Category Archive Uncategorized @sw-tz

Je kuna walioandikiwa mabaya  na wengine mema?

Swali: Unakuta mtu anapitia tatizo fulani, halafu anasema.. ndio nimeandikiwa hivyo! Na siwezi kubadilisha.. sasa je mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya yampate na mwingine mema?


Jibu:  Kifungu cha Biblia kinachosapoti kuwa mtu anaweza kuwa ameandikiwa mabaya au mema ni kutoka katika kitabu cha Yeremia..

Yeremia 15:2 “Kisha itakuwa, hapo watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi, WALIOANDIKIWA KUFA, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa upanga; AU KUFA KWA NJAA, WATAKUFA KWA NJAA, au kutekwa nyara, watakuwa mateka”.

Kwa haraka andiko hilo laweza kueleweka kwamba wapo watu walioandikwa na MUNGU matatizo tangu mwanzo, lakini kiuhalisia haiko hivo.. hakuna mtu aliyeandikiwa na MUNGU matatizo, au shida..

Sasa kama hivyo ndivyo, nini maana ya andiko hilo ya kwamba “waliondikiwa kufa watakufa? (Yeremia 15:2)”

Mantiki ya “kuandikiwa hapo” inarejea sheria za Mungu huko nyuma.. kwamba iliandikwa “Mtu asiyeishi kwa sheria za Mungu atadhibiwa kwa sheria”… Kwamfano iliandikwa hivi katika Kumbukumbu 28:15-18..

Kumbukumbu 28:15 “Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.

16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.

17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.

18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako”.

Sasa kulingana na andiko hilo, mtu Yule ambaye ataacha kusikiliza sauti ya Bwana na atafanya mabaya… basi maandiko hayo ya laana yatampata, na hapo ni sawa na kusema kwamba “ameandikiwa laana”

Lakini si kwamba Mungu anamchagua mtu na kumwandikia laana na mwingine anamchagua na kumwandikia Baraka!… La!..Bali laana zake na Baraka zake zinakuja juu ya mtu kwasababu ya matendo ya mtu.

Kwahiyo mtu aliyekufa kwa upanga huwenda ni kwasababu aliua kwa upanga, na hivyo andiko hili ndio aliloandikiwa na limetimia kwake..

Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga….”

Na makosa mengine yote ni hivyo hivyo, yameshaandikiwa adhabu yake.. kwahiyo mtu akiyatenda atakuwa anapokea malipo ya yaliyoandikwa na kuichukua hiyo nafasi.

Bwana atusaidie, tusitimize maandiko ya Laana, bali tutimize maandiko ya Baraka ili tuwe miongoni mwa waliondikiwa Baraka.

Je umempokea YESU, Umebatizwa kwa Roho Mtakatifu?.. kama bado unasubiri nini?…fahamu ya kuwa unyakuo wa kanisa umekaribia sana na siku yoyote parapanda ya mwisho inalia na wafu wanafufuliwa.

Maran atha!

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

FAIDA NYINGINE YA MAOMBI YA KUSHUKURU.

ILI TUONEKANE SAFI MBELE ZA MUNGU TUFANYE NINI?

LINDA CHEMCHEMI YA MOYO WAKO.

Print this post

USHUHUDA WA MATENDO NI MKUU KULIKO WA MANENO.

Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia Neno la MUNGU wetu lililo Taa na Mwanga wa njia  yetu (Zab. 119:105).


“Maneno” yanafaa kuthibitisha jambo, lakini “matendo” ni bora zaidi.. Hebu tujifunze kwa Bwana YESU ambaye alitumia matendo zaidi kuliko maneno.

Kipindi ambacho  Yohana Mbatizaji anawatuma wanafunzi wake kwa YESU kumwuliza kama yeye ndiye au wamtazamie mwingine, jibu la YESU halikuwa “Ndio mimi ndiye”.. bali aliwaambia wale watu wamrudie Yohana wamwambie wanayoyaona, viwete wanatembea, vipofu wanaona..

Mathayo 11:2 “Naye Yohana aliposikia huko gerezani matendo yake Kristo, alituma wanafunzi wake, kumwuliza,

3 Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?

4 Yesu akajibu akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana mnayoyasikia na kuyaona;

5 vipofu wanapata kuona, viwete wanakwenda, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema”.

Umeona hapo KRISTO hakutumia maneno kujieleza yeye ni nani bali matendo.. Kwa ufupi kazi zake zilimshuhudia yeye ni nani, na sio hapo tu bali kila mahali ilikuwa ni hivyo hivyo..

Yohana 10:24 “Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.

25 Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia”.

Umeona, kumbe kazi (yaani matendo) ya YESU ndio yaliyomshuhudia??…  Je na sisi tutumie kipi kutangaza ushuhuda wetu?.. maneno yetu au kazi zetu?..Bila shaka Matendo yetu yanafaa zaidi kuliko maneno.

Tutatambulika kuwa sisi ni wakristo kwa matendo na si maneno tu.. tutatambulika sisi ni watumishi kwa matendo na si maneno matupu tu!, tutatambulika sisi ni wakweli kwa matendo na si kwa maneno tu.

Ukisema umepata badiliko moyoni, uthibitisho wa badiliko hilo ni matendo ya mwilini, kwamba kama umebadilishwa tabia basi huwezi kuendelea kuiba, au kutukana au kuvaa vibaya au kufanya uzinzi, uthibitisho wa badiliko la ndani ni matendo ya nje, na si maneno tu..

Mathayo 5:16 “Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni”.

Hivyo tutie bidii kutengeneza matendo yetu zaidi ya maneno yetu.

Bwana YESU atusaidie..

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

ENDELEZA UPONDAJI.

USHUHUDA WA RICKY:

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

Print this post

BABA AKIMBIAYE

Luka 15:20

[20]Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. 

Habari ya mwanampotevu hufunua picha halisi ya rehema na huruma nyingi za Mungu kwetu. Baada ya yule mwana mdogo, kupoteza kila kitu, kwa maisha ya anasa..mwishowe alizingatia kurudi kwa baba yake, Akiwa na fikra za aidha kulaumiwa, Kutengwa, au pengine kuadhibiwa na kufanywa mtumwa…lakini mambo yalikuwa mbali sana na mategemeo yake..tena sanaa..

Kabla hata hajamwona Baba yake, Baba yake alishamwona kwanza yeye kwa mbali… lakini si hilo tu, mzee yule hakungoja kijana wake amfikie, bali alitoka saa ile ile akaanza kukimbia kumwelekea mwana wake..

Hilo jambo La ajabu sana, kwani kwa tamaduni za zamani, hata sasa…mtu mzima kukimbia, Ni aidha kuna jambo la taharuki sana…au la hisia kubwa kupita kiasi…kwasababu watu wazima hawakimbii ovyo..

Lakini kwa huyu mzee, ilibidi akaidi kanuni hiyo..akimbie kama mtoto mdogo kumwelekea mwanawe na alipomfikia akamkumbatia na kumbusu sana…unaweza tengeneza picha ni hisia gani kali yule baba alikuwa nazo kwa mwanawe..

Mambo kama hayo ni rahisi kuyaona kwa mzazi ambaye pengine mtoto wake ampendaye alikuwa amesafiri kwa wakati mrefu na sasa amekuja kumsalimia Nyumbani…lakini si rahisi kuona mzazi anaonyesha hivyo kwa mtoto mtukutu, mwenye kiburi, aliyeshindikana…pengine angemkaribisha tu, na kumsamehe, na kuongea naye kawaida…lakini huyu alichinjiwa mpaka mnyama na karamu juu..

Hii ni habari inayofunua hisia za Mungu kwa mwenye dhambi atubupo kwa dhati…

Kabla Hata hujamaliza ombi la toba tayari Mungu ameshakukimbilia na kukukumbatia, neema yake ya kusamehe inazidi wingi wa dhambi tulizomtenda…

Yawezekana wewe umekuwa mwana mpotevu kwa kurejea kwenye Dhambi ambazo ulishaziacha zamani…vipi kama ukitubu leo kwa kumaanisha.?

Ulitoka nje ya ndoa Yako…tubu sasa…ulirudia tabia ya uzinzi na kujichua..tubu sasa, Umerudia ulevi na anasa..embu tubu..Mungu yupo tayari kukukimbilia…Na kukusamehe zaidi ya matarajio yako.

Na kukusaidia…yule mwana mpotevu “alizingatia” embu na wewe zingatia pia leo.. kuacha hayo maisha ya kale…haijalishi umefanya makosa Mengi ya aibu namna gani..Tubu tu leo na kutupa hivyo vikoba vya kiganga, na ufiraji, na wizi na rushwa uzifanyazo. na Bwana atakuponya.

Kumbuka ukifa katika dhambi zako ni moja kwa moja kuzimu..kwanini iwe hivyo wakati akusameheaye anakukimbilia?

Usimzuie, achilia akili zako mrudie muumba wako.

Bwana akubariki.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>

https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

BWANA NISAIDIE, KUTOKUAMINI KWANGU

JAWA SANA MOTO ULAO.

TENGENEZA NJIA YAKO.

Print this post

JAWA SANA MOTO ULAO.

Waebrania 12:29

[29]maana Mungu wetu ni moto ulao.

Mungu huitwa moto, lakini si moto tu bali moto ulao, maana yake si ule wa kuunguza tu, bali Ule wa kulamba kila kitu, kutafuna Na kutowesha kabisa

Mfano wake ni kama ule ulioshuka juu ya madhabahu Aliyoijenga Eliya, uliposhuka, juu yake haukuchagua maji, wala kuni, wala sadaka..mahali pale palimezwa kila kitu…(1Wafalme 18:38)

Tofauti na mioto Mingine ambayo itaivisha tu kitu, au kugeuza umbile n.k. moto huu haubadilishi umbile Kama hii mioto mingine tuliyonayo…ambayo ikipita Juu ya chuma Haiwezi kuila yote, bali huiyeyusha Tu na kuibadili umbile, huo wa Mungu hulamba Vyote bila kubagua…

Huu ni moto wa rohoni sio mwilini.. ukijazwa huu, basi fahamu hakuna chochote ambacho hakifai kisichoungua….ugusapo popote..huharibu kabisa Kabisa kazi za shetani, ukaapo ndani yako huchoma kabisa kabisa mambo maovu.

Hivyo Bwana ametutaka kama watoto wake aliotuzaa tujawe na moto huu ndani yetu.. na namna ya kuupokea..ameeleza katika vifungu vifuatavyo;

Isaya 33:14

[14]…. Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele?

[15]Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung’utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu.

Umeona ni nani Awezaye kukaa na moto ulao? Kumbe si wote…bali ni wenye sifa hizo zilizotajwa..

Maana yake, kwa kauli ya ujumla ni yule yeye atafutaye kuishi maisha matakatifu na ya haki.

Hii ndio mbio yetu wote…

Nguvu ya ukristo baada ya kuokoka ni utakatifu. Ndio moto wetu ulao.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana.

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

Print this post

Kutawa ni nini? Sawasa na Luka 1:24

Swali: Kutawa kwa Elisabeti miezi mitano maana yake nini?


Jibu: Turejee..

Luka 1:24 “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKATAWA miezi mitano, akisema,

25 Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana katika siku zile alizoniangalia ili kuniondolea aibu yangu mbele ya watu”.

Tafsiri ya “Kutawa” ni “kujitenga”.. hivyo Kiswahili kingine cha mstari huo ni hiki… “Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba AKAJITENGA miezi mitano”

Hivyo Elisabeti alijitenga na jamii ya watu pengine kwasababu za kumshukuru MUNGU kwa muujiza aliomtendea wa kubeba mimba uzeeni, au kwa nia ya kuepusha uadui kutoka kwa watu ambao ungetokana na wivu, au pengine kwasababu nyingine za kupumzika na kumtafakari MUNGU kwa faragha!. Mojawapo ya hizo au zote zaweza kuwa sababu za kujitenga kwake.

Na tunaona lilikuwa ni jambo jema kwa Elisabeti kwani baadaye alipokutana na Mariamu ndugu yangu, alijazwa Roho Mtakatifu na kuzungumza  kiusahihi habari za Mariamu na Bwana Yesu aliye tumboni mwa Mariamu.

Hiyo inatufundisha nini?

Si kila Baraka kutoka kwa MUNGU inapokuja ni wakati wa kutangaza na kushuhudia wakati huo huo, wakati mwingine ni vizuri kujitenga/kutawa kwa muda ili kutumia kumshukuru MUNGU, na kuomba ulinzi wa Baraka ile,..kuwahi kutangaza Baraka za MUNGU au mlango MUNGU aliokufungulia kabla ya kupata utulivu ni hatari kwako na kwa utakaoenda kuwaambia.

Hivyo ni vizuri kutokuwa mwepesi wa kuzungumza bali ni vizuri kuwa mwepesi wa kupata faragha na MUNGU na kutafakari fadhili zake kabla ya kuzungumza au kushuhudia.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

JE BIKIRA MARIAMU ALIZAA WATOTO WENGINE?

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

Print this post

Yohana aliwatiaje waasi akili za wenye haki? (Luka 1:17)

Jibu: Turejee kuanzia ule mstari wa 11..

Luka 1:11 “Akatokewa na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.

12 Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.

13 Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.

14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.

15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.

16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.

17 Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, NA KUWATILIA WAASI AKILI ZA WENYE HAKI, NA KUMWEKEA BWANA TAYARI WATU WALIOTENGENEZWA”.

Haya ni maneno ya Malaikaa aliyokuwa anamwambia mzee Zakaria kuhusu mtoto atakayezaliwa (ambaye ni Yohana Mbatizaji), kwamba mtoto huyo atajazwa Roho Mtakatifu tangu akiwa tumboni, na atatembea na roho (yaani huduma) ya Eliya, lakini pia atawatejeza wengi wa Mungu, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa, na zaidi sana KUWATILIA WAASI AKILI ZA WENYE HAKI!

Sasa kabla ya kutazama ni kwa namna gani Yohana Mbatizaji “aliwatilia waasi akili za wenye haki” hebu kwanza tutazame alimwekeaje Bwana tayari watu waliotengenezwa..

Ikumbukwe kuwa baadhi ya wanafunzi wa Bwana YESU kabla ya kuwa wanafunzi wa Bwana Yesu walikuwa kwanza wanafunzi wa Yohana mbatizaji.. baadhi ya hao walikuwa ni Andrea na nduguye Petro (Soma Yohana 1:35-41).

Kwahiyo akina Andrea na wengine ni watu waliotengenezwa kiroho kabla ya kuanza kutembea na Bwana, hivyo kwao haikuwa ngumu kumwamini Bwana au kumwelewa.. (hiyo ndio maana ya kumwekea tayari Bwana watu waliotengenezwa)

Sasa terejee sehemu ya Pili ambayo ni “Kuwatilia waasi akili za wenye Haki

Hapa kuna mambo mawili, 1. Waasi, 2.Akili za wenye haki.

Waasi wanaozungumziwa hapo ni Wana wa Israeli ambao wameiasi sheria ya MUNGU na kumwacha Mungu (Soma 2Nyakati 29:6), Na anaposema “akili za wenye haki”.. maana yake zipo “akili za wasio haki” maana yake akili za watu wasiomjua MUNGU, Lakini akili za watu wanaomjua MUNGU/wenye haki ni zile zinazomfanya Mtu amwangalie Muumba wake katika jicho la usafi na utakatifu, ndio zile alizowaambia katika Luka 3:8-14..

Luka 3:7 “Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumwinulia Ibrahimu watoto.

9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

10 Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi?

11 Akawajibu akiwaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afanye vivyo hivyo.

12 Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi?

13 Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyoamriwa.

14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtoshewe na mshahara wenu”.

Akili za wasio haki, zinafundisha DINI tu, kwamba wao ni wayahudi wanaye Baba ambaye ni Ibrahimu, kwahiyo ni uzao mteule, lakini akili za wenye haki zinafundisha kwamba pamoja na kwamba wanaye Baba ambaye ni Ibrahimu bado wanapaswa kujitakasa maisha yao ili wakubaliwe na MUNGU, kuwa tu mwana wa Ibrahimu haitoshi, inahitaji matendo yanayoendana na hiyo Imani.

Hivyo wengi walipojua hilo walitubu na kumrudia Mungu kwa matendo yao.

Hali kadhalika hata leo tunahitaji hizi akili za wenye haki.. hatuwezi kusema sisi ni wakristo wenye madhehebu makubwa, na majina mazuri ya kibiblia halafu matendo yetu hayaendani na asili ya imani yetu, ni lazima tupate akili za wenye haki.

Bwana atusaidie.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Je kuna Yohana wangapi katika biblia?

Je biblia inajichanganya kwa habari za Yohana kuwa Eliya?

YOHANA MBATIZAJI

Nini maana ya “SAA INAKUJA” na “SASA IPO” (Yohana 4:23).

MGAWANYIKO WA ISHARA ZA UJIO WA BWANA YESU KRISTO.

Print this post

ENDELEZA UPONDAJI.

Mwanzo 3:15

[15]nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa..

Kitu pekee Ambacho kilitabiriwa kuweza kuvunja vichwa vya majoka(shetani), ni uzao wa mwanamke tu. Aliyetabiriwa kwenye (Mwanzo 3:15)

Uzao huu wa mwanamke ni Yesu Kristo.. kwasababu ni yeye tu pekee ndiye aliyezaliwa Bila mwanamume, sisi wote ni uzao wa mwanamume…kwasababu mbegu yetu imetoka kwa Baba zetu, lakini Kristo ni mbegu iliyoshuka Kutoka mbinguni, ndio maana hapo anatajwa Kama uzao wa mwanamke.

Yeye kwa ushindi alioupata dhidi ya nguvu za giza kwa kufufuka kwake kutoka kwa wafu na kupaa mbinguni..ni pigo Kubwa sana kwa shetani, ambalo lilimlenga moja kwa moja katika kichwa chake.

Kwasababu kwa njia hiyo wanadamu tumevuka kutoka mautini kwenda uzimani…

Lakini habari njema ni kuwa yeyote amwaminiye, anakuwa sehemu ya uzao huo kwa imani. Na hivyo anapokea mamlaka ile ile ya kuvunja mafuvu ya majoka…mpaka ufalme wa giza kutokomea kabisa katika uso wa ulimwengu..

Wagalatia 3:29

[29]Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

Luka 10:19

[19]Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Kumbuka uwezo huu, hakuna uzao mwingine wowote unaoweza kumuharibu shetani, waafrika hawawezi, wazungu hawawezi, wachina hawawezi, waarabu hawawezi, ukoo wa kiyahudi hauwezi, familia za kichifu, haiwezi, wanadamu wote hawawezi kuponda majoka, hata waungane kwa vifaru vyao na makombora ya nyuklia, bado hawawezi kinyume chake wao ndio watafanyika chakula cha hao majoka.Ni uzao mmoja tu wa Yesu Kristo ndio wenye nguvu hizo..

Swali ni je! Tunapondaje vichwa vya majoka.

Ni kwa kuendelea kuhubiri. Ukikaa tu bila kushuhudia habari za Kristo kwa wenye dhambi, kukaa bila kujishughulisha na shamba la Bwana..Fahamu kuwa ‘mabuti’ yako uliyopewa huko miguuni huyatendei Haki..yapo tu!

Unamridhia shetani, unafurahishwa na uwepo wake shambani mwa Bwana, ndugu njia pekee inayomdosha shetani kwa wepesi ni wewe kukutana na mwenye dhambi mmoja na kumshuhudia habari za wokovu.

Mitume walipoenda kuhubiri baada ya kutumwa na Yesu, waliporudi na ushindi, Yesu aliwaambia nalimwona shetani akianguka kutoka mbinguni kama umeme..

Luka 10:18

[18]Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.

Simama tumia mabuti yako vizuri, endeleza kuponda, ponda kweli kweli, haribu kisawasawa, kwa njia ya injili.

Sio kwa kuimba “nakuponda shetani” au

Kusema “toka shetani” bali kwa injili

Kuponda kwingine ni maombi na kuishi maisha ya utakatifu, huku nako kunahubiri injili ya Kristo na hivyo shetani anaumizwa vibaya sana.

Amka tumia buti zako, kila kichaka katika shamba la Bwana ambacho majoka yamejificha Ni kwenda kuponda tu, mpaka habari njema za ufalme zifike ulimwenguni kote.

Bwana awe nawe.

Amen.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

IHUBIRI INJILI, KILA MAHALI KWASABABU AKUZAYE NI MUNGU.

INJILI NI UWEZA WA MUNGU, UULETAO WOKOVU.

MBONA MMESIMAMA HAPA MCHANA KUTWA BILA KAZI?

Print this post

Je ni sahihi kutumia kumbi za kidunia kuendeshea ibada za kikanisa au semina?

Ni vema kufahamu Kanisa ni nini?

Kanisa sio jengo, au mahali, bali ni watu, walioitwa Na Mungu, waliookolewa wanakusanyika pamoja katika nia moja kumwabudu na kumtumikia yeye.

Hivyo watu hawa wanaweza kukusanyika maeneo yaliyo rasmi, lakini pia maeneo yasiyo rasmi kwa shughuli zao za kiibada..maadamu tu wamekidhi vigezo hivyo vya kiroho.

Kanisa la kwanza lilikusanyika Hekaluni (mahali rasmi kwa shughuli za kiibada tu). Lakini pia lilikusanyika majumbani…wakati mwingi pembezoni Mwa mito na kwenye madarasa..

Matendo ya Mitume 2:46

[46]Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,

Matendo ya Mitume 5:42

[42]Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.

Kama tunavyojua majumbani mahali ambapo, pana shughuli nyingi wakimaliza ibada huwenda sherehe zinafanyika hapo, au vikao vya kijamii, lakini hilo halikuwazuia kutimiza makusudi ya Mungu yaliyoyakusudia.

Hivyo yaweza kuwa ni sahihi endapo, hakuna mahali rasmi bado, ibada zinaweza kufanyika kwenye majengo ya shule, kwenye mabwalo, kwenye kumbi,.viwanjani, hata chini ya miti maadamu tu umoja huo upo na nia ni Kristo..hata hivyo yapo makanisa makubwa na yamefanikiwa lakini bado hayana maeneo yao rasmi ya kukutanikia…lakini kanisa Limesimama.

Mambo tu ya kuzingatia, ni nidhani yenu, adabu na utulivu wa mazingira ya kiroho kwa wakati huo,..ikiwa haya yapo hapo Mnapokusanyikia basi Mungu yupo nanyi..wala si dhambi.

Lakini ni busara na vema zaidi kanisa likatafuta eneo rasmi la kukusanyikia litakalokuwa ni kwa shughuli zao tu za kiibada.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?

MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.

UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?

Print this post

Siku ya kujiliwa inayozungumziwa katika  1Petro 1:12, ni ipi?

1Petro 1:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

Siku ya kujiliwa ni wakati ambao, Mungu anashuka ulimwenguni, aidha kwa kuokoa au kuhukumu.

Zote mbili ni siku za kujiliwa.

Kwa mfano kwa lengo la kuokoa. Upo wakati ambao neema ya Mungu humjia mtu, au taifa, na hivyo wakati huo mara nyingi uamsho mkubwa huwa unapita, Kwamfano, kipindi cha Kristo, kilikuwa ni kipindi maalumu cha Israeli kujiliwa lakini hawakukubali ..isipokuwa wachache..(Luka 19:41-44)

Lakini kwa lengo la hukumu ni siku ambayo kila mmoja wetu atahukumiwa kulingana na matendo yake.

Hivyo tukirudi kwenye 1 Petro 1:12, inayosema ‘Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa’.

Maana yake, matendo mema ya mwamini, hupelekea watu kuupokea wokovu na kumtukuza Mungu,siku neema yao inapowafikia, kwamfano wapo watu ambapo kwa kukuangalia, kwa kipindi kirefu, siku ya kujiliwa inapowafikia inakuwa ni rahisi kuamini na kumtukuza Mungu, kwasababu walishawahi kuona watu waliokoka walivyo na sifa zao njema, mfano upendo, amani, uadilifu..Lakini ukiwa na mwenendo mbovu, siku yao ya kujiliwa inapowafikia, wakikumbuka mwenendo mbovu waliouna kwako , ni ngumu sana kumtukuza Mungu,

Ndicho ambacho mtume Petro alikuwa anakieleza hata mbeleni kidogo, kuhusiana na Wanandoa, kwa upande wa wanawake, akasema, ikiwa mtu ana mume asiyeamini, anao uwezo wa kumvuta ndani ya Kristo kwa mwenendo wake tu.. (1Petro 3:1).

Kwa ufupi ni kuwa mwenendo wako mwema hulainisha njia ya neema ya Kristo Kutenda kazi vema juu ya mtu.

Mungu akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Biblia inamaana gani inaposema “Mungu wa neema yote” (1Petro 5:10)

Nini maana ya ombeni kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi wala siku ya sabato?.

MILANGO YA KUZIMU.

Print this post

UZURI WA MAJIVU.

Isaya 61: 1-3

1 Roho ya Bwana MUNGU i juu yangu; kwa sababu Bwana amenitia mafuta …
kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, WAPEWE TAJI YA MAUA BADALA YA MAJIVU, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na Bwana, ili atukuzwe.

Kitu kikishachomwa na kuteketea kabisa, kinachosalia cha mwisho kabisa huwa ni majivu. Majivu hayana thamani yoyote, ni vumbi jembamba, ambalo likikanywagwa, hutoweka kabisa.

Hivyo zipo nyakati ambazo, watu wanakuwa kama majivu mbele ya macho yao wenyewe, au kwa wengine. Yaani Kila kitu kimekufa na kuteketea kabisa, yale maono aliyokuwa nayo yamefutika, wengine afya zao zimekuwa jivu,hawana matumaini ya kupona tena, wengine maisha yamevurugika, akiangalia muda aliochezea  moyo unapoa kabisa, wengine mahusiano yao yametafunwa, haoni kuendelea mbele.. Rohoni akijiangalia ni jivu tu, kila mahali ni jivu  hajasaliwa na chochote, isipokuwa kukata tamaa na kupotea kabisa..

Ndio maana katika enzi za biblia mtu aliyekuwa katika maombolezo Makali, alijimwagia majivu mwilini kama ishara kuwa umepukutika kabisa..Mfano wa hawa ni Ayubu na Mordekai (Ayubu 2:8, Esta 4:1 )

Lakini Mungu afufuaye matumaini, alitoa unabii huu juu ya mwanawe atakayekuja kuukomboa ulimwengu, akasema..

Amemtia mafuta, “ili awape watu wake taji ya maua badala ya majivu..”

Tafsiri yake, ni kuwa sio tu atamwondoa kwenye majivu  na kumwacha, Hapana, bali anambadilishia na kumpa taji la maua.

Maua huwakilisha heshima, cheo, hadhi, baraka, afya.

Hivyo haijalishi utakuwa katika hali isiyoeleweka kiasi gani, Yupo Yesu wa kukuondoa majivuni na kukuvika maua, ‘Majivu yako leo ndio maua yako baadaye, lakini ikiwa tu utakuwa ndani ya Kristo’.

Usihofu wala usiogope, wala usikate tamaa..Magonjwa hugeuzwa afya.

Yusufu alikuwa majivu gerezani, lakini Mungu alimfanya maua katika kiti cha Farao. Petro alikuwa jivu kwa kumkana Bwana wake, lakini ndiye alikuwa mjenzi wa  kanisa la Kristo. Ruthu alikuwa mjane kwa kufiwa na mumewe, lakini Bwana alimwekwa kama mama wa uzao wa kifalme, Haijalishi hutafaa kwa jinsi gani leo, Kristo yupo kukugeuza, na kukuondoa majivuni.

Lakini hii inahitaji kumpokea na kuendelea kuishi ndani yake. Je upo tayari kuyakabidhi leo maisha yako kwake?

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.

Kwanini mkono wa Musa uingie ukoma?

UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.

Print this post