Jina la Mwokozi Mkuu YESU KRISTO, libarikiwe.
Kabla ya kusogea mbele kujifunza ujumbe huu, ni vizuri tukarejea sehemu ya kwanza ya ujumbe huu inayosema “FAHAMU JINSI YA KUPATA MAMLAKA YA DAMU YA YESU”
Katika ujumbe huo tuliona ni kwa namna gani tunaweza kuwa na uhalali wa kuitumia Damu ya YESU, ikiwa tutakuwa ndugu zake, fuatilia ujumbe huo hapa >>>FAHAMU JINSI YA KUPATA MAMLAKA YA DAMU WA YESU.
Sasa kuna umuhimu mkubwa sana wa “KUYAJUA” na “KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU”.. Kwani hiyo ndio tiketi ya ‘KUMWONA MUNGU’ siku ya mwisho.
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni”.
Na tena Neno la Mungu linatusisitiza kutafuta kuyafanya mapenzi ya Mungu kwa bidii muda tuliobakiwa nao hapa duniani..
1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali KATIKA MAPENZI YA MUNGU, WAKATI WENU ULIOBAKI WA KUKAA HAPA DUNIANI”.
Sasa Mapenzi ya MUNGU yamegawanyika katika sehemu kuu Mbili.. 1) Mapenzi ya Mungu kwa Mtu binafsi, na 2) Mapenzi ya Mungu kwa watu wote.
Ni lazima tufanya Mapenzi ya Mungu katika migawanyiko yote hii miwili.. ni kama sheria, zipo sheria ulizojiwekea wewe, na zile ulizowekewa na nchi, ni lazima zote iziishi. Hali kadhalika yapo mapenzi ya Mungu kwako wewe au mimi binafsi, na yale Mapenzi ya Mungu kwa watu wote.. hebu tutazame moja baada ya lingine.
1. MAPENZI YA MUNGU KWA MTU BINAFSI.
Hili ni kusudi ambalo Mungu anataka ulifanya ukiwa hapa duniani kupitia karama, au nafasi uliyopewa na MUNGU. Ni lazima ufahamu duniani umeitiwa kufanya nini wewe kama wewe.. Kama umeitwa kuwa Askofu, au mwalimu, au mchungaji, au nabii, au mtume, au mwinjilisti, au mtu mwenye kukirimu, au mshauri, au mwingine yoyote katika nafasi yoyote ile kwa ajili ya ufalme wa MUNGU.
Usipojua mapenzi ya MUNGU ni yapi ni ngumu kuishi kwa kumpendeza MUNGU, kwasababu utafanya jambo lisilompendeza Mungu, utaishi mahali pasipopendeza Mungu, utaenda katika njia ambayo Mungu hajaikusudia juu yako.
Na mapenzi ya Mungu yanatofautiana kwa mtu na mtu.. anavyotembea mwingine si sawa na utakavyotembea wewe,..lakini wewe umekusudiwa njia yako tofauti na mwingine, ni lazima uijue.
Sasa unajuaje kusudi/mapenzi ya Mungu kwako?
Njia ya kwanza ni ya kumpokea YESU na kutubu dhambi.. baada ya hapo, kuomba huku ukidumu katika kumpenda MUNGU, Roho Mtakatifu atakuongoza katika kusudi lake, na ukikaa katika kusudi/mapenzi ya MUNGU, utaona amani ya kiMungu ndani yako, na pia mafanikio katika utumishi huo.
Na utakapojaribu kuacha njia hiyo utaona mambo hayaendi kabisa..hapo utajua kuwa ulikuwa kwenye njia sahihi ya mapenzi ya MUNGU.
2. MAPENZI YA MUNGU KWA WATU WOTE.
Baada ya kujua mapenzi ya MUNGU kwako ni yapo, kwamba unapaswa ufanye nini, wakati mwingine uishi wapi, au utembee na nani safari bado haijaisha ni lazima pia uyajue mapenzi ya MUNGU kwa watu wote, aliyoyakusudia kila mtu ayaishi.
Sasa hayo mapenzi ya MUNGU kwa wote ni yapi?.. Tusome maandiko yafuatayo..
1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati; 4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima; 5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.
1Wathesalonike 4:3 “Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;
4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;
5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu”.
Kumbe mapenzi ya Mungu kwetu sote ni KUTAKASWA (Yaani utakatifu), na TUEPUKANE NA UASHERATI (wa mwilini na rohoni) na TUJUE KUIWEZA MIILI YETU KATIKA UTAKATIFU na HESHIMA.
Hapa ndipo shetani anapofumba macho wengi.. ni kweli tumejua mapenzi ya MUNGU kwetu ni kumtumikia, kumwimbia, kuhubiri, kufanya uinjilisti, lakini tumekosa kujua kuwa mapenzi ya MUNGU kwetu wote (kama watu wa Mungu) ni kuishi maisha matakatifu, yenye staha mwilini na rohoni.
Utakuta mkristo ameokoka anamwimbia Mungu, anahubiri na kweli wito wa MUNGU ndio uliomweka hapo, lakini tazama uvaaji wake, tazama maisha yake ya sirini, ni dhambi tupu imetawala.
Ni lazima kuyafanya mapenzi ya Mungu katika migawanyiko yote.
Bwana atusaidie sana kuliona hili, na yeye ni mwaminifu hajatuitia kwa hukumu bali tupate Baraka na faida, usiukimbie utakatifu ndugu mpendwa katika KRISTO, pasipo huo hatutaweza kumwona MUNGU (Waebrania 12:14).
Na kwa nguvu zetu hatutaweza kuishi maisha hayo ya usafi, lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu yote yanawezekana, tafuta ujazo wa Roho Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Ipi tofauti ya utakatifu na utukufu?
CHAGUA UTAKATIFU MWAKA HUU.
JAWA SANA MOTO ULAO.
JE! NINAWEZA KUPOTEZA FURAHA YA WOKOVU?
UVUKISHE MIPAKA UPENDO WAKO.
Print this post
Warumi 6:23
[23]Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Kwenye vifungu hivyo tunaonyeshwa kuwa Mungu hutoa zawadi(karama), lakini dhambi inalipa mshahara.. Na mpaka ilipe mshahara ni lazima kazi fulani ilifanyika..
Watu wengi hawajua kuwa kila tendo moja la dhambi, huhesabu mshahara fulani na mwishoni mtu huyo hulipwa wote, hata kama hakujua.
Unapokwenda kuzini leo, unarudia tena na kesho, na kesho kutwa hivyo hivyo, mshahara unajilimbikiza, siku isiyo na jina utashangaa tu ghafla mshahara wako huo hapo umekufikia…
Ndio hapo mauti ya kiroho au ya kimwili au ya jambo fulani humfikia mtu.
Sasa inapofikia wakati wa mshahara wengi hujifanya haiwahusu, lakini utaupokea tu.. upende usipende…wengi humdharau Yuda kwanini alijinyonga, si kwamba alipenda lakini ulikuwa ni wakati wa mashahara, ukiona leo watu wanakutana na madhara makubwa kwasababu ya dhambi zao, sio kwamba wana bahati mbaya, bali ni wakati wa mshahara.
Epuka dhambi, ikimbie dhambi.
Shalom
Yeremia 2:13
[13]Kwa maana watu wangu hawa wametenda maovu mawili; wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji ya uzima, wamejichimbia mabirika, mabirika yavujayo, yasiyoweza kuweka maji.
Ndugu Ipo tofauti kati ya chemchemi na birika, chemchemi ni chanzo cha asili ambacho hutoa maji yake yenyewe, haihitaji kuchimbwa, wala kukarabatiwa lakini birika ni hivi visima ambavyo mtu hutumia jasho lake kuchimba na hutegemea mvua ili kuwa na maji, lakini bado huvujisha maji yake chini ya ardhi ndio maana baadaye hukauka…maji ya visima kikawaida hayawagi masafi sana kwasababu hayatembei, ni rahisi kuona vyura, ngala, ruba, tofauti na ya chemchemi.
Sasa Bwana anasema watu wake wamefanya makosa MAWILI. Kwanza wamemuacha yeye aliye chemchemi ya maji ya uzima, Maana yake wana kiu, lakini hawataki maji yaondoayo kiu…hicho huitwa kiburi, au dharau na matokeo ya kiburi ni maangamizi. Ni sawa na mtu anajijua kabisa ni mgonjwa halafu analetewa tiba anasema sinywi dawa zako.
Lakini kama hilo halitoshi, wanaenda kufanya kazi ya kuunda chemchemi zao bandia, kwa kuchimba wenyewe ili wajihifadhie maji yao ambayo ni ya muda…hii ndio huitwa ibada ya sanamu..watu wanapoona fedha inaweza kusimama badala ya Mungu, hiyo ni sawa na kujichimbia birika ..wanapoona elimu, ushirikina, anasa, ulevi, ujuzi..vinatosha kuwa mbadala wa Mungu ni kujichimbia birika lako mwenyewe..
Ndio maana wanataabika, kutafuta ukweli wote ndani yake hawapati, wanapata raha za kitambo baada ya hapo ni majuto kurudi.
Ndugu tulia kwa Kristo ambaye alishamaliza kuunda chemchemi yake, kwake yeye huhitaji kutendea kazi, nenda tu unywe maji, kiu ya dhambi na mambo mengine maovu ya kidunia ife, uishi maisha ya amani na kustawi. Maji hayo ukinywa hata ukifa utakuwa unaishi, na kumpokea Yesu ndio kuyapokea maji. Ukimwamini Yesu na kumfanya Bwana na mwokozi wa maisha yako, na kumtii baada ya hapo ujue ndani ya roho ya maji yameshawasili.
Yohana 4:13-14
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; [14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
[13]Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
[14]walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.
Achana na mabiriki.
Mungu atusaidie.
Matumizi ya damu ya YESU hayaishii tu katika kutamka, kwamba tukiwa na haja na jambo tunatamka “Kwa Damu ya YESU” na jambo lile linatokea au linatii… hapana ni zaidi ya hapo, kwasababu hata mashetani wanamjua Bwana YESU na Damu yake.
Hivyo hayatishiki na mtu wa kawaida kulitaja jina la YESU au Damu ya YESU na huku mtu huyo hana uhalali, au mamlaka ya kutumia Jina hilo, soma kilichowatokea Wana saba wa Skewa (Matendo 19:4) unaweza kuelewa zaidi.
Sasa Mamlaka ya kutumia DAMU YA YESU, tunapataje?
Tunapata mamlaka ya kutumia DAMU YA YESU kwa kanuni moja tu!, nayo ni ile ya kuwa na UNDUGU WA DAMU NA YESU?
Utauliza mtu anaweza kuwa na undugu wa Damu na YESU na mwingine asiwe nao?..
Ndio!, hiyo inawezekana kabisa na nitakuonyesha kimaandiko…Lakini tambua jambo moja kuwa ili mtu aitwe ndugu yako ni lazima muwe na mfanano wa damu, mnaweza msifanane sura, au mwonekano lakini bado damu ikaeleza undugu mlio nao (hiyo imethibitika kisayansi na wanadamu).
Na YESU KRISTO anao ndugu zake wa damu.. sasa tunawajuaje?.. tusome maandiko yafuatayo Mathayo 12:47
Mathayo 12:47 “Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe. 48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani? 49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu! 50 Kwa maana ye yote ATAKAYEYAFANYA MAPENZI YA BABA YANGU aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu”.
Mathayo 12:47 “Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.
48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani? 49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!
50 Kwa maana ye yote ATAKAYEYAFANYA MAPENZI YA BABA YANGU aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu”.
Umeona? Ndugu za YESU wana sifa gani?… hawana sifa ya usomi, au uzuri, au ukuu au umaarufu… bali ni wale wote WANAOFANYA MAPENZI YA BABA ALIYE MBINGUNI.
Kumbe ili tuwe NDUGU WA DAMU WA YESU, ni lazima TUYAJUE na KUYAFANYA MAPENZI YA BABA MBINGUNI?.
Je unayajua mapenzi ya MUNGU kwako?.. Kama huyajui je unawezaje kuwa na ujasiri wa kuitumia DAMU YAKE, na ilihali huna muunganiko wowote na hiyo DAMU?
Ni lazima uyajue mapenzi ya MUNGU, na KUYAFANYA.. ili ile damu iweze kunena mema juu yako (Waebrania 12:24).
Je wewe ni ndugu wa YESU?… Je unayajua Mapenzi ya MUNGU kwako?.. kama bado huyajui au huna uhakika kama unayafanya mapenzi yake au la!, basi usikose sehemu inayofuata ya somo hili inayozungumzia MAPENZI YA MUNGU.
Waebrania 2:11 “Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake; 12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa. 13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu. 14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi, 15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.
Waebrania 2:11 “Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;
12 akisema, Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu; Katikati ya kanisa nitakuimbia sifa.
13 Na tena, Nitakuwa nimemtumaini yeye. Na tena, Tazama,mimi nipo hapa na watoto niliopewa na Mungu.
14 Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,
15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.
Bwana atusaidie..
MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.
Dunia inalewa-lewa kama mlevi, nayo inawaya-waya kama machela.
SAFARI YA KUUONA USO WA MUNGU.
Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?
Nini tofauti ya kushuhudia na kuhubiri?
WhatsApp
Nini maana ya “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”
Jibu: Turejee..
Mithali 11:22 “Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe, ndivyo alivyo mwanamke mzuri asiye na busara.”
Kabla ya kujua kwa undani maana ya mstari huu, hebu tujifunze kidogo juu ya Nguruwe, na pete inayowekwa puani mwake.
Nguruwe ni mnyama mwenye sifa ya uchafu, na asiyekuwa na ustaarabu, anaweza kuoshwa na baada tu ya kumaliza kuoshwa akarudi kwenye matope..Biblia inatuthibitishia hilo..
2Petro 2:22 “Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”
Sasa pamoja na tabia hiyo ya uchafu na kukosa ustaarabu nguruwe waliyonayo, bado wana tabia nyingine ya kuchimba chimba chini ya ardhi, au kwenye mashamba na kwenye zio kwa kutumia “pua zao” kwa lengo la kutafuta chakula, au utofauti wa mazingira.
Tabia hiyo ya kuchimba chimba kwa kutumia pua, inawafanya kubeba tabia nyingine ya uharibifu usiokuwa wa kawaida,
Sasa wafugaji wa nguruwe ili kulidhibiti hilo, huwa wanaweka pete katika pua zao lengo ni ili wanapojaribu kuchimba chimba kwa kutumia pua zao, basi ile pete iliyowekwa puani iwaumize na waache au kupunguza tabia hiyo ya uharibifu.
Sasa hizi pete si za urembo, bali zinakuwa kama Hereni kwenye pua ya nguruwe, na zinakuwa ni za chuma..tazama picha juu..
Sasa inapotokea Mfugaji anamwekea nguruwe pete ya dhahabu badala ya chuma isiyo na thamani..itakuwa ni jambo la ajabu sana na la kushangaza..kwani nguruwe kamwe hajawahi kuthamini kitu cha thamani, na hata yeye mwenyewe hajithamini soma Mathayo 7:6
Sasa anapowekewa kitu cha thamani puani mwake, ni kitu cha ajabu na kinachoshangaza..
Kwa mantiki hiyo hiyo Biblia inajaribu kuufananisha uzuri wa mwanamke na PETE YA DHAHABU, na mwanamke asiye na busara inamfananisha na NGURUWE.
Kwamba Mwanamke aliye na uzuri wa uso halafu akakosa busara ni sawa na kitu cha thamani kilichowekwa mahali pasipostahili.
Mwanamke mzuri wa uso/wa nje halafu hana heshima kimwonekano ni sawa na pete puani mwa nguruwe,
“Uzuri” na “Busara” ni lazima viende pamoja, lakini ukiwa ni mzuri halafu huna busara ya kiMungu, unafananishwa na nguruwe.
Sasa swali ni je hii busara inapatikana wapi?
Chanzo cha Busara halisi ni YESU KRISTO, kwamba unapompokea YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, basi hapo tayari umeshafungua mlango wa busara kuumbika nakuanza kufanya kazi ndani yako.
Na kazi hiyo ya kujaza busara ndani yako ni ya Roho wa Mungu atakayeingia ndani yako baada ya wewe kuokoka….Utaanza kuona kiwango chako cha hekima kinaongezeka, na ueledi katika masuala ya kiroho na kimwili.. na hiyo busara itaulinda uzuri wako wa nje na ule wa ndani kama maandiko yanavyosema..
Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako; 11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi”
Mithali 2:10 “Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;
11 Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi”
Wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe. Akawapa ruhusa.
USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.
Je? ni sahihi kwa watu wa MUNGU kutumia majina ya wanyama kuwaita wengine.
Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?
Kwanini Mungu aliwazuia walemavu wasimtumikie madhabahuni kwake?(Walawi 21:16-24)
Zaburi 42:8
[8]Mchana BWANA ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami,..
Biblia inataja nyakati mbili, ambazo mwamini anazipitia..nazo ni mchana na usiku.
Mchana ni nyakati za matumaini, nyakato za kuona njia, za kufanikiwa, za amani…hizi ni nyakati ambazo Bwana anasema ataagiza fadhili zake…maana ya fadhili ni kujitoa kwa upendo wa juu sana..Mungu huwafadhili watu wake hata katika nyakati za furaha, na amani.
Lakini pia anasema wakati wa usiku wimbo wake bado utakuwa nasi…usiku ni wakati wa huzuni, wakati wa upweke, wakati wa ukame wa kiroho, wakati wa majaribu, na mapito n.k.
Ni nyakati ambazo huoni chochote…kwasababu usiku sikuzote ni nyakati za ukimya na upofu..
Lakini pia huko Bwana anasema juu ya watu wake kuwa WIMBO WAKE, utakuwa pamoja nao.
Wimbo humaanisha faraja, kicheko, shangwe, yaani hatawaacha wawe kama walio gizani wanyonge, wapweke, bali kama watu wafurahishwao na nyimbo nzuri sana..
Kama mwana wa Mungu, nyakati za majaribu, Bwana yupo pamoja na wewe, nyakati ambazo huzielewi upo wimbo wake ndani yako.
Wakristo wafikiapo hatua hii huukimbia wimbo wa Bwana na kutazama zaidi changamoto zao, shida zao, magumu yao, na mengineyo kana kwamba Mungu amewaacha,
Lakini kama ukibakisha fikra zako kwake…utaona bubujiko kubwa sana likitiririka ndani yako, kwa jinsi ile ile ulivyokuwa katika nyakati za nuru..
Kwasababu hii ni ahadi yake. Na kamwe hawezi kudanganya. Unapojifunza kutulia uweponi mwa Mungu, kimaombi, kwa kutafakari, uwapo kwenye hizo nyakati hafifu..ghafla tu utaona furaha, amani, ushindi, kicheko, uwepo wa Bwana vinajaa ndani yako.
Kamwe usiukandamize wimbo huu?
UYATIE MACHOZI YANGU KATIKA CHUPA YAKO EE! BWANA.
JITIE NGUVU KWA BWANA MUNGU WAKO.
MAISHA YA UVUGUVUGU, YANAMFANYA MUNGU AUMWE.
Mithali 29:20
Je! Umemwona mtu mwenye kuhamaki katika maneno? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye
Mtu mwenye kuhamaki.
Ni mtu anayezungumza maneno kwa haraka, yaani anayezungumza bila kufikiri, au kujizuia.
Vitu kama mizaha, ugomvi, hasira, uongo, na mafarakano, huzaliwa na tabia kama hii ya watu kunena bila kufiriki.
Kwamfano, mtu anaweza kukutukana, na wakati huo huo hasira ikawaka ndani, sasa kwasababu huwezi kujizuia, unajikuta unarudisha majibizano, hatimaye na wewe unafungua kinywa chako unatukana.
Au labda unatambua jambo Fulani ambalo si jema, na pengine ukilisema linaweza lisiwe na maana yoyote, kinyume chake likazua ugomvi, au kumuabisha mwingine, au sintofahamu, lakini wewe kwasababu huwezi jizuia unalisema, mwishowe matatizo yanazuka makubwa yasiyokuwa na lazima.
Watu wanaoapa, ni matokeo ya kunena bila kufikiri, mafarisayo ambao walitenda dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni kwasababu ya maneno ambayo hayana hekima nyuma yake.
Mathayo 12:36 Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.
Mpaka hapo unaweza kuona ni kwanini mpumbavu anaweza kuonekana ana afadhali kuliko mtu mwenye kuhamaki.
Mstari huu unatukumbusha nguvu iliyopo katika maneno, biblia inasema ulimi ni kama moto ni kiungo kidogo lakini kinawasha misitu, hivyo hatuna budi kuwa wazito katika kunena, tukifiri kwanza ndipo tuseme. Yakobo 1:19
19 Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika;
Maneno yana nguvu, kila siku yatupaswa tujifunze kudhibiti vinywa vyetu.
KUMBUKA NI AMRI MPYA!
SHUGHULIKA NA HASIRA INAYOKAA KIFUANI
KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.
JIBU: Wakiwa jangwani wana wa Israeli walitenda makosa ya aina mbili.
Makosa yaliyopoteza Ahadi ndio yalikuwa yale ya kutokuamini. Mfano Mungu alipowatoa jangwani, na kuwavusha, mara nyingi walionyesha hali ya kutoamini, Kosa ambalo liliwafanya Mungu aghahiri kuwafikisha kule alipowaahidia, ambapo ni nchi ya Kaanani ibubujikayo maziwa na asali, Na kilele cha kosa hilo kilikuja pale wale wapelelezi waliporudi katika kuichunguza nchi, na kutoa ripoti za kule, kwamba wao wanaonekana kama mapanzi, hivyo wote wakaanza kulia na kutaka kurudi Misri, Ndipo Mungu akakasirika sana na kuapa kuwa wote hawataiona hiyo nchi ya Kaanani isipokuwa Kalebu na Yoshua, kwasababu wao hawakuonyesha kutokuamini.
Hesabu 14:21-24
21 lakini hakika yangu, kama niishivyo, tena kama dunia hii nzima itakavyojawa na utukufu wa Bwana; 22 kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu; 23 hakika yangu hawataiona hiyo nchi niliyowaapia baba zao, wala katika hao wote walionidharau hapana atakayeiona; 24 lakini mtumishi wangu Kalebu, kwa kuwa alikuwa na roho nyingine ndani yake, naye ameniandama kwa moyo wote, nitamleta yeye mpaka nchi hiyo aliyoingia; na uzao wake wataimiliki
Lakini hiyo haikumaanisha kuwa hawatakwenda mbinguni, kwasababu wapo waliotubu,hata wakati ule ule
Kwahiyo kusema adhabu ile ndio iliwapelekea moja kwa moja kupoteza mbingu si sahihi.
Kwasababu Mungu aliendelea kutembea nao kwa wingu lake, baadaye akawainua viongozi, wa kuwaaamua na Pamoja na wazee, akawamwagia Roho wake, (Hesabu 11:25). Hivyo kama Mungu kasingekuwa nao, basi hayo yote yasingefanyika, kwasababu Mungu hawezi kuwaongoza wafu.
Lakini yapo makosa ambayo yaliwagharimu adhabu ya kupoteza kabisa uzima wa milele. Na makosa kama hayo ndio yale ya makusudi kabisa, mfano wa hayo ni yale ya kuvunja amri za Mungu, kama vile kutengeneza sanamu ya ndama na kuiabudu, Kuzini, kuwa na miungu mingine, na kuhalifu sabato za Mungu .
Makosa kama hayo ndio yaliyopelekea kupoteza uzima wa milele, ndio maana ukichunguza utaona watu kama hawa walipokea adhabu za moja kwa moja. Hivyo ni kuwa makini sana na neema ya Mungu.
Hata sasa, zipo dhambi za aina mbili zinazozungumziwa kwenye maandiko, dhambi za mauti, na dhambi zisizo za mauti.
Kwa urefu wa maelezo yake, pitia hapa>>> DHAMBI YA MAUTI
Mungu akubariki.
Je shauri la kuipepeleza Kanaani lilitoka kwa wana wa Israeli au kwa BWANA?
Kwanini Roho Mtakatifu amzuie Paulo kuipeleka injili Asia? (Matendo 16:6-7).
Yohana 13:34
[34]Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.
Hapo mwanzo nilipokuwa nautafakari huu mstari, nilijiuliza maswali Yesu anaposema “AMRI MPYA..
Ni amri ipi hiyo mpya?
Maana ukitafakari anasema “mpendane” kwani kupendana ni amri mpya?
Mbona ilikuwepo tangu zamani? Na ilijulikana
Mambo ya Walawi 19:18
[18]Usifanye kisasi, wala kuwa na kinyongo juu ya wana wa watu wako; bali umpende jirani yako kama nafsi yako; Mimi ndimi BWANA.
Kupendana kulifundishwa tangu zamani za torati…lakini mpaka Kristo anasema amri mpya maana yake kupendana anakokusema yeye ni tofauti na kule kulivyodhaniwa…
“Ndio maana akasema…Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.”
Yaani mpendane kwa mfano wa upendo wangu, sio mfano wa upendo mwingine.
Upendo wa upeo.
Yohana 13:1
[1]Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.
Upeo ni ukomo wa mwisho kabisa…Yesu hakutupenda kwa wakati fulani tu…bali alitupenda (sisi tuliomwamini) mpaka mwisho, kabisa kutoka moyoni..
Ikiwa na maana alipiga gharama ikitokea huyu amenisaliti, Amenikana, amenizunguka…je nitakoma kumpenda?…hivyo akaamua kukubaliana na yote…liwalo na liwe nimempenda, na nitampenda mpaka mwisho..
Ndio maana ijapokuwa alijua Yuda atamsaliti, na Petro atamkana, hakuacha kuwapenda…sasa huo ndio upendo wa Kristo mpya..upendo wa upeo
Leo ni rahisi kupenda mtu kwa mema, au mazuri anayoyadhihirisha sasa…lakini ikitokea baadaye yule uliyemsaidia anakusaliti, uliyemhudumia anakudharau, uliyemsomesha hatimaye amekuwa na cheo kikubwa kuliko wewe sasa anakucheka,..hapo hapo unaanza kuumizwa, hata kumchukia, na kumlalamikia…sasa huo sio upendo wa upeo….ni upendo wa nyakati…lakini ikiwa anakutendea mambo yote hayo halafu hujali hapo ndio upendo ule mpya wa Kristo anapodhihirika.
Bwana anataka tupige gharama ya kuanzia mwanzo hadi mwisho…ukiamua kumpenda mtu..basi mpende daima. Bila sharti.
Upendo mpya.. ni ule wa kupenda wanaokuchukia, ule wa zamani ulikuwa mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.(Mathayo 5:43-44).. kilele cha upendo huu mpya ni kuwa tayari kugharimika lolote kwa ajili ya wengine..(Yohana 15:13)
Je amri hii mpya tunayo?
2 Yohana 1:5
Na sasa mama, nakuomba, si kwamba nakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo, kwamba tupendane.
Bwana awe nawe.
Shalom.
NYAKATI TOFAUTI- TOFAUTI ZA UPENDO.
JAWA NA UPENDO UNAOTAFUTA.
JE UPENDO WAKO UMEPOA?
1 Samweli 30:6
[6]Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake.
Zipo nyakati, ambazo watu wanaokuzunguka wanaweza kufarakana nawe, kama sio watu basi mazingira au hali zinazokuzunguka zinaweza kukupinga kabisa kiasi kwamba ukakata tamaa ya kusimama au kuendelea mbele.. ukiangalia kulia, ukiangalia kushoto hakuna linalokusapoti…si watu, si vitu.
Ndio lililomkuta Daudi, ambaye hapo mwanzo walikuwa wanamwimbia “ameua makumi elfu”, waliyempenda, lakini mambo sasa yamegeuka wanataka kumpiga mawe…afe,
Hakuona mtu wa kumshika mkono kumwinua au kumfariji…Hivyo na yeye hakukaa chini na kulia na kusema Bwana mbona sioni msaidizi, hakukaa chini na kusema Bwana ona fadhili zote nilizowatendea leo wanataka nipiga mawe,
Daudi ijapokuwa alikuwa katika mafadhaiko makubwa, maandiko yanatuambia AKAJITIA NGUVU MWENYEWE, katika Bwana..Mungu wake..
Hakutafuta kutiwa nguvu na mtu. Na matokeo yake alipolifuatilia jeshi, akalipata akawapiga, kisha akawarudishia mateka wao wote walioibiwa na mali nyingi..ukawa ushindi mkuu sana.
Lakini hiyo yote ilianza kwa kujitia nguvu mwenyewe ndani. Hayo ndio yalikuwa mafanikio ya Daudi.
Leo hii watu wengi, wanabakia kusubiri faraja za watu, kuinuliwa na watu, kuthibitishwa na watu…Ni kweli hayo ni vizuri lakini yanapoondoka basi na maono hufia hapo hapo…lakini tukijitia nguvu katika Bwana.. tutafanikiwa katika nyakati zote hata zile ngumu.
Hatufanikiwi ndipo tujitie nguvu katika Bwana…tunajitia nguvu kwanza ndipo ushindi unakuja, baadaye hiyo ndio kanuni ya kiroho.
Kabla ya mikakati, mipango, tunajitengeneza kwanza wenyewe nafsi zetu, humu ndani, tukimuamini Mungu aliyetuita kuwa ameahidi hatatuacha, wala kutupungukia. Ndipo tunapoelekea kutekeleza maono yetu.
Tembea na kanuni hiyo. Ondoa matarajio kwa wanadamu.
Bwana akubariki