Who Were the Hivites?
Answer: The Hivites were one of the seven nations that Israel drove out of the Promised Land. The other six were the Canaanites, Hittites, Jebusites, Amorites, Perizzites, and Girgashites (see Joshua 3:10).
The Hivites lived in the hill country of Lebanon, on the northern border of Israel:
Judges 3:3 “These are the nations the Lord left: to test all those Israelites who had not experienced any of the wars in Canaan … the five rulers of the Philistines, all the Canaanites, the Sidonians, and the Hivites living in the Lebanon mountains from Mount Baal Hermon to Lebo Hamath.”
Judges 3:3
“These are the nations the Lord left: to test all those Israelites who had not experienced any of the wars in Canaan … the five rulers of the Philistines, all the Canaanites, the Sidonians, and the Hivites living in the Lebanon mountains from Mount Baal Hermon to Lebo Hamath.”
They were also found in Mizpah, near Gibeon:
Joshua 11:3 “…to the Canaanites in the east and west; to the Amorites, Hittites, Perizzites and Jebusites in the hill country; and to the Hivites below Hermon in the region of Mizpah.”
Joshua 11:3
“…to the Canaanites in the east and west; to the Amorites, Hittites, Perizzites and Jebusites in the hill country; and to the Hivites below Hermon in the region of Mizpah.”
So, the Hivites lived in different parts of the land. They were the same people who deceived the Israelites into making a treaty of peace with them. They pretended to come from a faraway country, while in reality, they lived nearby (see Joshua 9:1–27).
The main reason God removed these seven nations from the Promised Land was their wickedness. They practiced sorcery, murder, immorality, oppression, injustice, and many other evil deeds without fear of God. That was the first reason. The second reason was God’s promise to Abraham.
Deuteronomy 9:4–6 “After the Lord your God has driven them out before you, do not say to yourself, ‘The Lord has brought me here to take possession of this land because of my righteousness.’ No, it is on account of the wickedness of these nations that the Lord is going to drive them out before you.
Deuteronomy 9:4–6
“After the Lord your God has driven them out before you, do not say to yourself, ‘The Lord has brought me here to take possession of this land because of my righteousness.’ No, it is on account of the wickedness of these nations that the Lord is going to drive them out before you.
It is not because of your righteousness or your integrity that you are going in to take possession of their land; but on account of the wickedness of these nations, the Lord your God will drive them out before you, to accomplish what he swore to your fathers, to Abraham, Isaac and Jacob.
Understand, then, that it is not because of your righteousness that the Lord your God is giving you this good land to possess, for you are a stiff-necked people.”
For these same reasons, Israel too was later removed from the Promised Land and taken into captivity in Assyria and Babylon.
2 Chronicles 36:14–17 “Furthermore, all the leaders of the priests and the people became more and more unfaithful, following all the detestable practices of the nations and defiling the temple of the Lord, which he had consecrated in Jerusalem.
2 Chronicles 36:14–17
“Furthermore, all the leaders of the priests and the people became more and more unfaithful, following all the detestable practices of the nations and defiling the temple of the Lord, which he had consecrated in Jerusalem.
The Lord, the God of their ancestors, sent word to them through his messengers again and again, because he had pity on his people and on his dwelling place.
But they mocked God’s messengers, despised his words and scoffed at his prophets until the wrath of the Lord was aroused against his people and there was no remedy.
He brought up against them the king of the Babylonians, who killed their young men with the sword in the sanctuary, and did not spare young men or young women, the elderly or the infirm. God gave them all into the hands of Nebuchadnezzar.”
And even today, for the same reasons, many of us lose the blessings and promises of God and end up living under curses.
Remember this always: the first poison to destroy a person is sin, not Satan. What drove the first man out of the Garden of Eden was sin. What reduced human life from eternity to only 120 years was sin. That’s why our greatest fear should be sin, not Satan—because Satan uses sin to destroy humanity.
If a person can overcome sin by remaining in the Word of God, Satan becomes powerless—like a soldier who has been stripped of his weapons.
The key to overcoming sin is found only in the Lord Jesus, and it begins with repentance, followed by true baptism, and finally the infilling of the Holy Spirit.
Acts 2:38 “Peter replied, ‘Repent and be baptized, every one of you, in the name of Jesus Christ for the forgiveness of your sins. And you will receive the gift of the Holy Spirit.’”
Acts 2:38
“Peter replied, ‘Repent and be baptized, every one of you, in the name of Jesus Christ for the forgiveness of your sins. And you will receive the gift of the Holy Spirit.’”
If a person sincerely completes these three steps, sin will not be able to defeat them, and they will continue to live in the promises and blessings of God—without the need for oil, salt, or so-called “anointed soil.”
May the Lord help us.
Print this post
Swali: Maandiko yanasema katika Mathayo 5:42 kuwa tumpe kila atuombaye na kila atukopaye tusimpe kisogo?.. Je hata kama mtu ni mzembe na kila wakati anatumia vibaya vile ninavyompa, nina amri ya kumpa mara kwa mara kila atakaponiomba?
Jibu: Turejee hayo maandiko..
Mathayo 5:42 “Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo”.
Haya ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo..ambayo anatufundisha umuhimu wa kutoa na kukopesha watu wote pasipo kuwa na vizuizi vingi, lakini swali ni je! Ni kila mtu anayekuja kutuomba tunapaswa tump kulingana na hilo andiko?
Jibu ni La!.. si kila mtu anayetaka kukopa tuweza kumpa, na si kila anayeomba tunapaswa tumpe!.. Kwasababu zifuatazo.
1. HUNA HIKO ANACHOKIOMBA.
Kama huna hiko anachokuomba, huwezi kumpa, kwasababu huwezi kumpa mtu kitu usichokuwa nacho au kilicho juu ya uwezo wako, kwamfano mtu anataka kukopa kwako milioni moja, na wewe huna hiko kiasi..hapo huwezi kufungwa na andiko hilo kwamba kila akuombaye unapaswa uumpe!
2. HAJAKIDHI VIGEZO VYA KUPEWA.
Vipo vigezo vya mtu kupewa kitu, kwamfano mtu anataka kukopa au kuomba pesa ya kwenda kununua pombe, au kwenda kufanya dhuluma au biashara haramu, au kwaajili ya kwenda kutoa sadaka kwa miungu hapo hata kama tunacho hiko kiasi, hatupaswi kumpa wala kumkopesha.
Hata Mungu wetu alituambia tumwombe naye atatupa
Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa;
Lakini ni huyo huyo Mungu wetu aliyetuambia tena kuwa, tukiomba nje ya mapenzi yake hatupati..
1Yohana 5:14 “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia”.
Yakobo 4:3 “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”.
Kwahiyo na sisi ni hivyo hivyo, ni lazima tuangalie anayekuja kuomba kama amekidhi vigezo.. wengine wanaomba kwaajili ya kwenda kufanya maasi, wengine uhalifu, wengine si makini, maana yake wana hali ya uzembe katika matumizi yao (hawa hawapaswi kurudia kupewa mara kwa mara mpaka watakapobadilika), wengine wanaomba kwa tamaa tu (mfano wa hao pia ni watoto wadogo) n.k
Kwahiyo tukirudi hapo katika hilo andiko Bwana Yesu alilosema kuwa “Kila akuombaye mpe”, tutakuwa tumeshaelewa kuwa si kutoa tu bila kufikiri wala kutafakari kwa kila mtu, bali ni kumpa kila akuombaye ambaye AMEKIDHI VIGEZO VYA KUPEWA!.
Kama mtu amekidhi vigezo vya kupewa nawe unacho hiko kitu, usimpe kisogo, kwasababu ni Mungu aliyemleta kwako huwenda ili amtengeneze na wewe pia upate thawabu, ukimpa kisogo mtu anayekuomba na ilihali unacho hicho kitu, ni dhambi!.. kwasababu uchoyo ni shina la dhambi.
Luka 12:15 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”.
Bwana atusaidie.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Ipi tofauti kati ya sadaka ya dhambi na sadaka za hatia?
Nini maana ya hekima ya maskini haisikilizwi? (Mhubiri 9:16)
USINIPE UMASKINI WALA UTAJIRI. (Mithali 30)
Je! Wamwona mtu mwenye bidii katika kazi zake?
Nini maana ya huu mstari; Mithali 10:22 “Baraka ya Bwana hutajirisha, Wala hachanganyi huzuni nayo”
Mtume Paulo, alipokamatwa kule Yerusalemu na kupelekwa mbele ya wafalme kuhukumiwa, tunaona ujasiri wake ulikuwa wa ajabu, badala atumie nafasi ile kujitetea, kimahakama, kinyume chake alitumia nafasi ile kuhubiri injili, kiasi cha kumfanya mfalme Agripa kushawishwa kwa muda mfupi kuiamini injili.. Ujasiri wa namna hiyo hakika, ni wa kuigwa sana.
Matendo 26:28
25 Lakini Paulo akasema, Sina wazimu, Ee Festo mtukufu, bali nanena maneno ya kweli na ya akili kamili. 26 Kwa maana mfalme anajua habari za mambo haya, nami naweza kusema naye kwa ujasiri, kwa sababu najua sana ya kuwa hapana neno moja katika hayo asilolijua; kwa maana jambo hilo halikutendeka pembeni. 27 Mfalme Agripa, je! Wawaamini manabii? Najua ya kuwa wawaamini. 28 AGRIPA AKAMWAMBIA PAULO, KWA MANENO MACHACHE WADHANI KUNIFANYA MIMI KUWA MKRISTO. 29 Paulo akamjibu, Namwomba Mungu kwamba, ikiwa kwa machache au ikiwa kwa mengi, si wewe tu ila na hao wote wanaonisikia leo wawe kama mimi, isipokuwa vifungo hivi.
Lakini Tunaona jambo moja, huyu mfalme Agripa alichomwa sana na maneno ya mtume Paulo, alishawishwa ipasavyo na injili ile, lakini hakuwa tayari kugueka moja kwa moja kwa Kristo, aliishia tu kushawishwa.. Ukweli ni kwamba mtu katika hatua hiyo bado hujaokolewa..
Ni sawa na leo hii, watu wengi wanapoisikia injili, ni kweli wanashawishwa, wanaiheshimu, wanaifurahia, wanachomwa mioyo yao, wengine wanaomboleza na kuhuzunika juu ya dhambi zao, lakini je! Wameikubali na kutii?
Utaona wataishia tu kusema, nimebarikiwa!, wataishia kusema Neno zuri linaonya!, wataishia kusema, Mungu nisaidie, nimeguswa leo, ndugu hiyo haimaanishi kuwa umeokoka, huna tofauti na Agripa.
Watu walioshawishwa kwelikweli, waliochomwa mioyo, ni lazima utaona kuna kitu cha ziada watafanya watauliza “Tufanyeje ndugu zetu?”
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU? 38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Matendo 2: 37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, TUTENDEJE, NDUGU ZETU?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Umeona?, hawakuishia tu kusema “asante Petro kwa Neno” hawakuishia kusema “ubarikiwe mtumishi” ..“Umetujenga mchungaji”. Walisema, tutendeje ndugu zetu?..Tuchukue hatua gani?
Utaona Wakabatizwa, wote siku ileile, wajazwa Roho, Wakadumu katika fundisho la mitume, kila siku. Ndio hao walioisambaza injili ulimwenguni kote.
Leo ndio tunahitaji kuona Kundi la watu wa namna hii, ambao wanachukua hatua ya kumpokea Yesu kikamilifu na kumfuata kwa mioyo yao yote, kimatendo. Na sio kama akina Agripa, ambaye hakuwa na matunda ya kuitii injili.
Saa ya wokovu ni sasa, usiseme kesho nitaokoka, hakuna wokovu wa kesho, acha kujidanganya, bali ni leo. Aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi usifurahie mafundisho, usifurahie miguso ya ki-mahubiri swali ni je umeokoka? Kristo leo akirudi utaenda naye?
Na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
WOKOVU NI SASA
Sauli (Mtume Paulo) alipokuwa anaelekea Dameski kwa lengo la kuwafunga na kuwatesa watakatifu, kama tunavyoifahamu habari alitokewa na Yesu njiani, mwanga Mkali ulimpiga machoni, akashindwa kuona, Wakamchukua mpaka ndani ya mji akiwa kipofu.
Lakini tunaona alipokuwa kule, hakuwa katika hali ya kawaida, bali katika maombolezo makubwa rohoni, hakula chakula chochote, wala maji..(maana Yake alikuwa katika mfungo), lakini si hilo tu zaidi sana alikuwa akiomba dua.
Baada ya hapo tunaona jambo lingine likitokea mtu mmoja aliyeitwa Anania anatokewa na Yesu, kisha anaagizwa amfuate Paulo. Lakini eneo analoagizwa ni katika njia iliyoitwa NYOFU…
Maana Yake “njia iliyonyoka”.
Matendo 9:8-12
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. [9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi. [10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. [11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba; [12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
[8]Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
[9]Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.
[10]Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.
[11]Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;
[12]naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Unaweza kujiuliza kwanini apelekwe njia ile ..tena iitwe kwa jina la NYOFU na si lingine labda “njia kuu”, au “nzuri” au “panda” bali nyofu?
Ni kwasababu rohoni, Kristo huwaweka watu wake Katika hiyo njia. Njia iliyonyoka.
Hapo mwanzo Paulo alikuwa katika njia iliyoharibika, mbovu, ya kuupinga ukristo, ya uuaji, ya utukanaji, ya dhambi, ya mauti.
Lakini alipokutana na YESU, akatolewa huko akawekwa katika njia iliyonyooka ya utumishi wake.
Ni ajabu kuona watu wengi leo wanampinga Kristo, hawataki kuokoka, wakidhani udini ndio utawanyooshea mapito yao, fedha ndio zitawasawazishia mabonde Yao, elimu ndio zitaangusha milima yao.
Kumbe hawajui kuwa njia iliyonyooka ni maisha ndani ya Kristo tu!. Kwingine kote ni mabonde, milima Na mwishowe shimoni na mauti. Hakuna pumziko Nje ya Kristo.
Yohana mbatizaji aliliona hilo akapaza sauti yake kwa nguvu Akisema..
Yohana 1:23
[23]Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.
Kumwamini Yesu ndio kuinyoshe njia ya Bwana..
Je upo katika njia ya nyofu.
Okoka leo, uponywe kila kitu ndugu, kumbuka Umepotea nje ya Kristo,hakuna mjadala na huo ndio ukweli, hakuna tegemeo kama Yesu hajakuokoa. Fanya haraka utubu, leo uiamini kazi ya Kristo ya ukombozi iliyokamilishwa kwa ajili yako pale msalabani. Muda ni mchache mlango wa neema hautadumu Milele.
Ikiwa upo tayari leo kumkabidhi Yesu maisha yako. Basi bofya bofya hapa kwa mwongozo wa sala ya toba. >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Jehanamu ni nini?
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 1)
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Awali tufahamu nini maana ya kumwabudu Mungu, Kumwambudu Mungu si kumwimbia tu Mungu nyimbo ya kuabudu tulizozizoea, Neno kuabudu limetokana na neno “ibada” hivyo kumwabudu Mungu ni “kumfanyia ibada”
Sasa ibada imebeba mambo mengi ikiwemo kuomba, kumwimbia Mungu, kumtolea Mungu, kujifunza Biblia, kushiriki meza ya Bwana n.k
Sasa ni kwa namna gani tutamwabudu Mungu?.. si kwa njia nyingine zaidi ya hizo, ambazo ni kuomba ambako kunaweza kuhusisha kwa kupiga magoti au kusujudu, pia kumwimbia nyimbo za kumshukuru na kumsifu, na kumtolea matoleo yetu, na kujifunza maneno yake na kuyaishi na mambo mengine yanayoendana na hayo..
Maana yake tukiyafanya mambo hayo katika ukweli wote na katika roho bila kupunja chochote tutakuwa tunamwabudu Mungu..
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba kumwabudu Mungu ni kumfanyia Mungu ibada katika ukweli wote na katika roho, kwanini ni katika kweli yote na katika roho??..Turejee maandiko yafuatayo..
Yohana 4:23 “Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”.
Hivyo mpendwa kama unataka kumwabudu Mungu kweli kweli usikwepe kukusanyika kanisani, na hakikisha unakusanyika katika usafi na utakatifu, pia usikwepe ushirikia wa meza ya Bwana, pia usikwepe maombi binafsi na ya pamoja, usikwepe kumtolea Mungu (ni jambo la msingi sana), pia usikwepe kumshukuru Mungu na kumsifu kwa njia ya nyimbo na tenzi za rohoni.
Wakolosai 3:16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu”.
Nini maana ya kumwabudu Mungu katika Roho na kweli?
EPUKA KUCHELEWA IBADA.
NA WATU WOTE WALIKUWA WAKIAMKA MAPEMA, WAENDE HEKALUNI.
NAWAAMBIA MAPEMA!
MWONGOZO WA MAOMBI YA ASUBUHI.
Je unafahamu asili ya kanisa la Kristo? Ni vema wewe kama mwamini ufahamu mapito ya Imani yako.
Mpaka leo hii injili iliyotokea Yerusalemu (Israeli) kunifikia mimi na wewe, fahamu kuwa kuna mapito ambayo waliyapitia , ambayo na sisi tunapaswa tuyafahamu ili tuweze kuifikisha injili hiyo kila mahali,duniani kote na kwa vizazi vyote bila kuwa na deni.
Mwanzoni kabisa kanisa lilikuwa mahali pamoja pale Yerusalemu, Lakini dhiki ilipotokea na kuwa kubwa, mpaka watakatifu kuuliwa hadharani mfano Stefano, iliwagharimu wengi wa wakristo wakimbie Israeli na kwenda mbali kwenye mataifa mageni.
Lakini kuondoka kwao haikuwa mwisho wa safari, kwenda kuanza maisha mapya ya utulivu..hapana kinyume chake kule walipofika ugenini waliendelea kulihubiri lile Neno, kama tu vile walivyokuwa nyumbani.
Matendo ya Mitume 8:1,4
[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume… [4]Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
[1]Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume…
[4]Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
Umeona asili ya kanisa la Kristo.. Ni sawa na leo, kuhama-hama kwa watu, pengine kwasababu za kikazi, kivita, kimasomo, kijamii n.k. unajikuta unaenda kijiji jirani, mkoa mwingine, au taifa lingine geni. Jiulize Je! Unalihubiri Neno kama kule nyumbani ulipokuwepo au ndio unabadilika tabia.
Kanisa la kwanza halikupoteza ubora mahali popoteugenini..Kwamfano utaona mtume Petro Aliendelea kuandika nyaraka zake kwa watakatifu walitoawanyika..mataifa mbalimbali, akijua kuwa injili ya Kristo inaendelea,
1 Petro 1:1
[1]Petro, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Utawanyiko, wakaao hali ya ugeni katika Ponto, na Galatia, na Kapadokia, na Asia, na Bithinia;
Mazingira hayapaswi kuwa kizuizi cha ushuhudiaji wako, kwasababu kanisa halizuiwi na mazingira..Shuhudia Kristo popote ulipo kwasababu popote walipo watu, Mungu yupo hapo. Usipumbazwe na fikra za kusema mimi nilipo nashindwa kushuhudia afadhali kule nilipotoka, hii kazi mpya niliyoipata siwezi kuwashuhudia watu, ndugu hilo si wazo la Mungu. Fikiri Mungu akupe hekima, na hakika utaona upenyo.
Shalom.
Uinjilisti kama agizo kuu la Bwana.
INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.
TUTAFUTE KWA BIDII KUKAA NDANI YA YESU.
Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Kuna mambo unaweza ukayafanya ukadhani ni sawa machoni pako. Lakini kumbe hujui kama unaleta huzuni kubwa kwa Kristo.
Mtume Paulo ambaye hapo mwanzo aliitwa Sauli, alikuwa akishindana na mawazo, na jamii ya watu waliomwabudu Mungu akidhani anashindana na ubaya kumbe anashindana na Kristo mwenyewe.
mpaka alipokutana na Kristo mwenyewe njiani alipokuwa anakwenda Dameski..akaambiwa maneno haya..Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Matendo 9:4-5
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi? [5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
[4]Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
[5]Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
Hilo Neno waniudhi, kwenye tafsiri ya asili linamaanisha hasaa “wanitesa”? Biblia ya kiingereza inaeleza vizuri zaidi inatumia neno “persecutest”…yaani kutesa..
Paulo alikuwa mfano wa wapagani waliomtesa Kristo, pale alipokuwa anawaburuta watakatifu, anawafunga, anawapinga, na kuwatukana…hakujua kuwa anamtesa Kristo mwenyewe..Leo hii makundi ya watu wanaowapinga watakatifu, wanaoyapinga makanisa ya kweli, wanaowatukana watumishi wa Mungu, wanaowapiga na kuwaua wafahamu kuwa wanamtesa Kristo.
Ikiwa wewe ni mmojawapo kuwa makini, uache mara moja, ni heri utubu leo umpe Yesu maisha yako. Akuokoe.
Lakini kundi la pili ni wale waamini- waliorudi nyuma. Mtu ambaye ameshaokoka, Halafu anaiacha Njia kwa makusudi anayafanya yale machafu aliyoyaacha nyuma huyo anamtesa Kristo, tena yale mateso ya msalabani kabisa.
Waebrania 6:4-8
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu, [5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo, [6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri. [7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu; [8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
[4]Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
[5]na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
[6]wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri.
[7]Maana nchi inayoinywa mvua inayoinyeshea mara kwa mara, na kuzaa mboga zenye manufaa kwa hao ambao kwa ajili yao yalimwa, hushiriki baraka zitokazo kwa Mungu;
[8]bali ikitoa miiba na magugu hukataliwa na kuwa karibu na laana; ambayo mwisho wake ni kuteketezwa.
Acha tabia ya kuzoelea dhambi, ukishaokoka ukitenda dhambi, haihesabiki kama kosa kama la wapagani bali uasi.
Kama Ulimpokea Kristo ili umtese, kuokoka kwako kuna maana gani? Ulishawahi ona mtoto anampiga Baba yake? Hiyo si laana?
Ndivyo ilivyo kwako unapozini na huku umeokoka, unapokunywa pombe na kufanya anasa.. Tubu haraka sana umrudie Kristo
Penda utakatifu, Ishi maisha matakatifu..
IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.
Kwanini Yeremia ailaani siku yake ya kuzaliwa? (Yeremia 20:14)
Nini maana ya Mithali 16:30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka;
WhatsApp
Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.
Kwa lugha rahisi kuna tofauti ya kuhubiri na kushuhudia.Yesu alituita tuwe mashahidi duniani.. Na hiyo ni kazi ya kila mmoja, Wito wa kumtangaza Yesu, sio wa kimahubiri, bali ni wa kiushuhudiaji.
Mhubiri ni mtu anayesimama na biblia, anayefundisha maandiko, anayefafanua, hadithi mbalimbali na mafunzo katika biblia kisha kutarajia watu kugeuka kwa mafundisho hayo. Huyu anaweza akawa mchungaji, mwinjilisti, mtume, Askofu, shemasi n..k
Lakini shahidi ni mtu aliyeona ukweli wa jambo Fulani, kisha akasimama kama mteteaji au mthibitishaji wa ukweli huo.Ndio kazi tuliyopewa sisi sote kufanya kuhusu Kristo, kuwa mashahidi wake ulimwenguni kote. Wa yale yote aliyotutendea sisi katika maisha yetu. Yaani yale aliyoyasema tukayathibitisha sisi wenyewe kuwa ni kweli katika maisha yetu.
Kwamfano pale aliposema njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo nami nitawapumzisha (Mathayo 11:28). Ulipokwenda kwake ukaona mzigo huo umetuliwa, Hivyo tukio hilo huna budi kusimama na kulithibitisha kwa wengine, na wao pia waamini, ili watendewe jambo hilo hilo.
Pale Yesu aliposema tukiamini tukabatizwa, tutapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.(Matendo 2:38) Na wewe sasa umepokea Roho Mtakatifu, umejua ni ukweli, sasa hapo ndipo unapokwenda kuwashuhudia kwa wengine ukweli huo.
Pale ulipoponywa, ulipofunguliwa, ulipoonyeshwa ishara, ulipopewa nguvu ya kushinda dhambi fulani.. Hapo ndipo unapopashuhudia..Na kwa kupitia ushuhuda huo, mwingine atajengwa Imani na kumwamini Yesu kama wewe ulivyoamini hatimaye kuokoka.
Sasa kazi hii haihitaji theolojia ya biblia, haihitaji ukomavu wa kiroho, haihitaji mifungo na maombi, inahitaji tu kufungua kinywa chako na kuanza kueleza uzuri ulioupata ndani ya Kristo, na kwa njia hiyo ndio Mungu atamshawishi mtu na kuokoka.
Ukiwa kama mkristo umeokoka labda tuseme leo, Kumbuka tayari una deni la kuanza kushuhudia uzuri wa Kristo kwa maneno hayo hayo machache uliyonayo kinywani mwako.. Ndicho alichokifanya Paulo baada tu ya kubatizwa..
Matendo 9:17 Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu.Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;19 akala chakula, na kupata nguvu. Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski.20 Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.21 Na wote waliosikia wakashangaa, wakasema, Siye huyu aliyewaharibu walioliitia Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuwa amekuja kwa kusudi hilo, awafunge na kuwapeleka kwa wakuu wa makuhani?22 Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.23 Hata siku nyingi zilipopita, Wayahudi wakafanya shauri ili wamwue.
Tatizo linatokea pale ambao tunaona kazi ya injili ni ya watu maalumu na ni nzito . Hapana, kumbuka anayeshawishi watu mioyo ni Mungu, sio kwa wingi wa vifungu vya maandiko au kwa uzoefu wa kuhubiri, bali kwa Roho Mtakatifu tu. Maneno mawili, tu yenye kumshuhudia Yesu, yana nguvu ya kugeuza mtu zaidi hata ya maneno elfu ya vifungu vya biblia.
Unapokwenda kushuhudia usifikiri fikiri ni nini utasema, wewe anzia pale ambapo ulitendewa na Yesu ikawa sababu ya wewe kuokoka.. muhadhithie huyo mtu Habari hiyo kwa taratibu. Utashangaa tu, huko huko Katikati Mungu anakupa hekima na kinywa cha kumhubiria mpaka utashangaa hekima hiyo umeitolea wapi. Pengine mtu atakuuliza swali umsaidie, lile jibu linalokuja kwenye kinywa chako liseme, wala usijidharau au usiogope, anayemshawi mtu ni Mungu, yeye kuelewa au kutokuelewa hiyo sio kazi yako ni ya Mungu, uwe tu na ujasiri, kwasababu hakuna Habari yoyote yenye maudhui ya Kristo ndani yake haina matokeo.
Anza sasa kumshuhudia Yesu, Na kwa Pamoja tuujenge ufalme wa Kristo. Anza na marafiki zako, familia, wafanyakazi wenzako, majirani zako kabla ya Kwenda hata mwisho wa nchi.
Mungu akubariki
JINSI YA KUSIMAMA NA KUFUNDISHA/ KUHUBIRI
YESU KATIKA KUCHOKA KWAKE.
Enendeni ulimwenguni mwote
SWALI: nini maana ya Yohana 17:20
[20]Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Ni akina nani hao ambao wataamini Kwasababu ya Neno lao, Bwana Yesu aliotaka kuwaombea?
JIBU: Sura hiyo ya 17 ni sura iliyoelezea kwa kina dua ambayo Bwana Yesu aliifanya kwa mitume wake kwa Baba.
Ambapo aliwaombea mambo kadha wa kadha ikiwemo walindwe katika umoja wa Roho, walindwe na yule mwovu, watakaswe na ile kweli.. Lakini pia Bwana Yesu hakuishia kuwaombea wao tu, bali na wengine ambao mitume wake watawahubiria injili na kuamini baadaye. Na hao pia maombi yake yalikuwa ni yaleyale kwao.
Maana yake ni kuwa watu wote walioamini kwa injili ya mitume walishiriki dua hiyo ya Kristo, Na hao si wengine zaidi ya wale watakatifu wa kanisa la kwanza, hadi sisi tuliopo sasa, hadi na wale watakaokuja baadaye.. sisi wote ni washirika wa dua ile (Yohana 17), kwasababu tumeamini katika injili moja ya mitume..
Ndio sababu kwanini maandiko yanasema Kristo anatuombea…maana yake ni kuwa sasa anatuombea kwa yule Roho Mtakatifu auguaye ndani yetu, lakini pia analituombea alipokuwa duniani ambapo sala hiyo tunaona matokeo yake hata sasa.
Waebrania 7:25
[25]Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai sikuzote ili awaombee.
Hii ni kututhibitishia Kuwa pale tunapomwamini Kristo upo ulinzi usioelezeka unawekwa juu yetu, kiasi kwamba malango ya adui hayawezi Kushinda..kinachohitajika ni kutii tu.
Warumi 8:34
[34]Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.
Je na wewe ni mshirika wa sala hiyo ya Bwana? Kwa kumpokea Bwana Yesu? Kama ni la! Basi nafasi ni sasa mwamini Yesu upokee uzima wa milele.
Lakini pia Bwana anatufundisha namna sahihi ya kuomba..hatupaswi tu kuyaombea yale matunda tunaoyaona..bali hata na yale yatakayokuja baadaye..wale watakaokoka baadaye kwasababu ya Neno letu.
WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.
MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.
“Akaiona imefagiwa na kupambwa” Maana yake nini (Luka 11:26).
Mariamu alipotokewa na Malaika na kuelezwa habari ya mambo ambayo hayawezekaniki kibinadamu, alionyesha tabia ya kitofauti sana…hakuanza kubisha, Hakuanza kukinzana na kusudi na mpango wa Mungu juu yake, ulio juu ya upeo wa ufahamu wake, kinyume chake aliukubali, tena si Kwa maneno ya juu juu tu, bali kwa ukiri wa utumwa…akasema
“Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema.”
Maana yake ni kuwa ikiwa jambo hilo linanilazimu kulitumikia mimi nitafanya hivyo kama Mtumwa..
Luka 1:34-35,38
[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? [35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu… [38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
[34]Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
[35]Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu…
[38]Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
Mariamu ni kielelezo kamili cha mwanamke thabiti wa kikristo, lakini sio tu mwanamke bali bali kwa kanisa la Kristo kwa ujumla.
Utii wa namna hii ndio Bwana anaoutaka kwa watu wote wamchao yeye..
Ijapokuwa kibinadamu haikuwezekana, akijua pia ikishatokea itamletea aibu katika jamii, atakaposadikika amepata ujauzito, kimiujiza hakuna atakaye mwelewa, watasema ni mzinzi, akijua pia kuna majukumu mengine mazito yatafuata..bado alilipokea kusudi la Mungu..lililo juu ya uwezo wake.
Hakukubali kuingia kwenye kosa kama la Musa, kusema mtume mwingine, hakulimbikia kusudi la Mungu kama Yona kukimbilia Tarshishi…bali alilipokea zaidi ya mtumwa.
Si ajabu kwanini Bwana alimpa neema kubwa namna ile…
Ndugu/kaka Bwana anatazama Utayari wako zaidi ya uwezo wako, anatazama utii wako zaidi ya umri wako.
Kila mmoja wetu leo, aliyeamini katika agano jipya ameitwa kufanya MAKUBWA mfano tu wa Mariamu…Hakuna hata mmoja ambaye hajaitwa kwa ajili ya mambo makubwa ya Mungu… kwasababu Mungu ni Mungu wa miujiza na yaliyoshindikana.
Isipokuwa Imani zetu ni haba Kwa Mungu ndio maana hatuoni matokeo makubwa. Kinachohitajika ni kujiachilia tu kwake..kisha kumwacha yeye atende kazi zake ndani yetu.
Haijalishi wewe ni mwanaume au mwanamke, mzee au kijana, una elimu au huna elimu, tajiri au maskini.. kubali kujiachia kama Mariamu katika kusudi lolote la Mungu.. unapoona una nafasi ya kuombea wagonjwa Fanya hivyo, una nafasi ya kuwashuhudia watu mitaani, masokoni, viwanjani fanya hivyo, huko huko Bwana atajifunua kwako kwa namna isiyo ya kawaida. Na Utukufu utamrudia yeye.
Kumbuka tu Mungu amechagua kutumia vyombo Dhaifu kukamilisha kusudi lake timilifu.
Je Mariamu alikuwa na umri gani alipochukua mimba ya Bwana YESU?
JE BIKIRA MARIAMU ALIKUFA?
USICHELEWE KUMPAKA BWANA MARHAMU!