Matokeo yakawa ni Misri kupoteza kila kitu, ambacho walikisumbukia kwa muda mrefu, pamoja na vifo vingi. Kamwe Usimtese mtu yeyote, awe mke wako, mtoto wa kambo, mkwe, kijakazi, yatima, mjane, fukara.
Hilo usiliruhusu kwasababu Vilio vyao vikimfikia Mungu, utakuwa mashakani.
Ufunuo 6:9-10
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. [10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
[9]Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
[10]Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Watakatifu waliapo, ni mbaya zaidi, kuliko hata makundi mengine yote wamliliapo Mungu. Adhabu yake, Mungu huikusanya, ambayo sehemu ya hiyo inamwagwa hapa hapa duniani(Ufunuo 16:4-7), lakini pia sehemu kubwa zaidi inakuwa ni baada ya haya maisha.
Kamwe usimtese mtu wa Mungu, usimdhulumu, usimwaibishe, usiwe mwiba kwake..Kwasababu vilio vyao Mungu huvisikia kwa haraka sana.
5) Kilio (Shangwe) cha waovu.
Anasa, na matendo mabaya ambayo watu wanayafanya…wakidhani ndio maisha…kubwe hawajua ni kilio kikubwa kinachoufikia moyo wa Mungu kwa haraka, kikisema mbona huji kuteketeza? Ndivyo ilivyokuwa kwa Sodoma na Gomora.
Mwanzo 18:20-21
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana, [21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
[20]BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,
[21]basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
Hii ni hatari ambayo ndio inayoendelea sasa karibu dunia nzima. Matendo ya Sodoma na Gomora (ulawiti & ufiraji), anasa, ulevi, starehe, huvuta haraka sana, hukumu za Mungu. Na kama tunavyojua hizi ni nyakati za mwisho, moja ya hizi siku hukumu ya Mungu itamwagwa Duniani.
Je! Umemwamini Yesu?
Je una uhakika kubwa Kristo akirudi Leo utakwenda naye?
Ikiwa bado hujaokoka na upo tayari kufanya hivyo sasa.. Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo mwisho wa makala hii.
Je! Yohana alimtilia shaka Bwana YESU? (Mathayo 11:3)
ENDELEZA UPONDAJI.
USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.
Swali: Unakuta mtu anapitia tatizo fulani, halafu anasema.. ndio nimeandikiwa hivyo! Na siwezi kubadilisha.. sasa je mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya yampate na mwingine mema?
Jibu: Kifungu cha Biblia kinachosapoti kuwa mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya au mema ni kutoka katika kitabu cha Yeremia..
Yeremia 15:2 “Kisha itakuwa, hapo watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi, WALIOANDIKIWA KUFA, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa upanga; AU KUFA KWA NJAA, WATAKUFA KWA NJAA, au kutekwa nyara, watakuwa mateka”.
Kwa haraka andiko hilo laweza kueleweka kwamba wapo watu walioandikwa na MUNGU matatizo tangu mwanzo, lakini kiuhalisia haiko hivo.. hakuna mtu aliyeandikiwa na MUNGU matatizo, au shida..
Sasa kama hivyo ndivyo, nini maana ya andiko hilo ya kwamba “waliondikiwa kufa watakufa? (Yeremia 15:2)”
Mantiki ya “kuandikiwa hapo” inarejea sheria za Mungu huko nyuma.. kwamba iliandikwa “Mtu asiyeishi kwa sheria za Mungu atadhibiwa kwa sheria”… Kwamfano iliandikwa hivi katika Kumbukumbu 28:15-18..
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. 17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia. 18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.
17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.
18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.
Sasa kulingana na andiko hilo, mtu Yule ambaye ataacha kusikiliza sauti ya Bwana na atafanya mabaya… basi maandiko hayo ya laana yatampata, na hapo ni sawa na kusema kwamba “ameandikiwa laana”…
Lakini si kwamba Mungu anamchagua mtu na kumwandikia laana na mwingine anamchagua na kumwandikia Baraka!… La!..Bali laana zake na Baraka zake zinakuja juu ya mtu kwasababu ya matendo ya mtu.
Kwahiyo mtu aliyekufa kwa upanga huwenda ni kwasababu aliua kwa upanga, na hivyo andiko hili ndio aliloandikiwa na limetimia kwake..
Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga….”
Na makosa mengine yote ni hivyo hivyo, yameshaandikiwa adhabu yake.. kwahiyo mtu akiyatenda atakuwa anapokea malipo ya yaliyoandikwa na kuichukua hiyo nafasi.
Bwana atusaidie, tusitimize maandiko ya Laana, bali tutimize maandiko ya Baraka ili tuwe miongoni mwa waliondikiwa Baraka.
Je umempokea YESU, Umebatizwa kwa Roho Mtakatifu?.. kama bado unasubiri nini?…fahamu ya kuwa unyakuo wa kanisa umekaribia sana na siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu wanafufuliwa.
Maran atha!
UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.
ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?
LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.