Hosea 10:12
[12]Jipandieni katika haki, vuneni kwa fadhili; uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA, hata atakapokuja na kuwanyeshea haki.
Tunaishi katika majira ambayo kumtafuta Mungu hakupaswi kuwe kwa juu juu tu… kumbuka Neno la Mungu linatufananisha sisi na wakulima wapandao na wenye malengo ya kuvuna kwa vile tuvipandavyo…
Na sikuzote mkulima yoyote labda tuseme yule wa nafaka hatupi mbegu zake tu juu ya ardhi akitarajia ziote, bali utamkuta Na jembe, tena lile imara analikita chini ardhini kwa nguvu, huku jasho likimtoka.
Kimsingi kupiga jembe chini ndio kazi aliyonayo mkulima, haijalishi ardhi itakuwa ngumu kiasi gani hana budi kuichimba kwa nguvu, ili mbegu izame aone matokeo… vinginevyo hatavuna chochote.
Bwana anasema…
Uchimbueni udongo wa mashamba yenu, kwa maana wakati umewadia wa kumtafuta BWANA,
Kumtafuta BWANA…ni kuchimba chini…
Yaani kama ni maombi basi ni Maombi ya masafa marefu sio yale mfano wa kuombea chai ya asubuhi, kama ni kusoma na kujifunza Neno, basi ni kufanya hivyo vya kutosha kila siku sio kuamka na mstari mmoja, au kusubiri Tu kuhubiriwa YouTube halafu basi..
Kama ni ibada, kujifunza Kudumu uweponi mwa Mungu kwa nyakati ndefu…huko ndiko kuchimba chini ambako Bwana anakutaka…
Tusipende mambo ya juu juu, yatatugharimu vibaya sana, na tutajikuta tunapata hasara ya mbegu zetu kuliwa na ndege..
Fahamu kuwa Yesu amekaribia kurudi.. Je umezama Kweli ndani yake? Je unamtafuta kwa bidii, je umejiweka tayari kumpokea? Kama ni hapana basi anza sasa..
Kwasababu mbinguni hakitaingia kinyonge.
Chimba ardhi yako.
Neema ya Bwana akufunike.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Print this post
Zaburi 29:3
[3]Sauti ya BWANA i juu ya maji; Mungu wa utukufu alipiga radi; BWANA yu juu ya maji mengi.
Ulishawahi kujiuliza kwanini ulimwengu ufunikwe kwanza na maji kote, ndipo Mungu atue juu yake lakini pia aseme Neno?(Mwanzo 1:1-2)
Vipi kama maji yasingekuwepo je Mungu asingesema lolote?….ndio ni kweli Neno la Bwana linasimama mahali popote lakini amejiwekea utaratibu wake wa kuzungumza..si kila eneo sauti yake yenye mamlaka ataiachia..
Palipo na maji sauti yake hutokea…
Ndio maana baadaye mwandishi wa zaburi Kwa uvivio wa Roho anasema…
Sasa ni lazima tufahamu kwamba Mungu hakai kwenye maziwa, au bahari au mito…hapana bali Mungu hukaa katika moyo wa Mtu..
Lakini moyo wenye maji mengi… na hapo ndipo Sauti yake yenye nguvu kama radi inaposikika…
Hata mawingi ili yatoe radi huhitaji yajawe kwanza na maji, bila hivyo kamwe huwezi sikia sauti yoyote nyuma yake
Biblia inasema…
Yohana 4:13-14
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; [14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Na mahali pengine anasema maji hayo ni Roho Mtakatifu. (Yohana 7:39)
Mtu yeyote anayempa nafasi Roho Mtakatifu, ndani yake, kwa kutii, kwa kuwa mwombaji, mwenye ibada nyingi kumtafuta Mungu, kujitenga na dhambi …Huyo Anaongeza wingi wa maji ndani yake na matokeo yake ni kuwa sauti ya Mungu inasikika, na sio tu kisikika lakini pia inakuwa na nguvu kama ngurumo.
Tukiwa wakame, au tuna maji machache, kinyume chake, ni kuwa hatuwezi kumwona Mungu, wala kuisikia sauti yake. Penda kumtii Roho Mtakatifu. Tafuta kwa bidii kumjua Mungu, ongeza maji yako, Bwana aseme.
Mafundisho mengine: